Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715 

Maua Sama atoa sababu za kuachia picha hizi tata

$
0
0

Msanii Maua Sama ameeleza sababu ya kuachia picha ambazo si za kawaida kabisa kutoka kwake,
Picha hizo ambazo zilimuacha wazi sehemu kubwa ya mapaja yake aliziweka mtandaoni kati ya February 19 na 22 mwaka huu.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma mpya ‘Nakuelewa’ ameiambia FNL ya EATV kuwa aliachia picha hizo kwa ajili ya ujio wake mpya na pia amefanya hivyo kuonyesha uzoefu wake katika muziki.

“Kiukweli ni photo shoot ambayo nilikuwa nahitaji kwa sababu nilikaa kimya sana,” amesema.

“Kuna ule ugeni sasa umeisha, hivyo nilikuwa mgeni nilikuwa sijui vitu vingi, nilikuwa sijui kwenye muziki natakiwa nifanye nini, kidogo kidogo nikaanza kuzoea mwisho wa siku nikawa vile nilivyokuwa nataka,” amesema.

Licha ya kuwa muimbaji mzuri katika nyimbo zake Maua Sama amekuwa miongoni mwa ma-chorus killer wazuri kwa hapa Bongo, mwishoni wa mwaka jana alisikika katika chorus ya ngoma ya Mwana FA ‘Sielewi’ na ile ya Roma na Stamina (Rostam) itwayo Kiba_100.

Mwadhama Kadinali Polycarp Pengo aukana Waraka wa Pasaka wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki

$
0
0

Mwadhama Kadinali Polycap Pengo amesema hakuwa anajua kama kuna waraka utatolewa kuhusu kwaresma na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania huku akisema waraka huo una mazuri mengi japo umechanganya dini na siasa.

Kadinali Pengo ameyasema hayo wakati akiadhimisha ibada ya Jumapili ya matawi huko Bagamoyo katika tamasha la vijana.

"Katika wiki chache zilizopita watu wamekuja kwangu wakaniuliza unaionaje ile barua ya Maaskofu kuhusu Kwaresma mwaka huu? Ninazungumzia hilo na wala mtu asiende aka-quote kitu kingine ndio maana nataka kusema wazi kabisa:-

"Barua ile ijapokuwa hata jina langu mnaliona limeandikwa pale kwamba na mimi ni mmoja wa waandishi au watamkaji...mimi nimeipokea, baadhi yenu mmeshaipokea.

" Kwahiyo sioni namna gani mimi naweza kuwa mwandishi au mhubiri kwenu wa ile barua ambayo imetungwa labda na maaskofu...naamini na baadhi ya maaskofu lakini mimi mwenyewe hata nilikuwa sijaiona, hata nilikuwa sijaambiwa kuna kitu cha namna hiyo kinakuja.

"Tuelewane vizuri, ninaposema hivi sitaki kusema ile barua ni mbaya. Moja tu ni kwamba barua nzima imechanganya vitu viwili; Mwalimu angekuwepo angepiga kelele Maaskofu msichanganye Dini na Siasa.

"Angepiga kelele sana kuhusu waraka huu katika nyakati zake. Na hilo nawambia sina hofu, muende mkamwambie mtu yeyote nimesema hivi. Ndio wala msione aibu, najua labda hata wengine mmekunja nyuso, kunjeni tu lakini huo ndio msimamo wangu.

"Zipo sehemu katika waraka huo zinazochanganya Dini na Siasa na si kazi ya maaskofu ni kazi yenu wanasiasa mkiwa ni wa CHADEMA, mkiwa ni wa CCM lakini haiwezi kuwa kazi yangu mimi.

"Siwezi kwanza nikaanza kuchambua na ku-criticize Serikali katika mambo yaliyo yake; sikupewa mamlaka hayo. Na kwanini niwe padri mpaka nikubali kuwa Askofu na huku kumbe wito wangu ni siasa?

"Itakuwa namsaliti hata yule aliyenipa wito huu. Tuchambue yale yanayohusu imani yetu katika ule waraka. Yale ambayo moja kwa moja yanahusu imani yetu Katoliki na tuyashike tuyazingatie kwa dhati kabisa.

"Lakini yale ya kuanza kusema Serikali ya awamu ya 5 inagandamiza uhuru inafanya nini...wewe Askofu uhuru wa kisiasa umeujua wapi? Umeujuaje? Na mambo ya ndani ya kisiasa huyajui na bado uje kutamka...nadhani tumeelewana.

"Yapo yaliyo mema mazuri kabisa katika waraka ule ingawaje sikujuia kama yameandikwa lakini siwezi kukataa yaliyo mema kwa sababu sikujua.

"Yanaendelea kuwa mema mpaka kesho na keshokutwa. Lakini yale ambayo yanachanganya Dini na Siasa hayo siwezi kuyakubali.

"Nyerere alifanya indoctrination kubwa mno kwa watu wa umri wetu. Mtu huwezi ukathubutu na ukalala salama usiku. Watu wa umri wangu ukichanganya dini na siasa utaota vitu vya ajabu utakosa usingizi(vicheko)

"Sasa ninyi vijana ninalotaka ni hili kwamba na ninyi mkichanganya dini na siasa muote vitu vibaya kama hivyo..muote vitu vibaya kabisa hata muone mnachungulia kaburi katika ndoto.

"Sisi sio wanasiasa tunahitaji wanasisia mtuendelee wale tunaokuwa wito huo. Wale tunaotaka kuwa mama wakuu, mababa padri, maaskofu. Fuateni wito kulingana na misimamo yake ya kiimani."

Mange Kimambi Atabiri Roma Mkatoliki Kuhamia CCM Kama Alivyotabiri Wema Kuhama na Ikawa

$
0
0

ANAYO ENDELEA MTANDAONI :
Unakumbuka kabla ya wema sepetu kurudi ccm Mange Kimambi aliandika kwenye page yake ya instagram na kutoa sababu mbili nzito zilizomfanya Wema kurudi CCM?

Awamu hii kamuibukia Roma Mkatoliki, anadai mda wowote anajiunga CCM

Muonekano wa sasa wa Abdul Nondo Anayeonekana Katikati amesimama

$
0
0

Muonekano wa sasa wa Abdul Nondo Anayeonekana Katikati amesimama ...Afya yake Inaonekana kudhoofu Kwa kukaa Lupango Muda Mrefu.

Dr. Tulia Azitaka Shule Binafsi Kusaidia Watoto Wenye Uhitaji

$
0
0
Dr. Tulia Azitaka Shule Binafsi Kusaidia Watoto Wenye Uhitaji
Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzanira Dr. Tulia Akson ameotoa wito kwa shule zote nchini hususani shule binafsi kujikita kusaidia watoto wenye uhitaji maalumu,kwa lengo la kuwawezesha kupata elimu jumuishi ili kuwafanya wajione sawa na watoto wengine na wenye umuhimu katika jamii.



Hayo yamesemwa leo na Naibu Spika wa Bunge katika matembezi ya siku ya Usonji Duniani yaliyoandaliwa na Shule ya Al Muntazir jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo wabunge ,yaliyobebaba kauli mbiu isemayo “TUWAPENDE NA TUWALIDE”.

Makumu MKuu wa Shule ya wasichana Almuntazir Mrs. Joan Soka akitoa utaratibu wa shughuli mbalimbali katika

Aidha Dr, Tulia amesema watoto wenye uhitaji maalumu wana haki sawa na wengine hivyo amezitaka shule binafsi kuweza kutoa mafunzo hayo kwa watoto wenye uhitaji maalumu kama inavyofanywa na Shule za Al Muntazir kwani itasaidia kuelimisha jamii kuhusu Usonji,(Autism) pamoja na kuwawezesha kuona kuwa watoto hawa wana haki ya kupata elimu na kuthaminiwa kama wengine.

” Jamii inapaswa kuwajali , kuwapenda na kuwalinda watoto wenye uhitaji maalumu wanauwezo wa kuelewa na kufanya vizuri darasani hata katika kazi mbalimbali kama kuchora kupaka rangi na wakifundishwa wanaweza hivyo jamii inapaswa kuwaona ni watoto wenye umuhimu kwa jamii hivyo wakiwezeshwa wanaweza kufanya zaidi”amesema

Watoto wenye usonji wakitoa burudani

Aidha Naibu Spika amewashauri viongozi wa Shule za Al Muntazir kujenga mabweni ya kuwawezesha watoto hao kupata sehemu ya malazi ili kuwawezesha watoto wenye uhitaji maalumu kutoka katika maeneo ya mbali kupata sehemu ya kulala,vilevile amezitaka Taasisi mbalimbali kujitokeza kutoa michango yao ili kuwawezesha watoto hao wasiokuwa na uwezo wa kuchangia gharama waweze kupata fursa ya elimu.

Spika wa bunge Dr Tulia akiteta jambo na rais wa shule za Al Muntazer.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dr. Faustin Ndungulile ameishukuru shule hiyo kwa kuanzisha kitengo cha watoto maalumu na kuona umuhimu wa watoto hao kuwa wana haki ya kupata elimu kama wengine hivyo ameahidi Serikali itashirikiana kikamilifu endapo watahitajika.

Naye Mkurugenzi wa Shule za Al Muntazir Mahmood Ladak amewashukuru viongozi wa seikali pamoja na wazazi waliojitokeza katika matembezi hayo, na kusema lengo la matembezi hayo ilikuwa ni kuielimisha jamii kuhusu Usonji (AUTISM),na kuwapenda kuwathamini watoto wenye uhitaji maalumu,kwani wana haki ya kupata elimu kama watoto wengine.

Maalim Seif: Hatima ya CUF Ipo Mikononi mwa Mahakama

$
0
0
Maalim Seif: Hatima ya CUF Ipo Mikononi mwa Mahakama
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema hatima ya mgogoro ndani ya chama hicho ipo mikononi mwa Mahakama ikiwa watashinda kesi yao iliyopo mahakamani.

Amesema hiyo ndiyo njia pekee itakayoirejesha CUF kuwa taasisi imara na chama kimoja kama ilivyokuwa awali.

Amesema kwa sasa CUF imeshindwa kushiriki shughuli za uchaguzi nje ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutokana na hujuma alizodai kufanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec).

Maalim Seif ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Machi 26,2018  jijini  Dar es Salaam wakati akisoma maazimio manne ya Kamati ya Utendaji ya Taifa ya chama hicho iliyokutana jana.

 “Mahakama  ni chombo cha haki pekee tunachotegemea. Wanaosema Mahakama inapendelea siyo kweli, tunajua mabadiliko ni makubwa, kila jaji  anataka aonekane akitenda haki.”

Amedai kuwa baada ya Mahakama kuwarudishia uanachama wabunge nane waliofukuzwa na Profesa Lipumba, mawakili wao wanafuatilia  kisheria ili kurejesha haki ya ubunge wa viti maalumu kwa wanachama hao.

Maalim Seif  aliyekuwa ameongozana na baadhi ya viongozi, amesema kamati hiyo imewataka wanachama wake kuwatenga wasaliti wote wanaomuunga mkono mwenyekiti huyo.

Kauli ya Anayetaka Kumrithi Tundu Lissu “Nitatoa Heka Kumi”

$
0
0
Kauli ya Anayetaka Kumrithi Tundu Lissu “Nitatoa Heka Kumi”
Ikiwa zimesalia siku kadhaa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kufanya uchaguzi wa kumpata Rais wake mpya ambaye atarithi nafasi ya Rais wa sasa anayekaribia kumaliza muda wake Tundu Lissu baadhi ya wanaowania nafasi hiyo wameshaanza kampeni zao katika maeneo mbalimbali. Ikumbukwe kwamba kwa mujibu wa sheria uchaguzi wa TLS hufanyika kila baada ya mwaka mmoja.

Miongoni mwa wagombea hao leo tunaye Godfrey Wasonga ambaye aliita Waandishi wa habari ofisini kwake Dodoma na kuelezea mikakati yake endapo atapata nafasi hiyo.

Wasonga amesema …>>>”Nimekuwa na maono ya nafasi hii kwa muda mrefu sana na naamini huu ndio wakati muafaka, endapo nitachaguliwa kwanza nitahakikisha tunaiomba Serikali ibadilishe sheria ili uchaguzi huu uwe unafanyika kila baada ya miaka mitatu na sio mwaka mmoja kama ilivyo sasa”- Godfrey Wasonga

“Kwa kuanzia nikipata nafasi hii nitatoa ardhi ya heka kumi katika eneo lililo karibu na inapojengwa Ikulu ya nchi kwa ajili ya sisi kujenga makao makuu ya chama chetu cha TLS na nitashawishi baadhi ya watumishi kuhamia Dodoma” – Godfrey Wasonga

Polisi Yamdaka Anayewapiga Picha za Utupu Wanawake na Kuzisambaza Mitandaoni

$
0
0
Polisi Yamdaka Anayewapiga Picha za Utupu Wanawake na Kuzisambaza Mitandaoni
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limemkamata mkazi wa mjini humo, Mabula Mabula maarufi Six kwa tuhuma za uporaji wa simu kwa kutumia pikipiki, kubaka na kuwapiga picha za utupu wanawake kisha kuzisambaza mitandaoni.

Akizungumza leo Jumatatu Machi 26, 2018, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ulrich Matei amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa baada ya makachero, kikosi cha kupambana na uhalifu  mitandaoni pamoja na kikosi cha kupambana na ujambazi, kumfuatilia kwa ukaribu.

Akihojiwa mara baada ya kukamatwa, Mabula ameeleza mbinu anazotumia ikiwa ni pamoja na kujifanya askari polisi, kuwakamata wanawake nyakati za usiku, kuwasingizia makosa mbalimbali na kuwapeleka maeneo yenye giza na kuwabaka.

Mtuhumiwa huyo ameyataja maeneo anayofanyia matendo hayo kuwa ni Msamvu Relini na kwamba amekuwa akitumia mapanga kuwatisha wanawake hao na kuwapiga picha za utupu na baadaye kutishia picha hizo kuzituma kwenye mitandao ya kijamii.

“Hizo picha huwa nawapiga kwa kutumia simu zao na anayekataa kunipa hela huwa naondoka na simu yake na kisha natuma hizo picha kwenye mitandao iliyopo kwenye simu hizo, baada ya hapo simu naiuza napata hela,” amesema mtuhumiwa huyo.

Katika  mahojiano na polisi, mtuhumiwa huyo amemtaja mwezake mmoja Ramadhani Salumu maarufu Miondoko mkazi wa Manispaa ya Morogoro kuwa ndio mnunuzi wa simu hizo za wizi.

Katika msako huo polisi wamefanikiwa kumkamata Salumu na kwamba wote watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.

TCRA Kutoa Hatima ya Times Fm Maojiano na Diamond Wiki Hii

$
0
0
TCRA Kutoa Hatima ya Times Fm Maojiano na Diamond Wiki Hii
Hatima ya Kituo cha Redio Times cha jijini Dar es Salaam kilichotakiwa kuwasilisha kipindi cha mahojiano waliyoyafanya na mwanamuziki Diamond Platinumz kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa ajili ya uchunguzi zaidi, itajulikana wiki hii.

Taarifa zilizoifikia MCL Digital leo Jumatatu Machi 26, 2018 zinaeleza kuwa kamati ya maudhui ya TCRA iliyokuwa ikifanya uchunguzi huo inakaribia kumaliza kazi hiyo.

Machi 22, 2018, Times ilipokea barua ya kuwataka wawasilishe kipindi hicho kilichorushwa Machi 19, 2018 na kutii agizo hilo.

Mwanamuzi Diamond alizua mjadala baada ya kuzungumzia suala la nyimbo za wasanii hao kufungiwa akimlalamikia Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kutowatendea haki wasanii.

Ofisa Mkuu Idara ya Utangazaji wa mamlaka hiyo, Andrew Kisaka ameieleza MCL Digital leo kwamba tayari kamati ya maudhui inakaribia kumaliza kazi yake ya kupitia maudhui ya kipindi hicho.
chanzo: Mwananchi

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.

Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi
+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Abdul Nondo Afunguka Baada ya Kuachiwa kwa Dhamana

$
0
0

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) Abdul Nondo kwa mra ya kwanza amefunguka na kuwashukuru watanzania baada ya kuachiwa kwa dhamana katika mahakama ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Iringa leo Machi 26, 2018

Nondo ameweka wazi hayo baada ya kuachiwa huru na kusema kuwa sasa anaweza kuendelea na masomo yake pamoja na kesi hiyo ambayo itakuwa ikiendelea mkoani Iringa.

"Namshukuru sana wakili Jebra Kombole na wakili wangu mwingine wa Iringa mbali na hapo napenda kuwashukuru wadhamini wangu kwa sababu masharti ya dhamana yalikuwa yanahitaji wadhamini kutoka mkoa wa Iringa kwa hiyo nimepata wadhamini mkoa wa Iringa Mungu awabariki sana, saizi nipo huru naweza kwenda kuendelea na chuo huku nikiendelea na kesi mkoa wa Iringa. Pia nawashukuru Afisa Magereza kwenye eneo ambalo nilikuwa nikiishi katika kusubiria dhamana wamenitunza vizuri kwa upendo na ushirikiano mkubwa hivyo nawashukuru wazazi wangu na Watanzania Mungu awabariki sina zaidi ya zaidi ya hayo" alisema Nondo

Kesi ya Abdul Nondo itatajwa tena tarehe 10 mwezi wa nne mwaka huu mkoani Iringa ambapo wataanza kusikiliza hoja za awali, wakili wa Nondo amewataka watanzani kuwa na subira juu ya jambo hilo kwa kuwa tayari lipo mahakamani hivyo litafahamika.

MAREKANI: Rais Trump ametoa amri ya kufukuzwa kwa wanadiplomasia 60 wa Kirusi

$
0
0

MAREKANI: Rais Trump ametoa amri ya kufukuzwa kwa wanadiplomasia 60 wa Kirusi, kufuatia Urusi kuhusishwa na shambulio la sumu kwa Jasusi wa zamani raia wa Urusi nchini Uingereza

Tayari nchi za kadhaa za Ulaya zikiwemo Ujerumani, Ufaransa na Ukraine zimetangaza kuwafukuza wanadiplomasia wa Kirusi katika nchi zao

Viongozi wa EU walikubaliana wiki iliyopita kuwa inawezekana sana Urusi ilihusika katika shambulio la sumu la Sergei Skripal(Jasusi) na binti yake kusini mwa Uingereza

Hata hivyo, Urusi imepinga kuhusika na shambulio hilo

Mwanasheria Miguna Miguna Akataliwa Kuingia Kenya

$
0
0

Mwanasheria wa upande wa upinzani wa Kenya,Miguna Miguna amekataliwa kuingia Kenya baada ya kukataa kuomba Visa, gazeti binafsi la The Star la ripoti.

Bwana Miguna anasafiri kwa kutumia kibali chake cha kusafiria cha Canada baada ya kuvuliwa uraia wa Kenya.

Mamlaka ya Kenya ilimrudisha Canada baada ya kushiriki katika kuapishwa kwa kiongozi wa upinzani Raila Odinga kama "Rais wa watu".

Wiki iliyopita Miguna aliiambia BBC kuwa mamlaka ya Kenya haijafuata maagizo ya mahakama ya kumpatia hati za kusafiria za Kenya.

Serikali ya Kenya ilimvua uraia Miguna na kumrudisha Canada ambapo pia ni raia huko.

Mahakama ya kenya ilitoa amri kwa serikali hiyo kurudisha hati za kusafiria za Miguna na kusaidia katika kurejea kwake lakini kwa mujibu wa Miguna serikali haija fanya hivyo.

Mwandishi wa BBC Ferdinand Omondi ambaye alikwenda katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta amesema vyanzo vinasema serikali inataka kumpa visa ya muda wa miezi sita na kuchukua pasipoti yake.

Waandishi wa habari wa Kenya wamekusanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta uliopo Nairobi, ili kupata taarifa ya ujio wa wakili huyo wa upinzani Miguna Miguna ambaye aliondolewa Kenya tangu tarehe 6 mwezi Februari mwaka huu.

Maalim Seif Alipongeza Baraza la Maaskofufu KKKT

$
0
0

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amelipongeza Baraza la Maaskofu la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kwa kutoa waraka mzito wa ujumbe wa Sikukuu ya Pasaka.

Waraka huo ulitolewa mwishoni wa wiki iliyopita ambao mbali na kuzungumzia masuala ya kiroho, umetaja changamoto tatu na kuzifikisha kwa waumini wake “ili ziongeze mzigo wa kuliombea taifa letu na viongozi wake.”

Changamoto zilizotajwa katika waraka huo uliopewa jina la “Taifa Letu Amani Yetu” na kusainiwa na maaskofu 27 wa kanisa hilo nchini ni hali ya kijamii na kiuchumi, maisha ya siasa na masuala mtambuka likiwamo suala la Katiba Mpya.

Akizungumza leo Machi 26, 2018 jijini Dar es salaam wakati akisoma maazimio manne ya Kamati ya Utendaji ya Taifa ya chama hicho iliyokutana leo, Maalim Seif amesema anafarijika kuona  viongozi wa dini  wanakemea mambo ambayo hayaendi sawa nchini.

"Nimefarijika kuona viongozi wa taasisi za dini wakizungumza pale ambao wanaona mambo hayaendi sawa. Tusitafsiri  kwamba wanafanya siasa, hapana ni haki yao kukemea, "amesema Maalim Seif.

Amesema angetamani kuona viongozi wengine wa dini  wakionyesha misimamo kama maaskofu hao.


Irene Amtupia Dongo Zito Wema Sepetu

$
0
0

Video vixen aliye jizolea umaarufu baada ya kuonekana kwenye video ya ‘Kwetu’ ya msanii Rayvanny Irene, amemtolea povu zito staa wa Bongo movie Wema Sepetu huku ikidaiwa kisa ni penzi la Diamond.

Tangu Zari aweke wazi kuwa kaachana na Diamond na kuwa single Kumekuwa na tetesi nyingi sana kwenye social media juu ya nani hasa anayechukua nafasi ya Zari na moja kati ya Wanawake waliotajwa kuwa na uhusiano na Diamond kwa sasa ni Irene na Wema.

Kuna stori ili trend sana kwenye mitandao ya kijamii siku za nyuma kidogo ambapo ilisemekana kuwa Irene na Wema wamepeana kichapo cha maana baada ya kugongana Madale nyumbani kwa Diamond.

Stori hiyo ilidai kuwa Diamond anatoka na Irene na Wema kwa wakati mmoja na wikiendi hii Irene kamtupia dongo Wema ambapo amemcheka kuwa anajiita African beauty wakati hata kiwanja hana!.

African beauty ni wimbo mpya wa Diamond na siku wimbo huo ulipotoka wasanii mbali mbali wa WCB akiwemo Harmonize alimtunuku Wema jina la African beauty jambo ambalo lilimfanya Wema ajitambe kuwa ni African beauty.

Fununu za Irene kuwa na Mahusiano na Diamond zilianza siku nyingi sana wakati bado Diamond yuko na Zari ingawa Diamond alikuwa anakataa kuwa hana Mahusiano naye.


Breaking News: Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Chamsimamisha Masomo Abdul Nondo

$
0
0
Breaking News: Chuo Kikuu cha Dar es Salaam  Chamsimamisha Masomo Abdul Nondo
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa William Anangisye, amemsimamisha masomo Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo hadi kesi yake ya kutoa taarifa za uongo mitandaoni na kudanganya kutekwa itakapomalizika.

Nondo alipewa dhamana na mahakama ya Iringa, jana Jumatatu,Machi 2018 baada ya kusota rumande kwa wiki kadhaa

Pata Huduma za Matibabu ya Asili na Nyota Pamoja na Pete za Bahati

$
0
0
Mtabibu Mongwa husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote
Tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .

Natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
Natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini

Kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa
Kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri piga simu

+255 764291657

Huu Hapa Undani wa Aliyemuua Mkewe na Kumficha Mbuyuni

$
0
0
Huu Hapa Undani wa Aliyemuua Mkewe na Kumficha Mbuyuni
UNDANI wa mwanaume mmoja aliyejulikana kwa jina Bernard Shumba mkazi wa Singida kugundulika na jeshi la polisi mkoani humo kuwa amemuua mke wake miaka minane iliyopita kisha kuufi cha mwili wa marehemu kwenye mbuyu, umeanikwa.



Habari kutoka chanzo cha kuaminika zinasema Shumba alikuwa mara kwa mara akiwa kwenye vilabu alikuwa akigombana na mtu anasema kwamba anaweza kumfanyizia kama alivyomfanya mkewe.



Kutokana na tambo zake hizo raia wema waliamua kuliarifu jeshi la polisi ambalo kwa weledi mkubwa walithibitisha kile alichokuwa akisema Shumba kwani alikwenda kuwaonesha polisi alikomfi cha  mkewe miaka minane iliyopita baada ya kumuua.


“Tuwapongeze polisi kwa kazi nzuri kwa sababu tambo za huyu bwana zimezaa matunda na kuonesha yalipo mabaki ya mkewe,” alisema mtoa taarifa wetu ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe.“Nitoe wito kwa wananchi kwamba, watu wabaya wasifi chiwe siri kama bwana,” alisema.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Deborah Magiligimba, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa baada ya kukamatwa alikiri kutenda kosa hilo na kwenda kuonyesha mwili wa marehemu aliokuwa ameuhifadhi ndani ya mbuyu ambapo jeshi hilo kwa kushirikiana na wananchi limefanikiwa kupata mabaki yake.


“Inadaiwa kuwa mnamo Julai 10, 2010 katika Kijiji “Baada ya 17, 2018 ambapo taarifa zilipopatikana zikidai kuwa alimuua.“Baada ya mtuhumiwa kukamatwa na kuhojiwa alikiri kufanya kitendo hicho na kuonyesha sehemu alipoufi cha mwili huo Machi 18, mwaka huu majira ya saa 10:00 jioni, “ alisema kamanda huyo wa polisi.


Mkuu wa polisi kituo cha Mkalama na timu yake ya makachero walifi ka eneo la tukio na kufanikiwa kupata mabaki ya mifupa yakiwa ndani ya mti huo. Baadhi ya mifupa imechukuliwa kwa ajili ya kupelekwa kwa mkemia wa serikali na iliyobakia ndugu wamekabidhiwa kwa ajili ya mazishi.

Maua Sama Afunguka Kuhusu Kufunga Ndoa

$
0
0
Maua Sama Afunguka Kuhusu Kufunga Ndoa
MKALI mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Maua Sama kwa mara ya kwanza ametaja mwaka wa kuolewa kuwa mambo yakienda sawa mwaka huu unaweza kuwa wake.

Awali zilienea tetesi kuwa, staa huyo anayebamba na Ngoma ya Nakuelewa amechumbiwa na mpenzi wake ambaye ni Mzungu lakini mwenyewe ameibuka na kukanusha.

“Nilishangaa kwa kweli hilo suala la kuchumbiwa na Mzungu kwani halikuwa la kweli, kuhusu kuolewa nimekuwa nikisikia kwa mashabiki sana, ndoa ni mipango, maombi yao yanaweza kunifanya nikatimiza hilo na inawezekana hata mwaka usiishe,” alisema Maua.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images