Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Askofu Kakobe ' Wakovu Wangu Sio wa Dhahabu Bandia...Shitishwi na Mtu'

$
0
0

Askofu Zakaria Kakobe amesema hatikiswi na upepo unaotikisa nyasi. Amewaasa waumini wake wasimame imara kila wanapokumbana na changamoto. Amesema hayo baada ya kuitwa na Idara ya Uhamiaji, Dar es salaam. Ameongeza kuwa hana hofu kwani wokovu wake siyo wa dhahabu bandia.

Idriss Sultan Aandika Ujumbe Huu Kuwasuta Wanaosema Amefulia

$
0
0

Idriss Sultan Anaandika:
"Nasikia watu wanauliza kama nimefulia. Kama kufulia ni kuwa ambassador wa brand 3 kubwa, kuwa kwenye series kubwa DSTV East Africa, kutoa one of the beat movies according to people, kuwa na brand ya viatu inayofanya vizuri sanaaaa, kuwa casted kwenye movie mbili Hollywood, kuwa na the first political satire comedy tv show Tanzania(SioHabari), kupata awards 3, kuwa growing presenter, kuwa one of the very few men from Tanzania wenye influence Africa entertainment and politically na sio musician basi jibu ni NDIO NIMEFULIA 😂.. As long as sijafika ninapotaka mimi hata niwe na bilioni 4 kwenye account yangu bado nipo broke. Na soon tunaingia Forbes ila ndugu yangu nipo broke, Tukutane kazini 🙌🏽" By @idrissultan

Mzungu wa Harmonize Amtumbua Jack Wolper....Aweka Wazi Messeji Wolper Aliyoandika Kwa Harmonize

$
0
0

wanadada @sarah__tz ambaye ni Mpenzi wa Mkali kutoka @wcb_wasafi @harmonize_tz ameonesha kukasirishwa na kitendo cha Mwanadada @wolperstylish kumtumia Picha na Jumbe Mpenzi wake katika Mtandao wa kijamii wa instagram

@sarah__tz ameweka Picha ambayo inaonesha Picha na jumbe ambazo Wolper amemtumia Harmonize na kuweka Ujumbe wa kumkanya Wolper kuwa aachane na Mpenzi wake na aishi Maisha yake kama inavyooneka hapo.

Ujumbe wa Wolper unaoonekana hapo unaonyesha kuwa kitendo cha Page mbalimbali kumtag kwenye Video na Post za zamani za yeye na Harmonize kinamuumiza kiasi cha kutaka kublock page zote zinazomfanyia hivyo kitu ambacho Kimemkera Sarah na kuamua kuandika hivi.

Breaking News: Ajali NYingine Yaua Nane Mbeya

$
0
0
Breaking News: Ajali NYingine  Yaua Nane MbeyaWATU nane wamefariki dunia papo hapo na mmoja amejeruhiwa baada ya gari dogo aina ya Toyota Noah kugongana na basi katika eneo la Igodima nje kidogo ya Jiji la Mbeya. Kaimu Kamanda wa Polisi Mbeya, Mussa Taibu amethibitisha.

Ajali hiyo imetokea leo Jumatatu Aprili 9, 2018 mchana ikihusisha Noah yenye namba za usajili T 649 DEA na basi la Igembesabo katika Barabara ya Chunya Mbeya huku chanzo cha ajali hiyo kikiwa hakijulikani.

Endelea kufuatilia habari zetu kwa taarifa zaidi kuhusu tukio hilo.

Ndugai Aungana na Mbunge CCM

$
0
0
Ndugai Aungana na Mbunge CCM
Spika wa Bunge, Job Ndugai amewashauri Wabunge wanawake kuungana na kupeleka hoja ya kuwasaidia kina mama wanaoteseka magereza kwa kufungwa kwa madeni madogo madogo huku wakiwa na watoto na wenye maradhi ambao serikali inapaswa kuwagharamia kila siku


Spika Ndugai ametoa ushauri huo baada ya Mbunge wa Tarime Mjini Esther Matiko kuhoji, kwanini serikali isitumie busara zaidi kwa wafungwa hususani wakina mama wenye watoto wachanga ambao wanafungwa kwa kesi za kudaiwa laki 1-2 halafu wanafungwa miezi 6 kwa maana wanakuwa wanaenda kutumia gharama kubwa kuliko deni wanalodaiwa.

Hata hivyo swali la Esther Matiko lilijibiwa na William Tate Ole -Nasha amesema suala hilo ni la kisheria hivy kama Mbunge huyo ameona sheria hiyo imepitwa na wakati na haitendi haki anapaswa kupeleka hoja ya sheria bungeni ili iweze kubadilishwa.

Naye Spika Ndugai ameongeza "Na kwa kweli wabunge wanawake mpo wengi hapa kama mambo hayo yapo kweli mnapaswa kuungani ili kuangalia mateso ya kina mama wa aina hiyo".

Mambo ni Hivi Joyce Kiria Naye Aenda Kumshitaki Mumewe kwa Kuwatelekeza Watoto

$
0
0
Mambo ni Hivi Joyce Kiria Naye Aenda Kumshitaki Mumewe kwa Kuwatelekeza WatotoMwanaharakati wa masuala ya usawa wa kijinsia na Mtangazaji wa kipindi cha ‘Wanawake Live’, Joyce Kiria ‘Super Woman’ (mwenye hereni pichani) amekuwa mmoja ya mamia ya wanawake waliojitokeza leo, Aprili 09, 2018 kwenye Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kupatiwa msaada wa kisheria baada ya kutelekezewa watoto na wazazi wenzao.M


Mamia ya wanawake wamemiminika leo katika ofisi hizo kufuatia wito wake kuwataka wanawake wote waliotelekezewa watoto na wazazi wenzao wa kiume wafike ofisini hapo na vielelezo halali ili waweze kupatiwa msaada wa kisheria.

Wanawake hao ambao kwa sasa wanalea watoto wao peke yao baada ya kutelekezwa, wamejitokeza kuanzia majira ya asubuhi japo kuwa mvua kubwa zilikuwa zikinyesha.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Kiria ameandika; Dar Es Salam Mpya! Wanawake tuliotelekezwa tunalea familia peke yetu!

Makonda ameanza rasmi kusikiliza shida za wanawake hao leo Aprili 9, 2018 ofisini kwake.



Sarah wa Harmonize Ashindwa Kuvumilia Ampa Onyo Kali Wolper "Unamsumbua Mpenzi wangu Kwenye Simu "

$
0
0
Sarah wa Harmonize Ashindwa Kuvumilia Ampa Onyo Kali Wolper "Unamsumbua Mpenzi wangu Kwenye Simu "


Mpenzi wa msanii Harmonize, Sarah amemuonya ex-girlfriend wa muimbaiji huyo Jacqueline Wolper kwa kile alichodai muigizaji huyo anamsumbua sana mpenzi wake katika mitandao.

Aliweka wazi hilo ni Wolper ambaye ameweka wazi jumbe alizotumiwa na Sarah kupitia mtandao wa WhatsApp na kueleza kuwa hawezi kumjibu kwa sasa zaidi ya kumuhurumia.



Harmonize na Wolper walikuwa wapenzi kipindi cha nyuma na couple yao ilikuwa na nguvu sana yenye kukodolewa macho na vijana wengi. Walionekana kushibana katika mapenzi yao kiasi kwamba Harmonize aliweza hata kumshirikisha Wolper katika video ya wimbo wake unaokwenda kwa jina la Niambie.

Baada ya kuachana Harmonize aliweka wazi kuwa katika mahusiano na Sarah binti kutoka nchini Italy na Wolper naye akawa na mahusiano na kijana maarufu mtandaoni, Brown, hata hivyo mahusiano yao pia hayakuchukua muda ukawa umevunjika.

Kumbe Mwanaheri Ameolewa Mke wa Pili Siri Imefichuka

$
0
0
Kumbe Mwanaheri Ameolewa Mke wa Pili Siri Imefichuka MAMBO ni moto! Saa chache baada kufungwa, ndoa ya kimyakimya ya staa wa Bongo Movies na Tamthiliya, Mwanaheri Ahmed ‘Mwana’ imekwaa skendo namba moja baada ya kuanza kupigwa zengwe kwamba eti ameolewa mke wa pili.



TUJIUNGE NA CHANZO

Kwa mujibu wa chanzo makini cha Gazeti la Ijumaa Wikienda ambacho ni mtu wa karibu wa familia ya Mwanaheri, mwanaume huyo aliyemuoa anajulikana kwa jina moja la Khamis ambaye ni mfanyabiashara maarufu na tayari ana mke mwingine na watoto.



Ilidaiwa kuwa, ndiyo maana mwanaume alifanya tukio hilo kwa siri kubwa bila mkewe kujua ndiyo maana hata baadhi ya rafiki zake Mwanaheri hawakualikwa.

Chanzo hicho kiliendelea kumwaga ubuyu kwamba, mipango hiyo ya ndoa ilifanywa na watu wachache mno.



“Kama hamna ubuyu kamili ni kwamba mwanaume aliyemuoa Mwanaheri ana mke wa ndoa na watoto. Ndiyo maana ameamua kufanya ndoa hii kuwa ya kimyakimya bila watu wengi kujua.

“Kingine ambacho watu hawakijui ni kwamba, huyo mwanaume aliyemuoa Mwanaheri amemzidi umri kwa kiasi kikubwa,” kilitiririka chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa gazetini.



MWANAHERI NA IJUMAA WIKIENDA

Kama ilivyo desturi ya Ijumaa Wikienda, mara baada ya kunyetishiwa skendo hiyo ambayo ndiyo habari ya mjini, lilimtafuta Mwanaheri ili afunguke anachokijua juu ya hoja hizo mbili- kuwa ni mume wa mtu na kwamba amemzidi umri mno ambapo mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo;

Ijumaa Wikienda: Mambo vipi Mwanaheri? Mbona umekula harusi mwenywe, kulikoni?

Mwanaheri: Sijala mwenyewe jamani…ilikuwa ya harakaharaka.

Ijumaa Wikienda: Kwa nini ikawa ya harakaharaka?

Mwanaheri: Basi tu, mume wangu alikuwa na safari ya ghafla ndiyo maana shughuli ikawa ya ghaflaghafla.



Ijumaa Wikienda: Mbona kuna taarifa kuwa huyo mwanaume aliyekuoa ni mume wa mtu na ana watoto?

Mwanaheri: Hapana… siyo kweli kabisa…mimi ninachojua ana watoto tu basi…

Ijumaa Wikienda: Sasa kwa nini ulikuwa unamficha asionekane kwenye picha za tukio lenu la kufunga ndoa hadi Ijumaa Wikienda likatumia nguvu ya ziada kupata picha zake?

Mwanaheri: Ni uamuzi wa mtu, unajua hapendi kufahamika kwa watu.

Ijumaa Wikienda: Pia inadaiwa kuwa unamficha kwa sababu amekupita umri kwa miaka mingi, yaani ni sawa na baba yako, je, unazungumziaje hilo?



Mwanaheri: Mimi nilichoangalia ni ndoa tu na stara yangu, lakini siyo kitu kingine.

Ijumaa Wikienda: Kwa hiyo inawezekana akawa kweli ni mume wa mtu kutokana na umri alionao?

Mwanaheri: Hapana, umri siyo kigezo kinachoweza kuonesha kuwa mtu ameoa maana inawezekana amechelewa kwa sababu zake binafsi.

Ijumaa Wikienda: Poa Mwanaheri.

Mwanaheri: Poa karibu sana.



IJUMAA WIKIENDA LASAKA RIPOTI KAMILI

Kufuatia skendo hiyo kuwa gumzo, kumekuwa na mengi yanayosema juu ya ndoa hiyo hivyo Gazeti la Ijumaa Wikienda lipo mitaani kusaka ubuyu kamili ili kuurusha hapahapa.

Kauli ya Ommy Dimpoz Baada ya Amber Lulu Kumwambia Hana Muonekano wa Kiume

$
0
0
Kauli ya Ommy Dimpoz Baada ya Amber Lulu Kumwambia Hana Muonekano wa KiumeMsanii Ommy Dimpoz amejibu kile anachodai Amber Lulu kuwa hana mvuto wala muonekano wa kiume.

Ommy Dimpoz ameiambia Bongo5 kuwa hawezi kuzungumzia hilo kwa sasa na hajui stori hizo zimetoka wapi.

“Mimi sijui chochote na sijui hizo stori zimetoka wapi na zimeanzia wapi lakini kikubwa sisi kama wasanii unajua kila siku vitu ambavyo vinatuzunguka ni mambo ya mitandao, kwa hiyo in short no comment,” amesema.

Wiki iliyopita katika mahojiano na Jonijoo kupitia Now You Know msanii Lulu aliulizwa kati ya Jux na Ommy Dimpoz anaweza kuolewa na nani endapo wakitokeza kwa pamoja.

“Jux sawa, Dimpoz hajakaa kama mwanaume, Ommy Dimpoz hawezi kukaa au kushindana na Jux ni zero, hana mvuto wowote , hamna chochote kinachonivutia kutoka kwake,” amesema.

Rais wa Zamani wa Brazil Ajisalimisha Gerezani Kutumikia Kifungo cha Miaka 12

$
0
0
Rais wa Zamani wa Brazil Ajisalimisha Gerezani Kutumikia Kifungo cha Miaka 12Leo April 9, 2018 stori ninayokusogezea ni kuhusu Rais wa zamani wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva amejisalimisha katika gereza la Curitiba tayari kuanza kutumikia kifungo cha miaka 12 baada ya awali kukwepa kufanya hivyo.

Ijumaa Mahakama ilimhukumu kwa mashtaka ya ufisadi, lakini alikimbilia katika makao makuu ya muungano wa wafanyakazi mjini Sao Paolo, ambako wafuasi wake walitaka asijisalimishe.

Televisheni nyingi nchini Brazil zimeonesha alivyowasili kwa helikopta katika Makao Makuu ya Polisi katika mji wa Curibita.

Lula alitoa hotuba katika mji wa Sao Bernardo do Campo kabla ya kujisalimisha, Lula amejitaja kuwa raia aliyekasirishwa na mashtaka ya kutungwa ya ufisadi.

Shule Yatangaza Kuruhusu Wanafunzi wa Kiume Kuvaa Sketi

$
0
0
Shule Yatangaza Kuruhusu Wanafunzi wa Kiume Kuvaa Sketi



Shule moja ya bweni nchini Uingereza ijulikanayo kama Uppingham School imetangaza kuruhusu wanafunzi wa kiume wa shule hiyo kuvaa sketi.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Richard Maloney ameeleza kuwa mwanafunzi yeyote wa kiume atakayeomba ruhusa ya kuvaa sketi ataruhusiwa kwani anaamini uhuru na uchaguzi wa mtu ni lazima viheshimiwe.

Inaelezwa kuwa suala hili la kuvaa uniform ya aina yoyote kutasaidia sana katika kuondoa ubaguzi wa kijinsia baina ya wanafunzi.

Simba, Mtibwa Sugar Kuonyeshana Ubabe Leo

$
0
0
Simba, Mtibwa Sugar Kuonyeshana Ubabe LeoKlabu ya soka ya Simba kupitia kwa kocha wake msaidizi Masoud Djuma imewataka mashabiki wao kujitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro kwenye mchezo wao dhidi ya Mtibwa Sugar leo.


Akiongea kuelekea mchezo huo wa leo Masoud amesema mashabiki wajitokeze kwa wingi kuipa nguvu timu hiyo na wao kama benchi la ufundi na wachezaji watafanya kazi yao uwanjani ambayo ni kusaka alama tatu.

''Nachoweza kusema ni kuwakaribisha tu mashabiki mana sisi tumeshafanya maandalizi yetu vizuri na wao wakija watupe nguvu tu sisi tutafanya kazi yetu uwanjani, ni mchezo mgumu lakini tumejiandaa kushinda'', amesema.


Simba ambayo inaongoza msimamo wa ligi ikiwa na alama 49 kwenye michezo yake 21 itakuwa na kibarua kigumu dhidi ya Mtibwa Sugar ambayo ipo kwenye kiwango kizuri ikitoka kushinda ugenini dhidi ya Singida United.

Jibu la Wolper Baada ya Kupigwa Stop na Sarah Kuwasiliana na Harmonize

$
0
0
Jibu la Wolper Baada ya Kupigwa Stop na Sarah Kuwasiliana na Harmonize


Muigizaji Jacquline Wolper kupitia instagram account yake amepost picha inayoonyesha ujumbe aliotumiwa WhatsApp ambapo mwanamke anamuomba akae mbali na mpenzi wake na aache ku-comment kwenye post zake anazozipost, ujumbe huo umeandikwa kwa lugha ya kiingereza kisichofasaha.

Baada ya ujumbe huyo Jacquline Wolper aliandika “😂😂😂😂😂😂😂😂 wewe acha nikuhurumie tuu siwezi kukujbu#temporary post#huruma”



Inawezekana  Jacquline Wolper ameamua kuweka mahusiano yake ya kimapenzi private maana tokea aachane na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Brown hajamuweka mwanaume yoyote katika mitandao ya kijamii na kuthibitisha kuwa ni mpenzi.

Kakobe Ajisalimisha Ofisi za Uhamiaji Kuhojiwa Uraia Wake

$
0
0
Kakobe Ajisalimisha Ofisi za Uhamiaji Kuhojiwa Uraia Wake
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zakaria Kakobe amefika katika Ofisi za Uhamiaji Makao Makuu jijini Dar es Salaam zilizopo Kurasini kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu kile kinachodaiwa kuwa ni mashaka juu ya uraia wake kufuatia barua aliyoandikiwa na Mamlaka hiyo Aprili 5, mwaka huu.


Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoka katika ofisi hizo, kakobe amesema kuwa lengo kuu lilikuwa juu ya uraia wake ambapo amewaeleza kuwa yeye ni Raia wa Tanzania na mzaliwa wa Kijiji cha Kibilizi wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma.

Kakobe amesema ameulizwa pia juu ya cheti cha kuzaliwa na akawambia enzi za kuzaliwa kwake mwaka 1955 vyeti hivyo vilikuwa havitolewi kwani harakati za kuanza kutolewa vyeti vya kuzaliwa zilianza mwaka 1981 hivyo akasema kama watahitaji zaidi ya ukoo wake wafike Kijiji cha Kanyonza kilichopo Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma.
Akizungumza wakati wa mahubiri yake jana, Askofu huyo alisema hatikiswi na upepo unaotikisa nyasi. huku nakiwaasa waumini wake wasimame imara kila wanapokumbana na changamoto na kuongeza kuwa hana hofu kwani wokovu wake siyo wa dhahabu bandia.

Utoaji wa Mahali Je Ni Kuchuma Mali Au Kurudisha Shukrani?

$
0
0
Image result for wakifunga ndoa

Kumekuwa na wasiwasi nchini Kenya kuhusu namna gharama ya mahari inavyopandishwa kadiri siku zinavyosonga katika jamii mbalimbali.

Hivi majuzi kiongozi wa kisiasa wa serikali katika Bunge la Kenya alishutumu gharama kubwa ya mahari katika jamii ya Wasomali.

Kiongozi wa wengi bungeni, Aden Duale anasema hicho ndicho chanzo kikuu kinachowavunja moyo vijana na kuwafanya wasusie ndoa.

Amelalamika kwamba gharama kubwa zinazotozwa zimeugeuza utamaduni huo kuishia kuwa kama ''kitega uchumi cha mamilioni ya dola''.

Lakini sio tatizo linaloshuhudiwa kwa Wasomali tu. Vijana wanataja kukwama kupiga hatua ya kufunga ndoa kutokana na gharama hizo kubwa za mahari wanazoshindwa kuzimudu.

Mahari inavyotozwa katika baadhi ya nchi za Afrika:
Somalia:
Idadi ya ngamia au pesa taslimu mwanamume anazoahidi kumlipa mkewe kama mahari huitwa Meher.

Sio lazima Meher ilipwe moja kwa moja lakini huwa ni kama ahadi wameandikiwa, na mume hana budi kulipa katika kipindi cha ndoa.

Zamani ngamia ndio waliotumika kulipa mahari hayo lakini siku hizi mtindo umebadilika na pesa taslimu ndio zinazothaminiwa zaidi katika jamii hii.

Harusi za kifahari zapigwa marufuku Somalia
Kijana anaweza kutakiwa kulipa hadi dola elfu kumi za Marekani kwa bibi harusi. Na kila thamani ya mahari inapokuwa kubwa ndio huonekana kuwa fahari kubwa kwa bibi harusi na familia yake na pia hudhihirisha ukubwa wa thamani ya mke anayeolewa.

Lakini tatizo kubwa ni kwamba vijana wengi hawawezi kugharimia mahari inayoitishwa na baadhi yao huishia kuwa na deni la maisha.

Thamani ya mahari inapokuwa kubwa ndio huonekana kuwa fahari kubwa kwa bibi harusi na familia yake
Tanzania:
Tanzania, ni nchi nyingine inayotajwa kushuhudia viwango vikubwa vya mahari katika baadhi ya jamii.

Huenda ndio moja ya sababu inayowafanya baadhi ya vijana kutooa kwa njia rasmi.

Vigezo ni vingi vinavyobaini kiwango cha mahari atkachotozwa kijana, mfano katika baadhi ya jamii - weupe wa msichana humaanisha mahari zaidi, lakini pia kiwango cha elimu cha msichana anyechumbiwa.

Kwa kukadiria kijana huitishwa ng'ombe au pesa zenye thamani ya kati ya shilingi milioni 5 hadi milioni 20 za Tanzania.

Uganda:
Utamaduni huu ni wa kawaida nchini Uganda, zaidi kwa jamii zilizopo katika maeneo ya mashinani, lakini pia hutolewa katika maeneo ya mijini.

Mahari nchini humu hufuata msingi ambao umekuwepo - kutoa kitu ili upewe mke.

Lakini sasa kuna mtindo kwa baadhi ya familia kuandikishana mikataba na bwana harusi kama ithibati ya kulipa mahari anayoitishwa.

Inaaminika kuwa iwapo mke amemtoroka mumewe baada ya kuteta na akarudi kwao, familia yake haina budi ila kurudisha mahari yote aliyolipiwa.

Mnamo 2010 mahakama nchini humo iliamua kuwa utoaji mahari ni halali, lakini majaji walipiga marufuku mtindo huo wa kurudishwa mahari wakati ndoa inapovunjika.


Je ni kweli gharama ya juu ya mahari inawazuia vijana kufunga ndoa Afrika Mashariki?
Kenya:
Katiba nchini Kenya haishurutishi ulipaji wa mahari, lakini ni jambo linalofahamika kuwa mahari hulipwa katika jamii tofuati nchini.

Baadhi ya jamii kwa mfano kwa wafugaji husisitiza mahari ya mifugo, huku kwa jamii nyingine mali, pesa taslimu na hata madini hupokewa kama mahari.

Mahari hapa huitwa "lobola", ambapo mwanamume hukabidhi ima mali au ng'ombe kwa familia ya mke au kwa mara nyingine vyote - kama ishara kwamba yuko tayari kumuoa.

Malipo ya lobola ni ishara ya uwajibikaji wa mwanamume kumhudumia mkewe na huonekana kama ishara muhimu na inayohitajika katika kuendeleza utamaduni, na sio kana kwamba amemnunua mwanamke.

Mahari ni nini?
Utamaduni wa kutoa mahari upo katika nchi nyingi ulimwenguni zikiwemo barani Asia, mashariki ya kati sehemu kadhaa za Afrika na pia katika baadhi ya visiwa vya pasifiki.

Kiwango kinachotolewa hutofautiana kuanzia zawadi ndogo tu za kuendeleza utamaduni huo hadi maelfu ya dola za Marekani kwa mfano kama inavyoshuhudiwa katika ndoa za baadhi ya jamii.

Tangu jadi, utoaji mahari umekuwa ni utamaduni unaoheshimiwa na kuenziwa pakubwa hata miongoni mwa jamii za watu waliosoma na kuishi maisha ya kisasa.

Kwa kawaida mahari huwa ni kama mkataba wa makubaliano kabla ya ndoa ambapo mali kama ng'ombe, ngamia, mbuzi au hata pesa taslimu hulipwa na bwana harusi kwa familia ya bibi harusi ili apewe mke.

Iwapo mume hatotimiza mahari iliyokubaliwa kwa muda uliotolewa, kuna jamii ambao humrudisha mke nyumbani mpaka mume akamilishe kulipa mahari.

Na kwa namna ambavyo mambo yamekuwa yakibadilika na gharama kuongezeka, baadhi ya wadadisi wanasema utamaduni huu wa kutoa mahari unageuzwa kuwa njia ya kujinufaisha na kujigamba kwa mali badala ya kuwa utamaduni wa kuonyesha upendo na shukrani.

Mchambuzi wa masuala ya kijamii kutoka Tanzania Betty Masanja anasema, "Suala zima limegeuzwa na kumfanya mwanamke kuwa chombo au bidhaa tu."


''Hali inazidi kuwa mbaya kutokana na kuwa, watu wana shida za kiuchumi, umaskini umekithiri hasa kwa familia ambazo hazikusoma."

Ndio maana unaona hata jamii zinawaozesha watoto wao wakiwa na umri mdogo ili mahari ilipwe kuitajirisha familia.

Lakini sio suala la kujitajirisha tu, Betty anasema kuna kutothaminiwa kwa mtoto wa kike ambapo wengi huozeshwa ili mali ipatikane kusaidia kumuelimisha mtoto wa kiume.

Ameeleza: ''suala zima limegeuzwa na kumfanya mwanamke kuwa chombo au bidhaa tu''.

Video: Makonda Ajitosa na kwa Wakina Baba Waliotelekezwa "Kama Kuna Kinababa Wametelekezwa Waje Tuwasaidie"

$
0
0
Makonda Ajitosa na kwa Wakina Baba Waliotelekezwa "Kama Kuna Kinababa Wametelekezwa Waje Tuwasaidie"

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amewataka kina baba wote ambao wametelekezwa na kina mama kufika ofisini kwake ili kutoa malalamiko yao ili wapatiwe msaada wa kisheria kama ilivyo kwa kina mama

Mwanaume Kuwa Rijali Kunako Sita Kwa Sita Kwa Kutumia Products Hizi

$
0
0

Bidhaa original na zilizothibitishwa kiafya zinapatikana NATURAL BEAUTY PRODUCTS sasa zinapatikana kwa bei ya punguzo la %10. 

Bidhaa hizi zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina kemiko wala madhara yoyote. Hakikisha unapewa risiti original ya natural beauty products

TUNAZO KAMA HIZI

1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @250,000/=

2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=

3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @200,000/= 

4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @170,000/=

5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @240,000/=

6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/=

7.BODY BOOSTER_ Hii ni yakuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @140,000/

8.DISCREET ORIGINAL_Hii ni dawa ya kuondoa mvi na zisiludi tena milele @150,000/= N.K

NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri na garantii ili kukuhakikishia ubora na usalama wa bidhaa za NATURAL BEAUTY LTD

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0659618585 au
0759029968

Ommy Dimpoz amjibu Amber Lulu

$
0
0

Msanii Ommy Dimpoz amejibu kile anachodai Amber Lulu kuwa hana mvuto wala muonekano wa kiume.

Ommy Dimpoz ameiambia Bongo5 kuwa hawezi kuzungumzia hilo kwa sasa na hajui stori hizo zimetoka wapi.

“Mimi sijui chochote na sijui hizo stori zimetoka wapi na zimeanzia wapi lakini kikubwa sisi kama wasanii unajua kila siku vitu ambavyo vinatuzunguka ni mambo ya mitandao, kwa hiyo in short no comment,” amesema.

Wiki iliyopita katika mahojiano na Jonijoo kupitia Now You Know msanii Lulu aliulizwa kati ya Jux na Ommy Dimpoz anaweza kuolewa na nani endapo wakitokeza kwa pamoja.

“Jux sawa, Dimpoz hajakaa kama mwanaume, Ommy Dimpoz hawezi kukaa au kushindana na Jux ni zero, hana mvuto wowote , hamna chochote kinachonivutia kutoka kwake,” amesema.

Godbless Lema Amshangaa RC Gambo

$
0
0

Mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema hajasita kuweka wazi hisia zake baada ya kutambulishwa na RC Gambo katika Ibada ya kusimikwa Mhashamu Isaack Amani kuwa Askofu Mkuu Jimbo la Katoliki la Arusha.

Lema kupitia ukurasa wake wa Twitter ameonekana kushangaa kitendo cha RC Gambo kumuita yeye rafiki.

Ameandika; “Katika Ibada ya kusimikwa Askofu, Rais aliongea neno la Mungu kuhusu Amani na Haki. Bila shaka demokrasia na haki vitashamiri tena. Askofu Amani yeye akasisitiza ushirikiano kisiasa bila kubaguana. Mrisho Gambo(RC) yeye akuogopa kuwa muongo madhabauni, eti aliniita Mimi rafiki yake."

Werrason Atua Bongo Kukinukisha Jumamosi

$
0
0
Werrason Atua Bongo Kukinukisha JumamosiWerrason akiwasili fukwe za Escape One na wanamuziki wenzake huku akiongozwa na mwenyeji wao ambaye ni mtangazaji wa Clouds FM, Hamisi Dakota.


MSANII wa muziki wa dansi kutoka  Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Werrason yupo nchini Tanzania kwa ajili ya kufanya shoo Jumamosi hii katika fukwe za Escape One Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Muda mfupi uliopita mwanamuziki huyo alipata fursa ya kuzungumza na waandishi wa habari katika kikao kilichofanyika katika fukwe hizo ambapo amesema hapa nchini anamfahamu Msanii Diamond Platnumz pekee maana amekuwa akimsikia mara kadhaa akitajwa huko Congo.


Werrason na wanamuziki wake wakitoa kionjo cha wimbo kabla ya kuhitimisha kikao na wanahabari.

Hivyo amewaomba wasanii wa hapa nchini  wamtafute kuanzia leo ili wabadilishane mawazo na hata ikiwezekana kufanya klabo ya pamoja kabla ya siku yake ya kufanya shoo yake hiyo ya Jumamosi na ile ya Jumanne katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.


Waandishi wa habari wakichukua matukio mbalimbali ya kikao hicho kilichofanyika katika fukwe za Escape One mapema leo.

“Waafrika ni kitu kimoja hivyo ningependa wiki hii moja ambayo nipo hapa nipate kubadilishana mawazo na wasanii wa hapa Tanzania, ila hata kama kuna mtu angependa tufanye ngoma ya pamoja nipo tayari kwani kufanya hivyo ni kukuza muziki wetu wa Afrika ambapo utapata promo ya nchi nyingi jirani,” alisema Werrason.
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images