Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

REMIX: Nick Minaj AJAMBA VIBAYA Kwenye video yake ya ANACONDA…..Bofya hapa Uvunje mbavu zako

0
0
Video  ya   Nicki Minaji  ambayo ni booty-shaking imefanyiwa cheeky remix ikiwa na addition ya sauti ya kujamba aka ushuzi!!!.

Team ya comedy ya South Africa and the Sunday Blues wali-share ngoma hiyo kwenye YouTube siku ya Jumane August 24.

Badala ya kuwa muziki wa Minaj the soundtrack ya video  ilikuwa ni Nicki Minaj  akijamba all the way!.

Lady Jay Dee Akanusha Tuhuma za Kutoka Kimapenzi Na ‘Serengeti Boy’

0
0
Lady Jaydee ameamua kujibu habari iliyoandikwa kwenye gazeti la udaku la Risasi kuhusu kuwa na uhusiano na aliyewahi kuwa mtuma salamu maarufu kwenye redio, Meddy Ahmed aka ‘Mtoto wa Vitoto’.

Kwenye habari hiyo, Risasi wanadai kuwa Jaydee ambaye anadaiwa kuachana na mume wake Gadner G Habash ameonekana mara kadhaa na Mtoto wa Vitoto na kwamba amewahi kuonekana akiwa na gari lake.

Kupitia Instagram, Jaydee ameandika:

Kuna habari za kuniudhi Ila hii imenichekesha. Kwahiyo mtoto wa vitoto ndio bwana angu???? Basi sawa nashukuru naona mmenianzia tena sasa picha za February Na nilizi post mwenyewe humu insta leo ndio mmeziona? Ukweli mnaujua mmeamua tu kuzingua ,,, wangapi wameshapiga picha na hiyo Range? Duuuh! !!!!! Shkamoooni Moyo wangu chuma. Pigeni mawe mpk mchoke Kama ambavyo mmekuwa mkifanya miaka yote na bado nipo hapa hapa.

Uraia Pacha Wabezwa Bunge Maalumu la Katiba

0
0
Suala la uraia pacha limeonekana ‘kupigwa chini’ na serikali na wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba baada ya wote kukubaliana zaidi juu ya hasara za kuruhusu uraia huo, ikiwemo hofu ya usalama wa taifa na uzalendo kupungua. 

Katika semina iliyoandaliwa kwa Wajumbe wa Bunge hilo na mada kutolewa na Idara ya Uhamiaji, Abdallah Khamis Abdallah ambaye ni Kamishna wa Udhibiti na Mipaka wa idara hiyo, imeonesha kuruhusiwa uraia pacha ni hasara zaidi kwa Tanzania kuliko faida. 

Suala hilo kwenye semina hiyo likawafanya wajumbe zaidi ya 12 kati ya 16 waliochangia kukataa uraia pacha na kumuacha mwakilishi wa Diaspora, Kadari Singo kutumia nguvu nyingi kutetea uraia pacha huo.  

Wajumbe wa Bunge wakizungumza na mwandishi wameeleza kuwa  Uhamiaji imeeleza kuwa Watanzania wameondoka nchini kwa sababu za kufuata elimu, viapo vilivyowafanya wawe watiifu kwa nchi walizopata uraia na wengine kwa kuitukana nchi haifai na hawawezi kuishi Tanzania.

Mjumbe Wazir Rajab Salum alisema Uhamiaji imetaja faida ya uraia pacha ni za kiuchumi pekee na nyingi ni hasara, ikiwemo kuangalia uzalendo ambapo imeonekana kuruhusu kutapunguza uzalendo na usalama wa taifa utakuwa hatarini

Majambazi Watano Wauawa kwa Kuzamishwa kwenye Maji ya Mto Mara

0
0
Watu watano wanaosadikiwa kuwa majambazi, wamepigwa kwa mawe hadi kufa wakijaribu kutoroka nguvu za umma kwa kutumia Mto Mara, wilayani Tarime huku wakiwa na bunduki mbili zinazotumika vitani aina ya sub machine gun (SMG). 

Tukio hilo lilithibitishwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya, Lazaro Mambosasa. 

Kamanda Mambosasa alisema watu waliouawa katika tukio hilo la juzi mchana hawajafahamika kwa majina wala uraia wao.
Hata hivyo alisema siku ya tukio, majambazi hao wakiwa na silaha za kivita, walionekana wamejificha vichakani karibu na makazi ya wananchi wa kitongoji cha Nyabirongo, kijiji cha Gibaso katika Kata ya Nyarukoba, Tarafa ya Ingwe iliyopo jirani na hifadhi ya Serengeti. 

Lakini baada ya kushitukiwa, walizingirwa na wananchi wenye silaha za jadi zikiwemo mawe, marungu na mapanga huku wakipiga mayowe ambapo majambazi hao walijibu kwa kurusha risasi hovyo ili wananchi wasiwakaribie. 

Wakati wakirusha risasi hizo zilimjeruhi mwananchi mmoja, Kagore Paul begani, na kuwaongezea hasira wananchi walioendelea kuwasakama katika eneo walilojificha. 

Mayowe waliyopiga yaliwaleta watu wengi zaidi muda ulivyokuwa unakwenda kiasi cha majambazi hao kuzidiwa na  kuamua kukimbia kwa kupitia Mto Mara, ili waende upande wa pili wa wilaya ya Serengeti. 

Kamanda anasema: “Wakazi wa kijiji hicho na vijiji jirani walijitokeza kwa wingi kwani ilikuwa mchana na kupambana na watu hao huku wakikimbilia mto Mara kutaka kuvuka mto huo  kwenda  wilaya ya Serengeti kuingia mbugani, lakini juhudi zao za kutaka kuvuka hazikifanikiwa. 

“Wananchi wa vijiji vya upande wa pili Wilaya ya Serengeti nao walijitokeza na kuziba njia hali iliyowalazimu watuhumiwa kuingia mtoni na kutaka kuogelea huku wakitupa silaha walizokuwa nazo majini  na hapo ndipo walipopigwa mawe na marungu wakiwa majini na kufa. 

Jeshi letu la Polisi lilifika na kusaidia kuopoa miili ya watu hao watano ambapo mmoja alikutwa na risasi 11 mfukoni na mwingine alikutwa na risasi nne na fedha za Kenya Sh 350 (sawa na fedha za Tanzania sh 7,000) ambapo inasadikiwa huenda watuhumiwa wakawa raia wa nchi jirani ya Kenya.” 

Kwa sasa, miili ya watu hao imehifadhiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Wilaya Tarime huku jeshi la polisi likiendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo. 

Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya Tarime, Dk Bernard Makonyu amethibitisha kupokea miili ya watu watano iliyofikishwa hospitali hapo na gari la polisi huku matumbo ya marehemu yakionekana kuvimba kutokana na kunywa maji mengi kabla ya kufikwa na mauti. 

Hilo ni tukio la pili katika kipindi cha wiki tatu ambapo Agosti 3 mwaka huu watu wanne, wakiwemo raia watatu wa Kenya na Mtanzania mmoja waliuawa kutokana na matukio ya ujambazi katika kijiji cha Mriba.

Rais Kikwete Iga Mfano wa Uhuru Kenyata Mapambano Dhidi ya Madawa ya Kulevya

0
0
Hakika raisi wa kenya ni mfano wa kuigwa:
Ni raisi ambaye awali sikufurahishwa na siasa zake lakini baada ya kuanza kuitumikia kenya anaonekana kuwa ni kiongozi makini na mwenye uzalendo wa kweli kwa taifa lake.
-hii ni kutokana na yeye kumwondoa mkuu wa idara ya usalama wa taifa wa nchi hiyo,ambapo licha ya kutambua umuhimu wake na uwezo wake lakini kutokana na matukio ya milipuko na mabomu ambavyo vililitikisa taifa hilo akaamua kumwajibisha mkuu huyo wa usalama bila kuangalia maslahi binafsi na kubebana kusiko na msingi wowote.
*=kubwa kuliko yote ni kitendo cha raisi huyu kuizamisha meli iliyokuwa imebeba madawa ya kulevya na kukamatwa bahari ya hindi ukanda wa mombasa.
Haya madawa yanakadiriwa kuwa na thamani ya trilioni 1.6 za kitanzania.
Huu ni ushujaa na ni ukomavu kama raisi kulitangazia taifa kuwa lazima hayo madawa yaharibiwe na meli husika izamishwe.
**jakaya kikwete iga mfano wa kiongozi huyu mwenzio.
-matukio kama haya yamekuwa yakijitokeza nchini lakini hatuoni hatua kali zikichuliwa.

Pombe Sio Chai Jamaa Bia Mbili Tu Kaanza Kuvua Nguo na Kuweka Mapozi ya Kimisi Watu Wampige Picha

0
0
Pombe usipoweza kuicontrol basi matokeo yake ita Control wewe ! Huyu Jamaa Alinawa na Kamera za Udaku Specially Katika Baa Moja Maarufu Mitaa ya Sinza , Inasemekana Alikuwa na Wenzake wanakunywa Baada ya Kupata Bia Mbili tu zikampanda Kichwani na Kuanza kuweka Mapozi ya Ajabu Ajabu na Mwisho Kuvua nguo na kuweka Mapozi ya Kimiss Watu Wampige Picha, Wenzake kuona Hivyo Wakamkimbia na Kumwacha Mchizi akiabika Kiaina..

Lady Jaydee: Hata Ndoa Yangu ikivunjika Haimaanishi Mnitafutie Story za Kunichafua

0
0
Lady Jay Dee, jana (August 30) kupitia Instagram alijibu kwa ufupi habari iliyoandikwa na gazeti la Risasi yenye kichwa cha habari ‘Jide, dogo dogo gumzo mjini’, Jana kupitia ukurasa wake wa Facebook amejibu kwa urefu zaidi juu ya habari hiyo. 

Hivi ndivyo alivyoandika Jide:

Zamani ilikuwa haipo sehemu ya kujitetea, gazeti likishaandika ndio limeandika.
Lakini sasa ulimwengu umebadilika, sio muda wa watu wote kulishwa chakula kisichofaa.

Kwanza hicho kichwa cha habari kimenivunjia heshma sana
Nafikiri lengo ni kuilazimisha jamii inayomuelewa JayDee tofauti imuone kuwa ni mtu asiefaa, sawa.
Dogo anaswa na mkoko? Huo mkoko mmemnasa nao wapi wakati hizo picha ni mimi nilizi post mwezi February Instagram?????

Picha ambazo zilipigwa Nyumbani lounge tena kutumia simu ya Gardner.
Jide, dogodogo gumzo mjini

Gumzo ni kitu kinachoongelewa sana na kilichoenea kila kona ,,,,,sasa hii habari ni gumzo wapi ambapo haisikiki, ……
Mngeandika tumeamua kumuanzishia Jide gumzo hili, ndio ningewaelewa.
Vitu vya kuzua.

Ni watu wengi tu wakija band wakipata nafasi wanaomba kupiga picha na mimi na wengine pia wanaomba kupiga picha na gari sababu wanaipenda.
Kama mtu yoyote anavyoweza kupiga picha na sanamu la kitu chochote anachokipenda.
Hivi je! Wimbo wa JayDee mgumba, JayDee tasa umechuja? Umeisha chati?? Nashangaa na najiuliza tu

Inawezekana wimbo huo umechuja ndio maana mnatafuta wimbo mwingine utakao hit zaidi ya ule
Ndio kinachopelekea kuandika story za namna hii
Sio nyinyi mliokuja kuomba radhi kwa yote mliowahi kuniandika na kudai kuwa mmejirekebisha, miezi kadhaa tu iliopita?

Sio boss wenu aliemfuata Gardner na kumwambia tumalize tofauti zetu?
Kama hizo tofauti zilikuwepo

Inawezekana nyie ndio mna tofauti na mimi, sijawahi kuwa na tofauti na mtu hata nisiemfahamu. ..
Nashukuru Mungu nilikataa msamaha wenu ni kama nilihisi hamkumaanisha
Au sababu sijawahi kukubali show mlizotaka kufanya na mimi?

Je! Hiki ni kisasi? Sielewi
Mungu alienisimamia ataendelea
Hii sio vita ya kwanza wala ya mwisho
Dunia ni mapambano.

Kama nia ni kufanya niishi maisha ya uoga, kudhoofika na msongo wa mawazo mmefeli ,,,,, wengine mkijidai ni wacha Mungu huku mkiumiza nafsi za watoto wa binadamu wenzenu.
No wonder mnaishi bila amani mbali na utajiri mlionao kwa kuogopa visasi.

Sikuzaliwa kukata tamaa
Pia wapo wanaopenda kuandikwa kwenye hayo magazeti yenu
Wafanyieni favor ya kuwapa hiyo nafasi mi sifanyi muziki wa magazeti ya udaku
Mkiachana na mimi nitashukuru sana

Hata ndoa yangu ikivunjika haimaanishi mnitafutie story za kunichafua
Ndoa ya Madiba ilivunjika sembuse yangu nina utofauti ipi na binadamu wengine?
Nyie ndoa zenu ziko perfect si ndio?
Hewala watakatifu nyie, mnaoficha yenu na kutangaza ya wenzenu.

Mwisho nawaomba watu mnaonielewa kutoamini tu habari yoyote ambayo haijatoka kwangu wala kwa muwakilishi wangu ambae ni “Webiro Wakazi Wasira”.
Kama kuna chochote cha watu kujua nitakiongea mimi kwa mdomo wangu sio kuwekewa maneno mdomoni.

Kila siku ooooh tulimpigia simu hapatikani, namba yangu yenyewe kwanza hata mnaijua???
Mngekuwa mnaijua msingekuwa mnahangaika mnawapigia watu wangu wa karibu kunitafuta , na hao watu hawawezi kunisaliti ndio sababu mpaka miaka 70 mtaishia kusema tulimpigia simu JayDee hapatikani.

Nyie muongee chochote mnachojiskia
Ila sie hatuna haki kujitetea ??
Hili nalo litapita kama mengine
Na inshallah nitakuwa hapa hapa nimesimama nawaangalia
Picha moja wapo ni hiyo ambapo mtoto wa vitoto alikuja siku hiyo hiyo na akapiga picha na Gardner, mbele ya gari hiyo hiyo mnayodanganya watu kuwa mmemkuta nayo na mahala ni hapo hapo Nyumbani Lounge, ,,,,, na picha nyingine ni hizo nilizowahi kuzi post mimi mwenyewe mwezi february leo zinanihukumu endeleeni kudanganya jamii

Na hizo ni chat alizoniandikia huyo mtoto wa vitoto ambae ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona na sijawahi kumuona tena. . Zaidi ya kuongea nae twitter ,,, sisemi kama mimi malaika lakini Ukweli huwa hauchanganywi na uongo.

Kwa hili mmenidhalilisha sana
Kama nia yenu jamii inione mwanamke nisiefaa na ninaependa dogodogo
Basi Mungu atawaonyesha ukuu wake

Dully Sykes atoa ushauri muhimu kwa Diamond na Alikiba

0
0
Msanii wa longtime kwenye familia ya Bongo Flava ambaye hujiita muasisi wa muziki huo, Dully Sykes amewataka Diamond na Alikiba kuweka tofauti zao na kufanya kazi pamoja

Dully amedai kuwa Alikiba na Diamond wanatakiwa wafanye kazi waweke tofauti zao pembeni na waingize hela. “Hivi we unadhani itoke nyimbo ya Alikiba na Diamond si itakuwa hatari sana! Maana hiyo ngoma itakuwa gumzo na pia wata watawafurahisha mashabiki wao. Huo ndo ushauri kwa wadogo zangu,” amesema Dully.

Katika hatua nyingine Dully ameiambia Bongo5 sababu za kutofanya vizuri kwa nyimbo zake za sasa. “Unajua nyimbo yangu kama ile ya “Joka” haikufanya vizuri kwakuwa watu walihisi kama nimemdiss mtu ndo maana haikufanya vizuri. Kwa wimbo wa “Binti Spesho” nao ulishindwa kufanya vizuri hasa ilivyofungiwa video yake lakini sasa wimbo wa ,’Togola’ unafanya vizuri nadhani pia umetoka kipindi kizuri na pia video yake ipo tayari inatoka muda wowote kuanzia sasa.

Kuhusu kazi yake kama mtayarishaji wa muziki, Dully amedai kuwa anazidi kuifurahia.

“Tokea nimekuwa producer naenjoy sana maana napenda sana kazi ya kuwa producer sasa hivi kuliko hata kuimba. Na pia sasa nimeshafanya kazi kadhaa za wasanii wakubwa zinakuja kama ya Chidi Benz vile imeshatoka na kuna zingine zinakuja. Unajua sasa hivi studio yangu ina vyombo vipya vya kisasa na pia ntakuwa narekodi live yaani napiga vyombo vyote.”

Hussein Machozi aelezea ukweli wa habari ya kufumaniwa na mke wa mwanasiasa Kenya

0
0
Star wa bongo Hussein Machozi hatimaye amezungumzia tukio lililotokea mwezi uliopita na kupelekea vyombo vingi vya habari nchini Kenya kuripoti kuwa amekamatwa akizini na mke wa mwanasiasa maarufu mjini Mombasa, Kenya.

Haya ndio maelezo ya hit maker wa ‘Kwaajili Yako’ kuhusu kilichotokea, alipozungumza na Millard Ayo kupitia Amplifaya ya Clouds FM jana (Agosti 28).

Ukweli ni kwamba hiyo story imekuzwa yaani imekuwa kubwa sana tofauti na jinsi mambo yalivyokuwa. Kama masaa 24 nilipewa sasa mbona bado nipo Kenya…Ile ishu ilikuwa hivi, tulikuwa tumekwenda kuingia deal hotelini kama tunavyokutanaga, sasa Yule mtu aliyekuwa ananipa deal alikuwa yupo pale hotelini akaniita twende tukaongee kupanga mikakati na kila kitu, lakini baadae kumbe alikuwa na beef sijui na mume wake au sio bana, kwahiyo mume wake alikuja pale kuanza kumletea fujo lakini mimi sikuwa kwenye uhusiano wowote, watu wakaleta fujo pale na nini mimi mbona nikaondoka fresh tu lakini hamna lolote ni kwamba tulikuwa tumekaa nae tunaongea mchakato wa biashara…hotelini kama maeneo ya kupumzika hivi kama sehemu ya mikutano hivi”.

Audio: Diamond Aonjesha Kipande cha Wimbo wake Ambao Haujatoka ‘Nitampata wapi’

0
0
Ni mara nyingi Diamond Platnumz huwa anasema kuwa ana nyimbo nyingi sana alizoisha rekodi na bado anaendelea kurekodi kila kukicha, lakini sio nyimbo zote alizonazo zitapata nafasi ya kutoka kama official singles.

Kupitia Instagram yake hit maker wa ‘Number 1’ ameamua kuwaonjesha kidogo mashabiki wake wimbo mmoja ulioko kwenye maktaba yake.

“wakati Mwingine natamanigi hata mngepata dakika moja tu ya kuskia nyimbo nilizo nazo ndani, … hii inaitwa #Nitampata_wapi? sjui kina @babutale wataitoa lini… maana haipo kabisa katika list ya nyimbo zitolewazo… ila, kwakuwa nyie ni watu wangu wa nguvu nimeamua kuwaibia kidoogo, sjui watanimind!#GermanyWeekEnd.” – Diamond

Diamond Aponea Chupu Chupu Kushushiwa Kipigo na Mashabiki wa Ujerumani, Polisi Wamuokoa

0
0
Usiku wa Jumamosi ya Tarehe  30.Augost 2014, majira ya saa 10 alfajiri, Mwanamuziki nyota wa Bongo Flava Nasib Abdul 'Diamond Platnumz' alijikuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart, Ujerumani, baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri show.

Washabiki hao waliokuwa wamelipa ticket euro 25 kwa kiingilio waliahidiwa kuwa show ingeanza saa 4.00 usiku, lakini walijikuta wakisubiri hadi majira ya saa 10 usiku au alfajiri ndipo mwanamuziki Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake Mr.Awin Williams Akipomiemie raia wa Nigeria anajiita kama Britts Event.

Hapo ndipo washabiki hao walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki  Diamond na promota wake.

Kilichowakera zaidi mashabiki ni pamoja na vyombo vibovu vilivyofungwa katika ukumbi huo kitu ambacho kiliwafanya mashabiki kuvunja vyombo vya muziki ma-Djs walishambuliwa na wapo hosptalini kwa sasa.

Moja wa Djs hao alipoteza Lap top yake, mwanadada DJ Flor alipatwa mstuko wa moyo na kukimbizwa hosptali, washabiki hao walimpa kipigo DJ Drazee naye yupo hoi hospatal.

Polisi nchini Ujerumani wamesema tukio hilo la aibu halijawahi kutokea, kwani msanii kuchelewa kufika jukwaani kwa ujerumani ni kitu cha hatari sana kwani mashabiki wa ujerumani wanaheshimu sana muda wao.

Mpaka sasa polisi wanamsaka mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema kuwa wanachunguza thamani ya hasara iliyosababishwa na ghasia hizo na pia itamfungulia mashataka promoter huyo raia wa Nigeria,ambaye pia anachunguzwa kwa kusemekana anajihusisha na mtandao fulani wa biashara.

Kupitia Instagram Diamond alidai kusikitishwa na tukio hilo.
 
Kiukweli nimesikitishwa sana na uandaaji wa kampuni hii ya BRITTS EVENTS iliyoandaa show ya Stuttgart Germany… kinachoniuma na kunisikitisha zaidi ni jins watu walivyoamua kujitolea kuja kwa wingi kutusupport vijana wao, halaf mwisho wa siku promoter anatupeleka wasanii kwenye show saa kumi alfajiri… najua ni kiasi gani mmeumia na kuwa disappointed… lakini naomba mtambue kuwa halikuwa ni kosa langu, coz mimi ni mgeni tu, na nafata maelekezo ya promoter…hivyo nisingeweza kujiamulia kuja muda ninaoutaka mimi….

Huddah Monroe Awasalimu Mashabiki Wake wa Bongo Kwa Kutupia Picha za Nusu Uchi

0
0
Huyu ni mwanadada kutoka Kenya, kwasasa yupo hapa Dar....(amekuja kula bata...PICHA ZAKE AKILABATA MCHANA HAPA akiwa Hyatt Regency Dar Es Salaam, The Kilimanjaro.. )..sasa usiku jana Alitupia  Picha hiyo Hapo Juu Kuwasalimu Mashabiki wa Bongo Tanzania

Kwa Utajiri Alionao Kajala Sasa Anaweza Kumwajiri Wema Sepetu

0
0
AMA kweli fedha mwanaharamu! Kama bado ulikuwa ukiamini kwamba Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu anayependelea kuitwa Madam ana mtonyo (fedha) kumzidi aliyekuwa shosti wake, mwigizaji Kajala Masanja ‘Kay’, umekosea sana kwani upepo umegeuka, ungana na Ijumaa Wikienda. Habari za ‘ufukunyuku’ zinadai kwamba, kwa utajiri alionao kwa sasa, Kajala anaweza kudiriki kumwajiri Wema kama kisemavyo chanzo.

TUJIUNGE NA CHANZO Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na wote kwa maana ya kutafuna pande zote, mwigizaji huyo ambaye enzi za ushosti wake na Wema alikuwa akionekana kama kijakazi, sasa fedha imemtembelea kiasi cha kutosha wakati mwenzake kwa bahati mbaya eti ‘anatembelea ringi’. Chanzo kilisema kwamba Kajala kwa sasa ana maisha ya ‘kitonga’, amepanga kwenye nyumba nzuri ya ghorofa, ana kampuni yake ya filamu (KAY Entertainment), magari manne, anatembea na wapambe (walinzi) huku akaunti yake benki ikiwa imetuna. “Kajala ameonesha jeuri ya fedha. Ametoka katika nyumba ya kawaida sasa analala angani. Kwa taarifa yenu amepanga ghorofa nzima maeneo ya Sinza-Madukani jijini Dar. “Yupo vizuri, anamiliki ofisi kubwa ya kuzalisha sinema, magari mawili ya ofisi pamoja na magari mawili ya kutembelea (Brevis na Harrier) na anaishi katika nyumba anayolipa kodi kwa mwezi dola 2,000 (zaidi ya Sh. milioni 3.2),” kilidai chanzo hicho na kudai kwamba si mbaya Kajala akamkumbuka mwenzake hata kwa kumwajiri kwenye kampuni yake.

KAJALA AMEHONGWA? Akizungumza na waandishi wetu, Kajala alisema anamshukuru Mungu kwani fedha hizo amezizalisha kupitia kazi zake pamoja na biashara mbalimbali alizokuwa akizifanya, hajahongwa na mtu yeyote. “Sijahongwa na mtu yeyote, kila mtu ana akili zake katika kutafuta fedha, nafanya biashara huku nikiigiza sinema zangu na Mungu amenijalia mambo yanakwenda vizuri,” alisema Kajala. Kuhusu kumwajiri staa mwezake huyo, Kajala hakutaka kulizungumzia hilo. WEMA HALI IPOJE? Utafiti uliofanywa na Ijumaa Wikienda umebaini kwamba Wema aliyemlipia Kajala Sh. milioni 13 asiende jela mwaka jana, ambaye kipindi kifupi kilichopita alikuwa na kampuni ya kuzalisha sinema, wapambe, akaunti iliyonona benki, magari ya kifahari ya kutembelea na samani nyingine, nyingi zimepotea kama si kuyeyuka kabisa.

Utafiti umeonesha Wema ambaye alikuwa akimiliki magari kadhaa likiwemo la kufanyia kazi za sinema, kwa sasa amebakiwa na gari moja tu ambalo ni Toyota Harrier. Kama hiyo haitoshi, ilidaiwa kuwa hata akaunti benki haijanona na hata wapambe wa kutembea naye wameyeyuka. WEMA ATAFUTWA Ili kutaka kujua anazungumziaje ‘challenge’ hiyo ya kudaiwa kuporomoka kiuchumi, wanahabari wetu walimtafuta Wema kwa siku tatu mfululizo lakini hakupatikana huku simu yake ikiita muda mrefu bila kupokelewa. SHOSTI WAKE Akizungumza na waandishi wetu kwa sharti la kutoanika jina gazetini, rafiki wa karibu wa Wema alikiri kuwa staa huyo mwenye nyota isiyochuja, ameshuka kiuchumi tofauti na enzi zile ambazo walikuwa wakitanua katika viunga mbalimbali na msururu wa watu huku Madam akisimamia shoo nzima ya malipo. “Madam kwa sasa ameshuka kiuchumi kwani hatutanui mjini kama ilivyokuwa zamani, yaani naamini anaweza kuajiriwa na Kajala ambaye wakati ule alikuwa chini kwake,” alisema rafiki huyo.

KUMBUKUMBU YA JUZIKATI Hivi karibuni, baadhi ya mashabiki wa Wema ambao wanajiita Team Wema, walimuonya staa wao huyo wakidai ananyonywa na mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ambaye pia amekuwa akimdhalilisha katika majukwaa pindi anapofanya shoo zake. Walimtaka abadilike kwani yeye ndiye mwenye nyota ya kung’aa lakini Diamond ananufaika yeye peke yake na muziki wake. DIAMOND ALINENA Baada ya Diamond kushambuliwa na Team Wema, naye alitoa majibu ambayo yalionesha dhahiri kwamba ndiyo sababu inayomfanya Wema ashuke kisanaa na kiuchumi. “Kama kweli mnampenda huyo msanii wenu (Wema) basi mngemshauri kwanza akaacha kufanya starehe kuliko kuelekeza lawama kwangu, mimi kama mume, jukumu langu ni kuhakikisha namwezesha kuanzisha biashara lakini jukumu la kuendeleza ni la kwake, mnataka hata kuigiza nikamuigizie?,” alihoji Diamond mtandaoni.

Rais Kikwete 'Nimetimiza Ahadi Zangu Kwa Asilimia 80' Ya Kweli Hayo?

0
0
Rais Kikwete alitoa kauli hiyo juzi katika Kijiji cha Gulwe, Mpwapwa mkoani Dodoma, alipokwenda kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja.

Mpwapwa
Rais Jakaya Kikwete amesema zaidi ya asilimia 80 ya ahadi alizotoa wakati anaingia madarakani zimetimizwa na zilizobakia atazimaliza kabla ya kuondoka madarakani.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo juzi katika Kijiji cha Gulwe, Mpwapwa mkoani Dodoma, alipokwenda kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja.

Alisema wakati anaingia madarakani mwaka 2005, alitoa ahadi mbalimbali katika maeneo tofauti zikiwamo zilizoandikwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambazo zimeendelea kutimizwa kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha.

“Sasa tumefikia asilimia 80 ya utekelezaji wa ahadi zetu, naamini tunaweza kufanikiwa kwa zote na kama tutashindwa basi tutaacha kidogo sana, lakini kumbukeni tumetekeleza hata yale ambayo hayakuwa katika ahadi,” alisema Rais Kikwete.

Akizungumzia daraja hilo la Gulwe, aliwaagiza makandarasi kufanya kazi usiku na mchana ili likamilike kama ilivyopangwa.Alisema wananchi wanataka kuona kazi hiyo inakwisha.

Kikao Cha Kikwete na Wapinzani, Kinastahili Pongezi? Au Kubezwa?

0
0
Kwa maoni yangu, kikao kati ya Rais Jakaya Kikwete na Wapinzani wakiwemo UKAWA, kinastahili pongezi na sio kubezwa, na huu ukimya wa matokeo ya kikao hicho, ni Ukimya Dawa!, yaani "silence is golden!".

Kuna msemo unaosema "No News, is Good News!", na "Kimya Kingi Kina Mshindo Mkuu!", tangu jana Rais JK alipokutana na Wapinzani kupitia TCD na miongoni mwao wakiwemo wana UKAWA, kumekuwepo na ukimya, unaopelekea kuzua speculations hizi na zile kuhusiana na matokeo ya kikao hicho, hali inayopekea wale wabunifu wa mambo kuanza kubuni au matokea hasi au matokeo chanya!.

Mtu yoyote anapokamatwa na polisi, duniani kote, kitu cha kwanza anachoelezwa ni kwa polisi kujitambulisha na kumweleza mhusika kuwa "Uko Chini ya Ulinzi""You have the right to remain silance!""anyathing you say, may be used for or against you before the court of law!" wakimaanisha unaruhusiwa kukaa kimya na chochote utakachosema kinaweza kutumika kama ushahidi mahakama kukuokoa au kukuangamiza!. Hivyo ukimya nao ni jibu tosha!.

Naomba tuchukue fursa hii kupongeza uwepo tuu wa kikao hicho regardless ya matokeo yoyote!, ile kukubali tuu, kukutana, kukaa na kuzungumza ni dawa tosha ya kutibu ule mkwamo wa maridhiano katika mchakato wa katiba!.
Hata mgonjwa anapokwenda kwa daktari, ile kuzungumza tuu na daktari kuhusu ugonjwa wake, ni tiba tosha ya ugonjwa huo kabla hata ya dozi kuanza kutolewa!. Hivyo uwepo wa kikao hiki unastahili pongezi na sio ridicule!.

Shilole Akiri live Kutotumia Condom Katika Mapenzi

0
0
Mwigizaji na Mwanamuziki Maarufu Bongo Shilole Amesema Kwake Matumizi ya Condom huyu yanamyima raha ya Mapenzi Hivyo alilazimika kwenda kupima ngoma na mpenzi wake ili wasitumie mipira
Shilole Amezidi Kusema kuwa raha ya mapenzi ni kukutana na mpenzi bila kuwa na kizuizi chochote asikwambie mtu raha ya kula ndizi ni kula ikiwa imemenywa maganda huondoa utamu

Wanawake Wanataka Ndoa Lakini Hawapati, Ni Kweli Hamna Waoaji?

0
0
Kuna kitu kinanichanganya ni kweli hamna waoaji siku hizi au wanawake wanachagua sana?

Sasa hivi hili limekuwa kama janga la Taifa.
Single ladies wengi sana unakuta mwanamke mpaka miaka 33 hana hata mchumba wa kusingizia.

Na ni wengi mitaani tunawaona na wengi wao wakiona umri unazidi basi wanaamua kuzaa na kuwa single mums.

Nyie mnaonaje ni tabia hazikidhi mwanamke kuolewa?

Au ni gharama za harusi?

Wanaume please please muoe watoto wasio na baba wanazidi kuongezeka.

Na hamuwatendei haki wanawake.

Diva Athibitisha Kutoweka Magodoro Kwenye Makalio Yake , Awajibu Wanao Mponda Instagram

0
0
Baada ya mtu anejiita TotoLaKimanga huko INSTAGRAM..Kumuandama mtangazaji wa Clouds FM, Loveness Malinzi aka DIVA kuwa hana shepu na huwa anavaa nguo za ndani zenye vigodoro ili kukuza makalio yake..sasa leo DIVA ameamua kumjibu kwa kuthibitisha ...soma alichokisema

Wema Sepetu: Simlishi Mpenzi Wangu Diamond Viporo na Wala Siweki Chakula Kwenye Hot Pot

0
0
MAHABATI! Beautiful Onyinye wa Bongo,
Wema Sepetu ‘ Madam’ amedhihirisha kuwa
yeye ni mwanamke tayari wa kuwekwa ndani
baada ya kusema anajitahidi kila siku katika
suala la mapishi ili asimlishe viporo
Akipiga domo na paparazi wetu, Wema
alisema kama mwanamke anajua thamani ya
mwanaume siku zote hata kama ‘ baby’ wake
atarudi usiku , lazima aingie jikoni kupika na
haweki chakula kwenye ‘ hot pot ’ .
“Siku zote si kwamba najisifia ila kwa jikoni
ndiyo mwenyewe sasa kwa nini nipike
chakula halafu niweke kwenye hot pot ?
Kwangu siruhusu kabisa itokee , ” alisema
Wema .

Mume wa Mtu Sumu, Look at What Happened to This Cute Lady

0
0
She was Caught Redhanded on Top of Mume wa Mtu, Luckly She Managed to Escape Through the window and that was the picture we managed to Capture during the ambush...
Ukiamua Kuiba Mume wa Mtu Hakikisha Hizo Style za Kuruka Ukuta Unazijua la Sivyo Utaishia Kusutwa.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images