Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Hizi Hapa Faida Zitokanazo na Kucheka

$
0
0

Bila shaka umewahinkusikia mtu akisema, wach nicheke niongoze siku za kuishi. Kama umewahi kusikia nataka nikuongezee kitu ya kwamba wataalam wa saikolojia wanasema kuwa kucheka au kufurahi ni moja ya tiba kwa afya ambayo huifanya miili yetu kubaki na afya bora zaidi.

Naomba leo nikwambie haya mambo kadhaa ambayo utayapata endapo utakuwa ni mtu wa kucheka na kufurahi.

1. Kwanza kabisa kitendo cha kucheka au kufurahi husaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza msongo wa mawazo na kumfanya mhusika kuwa vizuri kiakili.

2. Husaidia kuimarisha afya ya mapafu
Unapocheka husaidia mapafu yako kutanuka na kuingiza ndani hewa ya safi yaani oxygen. Hivyo unapocheka zaidi tambua kuwa unasaidia kiwango cha hewa kuingia cha kutosha ndani ya mwili na kusaidia damu kusambaa vyema mwilini.

3. Husaidia kuboresha utendaji kazi wa moyo
Kitendo cha kucheka au kufurahi husaidia kukuweka mbali dhidi ya shinikizo la damu la kushuka, kwa sababu husaidia kuongeza mzunguko wa damu mwilini na pia kusaidia mishipa ya damu kutenda kazi vizuri.

4.Huboresha kinga za mwili
Kucheka ni muhimu kwani husaidia kuongeza homoni za hisia ndani ya mwili. Kutokana na mabadiliko hayo huenda.

Hizo ni faida chache kati ya nyingi ambazo mtu akiwa nazo sinamsaidia pia hata kuishi miaka mingi.


Bila Uvumilivu Mapenzi Yatakushinda Kila Siku, Kuwa Makini Katika Hili

$
0
0

Ukiwa mtu wa kuangalia mambo kwa juu juu basi kila kitu kwako kitakuwa kigumu. Kusoma unaweza kuona ni kugumu, kufanya kazi kugumu, hata kusubiri mshahara unaweza kuona ni kugumu.

Urahisi kwako unaweza kuwa katika kutumia pesa, pengine  na kula tu. Ila watu waerevu na wenye uvumilivu kwako kila kitu kinaweza kuwa tofauti na wewe.

1. Unachoona kigumu kwao wanahisi si ugumu bali ni changamoto za kuzidisha jitihada na umakini tu. Kwenye mapenzi pia hali haiko tofauti sana. Wale wanao achana kila siku si kama ndiyo wanakosewa sana kuliko wale ambao hawaachani, hapana. Suala ni lile lile tu.

2. Wakati wengine wakiona tofauti zao ni kama changamoto za kusomana tabia na kuamua kuishi kutokana na kila mmoja kumjua mwenzake. Wenzao wanaona suluhisho la yote ni kila mmoja kuwa na maisha yake. Suala la uvumilivu kwao hamna.

3. Hakuna mapenzi duniani yanayoweza kushamiri bila suala hili. Usipokuwa na moyo wa uvumilivu katika mapenzi basi kila mtu utamuona hafai. Utamuona hafai na kila siku utakuwa mtu wa kuanzisha mahusiano mapya. Hayo si maisha sasa!

4. Mahusiano yaliyodumu si kwa kuwa wahusika hawakoseani au makosa wanayokoseana ni madogo sana. Hapana. Kila binaadamu ana mapungufu yake. Wote huwa wanakoseana ila tofauti yake na wengine ni kwamba busara na uvumilivu huwa msingi wa mapenzi yao na ndiyo maana tunaona wanadumu mpaka leo.

5. Ni binaadamu gani unaweza kuishi naye na msikosane? Ni nani mwenye uwezo wa kukupa unachotaka kila siku? Hakuna binaadamu wa aina hiyo.

6. Hivyo unavyotaka kuachana na uliye naye suala la kujiuliza ni kuwa mara ngapi umemueleza kuhusiana na suala unalotaka kumuachia. Na hiyo isitoshte tu pia jiulize ni sababu gani inayomfanya kutenda suala hilo. Ukimaliza hapo rudi nyuma na jiulize tena huwa unatumia maneno ya aina gani katika kumkanya.

7. Maana wengine baada ya kukosewa wao huwa hawawakanyi vyema wenzao wao bali huripuka kwa maneno makali na dharau. Matokeo yake sasa wahusika badala ya kuwasikiliza na kufanyia kazi maneno wanayoambiwa kutokana na makosa yao. wao huwapuuzia na kwaona ni wasema hovyo.

8. Ndiyo, kukosewa kunaumiza sana ila jiulize ni kitu gani kimetokea bila sababu? Kwenye makosa ya mpenzi wako kuna sababu nyuma yake, hebu itafute badala ya kulalamika.

9. Mapenzi yasiyo kuwa na uvumilivu ndani yake hayana maisha marefu. Kwa sababu binaadamu ni kiumbe mwenye kukosea.

10 Badala ya kukimbilia kuachana ebu geuka kuwa mwalimu wa mpenzi wako angalau kwa mara chache.

11. Mpenzi wako ni furaha yako kwa maana ndiyo mtu uliyeridhia naye kuwa naye katika masuala nyeti yahusuyo maisha yako. Sasa kwanini uwe tayari kumpoteza kisa kachelewa kurudi.

12. Kuwa mvumilivu . Watu wenye hekima ni wavumilivu. Watu wenye kujielewa ni wavumilivu.

13. Ukiwa hauna uvumuilivu kila siku utatangaza ndoa. Leo utaachana na Mugambara kwa sababu anaongea sana na wasichana ila, jua huyo unaeenda kuwa naye anapenda sana kitu ambacho hukipendi. Anakunywa pombe je, utawezana naye? Jibu unalo.

14. Kwa kuwa huyo uliye naye unampenda kwa dhati basi amua kwenda naye taratibu ukijitahidi kumbadilisha tabia zake. Usiogope, inawezekana, suala ni uvumilivu na kujiamini tu. Kukubali kumpoteza unayempenda kwa kukosa uvumilivu ni kujitakia kuingia katika maisha ya kutanga tanga tu.

15. Kumbuka, siku zote wanaovumilia ndiyo huwa wanabaki na ushindi.Bila uvumilivu Mandela asingekuja kuwa raisi wa afrika kusini.Uvumilivu ni kila kitu katika maisha.

Hivi ndio Vigezo Wanavyotumia Wanawake Kupenda

$
0
0

Watu wengu hujisikia vizuri wanapowavutia wenzao wa jinsia nyingine. Je, unafikiri ni kitu gani kinachomfanya mwanamke aonekane wa kuvutia?

Kuna vitu vingi vinavyojulikana vizuri zaidi kwa upande wa mwanamke kama vile; mwili mzuri, sauti yenye mvuto, nywele, mikono mizuri na mengineyo mengi. Lakini, kuna vingine ambavyo siyo vya kawaida vinavyohusu mwanaume kumvutia mwanamke.

Je, ni vitu au mambo gani ya kipekee ambayo, humfanya mwanamke aguswe na mwanaume fulani na huku mwanamke mwingine akishangaa ni kwa nini mwanamke mwenzake ameguswa sana na huyo jamaa?

Inawezekana yapo mengi ambayo, huyajui. Kwa mfano, mwanamke anaweza akavutiwa na jina la kwanza au la ukoo la mwananume fulani. Hapa mwanamke hufikiri kwamba, huyo mwenye hilo jina hawezi kuwa mtu wa kawaida, na kila kitu anachofanya ni lazima kiwe cha ajabu.

Labda ni kutokana na jina hilo kuwa ni la kigeni au anatoka kwenye ukoo ambao ni bora au wa kipekee au anafikiri labda huyo mwanaume atamwezesha kile ambacho, mara nyingi amekuwa hakipati.

Lakini, inawezekana kabisa kwamba, mwanamume huyo si mzuri sana wa kuvutia au ni mbaya sana kuliko wengine. Hakuna anayejua, labda anachotaka mwanamke huyo ni kujaribu bahati yake ili aone kitakachotokea kwa uhakika ziadi.

Inawezekana pia kuwa, mwanamke anaweza kuchanganyikiwa zaidi baada ya kuona umbo la mwanamume huyo au gari lake. Pengine mambo hayo ndiyo ambayo, amekuwa akiyapenda zaidi. Inawezekana ikawa ni dalili ya bahati kwake kwamba, ametokea katika maisha yake mtu ambae, kwa muda mrefu amekuwa akitamani kumpata.

Upo uwezekano pia kwamba, mwanamke akavutiwa na mwandiko au sahihi ya mwanamume fulani. Wakati mwingine mwanamke hutokea kuwa na uhakika zaidi na kuamini yale anayoambiwa kuhusu tabia ya mwanaume huyo, bila hata kufanya uchunguzi wa kina. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, upo uwezekano wa kuisoma tabia ya mwanaume huyo kwenye sahihi au mwandiko wake.

Mwanamke pia huvutiwa na lafudhi ya mwanamume, fani yake, hobi, na kitu kingine kisicho cha kawaida ambacho mwanamume huyo anakipenda na kukifanya. Hata hivyo, mwanamke anatakiwa awe mwangalifu mno na upande wa pili wa mtu huyo ambao, yeye haujui. Hapa ikiwa na maana kuwa , pamoja na sifa zote hizo alizozibaini kutoka kwake, anapaswa kujua kwamba, mwanamume huyo kama binadamu asiyekamilika pia ana mapungufu na udhaifu mwingi.

Kuufahamu ukweli huu, kutamsaidia katika kuimarisha zaidi na kumfanya awe makini anapotafuta mwanaume wa kuishi naye. Na akumbuke kuwa, wapo wanaume ambao huficha makucha yao au kasoro zao kwa wapenzi wao.

Kuna mwanamke mwingine hupenda mwanaume mwenye vituko, kilema au mwenye kasoro nyingine za kimwili. Yote hayo hutokana na asili ya mwanamke. Na ni mambo yanayoongea ndani mwake kwamba, anataka kumjali na kumhurumia mwanaume huyo.

Kwa kawaida, mwanamke huvutiwa zaidi na kwa urahisi, pale mwanaume anapoonyesha tabia ya usikivu na utulivu. Hata hivyo, mtazamo huu kwa upande wa mwanamke, huhesabika kuwa ni ushindi kwake.

Hali kadhalika, mwanamke huvutiwa na tabia fulani ya kipekee ambayo, mwanaume anayo. Kwa mfano, jinsi mwanaume huo anavyoutumia mkono wake wa kushoto, kwani watu wengi wanatumia mkono wa kulia. Ukweli ni kwamba, labda huyo ndiye mwanaume ambae mwanamke huyo anamtaka, kwani pia wanawake wengine hawawezi kujizuia kuwapenda wanaume wenye macho ya bluu. Hilo pia ni jambo la kawaida.

Mwanamke anaweza kumpenda mwanaume kutokana na jinsi anavyofanya kazi za nguvu au kutokana na mwili wake kuwa na misuli. Ni jambo la kawaida kwa wanawake kufurahia wanaume waliojazia, na inavyoonekana wanawake huwaona wanaume ambao ni lainilaini kuwa wana haiba ya kike au ni mashoga.

Hapo ndipo mwanamke anapolazimika kufikiria kwa makini, kuhusu mwanaume anayetumia muda mwingi kujipodoa na fedha nyingi kwa mambo ya urembo na vipodozi kuliko hata mwanamke, kama kweli anamvutia na anamfaa.

Na kitu kingine ni kwamba, mwanamke humpenda mwanaume anayesaidia kufanya kazi za nyumbani. Kwa kufanya hivyo, mwanamke huamini kwamba, mwanaume huo anamjali na kumthamni.

Kwa kumalizia ni kwamba, mambo mengi yanayomchanganya mwanamke kuhusiana na mwanaume anayemtaka, kwa kweli ni ya kipekee sana na wakati mwingine huonekana kuwa ni kituko, ingawa wakati mwingine yanaweza yakaeleweka vizuri. Mara nyingi vigezo hivyo huonekana kuwa sahihi, iwapo tu mwanamke huyo atajisikia vizuri na kupata ridhiko la nafsi yake.

Mchungaji Moshi Akamatwa na Polisi Kwa Kudaiwa ni Mchochezi wa Kisiasa

$
0
0

MOSHI, KILIMANJARO: Mchungaji Fredy Njama wa Usharika wa Karanga, KKKT Dayosisi ya Kaskazini, amekamatwa na Polisi kwa kinachoidaiwa kuwa ni “Uchochezi wa kisiasa”.

Mchungaji huyo wiki mbili zilizopita alisoma ripoti katika mkutano mkuu wa mwaka wa usharika wake ambayo ndo imepelekea kukamatwa kwake.

Katika ripoti hiyo, alibainisha kuwa mapato ya usharika yanapungua kwa sababu mbalimbali

Katika utangulizi wa ripoti alitaja changamoto 6 zinazoikabili nchi kwa sasa: Ukosefu wa ajira kwa vijana, Hali ya uchumi inayoyumba, Hali ya kisiasa ni ya mashaka, Gharama kubwa za matibabu, Sera ya elimu bure na Wastaafu kutolipwa mafao yao

Ripoti hiyo pia imechapwa ktk kijitabu na kiwanda cha uchapaji cha Dayosisi hiyo

Kundi la Polisi na maafisa usalama walimchukua Ijumaa asubuhi hadi kiwandani na kumtaka akusanye vijitabu vyote hadi vilivyosambazwa na kuvikabidhi Polisi. Aidha walimtaka aandike barua kuomba radhi na kufuta ripoti hiyo

Jioni ya leo, Polisi walifika ofisi ya usharika na kufanya upekuzi. Walichukua laptop na flash. Kisha walimpakia mchungaji katika gari lao na kuondoka naye.

Ni Simanzi na Majonzi Ibada ya Mazishi ya Mmiliki wa Mabasi ya Super Sami Aliyeuawa na Kutupwa Mtoni

$
0
0
Vilio, simanzi na majonzi vimetawala kwa  waombolezaji kutoka jijini Mwanza na maeneo jirani wanaendelea na ibada ya mazishi ya mfanyabiashara Samson Josia yanayofanyika nyumbani kwake mtaa wa majengo mapya wilaya ya Magu mkoani Mwanza.

Mwili wa mfanyabiashara huyo uliokutwa ukiwa umefungwa kwenye viroba ukielea ndani ya Mto Ndabaka mpakani mwa wilaya za Bunda mkoa wa Mara na Busega mkoani Simiyu umewasili asubuhi ya leo Machi 16 ukitokea Hospitali ya Rufaa Mara ulikohifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi tangu juzi.

Tangu asubuhi, mamia ya waombolezaji kutoka jijini Mwanza na maeneo jirani wamekuwa wakimiminika nyumbani kwa marehemu wakitumia mabasi ya kampuni aliyokuwa akimiliki.

Mabasi ya kampuni nyingine pia yanatumika kusafirisha waombolezaji kutoka jijini Mwanza bila malipo.

Marehemu Josia aliyezaliwa mwaka 1968 alipotea tangu Februari 27 kabla ya gari lake kukutwa likiwa limeteketezwa kwa moto ndani ya eneo  la hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara Machi 9.

Ibada ya mazishi inaongozwa na Mchungaji Jackson Meza kutoka Kanisa la African Inland Church of Tanzania (AICT) huku kwaya ya kanisa ambayo marehemu alikuwa mfadhili wake ikiimba nyimbo za maombolezo.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Jaffari Mohamed, watu wanne wanashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano kuhusiana na kifo hicho kilichoibua hofu na maswali yasiyo na majibu miongoni mwa ndugu, jamaa, marafiki na wakazi wa jiji la Mwanza ambako marehemu alikuwa akiendesha shughuli zake za kibiashara.

Paul Makonda Awaomba Msamaha Wananchi

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Mh. Paul Makonda amefunguka na kuwaomba msamaha baadhi ya wananchi ambao ameshindwa kutimiza ndoto zake na kusema anaamini ataendelea kuwatumikia na kujitahidi kuweza kugusa maisha ya kila mmoja.

Paul Makonda amesema hayo siku mbili baada ya kutimiza miaka miwili toka ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kusema kuwa ndani ya miaka miwili akiwepo madarakani anaamini amegusa maisha ya watu kwa kutumia kipaji chake, uwezo wake wote.

"Asante Mungu kwa neema zako, kama usingekuwa upande wangu na Dunia iseme sasa. Nawashukuru sana sana watumishi wenzangu Kwa kunivumilia na kunielewa katika kutimiza majukumu yangu. Zaidi nawashukuru sana wananchi naimani nimejitahidi kuwatumikia Kwa moyo wangu wote na vipaji vyote na pale niliposhindwa kutimiza ndoto yenu mnisamee"

Makonda aliendelea kufafanua na kutoa ahadi yake kwa wananchi kuwa

"Zaidi nawaahidi nitaendelea kujituma zaidi ili niyaguse maisha ya kila mmoja wetu kama ambavyo Serikali ya awamu ya 5 inavyokusudia. Mwisho si kwa umuhimu ni Kwa wadau wa maendeleo naomba mfahamu kila cent mliyoitowa ina thamani kwangu na kwa wananchi wangu. Tumefanya Mambo mengi na hakika na tumegusa na hata kuleta faraja Katika maisha ya Watu wengi. Kwakutambua mchango wenu ninaandaa siku ya kuwatambua na kuwatunuku tuzo kama asante yangu kwenu"

Machi 13,  2016 Paul Makonda aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam

TFF Wajibu Hoja za Michael Wambura Aliyefungiwa Kushiriki Mambo ya Mpira Maisha

$
0
0
Shirikisho la soka nchini TFF limejibu tuhuma zilizotolewa na makamu wa rais wa shirikisho hilo Michael Richard Wambura, baada ya hukumu ya kufungiwa maisha kutangazwa dhidi yake na kamati ya maadili inayoongozwa na mwenyekiti Hamidu Mbwezeleni.

Wambura alizungumza na waandishi wa habari kupinga hukumu iliyotolewa dhidi yake, huku akiweka wazi  baadhi ya mambo ambayo anaamini yamekua mzizi wa yeye kufanyia figisu hadi kuingizwa hatiani.

Mdau huyo wa soka alidai kuwa, kuna mambo mengi yanaendelea ndani ya TFF likiwepo suala la ubadhilifu wa fedha, ambao umekua kinyume na utaratibu, jambo ambalo aliahidi kulitafutia siku la kulianika hadharani kupitia vyombo vya habari.

TFF imejibu tuhuma hizo kwa kutoa ufafanuzi wa kina katika kila kipengele ambacho kilizungumzwa na Wambura alipokutana na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.


1.Matumizi mabaya ya fedha za TFF
JIBU : Wambura kama Mwenyekiti wa kamati ya fedha amehudhuria vikao zaidi ya 4 vya kamati na hajawahi kulalamika kokote mpaka amefungiwa.

Bajeti ya TFF iliyopitishwa Dodoma kwa Mwaka Mzima ni Bilioni 8.6 hivyo matumizi anayosema ya Bilioni 3 kwa miezi 7 yanaonyesha jinsi gani TFF inavyopambana na changamoto za kifedha hivyo kuhakikisha inapunguza matumizi.

Mapato yaliyopatikana kwa miezi Saba (7) iliyopita yalitumika katika maeneo yafuatayo :

Timu ya Taifa Taifa stars(Fifa dates),Kilimanjaro Stars  (Challange Cup),Kambi kwa Timu ya Taifa Under23, Kambi U20, U16, Wanawake U20, Ligi za Wanawake, Kombe la Shirikisho la Azam, kozi za makocha,kozi za waamuzi za nje na ndani, vikao vya kamati ya utendaji na  kamati ndogo ndogo, mishahara ya watumishi wa TFF na makocha wa timu za Taifa, kulipa madeni tuliyoyakuta na kuidhinishwa na kamati ya fedha, kozi za Grassroots na Live Your Goal na soka la Ufukweni

2.Ajira za TFF watu kupewa kwa kujuana.
JIBU : TFF haijawahi kuajiri nafasi yoyote ile zaidi ya Wakurugenzi 3 na meneja 1 tofauti na uongo unaozungumzwa,Wakurugenzi walioajiriwa ni Mkurugenzi wa Fedha,Mkurugenzi wa Mashindano,Mkurugenzi wa sheria na Wanachama na Meneja Masoko,katika kupunguza matumizi ya fedha Taasisi imebaki na Wafanyakazi 21 kutoka 44 wa awali waliokutwa na Ndugu Karia.

3.Kumteua Wilfred Kidao kuwa kaimu Katibu Mkuu wa TFF.
JIBU : Kaimu Katibu Mkuu alikaimishwa na Kamati ya Utendaji na yeye Wambura akiwa mmoja wa waliompitisha.

4.Mipira 100 kila mkoa kwamba kuna watu wamepiga fedha za TFF.
JIBU : TFF chini ya Rais wa TFF aliyekuwepo madarakani Ndugu Wallace Karia haijawahi kununua mipira,mipira iliyotolewa ilinunuliwa na uongozi uliopita ilichofanya TFF ni kuigawa kama ilivyofanya.

5.Kuwa na wafanyakazi wawili kwenye nafasi moja.
JIBU : TFF haijawahi kuajiri mfanyakazi zaidi ya mmoja kwenye nafasi moja,wengi waliokuwepo kwenye Shirikisho kwa sasa wanajitolea akiwemo Afisa Habari.

6.Suala la Waamuzi kuondolewa kuchezesha ligi kuu.
JIBU : Ili kuongeza ubora wa uchezeshaji TFF ikaamua kuchaguwa waamuzi wa juu(Elite) tofauti na awali ambako kulikuwa na idadi kubwa mchanganyiko ya waamuzi.

7.Kaimu Katibu kutuma majina ya Makamishina.
JIBU : Jina la Michael Wambura na Ahmed Mgoyi ndio yaliyopelekwa kama utaratibu unavyotaka ya kujaza kwenye fomu moja pekee na TFF haikuwahi kubadilisha wala kukata jina la mtu yeyote.

8.TFF ya sasa mpaka uwe na urafiki na watu 3 Karia, Mgoyi, na Nyamlani.
JIBU : TFF haiendeshwi kwa urafiki bali kwa utaratibu wenye kufuata kanuni.

Kikao kilichotoa maamuzi ni Kamati inayojitegemea (Independent) sio rahisi kuingiliwa kwa kuwa hata Rais wa TFF hawezi kuiingilia

Kumekuwa na upotoshaji mkubwa unaoenezwa kwa maslahi binafsi,ni vyema watu wakajikita kwenye kujibu tuhuma zao bila kuhusisha uongo na vitu visivyo vya kweli kwa Taasisi ambayo kwasasa ipo makini kwenye kuhakikisha kila kitu kinafuata utaratibu ikiwemo masuala ya kifedha pamoja na mambo mengine.

Imetolewa na Idara ya Habari na Mawasiliano TFF

Wema Sepetu Uvumilivu Umemshinda, Ashika Watu koo..'Nina Mdomo Mchafu Hasa ila Najitahidi Kujisitiri'

$
0
0
Muigizaji wa filamu mwenye nyota yake bongo na Afrika Mashariki Wema Sepetu, amedai amevumilia matusi vya kutosha anayotukanwa na kupitia mitandao ya kijamii bila kosa lolote hivyo kwa sasa ataenda nao hatua kwa hatua.


Wema Sepetu ametoa kauli hiyo alasiri ya leo (Machi 16, 2018) baada ya baadhi ya watu kupenda kumtolea maneno machafu na kumdhihaki kwa jambo ambalo yeye hakupenda awe nalo au limfike katika maisha yake.

"Naona mmeshanikariri hua nakaa kimya pale mnapo ona 'comment' ya matusi, nimepuuzia kwa muda mrefu mno ila tukumbuke kuwa na mimi nina moyo ambao una nyama tena ni binadam kama nyie tu. Kama vile usivyopenda kuona mtu anakukebehi basi ndio hivyo hivyo ninavyo 'feel', kwani lazima matusi?, hakuna asiyejua kutukana kwenye ulimwengu huu tena midomo michafu haswa ila tunajitahidi kujistiri", amesema Wema.

Aidha, Wema Sepetu amesema hakuna jambo ambalo linamkera kupita kiasi kama kuona anatukanwa kupitia 'social media' tena kwenye ukurasa wake mwenyewe.

"Kwani kuna ulazima ku-coment tena matusi 'sometimes' mtu anaweza 'ku-push ur buttons to the extent when it comes to me nina extents' zangu 'and u don't go there', navumilia vingi mno jamani kweli kweli. 'Try putting yourselves in my shoes for a minute and see if they fit'. Ukipost kitu chako kuna ile mijitu iliotapikwa inakuja na maneno yao ya chooni utasema imetumwa. Kwani ni mashindano?, sio poa jamani", amesisitiza Wema.

Kwa upande mwingine, Wema Sepetu amewakumbusha baadhi ya watu wenye tabia hiyo kuwa naye ni binadamu kama walivyo wao na mwenye moyo wa nyama na wala sio chuma hivyo anasikia maumivu makali kama wayapatao wao pindi wakitukanwa katika mitandao ya kijamii.

Pata Dawa za Kupunguza Uzito wa Mwili Ambazo Hazina Madhara

$
0
0
NI VIRUTUBISHO,
NI CHAKULA MBADALA
ZIMEHAKIKIWA NA TFDA
Ni uhakika kwa afya yako, kupunguza uzito na sumu mwilini, Mafuta/Sehemu mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbalimbali kwa msaada wako mfuate:

Instagram Napatikana kwa Jina la:
@my_health_my_wealth

Mtext WhatsApp +255783 566844 Or
DM /upate suluhisho la afya yako KARIBU

Pia Kama unataka Kuwa Mfanyabiashara wa Dawa Hizi Nicheki

Mimi Zimenisaidia kama unavyoona kwenye picha:


Nyota ya Wastara Yang'aa Apata Shavu Sweden

$
0
0
Wastara Apata Shavu Sweden
STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma ambaye hivi karibuni alikuwa nchini India kwa matibabu, baada ya kurudi Bongo na kupata nafuu amelamba shavu la kwenda nchini Sweden kuwakilisha wanawake walemavu wa Kiafrika.



Akiongea na Risasi Jumamosi juzi, Wastara alisema kuwa baada ya kutua nchini akiendelea na matibabu alipata mwaliko wa kwenda Sweden kwa ajili ya kuwawakilisha wanawake walemavu baada ya kuchaguliwa na Jumuiya ya Wanawake Afrika yenye makao yake makuu nchini Swenden akiwa kama balozi wa wanawake kutoka Tanzania.

“Nimelazimika kwenda kwa sababu hakuna mwanamke mwenye historia kama ya kwangu na wamenihakikishia kuwa nitakuwa salama kuanzia kwenye safari mpaka huko kwani bado nipo kwenye matibabu,” alisema Wastara



Mbali na safari hiyo, Wastara pia amezindua wimbo wa kuwashukuru Watanzania wote waliomchangia pesa za matibabu ambao umeimbwa na msanii ‘anayemmeneji’ aitwaye Kea.

“Nimeamua kuwashukuru Watanzania kwa kutumia mashairi ikiwa ni pamoja na kuwaburudisha lakini kubwa ni kuwashukuru kwani leo hii nilivyo ni kwa sababu ya wao, bila kumsahau Rais Magufuli,” alisema Wastara. Wastara alikwea pipa juzi kuelekea Sweden ambapo atakaa kwa siku chache.

Maneno ya Mstaafu Kikwete kwa IGP Sirro ‘Watanzania Ninaowapenda’

$
0
0
Maneno ya Mstaafu Kikwete kwa IGP Sirro ‘Watanzania ninaowapenda’Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro kwa kuwakamata watu waliokuwa wanatumia vibaya jina lake kwa kufanya utapeli mtandaoni na kuwaibia watu fedha.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Dr. Jakaya Kikwete ameandika >>>Natoa pongezi nyingi kwa IGP Simon Sirro na @tanpol kwa kuwakamata watu waliokuwa wanatumia vibaya jina langu, la mke wangu Salma na mwanetu Ridhiwani kuwahadaa na kuwaibia Watanzania ninaowapenda sana. Kubainika kwa mtandao huo na kukamatwa ni hatua nzuri ya kupongezwa.

Jakaya Kikwete

@jmkikwete
Natoa pongezi nyingi kwa IGP Simon Sirro na @tanpol kwa kuwakamata watu waliokuwa wanatumia vibaya jina langu, la mke wangu Salma na mwanetu Ridhiwani kuwahadaa na kuwaibia Watanzania ninaowapenda sana. Kubainika kwa mtandao huo na kukamatwa ni hatua nzuri ya kupongezwa.

5:11 PM - Mar 16, 2018
1,348
353 people are talking about this

Msukuma Asema Wametishwa na Kifo cha Mmiliki wa Mabasi

$
0
0
Msukuma Asema Wametishwa na Kifo cha Mmiliki wa Mabasi
Wamiliki wa mabasi mkoani Mwanza, wamesema kwamba wameingiwa na hofu ya usalama wa maisha yao baada ya mwenzao Samson Josia kupotea katika mazingira ya kutatanisha na baadaye mwili wake kukutwa ukiwa umefungwa kwenye viroba na kutupwa ndani ya Mto Mandaka.

Akizungumza jana kwa niaba ya wenzake wakati wa ibada ya mazishi ya mmiliki huyo mabasi ya Super Sammy iliyofanyika nyumbani kwa marehemu Mtaa wa Majengo Mapya mjini Magu, mmiliki wa mabasi ya Msukuma, Joseph Kasheku ‘Msukuma’ alisema tukio hilo limewafanya wajihisi kuwa yeyote miongoni mwao anaweza kufuata kutekwa na kuuawa.

“Wamiliki na wafanyabiashara wa mabasi tumejawa hofu kwa tukio lililomkumba mwenzetu; hatujui nani anafuata baada ya Super Sami. Tunaomba uchunguzi wa kina ufanyike kuwabaini na kuwatia mbaroni waliohusika,” alisema Msukuma ambaye pia ni mbunge wa Geita Vijijini

Akitoa salamu za Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa), Ofisa Habari wa chama hicho, Mustapher Mwalongo licha ya kukabidhi ubani wa Sh3 milioni kwa familia ya marehemu, alisema Taboa itashirikiana na vyombo vya dola kuhakikisha wahusika wanakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Pia, Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo Mapya, Renatus Ng’hula alisema mauaji ya aina hiyo yanachafua haiba na taswira ya Taifa, “Tumekuwa tukisoma na kuona matukio haya kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii; leo imefika kwetu kwa mtu tuliyemtegemea kwenye masuala mengi ya kiuchumi na maendeleo.”

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya mazishi, kiongozi wa ukoo wa Mzuri, Yusufu Kijika alisema wauaji licha ya kumchinja marehemu, pia walikata na kutenganisha na kiwiliwili miguu yote miwili.

Alisema ingawa bado uchunguzi unaendelea, wanahusisha mauaji hayo na madeni ambayo marehemu alikuwa akiwadai watu mbalimbali walioshindwa kurejesha, “Tunahisi ukaribu na moyo wake wa kusaidia wengine kupitia mikopo ndicho kimemponza; marehemu alikuwa hadaiwi na mtu, bali yeye ndiye alikuwa akiwadai aliowakopesha.”

Alisema saa chache kabla ya kutoweka, Samson alimpigia simu mmoja wa wake zake, Stumai Magembe akimwagiza kuandaa chakula cha kutosha na sehemu ya kulala wageni aliosema angefika nao kwenye mji wake mwingine ulioko jijini Mwanza.

“Kwa mujibu wa Stumai, simu hiyo alipigiwa saa 3:45 usiku wa Februari 27; lakini baada ya simu hiyo, marehemu hakuonekana wala kupatikana kwenye simu hadi mwili wake ulipokutwa Mto Ndabaka siku tano baada ya gari lake kukutwa likiwa limeteketezwa kwa moto katika Hifadhi ya Serengeti,” alisema

Alisema familia ilifanya jitihada na kubaini kuwa wakati anapiga simu usiku huo, alikuwa eneo la Buzuruga jijini Mwanza na kwamba mawasiliano ya mwisho yalionekana akiwa hifadhi ya Serengeti.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Jaffari Mohamed alisema jana kuwa watu wanaoshikiliwa kwa mahojiano kuhusu tukio hilo imefikia watano baada ya mwingine kuongezeka juzi jioni.

Katika tukio lingine, mmoja wa waombolezaji waliokuwa msibani hapo, alitiwa mbaroni na baada ya ndugu wa marehemu kumtambua kuwa alifika nyumbani hapo siku ambayo Samson alipotea akimuulizia na kuondoka bila kueleza alichokuwa akimtafutia licha ya kuulizwa.

Mwili wa mfanyabiashara huyo ulikutwa ndani ya mto siku tano baada ya gari yake ndogo aina ya Toyota Land Cruiser kukutwa ikiwa umeteketezwa kwa moto ndani ya eneo la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Baadaye mwili wake uliokotwa na wavuvi waliokuwa wakiendelea na shughuli zao ndani ya mto huo Machi 14.

Aunt Ezekiel Awatolea Povu Wanaomwita Mnafki Kisa Ushoga Wake na Wema Sepetu

$
0
0

Aunt Ezekiel Awatolea Povu Wanaomwita Mnafki Kisa Ushoga Wake na Wema Sepetu
Baada ya picha mpya kusambaa na kuonesha muigizaji Aunt Ezekiel akiwa karibu na Wema Sepetu, wafausi wa aliyekuwa mchumba wa Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wamemchachamalia Aunt kwa kumuita mnafiki hali iliyosababisha mrembo huyo aibuke na kutoa povu.



Akizungumza na Risasi Jumamosi hivi karibuni baada Zari kummwaga Diamond na yeye kuonekana ‘klozi’ na Wema, Aunt alisema wamuache na urafiki wake na Wema kwani yeye na Zari hawakuwa marafiki kama alivyo Wema.



“Sipendi kabisa watu wanavyoniongelea juu ya suala hilo la ukaribu wangu na Wema, waniache kabisa kwani sikuwa rafiki wa Zari na siwezi kumsema vibaya, Wema atabaki kuwa rafiki siku zote,” alisema Aunt.



Aunt alisema, kamwe hawezi kuhofia maneno ya watu kwani Wema atabaki kuwa rafiki yake bila kuangalia Diamond ana uhusiano na nani.

“Maneno ya watu hayawezi kuniweka mbali na Wema huu ni uamuzi wangu na siwezi kumtenga Wema kwa sababu nilikuwa karibu na Zari hayo ni mambo yao mimi hayanihusu,” alisema Aunt.

Hivi karibuni, Aunt na Wema walionekana kwenye pati ya Papii Kocha na Babu Seya iliyofanyika katika Ukumbi wa King Solomoni jijini Dar ambapo walivaa magauni sare na kucheza pamoja.



Kabla ya Zari hajammwaga Diamond, Aunt hakuwa akionekana mara kwa mara na Wema tofauti na sasa jambo ambalo ‘wambeya’ wengi mitandaoni wamekitafsiri kitendo hicho kuwa ni cha kinafiki baada ya hivi karibuni Aunt kuonekana karibu na Wema.

Rihama Afunguka Sababu ya Ubonge Wake

$
0
0
Rihama Afunguka Sababu ya Ubonge Wake
STAA wa filamu za Kibongo, Riyama Ally ameeleza sababu zilizomfanya anenepeane baada ya watu kumponda kwamba, amekuwa na ‘minyama uzembe’ hadi kaharibika.

Akifungukia unene wake huo, Riyama aliliambia Risasi Jumamosi kuwa amelazimika kunenepeana kwa sababu sasa hivi anacheza nafasi ya umama kwenye filamu mbalimbali hivyo ameona ili kuuvaa uhusika vizuri, ajiachie ili awe na muonekano wa kimama.

“SIWEZI kupungua kwa sasa hata iweje, iwapo nitapata kazi inayo­taka nicheze nikiwa nimepungua basi nita­fanya hivyo, lakini kwa sasa nimelipwa kuwa hivi nilivyo,” alisema Riyama.

Kunguni Wawatesa Wakazi wa Mbeya Waita Mganga wa Kienyeji Ili Kuwaondoa

$
0
0
Kunguni Wawatesa Wakazi wa Mbeya Waita Mganga wa Kienyeji Ili Kuwaondoa
WANANCHI wa Kata ya Igurusi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, wamechangishana fedha kwa ajili ya kumlipa mganga wa kienyeji ambaye walimuita ili awasaidie kuondoa kunguni katika makazi yao miongoni mwa wadudu wengine.


Mbali na kunguni, wananchi hao wamedai kuathiriwa na viroboto na chawa kwenye makazi yao wakiamini wadudu hao wamepelekwa hapo kishirikina.

Zoezi hilo hata hivyo limewagawa wananchi hao katika makundi mawili, baadhi wakiunga mkono na wengine kupinga kwa sababu ya imani za dini.

Mgongano huo umepelekea kuwapo kwa viashiria vya uvunjifu wa amani katika kata hiyo, kumfanya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla, kuingilia kati na kupiga marufuku zoezi hilo.

Makalla alisema yeyote atakayebainika kuliendeleza zoezi hilo atachukuliwa hatua za kisheria.

Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa na mkuu huyo wa mkoa jana, wananchi hao walidai kuwa waliamua kuchangishana fedha hizo na kumuita 'rambaramba' huyo baada ya kukithiri kwa matukio ya "uchawi".

Mmoja wa wakazi wa kata hiyo, Pilu Ibrahimu alisema wanashindwa kuishi vizuri kwenye nyumba kutokana na kukithiri kwa wadudu hao ambao hawajulikani walikotoka.

Alisema utitiri huo wa chawa, kunguni na viroboto uliwafanya kumuita mganga ili awasaidie kuwaondoa.

Alisema sangoma huyo aliitwa kwa nia njema na kwamba hakuna mtu aliyelazimishwa kuchanga fedha lakini zoezi likaharibika baada ya Mkuu wa Wilaya, Reuben Mfune, kupiga marufuku na kuagiza mganga huyo aondoke.

“Tunaomba turuhusiwe kuendelea na zoezi letu," alisema Ibrahimu. "Nyumba zetu zimejaa kunguni ambao hawafi kwa dawa yoyote ile.

"Rambaramba wetu alikuwa na msaada mkubwa maana walianza kupungua lakini baada ya kukatazwa tunaendelea kuumia.”

Naye Benard Mwambusi aliwatupia lawama wazee wa mila katika kata hiyo pamoja na viongozi wa dini kwa madai kuwa matukio mengi yamekuwa yakitokea lakini hawajawahi kukemea na kwamba ndiyo maana yanaendelea.

Alisema kumekuwa na matukio ya wanawake kuuawa wakiwa porini wanatafuta kuni na kisha kutelekezwa hukohuko pamoja na watoto kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Hata hivyo, akitoa tamko la serikali, Mkuu wa Mkoa Makalla alisema ni marufuku kwa mtu yeyote kuendeleza ushirikina katika kata hiyo na kwamba endapo watakamatwa sheria itachukua mkondo wake.

Alisema matukio kama hayo ni ya kuchonganisha watu na hivyo kuna uwezekano mkubwa wa kupotea kwa amani, hivyo akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa hawezi kukubali hilo litokee.

Makalla alisema hata kwa bahati mbaya hawezi kuruhusu watu kuamini uchawi katika mkoa wake hivyo akamwagiza Mkuu wa Wilaya hiyo kusimamia na kuhakikisha zoezi hilo haramu linaendelea.

“Mimi sasa hivi naelekea Dodoma kikazi, sasa nikiruhusu zoezi hilo ambalo ni kinyume na sheria za nchi sitafika hata Iringa, nitakuwa nimeshatumbuliwa na rais," alisema Makalla.

"Ni marufuku kuendelea... kila mtu apambane na hali yake.”

Tambo za Yanga, Simba Kujulikana Leo

$
0
0
 Tambo za Yanga, Simba Kujulikana Leo
NENO ‘tambo’ lina maana mbili. Kwanza ni jambo lililofumbika, jambo ambalo utatuzi wake haujulikani. Pili ni umbo kubwa aghalabu la mtu; jitu.

Maana zote mbili zazihusu Simba na Yanga ambazo zote zipo nnje ya nchi kwenye michuano miwili tofauti ya kimataifa. Naam, Yanga na Simba ni timu zilizoanzishwa zamani na ndizo zinazotambulika zaidi kimataifa.

Kwa mechi za kimataifa, mara nyingi Yanga imekuwa ikiondoshwa mapema, hasa na timu za Waarabu isipokuwa mara moja tu ilipofikia hatua ya nusu fainali.

Angalau Simba ilipata kutinga fainali lakini ikashindwa kutamba kwa timu ya Ivory Coast ilipofungwa mabao 2-0 mbele ya aliyekuwa Rais wa awamu ya Pili, Alhaj Alli Hassan Mwinyi jijini Dar Salaam na uvumi wa chini chini kuenea kuwa baadhi ya wachezaji ‘walinunuliwa’ na mfadhili fulani aokoe hela alizowaahidi wachezaji kama wangetwaa Kombe.

Hata hivyo kinachotakiwa si kufika nusu fainali au fainali yenyewe, bali ni kutwaa kile kinachoshindaniwa (Kombe).

Yanga itacheza na Township Rollers ya Botswana saa 10:45 leo jioni kwenye mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Mechi ya kwanza iliyochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, wageni kutoka Botswana waliiduwaza Yanga na mashabiki wao walipoifunga mabao 2-1.

Wakati Yanga wakicheza majira ya jioni, baada ya kuadhiriwa nyumbani, wenyeji wao watakuwa na ahueni kiasi kwa ushindi waliopata ugenini Dar es Salaam. Ni wazi kuwa Yanga watacheza kwa lengo la kupata ushindi wa haraka haraka ingawa wenyeji watacheza kwa kuzuia zaidi lango lao kutofikiwa na washambuliaji wa Yanga ili kulinda mabao 2-1 waliyopata jijini Dar es Salaam.

Simba wataingia uwanjani saa 2:30 usiku wa leo kupimana maarifa na wenyeji wao, Al Masry wa Misri jijini Cairo.

Ni mchezo utakaokuwa na ushindani wa vuta-nikuvute kutokana na timu hizo kufungana mabao 2-2 zilipokutana kwenye duru la kwanza jijini Dar es Salaam. Ilivyo ni kwamba Waarabu wana faida ya mabao mawili waliyofunga ugenini – Dar es Salaam – ingawa Simba nayo ilipata idadi kama hiyo.

Labda methali mbili zifuatazo zaweza kuwapa hamasa wachezaji wa Yanga na Simba ili wacheze kwa bidii na kuibuka na ushindi ugenini.

Mosi: “Mcheza hawi kiwete, ngoma yataka matao.” Matao ni mbwembwe na machachari. Maana yake mtu anayecheza ngoma hawi na kilema kwa kuwa uchezaji ngoma una machachari mengi.

Methali hii yaweza kuwanasihi wachezaji wa Yanga na Simba kuwa wadhamiriapo kupata ushindi, lazima wajitolee kufanya juhudi kubwa.

Hawapaswi kuwa na ulegevu au ajizi kwani ndiwo wanaoiwakilisha Tanzania. Ushindi wao ni sifa kwa Watanzania na nchi kwa jumla.

Pili: “Mcheza kwao hutuzwa.” Maana yake mtu anayecheza kwao hupewa zawadi au hutunzwa vizuri.

Hutumiwa kutufunza kwamba mtu anayefanya jambo lake vizuri au inavyopasa, hutuzwa au hupewa zawadi.

Hii ni tahadhari kwa Yanga na Simba kuwa zinapocheza nnje ya nchi, wananchi wa nchi hizo huzishangilia mno timu zao za nyumbani tofauti kabisa na sisi tunaozishangilia timu ngeni! Tahadhari hii yaihusu zaidi Simba kwani Waarabu wana mbinu nyingi za kuzidhoofisha timu ngeni zinapopambana na timu zao.

Kwa upande wa Yanga ambayo ina wakati mgumu zaidi, pia yapaswa kuwa makini kwani kwa mujibu ya magazeti ya michezo, Township Rollers ni timu inayopendwa sana Gaborone, jiji kuu la Botswana penye makazi ya Serikali.

Mengi yameandikwa na magazeti ya michezo nchini kuhusu mechi za leo.

Kadhalika viongozi mbalimbali wa vilabu vyetu wameeleza mengi kuhusu mechi hizo. Baadhi ya matajiri wameahidi kuwapa wachezaji fedha nyingi kama wakishinda.

Tahadhari kwa wachezaji wa Yanga na Simba: “Mbio za sakafuni huishia ukingoni.” Maana yake mbio za sakafuni humalizikia ukingoni.

Methali hii huweza kutumiliwa mtu anayejitia kufanya kazi fulani (kwa muktadha huu kandanda) kwa vishindo na makeke na hatimaye kushindwa kuimaliza kazi hiyo.

Wahenga walisema: “Jifya moja haliinjiki chungu.” Jifya ni jiwe mojawapo la kutelekea chungu. Mengi huitwa mafya. Maana yake mtu hawezi kubandika chungu juu ya meko yenye figa moja. Lazima yawepo mafiga matatu ndipo chungu kiweze kukaa vizuri.

Methali hii hutumiwa kuwashauri watu washirikiane katika shughuli zozote wazifanyazo. Hamna mtu anayeweza kufanya mambo yoyote yakafana bila kuwategemea watu wengine.

Kwa hiyo wachezaji wa Yanga na Simba leo wacheze kwa ushirikiano mzuri kwa lengo la ushindi na si vinginevyo. Wakumbuke kuwa penye nia pana njia nasi twaomba iwe hivyo.

Wakati hayo yakitokea huko, hapa nyumbani twasubiri kwa hamu yale maneno ya ‘wa kimataifa’ na ‘wa mchangani! Timu ipi itathibitisha maneno hayo leo? Yetu macho na masikio.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumamosi

$
0
0

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715 

Wambura Jembe Lisilokubali Kushindwa Katika Soka, Aamua Kukata Rufaa Akiwa na Hizi Sababu Tano Mkononi

$
0
0
Wakili anaemtetea Michael Wambura, Emanuel Muga amesema kwamba, wao wameamua kukata rufaa ili kutafuta haki ya mteja wake.

Muga amesema katika rufaa hiyo imesheheni masuala ya kisheria na kuna sababu tano za msingi zilizowafanya waamue kupeleka rufaa mbele ya kamati ya maadili ya rufaa.

“Kinachofuata ni hatua ya rufaa, tumeshaandaa rufaa na ipo tayari tumeshailipia kwa mujibu wa kanuni lazima ilipiwe silingi milioni moja (1,000,000) na tumeanza utaratibu wa kuisajili pale TFF ndani ya siku tatu ambazo zimetolewa.

“Rufaa imesheheni masuala ya kisheria, ina sababu tano za msingi na tutakuwa tayari kwenda mbele ya kamati ya rufaa ya maadili ili tuweze kuzifafanua hizo sababu tano.

Hukumu kutoka kamati ya maadili mmeshaipata?

“Hukumu tumeipata ikiwa imechapwa lakini kwenye tovuti na tuliisikiliza lakini kanuni hazisemi kwamba tuiambatanishe wakati kunakata rufaa kwa hiyo tumeamua kukata rufaa ingawa haijatufikia rasmi kwa sababu tumekata rufaa kwa hati ya dhalura kwamba kamati ya rufaa ya maadili iitwe haraka kwa hati ya dharura ili isikilize hili suala itolee maamuzi ili mambo mengine yaendelee.
“Wambura hawei akabaki amefungiwa tu ni mtu ambaye anamajukumu mengi ya kitaifa na kimataifa, ikumbukwe kwamba aliteuliwa kuwa mechi kamishna wa mechi itakayochezwa mwezi ujao ya U20 kati ya Kenya na Rwanda kwa hiyo hatima yake lazima ijulikane kabla ya mwezi Aprili ili aweze kufanya hayo majukumu.
“Kwa hiyo tunaiomba TFF kwa hati ya dharura iitwe hiyo kamati ya rufaa ya maadili ili iweze kusikiliza na hatma ijulikane.

Baada ya Jacob Zuma Kupokonywa Urais Mikononi Sasa Kushtakiwa Kwa Mashtaka Haya 18

$
0
0
Mkurugenzi wa mashtaka nchini Afrika Kusini amesema Rais Mstaafu wa nchi hiyo ambae alijiuzulu Jacob Zuma anatarajiwa kushtakiwa kwa makosa 18 ya rushwa dhidi yake.

Zuma mwenye umri wa miaka 75, alilazimishwa na chama chake cha African National Congress (ANC), kujiuzulu, amekana kufanya makosa hayo.

Mashtaka anayokabiliwa nayo Zuma yanahusu ununuzi wa silaha za serikali mwaka 1990 zilizokuwa na thamani ya dola za Kimarekani bilioni 2.5.

Zuma alikuwa anakabiliwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa mara ya 9 kabla ya kujiuzulu
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images