Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Diamond, Samatta Waitwa Marekani Kutunukiwa Tuzo

$
0
0
Diamond, Samatta Waitwa Marekani Kutunukiwa Tuzo
Mwanamuziki wa kizazi kipya, Nassib Abdul maarufu Diamond Plutnumz na mwanasoka wa kimataifa, Mbwana Samattapamoja na Watanzania watatu na raia wa Marekani, wameteuliwa kutunukiwa tuzo katika tamasha lililoandaliwa na Watanzania waishio ughaibuni (Diaspora) litakalofanyika Dallas nchini Marekani.

Katika tuzo hizo atapewa  Dk Steve Meyer ambaye ni daktari bingwa katika Hospitali ya Mercy iliyopo jiji la Sioux, Marekani aliyewatibu manusura wa ajali ya wanafunzi wa Lucky Vincent.

Akizungumza na gazeti hili kutoka Dallas jana, mratibu wa tamasha hilo, Ben Kazora alisema wanampa tuzo daktari huyo kwa kutambua mchango wake katika kuokoa maisha ya watoto hao.

“Sote tunatambua namna ajali ilivyokuwa mbaya na ilivyopoteza wapendwa wetu wengi. Dk Meyer na timu yake walifanya kila njia kuokoa maisha ya watoto wale watatu walionusurika,” alisema.


“Tunampa Diamond zaidi kwa kutumia kipaji chake cha muziki kuitangaza nchi kitaifa na kimataifa, vivyo hivyo Samatta kwa kutumia kipaji chake cha kusakata kabumbu kuitangaza Tanzania,” alisema.

Kwa mujibu wa Kazora, mwingine ni mwanariadha John Akhwari ambaye mwaka 1968, alimaliza mbio katika michezo ya Olympic iliyofanyika Mexico City licha ya kuumia mguu.

Naye meya wa Dallas Texas nchini Marekani, Mike Rawlings aliwakaribisha Watanzania hao kushiriki tamasha la Tanzania Day, litakalofanyika jijini humo kwa lengo la kutangaza fursa za biashara na utalii.



Real Madrid Yaichapa Juventus Bao 3-0

$
0
0
 Real Madrid Yachapa Juventus Bao 3-0
Klabu ya Real Madrid ya Hispania imeichapa Juventus ya Italia bao 3-0 katika Michuano ya Ligi ya Klabu Bingwa barani Ulaya usiku wa kuamkia leo.

Katika mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa nyumbani wa Juventus, Allianz Stadium, mabao ya Madrid yalifungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya 3 na 64 huku Marcelo akifunga ukurasa wa mabao kunako dakika ya 72.

Mchezo huo wa raundi ya kwanza unaitengenezea mazingira mazuri Real Madrid kusonga mbele hatua ya nusu fainali endapo italinda matokeo yake katika mzunguko wa pili.

Mbali na Madrid, Klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani imepata ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Sevilla ya Hispania.

Sevilla wakiwa katika Uwanja wao wa nyumbani, Estadio R. Sanchez Pizjuan walifungwa magoli hayo na Thiago Alcantara dakika ya 68 na Jesus Navas aliyejifunga 37.

Bao la Sevilla lilifungwa na Pablo Sarabia dakika 31 ya mchezo huo.

JUVENTUS (4-2-3-1): Buffon 6; De Sciglio 5, Barzagli 5, Chiellini 6, Asamoah 5 (Mandzukic 69, 5); Khedira 6 (Cuadrado 75, 6), Bentancur 6.5; Costa 5 (Matuidi 69, 6), Dybala 4, Sandro 5; Higuain 6.

BOOKINGS: Bentancur, Dybala



OFF: Dybala 67

SUBS: Szczesny, Cuadrado, Marchisio, Rugani, Lichtsteiner.

MANAGER: Max Allegri

REAL MADRID (4-3-1-2): Navas 6.5; Carvajal 6.5, Ramos 7, Varane 6, Marcelo 7; Modric 7 (Kovacic 82), Casemiro 6.5, Kroos 7; Isco 8 (Asensio 75, 6); Benzema 6 (Vazquez 59, 6.5), Ronaldo 9.



GOALS: Ronaldo 3, 64, Marcelo 72.

BOOKINGS: Ramos, Kovacic.

SUBS: Casilla, Vallejo, Bale, Hernandez.

MANAGER: Zinedine Zidane

REF: Cuneyt Cakir (TUR).

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Makao Makuu ya YouTube Yavamiwa, Wafanyakazi Wapigwa Risasi

$
0
0
Makao Makuu ya YouTube Yavamiwa, Wafanyakazi Wapigwa Risasi
Mwanaharakati mmoja wa wanyama nchini Marekani ametekeleza tukio la kisasi la kuwashambulia kwa risasi wafanyakazi wanne wa mtandao wa YouTube baada ya malalamiko yake mengi aliyokuwa akiwatumia kushindwa kufanyiwa kazi.

Nasim Aghdam, 39, has been identified as the woman who shot a man and two women with a handgun when she stormed YouTube's headquarters in San Bruno, California on Tuesday
Mwanaharakati Nasim Aghdam aliyetekeleza tukio hilo.

Mwanamke huyo aliyetambulika kwa jina la Nasim Aghdam (39) mkazi wa California Jana Aprili 04, 2018 alitembelea Ofisi za Makao makuu ya YouTube mjini San Bruno na kufyatua risasi kwa kutumia bastola ambapo baada ya tukio hilo alijiua kwa kujipiga risasi mwenyewe.

Mtandao wa Washington Post umeeleza kuwa mwanamke huyo alitekeleza shambulizi hilo baada ya kutuma malalamiko yake kwa zaidi ya mara tano kuhusu mtandao huo kuwa unanyanyasa watumiaji wake na umekuwa na sera za kidikteta.

Baadhi ya malalamiko ya Nasim kuhusu malipo ya mtandao wa YouTube
Aghdam was a prolific YouTuber who had ranted online against the company's new policies and for 'censoring her videos and not paying her'
Nasima alianza kuulalamikia mtandao wa YouTube kwa kuposti mabango kwenye mitandao miingine ya kijamii akitaka watu waususie mtandao huo kutokana na sera zake za kidikteta.

Mtandao wa YouTube umethibitisha taarifa hizo ambapo ulitangaza watu wanne kujeruhiwa vibaya lakini baadaye majeruhi watatu waliaga dunia.


Tayari Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao wa YouTube, Susan Wojcicki kupitia ukurasa wake wa Twitter ametoa pole kwa ndugu na jamaa waliyopatwa na tatizo hilo.

Hata hivyo, mpaka sasa hakuna taarifa yoyote mbaya kutoka kwa jeshi la polisi mjini California juu ya majeruhi hao wanne.

Rais wa Marekani, Donald Trump naye kupitia ukurasa wake wa Twitter ametoa pole kwa wafanyakazi wa mtandao wa YouTube.

Kesi ya Abdul Nondo Yapamba Moto Mahakama Kuu

$
0
0
Kesi ya Abdul Nondo Yapamba Moto Mahakama Kuu
Mahakama Kuu ya Tanzania imeahirisha kesi ya Abdul Nondo dhidi ya DPP, DCI na IGP mpaka tarehe 11, April mwaka huu ambapo itasikilizwa tena ambapo leo Jaji Rehema Sameji alipanga kutoa uamuzi.

Kulikuwa na mabishano ya pande zote mbili leo katika kesi hiyo ambapo Jaji Sameji aliahirisha kesi hiyo mpaka tarehe 4 ambapo Mahakama itaangalia kama itatoa maauzi au la!

Akiongea na Bongo5 leo, Mwanasheria wa Mtandao wa Wanafunzi, Paul Kisabo amesema kuwa “Leo tulifika Mahakama Kuu kwaajili ya kusikiliza kesi ya Abdul Nondo dhidi ya AG, DCI na IGP na Jaji Rehema Samuji alipanga kutoa uamuzi leo tarehe 4, April baada ya mabishano baina ya pande zote mbili leo katika Mahakama Kuu Mh. Jaji Sameji amesema kwamba amehairisha kesi mpaka tarehe 11 mwezi wa 4 ambapo itakuja kwaajili ya kusikilizwa na siku hiyo mahakama itaangalia kama siku hiyo itakuja kutoa tena maamuzi,” amesema Kisabo.

Mbunge Aukosoa Wimbo wa Taifa

$
0
0
Mbunge Aukosoa Wimbo wa Taifa
Mbunge wa Mbinga mjini, Sixtus Mapunda amedai bungeni kuwa, wimbo wa Taifa unaoimbwa bungeni si rasmi na amehoji kama ni sahihi kuendelea kuutumia.

Kwa mujibu wa Mbunge huyo, alieleza kuwa huo unaotumika bungeni una makosa matatu yakiwemo ya maneno, ala na midundo.

Ameyasema hayo kwenye kikao cha kwanza cha Mkutano wa 11 wa Bunge wakati anaomba mwongozo wa Spika baada ya kipindi cha maswali na majibu.

Kwa mujibu wa Mh.Mapunda, wimbo wa taifa unaotumika bungeni ni tofauti na ulioidhinishwa na lililokuwa Baraza la Muziki Tanzania (BAMUTA) na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA).

Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson amesema, kabla ya kutoa mwongozo alisema ni lazima ajiridhishe kwa kuusikiliza kwanza“Kwa hiyo kama kutakuwa na makosa nitatoa mwongozo hapo baadaye.” alisema Dk. Ackson.

Yondani, Chirwa, Tshishimbi Wapigwa Stop na CAF

$
0
0
Yondani, Chirwa, Tshishimbi Wapigwa Stop na CAF
Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limetoa taarifa kwa klabu za Yanga   na Wolaitta Dicha SC ya Ethiopia ambayo imesema wachezaji wanne wa Yanga na wawili wa Wolaitta hawatacheza katika mechi kati ya timu hizo ambayo itachezwa mwishoni mwa juma hili kutokana na kuonyeshwa kadi mbili za njano katika michezo iliyopita baina ya timu hizo.

Wachezaji wa Yanga watakaohusika ni Kelvin Yondani, Obrey Chirwa, Papy Tshishimbi na Said Juma, ambapo kwa upande wa Wolaitta ni Teklu Tafese na Eshetu Mena.


Riyama Amtolea Uvivu Aliyemsema kwa Kukosa Tuzo za Sinema Zetu

$
0
0
Riyama Amtolea Uvivu Aliyemsema kwa Kukosa Tuzo za Sinema Zetu
Leo April 4,2018 story ambayo imechukua headlines ni kutoka kwa muigizaji mkongwe katika tasnia ya Bongo Movie Riyama Ally hii ni baada ya ku-post maneno ya kashfa kutoka kwa shabiki ambaye alisema kuwa hajui kuigiza zaidi ya kuchamba na kuandika caption ambayo imejibu yale maneno ambayo yalitoka kwa shabiki.

Kupitia instagram account ya Riyama Ally ameandika>>> “Dah kweli ushabiki kitu kibaya sana hasa kushabikia kitu usichokijua nikujibu kwa faida ya wengine, mimi hizo tuzo sizifahamu kabisa na ndio maana sikuwahi ku-post chochote katika ukurasa wangu kwasababu sina taarifa yoyote pia sina taarifa rasmi kutoka kwa wahusika kuwa dada Riyama Ally” -Riyama

“Tulikuchomeka katika tuzo zetu na kingine nilikuta missed calls katika simu yangu nikakuta na ujumbe umeandikwa nikafate kadi siku moja kabla ya tuzo ambayo ni Jumamosi tarehe 31 nikafate kadi kwa wahusika wa tuzo husika tuzo zilikuwa jumapili tarehe 1 skujibu SMS nilikaa kimya na sikutaka kuliongea nilitaka wafanye walichokipanga kisha basi kwani zikifurahi nafsi zao na yangu itafurahi zaidi………..”

Maneno yamekuwa mengi kwenye mitandao ya kijamii baada ya tuzo hizo kufanyika siku ya Jumapili April 1,2018 na kusemekana kuwa tuzo hizo hazikutendewa haki kwa wale waliopokea tuzo hizo kwani kuna waigizaji wengi wenye vipaji.

Harmonize Atembelea Mbuga za Serengeti Kula Bata na Mpenzi Wake Sara

$
0
0
Harmonize Atembelea Mbuga za Serengeti Kula Bata na Mpenzi Wake Sara
Harmonize na mpenzi wake Sarah wameamua kwenda kupumzika kwa muda kwenye mbuga ya wanyama ya Serengeti.



Wawili hao wamelazimika kusimamisha ratiba zao zote na kuamua kwenda kujionea maajabu kwenye mbuga hiyo maarufu duniani iliyopo wilayani Serengeti, mkoani Mara na wameonekana kupokelewa kwa shangwe kubwa.







Haji Manara Awapa Somo Bongo Movie

$
0
0
Haji Manara Awapa Somo Bongo Movie
Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara amewataka Watanzania wawe wepesi wa kutoa pongezi pale wasanii wa filamu nchini Tanzania (Bongo Movie) wanapofanya vizuri, na sio kuwapeza na kuwaponda kila siku kwani kitendo hicho kinawakatisha tamaa waigizaji wetu.


Akizungumza wikiendi iliyopita kwenye sherehe za ugawaji wa tuzo za SZIFF, Manara amesema kuwa Tasnia ya Bongo Movie ni moja ya tasnia kubwa nchini Tanzania na wasanii wenyewe ndio waliyopigania kuifikisha hapa, hivyo ni wajibu wao kutaka kusonga mbele au kusalia hapa hapa.

Akitoa ushauri kwa waigizaji, Manara amewaomba wasanii wa Bongo Movie kama wanataka kufika mbali lazima wawe makini na wabunifu kwenye kazi zao na pia waache utoto na kutambua kuwa filamu ni kazi kama kazi nyingine.

Mwanamke Aliyetekeleza Shambulio You Tube Ajiua kwa Risasi

$
0
0
Mwanamke Aliyetekeleza Shambulio You Tube Ajiua kwa Risasi
Mwanamke mmoja nchini Marekani amefanya shambulio la risasi katika Makao Makuu ya Youtube karibu na eneo la San Francisco na kujeruhi watu watatu na yeye mwenyewe kujiua kwa kujipiga risasi.

Mpaka sasa polisi hawajafahamu nini hasa kilisababishwa mwanamke huyo kufanya shambulio hilo katika ofisi hizo. Mwanamke huyo anakadiriwa kuwa na umri kuanzia miaka 30 na kuendelea.

Inaripotiwa kuwa mwanamke huyo alisogea karibu na mlango wa kutokea wa ofisi hizo na eneo la kulia chakula wakati wa chakula cha mchana na kuanza kufanya shambulio hilo

Huu Hapa Ujumbe wa Elizabeth Michael “Lulu” Kutoka Gerezani

$
0
0
Huu Hapa  Ujumbe wa Elizabeth Michael “Lulu” Kutoka Gerezani
Inawezekana ukawa miongoni mwa watu walio-miss kuona au kusikia kazi za muigizaji Elizabeth Michael “Lulu” maana tokea apelekwe jela kutumikia kifungo chake cha miaka miwili imekuwa ngumu kusikia au kuona kazi zake za sanaa.


Hizi ni salamu zake kwa mashabiki kutoka kwa mtu wake wa karibu ambaye ni Dr Cheni ameandika salamu hizo kupitia instagram account yake.

>>>“Hongera sana @elizabethmichaelofficial( LULU)  Kwanza niwapongeze kwa hii program nimekuwa mfuaatiliaji na naamini itakuwa na ‘Impact’ kubwa kwenye jamii. Kikubwa mimi Mahsein @drchenitz ni Muwakilishi, nimeleta ‘pic kadhaa za Pads ambazo zitakuwa msaada kwa Wasichana wakitanzania.”

” Huu ni mzigo wa Elizabeth Michael (LULU),  Ameomba niwasilishe kwenu. Nimekuwa nikimtembelea mara kadhaa kumjulia hali na yeye ameomba ashiriki kwenye kampeni hii ingawaje hayupo. Yupo (jela) Zaidi amesema niwaambie. ANAWAPENDA saana, na anawataka mabint wa kitanzania wawe huru katika kutimiza malengo yao, wasikate tamaa na Mungu atawasimamia.”

Gavana Ashtakiwa kwa Tuhuma Ubakaji DRC

$
0
0
Gavana Ashtakiwa kwa Tuhuma Ubakaji DRC
Naibu Gavana wa jimbo la Ikweta kusini magharibu nchini Jamuhuri ya demokrasia ya Congo ,Tathy Bikamba ameshtakiwa kwa tuhuma za ubakaji wa binti wa miaka 20 ambaye inadaiwa kuwa alimfanyia unyama huo baada ya kumpa dawa za kulevya.

Gavana huyo anatarajiwa kufikishwa kinshasa kujibu tuhuma hizo mahakamani , ingawa wakili wake ametupia mbali tuhuma hizo.

Taarifa kutoka duru za karibu za uchunguzi wa kesi hiyo ya kubaka vinasema kwamba gavana huyo alimbaka binti huyo siku ya Jumamosi.

Bwana Bikamba ambaye kwa sasa yuko gerezani anatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo ili aweze kujibu mashtaka yake ya kumwekea dawa ya kulevywa na kumfanyia tendo la ngono binti bila idhaa yake.

Wakili wa gavana huyo, Imbambo Engulu ametupilia mbali tuhuma hizo na kushutumu mahakama ya jimbo hilo kwa kumzuia gavana huyo bila kujali na cheo chake

"Kushikwa kwake ni kama uonevu, tuliomba wamuzuie kwanza nyumba kwake badala ya kumuweka gerezani moja kwa moja, majaji hawakukubali ombi letu, Nawambia kweli kuwa gavana hakufanya kitendo hicho, ni uongo."

Waziri wa sheria ,Faida mwangiliwa ambaye pia ni miongoni mwa wanaharati wa haki za wanawake ameomba sheria kumhukumu vikali gavana huyo ikiwa tuhuma hizo zitathbitishwa na mahakama

Kesi za ubakaji zimeripotiwa nyingi nchini jamuhuri ya kidemokrasi ya kongo, idadi kubwa ya kesi imefanywa na waasi na wanajeshi wa taifa husuan mashariki mwa DRC.

Katika miaka ya hivi karibuni, serikali ya kongo tayari kuathibu vikali askari kadhaa na maafisa wa jeshi la Kongo wengi kwa kuwapa kifungo cha maisha .

Hatima ya Wema Sepetu Kujulikana Aprili 23

$
0
0
Hatima ya Wema Sepetu Kujulikana Aprili 23
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Aprili 23, 2018 itatoa uamuzi kama Wema Sepetu  na wenzake wawili kama wana kesi ya kijibu au la.

Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi watano wa upande wa mashtaka na kuufunga ushahidi wao.

Machi 23, 2018 upande wa utetezi uliwasilisha hoja katika Mahakama hiyo ili waone washtakiwa hao hawana kesi ya kujibu.

Mbali na Wema, wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya kutumia dawa za kulevya ni Angelina Msigwa  na Matrida Seleman Abbas.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

Polisi aeleza alivyokuta misokoto nyumbani kwa Wema

Inadaiwa  kuwa  Februari 4, 2017 katika makazi ya Wema huko Kunduchi Ununio  washtakiwa hao walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Wema anadaiwa kuwa Februani Mosi, 2017 katika  eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam, alitumia dawa za kulevya  aina ya bangi.

Nikki Mbishi Aeleza Hisia Zake Kuhusu Wasafi TV, Babu Tale Amjibu Hivi

$
0
0
Nikki Mbishi Aeleza Hisia Zake Kuhusu Wasafi TV, Babu Tale Amjibu Hivi
Rapa Nikki Mbishi amekuwa msanii wa kwanza kuonesha hisia zake kuhusu channel mpya ya Wasafi TV iliyoanza kurusha matangazo yake Jumapili Aprili 01, 2018, kwa kuwapongeza viongozi wa kituo hicho cha runinga.


Nikki Mbishi amesema alichofurahishwa zaidi na kituo hicho ni kwamba kimeanza kwa kupiga nyimbo mchanganyiko na bila ubaguzi kitu ambacho kinapelekea ushindani wenye usawa ambao awali haukuwepo kwenye media nyingine.

“Asante Wasafi TV nyie mmecheza wimbo wangu #NIMEKUMISS bila hata mimi kuwaletea, najua ndio mnaanza ila msisahau kuendelea hivi hivi. Hakuna kitu kinachojenga na kuimarisha misingi ya sanaa kama ushindani wenye usawa “Fair Competition” hii inamaanisha anayestahili na apate na asiyestahili akose japo fitna zipo tu,“ameandika Nikki Mbishi kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuelezea zengwe zilizokuwa zinafanywa na vituo vingine.

“Tumeshuhudia umwinyi na ubeberu kwa kipindi kirefu sana,wapo ambao walitaka uMungu mtu lakini walijishtukia wakabwaga na wengine walibwagwa na hiyo ni kwa sababu ya kuleta umatabaka wa kanda fulani na kanda fulani na kujuanajuana sana kiasi kwamba akina sisi tusiofungamana nao tukaishia kutengwa na kuonekana “VINEGA” Kila la kheri kwenye hii ligi ya mbuzi kuna siku daraja litapanda tutacheza ya ng’ombe na mpaka tembo nini simba. Ipo siku watajihoji na kujijibu wenyewe.“ameeleza Nikki Mbishi.

Hata hivyo, pongezi na ushauri huo umepokelewa kwa mikono miwili na Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale. Ambapo amemjibu kwa kushukuru “Asante bwana UNJU hii ni yetu sote na tunaamini hata kwengine wataanza kupiga kwenye kuweka usawa. Mwanzo mgumu ila Mungu atatusimamia sababu tunania ya kweli na sio ushindani na mtu. Haya mtag msanii yeyote ambaye aujamuona akichezwa kokote ili huku kwao aanze kupigwa maana hii ni ya kwetu sote @wasafitv “.

Mwaka 2016, rapa Nikki Mbishi aliingia kwenye headline baada ya kutoa wimbo wake wa ‘Babu Talent’ ambao mashabiki wengi waliutafsiri kama dongo kwa Babu Tale, ambapo wimbo huo unamzungumzia mtu ambaye ananyonya wasanii wa muziki na kubania baadhi ya kazi zao kutoka.

Wabunge wa Upinzani Wasusia Bunge Viti Vyao Vyabaki Tupu

$
0
0
Wabunge wa Upinzani Wasusia Bunge Viti Vyao Vyabaki Tupu
Wabunge wa upinzani wakiwamo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ni kama wamesusia Mkutano wa 11 wa Bunge ulioanza vikao vyake mjini Dodoma jana huku viti vyao vikionekana vitupu.



Aidha, kutokana na kutokuwapo bungeni kwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), swali laki ilibidi liulizwe na Mbunge wa Liwale, Zuberi Kuchauka (CUF).



Wabunge hao wameshindwa kuhudhuria vikao hivyo ambapo jana wabunge waliokuwapo walikuwa wanne tu kutoka Chama cha Wananchi (CUF) na wabunge wawili wa Chadema.



Hata hivyo, leo wabunge wa Chadema hawakuwapo kabisa ambapo baadaye walionekana wabunge wawili tu, akiwamo Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea na Mbunge wa Viti Maalumu, Rose Kamili ambao walionekana kwa muda mfupi kwa nyakati tofauti na kupotea.



Kubenea aliingia bungeni asubuhi na kutoka kabla ya kikao kuanza huku Kamili akionekana nje ya ukumbi wa bunge bila kuingia ndani.



Wabunge wa CUF walikuwapo lakini idadi yao ikiwa haifiki 20 wakati wa kipindi cha maswali na majibu na kubaki tisa pekee baada ya kipindi hicho.

Hatimaye Mtoto wa Gaddafi Afutiwa Mashtaka ya Mauaji

$
0
0
Mtoto wa Gaddafi afutiwa mashtaka ya mauaji
Leo April 4, 2018 stori inayoshika headlines za kimataifa ni kutoka Libya ambapo Mahakama ya Tripoli imefuta kesi ya mauaji iliyokua ikimkabili Saadi Gaddafi, mtoto wa tatu wa aliekua rais wa Libya, Muammar Gaddafi.

Saadi Kaddafi amefutiwa mashtaka yote dhidi yake katika kesi ya mwanamichezo Bachir al-Rayani ambaye alifariki dunia mwaka 2006 baada ya kupigwa kichwani. Bachir Rayani alifariki dunia baada ya malumbano katika nyumba inayomilikiwa na Saadi Gaddafi.

Mahakama hiyo imemuhukumu Saadi Gaddafi kifungo cha mwaka mmoja, kwa kosa la ulevi wakati wa kifo cha rafiki yake, Bachir al-Rayani, kilichotokea katika nyumba ya Saadi Gaddafi. Mahakama ya kaskazini ya Tripoli iliahirisha hukumu yake mara kadhaa, na hatimaye ilimsafisha katika kesi ya mwanamichezo huyo.

Mimba ya Zamaradi Yaleta Gumzo Mtandaoni

$
0
0
Mimba ya Zamaradi Yaleta Gumzo Mtandaoni
MIMBA ya mtangazaji maarufu wa TV, Zamaradi Mketema usiku wa Aprili Mosi ilizua gumzo katika ukumbini kutokana na kwamba, hapo awali hajawahi kubambwa akiwa na tumbo.

Zamaradi alionekana akiwa na ujauzito mkubwa ndani ya Ukumbi wa Mlimani City kulikokuwa na zoezi la utoaji Tuzo za Kimataifa za Sinema Zetu (SZIFF) hali iliyozua gumzo kwa watu waliohudhuria kwenye tukio hilo.

Gumzo lilizidi zaidi baada ya Zamaradi kuitwa jukwaani kwa ajili ya kukabidhi tuzo kwa mshindi katika kipengele cha Muongozaji Bora ambapo alimtangaza mshindi Daniel Manege aliyeshinda kupitia filamu ya Safari ya Gwalu.

“Si juzijuzi tu kaolewa mara hii tayari ana mimba? Ona gauni lake lilivyombana, tumbo lote linaonekana wakati alikuwa akifanya siri kwani hata kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii amekuwa akiweka picha za uso tu,” alisikika mmoja wa wahudhuriaji ukumbini hapo akijadiliana na mwenzake.

Zamaradi aliyewika na Kipindi cha Filamu cha Take One akiwa Clouds, aliolewa ndoa ya kimyakimya Septemba, mwaka jana ambapo kabla ya hapo alikuwa na watoto wawili aliozaa na Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.

Mzee Majuto: Wema Sepetu Awezi Kuwa Mkali Kushinda Rihama

$
0
0
Mzee Majuto: Wema Sepetu Awezi Kuwa Mkali Kushinda Rihama
Siku chache baada ya kufanyika kwa tuzo za Filamu zinazojulikana kama Sinema Zetu International Film Festival Award (SZIFF) na mrembo Wema Sepetu kuibuka mshindi kwa upande wa waigizaji wa kike, msanii mkongwe nchini Amri Athumani  ‘Mzee Majuto’ amesema mrembo huyo hawezi kuwa mkali kushinda Riyama Ally.

Katika kipengele hicho Wema alikuwa akichuana na wasanii nane na filamu walizoigiza kwenye mabano akiwemo Getrude Mwita (Bantu), Rachel Kayuga (Safari ya Gwalu), Aisha Mwajumla (Watatu), Riyama Ali (Mama wa Marehemu).

Wengine ni  Amina Rashid (Bandidu), Hawa Abeid (Genge), Sharifa Mansury (Kivuli cha ahadi) na  Neema Mangowi (Malaika) wakati Wema yeye aliingia kupitia filamu yake ya Heven Sent.


Akizungumza na MCL Digital leo Aprili 4, Mzee Majuto amesema kwake bado Riyama ni mkali na hawezi kufananishwa na Wema katika kuuvaa uhusika anapokuwa mbele ya kamera.

“Mimi nimekaa kwenye fani hii ya uigizaji siku nyingi, najua nani mwigizaji nani amevamia fani japo najua kuna watu wataniponda, lakini ukweli Riyama alistahili kubeba tuzo ile na sio Wema,” amesema msanii huyo anayewavunja watu mbavu kwa vichekesho.

Pia ametaja sababu ambazo ameona ndizo zilizomwezesha Wema kushinda kuwa zimetokana na mambo ya kidijitali, kwa yeye kuwa na mashabiki wengi mtandaoni ambao waliweza kumpigia kura tofauti na wasanii wengine alioshindanishwa nao.



Katika ushauri wake, Mzee Majuto amesema ni vizuri wakati mwingine majaji wasiangalie hilo la upigaji kura na badala yake waangalie vipaji vya watu kwani kwa kufanya hivyo itawavunja moyo wengine wanaotaka kufanya vizuri kwa kuona tayari wana washindi wao mfukoni.



Hata hivyo kwa upande wa msanii bora wa kiume, Mzee Majuto amesema Ahmed Salim ’Gabo’ amestahili kwa kuwa hakuna asiyejua kipaji cha msanii huyo tangu alivyoanza kung’ara kwenye filamu mbalimbali alizoigiza.



Katika tuzo hizo, vipengele 19 vilikuwa vikishindaniwa, ambapo kwa washindi bora wa kike na kiume kila mmoja aliondoka na tuzo na Sh5 milioni taslimu, wakati vipengele vingine walipata Sh1 milioni.

Tatua Matatizo yako Kwa Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu Pamoja na Mitishamba...

$
0
0

YULE MTAHALAM WA DUA NA DAWA ZA KIARABU NA ZA KIASILI YANI MITI SHAMBA SHARIFU LUKUMANI SASA YUPO HEWANI WENYE SHIDA ZITUATAZO CHEO KAZINI,KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI,MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME,ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA,KISUKARI,FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO

 ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE WASILIANA NAE KWA NAMBA
 0762899488
0656145170
WhatsApp namba +255620665635
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images