Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Je Wajua Faida za Kutokuvaa Chupi?

$
0
0
Je Wajua Faida za Kutokuvaa Chupi?Leo naomba nikukumbushe somo la Afya ya uzazi. Somo hili litafafanua faida na hasara au madhara yatokanayo na uvaaji wa nguo za ndani hasa Chupi. Uvaaji wa chupi kihistoria ulianza karne ya 19 baada ya uvumbuzi wa viwanda na mapinduzi yake yaliyoambatana na mapinduzi ya teknolojia.

Enzi za mama zetu na babu zetu uvaaji wa chupi haukuwepo hapa Tanzania. Uvaaji wa chupi uliletwa na wamisionari na wakoloni wakati wanaleta dini Africa. Kabla ya hapo waafrica hatukuwa na utamaduni wa KUVAA chupi.

Mtoto akizaliwa hakuvalishwa chupi kamwe kama ilivyo Leo. Mwanamke pia enzi hizo alikuwa havai chupi. Mwanaume naye pia alikuwa havai chupi? Watu wote walikuwa hawavai chupi. Mwanamke alikuwa hachuchumai chini pindi akijisaidia kutokana na kwamba hawakuwa wanavaa chupi hivyo wakitaka kujisaidia haja ndogo walikuwa wanasimama tu na kupanua miguu na kuanza kukojoa.

Nyakati za leo ambapo uvaaji chupi kwa wanaume na wanawake uko juu sana kuanzia watu tunapokuwa watoto wadogo hali ya Afya ya viungo vya uzazi imeendelea kuwa mbaya sana. Yafuatayo ni baadhi ya madhara ya kuvaa chupi :

1. Magonjwa ya "Urinary tract infection" au UTI hayataisha kwako.
Hii hasa ni kwa wanawake wanavaa nguo nyingi kwa wakati mmoja na kwa muda mrefu zaidi ya saa kumi. Unavaa chupi, lakini tight, suruali ya jinzi, nk halafu unashinda na hizo nguo kuanzia asubuhi unapoenda kazini hadi saa mbili usiku unaporudi home. Hiyo ni hatari sana.

Mwanamke anayefanya kazi zinazompasa kuwepo kazini zaidi ya masaa 8 namshauri asiwe anavaa chupi kabisa. Chupi ivaliwe nyakati za hedhi tu. Kama hauko kwenye siku zako vaa suruali tu bila chupi. Au vaa underskirt pekee yake kwa ndani na ndoo uvae nguo yako ya kawaida. Hii itakuepusha na kuugua UTI. Ukiacha sababu za ngono UTI husababishwa na bacteria wanaopendelea mahali penye unyevu na joto. Kwa hiyo mwanamke akivaa nguo nyingi bacteria hao hujipatia joto la kutosha kuzaana.
Mwanamke ni vyema ukaepuka kuvaa nguo za kubana mwili sana ili kuepukana na uwezekano wa kupafanya ukeni pawe na joto sana na ikitokea bacteria mmoja tu akaingia humo atazaa haraka sana na kujikuta UTI inakuwa rafiki yako. Vaa sketi bila chupi au kama kuvaa suruali ni lazima hakikisha unavaa suruali peke yake. Jizoeze tu utazoea. Na ukizoea kuvaa nguo bila chupi utainjoi sana.

2. Magonjwa ya kuvu au fungus hayatakoma kwako.
Bado niko kwa wanawake, kama nilivyoeleza mwanzo hapo magonjwa ya fungus yanasababishwa pia na kuvaa chupi kwa muda mrefu. Chupi inayovaliwa kwa zaidi ya saa 8 lazima italeta ukungu au uvundo sehemu nyeti. Huo uvundo waweza kuleta fungus ukeni. Fungus za ukeni hazina tofauti na zile za miguuni kwa wanaume wanaovaa viatu kwa muda mrefu bila usafi miguuni wa kutosha.

Chupi inakuwa kama socks za wanaume. Mwanamke avaae chupi muda mrefu bila kuruhusu upepo upite ndani ni watapata fungus ukeni sawa na mwanaume anayevaa socksi zisizofaa kiafya. Chupi au socks zinazofaa ni zile za pamba au cotton.

Of course sababu za kupata ugonjwa wa fungus kwa mwanamke siyo tu kuvaa chupi inayobanaaaa kwa muda mrefu ni pamoja na kutawadha kwa kutumia maji.

Wanawake wengi hawajui kutawadha kwa kutumia maji. Wengi wamalizapo kujitawadha haja kubwa ndipo hurudi kujisafisha ukeni. Hii ni hatari sana kwani bacteria watokanao na kinyesi unawahamisha kutoka nyuma na kuwaleta mbele.

Mwanamke unapaswa kutawadha kwanza mbele kisha umalizie nyuma.

Yaani hakikisha kuwa uchafu wa nyuma unaoweza kuwa umebakia kwenye vidole vyako usiuingize ukeni kwa namna yoyote. Tawadha pande zote lakini uhakikishe kuwa haviingiliani mbele na nyuma. Sawa dada yangu? Uko poa hapo?

Kikubwa hapa ni usafi wa mbele na nyuma. Usafi wa chupi zetu. Uvaaji chupi wetu.

Kwa mfano uwapo safarini tena safari ndefu ya zaidi ya saa 8 ni vyema ukasafiri bila kuvaa chupi isipokuwa tu kama uko kwenye siku zile za adabu. Hata kama uko kwenye siku za adabu ni vyema ukasafiri bila kuvaa manguo mengi sana yanayobana mwili. Vaa chupi na sketi au suruali isiyoubana sana mwili wako.


3. Chupi husababisha ugumba kwa wanaume.
Sababu nyingi za ugumba tunaweza ukizipata kutoka kwa madaktari wetu wa hospitali zetu. Lakini ukija kwangu mimi Daktari wa magonjwa ya tabia (Lifestyle Based Diseases Doctor) nitakuongezea sababu nyingine ya ugumba wa wanaume kuwa ni kuvaa chupi zinazobana sana.

Mwanaume shujaa havai chupi. Anavaa kaptura badala ya chupi. Tena havai kaptura inayobana sana. Anavaa isiyobana viungo muhimu kwa uzalishaji wa watoto. Mbegu za kiume huzalishwa kwa wingi wakati wa baridi. Kuvaa chupi inayobana kwa muda mrefu husababisha pumbu kuchemka sana na kushindwa kuzalisha mbegu nyingi. Mwanaume mwenye mbegu chache hushindwa kutungisha mimba kwani mbegu zake zinakwenda ukeni kwa uchache na kushindwa kuogelea ukeni.


4. Chupi husababisha miwasho sana kwenye mapaja ya mwanaume na mwanamke.
Epuka kuvaa chupi zinazobana ili kuepukana na miwasho.

5. Chupi husababisha michubuko ya mapaja.
Ukivaa chupi kwa muda mrefu utajikuta umepata michubuko mapajani karibu na uume au uke .

6. Uvaaji chupi usiku huchelewesha tendo la ndoa.
Mwanaume anapohitaji vitu adimu usiku wakatimwingine anapaswa kujichotea tu kirahisi kwani ni mke wake halali lakini akikutana na chupi inakuwa kikwazo. Mwanamke usilale na chupi usiku. Unaogopa nini? Hakuna majambazi wala moto. Nani alikwambia ulale na chupi eti unajihami na ajali za moto usiku.? Mbona tangu umelala na chupi usiku hakuna ajali ya moto iliyokwishatokea.

Acheni kuvaa chupi enyi wanawake ili ikitokea waume zenu tunahitaji naniii usiku tujipatie kwa wepesi! Au Siyo?

Tangu niache kuvaa chupi sijawahi tena kuwashwa mapajani wala mke wangu hajawa na taarifa za fungus na UTI kama zamani alipokea hajalielewa somo hili. Na wewe pia nakushauri uache kuvaa chupi kuanzia leo Uwe na afya bora maeneo yote nyeti.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715 

TFF Yamsaka Atakayechukua Mikoba ya Mayanja

$
0
0
TFF Yamsaka Atakayechukua Mikoba ya Mayanja
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeanika wazi vigezo vipya watakavyovizingatia mara baada ya kuanza rasmi kupitia ‘CV’ mbalimbali walizopokea zitakazowafanya kumpata kocha mpya atakayechukua mikoba ya kocha wa sasa, Salum Mayanga.



TFF inaingia katika mchakato wa kutafuta kocha mpya baada ya mkataba wa kocha wao wa sasa Mayanga kumalizika tangu mwezi uliopita, huku akiendelea kukitumikia kikosi hicho kwa maombi maalumu.



Akizungumza na Championi Ijumaa, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidau, alisema pamoja na Mayanga kuendelea kuitumikia Stars kwenye michezo miwili ya kirafiki iliyopo kwenye kalenda ya Fifa, mkataba wake ulishamalizika, hivyo TFF tayari ipo katika mchakato wa kuhakikisha inampata kocha mpya ambaye atakuwa na vigezo vya kuifikisha Stars katika anga za juu.



“Uongozi kwa sasa umejipanga kikamilifu kuhakikisha soka letu linafika mbali na ndiyo maana utaona karibia michuano yote ya kimataifa vikosi vyetu vya taifa vinashiriki na TFF inafanya kila liwezekanalo ili tuweze kufuzu kwa kila hatua inayoendelea mara tu baada ya kuingia katika michuano yoyote iliyo mbele yetu.



“Lakini kama hilo halitoshi, TFF tumejipanga kuhakikisha tunampata kocha mwenye CV kubwa zaidi ya aliyepo na kama atakosekana mwenye vigezo vya kumzidi Mayanga basi hatutakuwa na haja ya kutafuta kocha mpya.

“Kwa kuwa walimu wapo wengi wenye viwango, itategemea na hao wanaopitia majina maana makocha ni wengi.



“Kama unavyojua mwingine anaweza akapatikana na asiwe tayari kuja bila maelewano na timu yake hivyo zoezi la kumtangaza litategemea na muda utakaotumika kukamilisha mambo yote hayo,” alisema Kidau.

Sakata la Daimond, Waziri Shonza Lamuibua Stara Thomas Ataka Wakutane Kuweka Mambo Sawa

$
0
0
Sakata la Daimond, Waziri Shonza Lamuibua Stara Thomas Ataka Wakutane Kuweka Mambo Sawa
Msanii wa siku nyingi wa bongo fleva, Stara Thomas amesema anatamani msanii Naseeb Abdul ‘Diamond’ aliyeingia kwenye vita ya maneno hivi karibuni na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Juliana Shonza kukutana ili kuyaweka mambo sawa.



Wiki hii Shonza na Diamond wamejikuta katika vita ya maneno iliyosababishwa na kitendo cha kufungiwa kwa nyimbo 15 za baadhi ya wasanii ukiwemo wa Diamond wa Halleluya na Wakawaka.



Diamond amedai waziri huyo amekuwa akifanya mambo kwa kukurupuka kwa lengo la  kutafuta ‘kick’ kwenye vyombo vya habari au kuogopa kutumbuliwa.



Hata hivyo, Shonza amesema hayupo tayari kumjibu msanii huyo na kumtaka kufuata taratibu za kufika ofisini kwake au kuandika barua kama anaona hajatendewa haki badala ya kuzungumzia kwenye vyombo vya habari na mitandao, huku Diamond akisema kwa nini hakumwandikia barua kabla ya kumfungia.



Akizungumza na MCL Digital, Stara ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya maadili ya Chama cha Bongo Fleva (Tuma), amesema anajua Diamond alichokifanya si sahihi na alikuwa na hasira, wakati akitetea kile alichofanyiwa na kushauri kuwa ni wakati wake kukutana na waziri ili kuweka mambo sawa.



“Ifike mahali wasanii wajue kwamba huwezi hata siku moja ukashindana na Serikali hata kama unajiona hujakosa, zipo taratibu za kuweza kufuata kwa unacholalamikia na si kutumia lugha isiyo ya staha kwa kiongozi aliyepewa dhamana na Rais kusimamia sekta fulani,” amesema.



“Najua inaumiza wasanii tumekuwa tukipigania kazi zetu wenyewe na ndio maana hata mdogo wangu Diamond kajikuta anashindwa kuficha hasira zake, lakini hii kamwe haiwezi kumsaidia kwa sababu anashindana na mamlaka iliyopo juu kisheria.”



Kwa upande wa Serikali, amesema ni vyema ikawa na utaratibu wa kukutana mara kwa mara na wasanii kuwapa elimu ya mambo wanayotakiwa wayafanye na yapi hawatakiwi kuyafanya, jambo litakalowasaidia kuepuka kuingia nao katika migogoro ya aina hii.



Kuhusu kama tangu sakata hilo lianze kamati ya maadili ya bongo fleva imeshamuita Diamond, Stara amesema inakuwa vigumu kwa kuwa msanii huyo si mwanachama wao na kwamba, utaratibu wao ni kufanya hivyo kwa wanachama wao.

Serikali Yawaonya Maofisa Elimu

$
0
0
Serikali Yawaonya Maofisa Elimu
 Serikali imewaonya maofisa elimu nchini kutowapangia walimu wa sekondari wa masomo ya sanaa kwenda kufundisha shule za msingi kwa vigezo vya kuwaadhibu, bali wazingatie vigezo vilivyowekwa.

Kwa mujibu wa takwimu za Tamisemi, kuna upungufu wa walimu wa shule za msingi 85,000 nchini wakati ziada ya walimu wa masomo ya sanaa katika shule za sekondari ni 21,000.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na maofisa elimu wa mikoa na wilaya za Tanzania Bara leo Machi 23, Dodoma, Naibu Waziri Tamisemi, Joseph Kakunda amesema kuwahamishia walimu hao kwenda shule za msingi kunalenga kukabiliana na upungufu huo.

“Msiwapangie walimu hao wa sekondari kwenda shule ya msingi kwa kigezo cha kutoa adhabu kwa walimu bali mzingatie vigezo. Nimekwishaagiza kuwa kigezo cha mikondo ndio kiwe kigezo sahihi cha kupanga walimu. Nitalisimamia kwa karibu sana suala hili,” amesema.

Pia, amesema kigezo cha kuwapangia walimu shule za msingi kwa kutumia idadi ya wanafunzi kinazinyima shule zenye wanafunzi wachache kuwa na walimu wa  kufundisha darasa la awali hadi darasa la saba kwa ufanisi.

“Kulingana na takwimu hizo Serikali imeona ni vema walimu hawa wa masomo ya sanaa wapelekwe kufundisha shule za msingi kwani uamuzi huo wa Serikali umezingatia suala la matumizi mazuri ya raslimali watu,” amesema.

Amesema kutokana na wingi wa walimu wa sanaa katika shule za sekondari mwalimu mmoja wa sanaa alikuwa akifundisha chini ya vipindi 10 kulinganisha na mwalimu wa sekondari ambaye alikuwa akifundisha vipindi 20.

Mwenyekiti anayemaliza muda wake wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Wilaya, Mayasa Hashimu ameiomba Serikali iwasisitize wakurugenzi wa halmashauri kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa magari kwa maofisa elimu wa mikoa na wilaya.

Pia ameiomba Serikali kuweka msisitizo wa pamoja katika usimamizi wa ujenzi na ukarabati wa matundu ya vyoo, vyumba vya madarasa, maabara na hosteli shuleni.

Akijibu maombi hayo kwa niaba ya Jafo, Kakunda aliziagiza halmashauri zote 185 nchini kukamilisha miundombinu ya shule za msingi na sekondari pamoja na maabara na kuwaagiza makatibu tawala wa mikoa, wakurugenzi kutenga fedha za ununuzi wa magari kupitia bajeti zao.

Mama Samia Akutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Bill

$
0
0
Mama Samia Akutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Bill
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo (Ijumaa) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation, Rodger Voorhies.



Mhe. Samia amekutana na Voorhies kwenye makazi ya Makamu wa Rais, Kilimani mjini Dodoma.

Mahakama ya Afrika:Tanzania Ilikiuka Baadhi ya Haki za Babu Seya na Mwanaye

$
0
0
Mahakama ya Afrika:Tanzania Ilikiuka Baadhi ya Haki za Babu Seya na Mwanaye
Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu (AfCHPR) imeamua kwamba Tanzania ilikiuka baadhi ya haki za wanamuziki Nguza Viking maarufu Babu Seya na mwanaye, Johnson Nguza 'Papii Kocha' katika kesi ambapo wawili hao walikuwa wamehukumiwa kufungwa jela maisha.

Wawili hao waliwasilisha rufaa katika mahakama hiyo mwaka 2015 kupinga hukumu ya kifungo cha maisha iliyokuwa imetolewa dhidi yao.

Majaji wa mahakama hiyo wamesema haki zao zilikiukwa kwa kutowapa taarifa za mashahidi wa upande wa mashtaka na kwamba mashahidi hao hawakuhojiwa mahakamani.

"Mahakama inatambua kwamba taifa lililoshtakiwa halijapinga madai kwamba walalamishi hawakupewa taarifa za mashahidi na kwamba mashahidi wanne hawakuitwa kuhojiwa," majaji wamesema.

Majaji hao wamesema kila mshtakiwa ana haki ya kupata muda wa kutosha na rasilimali za kutosha kujiandaa kujitetea.

Aidha, kila mshtakiwa ana haki ya kuwahoji mashahidi waliowasilishwa dhidi yake.

"Katika kesi hii, walalamishi wangepewa nakala za mashahidi wa mashtaka kuwawezesha kujiandaa kujitetea. Kwa hili kutofanyika, waliwekwa katika hali iliyowabana ukilinganisha na upande wa mashtaka, kinyume na kanuni ya usawa wa nguvu ya silaha.

"Aidha, kwa kutowaita mashahidi hao wanne watoe ushahidi mahakamani, walinyimwa fursa ya kuwauliza maswali, na hili liliwaweka katika nafasi iliyowabana."

Majaji walisema hilo lilikuwa ukiukaji wa Kifungu cha 7 (1c) cha Mkataba unaounda mahakama hiyo kwa upande wa serikali ya Tanzania.

Hata hivyo, mahakama hiyo imesema madai ya wawili hao kwamba haki zao zilikiukwa wakati wa kutambuliwa hayana msingi.

Aidha, mahakama haikupata ukiukaji wowote wa haki kwa kukataliwa kwa ushahidi wao kuhusu eneo walipokuwa wakati wa kutekelezwa kwa uhalifu huo.

Kuhusu kwamba matokeo ya kupimwa mkojo na damu hayakuwasilishwa, mahakama hiyo imesema haki zao hazikukiukwa kwani matokeo hayo hayakutumiwa na Mahakama Kuu wala Mahakama ya Rufaa kuamua kwamba walikuwa na hatia.
Hata hivyo, kuhusu ombi la mmoja wa washtakiwa apimwe uwezo wake wa kuzaa, mahakama hiyo imesema Tanzania ingefanikishwa apimwe.

"Matokeo ya hilo yangebaini iwapo Bw Nguva angetekeleza uhalifu aliodaiwa kutekeleza. Mahakama inaamua kwamba kukataliwa kwa ombi hili, Tanzania ilikiuka haki zake kama zilivyoelezwa katika Kifungu 7 (1c) cha Mkataba unaounda Mahakama hii."

Kupitwa na wakati
Bw Nguva na mwanawe walikuwa pia wamedai jaji alikuwa anabagua lakini Mahakama hiyo imeamua hali kwamba baadhi ya washtakiwa walipatikana bila hatia na mashtaka yakapunguzwa, hiyo ni ishara kwamba kesi hizo ziliangaziwa kwa uzito wake.

"Walalamishi hawajatoa ushahidi wa kutosha kuonesha jaji alikuwa na mapendeleo," majaji hao wameamua.

Walalamishi walikuwa wameomba waachiliwe huru kwenye rufaa yao walipoiwasilisha mwaka 2015 lakini majaji wamesema hilo limepitwa na wakati kwani wawili hao waliachiliwa kupitia msamaha wa rais.

Tanzania imetakiwa "kuchukua hatua zote ziwezekanavyo kurejesha haki za walalamishi."

Walalamishi walikuwa wamewasilisha ombi la uamuzi kuhusu kulipwa fidia lakini majaji wamesema hakuna aliyewasilisha hoja kwa maandishi kuhusu ulipaji fidia.

Walalamishi wametakiwa kuwasilisha hoja yao katika kipindi cha siku 40 nayo serikali ya Tanzania ijibu katika siku 40 baada ya kuwasilishwa kwa hoja hiyo.

Bw Nguza na mwanaye walikuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa kuwabaka wasichana 10 wa shule waliokuwa na kati ya umri wa miaka 6 na 8 mwaka 2003 na walikuwa wametumikia kifungo cha miaka 13 kufikia wakati wa kupewa msamaha.

Babu Seya ambaye ni miongoni mwa wafungwa 1,821 waliosamehewa na Rais John Magufuli siku ya Uhuru wa Tanganyika mnamo 9 Desemba, 2017.

Wengine 8,157 walipunguziwa adhabu zao.

Wawili hao ndio walioimba kibao maarufu cha 'Seya' na walikuwa kati ya wafungwa 61 waliokuwa wamehukumiwa kufungwa maisha au kunyonga ambao walinufaika kutokana na msamaha wa rais.

Hukumu katika kesi yao ilikuwa imepangiwa kusomwa Jumatano wiki hii lakini baadaye ikaahirishwa hadi leo.

Hatua ya Dkt Magufuli kuwasamehea wawili hao ilishutumiwa na watetezi wa haki za watoto na wanawake.

Kate McAlpine, mkurugenzi wa shirika la Community for Children Rights lenye makao yake Arusha aliambia BBC wakati huo kwamba alikuwa "ameshtushwa lakini hakushangazwa" na hatua ya rais huyo. Alisema hatua hiyo ilionesha 'uelewa mdogo' wa kiongozi huyo kuhusu masuala ya udhalilishaji wa watoto.

Nguza Viking na wanawe walipokutana na MagufuliHaki miliki ya pichaIKULU
Image caption
Nguza Viking na wanawe walipokutana na Magufuli
Alilinganisha hatua hiyo na tamko la Rais Magufuli kwamba wasichana wanaoshika mimba hawafai kuwa shuleni.

Matamshi ya Magufuli yawakasirisha wanawake Tanzania
"Huwa hafahamu vyema mambo, hasa yanayohusu watoto kama waathiriwa. Wasichana wanaoenda shule hushika mimba kwa sababu mara nyingi ni waathiriwa wa udhalilishaji," alisema Bi McAlpine.

Ilikuwaje hadi tukafika hapa?
Nguza Viking na Johnson Nguza ni baba na mwanaye na ni raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambao walikuwa wanamuziki Dar es Salaam.

Wote walikamatwa 12 Oktoba, 2003 na kuzuiliwa kituo cha polisi cha Magomeni ambapo baadaye walifikishwa kizimbani Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu 16 Oktoba, 2003 na kufunguliwa mashtaka 10 ya ubakaji na 11 ya ulawiti.

Waathiriwa wao walikuwa watoto wa kati ya miaka sita na nane, na walikuwa wote kutoka darasa moja.

Waathiriwa hao walidaiwa kubakwa na kulawitiwa kwa zamu na wanaume watano.

Mnamo 25 Juni, 2004 hakimu aliwapata na hatia na kuwafunga jela Nguza na wanawe watatu. Mshtakiwa wa nne, ambaye alikuwa mwalimu, alipatikana bila hatia.

Washtakiwa walikata rufaa Mahakama Kuu lakini rufaa yao ikatupwa.

Walikata rufaa tena katika Mahakama ya Rufaa.

Mwaka 2010 rufaa yao ilisikilizwa na 30 Oktoba Majaji Nathalia Kimaro, akisaidiana na Mbarouk Mbarouk na Salum Masati katika Mahakama ya Rufaa wakawaachilia huru Nguza Mashine na Francis Nguza baada ya kuwapata bila hatia.

Babu Seya na mwanaye Papii Kocha walipatikana na hatia na hivyo kuendelea kutumikia adhabu ya kifungo cha maisha jela.

Majaji walisema kuwa kuna uthibitisho kuwa warufani hao wawili waliwabaka watoto wa shule ya msingi mwaka 2003.

Kesi hiyo iliwashtua mashabiki wa mwanamuziki Viking nchini Tanzania, na kanda nzima ya Afrika Mashariki.

Mwanamuziki huyo mwenye kuimba nyimbo za rhumba, ambaye ni mzaliwa wa DRC, ameishi Tanzania kwa miaka mingi na kuwa na mashabiki wengi.

Zitto Kuliburuza Jeshi la Polisi Mahakamani

$
0
0
Zitto Kuliburuza Jeshi la Polisi Mahakamani
Mahakama Kuu Kanda ya Dsm imepanga tarehe ya kusikiliza kesi iliyofunguliwa na Chama cha ACT Wazalendo kinachoongozwa na Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe dhidi ya jeshi la polisi ambapo itatangazwa Aprili 5.


Taarifa iliyotolewa na Afisa Habari, ACT Wazalendo ndg Abdallah Khamisi, imesema kuwa Chama hicho kilifungua  kesi ya Madai Na. 8/2018 Mahakama Kuu hapa Dar Es Salaam, kulishtaki Jeshi la Polisi, kutokana na Jeshi hilo kuingilia, visivyo halali shughuli za ziara yao ya kichama.

Mahakama imeipangia tarehe kesi husika, itasikilizwa kwa mara ya kwanza, Aprili 5, 2018 chini ya Majaji watatu, Jaji Ferdinand Wambari,  Jaji Sameja na Jaji Rose Teemba.

Hivi karibuni Msafara wa ACT Wazalendo ukiongozwa na kiongozi wa chama mkoani Morogoro uliripotiwa kuzuiliwa kwa muda kufanya shughuli zao za kichama katika kata wanazoziongoza.

Hali Sio Shwari Takwimu Zaonyesha watu 77 Wanakufa kwa Siku Tanzania Kutokana na Hili!!

$
0
0

Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani WHO Watu 77 hufariki dunia kila siku Tanzania kutokana na ugonjwa wa kifua Kikuu huku mkoa wa Dar-es-salaam ukitajwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaougua ugonjwa huo kwa asilimia 20.

Akizungumza na Waandishi wa habari Dodoma leo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu  amesema kutokana na hali hiyo zaidi ya shilingi milioni 35 zinatumika kugharamia matibabu ya mgonjwa wa kifua kikuu sugu.

Waziri Ummy Amewasisitiza wananchi kuwa TB inatibika na dawa zake zinatolewa bure katika vituo vya umma na binafsi nchini na kueleza jitihada zinazochukuliwa na serikali katika kukabiliana na ugonjwa huo ikiwemo kuimarisha mfumo wa uchunguzi na ugunduzi wa TB.

Wafungwa 740 Kuachiwa Huru

$
0
0

Umoja wa Ulaya upongeza serikali ya Burundi kwa kuwaacha huru wafungwa wapatao 740 waliokuwa wamekamatwa tangu mwaka 2015  kufuatia ghasia na vurugu zilizosababishwa na maandamano na jaribio la mapinduzi.

Mjumbe maalumu wa Umoja wa Ulaya nchini Burundi amepongeza uamuzi wa wizara ya sheria nchini humo kwa kuwaacha huru wafungwa 740 waliokuwa wamekamtwa katika matukio tofauti kufuatia jaribio la mapinduzi. Miongoni mwa watu walioachiwa huru, 450 walihusika na matukio ya mwaka 2015.

Taarifa hiyo ilitolewa katika tovuti ya Umoja wa Ulaya na kuomba vijana wachwe huru vijana wote waliokamatwa katika maandamano ya mwaka 2015.

Serikali Yawachagulia Wananchi Kifo

$
0
0

Serikali ya nchini Austria jana ilipiga kura kupinga katazo la kutouzwa na kuvuta sigara kwenye migahawa na baa nchini humo ambalo lilikuwa limewekwa na serikali iliyopita ya nchi hiyo, hii ikimaanisha sigara zitauzwa na kuvutwa kama kawaida maeneo hayo.

Utekelezwaji wa jambo hili utaanza rasmi mwezi May mwaka huu. Wabunge wameeleza kuwa jambo hilo linalenga kulinda ‘uhuru wa kuchagua’ wa wananchi wa Austria huku pia ikilinda maslahi ya wenye biashara ya migahawa na bar.

Hata hivyo mwanasiasa mmoja ameeleza kuwa uamuzi huo wa serikali ni kama kufanya maamuzi ya kuwachagulia kifo wananchi wa nchi hiyo. Inaelezwa kuwa jumla ya watu 13,000 wanakufa nchini humo kwa matatizo ya afya yanayotokana na uvutaji sigara.

Nyangumi Zaidi ya 150 Wafia Ufukweni

$
0
0

Kutoka nchini Australia, leo March 23, 2018 inaelezwa kuwa Nyangumi takribani 150 wamekwama katika ufukwe wa bahari Magharibi mwa Australia na kusababisha kufungwa kwa muda kwa eneo hilo la ufukwe.

Idara ya Uvuvi nchini humo wameeleza kuwa wanahisi nyangumi hao wamekufa na hivyo imebidi wafunge ufukwe huo kwa muda kwa kuhofia papa wanaweza kuleta madhara kwenye eneo hilo.

Idara hiyo imeeleza kuwa papa huvutiwa na viumbe waliokufa hivyo nyangumi hao ambao inaaminika wamekufa wanaweza kufanya papa wasogee eneo hilo la ufukwe na kusababisha madhara makubwa zaidi.

Maswali Mengi Yaibuka Baada ya Nisha Bebe Kutupia Picha Akiwa na Ex wa Wolper

$
0
0

Kwenye upande wa mitandao ya kijamii picha na videos ambazo zimekuwa ziki-trend ni za muigizaji Nisha Bebe na aliyekuwa mpenzi wa muigizaji Jaquline Wolper ambaye ni Brown na kusemekana kuwa ni wapenzi wapya.

Tetesi hizo zimeendelea kuhusu wawili hao kuwa wapo katika mahusiano ya kimapenzi kutokana na videos zinazosambaa wakiwa katika mahaba mazito ingawa wawili hawa hawajasema chochote kuhusiana na hilo mpaka sasa.

Brown alikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na muigazaji Jacquline Wolper kwa kipindi kirefu ila baadae waliachana kutokana na sababu zao binafsi ambazo hawakuziweka wazi.



Shahidi wa Loli la Mafuta Lililowaka Moto Aeleze Break za Gari Zilivyofeli na Matairi Kuanza Kuwaka Moto

$
0
0

Taarifa za kutokea kwa ajali ya lori lililoteketea na moto kwenye Mlima Sekenke mchana huu, mkoani Singida zinaendelea kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari, ambao Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt Mwigulu Nchemba tayari amefika eneo la tukio.

Waziri Mwigulu amefika kuangalia jinsi ajali ya gari hilo la mafuta lilivyoanguka na kuwaka moto na kusababisha vifo vya watu wawili ambao wameungua sana kiasi cha kutotambuliwa hadi sasa huku jitihada zinaendelea kuwatambua.

Kwa mujibu wa shuhuda Edward Lameck, 16, aliyekuwa anapita eneo hilo amesema gari hilo lilifeli break na matairi ya mbele kuanza kuwaka moto hali iliyosababisha gari hilo kutumbukia bondeni na kuwaka moto.

Inaelezwa kuwa imeshindikana watu hao kuokolewa kutokana na kutokana moto mkubwa uliokuwa unawaka. Juhudi zinaendelea kutambua mmiliki wa gari ili kufahamu waliokuwa kwenye gari hilo.

VIDEO: Muna Love Kafunguka kuwa Ameokoka, Apatwa na Kigugumizi Kuhusu Kuzaa na Casto

$
0
0

Muna Love ambaye jina lake ni Rose amezungumza na kusema kuwa yeye ameokoka na mtu aliyesababisha yeye kuokoka ni mwanae Patrick ambaye inasemekana amezaa na mtangazaji wa Clouds Tv Casto Dickson japo hakutaka kuzungumza lolote kuhusu Casto wala kile kinachoendelea kweye mitandao kati ya Casto na Tunda.



Kompyuta Ndogo Zaidi Duniani Yatengenezwa

$
0
0

Kampuni ya IBM ya Marekani imetangaza kuwa imetengeneza kompyuta ndogo zaidi duniani ambayo ni ndogo zaidi kuliko kidonge kikubwa cha chumvi.

Taasisi hiyo IBM imefahamisha kuwa  kompyuta hiyo ina upana wa milimita 1, inaweza kuchunguza, kuchambua, kutuma na hata kutekeleza data.

Kompyuta hiyo inatumia betri ya nishati ya jua (Solar) ina kumbukumbu iliyotulia isiyo na mpangilio maalumu SRAM, na inafanya mawasiliano kupitia LED.

Kampuni hiyo imeonesha kompyuta hiyo kwenye mkutano wa Think 2018 ulioisha March 22 huko Las Vegas, Marekani, itawekwa kwenye bidhaa ili kurekodi ujumbe mbalimbali kuhusu uzalishaji wa bidhaa hizo. Teknolojia hii itakuwa njia mpya ya kuhakikisha usalama wa vyakula, kuthibitisha bidhaa halisi na feki, na kurekodi viwanda vinavyozalisha bidhaa za anasa.

Kabla ya hapo, kompyuta iliyotengenezwa na chuo kikuu cha Michigan iitwayo “Michigan Micro Mote” yenye upana wa milimita 2 ilikuwa kompyuta ndogo zaidi duniani.


Viongozi 13 Wahukumiwa Jela Miaka 30 Kisa Hiki Hapa

$
0
0

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Juu Hispania amewasomea hukumu viongozi 13 wakubwa wa Jimbo la Catalonia nchini Hispania, wakikabiliwa na mashtaka ya uasi juu ya majukumu yao katika kura ya maoni na tamko la uhuru mwaka 2017.

Jaji huyo Pablo Llarena amewahukumu miaka 30 jela viongozi hao ikiwa ni pamoja na Rais Mstaafu wa Jimbo hilo Carles Puigdemont na Jordi Turul ambaye kesho anatarajiwa kupigiwa kura ya kuchukua nafasi hiyo.

Ameeleza kuwa viongozi hao kwa kushirikiana na vikundi vya asasi za kijamii kwa miaka sita iliyopita wamefanya njama kusuka mpango wa kutangaza Uhuru wa Catalonia, jambo lililo kinyume na utaratibu wa kisheria nchini Hispania.

Mahakama imetoa hukumu hiyo leo March 23, 2018 na kusema kwa ujumla imetoa hukumu hiyo kwa makosa ya kuasi, rushwa na kutotii kwa viongozi hao.

Hii Ndiyo Hukumu Aliyopewa Binti ‘Aliyewachapa’ makofi wanajeshi

$
0
0

Katikati ya mwezi December 2017 hadi mwishoni kabisa ya mwaka, binti wa Kipalestina Ahed Tamimi, 17, alikuwa gumzo mitandaoni na kwenye vyombo vya habari vya kimataifa baada ya kusambaza video iliyomwonesha akiwapiga makofi wanajeshi wawili.

Sasa jana March 21, 2018 imetolewa hukumu juu ya binti huyo, ambapo amehukumiwa kifungo cha miezi nane jela kutokana na kosa hilo la kuwapiga wanajeshi.

Katika video hiyo Ahed alionekana akiwapiga askari hao ambao walikuwa wamekwenda kwenye eneo la makazi yao, ambapo binti huyo kwa ujasiri alionekana kuwapiga makofi huku akiwaambia waondoke kwenye eneo hilo.

Madaktari Wamchoma Mtoto Sindano Kichwani Kimakosa Chaanza Kuoza

$
0
0

Stori ninayokusogezea ni kuhusu matukio ya kutokuwa makini katika idara ya afya hasa kwa madaktari yanazidi kuzua wasiwasi kwa wananchi nchini Kenya, tukio lililotokea siku za hivi karibuni  ni la mtoto kuchomwa dawa isiyofaa na kumfanya aanze kuoza kichwa.

Tukio hili lilianyika katika hospitali ya Malava General Hospital katika jimbo la Kakamega na lilitokea huku kukiwa na kesi dhidi ya Madaktari wa hospital ya Kenyatta  baada ya Daktari kumfanyia upasuaji mgonjwa asiyestahili.

Mtoto huyo aliyejulikana kwa  jina Clinton Luchivya alikuwa amepelekwa katika hospitali hiyo baada ya kuwa mgonjwa na madaktari kumchoma kichwani baada ya kukosa mshipa wa kumwekea dawa.

Kulingana na mama wa mtoto huyo, mwanae alikuwa na ugonjwa wa Malaria kabla ya kupokea matibabu katika hospitali hiyo.  Alisema kuwa mwanae alikuwa ameanza kubadilika badilika kabla ya kufahamu kuwa kichwa chake kinaoza.

Tafiti Zonyesha Kuwa Demokrasia Ipo Matatani Duniani

$
0
0

Utafiti mpya ambao umefanywa siku za hivi karibuni na kampuni ya Kijerumani inayojulikana kama Bertelsmann Foundation, ambao umeangalia mataifa 129 duniani umebaini kuwa demokrasia inazidi kushuka kwenye mataifa mbalimbali duniani.

Inaelezwa kuwa ubora wa demokrasia na mifumo ya uchumi wa masoko katika nchi zinazoendelea unaendelea kushuka kwa kiwango cha chini zaidi katika miaka 12 iliyopita, hii ni kwa mujibu wa utafiti huo ambao wameupa jina Mpango wa Mabadiliko (Transformation Index 2018).

Ripoti hiyo imeangalia katika nchi hizo 129 maeneo kama demokrasia, uchumi, utawala. Watafiti hao wameonya kuwa demokrasia iko “chini ya shinikizo” huku ukandamizaji na unyanyasaji wa kisiasa ukiongezeka.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images