Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Musiba Awashambulia Viongozi wa Dini Wanaomshambulia Rais Magufuli

$
0
0
Musiba Awashambulia Viongozi wa Dini Wanaomshambulia Rais Magufuli
MWANASIASA aliyekuwa ACT Wazalendo na hivi karibuni kutimkia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Cyprian Musiba ameujibu baadhi ya viongozi wa dini akisema walikuwa wakijipatia pesa kupitia mafisadi na wengine walikuwa wanauza madawa ya kulevya.

Musiba amesema kutokana na jitihada za serikali kuwabana mafisadi na wauza unga waliokuwa wakiwapa pesa hizo, baadhi ya vioongozi hao wanaongea maneno ya hovyo kuhusu Rais Dkt. John Magufuli na kutoa matamko ambayo yamekosa tija.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Jipu Pwaa...Siri Mpya Diamond Kutembea na Mastaa Yafichuka

$
0
0
JIPU pwaa! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia kuvuja kwa siri inayodaiwa kuwa ndiyo chimbuko la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuwa ‘mtundu’ wa watoto wa kike, Ijumaa linakujuza!

 TUJIUNGE NA NDUGU

Mwanafamilia mmoja ambaye aliomba hifadhi ya jina, alivujisha ubuyu mpya wakati kukiwa na madai ya jamaa huyo kurudiana na aliyewahi kuwa mwandani wake, Wema Isaac Sepetu kwamba, watu wamekwa wakimshangaa Diamond kuwa na ‘totoz’ nyingi pasipo kujua chanzo chake.

“Unajua wengi wamemuona Nasibu (Diamond) ukubwani, wanafikiri hii michezo kaanza leo, hawajui tu, Nasibu tunayemjua sisi, ameanza michezo hii siku nyingi tu sema wengi walishindwa kujua labda kwa sababu hakuwa maarufu,” alisema ndugu huyo.


AZIDI KUTIRIRIKA

Akiendelea kushusha madini mbele ya kinasa sauti cha Ijumaa, ndugu huyo wa Diamond alisema kuwa, mkali huyo wa Bongo Fleva anaonekana kuirithi tabia hiyo kutoka kwa babu yake.

“Huyu atakuwa amerithi haya mambo ya warembo kutoka kwa babu yake. Maana babu yake naye alikuwa hivihivi.

“Babu ya (mzee Jumaa) alikuwa mtu fulani ambaye alikuwa akijijali sana hivyo hata wanawake nao walikuwa wakimpenda kutokana na muonekano wake,” alisema ndugu huyo.


 Kama hiyo haitoshi, ndugu huyo alienda mbali zaidi kwa kubainisha kuwa, siku zote maji hufuata mkondo kwani mbali na babu yake, hata baba yake mzazi Diamond (Abdul Jumaa) naye alifuata mkondo huo.

“We’ enzi za ujana wake baba Diamond alikuwa baba Diamond kweli. Alikuwa anajipenda, mtu smati hivi na michezo ya kurukaruka na warembo alikuwa nayo sana.

“Wewe mtazame baba Diamond hata sasa hivi tu, licha ya uzee alionao, lakini popote utakapomkuta, lazima atakuwa kapendeza, wakati mwingine anapiga hadi cheni na nini utadhani bado kijana,” alisema ndugu huyo.

 Alisema kuwa, kama familia, mara nyingi wanapomuona Diamond mara yupo na huyu, mara yupo na mrembo mwingine, hawashangai sana maana wanafahamu asili yake.

“Watu waliomfahamu Diamond akiwa msanii ndiyo wanaweza kushangaa, lakini kwa sisi tunaofahamu zaidi asili yake, hatushangai kabisa,” alisema ndugu huyo.

Katika mahojiano hayo maalum, ndugu huyo alisema kuwa, wao kama ndugu, wanamuombea tu Diamond apate mtu sahihi ili atulie kwani hata kwa baba na babu yake, walipopata mtu sahihi walitulia na kufanya maisha.

“Wewe si unamuona hata baba Diamond, tangu alipoachana na mama Diamond, kwa sasa ametulia kabisa. Starehe yake kubwa sasa hivi ni bia kidogo basi,” alisema ndugu huyo.


 MSURURU WA WAREMBO

Mkali huyo anayetamba na Wimbo wa African Beauty aliomshirikisha Omario wa Marekani, ana rekodi baab’kubwa ya kutembea na warembo maarufu wasiopungua 17.


Listi ya warembo hao ambayo haipo katika mpangilio maalum, inawaonesha warembo kama Hawa wa Nitarejea, Irene Uwoya, Wema, Hamisa Mobeto, Jokate Mwegelo, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Penniel Mungilwa ‘Penny’ na Nuzrat.

Wengine ni Natasha wa Moyo Wangu, Rehema Fabian na Jacqueline Wolper, Tunda Sebastian, Lyn (Irene wa Kwetu), Najma na Hamisuu Malick.



DIAMOND ANAVYOJINASIBU

Mara kadhaa katika mahojiano yake na vyombo vya habari, Diamond amekuwa akijinasibu kuwa amekuwa ‘akiwatafuna’ warembo mbalimbali maarufu kwani kabla ya kuwa staa, walikuwa wakimdharau na kumuita majina ya ajabuajabu.

Anasema kuwa, baada ya kupata umaarufu na mkwanja, kweli ameamua kuwapitia warembo tofauti ili kukamilisha furaha ya moyo wake kwani ni ndoto aliyokuwa akiiota siku nyingi.


BABA DIAMOND ATIA NENO

Alipoulizwa kuhusu suala la ukoo wao kuwa ni watundu na watanashati, baba Diamond alikiri kweli wao ni watu watanashati na kwamba suala la wanawake kuvutiwa nao liko wazi, lakini haimaanishi kwamba ni watundu.

“Kuvaa kweli, tunavaa vizuri. Hilo la kwamba sisi ni watundu ni watu tu wanasema, lakini hatupo hivyo bwana,” alisema baba Diamond.

MHARIRI

Kwa kuwa, Diamond tayari ameshazaa watoto wawili na Zari, anapaswa kusaka mtu sahihi ili aweze kufanya naye maisha kwani umri nao unamtupa mkono.

STORI: MWANDISHI WETU, DAR/GPL

Joyce Kiria na Wema Sepetu Lindeni Brand Zenu

$
0
0

By Allen Kilewella
Nimeangalia Picha zinazozunguka mitandaoni za hawa mabinti mawili. Kwanza ya joyce Kiria ambaye anadai mwanaume anayetaka kutoka naye hivi sasa ni lazima alipie gharama za vitu atakavyokuwa amevaa kwa asilimia sabini (70%).

Joyce inawezekana kabisa ana machungu toka kwenye ndoa yake ya kwanza ambayo imevunjika. Katikati ya maelezo yake inaonesha amepata "request' nyingi sana tangu ijulikane kwamba ameachana na mumewe.

Lakini kwenye maelezo yake inaonekana anakazia sana kurudishiwa gharama zake kuliko mahusiano na huyo mwenye kurudisha hizo gharama. Kimanti ni kwamba yeyote mwenye kuweza kurudisha gharama kwa siku husika ndiyo atatoka naye.

Nimeona pia Video ya Wema Sepetu akiwa kwenye bwana la kuogelea. Kwanza jinsi anavyochezesha makalio yake na maneno anayoyasema na kijana aliye pembeni yake kwenye bwawa lile la kuogelea inatia kinyaa.

Nawaasa Wema na Joyce wajue kwamba maisha yao yanategemea sanaa ambayo wateja wao wakubwa ni wananchi wengi ambao hawapendi matendo na maneno ya kijinga.

Diva: Nimeshampata Boyfriend Mpya Mwenye Uwezo wa Kulipa Milioni 500

$
0
0
Mtangazaji wa kituo cha Redio cha Clouds FM, DIVA ameweka wazi kuwa kwa sasa hayupo single tayari ameshapata Boyfriend mpya baada ya kumwagana na mwanamuziki Heri Muziki.

Diva amesema kuwa mwanaume huyo tayari ameshakubali kulipia mahari ya shilingi milioni 500 ingawaje kwa sasa amekataa kumuweka wazi kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa upande mwingine Diva amesema kuwa kwa sasa anapata tabu kweli kutoka kwa mwanaume kitu ambacho kinamfanya abadilishe laini mara saba kwa mwezi.

Amber Lulu Aponda Muonekano wa Ommy Dimpoz..Adai Hajakaa Kiume

$
0
0
Kuna kale kamsemo kanasema ukiwazoea sana watoto wa kike bila kuwafanyia majambozi kuna siku watakushika wo.wo.wo..

Hii imejidhihirisha kwa mwandada Amber Lulu baada ya kumshukia staa wa bongo Fleva aliyeasi muziki na kuwa staa wa Instagram kwa kupost picha akiwa anakula bata ughaibuni, ambapo wadadisi wa mambo wanasema safari hizo za ng'ambo zinagharamikiwa

Akijibu swali la mtangazaji wa moja ya kipindi cha Online TV ambopo aliulizwa kama ikitokea Jux na Ommy Dimpoz wamepeleka posa nyumbani kwao atamchagua nani.Amberlulu alijibu "Obvious nitamchagua Jux" huku akifafanua kuwa msanii Dimpoz hana mvuto hajakaa kiume, hivyo hawezi kubattle na Jux hata kidogo.

Ushauri kwa vijana wa kiume: Usithubutu kuzoeana sana na wtoto wa kike bila hata kuchombeza hata kama atakunyima ila fresh ushamuonyesha kuwa una uwezo

VIDEO:


Pata Huduma za Matibabu ya Asili na Nyota Pamoja na Pete za Bahati

$
0
0
Mtabibu Mongwa husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote
Tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .

Natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
Natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini

Kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa
Kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri piga simu

+255 764291657

Wabunge Sita Walazwa Muhimbili...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya March 31

$
0
0


Wabunge Sita Walazwa Muhimbili...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya March 31

Katibu wa Bunge Azungumzia Ajali ya Wabunge 6

$
0
0
Katibu wa Bunge, Steven Kagaigai amesema chombo hicho cha dola kinafuatilia kwa ukaribu ajali ya wabunge sita iliyotokea jana usiku, Machi 29, 2018 mkoani Morogoro.

Kagaigai amesema baada ya kupokea taarifa hizo wamefanya mawasiliano na uongozi wa Hospitali ya Morogoro na walishauriwa kuwahamishia Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

“Ndiyo taarifa hizo ninazo, wamepata ajali huko Morogoro, tayari tumeshafanya taratibu za kuwapeleka Muhimbili kwa huduma zaidi na ofisi yetu inawajibika kwa kila hatua,” amesema Kagaigai.

Wabunge hao ambao wote ni kutoka Zanzibar ni Haji Ameir Haji (Makunduchi), Khamis Ali Vuai (Mkwajuni), Bhagwanji Maganlal Meisuria (Chwaka), Makame Mashaka Foum (Kijini), Juma Othman Hija (Tumbatu).

VIDEO: Cyprian Musiba Afunguka Mazito, Asema Mbowe na Lema ni Watu Hatari sana

$
0
0
Mkurugenzi wa kampuni ya CZI, Cyprian Musiba amekutana na waandishi wa Habari Dodoma ambapo


ANGALIA VIDEO:

Mwanamke Jikubali Unavaa Nywele za Bandia ili iweje?

$
0
0
Natumaini mko na afya njema katika jamii ya kitanzania wanawake wengi wanavaa nywele za bandia a.k.a mawigi.

Utafiti wangu wanawake hawa wavaa mawigi wanadai kuwa yametengenezwa kwa katani, Kitu ambacho sio kweli.

Ukweli ni kwamba mawigi ni nywele halisi za binadamu kwa sababu nywele huundwa na protein inayoitwa fibrous protein, Ukichoma nywele yako huwa inatoa harufu fulani ambayo ni unique hivyo basi hata haya mawigi ni nywele za wazungu walizonyoa ndo mnavaa eti mmependeza.

Mwanamke unayevaa mawigi anaweza kuwa kuwa na sifa kuu moja tu nayo ni mchafu wanawake acheni kuvaa mawigi mnavaa manuksi ya mizungu iliyokufa.

Mwanaume usiruhusu mwanamke akaingia na wigi ndani mwako asije akakuletea mapepo jikubali jinsi ulivyo wewe unaevaa Mawigi.

Mambo ya Kuzingatia Katika Kuchagua Mchumba Mwenzi wa Maisha

$
0
0
Ikiwa wale wanaokusudia kuoana hawataki kuwa na mashaka mengi wala kuwa na mambo kadha wa kadha ya kuwanyima furaha baada ya kufunga ndoa, imewalazimu kufikiria vyema na kwa moyo wote juu ya jambo hili na kwa wakati huu kabla ya kuoana. Ikiwa hatua hii itafanywa kipumbavu, itakuwa mojawapo ya mambo makuu mno yawezayo kuharibu mafao ya mvulana ama msichana wawapo wamekwisha kuoana. Kwao maisha yataonekana kuwa kama mzigo wa laana. Kaitka ulimwengu huu hakuna awezaye kumnyima mwanamke furaha, ama kumharibia maisha na kufanya yamuelemee na kumchoma moyo zaidi ya mumewe; na hali kadhalika hakuna mwenye uwezo wa kupooza matumaini na jitihada za mwanaume na kuposha nguvu zake, kuharibu mvuto wake na maendeleo yake zaidi ya mkewe. Mara nyingi ni tangu dakika ile baada ya harusi ambapo maisha huanza kuwaelemea wanawake na wanaume wengi. Ndoa ni jambo ambalo lina mvuto katika ulimwengu huu, na litakuwa na mvuto katika ulimwengu ujao pia.

Wengi hawaelewi vyema muungano huu wa ndoa. Wengi wao hudhani ya kwamba, muungano huu ni mojawapo ya njia ya kufikia upeo wa furaha; lakini laiti wangefahamu kiasi kidogo tu cha uchungu walionao wale waliounganishwa kwa kiapo cha ndoa ambacho kimewafunga kwa minyororo wasiyothubutu kuikata, hawangeshangaa kwa maelezo haya. Ndoa nyingi zinazofungwa huwa ni mkatale wa huzuni. Kuna maelfu ya watu waliounganishwa katika ndoa lakini hawapatani.

Wale wanaofikiria kuoa ama kuolewa ni lazima wajishauri vyema kuhusu hali na mwenendo wa ndoa wanayokusudia kuwa nayo. Ni lazima vijana wafanye uchunguzi wa kutosha katika mambo yanayohusu kuchagua mpenzi na kufanya uchumba. Ewe kijana mwenzangu, jihadhari ili kile unachodhania kuwa ni dhahabu ama lulu safi kisije kikawa takataka tu. Jambo hili halipaswi kufanywa haraka. Wakati ungali bado unaweza kupenda, jihadhari usije ukapenda kama kipofu.

Fikiria sana uone kama maisha yako na yule unayemchagua kuwa mwenzi wako wa maisha yatakuwa ya furaha ama ya kutopatana na kuhuzunisha baada ya harusi. Wanawake na wanaume wengi wameoana kana kwamba jambo la pekee lililowapasa kulijali ni kuwa wanapendana au la. Kuchagua mwenzi wa maisha kwafaa kufanywa kwa busara ili kuwawezesha wazazi na watoto pia, kuwa na hali nzuri kiroho, kiakili na kimwili.

Mambo ya kuzingatia katika kuchagua msichana wa maisha

Kijana wa kiume unapaswa uchague msichana ambaye atasiamama kando yake na ambaye ataweza kuchukua sehemu ya mzigo wa maisha yake, mke ambaye mvuto wake utamfanya mumewe na heshima na kumwezesha kuwa na mwenendo mwema, na ambaye kwa jili ya upendo wake, atamfanya kuwa na raha maishani mwake.

Ewe kijana wa kiume na mwanaume mwenzangu naomba ujishauri kwa uangalifu mkubwa kuhusu mambo haya yafuatayo na bila shaka kama yakizingatiwa kwa umakini yatakuwa msaada mkubwa kwako wewe mvulana mwenye nia ya dhati ya kuoa;


  • Je huyo unayekusudia kumuoa atafanya nyumba yenu iwe ya furaha?
  • Je yeye ni mwangalifu awezaye kutunza mali, ama akishaolewa hatapoteza mapato yenu tu bali pia atazitawanya mali zenu huku akionyesha upendo wa juu juu tu?
  • Je huyo unayemtaka awe mwenzi wako ana hofu na kumcha Mungu?
  • Je ana afya njema?
  • Je ana bidii katika kazi?
  • Je msafi wa kimwili na kiroho?
  • Je ni mlevi?
  • Je ni mtii, mnyenyekevu na mwenye adabu?
  • Je anajiheshimu na kuvaa mavazi yenye heshima?
  • Je ni mwaminifu?
  • Je ni mtu anayetunza siri katika uhusiano wenu?
  • Je ni mkristo, mpagani au mwislamu mwenzangu?
  • Je mwenendo na tabia yake ikoje kwa wakati huu?


Nafahamu kwamba mvulana ambaye ametumbukia katika kisima cha mapenzi atayadharau maswali haya kana kwamba hayana maana wala manufaa yoyote, lakini hayana budi kufikiriwa kwa umakini na kwa ungalifu mkubwa zaidi.

Wakati wa kuchagua mke, tafakari na uelewe tabia na mwenendo wale, uone kama atakuwa mstahimilivu na mwenye bidii. Uone kama atachoka kuwatunza wazazi wako walo wazee wakati ule ambao watahitaji msaada wako. Uone kama atakushawishi utengane nao na kukushawishi umpende yeye peke yake na kusahau baba na mama ambao badala ya kupata binti watakuwa wamempoteza mwana.

Mambo ya kuzingatia katika kuchagua mvulana wa maisha

Kabla msichana hajatoa mkono wake kwa mvulana na kuvishwa pete ya uchumba, kwanza na ajiulize kama yule mvulana wanayekaribia kuoana anafaa ama vipi. Mwenedo wake na tabia yake ya siku zilizopita ulikuwa wa namna gani? Je maisha yake ni masafi? Je upendo akuonyeshao unatoka moyoni na unaonyesha heshima na tabia njema ama ni upendo wa hivi hivi tu? Je anao mwendendo ambao utanifanya kuwa na furaha? Mimi kama mke nitaweza kuwa na furaha niwapo kwake? Je ataniruhusu kudumisha tabia yangu na kunipa uhuru ama itanilazimu kutupilia mbali yote na kufuata matakwa yake? Maswali kama haya yakizingatiwa kwa busara yatakuwa na manufaa sana katika maisha yajayo ya msichana ambaye anatarajia kuolewa.

Kila msichana anayetamani kuwa na familia yenye furaha na amani, ambayo haitakuwa na udhaifu wala huzuni katika siku za baadae na ajiulize maswali haya kabla ya kutoa ukubali wake wa upendo.


  • Je huyo unayemtaka awe mwenzi wako ana hofu na kumcha Mungu?
  • Je ana afya njema?
  • Je ana bidii katika kazi?
  • Je msafi wa kimwili na kiroho?
  • Je ni mlevi?
  • Je ni mtii, mnyenyekevu na mwenye adabu?
  • Je anajiheshimu na kuvaa mavazi yenye heshima?
  • Je ni mwaminifu?
  • Je ni mtu anayetunza siri katika uhusiano wenu?
  • Je ni mkristo, mpagani au mwislamu mwenzangu?
  • Je mpenzi wangu anaye mama?
  • Je tabia ya mama yake ikoje?
  • Je anatambua wajibu wake kwa mamaye?
  • Je anajali upendo na furaha ya mama yake?

Ikiwa hajali wala hamheshimu mama yake, kweli ataweza kuonyesha heshima na upendo, wema na usikivu kwa mkewe?
Je harusi itakapokwisha atakuwa na huruma kwa makosa yangu ama atakuwa ananikosoa mara kwa mara huku akiwa mgomvi na mkali?

Katika kuyajibu maswali haya shauklu nyingi yaweza kupishia mbali makosa na kasoro za mchumba wako, lakini upendo wa kweli hautaficha neno. Katika kuchagua mwenzi wa maisha, msichana na achague mvulana mwenye tabia na mwenendo safi wa kibinadamu, aliye na bidii, mwangalifu, mwenye heshima na aliye mwaminifu na mnyofu.

Ikiwa umefanya uchumba na mtu ambaye huelewi vyema tabia yake, usidhani kushika uchumba kutakulazimisha kuchukua kiapo cha ndoa na kuungana na mtu ambaye humpendi na ambaye wala hutamheshimu maishani mwako. Jihadhari sana unapofanya uchumba wenye masharti; lakini hata ukiwa ni uchumba wenye masharti, ni bora mara kumi kuuvunjilia mbali huo uchumba kabla ya kufunga ndoa kuliko kuja kuvunja ndoa baadae kama wengi wafanyavyo.

Written & Prepared by:
Young Master

Tatua Matatizo yako Kwa Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu Pamoja na Mitishamba...

$
0
0
YULE MTAHALAM WA DUA NA DAWA ZA KIARABU NA ZA KIASILI YANI MITI SHAMBA SHARIFU LUKUMANI SASA YUPO HEWANI WENYE SHIDA ZITUATAZO CHEO KAZINI,KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI,MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME,ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA,KISUKARI,FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO

 ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE WASILIANA NAE KWA NAMBA
 0762899488
0656145170
WhatsApp namba
+255620665635

Esma Afunguka Busu Tata Alilopigwa na Wema Sepetu " Busu Alonipiga Wifi Yangu ni Kwasababu Tunapendana"

$
0
0
Esma Afunguka Busu Tata Alilopigwa na Wema Sepetu " Busu Alonipiga Wifi Yangu ni Kwasababu Tunapendana"
DADA wa mwanamuziki maarufu wa Afro- Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Esma Abdul amefungukia busu alilopigwa na staa wa filamu ambaye amewahi kuwa wifi yake kwa kaka yake huyo, Wema Sepetu kuwa lilikuwa ni la kawaida tu kwani wanapendana sana.

Akizungumza na Ijumaa, Esma alisema hakuona kama kuna tatizo lolote kupigwa busu na Wema kwa sababu ni kitu ambacho wamekizoea siku nyingi tangu walipokuwa mawifi kwa hiyo kwao siyo kitu kigeni ni mambo ya kawaida tu.

“Busu alilonipiga wifi yangu ni la kawaida kabisa hakuna kitu kipya hapo ni upendo tu kwa sababu mimi na yeye tunapendana sana ndiyo maana umetuona hata kwenye busu hilo hatuna shaka na mtu,” alisema Esma.

Lissu Ashindwa Kuvumilia Afunguka Mazito Sakata la Mbowe na Viongozi Wengine wa Chadema

$
0
0
Lissu Ashindwa Kuvumilia Afunguka Mazito Sakata la Mbowe na Viongozi Wengine wa Chadema
Mbunge wa Singida, Tundu Lissu amesema kitendo cha viongozi wa Chadema kuendelea kushikiliwa na magereza licha ya Mahakama kutoa kibali cha kuachiwa kwa dhamana kuwa huko sio kuwaadhibu bali ni kuwapa upako mkubwa wa kisiasa mbele ya wananchi.


Lissu ametoa kauli hiyo jioni ya leo (Machi 30, 2018) kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii ikiwa imepita siku moja tokea Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Wilbard Mashauri kutoa uamuzi wa dhamana ya Mbowe na wenzake licha ya kuwa hawajafikishwa Mahakamani hapo kwa kile kilichoelezwa kuwa gari walikuwa wamepanda limeharibika.

"Ni ajabu iliyoje kwamba katika wiki ya Pasaka ambayo Yesu Kristo alitiwa kifungoni na baadae kuuawa msalabani, wakaamua viongozi wote wa juu CHADEMA wakamatwe kama alivyokamatwa Yesu Kristo na washtakiwe kama alivyoshtakiwa Yesu Kristo na wasulubiwe kwa kuwekwa mahabusu kama alivyosulubiwa Yesu Kristo msalabani. Hakimu Wilbard Mashauri anayesikiliza kesi ya Mwenyekiti Mbowe na wenzake, amesema wanastahili kupata dhamana na amewapa lakini Polisi wakaamua kutokuwaachia na kuwalazimisha kuwa kifungoni wakati huu wa Pasaka", amesema Lissu.

Pamoja na hayo, Lissu ameendelea kwa kusema "wanafanya hivyo kwa kufikiria kwamba wanawakomesha, hawajui watendalo na Mungu awasamehe pamoja na waliowatuma. Kuendelea kuwafunga watu ambao Mahakama imesema wapewe dhamana sio kuwaadhibu, bali ni kuwapa upako mkubwa wa kisiasa mbele ya wananchi. Ni kuwafanya wahanga wa ukombozi wa pili wa nchi yetu".

Tundu Lissu bado yupo nchini Beljium mpaka hivi sasa kwa lengo la kupatiwa matibabu zaidi kutokana na shambulio alilofanyiwa Septemba 7, 2017 la kupigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa mjini Dodoma na kisha baadae kupelekwa nchini Kenya.

Jina la Ngoma Mpya ya Roma Mkatoliki Lazua Gumzo, Mkewe Ahofia Kumpoteza

$
0
0
ina la ngoma mpya ya Roma Mkatoliki lazua gumzo, Mkewe ahofia kumpoteza
Kila mdau wa muziki nchini Tanzania kwa sasa anahamu ya kusubiri wimbo mpya wa rapa Roma Mkatoliki hii baada ya mkali huyo wa Hip Hop kupitia katika kipindi kigumu cha kufungiwa wimbo wake na yeye mwenyewe kupigwa marufuku ya kutojihusisha na muziki.

Sasa habari nzuri ni kwamba jina la wimbo wake mpya ambao unatarajiwa kuachiwa limeshavuja na sio lingine ni  “NIKIFA CHIMBENI MAKABURI MATATU” jina ambalo limevujishwa na mkewe.

Mkewe na Roma Mkatoliki, Nancy amesema anajua magumu anayopitia mumewe na anawaza endapo ataachia wimbo huo wa “NIKIFA CHIMBENI MAKABURI MATATU” maisha yake yatakuwaje? kwani ugumu wa mashairi yaliyomo kwenye wimbo huo yanamtia hofu.

“Dah Nawazaa Sijui Baba Ataimba Nini Sasa Round hii! Kila Angle Wanakukazia!! Nawaza Ukiachia Ile “NIKIFA CHIMBENI MAKABURI MATATU.“ameandika Mke wa Roma kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Hata hivyo, Nancy amemshauri Roma asiuachie wimbo huo kwani bado anampenda na anahofia kumpoteza.

“Lakini Daaah Bora Ukae Kimya Tu!! Bado Nakuhitaji Mume Wangu!! Nways Tutege Sikio Tu!!“ameandika Nancy.

Kwa upande mwingine, Mashabiki na wadau wa muziki wametoa maoni yao ambapo kila mmoja ameonekana kumsapoti mkewe na Roma wengine wanataka wimbo huo utoke.

saidipeter24 Bora akae kimnya coz hali si shwari
16_geniuz_paranawe ROMA ni kichwa. Ana vingi vya kuimba. Na kimsingi hakuna sababu y kumuwazia kwan ataimba1nin.Jamaa ana akili nyingi sna.
__ambrseBora Kwa kipind hiki aache tu maana wote bado tunamhitaji😳labda aimbe kwaya tu kama anaweza
tmpya Mwmabie asiwe muoga,Kina mandela,nyerere Nk wangekua waoga leo tusngekua hapa.
apologizekii Natamani Nikuunge mkono ila pia na tamani kusikia ladha ya baba
financial9870 Mbona zamani alikua anaimba vzr tu sa hyo kibamia ikipigwa kwenye daladala tunaoneana aibu ikipigwa tupo na famil tunabadili stesheni ikipigwa niko na baby kibamia anahisi namdedicat raha iko wapi?
Alhamisi ya  Machi 29, 2018 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Harrison Mwakyembe alitangaza kumfutia adhabu ya kifungo cha miezi sita rapa Roma Mkatoliki alichopewa na Naibu Waziri wa wizara hiyo Juliana Shonza.

Hakuna asiyefahamu makali ya ngoma za Roma Mkatoliki na wewe mdau wa muziki una lipi la kumshauri Roma Mkatoliki kwa jinsi unavyoona jina la wimbo huo?

Lema Afunguka Haya Baada ya Polisi Kusema Bado Aijafahamika Risasi Iliyomuua Akwilina

$
0
0
Lema Afunguka Haya Baada ya Polisi Kusema Bado Aijafahamika Risasi Iliyomuua Akwilina
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ameongea kuhusu taarifa iliyotolewa na Kamanda wa kanda maalum ya DSM Lazaro Mambosasa kuhusu silaha iliyotumika kumuua Akwilina kuwa bado haijajulikana na wanaendelea na upelelezi.

Lema kupitia akaunti yake ya Twitter ameandikia kuwa ameitafakari kauli ya Mambosasa kuhusu tukio la Akwilina juu ya silaha iliyotumika.

“Nimeitafakari kauli ya Mambosasa inayohusu tukio la Akwilini kuhusu silaha iliyotumika, bila shaka kuna dhambi kubwa inapangwa nawasihi Wana CHADEMA kuwa makini wakati huu kwani si ajabu ukasikia kuwa Ile silaha iliyotumika kumuua Akwilini imekutwa nyumbani kwa Kiongozi wa CHADEMA” -Lema

Nimeitafakari kauli ya Mambosasa inayohusu tukio la Akwilini kuhusu silaha iliyotumika,bila shaka kuna dhambi kubwa inapangwa nawasihi WanaChadema kuwa makini wakati huu kwani si ajabu ukasikia kuwa Ile silaha iliyotumika kumuua Akwilini imekutwa nyumbani kwa Kiongozi wa CHADEMA

Mpaka Kuitwa Mama si Kazi Rahisi – Linah

$
0
0
Mpaka kuitwa mama si kazi rahisi – Linah
Msanii wa muziki Bongo, Linah amecharukia vikali wale wanaokosoa picha za watoto wa wenzao zinapowekwa mtandaoni.

Muimbaji huyo akizungumza na kipindi cha Uhondo, E Fm amesema si vizuri kwa wenye tabia hiyo kwani hadi mtu kufikia hatua ya kuitwa mama si kazi rahisi hata kidogo.

“Mimi kama mzazi ninapoona mwenzangu ameposti picha ya mtoto wake halafu anakuja mtu anasema mtoto wake mbaya, siyo vizuri kwa sababu mpaka kuitwa mama si kazi rahisi,” amesema.

“Kwa hiyo unapokuwa unamsindika mwenzako maneno ya namna hiyo inakuwa siyo vizuri, labda huyo anayeongea hivyo hajazaa, akija kuzaa hajui itakuwaje,” ameongeza.

Soma Pia; Linah hajutii kupiga picha za utupu katika ujauzito wake

Linah alijaliwa mtoto wa kwanza July 25, 2017, kwa sasa muimbaji huyo anafanya vizuri na wimbo ‘Same Boy’ ambayo amemshirikisha Rachel ikiwa ni ngoma ya pili kufanya pamoja.

Hivi Mawakala wa Mabwanyenye Waliosababisha Ndege Yetu Ikamatwe Canada ni Akina Nani?- Tundu Lissu

$
0
0
 Hivi Mawakala wa Mabwanyenye Waliosababisha Ndege Yetu Ikamatwe Canada ni Akina Nani?- Tundu Lissu
Mbunge wa Singida, Tundu Lissu amesema ameona taarifa ya Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa, kwamba ndege aina Bombardier iliyokuwa imezuiliwa Canada inakuja nchini.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Lissu ameandika baadhi ya mambo ambayo angependa baadhi ya watu wanaodai kuwa alitumwa kipindi cha nyuma alipokuwa anazungumzia kushikiliwa kwa ndege hiyo Canada wafahamu.

 ==>>Hii ni kauli yake
Nimeona taarifa ya Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa, kwamba Bombardier yetu iliyokuwa imezuiliwa Canada inakuja. .

Kufuatia taarifa hiyo, baadhi ya watu wamedai mitandaoni kwamba kuletwa kwa ndege hiyo ni pigo na aibu kwa mawakala wa mabwanyenye waliosababisha ndege yetu kushikiliwa Canada.

Mimi nauliza: Hivi 'mawakala wa mabwanyenye' waliosababisha ndege yetu ikamatwe Canada ni akina nani hasa??? .
Here are some basic facts: .

1) Mwaka 2003, kampuni ya Sterling Construction and Engineering Ltd. (SCEL), ilivunjiwa mkataba wake wa ujenzi wa Barabara ya Bagamoyo. Mkataba huo ulivunjwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

2) Baada ya kuvunjwa kwa mkataba, SCEL ilishtaki Serikali ya Tanzania kwenye Mahakama ya Usuluhishi ya International Chamber of Commerce, London. Tunaambiwa baadhi ya hearings, au zote, zilifanyikia Dar Es Salaam. .

3) Mwezi December 2009 na baadae June 2010, Arbitral Tribunal ya ICC ilitoa uamuzi kwamba Serikali ya Tanzania ilivunja mkataba wa SCEL bila uhalali wowote na kuamuru Serikali kuilipa SCEL takriban USD milioni 25, na riba ya 8% kwa mwaka kuanzia tarehe ya hukumu hadi tarehe ya malipo ya mwisho. .

4) Kwa sababu tunazostahili kuambiwa , deni la SCEL halikulipwa kwa miaka saba hadi SCEL walipoenda kwenye Supreme Court of Quebec, Canada, na kupata amri ya mahakama kuikamata Bombardier .

5) Baada ya kusikia Bombardier imekamatwa, Waziri wa Mambo ya Nje, Dr. Augustine Mahiga, na Balozi wetu Canada, Jack Zoka, walitumwa kwenda Toronto kufanya mazungumzo na SCEL juu ya namna ya kujinasua na balaa hili. Waziri Mahiga na Balozi Zoka waliiomba SCEL isitoe habari za Bombardier kukamatwa hadharani. .

6) Tarehe 18 August, 2017, baada ya kupata nyaraka mbali mbali zinazohusu kukamatwa kwa Bombardier , nilitoa taarifa za kukamatwa ndege hiyo kwa waandishi wa habari Courtyard Hotel, Dar Es Salaam. .

7) Kesho yake tarehe 19 August, Kaimu Msemaji wa Serikali, Zamaradi Kawawa, alithibitisha kukamatwa kwa Bombardier  na kutulaumu sisi wapinzani kuwa ndio tuliosababisha ndege yetu ikamatwe Canada. .

8) Licha ya Serikali kukiri ukweli wa maneno yangu, tarehe 20 August, nilikamatwa na askari polisi walioniambia hawajui kosa langu ila wanatekeleza 'maagizo kutoka juu.' Nililazwa mahabusu Central Police Station hadi kesho yake nilipopelekwa kwa Mkemia Mkuu ili kupimwa mkojo. Nilipokataa kupimwa mkojo nilirudishwa mahabusu hadi kesho yake tarehe 22 August nilipoachiliwa huru bila kupelekwa mahakamani. .

9) Alfajiri ya tarehe 26 August, 2017, ofisi za kampuni ya Mawakili ya IMMA Advocates ya Dar Es Salaam, zilishambuliwa kwa mabomu na 'watu wasiojulikana.' Miaka ya nyuma, IMMA Advocates waliwahi kuwa mawakili wa SCEL. Hadi leo hakuna mtu aliyetuhumiwa au kukamatwa na kushtakiwa kwa kuhusika na shambulio hilo la kigaidi. Na hadi sasa Jeshi la Polisi halijatoa taarifa yoyote ya uchunguzi wa shambulio hilo.

10) Tarehe 7 September, 2017, siku kumi na moja baada ya shambulio la mabomu dhidi ya IMMA Advocates, ikawa zamu yangu kushambuliwa kwa risasi za submachine guns na 'watu wasiojulikana.' Nilijeruhiwa vibaya sana, lakini Mungu ni mwema sikufa. Hadi ninapoandika maneno haya, hakuna mtu hata mmoja aliyetuhumiwa au kukamatwa na kushtakiwa kwa kuhusika na shambulio hilo la kigaidi dhidi yangu. Na hadi sasa Jeshi la Polisi halijanihoji mimi wala dereva wangu kuhusiana na shambulio hilo na wala halijatoa taarifa yoyote ya uchunguzi wa shambulio hilo. .

11) Kwa kipindi chote tangu  alipovunja mkataba mwaka 2003 hadi tarehe 18 August, 2017, nilipozungumzia hadharani suala la kukamatwa kwa Bombardier Canada, Serikali ya Tanzania, haikuwahi kuwaambia Watanzania kwamba tunadaiwa mabilioni na SCEL kwa sababu ya kuvunja mkataba na baadae kushindwa kesi. .

12) Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa, na kabla yake Msemaji wa Serikali, Abbas, hawajasema, hadi sasa, ni kwa nini Bombardier yetu ilikuwa imezuiliwa Canada. Hawajasema kama ni kweli au la kwamba ndege yetu ilikuwa imezuiliwa kwa sababu ya  kuvunja mkataba kimakosa .

13) Nafurahi kusikia taarifa za kuachiliwa kwa ndege yetu. Nitafurahi zaidi tukiambiwa Bombardier hiyo imeachiliwa kwa masharti gani, kwa vile tulikuwa tunadaiwa karibu USD milioni 40 zilizotokana na kuvunja mkataba na Serikali kushindwa kesi na SCEL.

Nawatakieni Pasaka njema.

“Ni Vita Yetu Sote, Tukipata Viongozi Wabaya Tunaumia Wote” -Askofu Chengula

$
0
0
“Ni vita yetu sote, tukipata viongozi wabaya tunaumia wote” -Askofu Chengula
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mbeya, Evaristo Marc Chengula, amewataka waumini wa kanisa hilo nchini Tanzania kuchagua viongozi sahihi na watakaokidhi mahitaji yao badala ya kufanya makosa kwa kuchagua viongozi wasiofaa na kuanza kulalamika baada ya uchaguzi.

Askofu Chengula ametoa ujumbe huo katika mahubiri aliyotoa kwenye ibada ya Ijumaa Kuu inayofanyika katika Kanisa la Bikira Maria wa Fatima Parokia ya Mtakifu Francisco wa Asizi, Mwanjelwa mkoani Mbeya.

Amesema imekuwa ni kawaida kwa maaskofu na wadau wengine kuanza kukosoa viongozi baada ya uchaguzi, jambo ambalo halina faida, hivyo wao kama maaskofu mwaka huu wameamua kuwataka waumini wao kuwapima kwa umakini watu wote watakaojitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi zijazo.

“Ni vita yetu sote, tukipata viongozi wabaya tunaumia wote, tukipata viongozi wazuri tutafurahi wote, kila mmoja aone kiu ya Tanzania hii kuwa nchi ya upendo,” -Askofu Chengula
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images