Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo

$
0
0

Bond Aliyekuwa Mpenzi wa Wastara zamani Achukizwa na Kauli ya Wastara ya Kutopenda Wanaume Weupe...Amtolea Mbovu Mbovu

$
0
0
Bond Aliyekuwa Mpenzi wa Wastara zamani Achukizwa na Kauli ya Wastara ya Kutopenda Wanaume Weupe...Hili limekuja Baada ya Wastara Kuhojiwa na Kutaja Vigezo vya Mwanaume Anayependa Amuoe...Amtolea Mbovu Mbovu Kupitia Ukurasa wake wa Instagram:

Bond Ameandika
"Sinema ya kutisha nipale mtu anasema hapendi weupe halafu we umemukula miaka 4. Hukuwa na geto na umeishi nae miaka 4. Hapo lazima steringi awe geabox... Kudadeki wasukuma sisi hahaha , Heloo mazaaa... Bhawelage chizaaa koiii..."

Breaking News: Mwili wa Samson Josiah, Mmiliki wa Mabasi ya Super Sami Waokotwa Mtoni Kwenye Kiroba

$
0
0
Mwili wa Mmiliki wa mabasi ya Super Sami Samson Josiah umekutwa katika mto Ndabaka eneo la Bunda /Lamadi

Taarifa kutoka vyanzo vya habari zinasema kwamba mwili wa Samson Josiah umeokotwa na wavuvi wa samaki leo jioni Jumatano Machi 14,2018.

Watu wa karibu na marehemu wanasema mwili uliookotwa ni wa Samson Josiah.

Miongoni mwa habari zilizoteka vyombo vya habari Tanzania tangu Machi 9, 2018 hadi ni kuhusu kupotea kwa mmiliki wa mabasi ya Super Sami, Samson Josiah kwa zaidi ya wiki mbili sasa. 
Mapema ilielezwa kuwa gari yake ndogo aliyokuwa akiitumia aina ya Toyota LandCruiser ilikutwa imechomwa moto katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti iliyoko mkoani Mara siku ya Machi 9, lakini yeye mwenyewe alikuwa hajapatikana.

Kwa mujibu wa familia ya Bwana Josiah, ambayo inaishi mkoani Mwanza, ilidai kuwa siku ya kupotea kwa Josiah ambayo ni February 27, majira ya usiku, Josiah alimpigia simu mkewe na kumwambia kuwa atarudi nyumbani na mgeni, na hayo yakawa mawasiliano yao ya mwisho.

Mabasi ya Super Sami yanafanya safari zake kuanzia mkoa wa Mwanza, kwenda mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Iringa pamoja na Kagera.

Chanzo: Muafrika Halisi blog
JF

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715 

Inatisha! Mwili wa Mmiliki wa Mabasi ya Super Sami Waokotwa na Wavuvi

$
0
0
Inatisha! Mwili wa Mmiliki wa Mabasi ya Super Sami Waokotwa na Wavuvi

MWILI wa mmiliki wa mabasi ya Super Sami, Samson Josiah,  unadaiwa umekutwa na wavuvi mto Ndabaka eneo la Bunda – Lamadi akiwa amefariki dunia jana Jumatano, Machi 14,2018 jioni huku watu wa karibu na marehemu wakithibitisha kuwa mwili huo ni wake.

Machi 9, 2018 taarifa za kupotea kwa Josiah kwa zaidi ya wiki mbili zilianza kusambaa baada ya gari lake alilokuwa akitumia aina ya Toyota Land Cruiser kukutwa limechomwa moto katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti iliyoko mkoani Mara huku  akiwa hajulikani alipo.

Gari lake lilivyokutwa limechomwa moto.

Global Publishers imemtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Jafary Mohammed, ambaye amethibitisha kupokea taarifa hizo.

Panga lililokutwa eneo la tukio.

“Hata mimi nimesikia tu taarifa za kuokotwa kwa mwili wa Samson Josiah, sasa hivi ndiyo ninaelekea eneo la tukio ili kufahamu kilichojiri, kama ni yeye aliyeokotwa au ni mwingine. Lakini taarifa za kupotea kwake zilitufikia na tulizitoa kwa umma siku chache zilizopita, hivyo tuwe na subira, tutawaeleza baada ya kupata taarifa kamili,” alisema RPC.

Gari lake likiwa limeteketea kwa moto

Kwa mujibu wa familia ya Josiah, ambayo inaishi mkoani Mwanza, ilidai kuwa siku ya kupotea kwa kwake ambayo ni Februari 27, majira ya usiku, alimpigia simu mkewe na kumwambia kuwa atarudi nyumbani na mgeni, na hayo yakawa mawasiliano yao ya mwisho.


Eneo la tukio.
Mabasi ya Super Sami yanafanya safari zake kuanzia mkoa wa Mwanza, kwenda mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Iringa na Kagera.

Video: Uzinduzi wa Diamond Watikisa Kenya Awaliza Wakenya Jukwaani na Historia ya Maisha Yake

$
0
0
Video: Uzinduzi wa Diamond Watikisa Kenya Awaliza Wakenya Jukwaani na Historia ya Maisha Yake

MSANII wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amezindua rasmi albamu yake mpya ‘A Boy From Tandale’ jijini Nairobi na kufanya bonge la shoo akiwa na timu nzima ya WCB.

Mbali na WCB, wasanii wengine waliopada jukwaani na kutikisa katika shoo hiyo, ni msanii wa Marekani, Omario.


Albamu mpya ya Diamond imesheheni ngoma 20 kali zikiwemo alizowahi kuzitoa kipindi cha nyuma na nyingine mpya.



Rwanda Yapiga Marufuku Adhana

$
0
0
Rwanda Yapiga Marufuku Adhana
Marufuku ya matumizi ya adhana{ Wito kwa Waislamu kuhudhuria maombi} katika tarafa moja ya mji wa Kigali nchini Rwanda imepingwa vikali na baadhi ya Waislamu jijini humo.

Utawala katika tarafa ya Nyarugenge kunakopatikana jamii kubwa ya Waislam nchini humo umebainisha kuwa kumekuwepo muafaka wa kubadili mbinu za kuwaita waumini bila ya matumizi ya njia hiyo ambayo inatajwa kuwasumbua wananchi.

Kulingana na mwandishi wetu mjini Kigali John Gakuba wito huo wa Waislamu kuhudhuria maombi umetajwa kuwa kero miongoni mwa wananchi.

Tayari mkataba wa kuhakikisha kuwa mwafaka huo unaheshimiwa umetiwa saini kati ya viongozi wa msikiti na utawala wa eneo hilo.

Wito huo wa mamombi miongoni mwa jamii za Waislamu kote duniani hutumia vipaza sauti na hufanyika mara tano kwa siku.

Licha ya utawala wa eneo hilo kudai kwamba kumekuwa na mwafaka kutoka pande zote mbili baadhi ya Waislamu waliohojiwa wametoa hisia tofauti.

Kulingana na katibu mtendaji wa tarafa hiyo ya Nyarugenge, amri hiyo iliagizwa yapata miaka maiwili iliopita lakini ikapuuziliwa mbali.

''Pengine wakati ule sababu ambazo watu hawakupokea vyema ujumbe ilikuwa hakuwa umeelezewa sawa sawa ,lakini leo baadhi ya makanisa yalilazimika kufunga milango baada ya kushindwa kutimiza kanuni za ujenzi huku misikiti yenye vipaza sauti na makanisa yenye kengele tukiyataka kutotumia mtindo huo. Mtu aliye lala akiishi jirani na kengele hiyo inampigia kelele. Kwa hiyo ni uamzi unaohusu pande zote nna ni matarajio yetu kuwa hakuna aliyenyimwa haki.''

Naye mshauri wa Mufti wa Rwanda shekh Mbarushimana Suleinam alisema kuwa hatua hii ya kuzuiliwa kwa matumizi ya adhana misikiti inafuatia operesheni inayoendela ya kufungwa kwa makanisa na vigango Zaidi ya mia saba ambavyo viliripotiwa kuwa havijatimiza kanuni za ujenzi na amri ilitolewa kwanza kutimiza matakwa ili zipewe tena idhini ya kufanya kazi.

Mziki Umekwamia Hapa 2018 Rasmi Tunaenda Walipokwenda Ndugu Zetu Bongo Movie- Nay wa Mitego

$
0
0
Mziki Umekwamia Hapa 2018 Rasmi Tunaenda Walipokwenda Ndugu Zetu Bongo Movie- Nay wa Mitego
Moja kati ya stori kubwa zilizochukua headlines kwenye kiwanda cha Bongofleva ni pamoja na exclusive interview ya XXL ya Clouds FM na naibu waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Juliana Shonza iliyofanyika jana kwenye ofisi za BASATA.

XXL walifanya interview na naibu waziri Shonza na kuhoji masuala mbalimbali kuhusiana na sanaa ikiwemo maamuzi ya naibu waziri Shonza ya kufungia baadhi ya wasanii na nyimbo zao kwa madai ya ukosefu wa maadili kama Roma Mkatoliki aliyefungiwa miezi sita na Nay wa Mitego aliyepewa onyo na kuomba radhi.

Baada ya mahojiano hayo yaliyokuwa yamefanywa na kuhudhuriwa na viongozi wa BASATA, BAKITA huku Wakazi na Vanessa Mdee wakiwakilisha wasanii wenzao, kila mmoja amepokea majibu ya Naibu waziri kwa mtazamo tofauti.


Kwa upande wa Nay wa Mitego baada ya interview hiyo akaandika maneno haya katika ukurasa wake wa twitter “Kwa mahojiano ya leo mtakuwa mmeelewa tatizo ni nini? nauona mwisho wa huu muziki umekwamia hapa rasmi 2018, mkubwa atabaki kuwa mkubwa na mdogo ataendelea kuwa mdogo na tusivyo na umoja tunaenda walipokwenda ndugu zetu Bongo Movie”

Daimond Amtaja Msanii Huyu Ambaye Anampa Tabu

$
0
0
Daimond Amtaja Msanii Huyu Ambaye Anampa Tabu
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz jana alifanya show kubwa ya uzinduzi wa album yake ya ‘A Boy From Tandale’ nchini Kenya na kukonga nyoyo za mashabiki wake na wadau wa muziki waliohudhuria kwenye uzinduzi huo.

Akiwa jukwaani Diamond aliulizwa na MC, kuwa Kenya kuna wasanii maarufu wengi na wengine wakongwe kama Nameless ambaye ana miaka 20 kwenye muziki unawaonaje?

Diamond akajibu “Katika watu ambao kila nikikutana nao kwenye show na kwanza nina bahati ya kukutana naye kwenye show anayokuwepo Nameless anauwa yaani anaperform kichizi kuzidi hata mimi mtoto wa Tandale”.

Dj Fetty Kurudi Kwenye Fani Yake ya Utangazaji?

$
0
0
Dj Fetty Kurudi Kwenye Fani Yake ya Utangazaji
September 15 2015 mtangazaji wa zamani wa kituo cha radio cha Clouds FM DJ Fetty alitangaza kuacha kazi ya utangazaji na kuwaaga wafanyakazi wenzake akisema ameamua kupumzika na kuwa atakuwa akifanya biashara zake nyingine.

DJ Fetty alikaa kimya kwa muda mrefu lakini kwa kuwa ni mwanafamilia wa Clouds FM March 8 2017 katika siku ya wanawake duniani alirudi tena XXL na kutangaza katika kipindi maalum kwa ajili ya wanawake duniani na kutangaza tena kwenye XXL.



Kwa mujibu wa post zake mbili za instagram alizozipost usiku wa jana, ya kwanza aliandika “Tizi limeanza. U want me back? weka 👍🏻 zikifika 1000 Mama la mama hewani” lakini baada ya comment 1000 za ndio za kutaka arudi akapost post ni nyingine na kuandika “Pheewwwww 🤐🤐 “1000👍🏻” 🙏🏻🙏🏻 shidddaaaaaah. Now stay tuned for official statement. I love u all” hayo ni maamuzi mazuri kwa Fetty na mashabiki wake.



Naibu Waziri: Alikiba Ni Mfano wa Wasanii Wenye Maadili Kwenye Nyimbo Zake

$
0
0
Naibu Waziri: Alikiba Ni Mfano wa Wasanii Wenye Maadili Kwenye Nyimbo Zake
Mwanamuziki Alikiba atajwa kama mfano kwa wasanii wengine katika wasanii wanaotoa nyimbo zenye maadili ikiwemo upande wa audio na hata video zake huku akiisfiwa kuwa hajawahi kumba maneno yenye matusi au kutoa video yenye picha za watu wakiwa uchi , hivyo wasanii wengine washauriwa kuiga mfano wa msanii huyo.

Hayo yamesemwa jana tarehe 14 March na naibu waziri na baraza la sanaa walipokuwa wakifanya mahojiano na clouds media katika kipindi cha XXL, ambapo waliamua kufunguka na kusema sababu kubwa za kuwafungia wasanii wengi nyimbo zao.

"Kwa mfano Alikiba ni msanii mkubwa wa kimataifa na amekuwa akiwakilisha vyema nchi sehemu tofauti tofauti lakini mbona haimbi lugha chafu katika nyimbo zake wala video zisizokuwa na maadili .sisi kama wizara tunataka sanaa iende pamoja na ukuaji wa maadili ya nchi, tutoe burudani lakini tulinde utamaduni wetu." Aliongea Naibu Waziri Juliana Shonza.

Hivi karibuni wasanii zaidi ya kumi walifingiwa kucheza kwa nyimbo zao katika vituo vyote vya habari nchi , huku Roma akifungiwa kabisa kufanya kazi kwa muda wa miezi sita kutokana na sababu za kushindwa kufuata masharti ya kubadilisha wimbo wake wa kibamia. Download App Yetu  >> BOFYA HAPA << Tukutumie Habari na Burudani Zote FASTA Kila Time BURE Kabisa !

Baada ya Kupelekwa Kamati ya Maadili Wambura Kufunguka Kuhusu Mashtaka Yanayomkabili

$
0
0
Baada ya Kupelekwa Kamati ya Maadili Wambura Kufunguka Kuhusu Mashtaka Yanayomkabili

Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Michael Richard Wambura, leo atatolea ufafanuzi kuhusiana na mshataka yanayomkabili ndani ya Shirikisho hilo.

 Kwa mujibu wa TFF, Wambura anakibiliwa na makosa matatu, la kwanza ni kupokea fedha za TFF. Pili, malipo yasiyo halali na tatu ni kugushi  barua na kushusha hadhi ya TFF.

Mhariri wa Gazeti Akimbia Nchi Kuogopa Wauaji Apewa Ifadhi Finland

$
0
0
Mhariri wa Gazeti Akimbia Nchi Kuogopa Wauaji Apewa Ifadhi Finland
MWANAHABARI Ansbert Ngurumo aliyewahi kuwa mhariri wa Magazeti ya Tanzania Daima na Mwanahalisi, amekimbilia nchini Finland na kupewa hifadhi kwa muda baada ya kudai amewakimbia aliowaita “wauaji” wake.


Ngurumo amethibitisha kuikimbia Tanzania ili kulinda uhai wake baada ya kuanza kuwindwa na watu wasiojulikana.

“Tangu mwaka jana nimekuwa nikipokea vitisho vingi na vyenye kuogofya kufuatia makala zangu kwenye gazeti la MwanaHalisi. Nimenusurika kuuawa mara kadhaa, lakini nashukuru Mungu hadi leo niko hai, ili kunusuru uhai wangu, nililazimika kujificha Mwanza tangu mwaka jana na baadaye kwenda Kenya, kabla ya kwenda Sweden na sasa Finland, ambako nimepewa hifadhi,” alisema Ngurumo.


Aliongeza kwamba hadhi aliyopewa Finland, siyo ya ukimbizini, bali ni “hifadhi ya kimataifa,” kuunusuru uhai wa mtu ambaye yuko katika hatari ya kuuawa nchini mwake.

Aidha, vyombo vya habari vya Finland na mitandao ya kijamii, vimeandika habari ya Ngurumo kukimbia Tanzania kwa hofu ya kuuawa.

“Nimezungumzia mkasa wangu wa kunusurika kudakwa na watu wasiojulikana, ambao wamekuwa wakipanga kuniua na wamejaribu mara kadhaa bila mafanikio, sasa nikaona niwakimbie, kwani kufa kijinga ni dhambi kubwa,” amesema Ngurumo.

Asiyejua Kufa Akachungulie Kaburi- Jeshi la Polisi

$
0
0
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Jeshi la Polisi, CP Nsatu Marijan amesema hali ya usalama nchini imezidi kuimarika kwani hakuna tishio lolote la kiuhalifu linaloweza kutokea kwasababu Jeshi la Polisi limejipanga ipasavyo na halishindwi na chochote.


Kamishna Marijan ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anatoa salamu za kumuwakilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro katika uzinduzi wa vituo vidogo vya polisi vinavyo hamishika 'mobile Police Station' ambapo vitaanza kutumika katika mkoa wa kipolisi Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

"Jeshi liko imara, matukio ya uhalifu nchini yamepungua sana, hakuta tishio lolote ambalo lipo nje ya uwezo wa Jeshi la Polisi kushindwa kulikabiri. Sisi kama Jeshi la Polisi tutaendelea kuhakikishia nchi hii inaendelea kuwa salama ili wawekezaji na wananchi waweze kufanya shughuli zao bila ya taflani yeyote", amesema Kamishna Marijan.

Pamoja na hayo, Kamishna Marijan ameendelea kwa kusema "kama mtu ana wasiwasi na Jeshi letu basi ajaribu kufanya lolote maana wanasema asiyejua kufa basi akachungulie kaburi. Sisi tupo imara tutaendelea kuwa imara".



Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema vituo hivyo vilivyo zinduliwa leo vitatumika kwa kadri ya maelekezo ya maeneo yenye uhalifu utakapotokea eneo fulani na endapo utapungua basi watavihamishia na kwenda eneo jingine lenye uhalifu.

Breaking News: TFF Yamfungia Maisha Kujihusisha na Msuala ya Soka Michael Wambura

$
0
0
Habari za ndani zinasema Kamati ya Maadili ya TFF imemfungia makamu wa Rais wa Shirikisho hilo, Michael Wambura kutojihusisha na soka maisha yake yote.


TFF imetangaza rasmi maamuzi ya Kamati hiyo saa 6 mchana muda ambao Wambura pia amepanga kuzungumza na waandishi wa habari baada katika hoteli ya Courtyard Upanga jijini Dar es salaam.


Sekretariati ya Shirikisho la soka Tanzania TFF ilimfikisha Makamu wa Rais wa TFF Michael Wambura kwenye kamati ya maadili akikabiliwa na tuhuma tatu ikiwemo kupokea fedha za malipo TFF za malipo ambayo hayakuwa halali.

Jana mchana afisa habari wa TFF Clifford Mario Ndimbo aliwaambia waandishi wa habari kwamba Wambura amefanya makosa hayo huku akijua anashusha hadhi ya shirikisho hilo ikiwa ni kinyume na katiba ya TFF.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya TFF, baada ya kamati ya maadili kupokea malalamiko yanayomhusu Wambura na kukutana jana (Machi 14, 0218) kwa ajili ya kujadili, imemfungia maisha Wambura kujihusisha na masuala ya soka.

Kwa mujibu wa afisa habari wa TFF Clifford Ndimbo, Wambura alikuwa na uhuru wa kufika mwenyewe mbele ya kamati na kutoa utetezi wake kwa njia mdomo, kutuma kwa maandishi au kupeleka mashahidi au kutuma mwakilishi ambaye ataambatana na barua ya uwakilishi. Wambura alituma mwakilishi ambaye ni Wakili Emanuel Muga kwa ajili ya kumtetea


Emmanuel Muga amesema hakupewa nafasi ya kumtetea mteja wake kwa sababu kamati ilikuwa na dhamira yake ya kutaka kulimaliza suala hilo siku hiyohiyo (jana Machi 14, 2018).

“Ni kweli sikupewa nafasi ya kumtetea kwa sababu kamati ilikuja ikiwa na dhamira yake kutaka kulimaliza suala hilo siku hiyohiyo. Kwa hiyo nilivyowasilisha masuala ya kisheria ambayo ni ya kikanuni, kamati ilikataa ikasema sisi tunaamua tunavyoona”-Emanuel Muga, Wakili wa Wambura.

“Kwa hiyo wakalifunga suala kwamba yanaenda kufanywa maamuzi, lakini hayo maamuzi yatafanyika wakati Wambura hajasikilizwa na Wakili wake hajasikilizwa.”

Afande Sele Ajitoa ACT Atambulishwa Rasmi CCM Mbele ya JPM

$
0
0
Aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Morogoro Mjini kupitia ACT-Wazalendo mwaka 2015, Selemani Msindi maarufu Afande Sele, leo Alhamisi Machi 15, 2018 ametambulishwa rasmi kama mwanachama wa CCM mbele ya Rais John Magufuli.

Baada ya utambulisho huo uliofanyika baada ya Sele ambaye pia ni mwanamuziki wa kizazi kipya, kutumbuiza moja ya nyimbo zake zilizotamba mwanzoni mwa miaka ya 2000, alivalishwa sare za chama hicho tawala na kupeana mkono na Rais Magufuli.

Afande Sele amekaribishwa leo ndani ya CCM katika hafla fupi ya uzinduzi wa kiwanda cha sigara cha Philip Moris Tanzania kilichopo mkoani Morogoro.

Hata hivyo, msanii huyo alikihama ACT takriban mwaka mmoja uliopita na kujiunga na CCM.

Rais Magufuli Azindua Kiwanda cha Sigara Morogoro

$
0
0
Rais Magufuli Azindua Kiwanda cha Sigara
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Machi 15, 2018 amezindua kiwanda cha kutengeneza sigara cha Philips Moris International.


Magufuli ametembelea kiwanda hicho na kushuhudia namna sigara zinavyotengenezwa kuanzia katika hatua ya kwanza mpaka sigara inapokamilika kwa matumizi au kwa ajili ya kuuzwa

Mmiliki wa kiwanda hicho alifuguka na kusema kuwa mpaka sasa kwenye kiwanda hicho kimeajiri zaidi ya watu mia mbili na ishirini na nne ambao wanahusika katika kuhakikisha uzalishaji unakwenda salama.

Waziri Masauni Awapa Onyo Kali Wanaotishia Kuandamana April 26

$
0
0
 Waziri Masauni Awapa Onyo Kali  Wanaotishia Kuandamana April 26
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amejitosa sakata maandamano linalosambaa katika mitandao ya kijamii, kwa kuwaonya wanaotishia kuandamana kwa kusema kuwa vyombo vya ulinzi na usalama viko imara.

Masauni ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Machi 15, jijini Dar es Salaam wakati akipokea vituo sita vya polisi vinavyohamishika vilivyotolewa na kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni.

“Kuna watu wako ndani ya nchi na wengine nje ya nchi wanaotaka kukwamisha ajenda ya maendeleo watupeleke kwenye ajenda zisizo za msingi.

“Utasikia mwingine anasingizia polisi kuwa katekwa kumbe kajiteka mwenyewe, mwingine anataka watu waandamane, yaani watu waache kutumia fursa zilizopo kwa mfano jana Rais kazindua reli ya umeme ambayo mimi nilikuwa naiona Ulaya leo inajengwa Tanzania, waache  kutumia fursa za viwanda vinavyoibuka kwa wingi kama uyoga eti wakaandamane.

“Ninachoweza kuwahahikikishia ni kwamba vyombo vyetu viko imara,” amesema Masauni.

Lissu Amewekewa Chuma Katika Mguu Wake

$
0
0
 Lissu Amewekewa Chuma Katika Mguu Wake

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amewekewa chuma katika mguu wake wa kulia ili kuimarisha mfupa wa paja.

Rais huyo wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) jana Machi 14, 2018 alifanyiwa upasuaji wa mguu wa kulia kama alivyoshauriwa na madaktari wa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven, Gasthuisberg nchini Ubelgiji.

Akizungumza leo na Mwananchi Machi 15, 2018, Lissu amesema operesheni hiyo iliyochukua saa mbili ilifanywa na timu ya madaktari bingwa chini ya uongozi wa Profesa Willem-Jan Mertsemakers.

“Operesheni ilienda vizuri na kwa sasa naendelea na dawa na mapumziko hospitalini kwa muda wa angalau wiki tatu zinazokuja,” amesema Lissu.

 “Wameniwekea chuma cha kuimarisha mfupa wote wa paja la kulia. Pia wamechukua vipimo ili kuangalia kama hakuna tatizo la bacteria kabla hawajafunga kabisa sehemu ya kwenye goti ambayo haijaunga hadi sasa.”

Mke wa Lissu, Alicia amesema anamshukuru Mungu kwamba upasuaji huo umekwenda vyema.

Mwanza Yatajwa Kinara kwa Watumishi wa Ndani

$
0
0
Mwanza Yatajwa Kinara kwa Watumishi wa Ndani

Mikoa ya Kagera na Mwanza imetajwa kuwa vinara kwa wenyeji wake ambao ni watoto wenye umri chini ya miaka 14 kufanya kazi za ndani maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya mikoa hiyo.

Hayo yameelezwa jijini Mwanza leo Machi 15 na mjumbe wa sekretarieti ya kuzuia na kupambana na biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu, Ahmad Mwen-dadi wakati wa mafunzo maalumu kwa watekelezaji wa sheria za kupambana na usafirishaji wa watoto kwa ajili ya kazi za majumbani maeneo ya mijini.

Amewaeleza  wajumbe wanaohudhuria mafunzo hayo yanayoratibiwa na Shirika la Kutetea Haki za Wanawake na Watoto la Kiwohede, kuwa baadhi ya watoto wanaosafirishwa kwenda mijini kufanya kazi za ndani hujikuta wakifanyiwa vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na waajiri wao au ndugu wa familia wanakofanya kazi.

Mikoa mingine yenye idadi kubwa ya watoto wanaosafirishwa kwenda mijini kufanya kazi  kwa mujibu wa Mwen-dadi ni Dodoma, Tanga, Kilimanjaro na Dar es Salaam. 

Mafunzo hayo kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwohede, Justa Mwaituka yanahudhuriwa na askari polisi kutoka dawati la jinsia, watendaji wa idara ya mahakama, ofisi ya Mwanahseria Mkuu wa Serikali, Idara ya Uhamiaji, maofisa ustawi wa jamii na maofisa kutoka Tume ya Usuluhishi na Uamuzi.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images