Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Polisi Dar lapiga Marufuku Disko Toto

0
0

Je shi la Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam limepiga marufuku disko toto kipindi hiki cha msimu wa sikuku ya Pasaka, pia limeahidi kuimarisha ulinzi na usalama na hakuna mtu yeyote atakaepata nafasi ya kufanya vitendo vya uhalifu.

Jibu la Wema kwa Idris baada ya kuchokozwa, ‘Kwa sababu sina mtoto

0
0

Mrembo Wema Sepetu ametoa sababu ni kwanini kila mara anapenda kuposti picha za watoto tofauti tofauti katika ukurasa wake wa Instagram.

Ameeleza hayo baada ya kufanya hivyo na baadae mugizaji Idris Sultan kumwambia; si uanzishe tu nursery.

Mrembo huyo aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 2006 hakukawia kujibu comment hiyo ya Idriss, ni kama alichokozwa alivyoijibu kwa haraka;

Dah… mbona ningekuwa nae wa kwangu ningekuwa nampost all the time… ni kwasababu tu sina wangu… so i post every baby dat melts my heart…
Since i don’t have one to call my owm… ila ningekuwa nae mbona ungeni-unfollow… Smh…

Utakumbuka mwaka 2016 Idris na Wema walikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na ilifikia hatua wakaeleza kuwa wanatarajia kupata watoto mapacha, hata hivyo baadae ilikuja kuripotiwa kuwa ujauzito huo kuharibika.

Tatua Matatizo yako Kwa Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu Pamoja na Mitishamba...

0
0

YULE MTAHALAM WA DUA NA DAWA ZA KIARABU NA ZA KIASILI YANI MITI SHAMBA SHARIFU LUKUMANI SASA YUPO HEWANI WENYE SHIDA ZITUATAZO CHEO KAZINI,KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI,MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME,ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA,KISUKARI,FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE WASILIANA NAE KWA NAMBA 0762899488-0656145170-WhatsApp namba +255620665635

Makamo wa Rais wa Zambia Ahukumiwa Kwenda Jela Baada ya Kuvamia Kituo cha Utangazaji

0
0
Makamo wa Rais wa Zambia Ahukumiwa Kwenda Jela Baada ya Kuvamia Kituo cha Utangazaji
KIONGOZI wa chama wa Chama cha Movement for Multiparty Democracy (MMD) cha Zambia, Dr Nevers Mumba, ametiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha miezi mitatu jela kwa kosa la kutoa habari za uwongo kwa ofisa wa polisi.

Dr Mumba ambaye aliwahi kuwa makamu wa rais wa Zambia, amefutiwa shitaka jingine ambalo alikuwa akikabiliwa la kupita eneo kwa dhamira ya kufanya uhalifu.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Lusaka, David Simusamba, alimtia hatiani na kumhukumu Dr Mumba kifungo hicho cha miezi mitatu na kumpa fursa ya kukata rufaa mnamo siku 14.


“Nimeusikiliza upande wa utetezi wa Mumba kwa masikitiko na kwa maoni yangu ni kwamba kwa vile mtu huyo aliwahi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri na mtu maarufu, angejizuia kufanya aliyofanya. Hivyo namhukumu mhalifu huyo kwenda jela miezi mitatu tangu leo na anaweza kukata rufaa mnamo siku 14,” alisema Hakimu Simusamba.

Maelezo katika shitaka la kwanza yanasema Dr. Mumba, mnamo Novemba 8 mwaka jana, alitoa habari za uwongo kwa ofisa wa polisi Gladson Mwanza kwamba alikuwa na ahadi ya kukutana na mhariri wa shirika la Taifa la Utangazaji la Zambia (ZNBC).

Katika shitaka la pili, Dr Mumba akishirikiana na watu wengine, aliingia bila kibali chumba cha habari cha ZNBC kwa nia ya kuwatisha na kuwabugudhi wafanyakazi wa shirika hilo siku hiyohiyo.

Dr Mumba anadaiwa pia kwamba siku hiyohiyo aliyovamia chumba cha habari cha ZNBC alitoa vitisho kwamba angehakikisha kuapishwa kwa Rais-Mteule, Edgar Lungu, kusingefanyika.

Anadaiwa pia kusema kwamba ZNBC na wahariri wake walikuwa wanalipotosha taifa.
Hakimu Simusamba alisema baadhi ya mashahidi walithibitisha kwamba Dr Mumba alitumia maneno ya kabila la Kibemba ambayo yakitafsiriwa yana maana ya kutishia au kudharau.

Alisema maofisa wa polisi waliopochunguza suala hilo, waligundua kwamba Dr Mumba hakuwa na ahadi ya kukutana na mhariri yeyote wa ZNBC.

TP Mazembe Yamuwinda Ramadhani Kichuya

0
0
TP Mazembe Yamuwinda Ramadhani Kichuya
Baada ya kufanya vizuri kwenye mchezo wa kirafiki baina ya timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya DR Congo mshambuliaji wa klabu ya Simba, Shiza Ramadhani Kichuya “La Pulga” inadaiwa mchezaji huyo kuwindwa na TP Mazembe.

Duru za habari zinasema kuwa mabosi wa klabu ya TP Mazembe ya Congo wanajipanga kutua nchini kufanya mazungumzo na vinara wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC kwaajili ya kumnasa Kichuya ambaye hivi karibuni amepata jina la utani la Messi “La Pulga”  kutoka kwa msemaji wa timu hiyo, Haji Manara.



Kwa mujibu wa gazeti la Nipashe la hapa nyumbani limeandika kuwa rafiki wa karibu wa meneja wa mchezaji huyo, Profesa Madundo Mtambo ameliambia kuwa kwa sasa hawazingatii maslahi pekee bali ni kutaka kuona Kichuya anapata nafasi ya kubadili mazingira na kurejea tena nchini kuitumikia Taifa Stars akiwa na mbinu zaidi.

Shiza Kichuya ambaye alipachika bao la pili kwenye mchezo huo dhidi ya DR Congo baada ya Samatta kufunga la kwanza mkataba wake unatarajia kufikia tamati mwishoni mwa msimu huu wakati amejiunga na timu hiyo akitokea Mtibwa Sugar.

Wabunge Sita Wapata Ajari Morogoro Mmoja Hali Mbaya Awekwa ICU

0
0
Wabunge Sita Wapata Ajari Morogoro Mmoja Hali Mbaya Awekwa ICU
Wabunge sita wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamepata ajali ya gari jana usiku Machi 29, 2018 mkoani Morogoro wakati wakitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam.

Baada ya kutokea ajali hiyo saa 2 usiku katika barabara kuu ya Morogoro-Dodoma eneo la Bwawani, wabunge hao waliumia maeneo mbalimbali ya miili yao na kukimbizwa hospitali ya Mkoa wa Morogoro.

Wabunge hao ambao wote ni kutoka Zanzibar ni Haji Ameir Haji (Makunduchi), Khamis Ali Vuai (Mkwajuni), Bhagwanji Maganlal Meisuria (Chwaka), Makame Mashaka Foum (Kijini), Juma Othman Hija (Tumbatu).

Mganga mfawidhi hospitali ya rufaa Mkoa wa Morogoro, Dk Rita Lyamuya amesema majeruhi hao walipokelewa saa 3 usiku na kupatiwa huduma za awali.

"Jana tumepokea majeruhi sita walioumia sehemu mbalimbali na mmoja wao alilazimika kulazwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu (ICU) lakini hali yake inaendelea vizuri,” amesema.

“Leo asubuhi tayari tumewapa rufaa kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi  zaidi.”

Dk Rita amesema Kimbe na May ndio wameumia zaidi, kupata maumivu makali.

Taarifa zilizoifikia MCL Digital zinaeleza kuwa wabunge hao wanasafirishwa kwa ndege hadi Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Tanzania Inaweza Kuwa Taifa la Ovyo Tusipojifunza Siasa za Kuvumiliana- Nape Nnauye

0
0
Tanzania Inaweza Kuwa Taifa la Ovyo Tusipojifunza Siasa za Kuvumiliana- Nape Nnauye
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema Tanzania inaweza kuwa Taifa la ovyo iwapo itashindwa kujifunza siasa za kuvumiliana hata kama yale yanayosemwa hayapendezi.

Nape ambaye amekuwa akiibua mijadala kwenye mitandao ya kijamii kutokana na ujumbe mbalimbali anaotoa amesema ili Taifa liweze kutembea katika mstari ulionyooka, linapaswa kujenga utamaduni wa kuvumiliana.

Mwanasiasa huyo alisema hayo katika ibada ya kuaga mwili wa mmoja wa waasisi wa Chadema, Victor Kimesera aliyezikwa jana katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

“Kimesera alikuwa mwanasiasa wa aina yake na alivumilia mengi. Kwa maana hiyo, tunapaswa kujifunza siasa za kuvumiliana. Hata maneno tusiyoyapenda maana hii Tanzania bila kuvumiliana itakuwa nchi ya ovyo sana, lazima wakati mwingine tuvumilie hata tusikie maneno tusiyoyapenda,” alisema Nape.

Alisema amelazimika kufika Dar es Salaam akitokea Dodoma kwa ajili ya mazishi ya Kimesera kutokana na kuheshimu mchango wa kiongozi huyo.

Bila kutaja mwaka, Nape alisema alikutana kwa mara ya kwanza na Kimesera katika Klabu ya Gymkhana na tangu hapo aliendelea kushirikiana naye kwa mambo mbalimbali.

“Ndiye aliyenifundisha ustaarabu wa kucheza gofu na wakati mwingine tulitaniana mwishowe tunanunuliana kinywaji na yeye wakati wote alisisitiza sisi ni wamoja na tuishi kwa kuvumiliana. Atakumbukwa kwa hilo,” alisema.

Akimzungumzia Kimesera, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye alisema alikuwa mwanasiasa aliyepigania demokrasia ya kweli.

Sumaye amewataka Watanzania kuelewa kuwa bado wana safari ndefu ya kuifikia demokrasia ya kweli.

Alisema nchi bila kuwa na misingi inayozingatia demokrasia ya kweli inaweza kupotea njia, akisisitiza kuna haja ya kutambua matunda yaletwayo na demokrasia.

“Itakapofika wakati Watanzania watakapoona wamepata demokrasia ya kweli wataona wamechelewa lakini sasa wanaendelea kupitia katika mazingira magumu,” alisema.

Mbunge wa Simanjiro, James ole Millya akizungumza kwa niaba ya wabunge wa Chadema alisema daima wataendelea kumkumbuka mwanasiasa huyo kutokana na ujasiri wake wa kupigania haki bila woga.

“Alifanya kazi katika mazingira magumu na wakati mwingine alizunguka nchi nzima kuhubiri demokrasia. Tumepoteza mtu muhimu katika chama hata nasi jamii ya wafugaji tunamkumbuka namna alivyotupigania,” alisema.

Wanasiasa wengine waliohudhuria mazishi hayo ni mjumbe wa kamati kuu ya Chadema na waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa; Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher ole Sendeka na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita.

Kimesera alifariki dunia Machi 24 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kutokana na tatizo la saratani ya tumbo. Ameacha mjane, watoto watano na wajukuu 18.

Magari ya Wagonjwa na Polisi Marufuku Barabara za Udart

0
0
Magari ya Wagonjwa na Polisi Marufuku Barabara za Udart
Wakati uongozi unaosimamia barabara za mabasi yaendayo haraka (BRT), ukipiga marufuku magari ya wagonjwa na polisi kutumia barabara hizo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema watalazimika kuzitumia barabara hizo wakati wa dharura.

Barabara za mabasi yaendayo haraka zimejengwa kwa ajili ya kutoa huduma zake kwenye barabara za Morogoro na Kawawa.

Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari imesisitiza kuwa hakuna chombo chochote cha moto kitakachoruhusiwa kupita katika barabara hizo zaidi ya mabasi ya mwendokasi.

Akifafanua zaidi taarifa hiyo, mkurugenzi wa wakala wa mabasi hayo (Dart), Ronald Lwakatare alisema ni kweli magari ya wagonjwa hayaruhusiwi kupita katika barabara hizo mpaka ruhusa ya polisi wa usalama barabarani.

Katika kusimamia sheria za barabara hizo, alisema zipo kanuni na taratibu mbalimbali ikiwamo sheria za barabarani, halmashauri na nyinginezo.

“Ieleweke kwamba ni marufuku kutumia barabara hizo na mtu yeyote, kwani zimetengenezwa kwa ajili ya magari hayo tu na kama ikatokea likapita basi iwe ni kwa ruhusa ya polisi wa usalama barabarani ambao wao wanajua ni muda gani na sababu gani ya kuyaruhusu magari mengine yapite,”alisema Lwakatare.

Pia mkurugenzi huyo alisema tayari Rais (John Magufuli) alishatoa maagizo ya magari yafanywe nini inapobainika kutumia njia hizo na kuwataka wanachi kuwa makini ili kuepuka kuingia katika matatizo yatakayowapotezea mali na muda wao bila sababu za msingi.

Taarifa hiyo imeeleza pia kuwa magari ya vyombo vya ulinzi na usalama yanapopita katika barabara hizo, huchangia kwa kiasi kikubwa magari ya watu binafsi kufanya hivyo.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa kuanzia jana hakuna gari lolote litakaloruhusiwa kupita kwenye barabara hizo na kwamba hata magari ya wagonjwa hayaruhusiwi kwa kuwa yana utaratibu wake uliozoeleka sehemu zote duniani.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa kuna baadhi ya magari ya wagonjwa hasa yanayotokea mjini kwenda Kimara yamekuwa yakitumia barabara hizo bila kubeba abiria kwa kigezo cha kupitisha wagonjwa.

Akizungumza na Mwananchi jana, Mambosasa alisema anawaunga mkono BRT, lakini polisi itatumia barabara hizo endapo watakuwa na dharura.

“Kama hatuna dharura tutapita barabara za kawaida. Lakini tukiwa na dharura tutapita barabara zote,”alisema Kamanda Mambosasa.


Miguna Awaandikia Waraka Wakenya "Mipo Hai Lakini Nina Maumivu Makali"

0
0
Miguna Awaandikia Waraka Wakenya "Mipo Hai Lakini Nina Maumivu Makali"
Habari za asubuhi, mchana na jioni wazalendo wa Kenya na marafiki wa Kenya popote mlipo. Mimi niko hai. Namshukuru Mungu kwa hilo.

Lakini nina maumivu makali, msongo wa mawazo na usumbufu. Mkono wangu wa kushoto bado umevimba vibaya. Naamini majambazi ya Jubilee yalinidunga sindano ya IV kunifanya nisiwe na fahamu katika kipindi chote cha safari nikiwa kwenye ndege kati ya Nairobi na Dubai.

Upande wa kushoto wote unaniuma sana. Bado sijafanyiwa vipimo ili kubaini kemikali ambayo majambazi haya yalinidunga kwa nguvu na kinyume cha sheria Jumanne jioni.

Napenda kuwafahamisha mke wangu, watoto, familia, ndugu, marafiki, wafuasi wangu, wanaotutakia mema na wanachama wa vuguvugu la kundi la NRM kwamba nimetelekezwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai.

Nawasubiri wanasheria wangu wawasiliane nami kuhusu amri za hivi karibuni zilizotolewa na mahakama na hatua gani wameshachukua au wanatarajia kuchukua ili kukazia hukumu.

Narudia kusema kwamba ni lazima tuhakikishe kwamba kila mtu, bila kujali ana mabavu au dhaifu kiasi gani, anaheshimu, anazingatia na kutii amri za mahakama na atende kazi kwa kuzingatia utawala wa sheria.

Hakuna mtu ambaye yuko juu ya sheria!

Pili, mahakama zenye mamlaka zimetoa amri kwa serikali isiyohalali kunirejeshea au kunipa hati halali ya kusafiria ya Kenya. Nataka na ninatarajia amri hizo zitaheshimiwa kikamilifu.

Nasisitiza kwamba haki zangu za kikatiba za kuwa pasipoti ya Kenya ziheshimiwe na zizingatiwe.

Dk Miguna Miguna ashangaa amefikaje Dubai

Haki yangu ya kusafiri ndani na nje ya nchi kwa uhuru pia lazima iheshimiwe na izingatiwe wakati wote, katika namna ileile haki hizi zinavyotumika kwa Wakenya wengine.

Nasubiri kuruhusiwa na mamlaka za Shirika la Ndege la Emirates na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kupewa tiketi ya kurudi Nairobi.

Natarajia kurejea Nairobi kwa ndege mapema iwezekanavyo. Ni haki yangu ya kuzaliwa, kikatiba na kisheria pia. Sitaacha kudai haki zangu kwa sababu ya utawala wa kiimla na matakwa ya waliotwaa mamlaka kwa mabavu.

Nawataka wote tubaki imara, tuzingatie malengo na tusiogope. Hiyo ndiyo njia pekee kwetu sisi kujikomboa na kuikomboa Kenya kutoka kwenye makucha ya madikteta Jubilee pamoja na wasaidizi wao na washirika wao. Dk Miguna Miguna

Mkuu wa Wilaya Afunguka Shule Kuita Waganga wa Kienyeji

0
0
Mkuu wa Wilaya Afunguka Shule Kuita Waganga wa Kienyeji
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Said Mohamed Mtanda ametolea ufafanuzi suala la shule ya Msingi Kabwe kuita waganga wa kienyeji kutoka Kongo, ili kutatua tatizo la kishirikina linaloikabili shule hiyo.`


Akizungumza na www.eatv.tv. Mkuu wa Wilaya hiyo Said Mtanda amesema kwamba ni kweli alipokea simu kutoka kwa Mkuu wa shule hiyo kumuelezea matatizo yao hapo shuleni, na lengo walilofikia serikali ya kijiji ili kutatua tatizo hilo ambalo limekuwa likijitokeza mara kwa mara.

Licha ya hayo mkuu wa wilaya hiyo amesema yeye kama kiongozi wa serikali ni kulichukua tatizo hilo kitaalam kwa kupeleka madaktari ambao watatafuta njia sahihi ya kutibu wanafunzi hao, na sio kuruhusu mambo ya kishirikina, ingawa hawezi kuwakataza wazee wa kijiji hicho kwani anaheshimu mila zao.

“Nilipokea simu kutoka kwa mkuu wa shule hiyo akinielezea matatizo yao, akaniambia na uamuzi wa kijiji ulivyoamua, lakini mimi kama kiongozi wa serikali nitawajibika vile ipasavyo, nitapeleka mganga mkuu wa wilaya akaangalie na namna ya kuweza kulimaliza tatizo hilo, ni tatizo ambalo mara nyingi hujitokeza mara nyingi kwenye shule zetu, lakini wao kama wanakijiji na wazee na ndio wazazi, wana uamuzi wao ambao siwezi kuwakataza, suala la kuita waganga kutoka Kongo sio kweli isipokuwa wana mpango wa kufanya matambiko yao, hayo ya waganga wa Kongo halipo”, amesema Saidi Mtanda.

Wanafunzi wa kike wa shule ya msini Kabwe iliyopo Wilayani Nkasi mkoani Rukwa wanakabiliwa na tatizo la kiafya la kuanguka, kuzimia na kupiga kelele, jambo ambalo wakazi wa eneo hilo wanahisi linatokana na ushirikina, na kuamua kutafuta waganga wa kienyeji kuweza kutatua.

Mimi Mars Naye Afunguka Kuhusu Kuwa na Mtoto

0
0
Mimi Mars Naye Afunguka Kuhusu Kuwa na Mtoto
Baada ya Vanessa Mdee kusema kwa sasa hayupo tayari kuwa na mtoto, Mimi Mars naye pia amefunguka kuhusu hilo.

Mimi Mars amesema kupata mtoto au kuwa mama wa familia ni kitu ambacho wanakihitaji ila ni kwa kipindi cha mbeleni zaidi takribani miaka mitano ijayo.

“Mimi baada ya miaka mitano hivi itakuwa fresh, huku mbele anaweza nikawa mama mwenye familia labda nimeolewa Mungu akijalia lakini napenda sana watoto, napenda sana kuwa na familia na ninapenda kuwa mama familia, so hicho ni kitu kipo kwenye plan zangu,” Mimi Mars ameiambia Bongo5.

Vanessa Mdee na Mimi Mars ni mtu na dada yake na wote wanafanya kazi zao za muziki kupitia label ya Mdee Music pamoja na Brian Simba. Mimi Mars kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Papara’.

Panya Road Waibuka Wavamia Mitaa Tabata Wapora Mali

0
0
Panya Road Waibuka Wavamia Mitaa Tabata Wapora Mali
Kwa mara nyingine tena taharuki, hofu na wasiwasi mkubwa viliwakumba wakazi wa Tabata wilayani Ilala jijini Dar es Salaam kwa takribani saa tatu baada ya kundi maarufu la uporaji la Panya Road kuvamia mitaa mbalimbali na kupora mali.

Kundi hilo lililokuwa na vijana zaidi ya 30 waliokuwa wameshika nondo, visu, mapanga na bisibisi jana usiku Machi 29,2018 lilisababisha wakazi wa Tabata Kisiwani, Kimanga hadi Kinyerezi kujifungia majumbani mwao na baadhi kujifungia ndani kutokana na jinsi kundi hilo lilivyokuwa likivamia biashara na nyumba kupora.

Mmoja wa mashuhuda wa eneo la Tabata Kisiwani, Isaya Subi amesema tukio hilo lilianza saa mbili usiku ambapo kundi hilo lilivamia katika eneo hilo, kupora mali mbalimbali kwenye maduka pamoja na kuwapora wapita njia.

“Vijana hawa si mchezo walikuwa kama 30 hivi kila mmoja alibeba nondo, bisibisi, wembe na spoku wakikukuta njiani wanakupiga huku wakikusachi na kuchukua kila kitu ulichokuwa nacho wengine walivamia maduka na kuchukua bidhaa mbalimbali,”amesema Subi.

Mkazi wa Kinyerezi, Leila Lameki amesema eneo hilo walivamia saa tano usiku na kuanza kuporwa mali mbalimbali, lakini mmoja wa vibaka hao aliingia kwenye nyumba moja na alidhibitiwa na wananchi wa eneo hilo huku wenzake wakifanikiwa kutoroka.

“Kwa umoja wetu wananchi tuliweza kulidhibiti hili kundi kati ya hao mmoja alikamatwa na kuanza kupigwa na kusababishia kifo chake huku wenzake wakitimua mbio,” amesema Leila.

Kamanda wa Polisi  Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema usiku wa kuamkia leo kuna kundi lilivamia eneo la Kinyerezi na kupora mali mbalimbali, lakini kati ya wahusika mmoja aliuawa na wananchi.

Amesema polisi walifika eneo hilo na kukuta wahalifu hao wameshatoweka na kukuta silaha mbalimbali katika eneo hilo ikiwemo nondo, visu na bisibisi.

Dar es Salaam Fahamu Siri Kubwa ya Utajiri Ambayo Matajiri Hawataki Uijue

0
0
Hope wengi wetu tupo tuna jishughulisha na biashara  kama kilimo na biashara zingine tofauti tofauti

But tukumbuke Technology inaenda fasta sana hope mmeshasikia about Bitcoin , Ripple na Cryptocurrency zingine kwa ujumla. Ni decentralized digital money ambazo zinakuwa kwa kasi sana
Chini ya its innovative blockchain technology huku soko lake Duniani likifika zaidi ya billion 700 Jan 2018.

Juzi tu mlisikia mmiliki wa Ripple  Chris Larsen kawa tajiri namba 5 duniani kutokana na crypto.... Pia msanii 50 cent baada ya kufilisika juzi katangazwa ni millionea  mpya just because alikuwa ana hold bitcoin za kutosha.

Binafsi  I have been investing and trading katika hilo soko na ningependa na ndugu zangu wa mbeya mkalijua hilo soko vizuri.

Bado mapema ni muda wako muafaka upate elimu sahihi ili uweze kuendeleza safari ya mafanikio

Angalia coin ya Ripple january 2017 ilikuwa inauzwa 0.002 but leo inauzwa dola 1.

Kama unge invest dola 100 ungepata coin elfu 20.

Ambazo leo ungekuwa na dola elfu 20,000 sawa na zaidi ya million 40 za kitanzania.

Zipo coin nyingine very smart

Hakuna mtu aliyezaliwa na utajiri au umaskini.

ELIMU KWANZA, MENGINE BAADAE

Gamy
# CMC Co- Founder


Jiunge na group la whatsapp uwepo katika watu 200 wa mwazo kwa ajili ya free training class April 2018

bonyeza hapa chini kuweza kujiunga na group

https://chat.whatsapp.com/CB5jVNJ04a7IyW9MM7z0h

TP Mazembe yamuwinda Kichuya kimya kimya

0
0

Baada ya kufanya vizuri kwenye mchezo wa kirafiki baina ya timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya DR Congo mshambuliaji wa klabu ya Simba, Shiza Ramadhani Kichuya “La Pulga” inadaiwa mchezaji huyo kuwindwa na TP Mazembe.

Duru za habari zinasema kuwa mabosi wa klabu ya TP Mazembe ya Congo wanajipanga kutua nchini kufanya mazungumzo na vinara wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC kwaajili ya kumnasa Kichuya ambaye hivi karibuni amepata jina la utani la Messi “La Pulga”  kutoka kwa msemaji wa timu hiyo, Haji Manara.

Kwa mujibu wa gazeti la Nipashe la hapa nyumbani limeandika kuwa rafiki wa karibu wa meneja wa mchezaji huyo, Profesa Madundo Mtambo ameliambia kuwa kwa sasa hawazingatii maslahi pekee bali ni kutaka kuona Kichuya anapata nafasi ya kubadili mazingira na kurejea tena nchini kuitumikia Taifa Stars akiwa na mbinu zaidi.

Shiza Kichuya ambaye alipachika bao la pili kwenye mchezo huo dhidi ya DR Congo baada ya Samatta kufunga la kwanza mkataba wake unatarajia kufikia tamati mwishoni mwa msimu huu wakati amejiunga na timu hiyo akitokea Mtibwa Sugar.

Pata Huduma za Matibabu ya Asili na Nyota Pamoja na Pete za Bahati

0
0

Mtabibu Mongwa husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote
Tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .

Natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
Natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini

Kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa
Kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri piga simu

+255 764291657

Azam Yajipanga Kuimaliza Mtibwa Sugar

0
0
Azam Yajipanga Kuimaliza Mtibwa Sugar
Klabu ya soka ya Azam FC imeweka wazi kuwa itaingia na moto wake wote kwenye mchezo wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Mtibwa Sugar, utakaopigwa kesho Jumamosi kwenye uwanja wa Azam Complex.


“Mchezo huu ni muhimu sana kwetu lazima tuwashe moto wetu wote mana mshindi atasonga mbele zaidi kwenye nusu fainali na ukichukua kombe utapata nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika'', amesema Idd Cheche ambaye ni kocha msaidizi.

Azam FC na Mtibwa zimeonekana kuwa na rekodi sawa kwenye michuano hiyo msimu huu ambapo Azam FC katika hatua za awali ilizifunga Area C United (4-0), Shupavu (5-0) huku Mtibwa Sugar nayo ikizifunga Villa Squad ya Kinondoni kwa mabao 2-1.



Katika hatua ya 16 bora Mtibwa iliitoa timu ya Buseresere, ambao ni mabingwa wa Mkoa wa Geita. Kwa upande wao Azam FC waliitoa KMC ya Kinondoni ambayo imepanda kucheza ligi kuu kuanzia msimu ujao.

Msimu huu tayari timu hizo zilikutana kwenye ligi na ikashuhudiwa zikitoka sare ya bao 1-1, bao la Azam FC lilifungwa na winga Enock Atta huku lile la Mtibwa Sugar likifungwa na Kelvin Sabato ‘Kiduku’

Watumishi wa Umma Kushtakiwa

0
0
Watumishi wa umma kushtakiwa
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Joseph Kakunda amesema kwamba watumishi wa umma wanapaswa kutekeleza na kusimamia ipasavyo miradi mbalimbali, ili kuepusha serikali na hasara na athari za kiuchumi na kijamii.


Naibu Waziri Kakunda ametoa kauli hiyo na kueleza  kuwa mfanyakazi wa umma anaweza kushtakiwa kwa kosa la kiutumishi na kosa la kijinai, endapo itabainika miradi anayoisimamia imetekelezwa chini ya kiwango.

Waziri Kakunda ameendelea kusema kwamba kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma stahiki wanazotakiwa kuzipata kutokana na miradi ya maendeleo, hivyo kutosimamia kikamilifu miradi hiyo ni moja ya makosa ambayo mfanyakazi wa umma anaweza kushtakiwa.

Katibu wa Chadema Mkoani Arusha Ajitoa Ahamia CCM

0
0
Katibu wa Chadema Mkoani Arusha Ajitoa Ahamia CCM
Katibu Mwenezi wa CHADEMA wilaya ya Arusha Gabriel Kivuyo amekihama chama hicho kwa madai ya viongozi wake ikiwemo Mbunge kuwadharau pamoja na kitendo cha kutolewa nje kwenye kikao cha Mameya kwa tuhuma za kuwarekodi

Akizungumza wakati akipokelewa na Katibu wa CCM wilaya Musa Matotoka amesema hata akipata matatizo nakumtafuta Mbunge amekuwa hapatiwi ushirikiano

Duma Aingia Ndani ya Gari la Watalii Serengeti

0
0
Duma Aingia Ndani ya Gari la Watalii Serengeti
Britton Hayes na mjomba wake, wote kutoka Seattle, Washington, walikuwa safarini kujionea wanyama katika mbuga ya taifa ya Serengeti nchini Tanzania pale duma huyu alipoamza kuwa mtalii ndani ya gari lao.

Mgeni huyo wasiyemtarajia alikaa ndani ya gari hilo kwa dakika 10 katika eneo la Gol Kopjes la mbuga hiyo, kabla ya mwishowe kuondoka kwenda kuwinda swara.

Britton Hayes anasema walikuwa wamemuangazia duma mmoja aliyekuwa ameruka sehemu ya mbele ya gari lao pale mwingine aliporuka na kuingia kupitia sehemu ya nyuma bila wao kumuona.

“Tulianza kugundua duma hao walikuwa wameanza kuvutiwa na gari letu; lakini hatukuwa na muda wa kuondoka au kutoroka kwa sababu hutaki kuwashtua wanyama hao, ukifanya hivyo ndivyo mambo huenda mrama,” Hayes aliambia jarida la Komo News.

“Nilikuwa nimejawa na wasiwasi sana. Lakini wakati wote nilikuwa nauhisi uhai wangu,” anasema.

Operesheni Kumg'oa Mugabe Yaibua Mambo Mazito

0
0

Operesheni Kumg'oa Mugabe Yaibua Mambo Mazito
Matokeo ya uchunguzi wa Baraza la Taifa la Ukimwi (NAC) na Jeshi la Polisi la Zimbabwe (ZRP), unaonyesha kuwa maofisa wa jeshi la Wananchi wa Zimbabwe wanadai huduma ya ngono bure kutoka kwa wanawake wanaojiuza kama shukrani kwao kwa kusimamia 'Operesheni Rejesha Heshima', Novemba mwaka jana.

Uchunguzi huo uliofanywa mwezi uliopita baada ya operesheni hiyo iliyomuweka madarakani, Emmerson Mnangagwa ulilenga kupima uelewa wa maofisa wa polisi, tabia zao na ushiriki wao katika ngono, ushoga na matumizi ya dawa za kulevya.

Wakati wa utafiti huo, wanawake hao wanaojiuza waliwalalamikia wanajeshi kwamba baadhi yao wamekuwa wakitumia bunduki kuwatisha, ili wafanye nao ngono bure.

"Wanajeshi wamekuwa wasumbufu katika baadhi ya maeneo kwani wanataka ngono bure hasa baada ya kushiriki katika Operesheni ya Kurejesha Heshima,” inasema taarifa ya utafiti huo huku ikitaja matukio kuwa mengi zaidi kutokea katika eneo la Chiredzi.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images