Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

China Wapo Tayari Kumtunza Mtoto" - Paul Makonda

$
0
0

NA GERALD KITALIMA
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amefunguka na kusema kuwa yule mtoto ambaye anaonekana kuwa na asili ya nchini China ambaye mama yake alikwenda kulalamika katika ofisi yake wiki iliyopita, serikali ya China imeonyesha nia ya kutaka kumtunza. 


Makonda ameweka wazi hayo leo April 14, 2018 na kusema kuwa ameanza kufanya mawasiliano na serikali ya China kupitia Ubalozi wao na kudai tayari wamekubali juu ya hilo na kusema endapo vipimo vikibainisha kuwa mtoto huyo ni mtoto wa raia wao basi watakuwa tayari kumuhudumia. 

"Waliponipa taarifa zile niliamua kuwasiliana na ubalozi wa China na tukawapa taarifa na taarifa hizo tayari wameshatuma nchini kwao kwenye ile kampuni ambayo baba wa yule mtoto aliyekuwepo kwa hiyo tunafanya utaratibu wote inawezekana mzazi wake yupo hapa hapa nchini au nje, siyo huyo tu wengi wapo Oman kule yaani kuna wazazi wengi wa kiume wapo huko ila watoto wao wapo hapa Dar es Salaam. Kwa hiyo si kwamba tunawatafuta tu waliopo nje ya mikoa lakini hata hawa ambao wako nje ya nchi tunatumia Wizara yetu ya Mambo ya Nje kupitia kwa balozi zetu zilizopo huko" alisema Makonda 

Makonda aliendelea kutoa ufafanuzi kuhusu mtoto ambaye inasemakana raia wa China ambaye mama yake aliibuka kwenye ofisi zake na kusema kwa sasa hana mawasiliano na baba wa mtoto huyo ambaye anadai aliondoka nchini baada ya vibali vyake kuisha. 

"Kwa mazungumzo tuliyonayo ya awali na huo ubalozi wa China wamekubali kwamba endapo mtoto yule ikibainika wao kama nchi watakuwa na wajibu wa kumtunza kwa hiyo muda si mrefu yule mtoto naye maisha yake yanaweza kubadilika na kupata neema lakini sina maana kwamba Watanzania sasa wazae na wachina ili waendeleaa kupata huduma hapana, tubaki kwenye misingi yetu ya kukubaliana nani anakuoa kwa jinsi ambavyo unataka maisha yako ayaendeshe" alisisitiza Makonda

Mbunge Godbless Lema na Mkuu wa Mkoa Arusha Mrisho Gambo Wamaliza Tofauti zao

$
0
0

Mbunge wa Arusha Mjini, Mheshimiwa GODBLESS LEMA na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bwana MRISHO GAMBO wamemaliza tofauti zao za muda mrefu.

Baadhi ya wananchi wamesema hatua hiyo itatoa fursa ya kuunganisha nguvu zao kushughulikia masuala ya maendeleo na kutatua kero zinazoikabili jamii.

Lukuvi 'Kero ya Kulazimishwa Kulipia Nyumba Mwaka au Miezi Sita Inakwisha Hivi Karibuni'

$
0
0

Waziri wa nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.Willium Lukuvi amesema kero wanayopata wapangaji wa nyumba kulazimishwa kulipa kodi ya mwaka mzima ama miezi sita kwa mkupuo itafikia tamati siku chache zijazo.

Waziri Lukuvi amesema hayo mkoani Dodoma wakati akifungua maoenesho yanayohusiana na ujenzi wa nyumba na umiliki ardhi yanayoendelea katika viwanja vya Bunge na kusema Serikali ipo katika hatua za mwisho kuunda chombo maalum cha kusimamia sekta ya nyumba.

Yule Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu na za Kiasili Sharifu Lukumani Sasa Yupo Hewani

$
0
0
WENYE SHIDA ZITUATAZO:
CHEO KAZINI, KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI, MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA, KISUKARI, FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI, MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.

MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE

WASILIANA NAE KWA NAMBA 0762899488-0656145170-WhatsApp namba +255620665635

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya April 15

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya April 15

Mwigizaji Monalisa Kutoka Bongo Movie Ashinda Tuzo ya Kimataifa Ghana

$
0
0

Mwigizaji Monalisa Kutoka Bongo Movie Ameitoa Tanzania Kimasomaso Baada ya Kushinda Tuzo ya Best Female Movie Star in Africa huko Nchini Ghana...

Baada ya Kushinda Monalisa Ameandika yafuatayo kupitia Instagram:

From @monalisatz - Hahahaha Pozi LA Taifa.I had to do this kabisaaaaaaa
Tumeshindaaaaaaa narudi home na Tuzo za kutosha.Ahsante Watanzania,Nawapenda mno.

Ripoti: Mambo matano makubwa baada ya Alikiba kuoa hapo jana

$
0
0
Kama tulivyokuhabarisha hapo jana kuwa msanii wa muziki Bongo, Alikiba anaona huko Mombasa nchini Kenya, ni kweli hilo limejiri licha ya kugubikwa na usiri mkubwa.

Alikiba amemuoa mrembo Aminah Rekish ambaye inaelezwa kuwa anafanya kazi ya Fiscal analyst (Mchambuzi wa masuala ya fedha) serikalini, kaunti ya Mombasa.

Soma Pia; Nafasi za ajira zilizo Tangazwa Leo

Mwandishi wa habari kutoka Nairobi Kenya, Changez Ndzai ameiambia Bongo5 mara baada ya shughuli ya hapo jana leo hii pia kuna tarajiwa kuwa na hafla fupi ambayo Gavana wa Mombasa, Hassan Ali Joho anatajiwa kuwepo.

Ameeleza pia hafla ya leo kuna uwezekano kwa waandishi wa habari kupata baadhi ya picha pamoja na video ukilinganisha na hapo jana ambapo hakuna aliyeweza kufanya hivyo.

Jambo la pili ni kwamba wiki ijayo, April 19, 2018 kutakuwa na sherehe kubwa huko huko Mombasa lakini inatarajiwa watu wachache ndio wataalikwa na baada hapo itafanyika sherehe nyingine hapa Bongo nyumbani kwa Alikiba, Tabata, Dar es Salaam.

 Nne; inaelezwa kuwa katika sherehe ambayo itaifanyika Tabata ndipo Alikiba atahamia katika mjengo wake mpya ambao nao umefanywa siri hadi kukamilika kwake.

Tano; Taarifa zinadai mama mzazi wa Alikiba alimueleza mwanae hatoweza kuhamia katika mjengo huo hadi pale atakapokuwa ameoa.

Mwanamke ‘Aliyenyonyesha’ Tembo Kwa Maziwa ya Chupa Afariki Dunia

$
0
0
Kutoka nchini Kenya Mhifadhi wa Tembo Daphne Sheldrick amefariki dunia kwa maradhi ya saratani akiwa na umri wa miaka 83, jana April 13, 2018.

Alisaidia kuokoa maisha ya tembo zaidi ya 230 wengi wao ambao walipoteza mama zao kwa ujangili au ukame kwa kutengeneza mpango maalumu wa kuwapatia maziwa na kufanikiwa kwa ufanisi.

Daphne alizaliwa na kukulia nchini Kenya, alitumia takribani nusu ya miaka yake ya kwanza kazini, akifanya kazi pamoja na mume wake ambaye alikuwa Mwingereza David, ambaye ndiye aliyegundua Hifadhi ya Taifa Tsavo Mashariki nchini Kenya.

Baada ya kifo cha mumewe mwaka wa 1977, alianzisha mfuko wa David Sheldrick Wildlife Trust (DSWT), ambao unajulikana zaidi kwa kuokoa na kuimarisha tembo yatima porini.

Ilimchukua miaka yake 28 kufanikiwa kutengeneza formula maalum ya kunyonyesha tembo kwa maziwa ya chupa.


Nandy Aibukia kwa Dogo Janja

$
0
0
Ikiwa zimepita takribani siku mbili tokea mrembo Nandy kuomba radhi kutokana na video yake ya faragha kusambaa mitandaoni, msanii Dogo Janja ameibuka na kudai wasanii hawana umoja na wanafiki huwa wanafurahi sana kuona mwenzao amepatwa na majanga ili mradi apotee katika tasnia.


Dogo Janja ametoa kauli hiyo usiku wa kuamkia leo Aprili 15, 2018 kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii na kusema anahisi anaweza kuchukiwa leo hii na wasanii wenzake ila ni lazima yeye aongee ukweli ili mradi donda ndugu liliopo katika muziki limepone.

"Wasanii sisi ni ma-snichi sana aise, baada ya hii ishu ya Nandy ndio nimepata uhakika. Wakati wa ishu ya Roma nilianza kuliona jinsi kwenye makundi pembeni watu kibao walikuwa wanafurahi tena maneno kibao kama atakoma, amezoea huyo. Jana na juzi nimekaa na watu wasanii wakubwa tu na wote walikuwa wanasema bora limemtokea Nandy hili angalau spidi za 'show' zitapungua", amesema Dogo Janja.

Pamoja na hayo, Dogo Janja ameendelea kwa kusema "bora BASATA ingemfungia miezi 6 apotee kidogo, walikuwa wanapiga stori kama utani ila moyoni nimefikiria sana. Wasanii tuache roho mbaya, wote sisi masikini tunahangaikia ugali. Tukipata ajali kazini, tusiombeane mabaya tutafute amani".

Kwa upande mwingine, Dogo Janja amewashauri wasanii wenzake wawe na moyo wa upendo kwa wenzao na waache tabia ya kufurahia matatizo wanayowapata wakiwa kazini.

Taarifa Kwa Umma: Huduma za Mabasi ya Mwendokasi zimesitishwa Barabara ya Jangwani

$
0
0

DAR: Huduma za Mabasi ya Mwendokasi zimesitishwa kuanzia saa 11:00 alfajiri ya leo kutokana kufungwa kwa Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kwa sababu ya mafuriko yaliyosababisha maji kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi
-
Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, na Gerezani - Muhimbili
-
Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, UDA Rapid Transit (UDART), imesema huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa.

Kutana na Mtaalam Sharif Hamad Kalala Mchambuzi wa Nyota za Binadamu na Tiba Asili

$
0
0
KUTANA NA SHARIF HAMAD KALALA NI
SHARIFU MCHAMBUZI WA
NYOTA ZA BINAADAMU NA NI MWENYE UPEO MKUBWA KUTAFITI MATATIZO YAKO KABLA YA KUTOA USHAURI WAKE WA TIBA AlJALISHI MBALI ULIKO TIBA YAKE UMFIKIA YEYOTE MWENYE UITAJI POPOTE
DUNIANI.

 SHARIF HAMAD KALALA NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA QUR-AN, DAWA ZA ASILI ZA MITI SHAMBA PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.
ANATIBU KWA NJIA YA SIMU KWA KUTOA
MAELEKEZO NAMNA YA MATUMIZI YA DAWA UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-

 KUFANIKISHA NDOA KWA UNAYE MPENDA KWA HARAKA. KUMRUDISHA MPEZI NDANI YA MASAA 12 TU.
 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME) NDANI YA /IKI MMOJA TU
MIGUU KUWAKA MOTO KUTAFSIRI NDOTO MFARAKANO WA WANANDOA MFARAKANO KAZINIKUPANDISHWA CHEO NDANI YA SIKU SABA 7 TU.
KUTOA PETE YA BAHATI KUTOA MAJINI MACHAFU IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA. KUPATA MAFANIKIO YA MALI BILA YA MASHARTI. KUPANDIKIZANYOTA YA KUBASHIRI KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA KWENYE BIASHARA. ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE. ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA
KWA NJIA YAMSUKULE
NAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA MPYA NDANI SIKU 7 TU.
MENGINEYO MENGI ZAID YALIYO KUWA SUGU PIGA KWA WALE WALIYO ANGAIKA SEHEMU MBALI MBALI SHARIF HAMAD KALALA NI SULUISHO. ENDAPO UTAMSIKILIZA KWA YALE ATAKAYO KUSHAURI NA KUKUPA
ELEKEZI.
 TIBA NI KWA DINI ZOTE POPOTE ULIPO NJE NA NDANI YA NCHI.
MOBILE +255 -673 025 376
WhatsApp +255-757 069 066

Huwezi Amini. Wasanii Wengi wa Bongo Flava Wamefurahi Kilichomtokea Nandy

$
0
0
Ikiwa zimepita takribani siku mbili tokea mrembo Nandy kuomba radhi kutokana na video yake ya faragha kusambaa mitandaoni, msanii Dogo Janja ameibuka na kudai wasanii hawana umoja na wanafiki huwa wanafurahi sana kuona mwenzao amepatwa na majanga ili mradi apotee katika tasnia.

Dogo Janja ametoa kauli hiyo usiku wa kuamkia leo Aprili 15, 2018 kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii na kusema anahisi anaweza kuchukiwa leo hii na wasanii wenzake ila ni lazima yeye aongee ukweli ili mradi donda ndugu liliopo katika muziki limepone.

"Wasanii sisi ni ma-snichi sana aise, baada ya hii ishu ya Nandy ndio nimepata uhakika. Wakati wa ishu ya Roma nilianza kuliona jinsi kwenye makundi pembeni watu kibao walikuwa wanafurahi tena maneno kibao kama atakoma, amezoea huyo. Jana na juzi nimekaa na watu wasanii wakubwa tu na wote walikuwa wanasema bora limemtokea Nandy hili angalau spidi za 'show' zitapungua", amesema Dogo Janja.

Pamoja na hayo, Dogo Janja ameendelea kwa kusema "bora BASATA ingemfungia miezi 6 apotee kidogo, walikuwa wanapiga stori kama utani ila moyoni nimefikiria sana. Wasanii tuache roho mbaya, wote sisi masikini tunahangaikia ugali. Tukipata ajali kazini, tusiombeane mabaya tutafute amani".

Kwa upande mwingine, Dogo Janja amewashauri wasanii wenzake wawe na moyo wa upendo kwa wenzao na waache tabia ya kufurahia matatizo wanayowapata wakiwa kazini.

Wolper 'Nikiamua Harmonize Namchukua Hata Kesho..Sarah Atulie tu zamu yake ya Kulia Bado Haijafika'

$
0
0
STAA wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper baada ya kudaiwa ‘kumendea’ penzi la mwanamuziki Rajab Abdulhan ‘Harmonize’ na mpenzi wake Sarah, staa huyo ameibuka na kusema Harmonize hapindui kwake hivyo mpenzi wake huyo ajipange tu.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Wolper alisema kuwa ameshangazwa na habari ambayo aliiweka Sarah kwenye ukurasa wake wa Instagram uliokuwa ukionesha kuwa, Wolper alimtumia ujumbe Harmonize kupitia Instagram akieleza kwamba anamkumbuka, kitu ambacho hawezi kukifanya.

“Ninachoona mimi Sarah hajiamini kabisa, siwezi kufanya upuuzi huo kabisa, yeye yupo na mwanaume lakini bado anahangaika mitandaoni, hajui kuwa mwanaume wake hapindui kwangu hata siku moja, akae ajitulize tu zamu yake ya kulia bado haijafika,” alisema Wolper.

Shamsa Ford Apanga Kumpeleka EX Wake Kwa Paul Makonda, Adai Amuhudumii Mtoto Wake

$
0
0
MSANII wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford amesema kuwa siku akitibuka atampeleka moja kwa moja mzazi mwenzie Dickson Matoke kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda kwa ajili ya kudai haki ya kuhudumiwa mtoto wake.

Akipiga stori na Risasi Jumamosi, Shamsa alisema kuwa sio kwamba hana uwezo wa kumhudumia mtoto wake lakini kuna wakati unaumia kuona baba wa mtoto yupo, anakula bata tu akiwa hajui hata kula ya mtoto wake inatoka wapi.

 “Dawa ya wanaume wa sampuli hii ni kuwapeleka tu kwa Makonda. Mimi watu watashangaa sana siku watakaponiona pale lakini ni kwa sababu wakati mwingine ukifikiria unajikuta unapatwa na hasira kuona mzazi yupo lakini kama hayupo vile,” alisema Shamsa.
Tangu Jumatatu iliyopita, akinamama wengi waliotelekezewa watoto wamekuwa wakifika kwa Makonda ili kusaidiwa lakini hakuna staa wa kike aliyetinga hadi juzi Alhamis.

  STORI: IMELDA MTEMA

Mbunge Chadema Azuiwa Kuchangia Bungeni

$
0
0
MWENYEKITI wa Bunge, Mussa Zungu, amemzuia Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Upendo Peneza, kuchangia bungeni baada ya kuendelea kulitaja jina la Rais wakati wa kuchangia kwake licha ya kukatazwa kufanya hivyo.

Upendo alikuwa akimhusisha Rais na kuzuiwa kwa maandamano nchini na matangazo ya moja kwa shughuli za chombo hicho cha kutungwa sheria, yaani ‘Bunge Live’.

Kutokana na mbunge huyo kumtaja Rais katika mchango wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, aliomba kutoa taarifa ya kukiukwa kwa kanuni za 68(1) na 64(1) za Bunge akieleza kuwa Rais anawakilishwa na mawaziri ndani ya Bunge kwa mujibu wa Katiba.

“Na kanuni hii ya 64 inatukumbusha kwamba, haturuhusiwi kuzungumza mwenendo wa Rais na hasa anapokuwa katika madaraka ndani ya ofisi yake,” alisema.

Mhagama pia alisema hawatakiwi kuzungumza jina la Rais kutaka kushawishi namna ya kutoa uamuzi na kwamba kama Peneza anaona kuna shida azungumze na wawakilishi wake.

Akitoa majibu ya mwongozo huo, Zungu alisema kuwa jina la Rais halipaswi kutajwa kwa dhihaka, halaumiwi wala hatakiwi kusemwa kama alivyofanya Peneza.

Alimtaka mbunge huyo kuuliza utendaji wa mawaziri kwa kuwa kanuni inawataka wabunge kutohoji utendaji wa Rais ndani ya Bunge.

“Jina la Rais halitumiwi kwa namna ulivyokuwa unalitumia na kwa hiyo, nayafuta maneno yote kwenye hansard (kumbukumbu rasmi za Bunge),” alisema.

Hata hivyo, baada ya kupewa nafasi ya kuendelea kuchangia, Peneza aliendelea kusema juu ya kauli za Rais.

Kutokana na hali hiyo, Mhagama alisimama tena kutaka kutoa taarifa lakini Zungu alimzuia akisema: “Natumia kanuni ya 73 ukae chini hutazungumza tena.”

Wabunge wengine waliochangia walitaka Wakala wa Barabara Vijijini (Tarura), kuongezewa mgawo wa fedha za bajeti kwa kuwapa nusu ya fedha za Wakala wa Barabara (Tanroad) ili kutimiza majukumu yake ipasavyo.

Mbunge wa Lulindi, Jerome Bwanausi (CCM), alisema kama Tarura haijaongezewa bajeti yake, utakuwa ni wakala ambao umeanzishwa lakini haujaleta tija.

“Sasa hivi wakala huu umeazima watumishi kutoka halmashauri, wapewe watumishi wao na fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara ili ziweze kupitika,” alisema.

Mbali na Mbunge huyo wabunge wengine waliochangia sula hilo ni pamoja na Magdalena Sakaya (Kaliua-CUF), Livingstone Lusinde (Mtera- CCM), Fred Mwakibete (Busokelo-CCM) na Maftaha Nachuma (Mtwara Mjini - CUF).

Download Hapa Application ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu

 Bonyeza Hapa Chini

==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>
 

Life Style ya Ommy Dimpoz Yaacha Maswali Mengi, Afananishwa na Warembo Kama Sanchoka

$
0
0
NI kijana flani hivi mtanashati, kipenzi cha kinadada, akicheka mashavuni anabonyea pia ana sauti nzuri anaposikika nyuma ya biti. Anamiliki Lebo ya PKP (Pozi Kwa Pozi) na wimbo wake wa Me and You ulibeba tuzo tatu katika kinyang’anyiro cha Tuzo za KTMA 2013.

 Bado hujamjua tu? Sikia tena, yupo chini ya Lebo ya Rockstar400, ni mzaliwa wa Kigoma, wimbo wake wa mwisho kutoa unaitwa Cheche na anapenda maisha ya bata!

Hapo je? Kama bado hujamjua sasa hapo utakuwa ‘slow’ mtu wangu, lakini sio kesi, ngoja nikutafunie umeze, ninamzungumzia mkali kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva, Omari Nyembo ambaye anafahamika zaidi kwa jina la Ommy Dimpoz. Ommy ametengeneza hit kadhaa kwenye gemu la Bongo Fleva. Baadhi yake ni Nai Nai, Ndagushima na Baadaye.

Hata hivyo mbali na kupendwa na mashabiki kutokana na ngoma zake kali zenye kuburudisha, miaka ya hivi karibuni amevuna pia mashabiki wengi wanaofuatilia ‘life style’ yake ya maisha ya bata kwenye Mtandao wa Kijamii wa Instagram.

 Ommy amekuwa akitupia picha akiwa maeneo mbalimbali duniani, ikiwemo kwenye miji mikubwa kama London, Dubai, Sandton, Machester, New York na sehemu nyingine mbalimbali ikiwa ni pamoja na kwenye viwanja vikubwa vya michezo na mahoteli mbalimbali. Sasa ukianza kutazama life style yake hii, kwa kile anachokitupia kwenye Instagram, unaweza kufananisha na namna wanavyoishi mastaa wengi wa kike wakiwemo Tunda na Sanchoka!

 Hata hivyo ni life style yake hiyo inayoacha maswali. Ukisoma komenti kwenye ukurasa wake wa Instagram, unaweza kuona watu wanavyokuwa wanamuuliza maswali kuhusu bata zake. Kwamba nani yupo nyuma ya bata hizo na jeuri ya pesa anaitoa wapi.

Wengine wanafika hatua ya kuandika kwamba kwa muziki na mafanikio aliyonayo kwenye gemu la muziki hayatoshi pekee kuishi namna anavyoishi. Bata linazidi kipato chake kinachojulikana labda kama ikiwa ana madili mengine ambayo anayafanya kimyakimya!

 Sasa kama si muziki wake, nini kinampa jeuri ya fedha kiasi cha kuponda raha kama anavyofanya? Maana anamiliki lebo pia anamsimamia mwanamuziki Nedy Music, vyote hiyo ni vitu vinavyohitaji kuongozwa na pesa. Ukweli ni kwamba maswali haya hatuwezi kukwepa kujiuliza kama wadau wa burudani!

Mikito NusuNusu, imemtafuta mara kadhaa Dimpoz ili kuweza kuzungumzia bata zake lakini hajatoa ushirikiano, kwani ametumiwa sms, hajajibu, amepigiwa simu, hajapokea na gazeti limekwenda mpaka nyumbani kwake lakini halijafanikiwa kumpata. Hata hivyo, Dimpoz anafahamu kwamba mashabiki wake wana kiu ya kufahamu juu ya safari zake za nje na bata zake anapata jeuri wapi.

 Kwani hata hivi karibuni akizungumza na mtandao mmoja wa burudani amesema mashabiki wasijiulize sana kuhusu safari zake za nje kwani yupo bize nje kutokana na mambo ya kikazi kwamba toka asaini Rockstar400, ametakiwa kuandaa albamu. Kwa hiyo yupo bize kusafiri huku na kule kwa ajili ya kolabo. Lakini maswali ya kujiuliza, Old Traford anakwenda kufanya kolabo? Au mahotelini anakoonekana nako kuna kolabo?

 Kama ni kolabo mbona hatuoni picha za studio yupo ‘booth’ akiandaa kazi au yupo na msanii yeyote wa nje akiandaa mzigo mpya? Ipo wazi kwamba bado kuna maswali mengi ya kujiuliza. Ni vyema Dimpoz akaibuka na kukubali kutoa ushirikiano ili kukata kiu ya mashabiki wake ambao wamekuwa wakijiuliza maswali juu ya bata zake.

MAKALA: BONIPHACE NGUMIJE

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumapili

Ni Wakati wako Dada wa Kupendeza na Mwanaume Kuwa Lijali kwa Bidhaa za Natural Beauty

$
0
0

Zile tiba za asili zilizothibitishwa na kupewa kibali sasa zipo @natural beauty prod.
Ni wakati wako dada wa kupendeza na mwanaume kuwa lijali kwa bidhaa original zilizotengenezwa kwa mimea na matunda🍇🍓🍋🍒🥑

PATA KWA PUNGUZO LA BEI

1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @240,000/=

2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @145,000/=

3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 7.5 hadi 8 (wiki 2-3) @190,000/=

4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @160,000/=

5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @240,000/=

6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @140,000/

7.BOTCHO MULT PLUS_Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza ( Hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @190,000/=

8.BOTCHO CREAM HOLOGRAM_ Hii ni yakupaka ya kuongeza (HIPS na MAKALIO) @170,000/=

9.LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu (CHUPA YA BIA) @140,000/=

10.BODY BOOSTER_ Hii ni yakuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @140,000/= N.K

NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri na garantii ili kukuhakikishia ubora na usalama wa bidhaa za NATURAL BEAUTY LTD

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0659618585 au
0759029968 

Tanzia: Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kongwa Mkoani Dodoma Afariki Katika Ajali Mbaya

$
0
0

Taarifa zilizotufikia hivi punde, zinaeleza kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kongwa mkoani Dodoma, Mhandisi Ngusa Izengo amefariki dunia baada ya gari lake kuangukiwa na lori la mafuta usiku wa kuamkia leo

Tunaendelea kufuatilia taarifa zaidi kuhusu tukio hili.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images