Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live

Diamond Afanya lililokuwa Halitegemewi...Ali Kiba Ndani ya Wasafi TV

$
0
0

Kuna watu walikuwa wanajiuliza Je Wasafi TV na Radio Watacheza nyimbo za Ali Kiba? Jibu limepatukana.... Anyway Diamond Platinum ni professional musician na mfanyabiashara anayejua anachofanya... Huyu hapa King kiba ndani ya Wasafi TV

Nikki Mbishi afunguka kuhusu Wasafi TV Baada ya Kucheza Nyimbo yake

$
0
0

Rapa Nikki Mbishi amekuwa msanii wa kwanza kuonesha hisia zake kuhusu channel mpya ya Wasafi TV iliyoanza kurusha matangazo yake Jumapili Aprili 01, 2018, kwa kuwapongeza viongozi wa kituo hicho cha runinga.

Nikki Mbishi amesema alichofurahishwa zaidi na kituo hicho ni kwamba kimeanza kwa kupiga nyimbo mchanganyiko na bila ubaguzi kitu ambacho kinapelekea ushindani wenye usawa ambao awali haukuwepo kwenye media nyingine.

“Asante Wasafi TV nyie mmecheza wimbo wangu #NIMEKUMISS bila hata mimi kuwaletea, najua ndio mnaanza ila msisahau kuendelea hivi hivi. Hakuna kitu kinachojenga na kuimarisha misingi ya sanaa kama ushindani wenye usawa “Fair Competition” hii inamaanisha anayestahili na apate na asiyestahili akose japo fitna zipo tu,“ameandika Nikki Mbishi kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuelezea zengwe zilizokuwa zinafanywa na vituo vingine.

“Tumeshuhudia umwinyi na ubeberu kwa kipindi kirefu sana,wapo ambao walitaka uMungu mtu lakini walijishtukia wakabwaga na wengine walibwagwa na hiyo ni kwa sababu ya kuleta umatabaka wa kanda fulani na kanda fulani na kujuanajuana sana kiasi kwamba akina sisi tusiofungamana nao tukaishia kutengwa na kuonekana “VINEGA” Kila la kheri kwenye hii ligi ya mbuzi kuna siku daraja litapanda tutacheza ya ng’ombe na mpaka tembo nini simba. Ipo siku watajihoji na kujijibu wenyewe.“ameeleza Nikki Mbishi.

Hata hivyo, pongezi na ushauri huo umepokelewa kwa mikono miwili na Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale. Ambapo amemjibu kwa kushukuru “Asante bwana UNJU hii ni yetu sote na tunaamini hata kwengine wataanza kupiga kwenye kuweka usawa. Mwanzo mgumu ila Mungu atatusimamia sababu tunania ya kweli na sio ushindani na mtu. Haya mtag msanii yeyote ambaye aujamuona akichezwa kokote ili huku kwao aanze kupigwa maana hii ni ya kwetu sote @wasafitv “.

Mwaka 2016, rapa Nikki Mbishi aliingia kwenye headline baada ya kutoa wimbo wake wa ‘Babu Talent’ ambao mashabiki wengi waliutafsiri kama dongo kwa Babu Tale, ambapo wimbo huo unamzungumzia mtu ambaye ananyonya wasanii wa muziki na kubania baadhi ya kazi zao kutoka.

VIDEO: Mambo ni Hivi Kifesi Anena Mazito Kilichomtoa WCB

$
0
0
VIDEO: Mambo ni Hivi Kifesi Anena Mazito Kilichomtoa WCB
Aliekuwa mpiga picha wa muimba muziki maarufu Tanzania na dunian, Kifesi ambae amekuwa akimpiga picha kwa takribani miaka mitano ameamua kuacha kazi WCB kutokana na kile alichokisema kuwa ameamua kufanya hivi kutokana na kukosa muda wa kufanya ibada kutokana na siku ambazo ibada inafanyika mara nyingi anakuwa safarini kwaajili ya kupicha picha za show za WCB.

Wabunge wa upinzani wasusia Bunge

$
0
0

Wabunge wa upinzani wakiwamo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ni kama wamesusia Mkutano wa 11 wa Bunge ulioanza vikao vyake mjini Dodoma jana huku viti vyao vikionekana vitupu.

Aidha, kutokana na kutokuwapo bungeni kwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), swali laki ilibidi liulizwe na Mbunge wa Liwale, Zuberi Kuchauka (CUF).

Wabunge hao wameshindwa kuhudhuria vikao hivyo ambapo jana wabunge waliokuwapo walikuwa wanne tu kutoka Chama cha Wananchi (CUF) na wabunge wawili wa Chadema.

Hata hivyo, leo wabunge wa Chadema hawakuwapo kabisa ambapo baadaye walionekana wabunge wawili tu, akiwamo Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea na Mbunge wa Viti Maalumu, Rose Kamili ambao walionekana kwa muda mfupi kwa nyakati tofauti na kupotea.

Kubenea aliingia bungeni asubuhi na kutoka kabla ya kikao kuanza huku Kamili akionekana nje ya ukumbi wa bunge bila kuingia ndani.

Wabunge wa CUF walikuwapo lakini idadi yao ikiwa haifiki 20 wakati wa kipindi cha maswali na majibu na kubaki tisa pekee baada ya kipindi hicho.

Watuhumiwa 11,000 wakamatwa na dawa za kulevya

$
0
0

ZAIDI ya watuhumiwa 11,000 wa dawa za kulevya wamekamatwa nchini tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, bunge lilielezwa jana mjini hapa.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde, aliyasema hayo jana bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mwantumu Dau Haji.

Mavunde alisema tangu kuanzishwa kwa mamlaka hiyo, watuhumiwa 11,071 wameshakamatwa na kwamba kati ya hao, 3,486 ni wafanyabiashara wa dawa za kulevya na tayari wamefikishwa mahakamani.

Katika swali lake, Mbunge huyo alitaka kujua mpango wa serikali wa kuhakikisha inarejesha kasi ya kupambana na Dawa za kulevya.

"Kazi ya kushughulikia wimbi la dawa za kulevya nchini imekuwa ya kusuasua na kutoridhisha. Je, serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inarejesha kasi ya kupambana na dawa hizo?" alihoji mbunge huyo.

Akijibu swali hilo, Mavunde alisema idadi hiyo  ni ya watuhumiwa waliokamatwa hadi Februari, mwaka huu, ikiwa ni takribani mwaka mmoja sasa tangu kuundwa kwa chombo hicho Februari, mwaka jana, baada ya bunge kutunga sheria mpya ya kudhibiti na kupambana na dawa hizo namba 5 ya mwaka 2015.

"Kutokana na kuongezeka kwa kasi ya kupambana na dawa za kulevya imesababisha kupungua kwa kiasi kikubwa kwa matumizi ya dawa hizo nchini,"alisema Mavunde.

Alisema mamlaka hiyo imepewa nguvu kisheria za kukamata, kupekua, kuzuia mali na kuchunguza mashauri yote ya dawa za kulevya na makosa mengine yanayohusiana nayo ikiwamo mali zitakazothibitika kupatikana kutokana na biashara ya dawa za kulevya.

Aidha, alisema Zanzibar imekuwa ikitumiwa kama uchochoro wa kupitisha dawa hizo na kwamba vimekuwapo na vikao vya kutengeneza mfumo wa udhibiti katika eneo hilo.

Mavunde alitoa wito kwa wabunge kushiriki kikamilifu juhudi za serikali za kupambana na dawa za kulevya kwa kuwa madhara yanayotokana na matumizi ya dawa hizo,  yanaathiri wote ikiwamo kuongezeka vitendo vya uhalifu na matumizi ya serikali katika kuwahudumia waathirika.


Serikali yawataka Wakurugenzi kutoa asilimia 10 ya mapato ya ndani

$
0
0

Serikali imewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote 185 zilizopo Tanzania bara kuhakikisha wanatoa asilimia 10 ya mapato ya ndani ili kuepukana na tabia ya kuwasababishia kuandikiwa deni kwenye taarifa ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali.

Naibu waziri wa Tamisemi Josephat Kakunda, ametoa kauli hiyo leo (Aprili 04, 2018) kwenye mkutano wa 11 unaoendelea kufanyika mkoani Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalum Susan Mgonukulima ambaye alitaka kujua asilimia 10 za mfuko wa halmashauri kwa vijana na wanawake una kiasi gani.

"Kumekuwa na changamoto za kiutekelezaji ambazo zimekuwa zikisababisha utekelezaji wa azimio hilo usifikie asilimia 100. Naziagiza Halmashauri zote 185 nchini kutoa asilimia 10 ya mapato halisi ya ndani kwa ajili ya mikopo kwa wanawake (asilimia 5) na vijana (asilimia 5)", amesema Kakunda.

Kwa upande mwingine, Naibu waziri wa Tamisemi Josephat Kakunda amesema endapo wakurugenzi hao hawatotenga kiasi hicho kilichotakiwa basi watachukuliwa hatua stahiki dhidi yao.

Miili ya Wanajeshi wa Uganda Yarejeshwa

$
0
0
Miili ya wanajeshi wa Uganda yarejeshwa
Miili ya wanajeshi nane wa Uganda waliouawa katika shambulio lilitekelezwa na kundi la Al shabaab imerejeshwa nyumbani na kukabidhiwa familia zao kwa maziko.

Kwa mjibu wa msemaji wa jeshi la UPDF idadi wanajeshi wa Uganda waliouawa imeongeza hadi nane, baada ya wajeruhiwa wanne kufariki.

Jeshi la Uganda linasema zaidi ya wapiganaji 30 wa Al shabaab waliuawa katika shambulio la Jumapili.

Mwandishi wa BBC, Isaac Mumena anaelezea kuwa bendi ya jeshi la UPDF walipokea miili ya wanajeshi wa Uganda katika uwanja wa kijeshi wa Entebbe.

Naibu wa Kamanda wa majeshi ya nchi kavu Meja Jenerali Sam Kavuma ndiye aliyepokea miili ya wanajeshi wanne waliofikishwa Jumanne kuwapongeza marehemu hao kwa kazi waliofanya.

Kamanda Kavuma alisema "hawakufa bure, wamefanya kazi nzuri. Wapewe pongezi,waliweza kuwazuia wanamgambo wa Al shaabab wasifanye mashambulizi yao na kuwaangamiza."

Miili ya wanajeshi wanne walioletwa ni wale waliofariki papo hapo kwenye mapambano na kati ya majeruhi sita, wanne walifariki wakiwa hospitali na kuhitimisha idadi ya wanajeshi nane.

Kikosi cha wanajeshi kutoka Uganda wakipiga doria kwenye mji wa Afgoye kusini mwa Mogadishu mwaka 2014Haki miliki ya pichaAFP
Image caption
Kikosi cha wanajeshi kutoka Uganda wakipiga doria kwenye mji wa Afgoye kusini mwa Mogadishu mwaka 2014
Naibu wa msemaji wa jeshi la UPDF Luteni Kanali Deo Akii siku ya Jumatatu alifahamisha BBC kwamba wanamugambo walishababu zaidi ya 30 waliuwa.

" Wanamgambo 30 wa Alshababu waliuwawa kwa upande wetu kwa mapingano hayo tumepoteza wanajeshi wanne na saba kujeruiwa." alisema

"Mapigano hayo yamekuwa katika eneo la 'sekta one' , ambayo 'sekta one' ni eneo la wanajeshi wa Uganda, ni eneo ambalo Al shabaab wanapenda kulichukuwa, ni sehemu muhimu kwa serikali ya Somalia."

Licha ya maafa hayo ya wanajeshi wa Uganda kutokea, jeshi la Uganda limeapa kuendelea na juhudi zake za kulinda amani nchini Somalia chini ya kikosi cha AMISOM.

Pamoja na hayo wameahidi kuwasaka wanamgambo wa Al shabaab nchini Somalia hadi watakapowamaliza na wananchi wa Somalia kuishi kwa amani.

Julai 2016, Umoja wa Afrika ulitangaza mipango ya kuwatoa kwa awamu wanajeshi nchini Somalia, kuanzia Oktoba 2018 na kumalizia mpango huo mwishoni mwa waka 2020.

Waithiopia Wtinga Nchini Kwaajili ya Mechi yao na Yanga

$
0
0
Waithiopia Wtinga Nchini Kwaajili ya Mechi yao na Yanga
Klabu ya soka ya Welayta Dicha ya Ethiopia imetua nchini mchana wa leo, tayari kwa mchezo wake wa hatua ya mtoano kombe la Shirikisho Barani Afrika kuwania kutinga hatua ya makundi.


Welayta imetua na kikosi chake kamili kilichoiondoa Zamalek ya Misri kwenye michuano hiyo hatua ya kwanza na wachezaji wakionekana kuwa na morali kubwa kuelekea mchezo huo.

Timu hiyo inashika nafasi ya 8 kwenye msimamo wa ligi ya nchini kwao ikiwa na alama 23 katika mechi 17. Mchezo unatarajia kupigwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam April 7.



Kwa upande wa Yanga yenyewe imeweka kambi mkoani Morogoro kwaajili ya mchezo huo na itarejea Dar es salaam kesho Alhamisi tayari kwa mchezo huo ambao kama itautumia vizuri itarahisisha kazi ugenini wiki mbili zijazo.

Sakata la Abdul Nondo Lafikia Hapa Sasa Ahojiwa Uraia Wake

$
0
0
Sakata la Abdul Nondo Lafikia Hapa Sasa Ahojiwa Uraia Wake
Mwanasheria TSNP, Mkurugenzi wa Idara ya Sheria TSNP, Paul Kisabo amesema kuwa ni takribani wiki sasa Mwenyekiti wao wa Mtandao wa Wanafunzi(TSNP), Abdul Nondo amekuwa akihitajika uhamiaji ili akahojiwe uraia wake na pamoja na wazazi wake.

Kisabo ameeleza kuwa jambo hilo la kuhojiwa uraia wake wamelitimiza leo baada ya kutoka Mahakama Kuu kwenye kesi yake iliyohairishwa mpaka tarehe 11, April mwaka huu.

Soma taarifa kamili hapa;

Hello

Habari ndugu zangu wana TSNP.

Kwa muda wa takribani wiki moja mpaka sasa mwenyekiti wa TSNP Abdul Nondo amekuwa akihitajika uhamiaji ili akahojiwe kuhusu taarifa za uraia wake pamoja na za ndugu zake.

Hakupata nafasi ya kwenda sababu hakuwa sawa kutokana na changamoto alizokumbana nazo.

Jana pia tulipata wito kutoka uhamiaji ili tuweze kumpeleka na akahojiwe.

Jambo hilo tumelitimiza leo tar 4.4.2018. Baada ya kutoka mahakama kuu kwenye kesi yake ambayo imeahirishwa mpaka tar 11.4.2018.

Mnamo sa sita mchana tuliweza kumfikisha Abdul Nondo makao makuu ya ofisi za uhamiaji mkoa (makao makuu ya wizara ya mambo ya ndani)

Tulipata kuhoji alichoitiwa na anachotakiwa kujaza katika fomu aliyopatiwa.

Jibu tuliambiwa wanataka kupata taarifa zake binafsi, za wazazi wake, babu na bibi zake pande zote mbili (upande wa baba na upande wa mama)
pamoja na za ndugu zake,kwani Afisa uhamiaji mkoa alitamka kuwa sheria inawaruhusu kumuhoji mtu yeyote wanaotilia mashaka uraia wake .nakuwa wanamashaka na uraia wa Abdul Nondo,hivyo awathibitishie kuwa yeye ni Raia wa Tanzania.
Amejaza taarifa zile anazozifaham tu.

Baada ya hapo afisa uhamiaji aliyekabidhiwa jukum la kumhoji Abdul Nondo alisema kwamba tar 20.4.2018 Abdul Nondo anapaswa kupeleka cheti chake cha kuzaliwa, cheti cha kuzaliwa cha baba yake, mama yake, cha bibi na babu mzaa baba na mzaa mama.

Asanteni.

© Paul Kisabo
Mwanasheria TSNP, Mkurugenzi wa Idara ya Sheria TSNP.

JK Ajitosa Kumpeleka India Mzee Mjuto kwa Matibabu

$
0
0
JK Ajitosa Kumpeleka India Mzee Mjuto kwa Matibabu
LICHA ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume bado hali ya staa wa filamu za Kibongo, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ ni tete ambapo Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’, amejitosa baada ya kumuona alivyodhoofu kwa sasa.

JK na Mzee Majuto walikutana uso kwa uso wikiendi iliyopita katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar ambako kulikuwa na shughuli ya utoaji tuzo za filamu zilizojulikana kwa jina la Tuzo za Kimataifa za Sinema Zetu ambapo walionekana wakiteta kwa dakika kadhaa kabla ya kila mmoja akaenda kukaa kwenye siti yake.

Mzee Majuto alionekana akiwa amedhoofu kwani aliingia ukumbini akitembea kwa msaada wa fimbo huku akionekana kutokuwa mchangamfu kama ilivyo kawaida yake, hali iliyowahuzunisha mashabiki wake waliokuwa ukumbini hapo.

Risasi Mchanganyiko lilizungumza na Mzee Majuto ili kujua hali yake na kile alichokuwa akiteta na JK ambapo alisema kuwa, kutokana na hali yake kutokuwa nzuri licha ya kufanyiwa upasuaji, rais huyo alimuahidi kwamba watajadili na watampeleka India kwa matibabu zaidi kwani tiba za hapa hajaridhishwa nazo.

 “JK ameniahidi kwamba watanipeleka India kwa ajili ya matibabu ikiwa ni baada ya kwenda na kujadili na rais aliyeko madarakani Dk John Pombe Magufuli ‘JPM’ ili nikapate matibabu zaidi maana tiba nilizopatiwa hapa bado sijakaa sawa.

“Kwanza kwa sasa nimepatwa ugonjwa mpya tena ambapo mkono unaniuma mno, ninashindwa hata kushika chochote ndiyo nataka nirudi tena hospitalini nikawaeleze kuhusu hilo maana hali siyo nzuri kabisa,” alisema Mzee Majuto.

Hata hivyo, Mzee Majuto alisema kuwa, pamoja na hilo, JK alimuahidi kwamba atamnunulia trekta kwa ajili ya kulima kwenye mashamba yake ambako atapanda minazi huko Tanga ili aweze kuendesha maisha.

Ebitoke Afunguka Ishu ya Kumsaliti Ben Pol na Kutembea na Shemeji Yake

$
0
0
Ebitoke Afunguka Ishu ya Kumsaliti Ben Pol na Kutembea na Shemeji Yake
Mchekeshaji kutoka kundi la Timamu, Ebitoke amejibu tetesi za kutoka kimapenzi na Wyse ambaye ni msanii anayesimamiwa na Ben Pol.

Utakumbuku kuwa Ebitoke na Ben Pol kwa kipindi kirefu sasa wamekuwa wakieleza kuwa wao ni wapenzi hivyo, Wyse ni shemeji yake na Ebitoke.

Mchekeshaji huyo amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote kwani mapenzi yake na Ben Pol bado ni ya moto kabisa na picha zilizotoka wakiwa wana-kiss ni katika kutengeneza video ya Wyse.

“Director alituambia tu-kiss ili kuvaa uhalisia ila kati yangu na Wyse ni urafiki hakuna mapenzi,” Ebitoke ameiambia Bongo5.

Muimbaji Wyse anasimamiwa na Ben Pol na kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Siamini’, pia alishirikishwa na Ben Pol katika wimbo wake uitwao Bado Kidogo.

Diamond Kutoka Kulalamika Radioni Hadi Sikioni Kwa Rais

$
0
0

Wiki mbili zilizopita jina la Diamond Platnumz lilipamba vichwa vya habari. Hiyo iliyokana na mahojiano aliyofanya na kituo cha redio cha Times Machi 19 mwaka huu, akimlalamikia Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza kufungia nyimbo za wasanii bila kuzingatia hasara na usumbufu wanaopata.

Lakini Juzi ameonekana Akiteta jambo na Mh Rais... huwenda Kuna mambo makubwa yanakuja kufanyika katika tasnia Ya Bongoflava na sanaa Kwa Ujumla.

Madhara ya Kufanya Mapenzi Kupita Kiasi

$
0
0

Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono.

Kuna watu ambao hawezi kulala bila kufanya mapenzi na huku wengine wakikosa uwezo wa kuvumilia hata kwa siku mbili au tatu.

Mtu anaweza kuwa na mke na kujikuta kila siku anatumia ‘chakula cha usiku’ kwa sababu tu hakuna wa kumkataza na kwamba ana haki ya kufanya hivyo kwa sababu amelipa mahari, hapa nimeweka chumvi kidogo lakini huo ndio ukweli halisi.

Hilo linaweza kuwa jambo jema kwa upande mwingine, lakini uchunguzi unaonyesha kuwa watu wengi kati ya watu wanaolalamika kupoteza hisia za kimapenzi hutoka katika kundi la watu wapenda ngono.

Pamoja na tatizo hilo, yapo madhara mengine mengi ambayo mtu asiyekuwa na kiasi katika tendo la ndoa anaweza kukabiliana nayo, hivyo ni vema tukajifunza ili tusiwe watu wa kuendekeza miili kiasi cha kulazimika kufanya mapenzi kila tunapokutana.

Twende pamoja katika kutazama madhara hayo kwa kina.

1.    Kupoteza hamu ya tendo la ndoa.

Watu wenye pupa za kufanya mapenzi hupoteza haraka hisia za kimapenzi kwa wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia zinazoweza kujitokeza wakati wa ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa mara.

Sababu hizo zinaweza kuwa ni pamoja na zile za kumzoea mwenza kiasi cha kukosa msisimko hata anapomuona akiwa mtupu.

Aidha kukinai haraka staili za kimapenzi kunatajwa kujitokeza kutokana na kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza kumfanya mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake na hivyo kupoteza hamu naye na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa kikamilifu.

2.   Kuujaza mwili tamaa kubwa.

Tabia ya kufanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini na kuufanya mwili uwe na msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa tendo la ndoa bila kukosa na hivyo kumfanya mhusika asiwe mtu mwenye uwezo wa kuzuia tamaa na kukosa chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi na kwa wakati gani?

Watu wanaojiendekeza katika kufanya mapenzi mara kwa mara ndiyo wale ambao kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake.

Hawa ndiyo wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa watumishi wa ndani au kufanya mapenzi na watoto wao wa kuwazaa kwa vile akili zao huwa zimeathirika kwa tamaa ya mapenzi.

Unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi mara kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo akiondoka siku mbili unatamani kuwa hata na houseboy ili akukate kiu ya penzi.

3.   Kupoteza raha kamili ya tendo.

Raha ya tendo hutegemea sana hisia iliyokuzwa kutokana na mapenzi sahihi na kiu ya kufanya mapenzi, hivyo basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila mara unaweza kupoteza msisimko wa tendo na kujikuta unapata furaha ambayo haikutoshi kumaliza tamaa yako.

Kama ni mapenzi utakuwa unayafanya kwa mazoea tu na msisimko wako utakuwa mdogo!

4.   Kupoteza nguvu ya mwili.

Madhara mengine yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni pamoja na kupoteza nguvu nyingi za mwili.

 Kama tujuavyo tendo la ndoa hasa kwa wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili uchoke. Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa nguvu za kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha.

Sambamba na hilo mbegu za uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa dhaifu.

5.   Kupatwa na magonjwa.

Kama tulivyojifunza kuwa watu wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa na tamaa na hujikuta wanafanya mapenzi holela ambayo huweza kuwasababishia magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi, lakini ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na msukumo wa kutosha hasa kwa wanawake huwafanya waishiwe msisimko na kuzifanya sehemu zao za siri kutotoa ute unaoweza kuwakinga na michubuko wakati wa kujamiiana na hivyo kuwasababishia michubuko itakayoweza kuleta maambukizi ya haraka ya magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi.


Jinsi ya kunogesha mahusiano mapya ya kimapenzi

$
0
0

Ili kunogesha mahusino ya kimapenzi lipo japi kubwa sana ambalo unatakiwa kulifahamu na jambo hilo si jingine bali ni kuhakikisha unakuwa ni mtu mwenye kuomba msamaha hasa pale unapokesea.

Wanaume wengi wanaamini kwamba hata wakikosea, hawatakiwi kuomba msamaha kwa sababu kuomba msama­ha ni ishara ya udhaifu, matokeo yake wanaendekeza mfumo dume bila kujua kwamba mapenzi ni demokrasia!. Ambapo kila pande ni lazima mmoja wapo ajue kanuni na misingi ya kujishusha hapa pale anapokosea.

Bila kujali kwamba wewe ni mwa­naume au mwanamke, mkubwa au mdogo, una fedha au huna, inapotokea umeziumiza hisia za mwenzi wako, iwe kwa jambo dogo au kubwa, ni lazima uombe msamaha na kuahidi kutorudia makosa.

Ukishajenga utaratibu huu, hata kama mwenzi wako hakuwa na kawaida ya kuomba msamaha, taratibu utambadilisha. Utashangaa na yeye anaomba msamaha na huo unakuwa mfumo wa maisha yenu. Kuwa makini kwamba ukiomba msamaha leo, siyo kesho unarudia tena kosa lilelile, ataona unamfanyia makusudi.

Ukizingatia jambo hilo ukazidisha mapenzi na kumjali mwen­zi wako, ukawa mwaminifu na mkweli, hisia tamu za mapenzi unazozihisi leo, ni lazima utafutrahia mahusiano yenu.

Maswali Unayotakiwa Kujiuliza ili Kubaini Kama Mpenzi Uliyenaye ni sahihi

$
0
0

Inabidi kwanza wewe uwe ni mtu ulie sahihi  ndio utakapopata mtu sahihi , huwezi kupata mtu sahihi ikiwa wewe sio sahihi, au unaweza kupata mtu sahihi lakini wewe ukawa sio sahihi. ina maana kwamba lazima kwanza wewe uwe ni mwenye kujipenda ndipo utapenda na wengine

Pia ujifunze  kuwa mtu mkamilifu ili uje kupata mtu alie mkamilifu. kwa hio inabidi uwe na maswali mengi kabla hujaanza kuchukua maamuzi ya kutafuta mtu sahihi.Jiulize  , umekamilika au ni tamaa tu inakupeleka kutafuta mtu wa kukukampani.?

kama nia yako ni kupata mapenzi  tu , basi hapo bado  hujakamilika, lazima uwe na kazi kubwa ya kufanya ndani ya moyo wako kabla unahitaji kupata kazi ya kujifunza  kujipenda , na kujifunza majukumu ya kupenda wengine, uwe na hisia za kujisikia mkamilifu na usalama  za namba moja, yaani kupata na kutoa.

jiulize maswali yafuatayo.
1. Je ni mtu anyethubutu kujali, na ni mtu mwenye huruma na uelewa na mtu wa kukubalika na anakubali jinsi ulivyo. kukosekana kwa  uelewa  ni dalili ya moja kwa moja kuwa   sio sahihi

2. Je anajitahidi kulazimisha ili awe sahihi?
unaweza kuwa ,mnafanya vitu kwa pamoja , lakini bado unaona kama kuna upungufu fulani kwako huyomsio mtu sahihi kwako, hata ukijitahidi vipi huwezi kufika mbali nae.

3. Je mtu ulie nae ni muwazi kiasi cha wewe kujifunza kitu kwake?
mtu muwazi ni rahisi kjifunza  kujua kama anajipenda na kuwapenda wengine, lakini mtu wa kificho ni vigumu kujua , na hutaweza kujifunza kitu kwake. uwazi ni chombo  cha msingi sana katika mahusiano yeyote. hata kama kuna migogoro ni rahisi kurekebisha baina yenu . lakini watu wenye kificho ni ngumu hata kama kuna migogoro wanakuwa na hasira , hufoka , huhamaki, wanakuwa na hisia kali za kimwili zaidi. kwa hio sio sahihi.

4. Mnashirikiana katika kipato chenu?
mnakubaliana katika matumizi?, uzazi, kula  manunuzi ya vitu, mazoezi,usafi na kuwajibika kwa pamoja  na mnaelewana?.

5. Unapata zile hisia  za msingi , zile cheche  zinazokuvuta  kwake? unapenda kuwa karibu nae? unapenda jinsi alivyo?
Inawezekana ana harufu fulani hupendi,  kama huna hizi hisia ndani ya miezi 6 ya kuwa na huyo mtu basi hakufai, uelewe huyo ni rafiki tu wa kupita hawezi kuwa mwenza wa maisha .


Kauli Sumu Kwenye Mapenzi

$
0
0


Uhali gani mpenzi msomaji wa Muungwana blog, bila shaka u mzima na unanendelea vyema na majukumu yako ya kila siku.  Nakukaribishe siku ya Leo mpenzi msomaji wa safu hii, nimekuja na mada mpya ambayo imenisukuma kuwaandikia wanandoa na wapenzi walioko kwenye uhusiano kwa muda mrefu kwani wengi hujikuta wameachana.

Kauli anazozitoa mwanaume wako ni wazi kabisa kuwa amekuchoka wengi miongoni mwa kauli hizo ni kama ifuatavyo;

1. Tukiachana sisi si wa kwanza.
Kauli kama hii mwanaume hawezi kukuambia mkiwa kwenye mapenzi kwa mara ya kwanza, hivyo ni lazima kwa kukutamkia hivyo ujue moja kwa moja umechokwa.

Hivi ni nani ambaye hajui kuwa mapenzi ni malumbano ya mara kwa mara hata kwa vitu vidogo? Kama hampendani hamuwezi kutofautiana kwani mtakutana wapi au mtakutanishwa na nani hasa?

2.  Harafu we mwanamke una mdomo sana
Ukiona mpenzi wako anakerwa na mdomo wako mara kwa mara na anakutamkia jua wazi mapenzi hakuna. Wanaume wengi hawapendi mwanamke anayeongea hasa kama anamkosoa kwa jambo fulani.

Mfano kama kuna vitu ulikuwa ukimwambia mwanzo anakubali na kuendana na wewe lakini akishakuchoka ukiongea tu anakuona kero, hii pia ni dalili ya kuachwa.

Ulipoingia kwenye penzi kwa mara ya kwanza hata alipokuwa akikukwaza uliomba yaishe mapema na wala hukuwahi kufikiria kukwambia kuwa tukiachana sisi si wa kwanza, ulitumia nafasi yako kikamilifu kwa kumbembeleza na akakuelewa mkamaliza mzozo.

3. Ipo siku utajutia hili penzi
Maana yake nini? Mpaka mnafikia hatua anakwambia hivyo ni wazi anashindwa kujitoa lakini pia anao uwezo wa kujitoa hivyo anakuandaa kisaikolojia.

Kwa mtu unayempenda kwa dhati huwezi kumwambia ipo siku atajutia penzi ni neno lisilostahili kwa mpenzi wako, ukiona unaambiwa hivyo jua siku zako zinahesabika.

4. Kwani nilikukuta mtoto, tumejuana ukubwani
Wanaume wengi wanapenda kutumia kauli hii pale wanapowachoka wapenzi wao hasa wanapokuwa kwenye malumbano,  bila shaka msomaji utakuwa na ushahidi wa hili hasa kwa wale waliowahi kukutana na maneno haya wataniunga mkono.

Ni maneno yanayouma na kujirudia kwenye ubongo wa mwanamke pia hupunguza mapenzi kwani mwanamke akitamkiwa hivyo mara kwa mara hujikuta ubongo unaanza kukubali na kupunguza mapenzi kwa yule aliyekuwa akimpenda.

Tabia Ya Kuzoeana inavyoweza kuathiri Maisha yako ya kimahusiano

$
0
0

kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususani kwa upande wa mwanamke kwa kutojali usafi wake, mavazi anayovaa, chakula anchopika, nidhamu ya nyumba na mpangilio kwa ujumla.

Matatizo mengi ndani ya nyumba yanaweza kusababishwa na moja au baadhi ya tabia hizo, ambazo huenda ikawa hazitokani na dharau, bali kuzoeana, kwa mfano, siku za mwanzo wa ndoa mwanamke huwa anajali sana usafi wa mwili wake, umaridadi wa nguo anazovaa, usafi wa nyumba na nidhamu ya hali ya juu, upishi wa chakula unaozingatia vionjo na ubunifu, mapokezi yenye bashasha na wakati mwingine hata kumkumbatia mumewe arudipo kutoka kazini.

Lakini baada ya kuzoeana yote hayo hubadilika, mwanamke huhisi kuwa hana jipya la kumuonyesha mumewe, hujiona wameishakuwa watu wazima sasa, na mara nyingi utakuta mwanamke huyu anashinda na sare (uniform) moja kuanzia asubuhi hadi anapopanda kitandani usiku, mambo ya Hinna, nguo za fashion, salon, manukato, kujipamba na dhahabu huyafanya pale anapotoka kwenda harusini na sio nyumbani. Huku ndio kuzoena, na tafsiri sahihi ni kudharau.

Hivyo ili kulinda kibarua cha chako cha mahusiano ni vyema ukajifunza kila wakati kutofanya vitu ambavyo vimekuwa havijayajengi mahusiano yako.

Asante kwa kuwa msomaji wa muungwana blog.

Zijue sifa za mpenzi asiyekupenda kwa dhati

$
0
0

Watu wengi hawapendi kutambua kwamba mtu anayempenda yeye hampendi, kwasababu ni maumivu makubwa sana moyoni. Unapokuwa kwenye mahusiano na mtu huyo nae inamuwia vigumu kukwambia "sikupendi" hufanya hivi katika kuzihurumia hisia zako juu yake.

Hivyo ukiona dalili hizi zifuatazo lazima ujue kwamba uliyenaye hakupendi.

1. Anapokuwa nawe inamuwia vigumu sana kukwambia neno NAKUPENDA mara kwa mara, utajikuta wewe ndio unakuwa mtumwa kwake kwa kumwambia nakupenda kila mara.
Majibu yake baada ya neno hilo, mara nyingi atakwambia asante kwa kunipenda basi, na akikuhurumia sana atakwambia nakupenda pia ili kukuridhisha wewe na moyo wako.

2. Utajikuta una mawazo sana juu yake na kujiuliza "hivi kweli mtu huyu ananipenda?"
Utajaribu kumuuliza, "je unanipenda?"
Jibu lake kwanza litafikiriwa sana, sababu ya kufanya hivyo ni kwa vile anatambua kwamba hakupendi sasa kukwambia ukweli wa swali lako anahisi utaumia, kwahiyo baada ya swali hilo anaweza kukuuliza swali na wewe "kwani unaonaje?" kwavile unampenda sana utamjibu, "naona kuwa unanipenda" naye atakwambia "basi ndio hivyo".

Mara nyingine baada ya wewe kumuuliza swali kuwa je anakupenda kweli, atakujibu "ukweli unaujua ila kwanini unapenda kuniuliza swali hilo kila mara?" kama umeshaingiza dosari juu ya upendo wake utajikuta unamuuliza "ukweli upi?" naye atakujibu "kuwa nakupenda", hapo utajikuta umepata furaha kugundua kuwa anakupenda kumbe mwenzio amekuhurumia tu.

3. Huwa hajali mambo yako unayomwambia, ukimueleza muda huu badae anajifanya kusahau ili tu akupotezee mueleleo.

4. Unapopanga kukutana nae huwa ni mtu asiyeishiwa na sababu za kushindwa kufika, huwa na aibu ya kukutambulisha kwa watu.
Unaweza kufika nae mahali akakwambia kuwa "kuna watu wanafahamiana na mama/baba mahali hapa kwahiyo tusiongozane karibu", hapo anaweza yeye akatangulia mbele au kukuacha wewe utangulie.

5. Hufanya tabasamu la kuigiza au kicheko cha kejeli ili wewe uridhike kwamba anafurahishwa na uwepo wako kwake.

6.Wakati mwingine inampasa mtu kujitambua na kumpa uhuru huyo umpendaye aweze kuamua mwenyewe labda kuendelea na wewe au kumfata anayempenda yeye.
Cha muhimu ni kuwa using'ang'anie mahusiano ambayo yanayoumiza moyo kwani yanaweza pasua moyo wako kwa mawazo.

Mambo Ambayo Msichana Ambaye Yupo Single Anatakiwa Kuyafahamu

$
0
0

Siku ya leo naomba nizungumze na wale wadada wote ambao hawajoelewa au kwa kibantu huitwa (single ladies).  Ewe mwanadada yapo mambo ya msingi ambayo unapaswa kuyafahamu kabla ya kuolewa na mambo hayo ni;

1.    Usiharakishe kutoka nyumbani kwa wazazi wako kwa gia ya kwenda kuolewa.
2.    Usimsubiri mwanaume mpaka aje ndio uanze kuishi. Unaweza kuishi maisha timilifu hata ukiwa huna mwanaume.
3.    Achana na pombe zimewauwa wenzako wengi kwa kisingizio cha kuondoa stress na wewe unaweza kufa pia.
4.    Usiwe mtu wa kuendekeza kuzipokea na kuzijibu namba ngeni za simu hasa nyakati za usiku.. sio njia sahihi ya kupatia mpenzi.
5.    Tengeneza mazingira ya kuilinda afya. Jitahidi Kunywa maji mengi na Chakula kwa diet achana na viofa ofa vya bure, vimesha waponza wenzio wengi mpaka sasa.
6.    Vaa vizuri na kiheshima. Watu watavutiwa na wewe ulivyo kabla ya kuongea nawe

Epuka kufanya Mambo hayo kwa Mpenzi Wako

$
0
0

Unapokuwa na mpenzi wako katika mahusiano, epuka sana kufanya vitu vya aina hii ambavyo vitasababisha mahusiano yenu kufa.

1. Kuanza kuchelewa kutoka kazini mara kwa mara.
Sio kwamba kila mtu anapochelewa kutoka kazini basi anakuwa sio mwaminifu, lakini zaidi ya asilimia 75 (kutoka kwenye tafiti) ya ambao wamekuwa na mahusiano nje wamekuwa wakitoa visingizio vinavyohusiana na kazi, vikao, mikutano na safari za kikazi, yamkini wewe ni shahidi wa hili.

2. Mazingira tatanishi ya simu :
Gafla simu zinaanza kumiminika mpaka mida ya usiku. Yamkini pia alikuwa yuko huru hata simu yake inapolia waweza ichukua na kumpatia lakini gafla anakuwa na hofu kubwa na kuificha simu yake, nimeongea na wengine ambao wanakwenda na simu hadi bafuni isije ikasikika.

Wengine wanaondoa milio katika simu zao wakati haikuwa kawaida yao, kuwe siri (password) ngumu hadi mwenyewe anashindwa kuikumbuka, wako ambao simu zao zikipigwa hawawezi kupokea na kuongea kwa uhuru kama kawaida, ataondoka na kujitenga pembeni akijifanya anaongea kiuaminifu kabisa.

3. Harufu ambazo hujazizoea
Kwa kuwa wapendanao huwa wamezoeana, maranyingi hata aina ya manukato mmoja anayotumia yanakuwa yanajulikana kwa mwenzake, Sasa hembu fikiri unamkuta mpenzi wako ametokea na ana harufu ya tofauti kabisa na uliyoizoea, umeisikia harufu hiyo akiwa amerudi toka kazini wakati asubuhi alipoondoka alikuwa na harufu ile uliyoizoea.

4.Tabia za kuanza kukufuatiliasana au hata kukuganda.
Wapo wanaotawapeleka wapenzi wao kila wanakotaka, nakutoruhusu mazingira ya wapenzi hawa wakike kuwa huru kufanya mambo yao wenyewe, wengine waliitafsiri hali hii kama penzi kubwa lakini baada ya muda unagundua kuwa ile ilikuwa ni ujanja wa kuficha uhalisi wake na kuzuia mazingira kwa mpenzi wake kugundua au kupewa taarifa ya tabia zake.

5. Kuzungumza sentensi za kutatanisha:
Unaweza kukuta katika mapenzi yenu mpenzi wako anaanza kuwa na sentensi ngumu na zisizo kuwa na msingi kwa mfano anasema “kwa jinsi hii sidhani kama tutafika” “mi siamini kama mapenzi yanadumu” “yani ndio maana watu wanashindwa kukaa na mpenzi mmoja” na maranyingine anaweza kukuuliza baadhi ya maswali moja kwa moja ili kukuona utajibuje. Sentensi hizi zina chanzo moyoni, kuwa macho.

6. Tabia za kuficha fedha:
Hii utaiona ghafla mpenzi wakeo anaanza kuwa na siri kuhusu fedha zake au matumizi yake, na wala hapendi kuulizwa ulizwa kuhusu suala hilo. Tabia hii ikidhihirika katika mapenzi yenu usichelewe kuchunguza maana kwa kukaa kimya unaweza kujikuta umechelea mwana na maji ya moto.


Viewing all 104694 articles
Browse latest View live




Latest Images