Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Mafufu Kumtolea Mahari Mchumba Wake Mpya Jumamosi

$
0
0
Mafufu Kumtolea Mahari Mchumba Wake Mpya Jumamosi
MWIGIZAJI wa Bongo Movies, Jimmy Mafufu, baada ya kuokoka na kuachana na mambo ya kidunia huku mkewe akimwacha, hatimaye Jumamosi hii anatarajia kumtolea mahari mchumba wake mpya, Upendo Meja atakayemuoa ndani ya mwaka huu.



Akistorisha na Za Motomoto News, Mafufu alisema kuwa, shughuli hiyo ya kutoa mahari na kumvisha pete ya uchumba Upendo itafanyika nyumbani kwa wazazi wa mwanadada huyo mkoani Mbeya na wanatarajia kufunga ndoa mwezi wa nane.


“Kwa sasa ninaanza maisha upya na mke wangu mtarajiwa, Upendo ambaye nimepewa na Mungu maana alinionesha maono juu yake, vitu vyote nilivyokuwa navyo zamani nimempa aliyekuwa mke wa awali ambaye ni mama mtoto wangu.



Kiukweli kwa sasa nina furaha sana maana licha ya awali kuwa kwenye ndoa, sikuwahi kufahia maisha ya uhusiano,” alisema Mafufu.

Haji Manara Ajitosa Sakata la Daimond na Waziri Shonza " Tuwe na Staha na Tupende vya Kwetu"

$
0
0
Haji Manara Ajitosa Sakata la Daimond na Waziri Shonza " Tuwe na Staha na Tupende vya Kwetu"
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara amefunguka na kumkingia kifua msanii Diamond na wenzake ambao wamekuwa wakitetea haki zo kwa Naibu waziri ambae ameibuka na sera ya kuwafungia wasanii kwa madai kuwa wanaimba nyimbo zisozokuwa na maadili katika jamii.

Hivi karibun Diamond aliongea katika media moja na kusema kuwa hata kama atatakiwa kulala jela kwa sababu ya muziki basi atafanya ilimradi kutetea haki ya muziki kwa sababu watu wanaofungia muziki huo hawajui historia ya muziki wala msanii wanaemfungia.

Haji Manara amesema  kuwa pamoja na kwamba wasanii wanaweza kuwa wamefanya kosa lakini wanapaswa kuangaliwa kwa jicho la pili na kwa upande wa Diamond ni msanii mkubwa mbaye amekuwa akiiwakilisha nchi katika mambo mbalimbali.

"Ngoja na mimi nispitwe na hili..inawezekana kuwa kama binadamu anaweza kuwa amekosea , lakini inabidi tutambua kuhusu muziki wa kisasa na soko lake linataka nini..by the way diamond na wenzie tunawatumia sana katika maswala ya kijamii  na hata kampeni zetu za kisiasa,na huyu ni brand kubwa ,,,walau tufanye staha kidogo na tujitaidi tupende vya kwetu.

NB.mimi napenda muziki mzuri sina cha timu wala cha baba yake na timu….hawakawii wabongo. @diamondplatinumz"

Shilole: Mume Wangu Uchebe Hakasiriki Akiniona Nakata Viuno Jukwaani

$
0
0
Shilole: Mume Wangu Uchebe  Hakasiriki Akiniona Nakata Viuno
Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefunguka na kukiri haoni ubaya wa yeye kukata mauno stejini maana yupo kazini.

Suala limekuwa ishu baada ya video yake akiwa anatumbuiza stejini huku anakata  mauno kihasara hasara stejini kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

Ndipo watu kuanza kuhoji inakuwaje mke wa mtu anafanya mambo yake hadharani lakini Shilole amewazima watu hao na kusisitiza kuwa Mume wake anajua anachofanya hivyo haoni kama kuna tatizo.

Shilole amefunguka alipohojiwa na Global Publishers kuhusu hilo na kuweka wazi kuwa anawashangaa watu wanaozungumza kuhusu hilo wakati wanajua wazi kuwa ile ndio kazi yake na mume wake Uchebe analitambua hilo hivyo hana neno juu ya hilo.

"Mume wangu Uchebe (Ashraf) anajua nikiwa kazini, chochote naweza kufanya jukwaani, haoni shida maana ananipenda na kazi yangu hivyo wanaosema ninawasihi waache kwani pale nilikuwa kazini kwa hiyo lazima niwapagawishe mashabiki wangu”.

Rais wa Myanmar Htin Kyaw Ajiuzulu

$
0
0
Rais wa Myanmar Htin Kyaw Ajiuzulu
Rais wa Myanmar Htin Kyaw amejiuzulu, kulingana na afisi yake.

Hakuna sababu ilitolewa lakini kumekuwa na wasiwasi katika miezi ya hivi karibuni kuhusu afya ya rais huyo mwenye umri wa miaka 71 baada ya kuonekana amedhoofika katika hafla moja.

Htin Kyaw alliapishwa kuwa rais 2016 baada ya uchaguzi uliositisha miongo kadhaa ya uongozi wa kijeshi.

Lakini alikuwa kiongozi asiye na mamlaka huku aliyekuwa kiongozi wa upinzani wa muda mrefu Aung San Suu Kyi akiwa kiongozi mwenye mamlaka.

taarifa iliochapishwa katika mtandao wa facebook wa rais huyo ilisema kuwa Htin alitaka kupumzika.

Makamu wa rais Myint Swe , jenerali wa zamani atakuwa kaimu rais hadi pale rais mpya atakapochaguliwa katika muda wa siku saba sijazo, taarifa hiyo ilisema.

Mzee Akilimali Aitaka Yanga Kufanya Uchaguzi

$
0
0
Mzee Akilimali Aitaka Yanga Kufanya Uchaguzi
Mjumbe wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali, ameuomba uongozi wa timu hiyo kuitisha uchaguzi huku akisema hapingi mabadiliko.

Akizungumza na ripota wa Saleh Jembe, Mzee Akilimali amesema Yanga haina Mwenyekiti mpaka sasa, na badala yake ni vema ikaitisha uchaguzi ili mabadiliko yaende kasi.

Akilimali ambaye amekuwa akilipigia kelele suala kwa muda mrefu, anaamini pale Mwenyekiti atakapopatikana, mchakato wa mabadiliko utaenda vizuri.

Aidha, Akilimali ameeleza kuwa, Mwenyekiti wao wa zamani Yusuph Manji, tayari alishajiondoa hivyo ni vema akapewa muda apumzike na endapo akitaka arudi anakaribishwa.

Manji alijiudhulu nafasi ya Uenyekiti ndani ya Yanga baada ya kukumbukwa na mashtaka ya kesi ikiwemo la Uhujumi Uchumi mwaka 2017.

RC Makonda Afunguka Kuhusu Kushambuliwa kwa Afisa Ubalozi wa Syria

$
0
0
RC Makonda Afunguka Kuhusu Kushambuliwa kwa Afisa Ubalozi wa Syria
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa ameshtusha na taarifa zilizosambaa mitanaoni kuhusu tukio la Afisa mmoja wa Ubalozi wa Syria ambaye amedaiwa kushambuliwa na kuporwa kiasi kikubwa cha fedha.


Afisa wa Ubalozi wa Syria anayetajwa kushambuliwa na kuporwa fedha

Mhe. Makonda ametoa taarifa yake kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa ambapo amewataka wananchi kutulia na vyombo vya usalama wanafuatilia kwa umakini tukio hilo.

Soma taarifa hiyo hapa chin:

TAARIFA YA MKUU WA MKOA DAR ES SALAAM KUHUSU TUKIO LA KUSHAMBULIWA KWA AFISA UBALOZI WA SYRIA.

Kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar Es Salaam nimeshtushwa na taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Afisa Ubalozi wa Syria ameshambuliwa na kuporwa kiasi kikubwa cha fedha leo mchana Jijini Dar Es Salaam. Taarifa hiyo imeenda mbali zaidi na kusema kwamba Dar Es Salaam sio salama na kueleza watu wawe makini zaidi.

Nawaomba sana wananchi wa Dar es Salaam muendelee kuwa watulivu na mkielewa kwamba Mkoa wenu ni salama salama sana. Vyombo vya usalama vinalifanyia kazi tukio hili na taarifa za awali nilizopokea zinaonyesha tukio hili linaweza kuwa limepangwa na watu wa ndani. Tunafuatilia zaidi kujua kwa nini Afisa huyo hakuomba ulinzi wa polisi akiwa amebeba kiasi hicho kikubwa cha fedha na pia kwa nini dereva wake amekimbia.

Kwa hali ilivyo mpaka sasa kuna uwezekano ikawa ni tukio la kupangwa na watu wa ndani. Hatutaruhusu watu wachache wachafue taswira ya Mkoa wetu.

Uchunguzi ukifikia sehemu nzuri taarifa rasmi itatolewa na vyombo vyetu vya usalama. Ulinzi na usalama wa wananchi wetu ni muhimu sana.

Mh. Paul Makonda
Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam

Video: Mwanasheria wa TSNP Afunguka Sababu za Kumburuza IGP Sirro Mahakamani

$
0
0
Video: Mwanasheria wa TSNP Afunguka Sababu za Kumburuza IGP Sirro Mahakamani

Mwanasheria wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Paul Kisabo ameshawasili Mahakama Kuu kwaajili kusikiliza shauri la maombi ya kutaka DPP, DCI, IGP wajibu mashtaka kwanini hawajamleta Abdul Nondo Mahakamani na wamemshikiria kinyume na sheria.


Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo


BREAKING NEWS: Abdul Nondo afikishwa Mahakamani

$
0
0


Mwenyekiti wa Mtandao wa wanafunzi TSNP, Abdul Nondo amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya  Iringa kusomewa mashtaka yanayomkabili. Mwanasheria wa TSNP amethibitisha taarifa hiyo.

Basata Wasema Diamond Amefanya Makosa Makubwa kumjibu Waziri Shonza

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Godfrey Mngereza amesema mwanamuziki Nassib Abdul maarufu Diamond amefanya makosa kumjibu Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza akifananisha kitendo hicho na kuitukana Serikali.

Diamond Platnumz na naibu waziri huyo waliingia katika vita ya maneno baada ya Serikali kufungia nyimbo 15 mwezi uliopita, zikiwemo mbili za mwanamuziki huyo.

Mngereza amesema Diamond anapaswa kuelewa kwamba maneno machafu anayoyatoa dhidi ya waziri huyo  ni sawa na kuitusi serikali jambo ambalo hata ukienda katika sheria za kimtandao anaweza kujikuta anaingia matatizoni.

Mngereza amesema wamesikitishwa na kauli ya Diamond na kusisitiza kwamba ni vyema akafuata taratibu katika kulalamikia suala hilo ikiwemo kuandika barua kama alivyomuelekeza Waziri Shonza.

Ameongeza kuwa si lazima msanii aandikiwe barua pale anapokosa kama ambavyo Diamond ameeleza katika ukurasa wake wa Twitter, kwamba Shonza angemwandikia barua kabla ya kumfungia.

Amebainisha kuwa si kila mwanamuziki anayefanya makosa huwa anaandikiwa barua.

Katika malalamiko yake, Diamond amesema naibu waziri huyo amekuwa akikurupuka kufungia nyimbo na pia kutowaandikia barua rasmi ndio maana ameamua kuyazungumza kwenye redio na mitandao ya kijamii.

Jana Waziri Shonza alisema hawezi kujibizana na Diamond kwa sababu alichofanya si maamuzi yake binafsi na kwamba kama anaona ameonewa apeleke malalamiko yake kwa maandishi.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715

Jinsi Wema Sepetu Anavyokwepa na Kupinga Maandamano Ya Mange Kimambi

$
0
0
Baada ya Mange Kimangi kupanga na kuhimiza maandamano nchni, Wema Sepetu naye apanga kuelekea marekani siku hizo hizo za maandamano. Inasemekana hii ni kutoonyesha sapoti au kuyapoteza nguvu maandamano ya Mange Kimambi,


Wemasepetu: Listen to it very carefully... Its a Not Miss.... Hee...!!! Kumbe maandamano mi apa yatanipita....!!! .
Ntakuwa SIIIIIIIPO... Ntaungana na Watanzania wengine Tutakuwa Marekani kwenye Tanzania Deeeeeiiiii....

Anyways Tell a Friend, to Tell a Friend that Tz Day is Happening from 27th- 29th of April this Year......!!! See you there... .
Tanzania Day baby...

Je Wajua Kuna Wakati itakulazimu Kutoa Huduma/Kufanya Kazi Bila Malipo yoyote ?

$
0
0
Kuna wakati itakulazimu kutoa huduma/kufanya kazi bila MALIPO yoyote au kwa Malipo Kidogo Sana,sio kwa sababu unachofanya hakina thamani bali ni kwa sababu watu hawajaiona thamani bado.

Siku zote kumbuka uwezo/kipaji ulichonacho kina hatua kubwa tatu:

1.KUGUNDUA:
Kipaji/eneo lako:Hapa kazi kubwa ni kujitambua na kama haujajitambua hakuna atakayekutambua.

2.KUNOA UWEZO WAKO:
Hapa kazi kubwa uliyonayo ni kuongeza thamani na mara nyingi utakuwa unafanya mambo nyuma ya PAZIA.Mara nyingi watu watakuwa hawakuamini sana na it atakuja Ufanye mazoezi ya Muda mrefu kuongeza thamani YAKO.Kipindi hiki unatakiwa utafiti nafasi sio kwa sababu unataka KULIPWA bali kwa sababu unataka KUJINOA.

3.KUUZA UWEZO/KIPAJI CHAKO
Hapa ndio sasa unaanza kubadilisha huduma/ujuzi/Kipaji chako na Fedha ambazo watu wako tayari Kukulipa.

Unatakiwa uanze na wale ambao wameshakukubali na kukuamini.Hata kama una maono makubwa sana, uwe tayari kuanzia chini huku unaongeza thamani YAKO

UKO HATUA GANI?

See YouAt The Top

@JoelNanauka

Rayvanny Ampa Somo Diamond "Hakuna Anayefanikiwa Akakosa Maadui"

$
0
0
Rayvanny Ampa Somo Diamond "Hakuna Anayefanikiwa Akakosa Maadui"
Msanii kutoka WCB, Rayvanny amefunguka mambo kadhaa kwa kile anachopitia Diamond kwa sasa katika muziki wake.

Muimbaji huyo ameeleza kuwa hakuna anayefanikiwa akakosa maadui na ndicho kinachotokea kwa Diamond sasa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Rayvanny ameandika;

Kuna Vitu Pengine Unaweza Ukawa Unapatia Au Vingine Unakosea Sitaki Kuongelea Hilo Sababu we nawe Ni Binadamu. ILA KWENYE KUSEMA UKWELI NITASEMA!!!! Si kwa Sababu wewe Ni boss Wangu Hapana!!! Ila Mara Nyingi Thamani Ya mtu Na Umuhimu Wa Mtu wengi Wanaujua Akishaondoka…. MZIKI NI KAZI NA NI AJIRA Namaanisha Kuna Familia Nyingi Zinaishi kupitia Huu huu mziki.

DIAMOND KATIKA WASANII WOOOTE Umekua chachu Ya Kuongeza Thamani Ya Muziki Nakupitia wewe naamini Wengi Wanafanikiwa…. KUJITOA KWAKO, KUAMINI KATIKA UMOJA NA PIA KUTHUBUTU Ndiko kunafanya Unafanikiwa…. USHAAMBIWA HUJUI KUIMBA ila ukaimba ukafanikiwa… USHAAMBIWA UNAVIMBA UNAIGIZA MAISHA Lakini sasa Unayaishi hayo Maisha… Hakuna Anaefanikiwa Akakosa maadui ndivyo Dunia Ilivyo ..

MIMI ULINISAIDIA ULIJUA SHIDA ZANGU Naamini Mungu Alikutumia wewe Ukawe Mkombozi Wangu ……. KWAIO KUMBUKA ( ILI MBEGU IOTE LAZIMA IOZE ) SINA MUDA KUMSEMA MTU ILA NAKUPA MOYO FANYA KAZI SIMBA……. kama Wewe Unaamini Katika Upendo Na sio Chuki, Vita Na Matusi JUS COMMENT ( LOVE )

Kwa siku za hivi karibuni Diamond amekuwa kwenye drama kibao kufuatia kutofautina na baadhi ya vyombo habari kitu kilichopelekea kutochezwa kwa nyimbo zake katika vyombo hivyo, pia kufungiwa kwa nyimbo zake mbili ‘Waka na Hallelujah’ ni moja ya mambo ambayo hayajakaa vizuri kwa upande wake.

Masogange Amelazwa Hawezi Kutembea, Ashindwa Kufika Maakamani Kusikiliza Hukumu Yake

$
0
0
Masogange Amelazwa Hawezi Kutembea, Ashindwa Kufika Maakamani Kusikiliza Hukumu Yake
Leo March 2018  Video Queen, Agnes Gerald maarufu ‘Masogange’ ameshindwa kufika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kusikiliza HUKUMU ya kesi yake ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam kwa sababu amelazwa hospitalini amewekewa Dripu na hawezi kutembea.

Hayo yameelezwa na Mdhamini wa Masogange, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri baada ya Wakili wa serikali, Adolf Mkini kueleza kuwa kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya hukumu.

Mdhamini wa Masogange, alisimama na kumueleza Hakimu Mashauri kuwa Masogange ameshindwa kufika mahakamani kwa sababu anaumwa.

“Masogange anaumwa yupo hospital amelezwa na kuwekewa Drip, pia hawezi hata kutembea,” -mdhamini.

Katika kesi hiyo, Masogange anawakilishwa na Wakili Ruben Simwanzi ambaye ameeleza kuwa mteja wake anaumwa.

Baada ya kuelezwa hayo, Hakimu Mashauri ameahirisha hukumu hadi April 3,2018.

Awali katika ushahidi wake Masogange alidai kuwa hajawahi kutumia dawa za kulevya, hivyo anaiomba Mahakama imuachie huru kwa sababu hana kosa.

Masogange anadaiwa kuwa kati ya February 7 na 14, 2017 katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Diacety Imophine).

Pia anadaiwa kuwa kati ya February 7 na 14, 2017 alitumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.

Sitegemei mpenzi wangu kupaka make-up -Nikki

$
0
0
Sitegemei mpenzi wangu kupaka make-up -Nikki
Msanii kutoka kampuni ya Weusi, Nikki wa Pili amesema uzuri wa msichana au mwanamke unatoka na asili yake aliyozaliwa nayo na wala haitokani na vitu vya kujiremba na kudai haitokuja kutokea mke wake kuonekana amejiremba kwa kuwa anataka awe 'natural'


Nikki wa Pili ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha eNewz kutoka EATV baada ya kupita siku kadhaa tokea msanii mwenzake Dogo Janja ku-comment katika ukurasa wake kwa kumwambia vitu 'natural' aviachie misitu na kumtaka aache ubahili wake amtunze mke wake wa kumrembesha na urembo.

"Sisi binadamu wenye ni wazuri kwasababu ni asili kwahiyo hakuna uzuri wowote duniani unaoweza kuzidi asili. Ninachoamini mimi ni kwamba uzuri wa msichana upo katika asili yangu", amesema Nikki wa Pili

Pamoja na hayo, Nikki wa Pili ameendelea kwa kusema "mimi ni mtu creative kwa hiyo siamini kwenye 'material' ninaamini kwenye nguvu ya ubunifu, kwenye kazi yangu naekeza kwenye ubunifu so labda watu wanatafsiri hivyo lakini ubunifu unanguvu mara elfu. Mimi napenda asili kwa hiyo sitegemei kumuona mpenzi wangu akiwa amejipaka make-up".

Rais Trump Ashtakiwa Mahakamani kwa Ubakaji

$
0
0
Rais Trump ashtakiwa Mahakamani kwa ubakaji
Leo March 21, 2018 Idadi ya wanawake wanaomshtaki Rais wa Marekani Donald Trump mahakamani kwa madai ya kuwa na uhusiano nao kimapenzi inaendelea kuongezeka ambapo sasa wamefika wanawake watatu.

Mtaalamu wa kujenga mwili na Mwanamitindo Karen McDougal alifungua kesi jana March 20, 2018 kwenye Mahakama ya Juu jijini Los Angeles akiwa anahitaji haki ya kuzungumza hadharani kuhusu uhusiano wake na Rais Trump.

Huyu ni mwanamke wa pili, baada ya Staa wa sinema za ponografia Stormy Daniels pia kufungua mashtaka dhidi ya Rais Trump mwanzoni mwa mwezi March, 2018.

Jana hiyo hiyo pia, Mahakama ya Juu ya New York ilieleza kuwa mashtaka mengine dhidi ya Rais Trump yamefunguliwa na aliyekuwa mgombea wa kipindi cha television Marekani cha The Apprentice, Summer Zervos akidai kuwa alibakwa na Rais huyo.

Mkuu wa Wilaya Aagiza Polepole Akamatwe

$
0
0
Mkuu wa wilaya aagiza Polepole akamatwe
Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Ruyango ameliagiza jeshi la polisi katika wilaya hiyo kumkamata na kumfikisha mahakamani Mganga wa zahanati ya Kibanga wilayani humo Ruiz Polepole.


Mkuu wa Wilaya huyo ametoa agizo hilo kufuatia wananchi wa kijiji cha Kibangu kutega mtego ambao ulimnasa Mganga huyo wa zahanati ya Kibanga akiuza dawa zinazotolewa na Serikali ambazo zinapaswa kutolewa bure.

Aidha upelelezi ukikamilika mganga huyo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo za kuuza dawa za serikali kinyume na utaratibu wa serikali.

Watu 38 Wauawa kwa Bomu Katika Eneo la Soko

$
0
0
Watu 38 Wauawa kwa Bomu Katika Eneo la SokoKutoka nchini Syria taarifa ni kwamba watu 38 wameuawa kwa bomu lililolipuliwa kwenye eneo la soko katika mji mkuu wa nchi hiyo Damascus siku ya jana March 20, 2018.

Tukio hili linaelezwa kuwa sehemu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe ambapo kwa sasa serikali ya nchi hiyo inataka kuukomboa mji wa Ghouta Mashariki ambao unashikiliwa na kikundi cha waasi.

Inasemekana kuwa ndege aina ya rocket zinazomilikiwa na waasi hao ndizo zilizorusha na kulipua eneo hilo la soko na kusababisha maafa hayo huku 20 wengine wakijeruhiwa.

Jitihada hizo za serikali ya Syria kuchukua eneo hilo la Ghouta Mashariki ambapo ni makazi kwa watu takribani 400,000 kutoka kwa waasi, zimesababisha vifo vya 1,400 huku watu 45,000 wakikimbia makazi yao.

Mange Kimambi Awaponza Watu Wawili Wakamatwa na Polisi Kisa..

$
0
0
Mange Kimambi Awaponza Watu Wawili Wakamatwa na Polisi  Kisa..Jeshi la polisi mkoa wa Dodoma limewakamata na kuwawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuhamasisha maandamano kwenye mitandao ya kijamii yanayotarajiwa kufanyika April 26 mwaka huu.


Akizungumza na www.eatv.tv kamanda wa polisi wa mkoa Dodoma Gilles Muroto amesema Watu hao wamekua wakisambaza ujumbe kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu kuandamana huku wakijua ni kosa kisheria.

Aidha Kamanda Mruto ametoa wito kwa watu kutofuata mkumbo kuhamasisha watu kufanya maandamano kwani ni kosa kisheria na kuwa yeyote ambaye atakamatwa atashughulikiwa kisheria

Mbali na hilo Kamanda Mruto amesema kuwa upelelezi ukikamilika watu hao watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao kuhusu kuhamasisha watu kufanya maandamano kupitia mitandao ya kijamii ambayo yamepangwa kufanyika April 26, 2018 nchi nzima na yakiratibiwa na mwanadada Mange Kimambi kupitia mitandao ya kijamii.
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images