Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Download Hapa Application ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu

 Bonyeza Hapa Chini

==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>
  

Mkuchika ageuka mbogo Bungeni: "Mimi nitafanya kazi gani wewe ukiniamulia"

0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika amefunguka na kusema kuwa atawachukulia hatua watumishi wa serikali ambao wanazuia barua za watumishi wengine hasa walimu wanaotaka uhamisho zisimfikie yeye au Katibu au Waziri Mkuu.

Mkuchika amesema hayo bungeni na kudai kuwa yapo malalamiko ya baadhi ya walimu kushindwa kuhama kutokana na viongozi wao kuzuia barua zao zisifike kwake au viongozi wengine ambao wana mamlaka.

"Sasa naomba kulieleza bunge hili tukufu mwenye mamlaka ya kumkatalia uhamisho ni yule anaye andikiwa barua

"Wewe uliyeandikiwa pale kupitia kwa kiswahili sanifu kabisa, wakishasema kupitia kwa wewe si muamuzi wa mwisho, peleka barua kwa mwajiri ili mwajiri apate kuamua

"Mimi natembelea mikoani nimepata kupita mkoa mmoja naambiwa hii ofisi yetu haijapitishwa barua ya mtu kuhama hata moja, mimi nasema mimi ndiyo Waziri wa Utumishi wa Umma, nikimbaini kuna kiongozi wa utumishi anakataa kupitisha barua isinifikie mimi, isimfikie Katibu Mkuu Kilimo, isimfikie Waziri Mkuu nitamshughulikia mwa mujibu wa sheria na taratibu

"Nitafanya hivyo kwa sababu mtu huyo amejichukulia madaraka ambayo si yake,  hukuandikiwa wewe barua halafu wewe ndiye unaamua sasa mimi niliyejuu nitafanya kazi gani kama wewe unaniamulia" alihoji Mkuchika

Mbali na hilo Mkuchika amesema kuwa zoezi la kuajiri sasa linatarajiwa kuendelea baada ya zoezi la uhakiki wa vyeti feki kukaribia kukamilika na kusema serikali itaendelea na kutoa ajira mpya.

"Tutaendelea na ajira mpya kama nilivyosema 50,200 wa mwaka jana na mwaka ujao serikali imejipanga kuajiri 49,000" alisema Mkuchika

Mkuchika: Kazi ya usalama wa taifa si kufuatilia wahalifu wala Kukamata watu

0
0
Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema kazi kubwa ya usalama wa taifa ni kukusanya habari na kuishauri serikali na wala si kukamata watu kwa mabavu.

Mkuchika ameyasema hayo jana Aprili 16 bungeni wakati akijibu hoja za wabunge waliochangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

“Naomba nichukue nafasi hii kufafanua sheria ya usalama wa taifa inasema nini, usipojua kazi za idara ya usalama wa taifa, utawapa lawama kwa kazi ambazo si zao,” alisema.

Alisema idara hii hutekeleza majukumu kulingana na sheria ya usalama wa taifa namba 15 ya mwaka 1996 na sheria hiyo katika kifungu cha nne, inasema kazi yake ni kukusanya, kuchambua na kuishauri serikali hatua za kuchukua.

Alisema ameamua kulisema hilo kwa kuwa wabunge wengi wamezungumzia kuhusu watu wa idara ya usalama kukamata watu ovyo na kwa kutumia mabavu.

“Pili haitakuwa kazi ya idara ya usalama, kumfuatilia fuatilia mhalifu. Nimeona niiseme hiyo kwa sababu mazungumzo mengi yameelekeza huko, mtu ameuawa ni ‘polisi kesi’, hakuna nchi ambayo idara ya usalama ina shughuli ya kukamata watu,” alisema.

Alisema:  “Kama mnataka usalama wa taifa wafanye kazi ya kukamata watu basi walilete suala hilo bungeni.”

Punguza Unene Unaokusumbua Katika Mwili Kwa Kutumia Bidhaa za Edmark

0
0
Ni Vurutubisho na Chakula Mbadala na Zimehakikiwa na TFDA...

Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini, Mafuta Sehemu Mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbalimbali kwa msaada wako mfuate instagram: @afyayanguutajiriwangu @afyayanguutajiriwangu


Au Mtafute WhatsApp Huyu Dada kwa kutumia Namba +255783 566844

Pia Dawa za Edmark Zinaweza kupa Fursa ya Biashara Uweze pata Kipato Kirahisi kwa Kuwasaidia watu Kuimarisha Afya zao

Simba Waendelea Kutoa Dozi Okwi, Bocco Wazidi kung'aa

0
0
Simba Waendelea Kutoa Dozi Okwi, Bocco Wazidi kung'aa
Vinara wawili wa mabao kwenye ligi kuu soka Tanzania Bara ambao pia ni washambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi na John Bocco wamefunga mabao mawili leo na kuipa ushindi Simba dhidi ya Tanzania Prisons.


Simba wameendelea kuhifadhi mwendelezo wao wa kutopoteza mchezo kwenye ligi msimu huu baada ya kuiadhibu Prison mabao 2-0 kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam jioni hii.

Mabao ya Simba yamefungwa na John Bocco dakika ya 35 ambaye sasa amefikisha mabao 14 msimu huu huku bao la pili likifungwa na Emmanuel Okwi kwa njia ya penati dakika ya 80 na kumfanya sasa afikishe mabao 19.

Baada ya ushindi wa leo Simba sasa imefikisha alama 58 katika michezo 24 ya ligi msimu huu hivyo kuendelea kujikita kileleni ikiwakimbia wapinzani wao Yanga ambao wapo katika nafasi ya pili wakiwa na alama 47.

Simba iko mbele ya Yanga kwa michezo miwili ambapo Yanga inayowakilisha taifa kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho imecheza mechi 22 pekee hivyo ikishinda viporo vyake inaweza kufikisha alama 53.

Takukuru Kuwafikisha Mahakamani Viongozi kwa Ubadhirifu wa Bilioni 2

0
0
Takukuru Kuwafikisha Mahakamani Viongozi kwa Ubadhirifu wa Bilioni 2
Leo April 17, 2018 Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) iko katika hatua za mwisho kukamilisha upelelezi wa tuhuma za ubadhirifu wa zaidi ya shilingi Bilioni mbili zinazowakabili viongozi wa kiwanda cha kukoboa Kahawa cha mkoani Kilimanjaro.

Viongozi kadhaa wa kiwanda hicho kinachomilikiwa na Vyama vya Ushirika katika Kanda ya Kaskazini wanatuhumiwa kuuza nyumba za ushirika kisha kununua mtambo feki wa kukoboa Kahawa ambao haujafanya kazi tangu ununuliwe miaka minne sasa.

Kaimu Kamanda wa TAKUKURU mkoani Kilimanjaro, Moses Oguda amewaambia waandishi wa habari kuwa baadhi ya majalada ya kesi hiyo yamerejeshwa kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini kwa ajili ya utekelezaji.

TAKUKURU pia imepokea taarifa za rushwa zipatazo kumi na tano na kuzifanyia kazi, nyingi kati ya hizo zikiwa ni kutoka idara za Elimu, serikali za mitaa, polisi na Mahakama.

Monalisa Kuipeleka Tuzo ya APA Bungeni Leo

0
0
Monalisa Kuipeleka Tuzo ya APA Bungeni Leo
Siku mbili baada ya msanii Yvonne Cherrie ‘Monalisa’, kuibuka msanii bora wa kike katika tuzo za African Prestigious Awards (APA), anatarajia kuipeleka tuzo hiyo Bungeni leo.

Utoaji wa tuzo hizo ulifanyika Aprili 14, mwaka huu Accra, nchini Ghana, ambapo lengo lake ni kutambua maendeleo na tija aliyonayo mtu kwenye nyanja za uongozi, biashara, sanaa na kadhalika.

Taarifa kutoka kwa mama yake, Susan Lewis’Natasha’ zimeiambia MCL Digital leo kwamba baada ya msanii huyo kutua leo asubuhi, kesho anatarajiwa kwenda mjini Dodoma kwa mwaliko wa kuipeleka tuzo hiyo bungeni.

Kwa upande wake Monalisa kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram, amewashukuru watanzania kwa namna walivyoweza kumpigia kura.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Monalisa amesema” Tuzo ni ya kwenu, mmekuwa nami kwa zaidi ya miaka 19 ya kazi yangu ya Sanaa hamjaniacha mnaendelea kunifurahia nashukuru mno mno, ahsante kwa muda wako uliotumia kunipigia kura.

Katika kipengele hicho cha muigizaji bora wa Kike, Mona alikuwa akichuana na wasanii maarufu wa kimataifa akiwemo Lupita Nyong’o ambaye ni mwigizaji wa Hollywood mwenye asili ya Kenya na Jack Apia mwigizaji kutoka nchini Ghana.

Waigizaji wengine waliong’aa kwenye tuzo hizo mbali na Monalisa ni Vicent Kigosi’Ray’ aliyeshinda kipengele cha muigizaji bora wa kiume na Moise Hussein aliyeshinda kwenye kipengele cha mpiga picha bora barani Afrika kwa mwaka 2017.

Hata hivyo mchekeshaji maarufu, Omar Athuman’Mzee Majuto ‘aliyekuwa akiwania kipengele cha mchekeshaji bora bahati haikuwa yake.

Kutokana na ushindi huo, sasa Monalisa ndio mwigizaji bora wa kike Afrika kupitia tuzo hizo za (APA) mpaka hapo shindano hilo litakapofanyika tena.

Kuna Tatizo ya Namna Ambavyo Ripoti ya CAG Inavyoshughulikiwa- Zitto Kabwe

0
0
Kuna Tatizo ya Namna Ambavyo Ripoti ya CAG Inavyoshughulikiwa- Zitto Kabwe
Mjadala mkali unaendelea nchini Tanzania baada ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, CAG, Prof. Mussa Assad kutoa taarifa yake ya ukaguzi wa mapato na matumizi ya fedha za umma kwa mwaka 2016/17. Taarifa hiyo ilio wazi kwa umma, baada ya kukabidhiwa rasmi bungen imepokewa Kwa hisia tofauti huku baadhi wakihoji upotevu wa fedha za umma ambazo inasemekana huenda zimepotea.

Zitto Kabwe ambae ni mwanzilishi wa Chama cha ACT Wazalendo amezungumza na BBC kuhusu matokeo ya ripoti hiyo:

Wachunguzi wa Silaha za Kemikali Nchini Syria Waruhusiwa Kuzuru Eneo Lililoshambuliwa

0
0
Wachunguzi wa Silaha za Kemikali Nchini Syria Waruhusiwa Kuzuru Eneo Lililoshambuliwa
Wachunguzi wa silaha za kemikali nchini Syria wataruhusiwa kuzuru katika eneo linalodaiwa kushambuliwa na silaha za sumu siku ya Jumatano, kulingana na uUrusi.

Kundi hilo la kimataifa limekuwa nchini humo tangu siku ya Jumamosi lakini halijaruhusiwa kuingia Douma.

Shambulio hilo la siku ya Aprili 7 lilivutia shambulio dhidi ya serikali ya Syria lililotekelezwa kwa pamoja na Marekani, Uingereza na Ufaransa wiki moja baadaye.

Syria na mshirika wake Urusi wamekana shambulio lolote la kemikali huku Urusi ikitaja madai hayo kama 'yaliopangwa'.

Mapema siku ya Jumanne , chombo cha habari cha Syria kilisema kuwa ulinzi wa angani wa taifa hilo ulikabiliana na shambulio la makombora juu ya nga ya magharibi mwa mji wa Homs.

Makombora hayo yalilenga kambi za wanahewa wa Shayrat lakini haikusema ni nani aliyetekeleza mashambulio hayo.

Ripoti nyengine kutoka kwa wapiganaji wanaoungwa mkono na Iran-Hezbollah ilisema kuwa mtambo wa ulinzi wa angani ulitungua makombora matatu yaliolenga kambi ya wanahewa ya Dumair, kaskazini mashariki mwa mji mkuu wa Damascus.

Msemaji wa Pentangon aliambia Reuters : Hakuna shughuli za kijeshi za Marekani katika eneo hilo wakati huo.

Mapema siku ya Jumamosi saa za Syria, Marekani, Uingereza na Ufaransa zilitekeleza mashambulio ya pamoja katika maeneo tofauti nchini Syria.

Operesheni hiyo ilikuwa ikijibu shambulio la silaha za kemikali iliotekelezwa na serikali ya Syria na kulenga raia na kuwaua makumi ya watu.

Wachunguzi kutoka shirika la kuzuia utumizi wa silaha za kemikali OPCW wako katika mji mkuu wa Damascus , lakini wamekuwa wakisubiri kuanza uchunguzi.

Wakati watakapowasili katika eneo hilo siku ya Jumanne, itakuwa siku 11 tangu shambulio hilo.

Wanatarajiwa kuchukua mchanga na sampuli kusaidia kutambua kemikalizilizotumika katika shambulio hilo.

Mjumbe wa Marekani katika shirika la OPCW hatahivyo ameonyesha wasiwasi wake kwamba Urusi ilitembelea eneo hilo na huenda iliharibu ushahidi ili kuzuia uchunguzi.

Lakini katika mahojiano na BBC, waziri wa maswala ya kigeni nchini humo Sergei Lavrov alisema: Nawahakikishia kuwa Urusi haijaharibu ushahidi wowote katika eneo hilo.

Alisema kuwa ushahidi uliodaiwa na Marekani , Uingereza na Ufaransa ulitokana na habari za vyombo vya habari na mitandao ya kijamii na kwamba ushahidi kama huo ni kitu kilichapangwa.

Bwana Lavrov na wengine pia wamekosoa mataifa hayo matatu kwa kutekeleza mashambulio hayo kabla ya kundi la wachunguzi wa OPCW kufanya uchunguzi wao.

Wakati shambulio hilo lilipodaiwa kufanyika tarehe 7 Aprili, Douma, katika eneo la mashariki mwa Ghouta, lilikuwa eneo linalodhibitiwa na waasi karibu na mji mkuu wa Damascus baada ya mwezi mmoja wa mashambulio.

Kwa sasa mji huo uko chini ya udhibiti wa majeshi ya Syria na Urusi.

Mabomu mawili yaliokuwa na kemikali yalidaiwa kuangushwa saa kadhaa tofauti katika mji huo.

Ramani inayoonyesha eneo la shambulio la kemikali huko Douma, mashariki mwa Ghouta , Syria
Duru za kimatibabu nchini Syria zinasema kuwa miili kadhaa ilipatikana ikitoa mapovu mdomoni mbali na kuwa na ngozi iliokosa rangi na macho yaliochomeka.

Duru za Marekani zinasema kuwa zilipima sampuli za mikojo na damu kutoka kwa waathiriwa na kufanikiwa kupata kemikali ya khlorine na gesi ya neva.

Maafisa Watatu Tume ya Uchaguzi Kenya Wajiuzuru Kisa Hiki Hapa

0
0
Maafisa Watatu Tume ya Uchaguzi Kenya Wajiuzuru Kisa Hiki Hapa
Maafisa watatu wakuu wa tume ya uchaguzi nchini Kenya (IEBC) akiwemo naibu mwenyekiti wamejiuzulu wakidai kutokuwa na imani na mwenyekiti wa tume hiyo, Wafula Chebukati.

Makamishna hao wamedai kuwa bodi hiyo imeshindwa kutimiza wajibu na imeeingiliwa na watu wengine.

Wakihutubia wanahabari jijini Nairobi, makamishna hao Consolata Nkatha, Paul Kurgat na Margaret Mwachanya wamedai kuwa Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati ameshindwa kuiongoza tume hiyo na kudai kwamba tume hiyo imeingiliwa na watu kutoka nje wanaoshawishi jinsi inavyofanya kazi.

''Kwa muda murefu sasa, mwenyekiti ameshindwa kutoa muongozo wa utaratibu kwa wakati mgumu na anapohitajika kufanya hivo.

Katika taarifa yake hivi punde kwa waandishi wa habari, mwenyekiti wa tume hiyo ya IEBC - Wafula Chebukati amesema kwamba hakujakuwa na mawasiliano rasmi kuhusu kujiuzulu kwa makamishna hao watatu na kwamba amepata kusikia kuhusu taarifa hiyo kupitia vyombo vya habari nchini.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

0
0

Diamond Platnumz Amefikishwa Polisi Kisa Video Zisizo na Maadili

0
0

BUNGENI: Msanii Naseeb Abdul Maarufu kama Diamond Platnumz amefikishwa Polisi jana kuhojiwa kutokana na kusambaza kwa video zake zisizo na maadili katika mitandao ya kijamii

Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari, Michezo, Utamaduni na Sanaa Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa Bungeni wakati akijibu swali juu ya kanuni za maudhi ya Mitandaoni

Aidha, Dkt. Mwakyembe amesema Msanii Faustina Charles (Nandy) naye atahojiwa na Polisi kufuatia video yake ya faragha akiwa na Msanii mwenzake Billnass kusambaa mitandaoni

Vigogo Chadema Waomba Kesi Kuhamishiwa Mahakama Kuu

0
0
Vigogo Chadema Waomba Kesi Kuhamishiwa Mahakama Kuu
Leo April 17, 2018 Wabunge wa CHADEMA, wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, wamewasili katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Miongoni mwa waliofika mahakamani ni pamoja na Katibu Mkuu wa chama hicho, Vincent Mashinji, Esther Bulaya wa Bunda, Halima Mdee, Esther Mati, Naibu Katibu Mkuu bara, John Mnyika na Naibu Katibu Mkuu visiwani, Salum Mwalimu.

Mbowe, wenzake waomba kuhamia Mahakama Kuu wamefika mahakamai hapo kutokana na kesi inayowakabili namba 112 ya mwaka huu Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri ataongoza kesi hiyo huku Wakili wa Serikali Mkuu Faraja Nchimbi akijibu hoja zilizowasilishwa jana na Wakili wa utetezi Peter Kibatala.

Serikali ya DRC Yawafukuza Kazi Mahakimu 250

0
0
Serikali ya DRC Yawafukuza Kazi Mahakimu 250
Leo April 17, 2018 moja ya stori ya kuifahamu ni hii kutoka katika Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo imewafuta kazi Mahakimu 250 ambao hawana elimu ya sheria pamoja na wale ambao walikuwa wameshtumiwa kuwa mafisadi.

 Waziri wa Sheria Alexis Thambwe Mwamba amesema hatua hii imechukuliwa ili kuwazuia watu waliokuwa wanaingia katika idara ya Mahakama wakiwa na lengo la kujipatia fedha badala ya kuwatumikia raia wa nchi hiyo.
Hii sio mara ya kwanza kwa serikali ya Kinshasa kuwachukulia hatua maafisa wa juu wa idara ya Mahakama, Mwaka 2009, rais Joseph Kabila aliwafuta kazi Majaji 96 baada ya kubainika kuwa walikuwa wafisadi.

Hatua hii inakuja ikisalia miezi 7 ili kufanyike Uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Desemba 23 mwaka huu

Mvua Yaleta Maafa Mwanza....Watatu Wafariki Dunia kwa Kuangukiwa na Nyumba

0
0
Mvua Yaleta Maafa Mwanza....Watatu Wafariki Dunia kwa Kuangukiwa na Nyumba
Usiku wa kuamkia Aprili 9, watoto wawili wa familia moja, Mussa Baraka (2) na Mariam Simoni (4) walifariki dunia kwa  kuangukiwa na ukuta wa nyumba walimokuwa wamelala katika Mtaa wa Buguku eneo la Buhongwa jijini Mwanza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema watu watatu akiwamo mama mzazi wa watoto hao, Dabacha Simon; bibi yao, Linda Kulwa na kaka yao, Simon Samson (5) walijeruhiwa katika tukio hilo lililotokea saa nane usiku na kulazwa katika hospitali ya Wilaya ya Nyamagana ya Butimba.

Pia, Usiku wa kuamkia leo April 17, mtu mmoja amefariki dunia baada ya nyumba yake kubomoka na kuanguka kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

Tukio hilo limetokea Kata ya Kiseke mtaa wa Kabambo Wilaya ya Ilemela. Aliyefariki ametambulika kwa jina moja la  Laurent

Ray Afunguka Sababu ya Kutohudhuria Katika Tuzo za APA

0
0
Ray Afunguka Sababu ya Kutohudhuria Katika Tuzo za APA
Muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Ray Kigosi amefunguka sababu ya kutohudhuria katika utoaji wa tuzo za The African Prestigious Awards (APA) 2017.

Tuzo hizo zilizotolewa usiku wa kuamkia April 15, 2018 mjini Accra nchini Ghana, Ray na Monalisa waliibuka washindi kutoka Tanzania.

Ray Kigosi amesema alishindwa kuhudhuria utoaji wa tuzo hizo kutokana alikuwa safarini nje ya nchi.

“Sikufanikiwa kuhudhuria kwenye Awards hizo kwa sababu niko South Afrika kikazi sina cha kuwalipa ndugu zangu zaidi ya kuendelea kuwaletea Watanzania kazi nzuri zenye viwango boraili tuendelee kuiletea heshima nchi yetu,” amesema Ray Kigosi.

Soma Pia; Monalisa, Ray Kigosi washinda tuzo nchini Ghana

Katika tuzo hizo Ray Kigosi alishinda katika kipengele cha msanii Bora wa Kiume Afrika na Monalisa alishinda katika kipendele cha Msanii Bora wa Kike barani Afrika.

Viingilio Mechi ya Simba na Yanga Vyatajwa Hivi Hapa

0
0
Vingilio Mechi ya Simba na Yanga Hivi Hapa
Wakati homa ya pambano la watani wa jadi ikiendelea kushika kasi, tayari viingilio vya mchezo huo vimeshatajwa.

Selcom ambao ni waandaji wa tiketi za michezo ya ligi kuu, wametaja viingilio vya mchezo huo utakaopigwa Aprili 29 2018 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Viingilio hivyo ni Tshs 30,000 kwa VIP A, VIP B na C ni 20, 000 huku Mzunguko ikiwa ni 7000 tu.

Tayari Selcome wameshaanza kuuza tiketi hizo ambazo ni za mfumo wa kielektroniki.

Mwakyembe Awaonya Watumiaji wa Mitandao ya Kijamii

0
0
Mwakyembe Awaonya Watumiaji wa Mitandao ya Kijamii
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa wito kwa vijana wa Tanzania kutumia vizuri mitandao ya kijamii kwa faida yao binafsi na sio kupeleka uchafu ambao umezuiwa na sheria zingine.


Dkt. Mwakyembe ametoa kauli hiyo leo Aprili 17 Bungeni jijini Dodoma kwenye kikao cha 11 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akijibu swali la Mbunge Goodluck Mlinga alipoihoji serikali kuwa ina mpango gani wa kuwadhibiti watumiaji wa mitandao ya kijamii hususani 'instagram' kutokana kumekuwepo na vikundi vya 'timu Wema', 'timu Zari' na 'timu Shilole' n.k kuwa wanatoa lugha chafu za kutukana watu jambo ambalo linachangia upotoshaji wa maadili na utamaduni wa kitanzania.

"Tulitunga sheria ya EPOCA mwaka 2010 ilikosa kanuni za kubana maudhui hasa upande wa mitandao. Sasa tunazo hizo kanuni na zimeshaanza kufanya kazi. Naomba nitoe wito kwa vijana wote nchini, mitandao sio kokolo ya kupeleka uchafu wote ambao umezuiliwa na sheria zingine, hii nchi ina tamaduni zake. Tunahitaji kulinda kizazi cha leo, kesho na kesho kutwa cha taifa hili", amesema Dkt. Mwakyembe.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza amesema changamoto kubwa inayoikabili taifa la Tanzania ni athari ya utamaduni wa nje kwa maadili mila na desturi kupitia muingiliano mkubwa wa watu wa dunia kwa njia ya utalii, biashara n.k.

Kutana na Mtaalam Sharif Hamad Kalala Mchambuzi wa Nyota za Binadamu na Tiba Asili

0
0
KUTANA NA SHARIF HAMAD KALALA NI
SHARIFU MCHAMBUZI WA
NYOTA ZA BINAADAMU NA NI MWENYE UPEO MKUBWA KUTAFITI MATATIZO YAKO KABLA YA KUTOA USHAURI WAKE WA TIBA AlJALISHI MBALI ULIKO TIBA YAKE UMFIKIA YEYOTE MWENYE UITAJI POPOTE
DUNIANI.

 SHARIF HAMAD KALALA NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA QUR-AN, DAWA ZA ASILI ZA MITI SHAMBA PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.
ANATIBU KWA NJIA YA SIMU KWA KUTOA
MAELEKEZO NAMNA YA MATUMIZI YA DAWA UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-

 KUFANIKISHA NDOA KWA UNAYE MPENDA KWA HARAKA. KUMRUDISHA MPEZI NDANI YA MASAA 12 TU.
 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME) NDANI YA /IKI MMOJA TU
MIGUU KUWAKA MOTO KUTAFSIRI NDOTO MFARAKANO WA WANANDOA MFARAKANO KAZINIKUPANDISHWA CHEO NDANI YA SIKU SABA 7 TU.
KUTOA PETE YA BAHATI KUTOA MAJINI MACHAFU IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA. KUPATA MAFANIKIO YA MALI BILA YA MASHARTI. KUPANDIKIZANYOTA YA KUBASHIRI KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA KWENYE BIASHARA. ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE. ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA
KWA NJIA YAMSUKULE
NAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA MPYA NDANI SIKU 7 TU.
MENGINEYO MENGI ZAID YALIYO KUWA SUGU PIGA KWA WALE WALIYO ANGAIKA SEHEMU MBALI MBALI SHARIF HAMAD KALALA NI SULUISHO. ENDAPO UTAMSIKILIZA KWA YALE ATAKAYO KUSHAURI NA KUKUPA
ELEKEZI.
 TIBA NI KWA DINI ZOTE POPOTE ULIPO NJE NA NDANI YA NCHI.
MOBILE +255 -673 025 376
WhatsApp +255-757 069 066

Mimi si Shabiki wa WCB Bali Daimond- Wolper Afunguka

0
0
Mimi si Shabiki wa WCB Bali Daimond- Wolper
Msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper amefunguka kuhusu ukaribu wake na label ya WCB kwa sasa.

Wiki iliyopita moja ya mtandao uliripoti kuwa muigizaji huyo kaeleza kuwa yeye si shabiki wa WCB bali Diamond.

Wolper amesema hilo halina ukweli wowote na kueleza kuwa watu wanaoelewa ukaribu wake na WCB hawawezi kutilia maanani hilo.

“Mtu akiangalia kauli kama hiyo atashangaa mimi siyo shabiki wa WCB, how ?, mimi nilijibu kutokana na swali, kwa hiyo watu wenye akili zao hawezi kufuatilia hivyo vitu” Wolper ameiambia Bongo5.

Wolper aliwahi kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na muimbaji kutoka WCB, Harmonize ambaye pia alimshirikisha mrembo huyo katika video ya wimbo wake unaokwenda kwa jina la Niambie.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images