Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Picha: Diamond Platnumz Awa Kivutio Uzinduzi wa Bombadiier ya Tatu...Akutana na Rais Magufuli uso Kwa uso

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza mwanamuziki wa Bongo flavor Naseeb Abdul-Diamond platinum mara baada ya kuweka jiwe la msingi mfumo wa usimikaji wa Rada katika viwanja vinne vya ndege (Mwalimu Julius Nyerere-Dar es Salaam, Mwanza, KIA-Kilimanjaro na Songwe katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza mwanamuziki wa Bongo flavor Naseeb Abdul-Diamond platinum mara baada ya kuweka jiwe la msingi mfumo wa usimikaji wa Rada katika viwanja vinne vya ndege (Mwalimu Julius Nyerere-Dar es Salaam, Mwanza, KIA-Kilimanjaro na Songwe katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU


Rais Magufuli Awashangaa Maaskofu....Ahoji Kwa nn Hawakutoa Waraka Wakati wa Mauaji ya Kibiti

$
0
0

Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa makanisani saizi zaka zimepungua kwa kuwa mafisadi ndio walikuwa wanatoa zaka na kudai kuwa watu ambao walikuwa wamezoea kupata pesa za bure ndiyo wanapiga makelele.

Rais Magufuli amesema hayo jana  alipokuwa akihutubia uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam, wakati akiweka jiwe la msingi kwa ajili ya mradi wa kuongozea ndege katika vituo vinne hapa nchini.

"Ni uhakika pia wapo watu ambao walizoea fedha za bure za kuibia masikini wale ndio wanapiga kelele kweli.

"Nina fahamu hata makanisani zaka zimepungua kwa sababu zingine zilikuwa zinatolewa na mafisadi, lakini sisi Watanzania tusimame twende mbele .Ninawaeleza kwa dhati kwa sababu najua tulikotoka na tunakokwenda. Watendaji wangu hawa wanafanyakazi kubwa kweli" alisema Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli alisema kuwa nchi sasa ipo salama kutokana na jitihada za maafisa wa ulinzi na usalama na kusema anashangaa kuona watu wakati wa mauaji wa kibiti hawatoi waraka.

"Wakati wa mauaji ya Kibiti hatukuona mtu yoyote analaani, kufa kwa Kibiti ni salama hakuna hata waraka uliotoka ingawaje sipendi sana kulizungumzia hili kwa sababu nalijua wala halina msingi sana na wala halitafanikiwa na wala hakuna lolote kwa sababu serikali ipo na nimekabidhiwa na wananchi kuilinda kwa nguvu zote na ninasema kweli kweli wengine nawaangalia tu"

Aunty Ezekiel Ajibu Tuhuma za Kuazima Nguo kwa Wema Sepetu

$
0
0
Mwanadada Aunty Ezekiel amefunguka na kujibu tuhuma zilizokuwa zikimkabili kuhusu tabia yake ya kuazima nguo kwa rafiki yake wa karibu Wema sepetu , tuhuma ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao kila kukicha.

Aunty Ezekiel  amesema kuwa nguo wanayosema ameazima zilishonwa mbli na yeye ndiye  aliyekuwa wakwanza  kuvaa nguo hiyo lakini anashangaa sana watu wanapokuja na kumtuhumu kuhusu swala hilo.

Hata hivyo Aunty anasema kuwa bado kwao sio shida kuvaliana nguo kwa sababu ni marafiki hivyo ni swala la kawaida.

"Kwanza kuazima nguo sio shida kwetu kwa sababu ni rafiki yangu lakini cha ajabu ni kwamba nguo wanayoizungumzia wao zimefanana wala hakuna aliyenda kugonga hodi kwa mwenzake."-Alijibu Aunty

Wawili hao wamekuwa marafiki kwa muda mrefu sasa ingawa hapo katikati walikuwa wakionekana kutokuwa pamoja lakini sasa ivi mapenzi yamerudi na kuwa mapya kabisa.

Download Upya Application Yetu Ya Udaku Special .....Ile Ya Zamani Tutaifuta

Kujichua Ama Kupiga Punyeto Kwa Wanawake/Wanaume, Faida na Hasara zake

$
0
0
Kujichua a.k.a kujichezea a.k.a “a little help from ur hand” (kupiga puri au punyeto sounds manly) sio kwa wanaume tu bali hata wanawake tunafanya hivyo ila wengi wetu huwa hatuko “comfortable” kulizungumzia au kukili kuwa tukizidiwa huwa tunajisaidia…….wakati mwingine mtu unashindwa kabisa kupata usingizi mpaka upige moja-mbili ndio usingizi unakuja au asubuhi unajisikia mzito kuamka kitandani mapaka upige moja ndio nguvu zinakuja…hasa kama umezoea dozi za maana lakini sasa mpenzi hayupo karibu.


Kujichua au kujichezea ni njia pekee ya kujifunza kufika kileleni, kuujua na kuuelewa mwili wako na kujua utamu wa ngono ukoje(incase hujui utamu huo ukoje). Kwa kujichua utajua jinsi kutoa na kupokea raha ya kufanya mapenzi na mpenzi wako, utasaidia ngozi yako kuwa nzuri na laini (mambo ya Urembo hayo) na vilevile utajua jinsi ya kuzuia (kuchelewa kwa makusudi kufikia mshindo) au kumsubiri mwenzio ili mfike pamoja, hakuna raha ya kufanya mapenzi kama kufika kwa wakati mmoja.

Faida za kujichua/chezea:-
1)Kuujua mwili wako na kujiamini zaidi linapokuja swala la kungonoka(fanya mapenzi)
2)Kuongezeka kwa hamu ya kufanyamapenzi kwa vile utakuwa unajua utamu wake.
3)Kujua “vipele vyako viliko”.
4)Kutokuusaulisha mwili wako ikiwa uko nje ya uhusiano au umeamua kuwa single kwa muda.
5)Kuepuka mimba na maambukizo ya virusi vya UKIMWI na magonjwa mengine.

*Kama kuna faida nyingine unaijua basi si mbaya kama utachangia hapa.

Madhara ya kujichua/chezea:-
1)Uchovu wakati wote / Fatigue. Feeling tired all the time.
2)Kujichua kwa kutumia sanamu a.k.a Dildos ni kusamburuka kwa nyama za nyeti zako(inategemea na aina ya sanamu), kupoteza hisia za uume halisi kutokana na kuzoea “dubwana” hizo, kifo kutokana na “shock” ikiwa unatumia ya umeme, vilevile saratani ikiwa unatumia vilainishio ili kurahisisha “dubwana a.k.a toy a.k.a Dildo” kuingia.
3)Maumivu ya nyonga / Lower back pain.
4)Kusinyaa kwa Nywele / Nywele kunyonyoka / Thinning hair / Hair Loss
5)Maumivu ya kiuno

Mke wa Zamani wa Nelson Mandela, Winnie Mandela Afariki Dunia Afrika Kusini

$
0
0
Mke wa Zamani wa Nelson Mandela, Winnie Mandela Afariki Dunia Afrika Kusini
Winnie Mandela, mke wa zamani wa Nelson Mandela, ambaye pia alipigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na miaka 81.

Habari za kifo chake zimethibitishwa na msaidizi wake.

Msemaji wa familia Victor Dlamini amesema kupitia taarifa kuwa: “Amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu, ambapo amekuwa akiingia na kutoka hospitalini mara kwa mara tangu mwnazo wa mwaka.

“Alifariki kwa amani mapema Jumatatu adhuhuri akiwa amezungukwa na familia na wapendwa wake.”

Askofu mstaafu na mshindi wa tuzo ya Nobel Desmond Tutu amemsifu kama “ishara kuu ya vita dhidi ya ubaguzi wa rangi,” kwa mujibu wa AFP.

Bunge la Bajeti Kuanza Leo Dodoma Bila Spika Ndugai

$
0
0
Bunge la Bajeti Kuanza Leo Dodoma
Mkutano wa 11 wa Bunge, ambao ni mahsusi kwa ajili ya bajeti ya serikali kwa mwaka 2018/2019,  unaanza leo mjini Dodoma bila Spika wa Bunge Job Ndugai, ambaye yuko nchini India kwa ajili ya kupatiwa matibabu.


Ndugai yuko nchini humo tangu mwanzoni mwa mwaka huu akipatiwa matibabu na hakuwapo hata wakati wa Mkutano wa 10 ulioongozwa na Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson na Wenyeviti wa Bunge.

Hata hivyo, Bunge lilithibitisha jana (Aprili 02, 2018) kuwa Ndugai hata kuwapo mwanzoni mwa mkutano huo na atarajiwa kurejea nchini wakati wowote kuanzia sasa.

Mbali na Ndugai, mkutano huo unaanza bila kuwapo Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, ambaye yuko rumande pamoja na wabunge wengine wa chama hicho kutokana na kukabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwamo ya kufanya maandamano yaliyosababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline.

Wabunge wengine ni Peter Msigwa (Iringa Mjini), John Mnyika (Kibamba), Esther Matiko (Tarime Mjini) na viongozi wengine wa Chadema ambao ni Katibu Mkuu Dk. Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu.

Pia Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, anashikiliwa na jeshi la polisi baada ya kukamatwa juzi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam, alipokuwa akitoka Afrika Kusini kwa matibabu.

Prof. Tibaijuka Amwaga Machzozi Hadharani Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Prof. Tibaijuka Amwaga Machzozi Hadharani Kisa Hiki Hapa
Mbunge wa jimbo la Muleba Kusini Prof. Anna Tibaijuka amejikuta akimwaga machozi baada ya kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Diwani viti maalumu na Katibu wa umoja wa wazazi {UWT} wilaya Muleba, Paulina Francis ambaye ametumikia nafasi ya udiwani kwa zaidi ya miaka 27 mpaka mauti yanamkuta.

Akiongea baada ya mazishi Prof. Tibaijuka amesema baada ya kutoka Umoja wa mataifa na kuamua kuingia kwenye siasa, marehemu ndo alikuwa mwalimu wake amemuelekeza vitu vingi hivyo anaamini pengo lake si rahisi kuzibika.

Aidha amesema kuwa kwa awamu hii tayari amewapoteza madiwani watatu katika jimbo lake hali ambayo inampa wasiwasi katika utendaji na utekelezaji wa shughuli za maendeleo, huku akisema kuwa alianza Diwani wa kata Kimwani, akafuata diwani wa kata Buhangaza na sasa Diwani viti maalumu wilayani humo.

Hatima ya Akina Mbowe na Wenzake Kujulikana Leo

$
0
0
Hatima ya Akina Mbowe na Wenzake Kujulikana Leo
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wengine watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, leo watafika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ukamilishaji wa masharti ya dhamana waliyopata mwishoni mwa wiki iliyopita.

Machi 27, Mbowe na wenzake walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na makosa nane, ombi lao la dhamana likaahirishwa uamuzi kwa siku mbili ili Hakimu akajiridhishe.

Alhamisi, Hakimu Wilbard Mashauri alikubali ombi la dhamana licha ya washitakiwa kutokuwepo mahakamani siku hiyo kutokana na gari la kuwatoa mahabusu ya Gereza la Segerea kuharibika.

Mbali na Mbowe (56), washitakiwa wengine ni Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (52), Mbunge wa Kibamba John Mnyika (37), Mbunge wa Musoma Mjini, Esther Matiko (41), Katibu Mkuu, Vincent Mashinji (45) na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu (39).

Hakimu Mashauri alisoma masharti ya dhamana kuwa ni washtakiwa kujidhamini kwa hati ya maneno ya Sh. milioni 20, wadhamini wawili kwa kila mshtakiwa wanaotoka taasisi zinazotambulika watakaosaini hati yenye thamani hiyo ya fedha.

Aidha, itakuwa ni mara ya kwanza kwa Mbowe na wenzake kukaa gerezani kwa siku saba.

Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa Februari 16, mwaka huu katika Barabara ya Kawawa eneo la Mkwajuni Wilaya ya Kinondoni, kwa pamoja washtakiwa na wenzao zaidi ya 12, walifanya mkusanyiko na kukaidi amri halali ya ofisa wa Jeshi la Polisi, Gerald Ngiichi na kusababisha kifo cha Akwilina Akwiline na askari polisi wawili Konstebo Fikiri na Koplo Rahim Msangi kujeruhiwa.

Shtaka la tatu, ilidaiwa katika siku ya tukio la kwanza katika viwanja vya Buibui vilivyopo Kinodnoni, Mbowe wakati akiwahutubia wakazi wa Kinondoni, alitamka maneno ya uchochezi kuwa "Ninapozungumza hapa kiongozi wetu wa kata ya Kinondoni Hananasif yupo mochwari... Amekamatwa na makada wa CCM kwa msaada wa vyombo vya ulinzi na usalama... Wamemnyonga, wamemwua halafu sisi tunaona ni jambo la kawaida... Tunacheka na polisi... Tunacheka na CCM", alinukuliwa kwamba alitoa maneno hayo ya kuleta chuki na uchochezi kwa Watanzania.

Pia shtaka la nne ambalo ni kosa la uchochezi na kusababisha chuki miongoni mwa jamii, Jamhuri imedai Februari 16, mwaka huu katika mkutano wa umma uliofanyika viwanja vya Buibui wilayani Kinondoni Dar es Salaam, Mbowe alifanya uchochezi na kusababisha chuki kinyume na sheria kwa kutamka yafuatayo:

"Tumejipa kibali cha kutangulia mbele ya haki... haiwezekani wanaume wazima na akili zetu na wake zetu na watoto wetu tukafanywa ndondocha.. hii ni nchi ya ajabu. Mimi leo nipo hapa kulinda taifa... kule Afrika Kusini Jacob Zuma amelazimishwa kujiuzulu... Robart Mugabe wa Zimbabwe kang'olewa, kang'olewa Waziri Mkuu wa Ethiopia... juzi ameondoka kwa people's power. Magufuli ni mwepesi kama karatasi".

Katika shtaka la tano la uchochezi wa uasi linalomkabili Mbowe peke yake, inadaiwa katika tarehe na maeneo hayo, alihutubia mkutano wa hadhara akiwa na nia ya kupandikiza chuki na dharau kwa Watanzania dhidi ya uongozi wa kisheria uliopo madarakani kwa kusema "Nitaongoza mapambano nchi hii kwasababu tumechoka kuuawa... matokeo ya Watanzania 100 watakaokufa wataleta haki katika taifa hili. Wangapi wapo tayari kuchukua bei hiyo?"

Katika shtaka la sita la uchochezi wa uasi, wakili Nchimbi aliendelea kudai, katika tarehe hiyo hiyo na maeneo hayo mkoani Dar es Salaam, Mbowe alitoa matamshi ya kupandikiza chuki na dharau kwa upande wa raia wa Tanzania dhidi ya mamlaka halali kuwa; "Hii nchi inadharaulika... imejengewa misingi wa uwoga, kwa lugha nyingine wanaume ni kama mademu, si unawaona hao wanavaa suruali, waoga, bure kabisa... juzi ametekwa kijana wetu, wanasema yupo mochuari, haki ya Mungu ingekuwa nchi nyingine Kinondoni ingekuwa majivu... Lissu amepigwa risasi machine gun na vyombo vya dola... Watanzania mnarudi nyuma... kuna mwandishi wa habari leo ana siku 86 amebebwa na vyombo vya dola... suluhu ya nchi hii haipo bungeni. Suluhu ya nchi hii ipo kwa wananchi wenyewe... lakini ili tupate suluhu hiyo... ni lazima tukubali kubeba majeneza... Inawezekana leo mnaogopa kufa... Ni bora tuwabebe wachache hata wakiwa 200 waliokufa katika ukombozi ili hatimaye nchi hii isimame kama nchi ya wanaume wengine katika dunia hii".

Katika shtaka la saba la kushawishi kutendeka kwa kosa la jinai , inadaiwa katika tarehe hiyo hiyo na maeneo hayo, Mbowe alishawishi wakazi wa Kinondoni kutenda kosa la kufanya maandamano na mkusanyiko usio halali.

Katika shtaka la nane la kushawishi utendaji wa kosa la jinai, linalomkabili mshtakiwa wa pili Msigwa, ilidaiwa katika maeneo hayo hayo Msigwa alishawishi raia na wakazi wa eneo hilo kutenda kosa la jinai kwa kutembea mbele ya umma wakiwa na silaha.

Askofu Anusurika Kukatwa Mapanga Kanisani

$
0
0
Askofu Anusurika Kukatwa  Mapanga Kanisani
ASKOFU Wilberforce Luwalira wa Kanisa la Roma la Mtakatifu Paulo, Namirembe nchini Uganda  alinusurika kifo baada ya Herbert Kadu (35), kuibuka ghafla kanisani akiwa ameshika panga na kumkimbilia nalo madhabahuni wakati ibada ya Pasaka ikiendelea.


 Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi nchini Uganda wakati Askofu Luwalira akiendesha ibada ya Pasaka kanisani hapo.

Ujumbe wa video fupi uliosambaa jana kwenye mitandao ya kijamii unaonyesha ibada hiyo ikiendelea,  ghafla Kadu akiwa amebeba panga alianza kumkimbilia eneo la madhahabuni alikokuwa askofu huyo.

Kabla ya kumfikia askofu huyo, Kadu alijaribu kuruka kizingiti kilichotenganisha eneo la madhabahu na waumini na katika jitihada hizo alianguka na kukamatwa na wasimamizi na waumini ndani ya kanisa hilo.

Kijana huyo alijaribu kuruka kizingiti ili kwenda kwa askofu ambaye wakati huo alikuwa amesimama na msaidizi wake wakiendelea na ibada, na baada ya kuruka alidondoka upande wa madhahabu.

Wasaizidi wa askofu huyo walimdhibiti kijana huyo na kumbeba kumwondoa ndani ya kanisa hilo ili asitekeleze kusudio lake.

Taarifa zilizopatikana kanisani hapo zilisema kijana huyo aliwasili kanisani hapo akiendesha gari aina ya 'kipanya' Super Custom na kuegesha lango kuu la kuingilia kanisani hapo.

“Alipoingia alimpiga mlinzi wa getini na kuingia kwa nguvu kanisani na alikaa kanisani muda mrefu hadi ibada ilipokaribia kuisha ndipo alipojaribu kwenda madhabahuni,” shuhuda alisema katika video hiyo.

Taarifa ilisema baadaye askari walimkamata na kumpeleka kituo cha polisi Namirembe kwa mahojiano.

Tatua Matatizo yako Kwa Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu Pamoja na Mitishamba...

$
0
0
YULE MTAHALAM WA DUA NA DAWA ZA KIARABU NA ZA KIASILI YANI MITI SHAMBA SHARIFU LUKUMANI SASA YUPO HEWANI WENYE SHIDA ZITUATAZO CHEO KAZINI,KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI,MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME,ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA,KISUKARI,FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO

 ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE WASILIANA NAE KWA NAMBA
 0762899488
0656145170
WhatsApp namba +255620665635

Video: Hivi Ndivyo Daimond Alivyoimba Mbele ya Rais Magufuli

$
0
0
Video: Hivi Ndivyo Daimond Alivyoimba Mbele ya Rais Magufuli
Msanii nyota Diamond Platnumz leo amepata fursa kuimba mbele ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli mapema leo jioni wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi mradi wa radar nne leo, ambapo pia Rais Magufuli alipokea ndege mpya aina ya Bombadier Q400.

Mtanange wa Simba na Njombe Mjini Kupigwa Leo

$
0
0
Mtanange wa Simba na Njombe Mjini Kupigwa Leo
Mtanange wa kiporo cha Ligi Kuu Bara uliokuwa unasubiriwa kwa hamu kati ya Njombe Mji dhidi ya Simba SC unapigwa leo Sabasaba Stadium.

Simba inaingia kucheza mechi hiyo baada ya awali kusogezwa mbele ili kuipa nafasi ya kujiandaa na mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Al Masry SC.

Kuelekea mechi hii, Simba inaweza ikamkosa mchezaji wake, kiungo Jonas Mkude, aliyeumia kifundo cha mguu japo siku mbili zilizopita alianza mazoezi mepesi chini ya unagalizi wa daktari, Yassin Gembe.

Endapo Simba wataibuka washindi katika mchezo huo, watazidi kuipa kisogo Yanga kwa kufikisha alama 49 dhidi ya 46 za Yanga iliyo nafasi ya pili.

Mara ya mwishi timu hizi zilipokutana, Simba ilishinda kwa jumla ya mabao 4-0 kwenye mzunguko wa kwanza wa ligi. 

Nafasi za Ajira zilizotangazwa Leo

Breaking News: Mahakama Yamtia Hatiani Masogange kwa Matumizi ya Dawa za Kulevya

$
0
0
Breaking News: Mahakama Yamtia Hatiani Masogange kwa Matumizi ya Dawa za Kulevya
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemtia hatiani msanii wa video za muziki wa kizazi kipya Agnes Gerald, maarufu Masogange kwa kosa la kutuma dawa za kulevya. Hukumu bado haijasomwa.

Breaking News: Agnes Masogange Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela

$
0
0
Breaking News: Agnes Masogange Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu video queen, Agnes Gerald ‘Masogange’ kulipa faini ya Shilingi Milioni 1.5 ama kwenda jela miaka 3 baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Kutokana na hukumu hiyo, Wakili wa utetezi Nehemiah Nkoko amesema kuwa watalipa faini.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri amesema kuwa katika ushahidi wa kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi 3, huku utetezi ukiwa na shahidi 1.

Hakimu Mashauri amesema kuwa ameridhishwa pasina kuacha shaka juu ya ushahidi wa upande wa mashtaka hasa kwa uthibitisho uliotolewa na Mkemia Mkuu wa serikali kwamba mkojo wa mshtakiwa ulikutwa na chembe chembe za dawa za kulevya.

“Kutokana na kujiridhisha na ushahidi huo, namtia hatiani mshtakiwa kwa makosa hayo ya kutumia dawa za kulevya,”-Hakimu Mashauri

Baada ya Masogange kutoa utetezi wake, Hakimu Mashauri amesema kuwa ameusikia utetezi wa mshtakiwa kwamba apewe adhabu ndogo, huku upande wa mashtaka ukitaka apewe adhabu kali.

“Nimesikiliza maelezo ya pande zote, katika kosa la kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin namuhukumu mshtakiwa kulipa faini ya Sh.Mil 1 ama jela miaka 2.

” Katika kosa la pili la kutumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam, nakuhukumh kulipa faini ya Sh.Laki 5 ama jela miezi 12,”  amesema Hakimu Mashauri.

Je Kweli Tanzania imeshikwa tu na WCB

$
0
0
WCB wameshawapumbaza wabongo kweli...Diamond akifanya kitu tu ni Breaking News ..kiato kimekatika breaking news. kifesi kuachishwa kazi breaking news.. kiba kuoa mombasa wamemupotezea... kiba sijuwe kafanya nini hawataki kujuwa ... kila wanachotaka kujuwa nikujuwa ya WCB whyyyyy whyyyyy yoooooooooo

Mtulia, Mollel wa Siha Waapishwa Leo Bungeni

$
0
0
BUNGE la kumi na moja limeanza leo Aprili 3 ambapo Naibu Spika, Tulia Ackson, amewaapisha wabunge wawili, Dkt. Godwin Mollel wa Siha na Maulid Mtulia wa Kinondoni.



Wabunge hao wameapishwa kufuatia uchaguzi mdogo katika majimbo ya Siha na Kinondoni,  ambapo wabunge hao walihamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).



Mtulia, alikuwa mbunge wa Kinondoni kupitia Chama cha Wananchi  (CUF), kabla ya kuhamia CCM na kugombea tena jimbo hilokupitia chama hicho.  Mollel, alikuwa mbunge wa Siha kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo  (Chadema) kabla ya kujiunga na CCM.



Hata hivyo,  kiapo hicho hakikushuhudiwa na idadi kubwa ya wabunge wa upinzani ambao hawakuwepo katika kikao hicho.

FA Amwagia Sifa Lady Jay D

$
0
0
FA Amwagia Sifa Lady Jay D
MARA baada ya kushuka jukwaani katika shoo ya Anaweza iliyofanyika usiku wa kuamkia Aprili Mosi, ndani ya Ukumbi wa Police Officers Mess uliopo Oysterbay jijini Dar, kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka mitano, mkongwe wa Bongo Fleva, Hamis Mwinjuma ‘FA’ alimfagilia mkongwe mwenzake, Judith Wambura ‘JayDee’ kuwa ameonesha ukakamavu kuandaa shoo kivyake bila kutegemea promota.



Kwa muda mrefu, FA na JayDee walikuwa ‘hawapikiki chungu kimoja’ huku chanzo kikitajwa ni kuharibiana kwenye kuandaa shoo, lakini kipindi cha hivi karibuni wawili hao walipatana baada ya kupostiana mitandaoni kazi zao, shoo ya Anaweza imewaleta tena karibu zaidi.



Katika usiku huo, JayDee ndiye aliyemkaribisha jukwaani FA na kuimba naye baadhi ya ngoma walizotamba nazo ambapo walikumbushia Ngoma ya Msiache Kuongea na Hawajui huku shangwe zikiwa za kutosha jukwaani ‘mixer’ mapichapicha ya kamera za simu mpanguso.



Akichonga na Star Showbiz, mara baada ya kushuka jukwaani, FA alianza kwa kumfagilia JayDee; “Wasanii wakubwa kiwango cha Lady JayDee walitakiwa kuwa na shoo zao siyo kutegemea mapromota wawaandalie, kwa hiyo kitu kilichonivutia kwake na kuamua kumsapoti ni kitendo cha kuandaa shoo mwenyewe,” alisema FA.



Kivutio kikubwa kwenye shoo hiyo kilikuwa kwa mkongwe mwingine wa Bongo Fleva, Bushoke ambaye aliwa-kumbusha mashabiki kwa kibao chake cha zamani cha Usiende Mbali Nami. JayDee alipiga nyimbo zake nyingi kama vile Ndi Ndi Ndi, Sawa na Wao na mwisho alimaliza kwa kuutambulisha wimbo wake wa Anaweza alioshirikiana na mkongwe wa Muziki wa Reggae kutoka Jamaika, Luciano.



Sapraiz nyingine katika usiku huo wa Anaweza alikuwa Ben Pol ambaye aliingia na kuimba ‘live band’ vibao vyake kadhaa kama vile Maneno, Phone na Moyo Mashine.Msanii Alawi Junior pamoja na Nikki Mbishi nao walipamba usiku huo kwa kuliteka jukwaa.

Wema Sepetu ni Maliasili ya Taifa – Idris Sultan

$
0
0
Wema Sepetu ni maliasili ya taifa – Idris Sultan
Baada ya kuvuja kwa picha na video zikimuonesha mrembo Wema Sepetu akiwa kwenye Swimming Pool, video ambazo zilizua gumzo mitandaoni wiki iliyopita. Hatimaye aliyewahi kuwa Boyfriend wake Idris Sultan amesema picha hizo aliziona na amechukulia kawaida.

Akiongea na waandishi wa habari Jumapili Aprili 01, 2018. Idris amesema kuwa Wema Sepetu ni maliasili ya taifa hivyo hakuna tatizo kama akiamua kuonesha mwili wake kwani watu wengi wanataka kuuona.

Idris alipoulizwa tukio la kuvuja kwa video hizo za Wema alilipokeaje? alijibu “Maliasili ya taifa i think ina haki ya kuoneshwa kwa wananchi wanaotaka kuiona”



Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images