Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104423 articles
Browse latest View live

KWA PENZI HILI NADHANI NAKARIBIA KUNYOOSHA MIKONO JUU...PAPUCHA SIPEWI ILA NACHUNWA

0
0
Mhhhhhhhh! Kwa penzi hili nadhani karibu nanyoosha mikono juu!

Mhhhh! Baada ya kuwa mpweke kwa muda mrefu, uzalendo ulinishinda nikaamua angalau na mimi nitafute binti wa kuniliwaza. Mchakato huu ulianza kwa binti mmoja ambaye tulikutana kwenye dala dala tukitoka Posta kuelekea Mwenge. Nilivutiwa na mwonekano wa Binti huyu nikaamua niombe namba ya simu. 

Mungu si athumani alitoa namba bila hiyana! Kutokana na furaha ya kupewa namba sikuweza kuongea chochote siku hiyo kama mtu aliyewekewa matambala ya nguo mdomoni hadi muda wa kushuka Mwenge ambapo tuliagana tu na nikamuahidi kumtafuta. Kwa mwonekano, binti huyu ni mwembamba, ana baby face, mweupe wastani pia ni mrefu kidogo. Alikuwa na SmartPhone ya Nokia ambayo gharama yake nakisia sio chini ya Laki Tatu! 

Pia alikuwa amejitupia micheni siku hiyo, cjui ya madini gani mshamba mie. Msije Mkaniomba Picha! Sina. Tulianza mawasiliano ya hapa na pale huku nikijaribu kumuonesha kwamba najali. Urafiki wetu ulidumu kwa muda kama wa mwezi mmoja ndipo nilipoamua kumtamkia wazi kwamba ……………….! 

Katika urafiki wetu nilipata kujua kwamba binti yule alikuwa anasoma Procurement kwenye chuo Fulani hapa hapa Mjini. Nilizungushwa kukubaliwa ombi langu kwa muda kama wa mwezi mmoja. Sikukata tamaa kwa sababu nawajua watoto wa kike: Kwanza kukubali moja moja ni udhaifu na pia mapozi kwa mtoto wa kike ni ya muhimu kama ilivyo tendo la ndoa kwa walio oana. Baada ya kubembeleza sana ombi langu lilikubaliwa na nikawa rasmi mpenzi wa Fulani. 
Kukubaliwa huko kulileta Joto na Raha ndani ya moyo wangu! Kusema kweli nilifurahi wiki ya kwanza huku nikishindwa kujenga taswira kwenye ubongo wangu siku ya kugegedana itakuwaje?????????!!!!. Kitumbua kiliingia mchanga baada ya kuombwa Laki Moja ili aongezee kwenye ada alipe chuo. Nilijiuliza maswali mengi ambayo yalikuwa hayana majibu. - Kwanza kwa nini asimuombe mzazi wake. Mi sio mzazi!!!!! - Miaka yote nani alikuwa anamlipia ada? - Kama mimi nisingekuja kwenye maisha yake, nani angelipa hicho kiasi cha ada! Na mengine mengi. Labda wana MMU mnisaidie kumjibia. Nilitoa laki moja kwa shingo upande. Baada ya hapo nimekuwa mtu wa kupigiwa simu, mara dia sijala, mara dia naumwa naomba hela niende hospitali. 

Nimegeuzwa ----- mie kila siku natoa hela tu. Siku alipokuja kunichosha ni pale aliponiambia kwamba SmartPhone yake imetumbukia kwenye maji na imezima kabisa haitaki kuwaka kwa hiyo kwa sasa ameweka kadi ya simu kwenye simu ya mwenzake. Kama umesoma “Critical Thinking and Argumentation” inabidi uwe umeshatambua kwamba nilitakiwa kukununua SmartPhone nyingine labda ya gharama Zaidi kuliko ile aliyokuwa nayo mwanzo. 

Nikijiangalia mwenyewe natumia Nokia tena yenye tochi – gharama yake haizidi elfu hamsini. Hata hiyo SmartPhone sijui una-touch vipi kwa sababu nahisi siku nikipewa itanishinda kutumia. Nipo hapa hapa mjini ila mshamba haswa wa mambo hayo! Muda huu nilimwambia kwamba sina hela ya kumnunulia simu hiyo. Ila siku hizi huwa namkuta na Samsung Galaxy S3 Mini. Baada ya kumkatalia kumpa hela ya simu, kwa sasa tunaendelea na mizinga midogo midogo. 

Papuchi sijapewa hadi leo. Nikimwita Faragha nijibiwa “Akhu”- msamiati ambao nilikuwa sijawahi kuusikia kabla isipokuwa kwa huyu binti. Penzi letu limekuwa la kukutana pale Mwenge – New Jamarat na kunywa Juisi. Sijawahi hata kugusa kalio mie. Natamani kuachana nae ila roho inaniuma – hela zangu. 

Wana MMU naomba mnisaidie kwenye mazingira haya manake naweza nikafa mawazo– angalau nipewe papuchi tu na moyo wangu utapona.

RIDHIWANI KIKWETE ALIUMBUA GAZETI LAA TANZANIA DAIMA KWA KUANDIKA UONGO

0
0


"Nimesikitishwa sana na jinsi Gazeti la kaka yangu Mbowe (Tanzania Daima) la leo Disemba 20, 2013 lilivyotumia jina langu kutafuta mapato na labda kwa nia nyingine.

Gazeti hilo katika ukurasa wake wa kwanza na wanne linaripoti kwamba jana Disemba 19, 2013 nilikuwa mkoani Mwanza kumuwakilisha Mheshimiwa Rais!

Napenda jambo hili lifahamike na lieleweke:


Ukweli ni kwamba jana, Disemba 19, 2013 sikuwepo Mwanza na wala sikutoka nje ya wilaya ya Kinondoni

Ni imani yangu kuwa taarifa hii ilichapishwa makusudi. Ninaheshimu sana uhuru wa vyombo vya habari lakini kwa hili sasa mmezidisha.

Nakaribisha maoni yenu, kama taarifa kama hii isiyo sahihi na ya kupotosha ingechapishwa dhidi yako, ungechukua hatua gani?

Jumaa Kareem!

ALINIOMBA NIMPIGE PICHA AKIWA UCHI, NA HII SIO MARA YA KWANZA...SIMUELEWI

0
0
Sisi ni majirani tumetokea kuzoeana tu kidogo kwakuwa mwenzangu  yeye ni mwenyeji mimi nimemkuta tu hapo nilivyo hamia, lakini naona kama kuna mazoea fulani ya ajabu, hii ni mara ya tatu huyu dada ananiomba nimpige picha tena akiwa amevaa kiajabu ajabu, siku nyingine anadiriki hata kunigongea chumbani kwangu ili nitoke tu nimpige picha halafu aendelee na shughuli zake. sasa imekuwa kero Simuelewe kabisaaaa.

TAZAMA PICHA KIJANA HUYO AKINYONYANA NDIMI NA MAMA YAKE WA KUMZAA

0
0
SAWA anamkiss mama yake mzazi lakini hapa hatuelewielewi kinachoendelea? Busu hilo linatupa maswali mengi sana kichwani...!
Alafu cheki alichokiandika hapa chini, Mmh...?

TAZAMA JINSI MTOTO WA NANCY SUMARI ALIVYOKUWA MKUBWA NA ALIVYOPENDEZA KWENYE HII PICHA

0
0

Mtoto wa Nyoka ni Nyoka tuuu...Daaahhh Kazuri kama mama yake ....MMhh nani anabisha?

DAVIS TPF4 WINNER"WANAWAKE WA KENYA WALIMALIZA HELA ZANGU NILIZOSHINDA KABLA SIJARUDI KWETU"

0
0
Talented Ugandan singer, Davis, weathered the storm and clinched the Tusker Project Four season title amidst tight competition from his fellow contestants.

After clinching the title, he was awarded a whooping ksh 5 million among other goodies.
Speaking in a media interview, the Ugandan singer revealed that he squandered all the ksh 5 million in Nairobi even before going back to his country.

“I rented an apartment in Hurlingham and squandered all the money with Nairobi women.” he said.

The talented singer further blamed Nairobi’s fast life and cunning women in Kenya for squandering all his hard earned cash.

Rumour has it that Davis has gone totally broke and even lives with his parents. This is a lesson to TPF 6 winner Hope that he needs to go back to his country as soon as possible or else fall into the trap of cunning Nairobi women.


The Kenyan DAILY POST.

HII NDO KAULI YA MANJI BAADA YA KIPIGO CHA JANA TOKA KWA SIMBA CHA BAO 3-1

0
0
Mwenyekiti wa Yanga Bw.Yusuf Manji akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu, kushoto ni makamu mwenyekiti Clement SangaMwenyekiti wa klabu ya Young Africans Bw. Yusuf Manji ameaomba wanachama, wapenzi na washabiki wasivunjike moyo kwa matokeo ya jana ya mchezo wa kirafiki dhidi ya ya Simba SC, mechi iliyochezwa katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga makutano ya mitaa wa 
Twiga/Jangwani Manji amesema anajua wanachama, na wapenzi wameumia sana hakuna aliyefurahishwa na matokeo ya kufungwa mabao 3-1 lakini isiwakatishe tamaa uongozi unafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza.
"Mechi ya jana ilikuwa ni bonanza, ndio maana hapakuwa na timu iliyopata pointi katika mchezo huo zaidi ya kusherehekea, sisi tumepata zawadi ya milion 98 wakati wenzetu Simba SC wamepata milion 1, hivyo zaidi sisi tumeendelea kuimarika kiuchumi zaidi wenzetu wameishia kusherehekea" alisema Manji. 
Aidha amesema wachezaji zaidi ya tisa wa Yanga hawajapata muda wa kupumzika tangu mwezi Novemba baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu kwani walijiungana timu za Taifa na wamekua huko kwa takribani mwezi mzima bila kupumzika tofauti na wenzetu Simba SC ambao hawana wachezaji wengi timu ya Taifa.
Manji pia alisema anaapa hongera kwa kushinda bonanza la jana, anasema mchezo wa jana walicheza vizuri hivyo wanastahili pongezi kwa hilo.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari juu ya mapungufu yaliyojitokez katika mchezo wa jana, amesema kamati husika inayafanyia kazi na kwa kuwa yeye anasafiri leo kwenda nje ya nchi  majukumu yote amemkabidhi makamu mwenyekiti Clement Sanga mpaka yeye atakaporejea.

UWEZI AMANI HIZI NDIO PICHA TATU ZA LULU AKIWA MAZOEZINI..MSAMBA HUOO DAHH

0
0


Kweli Mwanadada kaamua kupunguza mwili ...Huo msamba dahhhhhhh

NAPE AFURAHIA MAWAZIRI KUVULIWA KUONDOLEWA MADARAKANI

0
0
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye ameeleza kupokea kwa faraja, hatua ya mawaziri wanne kuenguliwa nyadhifa zao kwa ridhaa ya Rais Jakaya Kikwete.

Mawaziri hao, Khamis Kagasheki wa Maliasili na Utalii, Dk Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani), Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamshi Vuai Nahodha na Waziri wa Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi, Dk Mathayo David Mathayo walijiuzulu nyadhifa zao baada ya wizara zao kuelezwa kushindwa kusimamia Operesheni Tokomeza Ujangili, ambayo ripoti yake iliwasilishwa bungeni juzi na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, James Lembeli.

 “Najisikia vizuri, maana kwa kitendo cha mawaziri hao wanne kuchukuliwa hatua, ninaamini kitasaidia wale wengine waliolala nao waamke. Bila shaka sasa hakuna atakayelala na akilala anajua itakula kwake,” alisema Nape alipokuwa akizungumza na Kituo cha Televisheni cha ITV cha jijini Dar es Salaam alipotakiwa kueleza hisia zake kwa uamuzi huo wa Bunge.

Wakati Waziri Kagasheki akiwa ametangaza mwenyewe hatua ya kujiuzulu wadhifa wake, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alitangaza hatua ya Rais Jakaya Kikwete kubatilisha uteuzi wa mawaziri hao baada ya wabunge kushinikiza wajiuzulu kutokana na Kamati ya Kudumu ya  Ardhi, Maliasili na Mazingira kubaini ‘uozo’ katika Operesheni Tokomeza Ujangili iliyofanyika hivi karibuni.

Chini ya Mwenyekiti wake, James Lembeli, Kamati hiyo ilieleza pamoja na mambo kadhaa iliyoyaeleza kuwa ya ovyo yaliyojitokeza kwenye operesheni hiyo, vitendo vingi ikiwemo ubakaji na udhalilishaji vilifanyika ambapo ni kinyume na utu na haki za binadamu.

Kutokana na kadhia hiyo, kamati hiyo kupitia kwa Lembeli, iliwataka mawaziri wanaohusika kutazama kama wanafaa kuendelea na nyadhifa zao au wajiuzulu, pia kamati hiyo ikaenda mbali zaidi kwa kumwomba Rais Jakaya Kikwete kuchukua hatua ya kuwawajibisha.

Akizungumzia zaidi hatua hiyo, Nape alisema kuwa pamoja na mawaziri hao kuwajibika, ipo haja ya kwenda mbali zaidi kwa kutazama mifumo na sheria zilizopo sasa kwa kuwa inaonekana kuwa miongoni mwa vyanzo vya vikwazo katika utekelezaji wa utawala bora.

“Kwa mfano leo hii, mawaziri wameng’oka, sawa ni jambo jema, sitetei, lakini inawezekana kabisa kuna mifumo na sheria ambazo zilimkwaza waziri huyu kutimiza wajibu wake. Mfano, alihitaji kumfukuza mtu kazi kwa kuzembea jambo fulani, lakini mamlaka ya kufukuza kazi mtumishi yapo kwa Katibu Mkuu wa Wizara, hapa atafanyaje,” alisema Nape na kuongeza;

“La msingi hapa ni lazima hatua hizi ziende mpaka chini huku kwa watendaji, ili isiwe mawaziri wanawajibishwa tu kwa sababu ya dhamana zao za kusimamia kisiasa, huku watendaji wanazidi kuvuta shuka bila hofu wakati baadhi yao ni sehemu ya matatizo”.

Alisema kuwa hatua ya sasa inayofanywa na CCM kusimamia Serikali ni ya kawaida kwa kuwa kazi hiyo haipaswi kufanywa na wapinzani kwa kuwa sera inayotekelezwa ni ya chama hicho.

Nape aliahidi CCM kukomba viti vyote vya ubunge na udiwani vilivyopo chini ya wapinzani, akisema, baada ya wapinzani kujaribiwa wameshindwa kuonyesha matunda yoyote ya kusaidia wananchi na hivyo kutokuwa mbadala wa CCM

DADA WA KAZI ANAVAA HIVI , MAMA MWENYE NYUMBA UPO UNAANGALIA TU, UNATEGEMEA NINI?

0
0
Wapo watu ambao bado hawajajua madhara ya mavazi, mavazi yanaweza kuharibu nyumba, dada wa kazi akijiachia namna hii na mwenye nyumba unaangalia tu madhara ni makubwa labda kama mnaishi wawili tu hapo ndani ila kama unaishi na mumeo kazi unayooo..!!

WAKATI UNALALA,IKA HUNA HELA, CHEKI MBONGO MWENZAKO ANASWA ANAENDESHA GARI HILI LA THAMANI DAR

0
0

Usiseme Hamna Hela,sema Sina Hela....That was the statement that kept playing on my head os Sunday Morning when I came in contatc with this beast along Dar es Salaam streets...

Yes,its the famous Lamborghini and it belongs to a Tanzanian! So...I moved closer to get a better look at it...

MADAM RITA AFICHUA SIRI"NILIZAA KATIKA UMRI MDOGO SANA"

0
0
Mkurugenzi wa Benchmark Production, Rita Paulsen aka Madam Rita amesema yeye ni miongoni mwa wanawake waliopata ujauzito wakiwa na umri mdogo lakini alikuwa jasiri wa kukabiliana na hali hiyo hadi akafanikiwa.

Kupitia Facebook, Madam Rita amewashauri wasichana wanaojikuta katika katika hali hiyo kutokata tamaa kwakuwa bado wanaweza kufanikiwa.

“Jambo mmoja msilofahamu kuhusu mimi,Nilipata ujauzito nikiwa na umri mdogo sana. Kwa jamii yetu inayotuzunguka, ukizaa katika umri mdogo, watu huwa wanakunyanyapaa, hukuona haufai kuwa katika jamii na hata kukuhukumu. Kwa umri ule niliona ni kama hamna tena maisha kwangu lakini sikukata tamaa na leo hii ujasiri wangu na kitu kinachonipa msukumo wa maisha hadi kufika hapa nilipo ni hicho kilichonikuta nikiwa na umri mdogo.Kukataa tamaa isiwe ndio chaguo lako la kwanza,” aliandika Rita.

DADA ZETU IFIKE HATUA MJIKUBALI..DADA HUYU MKOROGO WAMUUMBUA JUU FANTA CHINI BALAA

0
0

Wa Design hii Hata kwetu Wapo....Kwenu Je?

HII NDIO TAARIFA RASMI YA KUFUKUZWA KOCHA WA YANGA ERNST BRANDTS

0
0
Uongozi wa klabu ya Young Africans SC umempatia taarifa (Notice) ya siku ya thelathini (30) kocha mkuu mholanzi Ernie Brandts juu ya kusitisha mkataba wake kuanzia jana Disemba 22 mwaka huu.
Maamuzi hayo yanafuatia muenendo wa matokeo mabaya katika michezo iliyopita ya Ligi Kuu, kirafiki na bonanza la Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba SC mwishoni mwa wiki.
Hatua ya Young Africans SC kusitisha huduma na Brandts isichukuliwe kama chuki bali ni moja ya sehemu ya kuhakikisha tunaboresha benchi la ufundi ili tuweze kupata matokeo mazuri katika Mashindano yanayotukabili.
Ukitazama uwezo wa mchezaji mmoja mmoja wa Yanga SC na wapinzani wetu, na soka tulilocheza kwenye mchezo wa mwishoni mwa wiki kwa kweli ni dhahiri mwalimu amefikia mwisho kimbinu na hana njia mbadala.
Young Africans SC imekua ikicheza chini ya kiwango katika michezo ya Ligi Kuu hali iliyoplekea kupata ushindi kwa tabu na wakati mwingine timu kupoteza pointi.
Kufuatia kupewa taarifa ya siku 30, Brandts ataamua mwenyewe kama ataendelea kusimamia mazoezi ya timu au kuondoka moja kwa moja kabla ya muda huo ukiwa haujakamilika.
Ikiwa Brandts ataondoka mapema timu itaendelea na mazoezi kama kawaida katika kila siku asubuhi katika uwanja wa bora kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa chini ya kocha msaidizi Fred Felix “Minziro”.
Ili kuhakikisha timu inafanya vizuri katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya kimataifa uongozi unakamilisha maandalizi ya safari ya kambi nje ya nchi na taratibu zote zitakapokamilika tutawajulisha.
Aidha uongozi upo katika mchakato wa kumapata mrithi wa Brandts ambaye ataungana na timu kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili na Mashindano ya klabu Bingwa Afrika.
Mwisho tunawaomba wanachama, wapenzi na washabiki wa Yanga wasivunjike moyo kufuatia matokeo ya bonanza mwishoni mwa wiki, uongozi unajipanga kuhakikisha timu inaimarika kwenye benchi la ufundi na kurudisha furaha katika mzunguko wa pili wa VPL.


Abdallah Bin Kleb
Mwenyekiti - Kamati ya Mashindano
Young Africans Sports Club.

MCHAWI AANGUKA PEMBENI YA KANISA AKIWA NA KIGANJA CHA MKONO WA MTU MDOMONI.

0
0
Dada mmoja aliye julikana baadae kama Esther
alianguka pembeni ya kanisa huko Naija huku akiwa na kiganja cha mkono wa mtu mdomoni na gongo kubwa mkononi, baada ya kuhojiwa baadae alisema kwamba yeye alikuwa kwenye safari zake tu na baadae kujikuta amepoteza fahamu eneo hilo.

NI NADRA KWA DIAMOND COLABO..ILA SASA NI ZAMU YA GODZILLA..PATA PICHA

0
0
Ni nadra sana kwa Diamond Platnumz kufanya collabo na tena na msanii wa Hip Hop. Mwaka huu hitmaker huyo wa ‘My Number One’ alishirikishwa na Nay wa Mitego kwenye ‘Muziki Gani’ na kushuhudia mafanikio makubwa kwa Nay ambayo ni pamoja na kuongeza mashabiki zaidi na kupata show nyingi zilizomfanya kuwa miongoni mwa wasanii walioingiza mkwanja mwingi mwaka huu.
Sasa ni zamu ya Godzilla kupata neema za Diamond Platnumz, kipenzi cha wengi. Wakali hao watasikika kwenye ngoma ya pamoja iliyofanyika MJ Records na ambayo itatoka mwaka 2014.
“Zilla &diamond platinum&za chaa&marco chalii . ..on the same page ,whts my name jan ....see you 2014,” ametweet Godzilla jana.
Hakuna wasiwasi kuwa hiyo itakuwa hit ya mwaka 2014.

SHILOLE AYASIFIA MAKALIO YAKE KWA KUYAONYESHA INSTAGRAM NA KUSEMA NI ORIGINAL

0
0

Sifa Jipe Mwenyewe bwana ...Usisubiri ..ukisubiri utangoja sana

SIRI NZITO YAFICHUKA...HIRIZI ZATUMIWA NA WACHUNGAJI MAKANISANI

0
0
Stori:  Makongoro Oging’ na Haruni Sanchawa
SIRI nzito imefichuka! Baadhi ya maaskofu na wachungaji (baadhi lakini) wa makanisa ya kilokole nchini wanadaiwa kutumia hirizi ili kujaza waumini, Uwazi limenyetishiwa.
Askofu Kakobe.
SEHEMU ZINAZOKAA HIZIRI
Kwa mujibu wa mfichua siri huyo, watumishi hao wa Mungu wanaojihusisha na ushirikina wamekuwa wakizifunga hiziri hizo sehemu ya juu ya mkono wa kulia na kufichwa na shati la mikono mirefu ambalo nalo huwa ndani ya koti la suti.
Ikadaiwa kuwa, wengine huficha sehemu ya siri ya nguo ya ndani kulingana na maelekezo ya waganga wanaowatengenezea hirizi hizi

WAUMINI NAO WANENA
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mapaparazi wetu jijini Dar juzi, baadhi ya waumini wa makanisa hayo ya kiroho walisema wamegundua kuwa, wapo viongozi wa makanisa hayo ambao hutumia nguvu za giza ili kuvuta waumini wengi.
LENGO LA KUTUMIA HIRIZI
Waumini hao ambao walidai wana uhakika kuna watumishi wa Mungu feki wengi siku hizi, walisema maaskofu na wachungaji wanaotumia hiziri wana lengo la kujipatia ‘kondoo’ wengi hivyo kuwa na uhakika wa kukusanya sadaka nyingi.
Kaldinali Polycarp Pengo.
NI WALE WENYE NIA YA UTAJIRI TU
Habari zaidi zinadai kuwa, watumishi wa Mungu waliotumbukia kwenye ushirikina huo ni wale wanaosaka utajiri tu na neno la Mungu kwao si kitu cha lazima.
Watumishi hao wanadaiwa kusema kwenye madhabahu ya makanisa yao kwamba wameokoka, wanatembea na Bwana Yesu, lakini ndani ya mioyo yao hakuna ulokole wala uinjilisti zaidi ya blaablaa tu.
ROMANI, KKKT, ANGLIKANA WALIA
Ikazidi kudaiwa kuwa, pigo kubwa la kuwepo na kutanuka kwa makanisa ya kiroho nchini ni kwa Romani Katoliki (chini ya Kaldinali Polycarp Pengo) Walutheri, KKKT (chini ya uongozi wa Alex Malasusa) na Anglikana (lililokuwa likiongozwa na Valentine Mokiwa) ambao miaka ya karibuni makanisa yao yamemegwa, baadhi ya waumini wamekimbilia katika makanisa ya kiroho.
Askofu Alex Malasusa.
Hata hivyo, si waumini wote waliokimbilia kwenye makanisa hayo wapo kwa watumishi wanaodaiwa kutumia hiziri, wengine wapo kwenye makanisa salama.
WATUMISHI WA MUNGU WASAKWA
Kufuatia kufichuka kwa siri hiyo, Uwazi liliwatafuta viongozi mbalimbali wa makanisa nchini ili kuzungumzia madai hayo.
Aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania  ambaye sasa ni Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam, Dk. Valentine Mokiwa alipoulizwa juzi na Uwazi kuhusu kuwepo kwa matumizi ya hirizi kwa baadhi ya watumishi wa Mungu, alisema:
“Watu wanasema kuwa nguvu za giza hutumika katika baadhi ya makanisa ya kiroho, lakini kwa upande wangu sijaujua ukweli wala sijathibitisha kwa sababu ni mambo ya kishetani.
“Siku hizi dini imekuwa kama soko  kwani wengi hutumia uongo kanisani  kwa lengo la kuwajaza watu.”
Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo katika Viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam, Josephat Gwajima kwa upande wake alisema wingi wa waumini katika makanisa mbalimbali ya kilokole hutokana na huduma nzuri na mafundisho mema yanayotolewa na wasimamizi wa makanisa hayo.
Kwa upande wake Kiongozi wa Kanisa la Huduma ya Maombezi,  Mbezi Salasala jijini Dar es Salaam, Nabii Flora Peter alisema mtumishi wa Mungu  kutumia hirizi katika kuendesha Neno la Mungu ni dhambi kubwa katika utumishi. 
“Mungu hapendi, kama kuna  mtu wa namna hiyo  basi huyo hafai kuongoza kanisa  kwa sababu dini ni imani ya mtu, sasa haiwezekani utumikie  mabwana wawili,” alisema Nabii Flora.
Makamu wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Magnus Muhiche  yeye alisema hajawahi kuona ila anachokijua wingi wa watu katika makanisa ni sawa  na biashara.
Askofu John Said  wa Kanisa la Victoria lililopo Mabibo External jijini Dar es Salaam alipoulizwa kuhusu hilo  hakupenda kuchangia kitu chochote.
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi la Ubungo Kibangu jijini Dar, Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako’  alipigiwa simu, hakupokea, akatumiwa ujumbe wa simu wa meneno (SMS) hakujibu licha ya ujumbe huo kurudiwa mara mbili kwa saa tofauti.
Mwaka 1993, Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel & Bible Fellowship, Zakaria Kakobe alifanya mkutano wa Injili kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi, Gangilonga, Iringa ambapo baadhi ya wachungaji wa makanisa wa mkoa huo walifika kumshuhudia.
Baada ya mkutano kumaliza, wachungaji hao walisikika wakisema kuwa, walifika kwa lengo la kuthibitisha kwa macho yao uvumi ulionea kwamba, Kakobe anatumia hirizi kuhubiri, hasa wakati wa kuponya wagonjwa akiwa ameishika mkononi.
Wachungaji hao walishangaa mpaka mwisho wa mahubiri, Kakobe hakuwa ameshika hirizi na kumpongeza kwamba, kumbe maneno ya watu juu ya mtumishi huyo wa Mungu hayakuwa na ukweli hasa kwa jinsi alivyoliitia jina la Yesu kuponya watu.

BILIONEA ALIYEJIUA... MKE WAKE AIBUA MAZITO

0
0
Stori: Haruni Sanchawa na Makongoro ogin’g
MKE wa marehemu bilionea Suleiman Muhema, Zihija Muhema ametoboa siri kuhusiana na kifo cha mume wake aliyekutwa amefariki dunia kwa kujipiga risasi akiwa ndani ya gari lake Kisarawe, Pwani.

Akizungumza na gazeti hili juzi, Zihija alisema kifo cha mume wake kimegubikwa na usiri mkubwa baada ya mumewe siku ya tukio kumwambia kuwa anamfuata mama yake aliko, hali ambayo ilimshitua kwa kuwa mama yake mzazi alishafariki siku nyingi zilizopita.

“Mume wangu alikuwa na siri kubwa  kwani baada ya kifo chake nimeamini kuwa kuna mambo mengi alifanya bila kunishirikisha.

“Hadi anakufa nilikuwa sijui kama anamiliki bastola, hali ambayo imenipa imani kuwa huenda chanzo cha kujiua alikuwa anakijua,” alisema.

Aliongeza kuwa siku ya tukio mume wake alimpigia simu na kumwambia ikifika saa 4.30 usiku ampigie simu na wakati huo ilikuwa ni saa 2.

Akasema kuwa alimjibu kuwa atakuwa amelala lakini alimsisitizia afanye hivyo na baadaye alisema anakwenda kujiua.
“Ilipofika saa nne usiku nilimpigia na kumuliza yuko wapi, aliniambia yupo kati ya Minaki na Kisarawe anakwenda kujiua hali ambayo ilinipa wasiwasi mkubwa.

“Nilipomuuliza kwa nini anataka kufanya hivyo? Aliniambia maelezo yote atayaacha polisi.
“Tuliendelea kuongea na mume wangu ili aniambie yuko wapi ili niweze kumfuata lakini akanijibu kuwa anamfuata mama yake alipo.

“Nilimuliza kama ni kujiua kwa nini aende mbali akajibu kuwa anaweza kuchukua maamuzi ya kujiua halafu asife hivyo anaona ni heri awe mbali na hospitali ili iwe kazi kupona kama ataenda kuokolewa.
“Nilimuliza tena sababu ya kujiua, alikata simu. lakini kabla ya hayo yote nilimuuliza akifa tukamzike wapi? Akajibu Dar karibu na watoto wake,” alisema mke huyo.

Uchunguzi wa gazeti umebaini kuwa marehemu aliwahi kulalamikiwa na mkewe huyo Kituo cha Polisi Oysterbay, Dar kuwa alimtishia maisha na likafunguliwa jalada lenye kumbukumbu namba  OB/RB/12734/2013, Julai 20 mwaka huu.
Hata hivyo, jalada hilo lilifungwa Agosti 5, mwaka huu baada ya wanandoa hao kuelewana.

Mke wa marehemu alipoulizwa kuhusu hilo alikiri na kusema katika ndoa mambo kama hayo yapo  na waliyamaliza.
Akizungumzia mali za marehemu, mama huyo alisema hivi sasa kuna maneno mengi yanasemwa kuhusu magari makubwa, akasema yapo na hayajapotea ambapo ni Scania namba T 793 CHE, T 159 CGF na  T 331 CHK ambayo aliyanunua yeye (mke) lakini alimkabidhi mumewe kusimamia.

“Ninasikitika kusikia kuna watu wanaosema vibaya, kama ni ndugu wa marehemu wafike kuniona kwa ajili ya kuwekana wazi,” alisema.
GPL

ZITTO AWAOMBA WAKAZI WA KIGOMA KUMUUNGA MKONO KWENYE VITA YAKE NDANI YA CHADEMA

0
0
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amewaomba wakazi wa Mkoa wa Kigoma kumuunga mkono katika mapambano yake ndani ya chama hicho. 
Akizungumza Mjini Kasulu katika mkutano wa hadhara, Zitto alisema atahakikisha anapigania haki yake ndani ya Chadema kwa kufuata taratibu zote zilizowekwa kwa mujibu wa Katiba ya Chama hicho ili aweze kurudishiwa nyadhifa zake, hususan nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Bara aliyovuliwa na Kamati Kuu Novemba 21, 2013.

“Najua nakabiliwa na vita kubwa ndani ya Chadema, lakini kwangu mimi (Zitto) hii ni changamoto, naamini nitashinda tu. Lakini lolote litakalotokea ndani ya Chadema hata kama ni kunifukuza, nitarudi kwenu ndugu ili tuamue kwa pamoja nini tufanye, wapi twende kwa pamoja kama tulivyo kwani nguvu ya mamba ipo kwenye maji,” alisema Zitto.
Amesema kwa kipindi kirefu anaonekana kama msaliti ndani ya chama na anatuhumiwa kutoa siri za Chadema kwa CCM na Serikali. “Tuhuma hizi hazina ukweli, nalaumiwa na kubambikiwa mambo kutokana na msimamo wangu ndani na nje ya chama
“Watu wa Kigoma ambao ndiyo tulipokea mageuzi kabla ya wengine, tunaitwa wasaliti ndani ya Chadema, lakini waliokuja baadaye kutoka mikoa mingine hawa ndiyo wanajiona wasafi. Wapo Watu waliingia Chadema baada ya kukosa fursa za kugombea huko walipokuwa awali na sasa wanajifanya ndiyo Chadema damu-damu. Sitoki Chadema ng’o, labda wanifukuze,” alifafanua Zitto. “Mnakumbuka misukosuko iliyomkuta Dr Kabourou (Aman) alipokuwa Kiongozi wa Chadema, pia walimwondoa Kafulila (David) na sasa mimi (Zitto) natafutwa ili niondolewe. Lazima tuungane pamoja kutetea masilahi yetu watu wa Kigoma,” aliongeza Zitto.
Viewing all 104423 articles
Browse latest View live




Latest Images