Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live

Tetesi: Kocha wa Mbao FC Mrundi, Etiene Ndayiragije kutua Yanga SC

$
0
0

Kocha Mkuu wa klabu ya Mbao FC Mrurundi, Etiene Ndayiragije huwenda akaingia mkataba wa muda na mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu soka Tanzania Bara Young Africans kufuatia timu hiyo kukosa huduma ya George Lwandamina aliyekwenda kwao Zambia.

Taarifa za chini ya kapeti zinaeleza kuwa kocha huyo wa Mbao, Ndayiragije anahusishwa kujiunga na Yanga SC kurithi mikoba ya Lwandamina aliyetangazwa rasmi kutoka ndani ya klabu ya Zesco United, Aprili 10

Aprili 11 mwaka huu Kocha, Etiene Ndayiragije alikosekana kwenye eneo la benchi la ufundi la timu ya Mbao FC wakati wa mchezo wao wa ligi kuu ya Tanzania Bara raundi ya 24 wakiwa nyumbani licha ya kuchomoza na ushindi wa  mabao 2 – 1 dhidi ya Njombe Mji jambo ambalo likaongeza uvumi wa kutua Yanga SC.

Moja ya chombo cha habari kimepata kumhoji, Etiene Ndayiragije juu ya tetesi hizi za kutakiwa kujiunga na mabingwa hao wa tetezi wa ligi ya Vodacom, Yanga SC na kusema kuwa hupokea taarifa kutoka kwa wasimamizi wake ‘management’ pale jambo linapo kamilika na sio tetesi na kwakuwa hajaambiwa chochote anaamini kuwa dili hilo halikukamilika.

Muda sio Mrefu King of Music wa Tanzania Anaoa Lakini Kinachonisikitisha ni Kweli Aly kiba Hajaona Bongo

$
0
0
Siku zote inajulikana king of music wa bongo hana skendo mbaya anajitahidi sana kuziepuka na sasa king kiba anaoa hivi karibuni
Ameshatoa taarifa kwa watu muhimu muhimu akiwa na mpambe wake ommy dimpoz

Sasa kinachonisikitisha kweli Tanzania nzima hakuna msichana anaejielewa mpaka amehama nchi ameenda kutafuta Kenya
Kweli wasichana wa bongo hapa mmekosa sifa ya kuolewa na king kiba
Hii ni aibu mpaka kijana kama huyu anaenda nje ya nchi kuoa

Dada zetu mjirekebishe jamani au ally kiba kaamua kuwachunia tu
Ay naye nasikia alioa Rwanda huko

Mpunguzeni mapepe wasichana wa Bongo

Tanzania Yapaa FIFA

$
0
0
Tanzania imepaa kwa nafasi 9 hadi nafasi ya 137 kutoka nafasi ya 146 kati ya mataifa 211 katika viwango vya ubora wa soka duniani vilivyotolewa na FIFA siku za hivi karibuni.


Hivi karibuni, timu ya Taifa Stars kutoka Tanzania imekuwa ikicheza katika kiwango kizuri ambapo iliwashinda DR Congo katika mchezo wa kirafiki kwa mujibu wa ratiba za FIFA.

Katika viwango hivyo vipya vya mwezi Aprili, Germany imeendelea kushika usukani wa dunia huku Brazil ikiwa nafasi ya pili na Ubelgiji imefanikiwa kupanda nafasi mbili juu na kufikia nafasi ya tatu.

Katika 'top ten' mataifa yanayofuata ni Ureno, Argentina,Uswiss, Ufaransa, Hispania, Chile na Poland inakamata nafasi ya 10.

Barani Afrika Tunisia inaongoza ikiwa nafasi ya 14 ikifuatiwa na Senegal katika nafasi ya 28, Congo DR nafasi ya 38, Morocco nafasi ya 42, Nigeria nafasi ya 47, Cameroon nafasi ya 51, huku Burkina Faso akiangukia nafasi ya 53.

Kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Uganda imepanda juu nafasi nne mpaka kufikia 74, ikifuatiwa na Kenya ikiwa imeporomoka kwa nafasi 8 hadi kufikia 113, Rwanda nayo ikiporomoka kwa nafasi 11 hadi kufikia 123, Tanzania ikiwa imepanda nafasi 9 hadi kufikia 137, Ethiopia ikiporomoka kwa nafasi 8 mpaka kufikia 145 huku Burundi ikidondoka kwa nafasi 3 na kufikia 145.

Wengine ni Djibouti ambayo iko nafasi ya 198 huku Eritrea na Somalia zikiwa mkiani kabisa katika nafasi ya 206

Mkuu wa Mkoa Atoa onyo Sakata la Boti

$
0
0
Serikali imetoa boti yenye thamani ya zaidi ya shilingi billion nne ili kusaidia doria katika mwambao wa bahari mkoani Tanga lengo likiwa ni kukabiliana na uingizwaji wa bidhaa zinazopitishwa kwa njia ya magendo ili kukwepa kodi.

Akizungumza mara baada ya kuzindua boti hilo mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigela ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha kuwa boti hilo linafanya kazi kwa saa 24.

Mhe. Martine Shigela amesema kuwa kwa sasa wafanyabiashara wa magendo wasifikiri tena kuna njia katika pwani ya bahari Hindi hivyo ameagiza meli hiyo ifanye kazi ipasavyo.

Kwa upande wake meneja wa bandari mkoa wa Tanga Percival Salama amesema uboreshaji wa Bandari hiyo unaoendelea ambapo mpaka sasa ujenzi wa gati namba mbili unaoendelea bandarini hapo umefikia karibu asilimia 70 wa wanatarajia ifikapo mwezi wa sita itakua imekalika.

Okoa Ndoa yako Sasa...Umepungukiwa na Nguvu za Kiume na Unashindwa Kupanda Mlima Vizuri

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA : JE UMEPUNGUKIWA NA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO AU MPENZI WAKO HAKUTIMIZII UTAKACHO:


Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sababu ya kutokuwa na nguvu za kiume au Uume wako mdogo

Dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa Kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA MWENZI WAKO BADO AJAKOJOA

KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA

UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE

KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

Dawa hii utumiwa ata na wazee wenye umri mkubwa na haina madhara yoyote

MAKAKANUA HII NI dawa ya maumbili madogo urefusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5 kwa mini huabiki kwa kuwa na UUME mdogo wai sasa upate tiba sahihi kabisa na ni tofauti na ulizowai kutumia :

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba dawa za uzazi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA p

Piga simu 0743362017 au 0789234653

DR AGU

“Mawaziri Hawa Wamevunja Sheria, Wachukuliwe hatua” –Zitto Kabwe (+video)

$
0
0
Ikiwa zimepita siku kadhaa tangu mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali  (CAG) Profesa Mussa Assad  kutoa taarifa ya mwaka ambayo iliibua mambo mbalimbali na baadae baadhi ya Mawaziri kuonekana wakiitasha mikutano na Waandishi wa habari kwa ajili ya kutolea ufafanuzi wa hoja za CAG Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe ametoa onyo kwa wahusika.

“Zoezi linaloendelea hivi sasa kwa baadhi ya Mawaziri kutoa majibu ya hoja za CAG ni kinyume cha sheria , Sheria ya ukaguzi wa umma kifungu cha  38 (1), (2) kinaeleza utaratibu wa namna ambavyo hoja za ukaguzi zinapaswa kujibiwa na Mawaziri hawatajwi kabisa katika kifungu hicho” –Zitto Kabwe

“Wanaopaswa kujibu ni Makatibu wakuu wa Wizara na sio kujibu kwa kuita mikutano na Waandishi wa habari, hiki kinachofanyika na Mawaziri ni kinyume cha sheria na sheria imeweka adhabu kwa makosa hayo ambapo adhabu yake ni kifungo cha miaka miwili jela au faini ya Shilingi Milioni tano” –Zitto Kabwe VIDEO:

Muhubiri Dar afunguka kutoza malipo kwa kila anaetaka kuombewa na yeye

$
0
0
Prophet Nicolaus Suguye wa Kanisa la WRM Kivule Dar es salaam amefunguka kuhusu taarifa za yeye kulazimisha kila Mtu anaetaka kuombewa na yeye kulipia maombezi hayo kwa lazima kanisani kwake Kivule Dar es salaam.

Phrophet Suguye ameongea na millardayo.com na AyoTV na kusema kilichotokea ni kwamba aliomba Watu wanaokwenda kuombewa nae kuchangia pesa kwa ajili ya kuanzisha TV ya kanisa iitwayo WRM ambayo inapatikana STARTIMES na kwenye AzamTV, hivyo hakulazimisha.

“Nilisema wale wanaotaka kuja kuombewa kwenye ibada kanisani iliku bure kabisa lakini kwa waliotaka kuniona wenyewe ofisini kwangu ndio nilisema wachangie TV, hata hivyo hakuna tena huo utaratibu wa kuchangia TV, hiyo laana ya kutoza watu pesa kwa maombezi sina” – Nicolaus Suguye

Yanga imemtangaza Atakaekaimu Nafasi ya Lwandamina

$
0
0
Uongozi wa Yanga umemtangaza atakaekaimu nafasi ya kocha mkuu iliyoachwa wazi na George Lwandamina ambaye katikati ya juma hili alirejea kwao na kuijiunga na klabu yake ya zamani ZESCO united.

Katibu Mkuu wa Yanga Charles Boniface Mkwasa amesema kuwa uongozi wa Yanga umemwandika barua George Lwandamina kumuomba ajiunge na timu Ethiopia ambapo itakuwa ikicheza mchezo wa marudiano dhidi ya Wolaitta Dicha kuwania kufuzu hatua ya makundi ya kombe la shirikisho Afrika.

“Ambaye alikuwa kocha msaidizi Noel Mwandila amekuwa kaimu kocha mkuu kwa sababu mwalimu hayupo na timu haiwezi kuwa bila kocha mkuu kwa hiyo mkuu wa benchi la ufundi kwa sasa atakuwa Noel Mwandila akisaidiwa na Shadrack Nsajigwa.”

“Tumejaribu kumjibu barua ya kujiuzulu lakini pia tumemwandikia kwamba bado tuna nia nae na akaungane na timu Ethiopia lakini bado hatujapata majibu na hatujajua ni kwa sababu gani lakini tumejitahidi hatujapata jibu sahihi.”

“Aliwasilisha barua ya kujiuzulu lakini barua lazima ikubaliwe, sisi tukajibu kwa sababu klabu bado ilikuwa na nia na huduma yake na ilikuwa imebaki miezi mitatu ni bora angemalizia lakini sasa kama masuala ya kutokujibu ni ya kwake. “

Mkwasa pia amekanusha taarifa kwamba yeye atarejea kwenye benchi la timu hiyo baada ya kuondoka kwa George Lwandamina.

Juma Abdul ametaja kinachokwamisha wachezaji wa Tanzania kwenda Ulaya

$
0
0
Ndoto ya wachezaji wengi ni kucheza Simba na Yanga na baada ya hapo ndipo inaanza mipango ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi. Juma Abdul ameshacheza nchini kwa kiwango cha juu akiwa na klabu ya Yanga na kufanikiwa kuchaguliwa mchezaji bora wa ligi kuu Tnzania bara.

“Nawaza sana kuchezaja nje ya Tanzania na sio mimi pekeyangu, kuna wachezaji wengi ambao wana vipaji vya kucheza nje lakini changamoto imekuwa nafasi au mawakala wetu kuwachukuwa wachezaji kuwapeleka sehemu wafanye majaribio kuona kama wanaweza kufanikiwa. Wachezaji wenzetu wa Afrika Magharibi wanaamini kile wanachokiamini mchezaji anaweza kuwa hana hata kipaji lakini anaamini nikifika sehemu fulani nikifanya kazi nitafanikiwa”-Juma Abdul wakati anazungumza na Yahaya Mohamed ‘Mkazuzu’.

“Kinachotukwamisha sisi waliotutangulia mwanzo kabisa hawakuweka njia nzuri mimi naamini hata Nigeria sasa hivi wachezaji wengi wanatoka kwenda kucheza Ulaya siyo kwamba ni wachezaji hatari lakini ni njia ambayo imewekwa na waliowatangulia kwa hiyo sasa hivi ni rahisi kwa wakala kwenda Nigeria kuangalia wachezaji na akifika kweli anakutana nao ambao anajua wakifundishwa baadhi ya vitu wanakuwa wachezaji wazuri.”

“Tunachokosa sisi ni watu wa kutushika mkono kutupeleka sehemu fulani lakini  kwa mfano akipatikana mtu akaamua kunishika mkono mimi, Hassan Kessy, Shomari Kapombe au Ibrahim Ajib naamini tunaweza kufanikiwa. Mfano mzuri ni Msuva sio kwamba ile timu ilimuona lakini kuna mtu alimwambia nakupeleka sehemu fulani naamini utafanikiwa kweli Msuva kafanya kazi amefanikiwa.”

Ameongelea pia kuhusu watu wakahoji kwamba Juma Abdul amecheza pamoja na Msuva katika klabu Yanga je amewahi kuzungumza na Msuva ambaye kwa sasa anacheza Morocco ili kuona ni kwa namna gani anaweza akamsaidia?

“Huwezi kusema sasa hivi Msuva anaweza kutusaidia sisi kwa sababu yeye mwenyewe bado anatafuta njia ya kufika sehemu, kwa mfano Samatta ametoka Tanzania akaenda Congo leo yupo Ubelgiji ni rahisi Samatta kuzungumza na watu wa Mazembe kuwambia kuna kijana mzuri yupo sehemu fulani mfuatilieni anaweza kuwasaidia hizo ndiyo nja ambazo mchezaji anaweza kuwasaidia wengine lakini sio yeye ndio kwanza anajenga jina lake aanze kusaidia wengine.”

Zari Amtukana Diamond Kwa Kushindwa Kuwajali Watoto

$
0
0
Aliyekuwa mpenzi wa Diamond Platinumz ambaye ni mama wa watoto wawili wa msanii huyo, Zari The Boss Lady ameshindwa kuficha hasira zake na kumshambulia kwa matusi mtandaoni.

Mashambulizi ya Zari aliyoyatoa kupitia snapchat, muda mfupi kabla hajaelekea kanisani yalionekana yakihusishwa na ujumbe ambao Diamond aliuandika kwenye Instagram kuhusu wanawake akipigia debe tukio linalofywa leo na Zamaradi Mketema.

“Ikiwa Mama yangu alinilea Pekee hadi kufika hapa…Naamini Mwanamke ni Kiongozi bora Mwenye kuweza kuleta Maendeleo na Furaha ya Kweli Ulimwenguni….Please Tag wanake wote Wapambanaji na Wapenda Maendeleo waambie @zamaradimketemaKawaandalia jambo Kesho [leo],” aliandika Diamond.

Dakika chache baadaye, Zari aliweka ujumbe wake uliojaa hasira akitumia maneno makali na kumuita Diamond ‘mjinga’. Ingawa hakumtaja jina, kitendo cha kumkosoa kwa kushindwa kuwaona watoto wake kwa muda mrefu kinaonesha kuwa anayezungumziwa ni baba Tifah.
Baadaye, Zari aliweka picha inayomuonesha akiwa mbele ya kioo na nguo nyingi na kuandika ujumbe kuwa ni muda wa kanisani.

Mkurugenzi Halmashauri ya Kongwa afariki dunia
Mange Kimambi kuwaburuza mahakamani ndugu zake
“Some manages need to do quality assurance  before their artist alter nonsense for public whatever… when last did you see your kids I believe they forgot all about you dummy… Think before you caption. Idiot. Mxuiiii,” aliandika.

Kwa tafsiri isiyo rasmi, “Mameneja wengine wanapaswa kuhakikisha ubora kabla wasanii wao hawajaweka upuuzi kwenye mitandao ya kijamii kwa kupata kiki kivyovyote… hivi ni lini mara ya mwisho umewaona wanao.. Nina amini wamesahau yote kuhusu wewe mpuuzi…. fikiria kabla ya kuandika kwenye picha. Mjinga.”

Zari alitangaza kuachana na Diamond, akaiachia rasmi funguo za ikulu ya WCB ya Madale na kuhamia nchini Afrika Kusini.

Rais Mpya Fatuma Karume Atangaza Mikakati yake TLS

$
0
0
Rais mpya wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), Fatma Karume aliyechaguliwa kwa kishindo wikendi hii, amesema katika kipindi chake atahakikisha anashughulikia zaidi suala la utawala wa sheria.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, muda mfupi baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo akipokea kijiti kutoka kwa Tundu Lissu, Fatma amesema kuwa moja kati ya suala linalolalamikiwa na wanachama wengi ni watu kushikiliwa mahabusu kwa muda mrefu bila kupelekwa mahakamani.

“Wanachama wetu wametaka tushughulikie suala la watu kushikiliwa kwa miaka mingi bila kupelekwa mahakamani. DPP anasema bado upelelezi haujakamilika. Sasa wanataka watu wasiendelee kushikiliwa kama upelelezi bado haujakamilika au wafikishwe mahakamani,” alisema.

Akizungumzia tathmini yake kwa mtangulizi wake, alisema alifanya kazi nzuri katika kipindi kifupi alichokuwa ofisini lakini pia hata baada ya kupata matatizo makamu wake aliendelea kufanya kazi nzuri pia.

Fatma ameahidi kutumia nafasi hiyo kuhuisha utawala wa sheria nchini na kuepuka baadhi ya viongozi kufanya kazi kwa kufuata matamko kinyume cha matakwa ya katiba.

Mwanasiasa huyo alipigiwa kura 820 akimuacha kwa mbali Ngwilimi aliyemfuatia akipata kura 363, Mwapongo kura 12 na Wasonga akipata kura 6 kati ya kura 1,195 zilizopigwa na kuhesabiwa. Kipindi chake cha urais kitakamilika baada ya mwaka mmoja.

Makonda Kula Sahani Moja na Vigogo Waliogoma Kupima DNA....."Tusijaribiane, Mimi sio Mtoto Wenu"

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa atahakikisha anawashughulikia kwa mujibu wa sheria na mamlaka aliyonayo, wanaume wanaokataa kuitikia wito wa kufika katika ofisi zake kujibu tuhuma za kutelekeza watoto na kupima vina saba (DNA).

Akizungumza kupitia TBC1, Makonda amesema kuwa wanaokataa wito huo wakidhani kuwa hadhi yao ni muhimu zaidi wanapaswa kufikiria tena kwani bahati nzuri watu hao  wanamfahamu hata kabla hajawa mkuu wa mkoa.

“Yoyote anayekaidi wito wa Ustawi wa Jamii ambao wako chini yangu, achilia mbali kwamba anakuwa amefanya kosa kwa mujibu wa sheria, kwa mamlaka tu niliyonayo mimi nakutia ndani,” alisema.

“Yaani na bahati mbaya niwaambie tu Watanzania, kwangu sheria ina nafasi kubwa sana kuliko hadhi unayojitengenezea ambayo kimsingi huna kama umeamua kutelekeza mtoto. Tusijaribiane,” aliongeza.

Mkuu huyo wa mkoa alieleza kuwa anayetunisha misuli ya kutoitikia wito anapaswa kufikiria kuwa kama anaweza kumuondoa mtu kwenye mkoa huo anapoona anahatarisha usalama na kuvunja amani, itakuwaje kwa hilo la mtu kumtelekeza mtoto.

Alisema kuwa awali, wanasiasa waliokuwa wanajinasibu kuwa hawahusiki na kinachoendelea na kwamba ni mpango wa kuchafuana kisiasa wameanza kuwa wapole baada ya kuona mama na watoto waliowatelekeza wakijitokeza na kuzungumza hadharani.

Akizungumzia hatua anazoweza kuwachukulia watu hao, Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa baada ya Ustawi wa Jamii na dawati la wanawake la Polisi kukamilisha kazi ya kuwaita wanaolalamikiwa kukamilika, watampa ripoti ya walioitikia wito na waliokataa pamoja na hatua walizofikia na ndipo waliokaidi watajua wigo wa mamlaka yake.

“Nikiambiwa haya mashauri yamebaki hayajashughulikiwa kwa sababu walioitwa wamegoma kuja… sasa hapo ndipo utaelewa Makonda ni Mkuu wa Mkoa, mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama au  ni mtoto wako unayeweza kumuendesha kama unavyoweza kuchezea sharubu za Simba aliyelala,” alisema.

Miongoni mwa watu maarufu wanaotakiwa kufika katika ofisi za mkuu huyo wa mkoa ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ambaye analalamikiwa na mwanamke mwenye umri wa miaka 31 kuwa ni mtoto wake aliyemtelekeza. Mama mzazi wa mtoto huyo pia alifika katika ofisi hizo na kueleza kuwa anachosema mwanaye ni kweli kwamba baba yake ni mzee Lowassa.

Mwingine aliyeguswa na sakata hilo ni mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa ambaye naye amekataa kufika ofisi za mkuu wa mkoa na kumtaka mwanamke anayedai kuwa alizaa naye na kumtekeleza afike katika ofisi za bunge ataonana naye.

Msigwa alisema kuwa endapo itathibitika kuwa ni mwanaye yuko tayari kuacha ubunge.

Mama Atiwa Mbaroni Kwa Kumuua Mtoto Wake Kisa Kala Chakula cha Mdogo wake

$
0
0
Polisi wamemkamata mwanamke wa kijiji cha Sokoni wilayani Tarime, kwa kumuua mtoto wake wa miaka minane kwa kumpiga na mwiko.

Kamanda wa polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe alisema tukio hilo lilitokea Machi 25 .

Mwaibambe alisema chanzo ni baada ya mtoto Debora Jomo kula chakula ambacho mama yake alikiandaa kwa ajili ya kula mdogo wake ambaye ni mgonjwa.

Alisema mtoto huyo alifariki dunia Machi 26 saa 11:00 asubuhi kutokana na kutopelekwa hospitalini.

‘’Inasikitisha sana kuona mama anaua mtoto wake tena wa kumzaa mwenyewe, mtoto alitoka shuleni akakuta chakula alikuwa na njaa na alijua aliachiwa akala,” alisema.

Naye diwani wa Sirari, Paul Nyangoko aliwataka wazazi kuangalia adhabu za kuwapa watoto kwa kuwa vipigo vikali vinaathiri afya ya mtoto na kumsabaibishia kifo.

Alisema kwenye kata yake hakuna njaa na debe la mahindi linauzwa kwa Sh7,000.

Mange Kimamhi Akerwa na Kitendo cha Mdogo wake kwenda kwq RC Makonda

$
0
0
Kufuatia mdogo wake Mange Kimambi kufika Ofisini kwa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa ajili ya kusuluhisha mgogoro wake wa kutelekeza mtoto Mange amesema kuwa hajafurahishwa na kitendo hicho.

Amesema kuwa amechukizwa na kitendo hicho cha mdogo wake kufika ofisini kwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda, ambapo ameandika kwenye ukurasa wake Instagram ataifufua kesi ya mirathi iliyoamuliwa mwaka 2016.

Aidha, katika hatua nyingine Mange ameituhumu familia yake kwa kuuza machimbo ya urithi ya kokoto kwa bei ndogo yaliyopo Tegeta jijini Dar es salaam bila kupewa taarifa wala kutumiwa mgao wake.

“Nilikuwa tayari niishi vibaya ila nyinyi muishi vizuri ndio maana sikuwasumbua na mali za baba yetu, Mgao wangu wa machimbo ya kokoto mliyouza muanze kunitafutia. Mlidhani sijui? Kweli mnadhani sijapewa habari za nyinyi kuuza machimbo yetu ya kokoto? Nilikuwa najua Ila niliamuwa kukaa kimya sababu nawapenda na bila nyinyi kwenye maisha yangu nahisigi siwezi kuishi ila labda nahitaji kujifunza kuishi bila nyinyi,”ameandika Mange kwenye ukurasa wake wa Instagram

Hata hivyo, amesema kuwa mpaka sasa hajachukua chake kwani hadi leo ni miaka 12 sasa imepita tangu jaji awagawanye mali za urithi

Mwanamke Aliyedai Lowassa ni Baba Yake Amemtelekeza Aomba Radhi

$
0
0
Mwanamke Aliyedai  Lowassa ni Baba Yake Amemtelekeza Aomba Radhi
MWANAMKE Fatuma ambaye video yake ilisambaa katika mitandao ya kijamii ikimwonyesha akidai kwamba amekuwa akimtafuta baba yake tangu akiwa darasa la sita, amemwomba radhi Waziri Mstaafu, Edward Lowassa kwa kumdhalilisha.

Fatuma amesema hakutegemea kama ingekuwa hivyo ilivyotokea na kwamba, jambo hilo linamnyima amani. Pia ameiomba radhi familia ya mwanasiasa huyo na Watanzania kwa ujumla kutokana na kitendo hicho.

SOMA PIA: Nafasi za Ajira Serikalini Zilizotangazwa Leo

Monalisa, Ray Wapeperusha Vizuri Bendera Wanyakua Tuzo Ghana

$
0
0
Monalisa, Ray Wapeperusha Vizuri Bendera Wanyakua Tuzo GhanaMuigizaji wa filamu nchini Tanzania, Yvonne Cherry maarufu kwa jina la Monalisa ameshinda tuzo ya The African Prestigious Awards (APA) 2017 kwenye kipengele cha Msanii Bora wa Kike barani Afrika.

Tuzo hizo zilizotolewa usiku wa kuamkia leo mjini Accra nchini Ghana ambapo waigizaji wengine kama Ray na Mzee Majuto nao walikuwa nominated kwenye tuzo hizo, ambapo Ray Kigosi pia ameshinda tuzo ya muigizaji bora wa kiume barani Afrika.

Kwa upande mwingine, Mtanzania Moise Hussein ameshinda tuzo hizo kwenye kipengele cha mpiga picha bora barani Afrika kwa mwaka 2017.

Dogo Janja Awapa Makavu Wasanii Wenzake "Wasanii Sisi ni Ma-snichi Sana Aise"

$
0
0
Dogo Janja Awapa Makavu Wasanii Wenzake "Wasanii Sisi ni Ma-snichi Sana Aise"
Ikiwa zimepita takribani siku mbili tokea mrembo Nandy kuomba radhi kutokana na video yake ya faragha ku
sambaa mitandaoni, msanii Dogo Janja ameibuka na kudai wasanii hawana umoja na wanafiki huwa wanafurahi sa
na kuona mwenzao amepatwa na majanga ili mradi apotee katika tasnia.
Dogo Janja ametoa kauli hiyo usiku wa kuamkia leo Aprili 15, 2018 kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii na kusema anahisi anaweza kuchukiwa leo hii na wasanii wenzake ila ni lazima yeye aongee ukweli ili mradi donda ndugu liliopo katika muziki limepone.

"Wasanii sisi ni ma-snichi sana aise, baada ya hii ishu ya Nandy ndio nimepata uhakika. Wakati wa ishu ya Roma nilianza kuliona jinsi kwenye makundi pembeni watu kibao walikuwa wanafurahi tena maneno kibao kama atakoma, amezoea huyo. Jana na juzi nimekaa na watu wasanii wakubwa tu na wote walikuwa wanasema bora limemtokea Nandy hili angalau spidi za 'show' zitapungua", amesema Dogo Janja.

Pamoja na hayo, Dogo Janja ameendelea kwa kusema "bora BASATA ingemfungia miezi 6 apotee kidogo, walikuwa wanapiga stori kama utani ila moyoni nimefikiria sana. Wasanii tuache roho mbaya, wote sisi masikini tunahangaikia ugali. Tukipata ajali kazini, tusiombeane mabaya tutafute amani".

Kwa upande mwingine, Dogo Janja amewashauri wasanii wenzake wawe na moyo wa upendo kwa wenzao na waache tabia ya kufurahia matatizo wanayowapata wakiwa kazini.

Marekani Yaionya Syria: Tutawashambulia Tena

$
0
0
Marekani yaionya Syria: Tutawashambulia tena
Rais wa Marekani Donald Trump ameiambia serikali ya Syria akisema Marekani iko tayari kuishambulia tena ikiwa itafanya shambulizi lingine la kemikali.
Onyo hilo lilikuja bada ya Marekani, Uingereza ba Ufaransa kushambulia vituo vitatu kujibu shambulizi linaloshukiwa kuwa la kememikali kwenye mji wa Douma wiki moja iliyopita.
Syria inakana kufanya shaambulizi lolote la kemikali na badala yake inasema kuwa lilifanywa na waasi.
Kura iliyoletwa na Urusi kwa Baraza la usalama la Umoja wa Mataiafa, kulaani mashambulizi yaliyoongoznwa na Matekani ilikataliwa.
Mashambulizi hayo ndiyo makubwa zaidi dhidi ya serikali ya Rais Bashar al-Assad, yaliyofanywa na nchi za magharibi katika kipindi cha miaka saba nchi hiyo imekuwa kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Marekani, Uingereza na Ufaransa wamewapa azimio jipya wanachama wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, wakitaka kufanya uchunguzi huru kuhusu matumaini ya silaha za kemikali nchini Syria.
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amelaumu ukosefu wa ushirikiano kutoka Urusi kwa kuchagua kufanya mashambulizi ya kijeshi akisema hawakuwa na njia nyingine.

Kauli ya Tundu Lissu Baada ya Bi. Fatma Karume Kutangazwa Mshindi wa Urais wa TLS

$
0
0
Kauli ya Tundu Lissu baada ya Bi. Fatma Karume kutangazwa mshindi wa urais wa TLS
Jana Aprili 14, 2018 Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kilipata Rais mpya mteule Bi. Fatma Karume, Hatimaye Mhe. Tundu Lissu ambaye ndiye aliyemuachia kiti hicho ametoa pongezi kwa wana


Mhe. Lissu ambaye yupo hospitalini nchini Ubelgiji tangu mwezi Januari mwaka huu, amesema kuwa uchaguzi huo umethibitisha kuwa TLS ni chama ambacho kinaweza kujisimamia na kujiendesha bila kuingiliwa na mtu.
“Napenda kuwapongeza wanachama wote wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kwa kumchagua Bi. Fatma Karume kuwa Rais mpya wa TLS. Uchaguzi huu umethibitisha, kwa mara nyingine tena, umuhimu wa Chama cha kitaaluma cha mawakili kujisimamia na kujiendesha bila kuingiliwa,“ameeleza Tundu Lissu na kutoa pongezi kwa Bi. Fatma .
“Namtakia Rais Mteule Fatma Karume kila kheri katika kutelekeza majukumu yake mapya na muhimu katika kipindi hiki cha historia ya nchi yetu.“ameandika Mhe. Lissu kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Wakili Fatma Karume amechaguliwa kuwa Rais mpya wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) jana mjini Arusha kwa ushindi wa kura 820 akiwamwaga Godwin Ngwilimi kura 363, Godwin Mwapongo 12 na Godfrey Wasonga kura 6.

Mvua Zinazoendelea Kunyesha Zaleta Maafa Dar Yaua Saba

$
0
0
Mvua Zinazoendelea Kunyesha Zaleta Maafa Dar Yaua Saba Watu saba wamefariki dunia kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es salaam.
Kamanda
wa polisi kanda maalum jiini Dar es salaam Lazaro Mambosasa amethibitisha vifo hivyo, na kueleza kwamba mwili mmoja umekutwa ukielea kuelekea maeneo ya Jangwani jijini Dar es salaam.
Sambamba na hilo Kamanda Mambosasa amesema maeneo mengi jijini Dar es salaam yamejaa maji, na kuwataka watu kuwa makini wanapotumia barabara hasa sehemu zenye makorongo, na kuwaangalia zaidi watoto ambao wanapita mara kwa mara wakienda shule au wakiwa wanarudi kutoka shule.
“Watu wasijaribu maji, ukijaribu maji ujue utaondoka nayo, kwa hiyo watoto wetu wanapokwenda shuleni tuwasindikize, sehemu nyingi zenye makorongo kwa mfano kule Kinyerezi, kule Goba kule Makongo, zile shortcut zote maji yamejaa, watu wajiepushe kutumia njia hizo, watapoteza watoto wakiwa wanaenda au kutoka shule”, amesema Kamanda Mambosasa.
Jeshi la Polisi limesema litaendelea kutoa taarifa za sehemu mbali mbali kuhusu hali ya mvua, ambayo inaendelea kuathiri sehemu kubwa ya nchi.
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live




Latest Images