Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Waziri wa Mkuu Mizengo Pinda Avunja Ukimya na Kutangaza Kugombea Uraisi 2015

$
0
0
Waziri wa Mkuu Mizengo Pinda, amevunja ukimya na kuamua kutangaza nia yake ya kutaka kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.

Pinda alitangaza nia hiyo juzi usiku Ikulu ndogo ya Mwanza jijini Mwanza, mara baada ya kuwaalika wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) toka mikoa sita ya Kanda ya Ziwa.

Habari kutoka vyanzo vyetu vya kuaminika zilieleza kuwa Waziri mkuu aliwaalika wajumbe tisa kutoka katika wilaya zote za mikoa ya Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Geita na Kagera.

Pinda aliyekuwapo jijini Mwanza kwa ajili ya kuendesha harambee ya Mfuko wa Taasisi ya Benjamin Mkapa iliyofanyika jana usiku, alikutana kwa ‘mafungu’ na wajumbe zaidi ya 50 kutoka Mara, baadhi toka Mwanza, Geita na Kagera.

“Wajumbe wengine wa Shinyanga, Simiyu na wale Mwanza na Geita alikutana nao jana (juzi) jioni ili kuwashawishi wamuunge mkono  baada ya jina lake kupitishwa na NEC,” kilisema chanzo chetu.

Chanzo hicho kilisema wajumbe toka wilaya hizo za Kanda ya Ziwa, walianza kuwasili Ijumaa mchana jijini Mwanza kwa lengo la kuitikia wito wa Waziri Mkuu kabla ya hawajatangaziwa nia yake.

SABABU ZA KUTANGAZA NIA
Waziri Pinda aliwaeleza wajumbe hao sababu kubwa zilizomfanya aguswe kutangaza kuwania nafasi ya Rais 2015, ni kutokana na ushawishi mkubwa toka kwa maaskofu, masheikh, baadhi ya wabunge, watu maarufu pamoja na mke wake.

Sikuwa na nia hiyo kwa vipindi vyote vitatu vya ubunge wangu, lakini watu hao akiwamo mke wangu, nimeshawishika kutaka nafasi hiyo,” alisema Pinda.

Alisema ameona hana sababu ya ‘kuzembea’ kutangaza nia ya kumrithi Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu ujao.

SIFA
“Ninazo sifa za kunitosheleza kuwania nafasi hii, ikiwamo kutokuwa fisadi, pia nimekuwa ndani ya viongozi wa nchi wa awamu zote nne tangu 1974 enzi za Nyerere (Julius), Ali Hassan Mwinyi, Mkapa (Benjamin) na sasa Kikwete,” alidai.

Aidha, alisema kutokana sifa hizo hataweza kuchangishiwa pesa za kuingia madarakani kama wengine (hakuwataja), bali atawapa kiasi alichonacho ili kuwawezesha kumsaidia.

Pinda maarufu kama “mtoto wa mkulima”, alidai anaamini viongozi wakuu waliopita madarakani na kuongoza nchi, wanamuunga mkono.

VIKAO VYA CHAMA
Kutokana na nafasi yake ya ujumbe wa kamati ya Maadili, Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ana uhakika jina lake halitaweza kukatwa na litafikishwa katika mkutano mkuu wa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama.

“Kama wajumbe wa mkutano mkuu, mjiandae ‘kunibeba’ kwani kati ya majina matano yatakayotajwa na kamati kuu, nitakuwamo na pia na kati ya matatu pia nimo…nguvu zenu ni katika mkutano mkuu.”

Ilielezwa kati ya majina matano ambayo yatapelekwa Kamati Kuu, moja ni la Pinda, mwanamke, kijana, mgombea toka Visiwani na waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa.

Hata hivyo, hofu ya Pinda ilielezwa ni baadhi ya wajumbe walioalikwa kuwa miongoni mwa wapiga debe wa baadhi ya walionyesha nia ya kugombea nafasi hiyo akiwamo Lowassa.

Aidha, habari toka ndani ya kikao hicho zilidai, wajumbe walioalikwa kuhudhuria mkutano huo waligoma kupokea mgawo wa Sh. 50,000 zilizotolewa baada ya kumalizika kwa kikao.

NAPE
Uamuzi huo wa Waziri Mkuu kutangaza nia unaenda kinyume na chama chake ambacho hivi karibuni kiliwafunga ‘midomo’ wanachama wake kutangaza nia hiyo kabla ya muda akiwamo Lowassa, Bernad Membe na Frederick Sumaye.

Juhudi za NIPASHE kumpata Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye, kuzungumzia ‘nia’ hiyo ya Pinda, zilishindikana kutokana na simu yake ya mkononi kutopatikana.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Isingizi ni Popote Ila Huyu Nae Kazidi au Kachoka na Maisha?

$
0
0
Isingizi ni Popote Ila Huyu Nae Kazidi au Kachoka na Maisha?

Denti Amuua Mwanaye kwa Kumnyonga na Kisha Kumficha Uvunguni

$
0
0

Mwanafunzi wa Chuo cha Uuguzi Chimala wilayani Mbarali, Mkoa wa Mbeya,  Vena Mtati (27) (pichani) anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa kwa madai mazito ya kumuua mtoto wake kwa kumnyonga, kumtumbukiza kwenye mfuko wa rambo na kuutia ndani ya mfuko wa salfeti kisha kuuficha chini ya kitanda.

Tukio hilo la kikatili ambalo limewashangaza wengi, hasa ikizingatiwa kuwa mtuhumiwa huyo anajua sheria kwa sababu anajifunza uuguzi, lilijiri Agosti 21, mwaka huu ndani ya nyumba moja iliyopo Kijiweni, Kata ya Mvinjeni mjini hapa.

Kwa mujibu wa shuhuda ambaye anaishi jirani na nyumba inayodaiwa kufanyika mauaji hayo (jina lipo), wiki mbili zilizopita, mtuhumiwa huyo alifika kwenye nyumba hiyo akitokea chuoni akiwa na ujauzito.

“Wiki mbili zilizopita, Vena alifikia kwa rafiki yake anayeitwa Joyce ambaye alikuwa amepangisha katika hiyo nyumba. Vena alikuwa na mimba kubwa, baada ya siku tano tu akajifungua,” kilisema chanzo hicho.

Kikaongeza: “Siku ya tukio, Joyce yeye ambaye ni mwenyeji alitoka kwenda katika shughuli zake, akamuacha Vena akiwa chumbani. Nadhani ndipo aliposhikwa na uchungu, akajifugua mtoto wa kike.

“Ilikuwa asubuhi, sisi tukasikia kelele kutoka kwenye chumba hicho. Zile kelele zilikuwa si za kawaida! Ilikuwa kama vile kuna mtu anakabwa.

“Tuliposikiliza kwa makini, mara sauti ya redio ikaongezwa ili kufanya kelele hizo zisisikike kwa nje. Lakini kwa vile sisi majirani  tulijua kwamba ndani ya chumba kile kuna mjamzito na kelele alizopiga mtoto si za kawaida ndipo tulipomtafuta mwandishi wa habari (hizi),” kilisema chanzo hicho.

Mwandishi wetu alipopatikana na kunyetishiwa kuhusu kuwepo kwa uwezekano wa mama ambaye ni nesi kumuua mtoto wake aliyejifungua, aliwasiliana na Polisi wa Dawati la Jinsia.

Polisi hao, awali walimtafuta mwenyeji wa mtuhumiwa huyo, yaani Joyce ambaye alikuwa kwenye  mihangaiko yake.
Alipopatikana alipokonywa simu yake ya mkononi ili asiweze kuwasiliana na mtuhumiwa.


Aliulizwa kama ana mgeni nyumbani kwake, akakiri. Akaulizwa kama mgeni huyo amejifungua, akakataa ndipo wakamchukua kwenda naye nyumbani kwake kumfuata mtuhumiwa huyo.

Mwandishi wetu akiwa ameongozana na askari hao walifika kwenye chumba hicho na kumkuta Vena akiwa amesimama mlangoni.

Alipoulizwa kama amejifungua, awali alikataa katakata lakini baada ya  kubanwa na kutishiwa kuswekwa ndani, alikiri kujifungua na kusema kwamba mtoto huyo amemficha uvunguni mwa kitanda.

Ndani ya chumba hicho, sakafuni kulikuwa na damu  zilizodaiwa kumtoka mtuhumiwa huyo wakati akijifungua mwenyewe!

Polisi walizama chumbani, wakainama kuchungulia chini ya kitanda. Walichoanza kukiona ni mfuko wa salfeti, wakauvuta  kuutoa. Walipofungua ndani, wakakuta mfuko wa rambo, wakaingiza mkono na kutoa kifurushi kikiwa kimeviringishwa nguo nyingi na ndiye mtoto huyo alimohifadhiwa.

Mbali na mwili wa mtoto huyo kuviringishwa nguo hizo, pia ulimwagiwa chumvi na vumbi la mkaa ambapo ilidaiwa mtuhumiwa alifanya hivyo ili mwili huo usitoe harufu utakapotupwa porini.

Majirani walisema maarifa hayo, mtuhumiwa aliyapata kwa sababu tayari anajua namna ya kuhifadhi mwili wa mwanadamu, kwa mwanamke asiye na ujuzi asingeweza kufanya hivyo.

Kuna madai kwamba, mtuhumiwa huyo aliwaambia polisi kuwa alifikia uamuzi wa kumuua mtoto huyo kufuatia mwanaume aliyempa ujauzito aishiye jijini Dar es Salaam kumuahidi ndoa lakini akaingia mitini.

Baada ya polisi kusikiliza maelezo ya mtuhumiwa huyo, walimkamata yeye, mwenyeji wake Joyce na mmiliki wa nyumba hiyo ambaye jina halikupatikana mara moja.

Polisi walisema mmiliki wa nyumba hiyo alikamatwa kwa sababu alikiuka sheria za mji ambapo alitakiwa kutoa taarifa za kumpokea mgeni huyo kwenye serikali za mitaa lakini hakufanya hivyo huku Joyce akidaiwa kutambua kuwa mgeni wake alijifungua lakini akawaambia hakujifungua.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Nimerekodiwa Video ya Ngono Bila Kujijua. Nifanyeje?

$
0
0
Wadau natumaini mu wazima Mi ni mjasiriamali toka Arusha but huwa nakuja Dar kwa ajili ya kuchukua bidhaa, nikiwa Dar napenda kujibururdisha aama MEEDA au KONA BAA/AMBIANCE AFRIKA SANA huwa nikipata demu wa kupiga nampelekaga Guest/hotel niliyofikia tunafurahia "game" asubuhi namlipa chake anatambaa.

    Sasa katika kuingia guest kadhaa za hapa Dar nimegundua hawa jamaa wa guest wanaweka SECURITY CAMERAS kuanzia kwenye parking, kwenye korido, karibu na milango, vyumbani hadi bafuni. Je, ni haki kuweka security camera hadi vyumbani/bafuni?

    Jana nikiwa kwenye foleni Magomeni Mapipa dogo mmoja akaja na DVD kibao za dini, chini yake ameweka DVD ya X ina picha ya WEMA nikainunua ile kufika hotelini nikaweka kwenye laptop katika Clip Mojawapo najiona mimi na demu niliyemchukua week Mbili zilizopita.

    Hakika nilichoka, sijui cha kufanya nishaurini wadau.

Baada ya Pinda Kutangaza Nia ya Urais, Wanzazibari Wasema Hawamtaki Kwani Alisema Zanzibar Sio Nchi

$
0
0
Zanzibar. Madai ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuingia katika kinyang’anyiro cha urais yameibua mjadala mkali kutoka kwa baadhi ya wanasiasa, wasomi na wananchi wa Zanzibar ambao wamesema hafai kutokana na kauli yake kuwa ‘Zanzibar si nchi’.

Wakizungumzia uamuzi huo ulioripotiwa na vyombo vya habari juzi, baadhi ya wananchi hao wamempinga na wengine kumuunga mkono.

Aliyekuwa mgombea mwenza wa TLP katika Uchaguzi Mkuu 2010, Abdallah Othman Mgaza alisema Pinda anaponzwa na kauli yake kuwa Zanzibar si nchi... “Zanzibar ni nchi kamili ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutojua kwake akasema si nchi na kuwakera Wazanzibari. Anapoteza muda wake bure kwa kufikiria urais wa Muungano, sehemu moja ya dola hawana imani naye.”
.

Mkurugenzi wa Uenezi, Habari na Mawasiliano kwa Umma wa CUF, Salum Abdallah Bimani alisema chama hicho kimepata mshangao kusikia Pinda akitaka kuwamo katika orodha ya wanaojitaja kuwania urais wa Muungano wakati upande mmoja wa Muungano bado una kinyongo naye kwa matamshi yake yaliyodai Zanzibar si nchi.

“Ndugu zetu CCM Zanzibar wana kawaida ya kutotusikiliza na kutubeza, kwa hili tunawaomba chondechonde wafungue masikio yao, akiwa waziri mkuu alisema Zanzibar si nchi, akipata urais ataitangaza nchi yetu mkoa na kutuletea gavana mkaazi,” alisema Bimani.

CHADEMA Kosa Hili Hamjaliona, Slaa Tukulaumu?

$
0
0
Leo hii naomba kutoa maoni yangu kuhusu makosa ambayo yanafanywa na viongozi wa juu.
Niseme wazi kuwa kuanzia mwaka 2007 hadi kuendelea hasa 2009-2010 kijana yeyote aliyejitokeza na kusema yeye ni mwanachama wa ccm alikuwa anazomewa sana, kwani kwa asilimia 90 vijana wote hasa vyuo vikuu walikuwa ni wapenzi wa chadema.
Leo hii Chadema haina vijana wengi wenye kupambana kama ilivyokuwa hapo mwanzo, inaonyesha wazi kuwa chadema imefanya makosa makubwa kushindwa kuhakikisha vijana hawa watatumika vyema kueneza elimu kila kona ya nchi kuelekea katika ukombozi wa utawala wa CCM

Chadema dhana ya usaliti mnayoitumia kwa Vijana ni kosa kubwa na itawapotezea umaarufu wenu, hebu watumieni vijana wanaomaliza vyuo wakafanye kazi za kueneza chama na muwaamini na muwaheshimu ili waweze kusaidia kuleta mabadiliko na sio kukaa na kutuhumiana usaliti na umamlukiki kila siku.

Agness Masogange Awatukana Wanaume wa Bongo Wanampelekea Umbea Bwana Ake wa South Africa

$
0
0
Kama mnavyojua AGNES MASOGANGE kwasasa yupo BONGO na Yule jamaa yake yupo SAUZI..sasa kutokana na taarifa za kile ambacho MASOGANGE anakifanya hapa mjini kumfikia jamaa yake  huko SAUZI kupitia jamaa ambao wanampa ripoti zote kutoka hapa BONGO na hivyo kupelekea kuhatarisha penzi la MASOGANGE na huyo jamaa…MASOGANGE AMEAMUA KUFUNGUKA

Kupitia ukurasa wake wa INSTAGRAM aliweka picha hiyo na kuandika kama unavyoona hapa!

Msemaji wa Mariah Carey anena kuhusu ndoa ya Mariah na Nick Cannon

$
0
0
Msemaji wa Mariah Carey amezungumza kuhusu ndoa ya Mariah na mumewe Nick Cannon ikiwa ni siku chache tangu Nick aweke wazi kuwa walitengana miezi kadhaa iliyopita.

Akiongea na mtandao wa UsMagazine, msemaji huyo wa Mariah ameeleza kuwa hivi sasa mwimbaji huyo amejikita katika tour yake barani Asia na katika kuwaangalia watoto wake mapacha wenye umri wa miaka mitatu, Moroccan na Monroe.

“I don't comment on Mariah's personal life, but Mariah is focusing on her children and her tour.” Ameesema.

Mariah ambaye bado yuko kimya kuhusu suala hilo, anaendelea na tour yake barani Asia na amemaliza kupiga show Tokyo, Japan wikendi iliyopita na anaelekea Manila, Ufilipino ambapo atafanya show October, 28.

 Inaaminika kuwa Nick na Mariah walitengana mara baada ya Nick kuweka wazi kupitia kituo cha radio mwezi Machi kuwa aliwahi kuwa na uhusiano na Kim Kardashian na wasichana wengine maarufu.

Meninah: Sihitaji Marafiki wa Kike, sio Watu Wazuri Kabisa (Audio)

$
0
0
Meninah La Diva anautekeleza kivitendo msemo wa Fid Q ‘sihitaji marafiki’ na ameamua kuutupa kule urafiki na wasichana aka mashost.

Akiongea na tovuti ya Times Fm katika mahojiano maalum aliyofanya na Josefly, Meninah amesema kuwa hapendi kabisa kuwa na marafiki wa kike kwa kuwa sio watu wazuri.

“Sina rafiki, yaani hivi unavyoniona mimi ndo hivi ninavyotoka hapa nyumbani, nyumbani shughuli zangu. Sipendi kuweka marafiki, marafiki sio watu wazuri kabisa. Yaani sipendi ndo Mungu alivyoniumba.” Amesema.

“Yaani zile tu labda kazini kuna msichana labda nafanya nae kazi ile ‘mambo poa basi’. Lakini ile ‘shoga sijui tutoke twende out..’ sitokagi kwenda club, sitokagi kunywa pombe. Sinywi, siwezi kuenjoy sehemu kama hizo kwa sababu sio mlevi. Raha ya mlevi uwe na mlevi mwenzako sasa mimi sio mlevi. Mara nyingi mimi napenda kukaa nyumbani kufanya mazoezi na dancers basi.” Ameeleza.

Meninah amesisitiza kuwa anachokieleza ni ukweli na kwamba kama kuna msichana ambaye ni rafiki yake basi ajitokeze.

Sikiliza mahojiano yote hapo kufahamu mambo mengi kuhusu muziki wake, uhusiano wa mapenzi na mengine mengi.

Upaja Wangu Ndio Silaha Yangu, Nikivaa Nguo Ndefu Sijiamini Kabisa Nakosa Confidence

$
0
0
Admin 
Nimeona Nikuandikie e-mail Udaku Special Watu Wanipe Ushauri , Mimi ni Msichana Bado Mbichi Sana ila Tatizo langu ni Mavazi yaani Sijui inakuwaje kila nikitoka out ama Kwenda kazini nikivaa nguo ndefu sijiamini hata kidogo nakosa amani na hata furaha , ila siku nikiwa nimevaa nguo fupi basi najiamini si mchezo naweza kumface mtu yoyote , alafu napenda vile Kila mtu anavyoniangalia nikitembea with my High Heels..Je Nitakuwa nimeathirika kisaikologia kimavazi ama ni Kawaida hata wadada wengine inawakuta hivyo?

Mwanamuziki Oliver Mtukudzi Aonyesha Matokeo ya Vipimo vyake vya Ugonjwa wa Ukimwi

$
0
0
Mwanamziki mkongwe Oliver Mtukudzi, ameonyesha hadharani matokeo ya vipimo vyake vya ugonjwa wa ukimwi baada ya kuwepo kwa maneno maneno mtaani kwamba mwanamziki huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 60 kuwa mgonjwa wa ugonjwa huo hatari.

Hata hivyo katika majibu ya vipimo hivyo mwanamziki huyo alionekana kutokuwa na ugonjwa huo, alikiri kuwa ndugu zake wengi wamefariki kwa ugonjwa huo, lakini yeye anasumburiwa na ugonjwa wa kisukari na sio mwathirika wa Ukimwi.

Jeshi la Polisi Ladai Kuwashika Watu Walio Muua Mtoto Akizuia Gari la Baba yake Lisiibiwe na Majambazi Hao

$
0
0
JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha limewatia mbaroni watu saba wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya wanawake pamoja na uporaji wa kutumia silaha mjini hapa.

Taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa habari jana na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, ilisema kuwa kati ya watuhumiwa hao, wawili walifikishwa mahakamani juzi na kusomewa mashtaka.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, waliokamatwa wanahusika pia na tukio la kumpiga risasi mtoto wa miaka mitatu, Christen Nickson, aliyeuawa wakati akiwazuia wahalifu hao 

wasipore gari la wazazi wake, Agosti 21, mwaka huu.

Kamanda Sabas aliwataja watuhumiwa waliofikishwa mahakamani juzi kuwa ni Japhet Lomnyaki (25), mkazi wa Sakina na Nehemia Kweka (34), mkazi wa Ngaramtoni.

Watuhumiwa wanaoendelea kuhojiwa aliwataja kuwa ni Adam Mussa, maarufu kwa jina la Badi Makonde (30), mkazi wa Majengo, Tito Loomoni (25), mkazi wa Shamsi, Joseph Loomoni (29), mkazi wa Shamsi, Abdallah Maglan (22), mkazi wa Oldadai na Emmanuel Maglan (23), mkazi wa Oldadai.

“Watuhumiwa hao wanadaiwa kuhusika katika tukio la Agosti 21, mwaka huu, lililotokea eneo la Olasite, kwani siku hiyo walikuwa na pikipiki aina ya Toyo na walimjeruhi kwa kumpiga risasi mtoto Nikson na kumuua,” alisema Kamanda Sabas.

Jakaya Aishi Kwa Matumaini Upatikanaji wa Katiba Mpya, Asema Yupo Tayari Kukutana na Ukawa Kunusuru

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete amesema yupo tayari kukutana na viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), ili kunusuru mchakato wa Katiba mpya.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete imekuja siku chache baada ya baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kupinga hatua ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumtuma Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana, kusaka suluhu na viongozi wa Ukawa.

Akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro juzi, mara baada ya kusoma risala yao na kuunga mkono Bunge la Katiba, Rais Kikwete alisema hana 

sababu ya kutokutana na viongozi waliosusia vikao vya Bunge.

Alisema kutokana na hali hiyo, yupo tayari kukutana nao, na kwamba wanajua namna ya kukutana naye ili waweze kufanya mazungumzo yatakayoliwezesha taifa kupata Katiba mpya.

“Mimi sina tatizo la kukutana nao. Wanajua jinsi ya kukutana nami ili tuweze kutafuta namna ya kumaliza tofauti hizi.

“Mimi naishi kwa matumaini. Naamini kuwa tutafika mwisho vizuri. Mchakato ni mgumu, lakini barabara ndefu haikosi kona. Tukidhamiria kweli kweli tutafika tuendako vizuri,” alisema Rais Kikwete.

Alisema anasikitishwa na tofauti za viongozi wa siasa na kuleta mfarakano kwa taifa, hali ya kuwa tangu awali aliwaambia kuwa wakijiruhusu kushindana na kuviziana ni wazi mchakato wa Katiba utakwama.

Namna ya Kuondokana na Tatizo la Kutojiamini

$
0
0
Kila kitu ambacho ni halisi kinawezekana. Bila shaka unakumbuka vizuri kuhusu namna kutojiamini kwetu kunavyojengwa. Kwa kuwa tunajua chanzo, ni rahisi kupata tiba.

Njia zifuatazo zinaweza kukusaidia katika kujenga kujiamini. Kuna njia nyingi zinazopendekezwa, lakini kuna zile ambazo zimetumika sana katika kufanya kazi hiyo. Hizi zifuatazo ni baadhi yake.

1. Yachunguze mawazo yako na vitendo vyako kwa uangalifu ili kujua ni kitu gani hukufanya usisimke. Anza kufanya mambo ambayo unaona kwamba una uwezo kuyafanya bila wasiwasi na kuchukua uamuzi unaojitegemea kufuatana na utashi wako. Ikibidi unaweza kuomba msaada wa wengine, lakini jaribu kila mara kufanya mambo kufuatana na unavyoyaona.

2. Jifunze kujithamini. inawezekana kwa miaka na miaka umekuwa unajiona kama mtu usiye na thamani. Pia unaweza ukaona kwamba, hadhi uliyokuwa nayo mbele ya ndugu, jumuiya na jamii imepungua. Jali ujuzi na vipaji vyako; hata kama kuna ndugu wametajirika pamoja na kuwa ni mbumbumbu hiyo isiwe chanzo cha kukuvunja nguvu. Iko siku utafanikiwa kama utaanza kujiamini.
3. Jisamehe bila masharti yoyote. Kama maisha yako ya awali yalikuwa si ya kiungwana, jisamehe na anza maisha yako upya. Njia bora ya kujisamehe ni kujipenda bila masharti yoyote.

4. Pambana na hofu. Hofu ni kitu kibaya sana kwa sababu inaingilia kwenye uwezo wako wa kufikiri. Ili ufanikishe malengo yako ya maisha huna budi kuhakikisha kuwa huna hofu tena.

5. Fanya vitu unavyoviogopa. Orodhesha idadi ya vitu ambavyo ulikuwa unaviogopa. Kisha anza na vitu ambavyo unaviogopa zaidi na jiulize kwa nini usiweze kuvifanya.

6. Jifunze kupambana na kushindwa. Kubali kwamba kushindwa ni kama chombo cha kujifunzia na si kitu cha kukukatisha tamaa. Jua, na amini kwamba, bila kushindwa hakuna kukua. Pia elewa kwamba, kushindwa siyo dalili ya udhaifu, bali uimara.
7. Kubali kupingwa kwa moyo mkunjufu. Watu wa nje wanaweza kukusaidia kwa mambo yako mengi ambayo huyaoni. Watu wakikusoa, hata kama ni kifedhuli, chukua yaliyo mema na yafanyie kazi.

8. Fanya mazoezi ya kujiamini. Jifunze kusimama kwa miguu yako mwenyewe kimawazo, kiimani na kimatendo. Bila kuonyesha ujeuri unaweza kulinda haki zako, matarajio yako na maadili yako. Anza kujifunza kujenga taswira ya kujiona uko mwenyewe na unamudu kila kitu. Bila msaada na utegemezi kwa wengine.

9. Jipongeze kwa maneno mazuri. Jiamini na daima jipe moyo kwa maneno ambayo yatakutia moyo ili kwenda vyema katika shughuli zako. Usitumia maneno ya kejeli, kashfa na chuki dhidi yako mwenyewe, ‘mimi ni mjinga kweli yaani jambo dogo kama hili limenishinda….’ Unaweza kujisemea baada ya kukosea. Kama umekosea, jiambie maneno mazuri ya kujipa moyo na siyo maneno ya kero na fadhaa.

10. Usijilinganishe na wengine, bali iga. Kama wengine wanakuzidi isikukatishe tamaa ila iwe ni chachu ya maendeleo . jiambie, ‘kama wanaweza, maana yake ni kwamba, inawezekana, nami nitaweza tu.’

11. Fikiria mambo ambayo yanakufanya usiwe na furaha na jaribu kupambana nayo na kuondokana nayo. Kila wakati jiulize, ni kwa nini uko kwenye hali ya kihisia uliyo nayo. Usikubali kufuga huzuni kwa muda mrefu ndani mwako.
12. Fanya mambo uyapendayo zaidi. Kujiamini kutaongezeka kama utafanya mambo unayoyafahamu zaidi kwa sababu ni rahisi kuyafanikisha na kukuletea furaha.

13. Jifunze namna ya kushughulikia hasira zako. Mtu asiyejiamini ana kawaida ya kutaka kupendwa na watu, na katika kufanya hivyo, hapendi kuonekana kuwa ni mtu mwenye hasira na hivyo kuendelea kubakia na hasira zake moyoni hata kama ameudhiwa.

14. Kuzuia hasira hakusaidii, zaidi ya kukuongezea kuchanganyikiwa na kukufanya kuwa mtu usiye na furaha au kisirani. Ukiudhiwa, mwambie aliyekuudhi kinaganaga, lakini katika mazingira ya kistaarabu ambayo hayawezi kukuumiza wewe wala mtu ambaye amekuudhi.



Daktari Kanjanja Anaswa na Maiti Duka la Dawa Aliloligeuza Kama Hospitali

$
0
0
UKANJANJA! Jeshi la Polisi wilayani Ikungi, Singida linamshikilia daktari anayedaiwa kuwa ni feki, Prosper Samson (pichani) kwa madai ya kumtibu mgonjwa Jibuli Mahende, mkazi  Kijiji cha Iyumbu, Sepuka na kumsababishia kifo chake

Habari zinadai kuwa, Jibuli alifariki dunia hivi karibuni baada ya kutibiwa na mtu huyo anayejiita daktari kutokana na kile kilichodaiwa kuwa alizidishiwa dozi kwa kuongezewa chupa tisa za maji ya drip sanjari na vidonge sita ambavyo havikujulikana jina mara moja.

HISTORIA YA MAREHEMU
Kwa mujibu wa ndugu, marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua, kiuno na mgongo ambapo daktari huyo alimpa dawa hizo muda mfupi baadaye Jibuli alipoteza maisha akiwa kwenye duka la dawa, nyumbani kwa Prosper.

GANGA MKUU WA WILAYA ASIMULIA
Akizungumza kwa niaba ya mganga mkuu wa Wilaya ya Ikungi, mmoja wa madaktari wa wilaya hiyo, Philip Kitundu alisema tukio hilo lilitokea juzikati saa nne asubuhi kwenye vyumba maalum vilivyotengwa na daktari huyo kwa ajili ya kutolea huduma mbalimbali za matibabu.

“Baada ya kupewa taarifa za kifo hicho na utete wake, kesho yake tulikwenda kukagua duka la dawa la mtu huyo,” alisema daktari huyo.

Kwa mujibu wa daktari huyo, walipofika dukani kwa Prosper anayejitangaza kuwa ni daktari wa magonjwa ya binadamu, walilikagua na kugundua kuwa hakuwa na leseni kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) inayomruhusu kufanya biashara hiyo na alikiri kuwa hakuwa na cheti  cha chuo chochote alichosomea udaktari.

“Hata tulipopekuwa dukani kwake tulikuta dawa ambazo haziruhusiwi kabisa kwenye maduka ya dawa muhimu, tulikuta dawa na sindano na dawa za vidonda. Alikuwa anawafunga vidonda watu, analaza na anatoa huduma za kujifungua kwa akina mama,” alifafanua daktari huyo.

YADAIWA NI MTU WA TATU KUFA
Daktari huyo wa wilaya aliongeza kusema kwamba katika ukaguzi huo walikuta pia dawa zilizokwisha muda wake wa matumizi na kuwa tukio la Jibuli kupoteza maisha ni la tatu kwa watu waliopatiwa matibabu katika duka hilo, wawili walifia nje ya duka.

MTUHUMIWA ATOA MAELEZO
Kwa upande wake daktari huyo anayedaiwa ni feki, licha ya kukiri kumpokea mgonjwa huyo akiwa na hali mbaya na kwamba baada ya kuchukua historia yake aligundua alikuwa akisumbuliwa na kifua na kabla ya kupelekwa kwake alianza matibabu kwa waganga wa tiba asilia.

“Walikuja kwangu ili wapate ushauri lakini jinsi nilivyomwona mgonjwa nikawashauri wafanye mikakati apelekwe sehemu nyingine kwani niligundua ana matatizo tangu Juni, mwaka jana,” alisema Prosper.

MTOTO WA MAREHEMU NAYE ANENA
Naye mtoto wa marehemu Jibuli aitwaye Jilala alisema siku ya tukio asubuhi alikwenda kumsalimia baba yake na kumkuta akiwa hoi, ndipo alipoamua kumpeleka kwenye duka hilo la dawa ambapo baada ya uchunguzi wa ‘daktari’ huyo aliambiwa baba yake alisumbuliwa na kifua, mgongo na kiuno.

“Baada ya dokta kunifahamisha ugonjwa unaomsumbua baba, niliondoka kurudi nyumbani kutafuta fedha za kumuondoa pale dukani ili  kumpeleka Hospitali ya Mkoa wa Singida kwa matibabu zaidi,” alifafanua mtoto huyo.

Akaendelea: “Hata hivyo, kabla ya baba hajapoteza maisha alipokuwa dukani kwa dokta alipewa vidonge sita vya dawa ambazo sikufahamu zinatibu ugonjwa gani na ilipofika saa nne asubuhi alifariki dunia, nikamsusia na kuita watu kuja kuiona maiti ya baba.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, SACP Godfrey Kamwela amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Gari la Lulu Alilodai Kanunua Kwa Hela Yake Lazua Utata, Kadi yake ina Anuani ya Wizara ya Mambo ya Ndani

$
0
0
Stori: Musa Mateja na Shakoor Jongo 
MAKUBWA! Mambo yamekuwa mambo, kadi ya gari jipya la staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ imeibua mazito kufuatia Jeshi la Polisi Dar es Salaam kubaini kuwa namba ya Sanduku La Posta (SLP) iliyoandikwa kwenye kadi hiyo ni Wizara ya Mambo ya Ndani Tanzania.

IMEVUJAJE?!
Hilo lilibainika baada ya gazeti dada na hili, Ijumaa toleo la Ijumaa iliyopita kuandika habari yenye kichwa kisemacho; LULU AANDIKA HISTORIA.

Katika habari hiyo, Lulu alipewa shavu kwa vile alinunua gari aina ya Toyota Rav 4 New Model kwa pesa zake mwenyewe tofauti na baadhi ya mastaa wa Bongo ambao huhongwa magari na wanaume.

SIMU YAPIGWA
Wakati gazeti hilo likiwa mitaani, mtu mmoja aliyedai kuwa ni afisa wa jeshi la polisi jijini Dar es Salaam alipiga simu kwenye chumba cha habari cha Global Publishers na kusema kuwa S.L.P ya 9140 iliyotumika kwenye kadi ya gari la Lulu ni ya jeshi hilo.

NI KOSA LA JINAI
Ofisa huyo aliliambia gazeti hili kuwa raia wa kawaida haruhusiwi kutumia sanduku la barua la jeshi kitu alichodai kinaonesha jinai ilifanyika wakati wa usajili ya gari hilo.
“Haiwezekani Lulu atumie Postal Office Box (P.O.Box au S.L.P) ya jeshi kwenye kadi ya gari lake ikizingatiwa kuwa yeye ni raia wa kawaida.

“Ukiachana na hilo hata sisi maofisa wa jeshi la polisi hatuwezi kuitumia hiyo anuani kwa shughuli zetu binafsi labda kuwe na kibali maalum,” alisema afisa huyo ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa vile yeye si msemaji wa jeshi hilo.

LULU ANASEMAJE?
Baada ya kupata maelezo hayo, gazeti hili lilimtafuta Lulu ili kujibu madai hayo yenye utata ambapo alisema kuna mtu alimtengenezea namba yake ya TIN (Taxpayer Identification Number) ndiye aliyemwekea anuani hiyo bila yeye kujua.

Huku akisita kumtaja kwa jina mtu huyo lakini akimtaja kwa cheo ambacho kiko wazi na mapaparazi wetu wakamjua, Lulu alifunguka hivi:

“Namiliki gari langu kihalali kabisa na nina kila kitu, niko tayari kwenda kokote kuonesha uhalali wa umiliki wangu. Kuhusu hiyo anuani, mtu aliyenitengenezea TIN Number ili nipate leseni ya udereva ndiye aliyetumia hiyo anuani, mimi sijui chochote jamani.”

AOMBA AHIFADHIWE SIRI
Katika hali ya kushangaza, Lulu aliwaambia mapaparazi wetu wasimtaje jina gazetini mtu huyo aliyemsajilia TIN akisema asitiriwe siri yake


POLISI NAO WANENA
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, ambako ndiko usajili wa gari hili ulifanyika katika ofisi za TRA, Zakaria Sebastian, alisema jeshi lake halina taarifa za kuwepo kwa jambo hilo lakini watalifuatilia kwa karibu.

“Huenda ni mke wa askari au mwanafamilia. Unajua kuna baadhi ya maofisa wana msamaha, huenda alitumia hivyo, lakini tutafuatilia,” alisema kamanda huyo ambaye alielezwa kuwa, Lulu hajawahi kuwa mke wala mwanafamilia ya mwajiriwa wa jeshi la polisi.

“Kama hajawahi kuwa mwenye kustahili kutumia anuani hii, basi tutafuatilia ili kujua wakati akiitumia, je alikuwa anakusudia kufanya jinai? Tukijiridhisha hivyo bila shaka sheria itafuata mkondo wake.”
GPL

Baby Madaha Baada ya Kuachana na Manager Wake Sasa Amejiweka Kwa Mwanamuziki Wyre

$
0
0
Kuna Habari Hapa mjini Udaku Special Imezipata kwamba Mwanamuziki Mrembo wa Bongo Flava Baby Madaha Amabae alihamishia Makao Yake Kenya Kwa Sasa etiii Amejiweka Kimapenzi kwa Mwanamuziki Wyre wa Kenya hii Ni Baada ya Kutemana kimapenzi na Bosi Wake Joe Kairuki
Baba Madaha Alipoulizwa alijibu Hivi:
"Mimi nina uhuru wa kufanya chochote ninachojisikia na hakuna mtu atakayeweza kuniingilia katika maisha yangu wala uhusiano wangu kwa sababu sigongi kwa mtu kuomba msaada"

Van Gaal: Huenda ikatuchukua Mwaka Mzima Kuepuka Madhila Haya ya Aibu Kwa Team ya Man United

$
0
0
Meneja wa klabu ya Man Utd Aloysius Paulus Maria van Gaal amelia na kikosi chake ambacho usiku wa kuamkia hii leo kiliendelea kula msoto wa kutopata matokeo mazuri tangu msimu wa soka huko nchini Uinmgereza ulipoanza August 16.

van Gaal amesema kikosi chake hakikucheza vizuri wakati wa mchezo wa michuano ya kombe la ligi dhidi ya klabu ya Milton Keynes Dons ambao waliibuka na ushindi wa mabao manne kwa sifuri na kuwatupa nje ya michuano hiyo mashetani wekundu.

van Gaal amesema makosa ya kipuuzi yaliyofanywa na wachezaji wake hususan waliocheza safu ya ulinzi yalikuwa chagio kubwa kwa wapinzani wao kupata mabao kwa urahisi, hivyo hana budi kuwasilisha lawama zake kwa wachezaji aliokuwa amewapa jukumu la kucheza hapo jana.

Wakati huo huo van Gaal amesema bado anaendelea na falasafa yake ya kutengeneza mazingira mapya ya kikosi na anaamini mpango huo utafanikiwa licha ya kupita kwenye mazingira magumu katika kipindi hiki cha mwanzoni mwa msimu wa mwaka 2014-15.

Amesema suala hilo linapaswa kufahamika hata kwa mashabiki wa Man Utd ambao wanahitaji kuona mafanikio yanapatikana kwa haraka haraka, lakini yeye kama meneja anatambua kipindi hiki cha mpito kinaweza kuchukua muda mrefu.

Karrueche Aomba Radhi Baada ya Kudiss Nywele za Mtoto wa Beyonce

$
0
0
Karrueche Tran amewaomba radhi mashabiki wa Beyonce waliomshambulia kwenye mitandao ya kijamii baada ya kudiss muonekano wa nywele za Blue Ivy kwenye tuzo za MTV VMAs, wakati akifanya kipindi cha 106& Park cha BET.

Karrueche aliponda muonekano wa nywele za Blue Ivy katika kipengele cha kipindi hicho kilichopewa jina la ‘Top 6 Things Blue Ivy thought about the VMA’s’, ambapo alisikika akisema kwa kumkariri Blue Ivy kuwa ‘Kweli niliamka hivi kwa sababu wazazi wangu hawakunichana nywele. Pole Blue! Nakupenda!”

Mashambulizi yaliyoendelea ndani ya siku mbili mfululizo yamemfanya mrembo huyo kuomba radhi kupitia Instagram akikiri kufanya makosa kwa kuwa yeye ni binadamu.

Katika maelezo yake, ameomba radhi kwa kutamka sentensi hiyo ambayo amesema ilitengenezwa kwenye muongozo wa kipindi na BET na ikapitia kwake.

BET wamewajibika pia na kueleza kuwa Karrueche alikuwa anasoma maelezo hayo kwenye teleprompter (screen ya kusomea habari kwenye TV) kama sehemu ya script na kwamba ilifanyiwa mabadiliko dakika kumi kabla ya kwenda hewani na hakupata nafasi ya kuipitia tena.

Huenda angekataa kuisoma kama angeipitia awali.

Picha Mpya za Mwanamuzi Shilole Alizotupia Instagram ni Shidaaa..So Cute!

$
0
0


Kweli Nuhu Mziwanda anafaidi...Hizo ni Picha Mpya za Mrembo wa Bongo Movies na Bongo flava Shilole...Cute or Not?
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images