Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Serikali Yaweka Mkakati wa Kuwafuata Baa Kuwapima Watu Ukimwi naTB

$
0
0

Serikali Yaweka Mkakati wa Kuwafuata Baa Kuwapima Watu Ukimwi naTB
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto imesema katika mikakati yake ya kuwatambua wagonjwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI pamoja na TB wameazimia kutembea maeneo yenye mikusanyiko ya watu wengi ikiwemo baa, migodini na mahali penngine ili waweze kuwatambua kiurahisi.
Hayo yameelezwa na serikali ya awamu ya tano kupitia Naibu Waziri wa Wizara hiyo Dkt. Faustine Ndugulile leo Aprili 23, 2018 Bungeni jijini Dodoma kwenye kikao cha 15 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akijibu la nyongeza kutoka kwa Mbunge Masoud Abdallah aliyetaka kufahamu serikali ina mikakati gani katika kutoa elimu maalum ambayo itaweza kuenea kwa kasi zaidi katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu wengi zaidi.
"Serikali baada ya kuona kumekuwa na changamoto kubwa sana katika utambuzi wa makundi maalum ambayo wengi wamekuwa wakiathirika na ugonjwa wa TB na UKIMWI. Hivyo tumeamua kujielekeza kutoa elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari lakini vilevile tuna mkakati mahususi wa kuwatafuta wagonjwa wa TB katika migodi sambamba na hilo tumetengeneza tumetengeneza mikakati jumuishi kati ya ugonjwa wa TB na UKIMWI", amesema Dkt. Ndugulile.
Pamoja na hayo, Dkt. Ndugulile ameendelea kwa kusema "sasa hivi tumeanza kujielekeza mahali kwenye watu wengi ili tuweze kuwapata kwa pamoja hususani wanaume ambapo mara nyingi wanakuwa katika bar. Msishangae kutuona na sisi tunapita huko kuwaomba kufanya upimaji wa suala la ugonjwa wa UKIMWI pamoja na TB".
Kwa upande mwingine, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile amesema kumgundua mgonjwa wa TB mapema na kumuweka katika matibabu ndio njia kuu ya kupambana na kulishinda tatizo la kifua kikuu jambo ambalo lipo kwenye mikakati ya serikali katika kufufua uwezo wa kufikia watu wote wanaohitaji huduma za TB ili kuwagundua mapema na kuwatibu kikamilifu.

Mahakama Yamkuta na Kesi ya Kujibu Wema Sepetu

$
0
0
Mahakama Yamkuta na Kesi ya Kujibu Wema SepetuMahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema msanii Wema Sepetu na wafanyakazi wake wanaokabiliwa na tuhuma za kutumia dawa za kulevya wana kesi ya kujibu, hivyo wataanza kujitetea.
Uamuzi huo, umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya wakili wa serikali, Constantine Kakula kuele
za kuwa kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya uamuzi kama washtakiwa wana kesi ya kujibu ama lah.
Katika uamuzi wake Hakimu Simba amesema kwa mujibu wa sheria kama washtakiwa wakipatikana na kesi ya kujibu watatakiwa kujitetea, pia kama hawana kesi ya kujibu wataachiwa huru.
“Baada ya kupitia hoja zote, mahakama imejitosheleza kwamba washtakiwa wote wana kesi ya kujibu katika mashtaka yote, hivyo wana haki kisheria kuanza kujitetea,” amesema Hakimu Simba.
Baada ya kusema hayo, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi May 14 na 15,2018 ambapo washtakiwa watajitetea mfululizo.
March 23,2018 upande wa utetezi kupitia wakili Alberto Msando, uliwasilisha hoja katika mahakama hiyo kwamba washtakiwa hawana kesi ya kujibu.
Mbali na Wema washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya kutumia dawa za kulevya ni Angelina Msigwa  na Matrida Seleman Abbas.
Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.
Inadaiwa kuwa February 4,2017 katika Makazi ya Wema huko Kunduchi Ununio  washtakiwa hao walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.
Kwa upande wa Wema yeye anadaiwa kuwa February Mosi, 2017 katika  eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam, alitumia dawa za kulevya aina ya Bangi.

Belle 9 Afunguka Alivyompa Jina la Masogange

$
0
0
Belle 9 Afunguka Alivyompa Jina la Masogange
MKALI wa Bongo Fleva, Abednego Damian ‘Belle 9′ ndiye ‘aliyembatiza’ jina la Masogange mrembo maarufu wa kuuza sura kwenye video za wasanii, marehemu Agness Gerald.
Kabla hawajakutana na kumuuzisha sura kwa mara ya kwanza katika wimbo wake wa Masogange, wengi walikuwa hawamfahamu Masogange, lakini baada ya wimbo huo, kila mmoja aliweza kumjua kutokana na kuutendea haki wimbo huo.

Mbali na kuuza sura, Masogange alikuwa na sifa ya ziada iliyowafanya wasanii wengi wavutiwe kufanya naye kazi. Muonekano wake ulikuwa kivutio kikubwa na hapo ndipo umaarufu wake ulipozidi kushika kasi kama moto wa kifuu.
Katika makala haya, tumezungumza na Belle 9 ambaye amefunguka mambo mengi kuanzia walipokutana, hadi kufanya video yake ya Masogange na jinsi alivyoguswa na kifo chake kilichotokea Aprili 20, mwaka huu katika Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar

Habari Njema, Daraja la Nyerere Laingiza Bilioni 14.9

$
0
0
Daraja la Nyerere Laingiza Bilioni 14.9
Daraja la Nyerere, Kigamboni Dar es Salaam limeingiza Tsh. Bilioni 14.9 kwa kipindi cha July 2017 hadi March 2018.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa hivi karibuni kwenye mkutano mkuu wa Baraza la wafanyakazi wa shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), makusanyo hayo ni wastani wa Sh. milioni 650 kwa mwezi. Makusanyo hayo yametokana na wastani wa magari 10,393 yanayopita kwa siku.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara alisema mafanikio hayo yametokana na uamuzi wa kusimamia uendeshaji wa daraja hilo kwa kutumia wafanyakazi wake.
“Kutokana na uwekezaji huo shirika linategemea kupata jumla ya Sh. bilioni 14.53 zitakapoiva. Kwa maana hiyo mpaka sasa thamani ya makusanyo ni sawa na shilingi bilioni 29.4,” alifafanua.
“Mtindo huu wa uendeshaji (kutumia wafanyakazi wa shirika) unatoa uhakika wa kuendesha daraja kwa faida pamoja na kurudisha fedha za wanachama,” alisema.

Daraja la Nyerere lenye urefu mita 680 lilizinduliwa Aprili 19, 2016 na Rais John Magufuli, ujenzi wake ulianza mwaka 2012 na kufanywa na kampuni ya China Railway 15 Group ikishirikiana na kampuni ya China Bridge Engineering Group ambapo ujenzi wake uligharamiwa na serikali kwa asilimia 40 na NSSF kwa asilimia 60.

Hii Hapa Tarehe Ambayo TTF Itakayowakabizi Yanga Milion 600 za CAF

$
0
0
Hii Hapa Tarehe Ambayo TTF Itakayowakabizi 600 M za CAF
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeibuka na kusema kuwa Klabu ya Yanga itakabidhiwa fedha zao za kuingia hatua ya makundi ya Caf mara baada ya kumalizika hatua hiyo na si sasa kama wadau wengi wanavyodhania kuwa watapata mara baada ya kuingia katika hatua hiyo.

Yanga imefanikiwa kuingia katika hatua ya makundi mara baada ya kuiondoa Wolaitta Dicha ya Ethiopia kwa jumla ya mabao 2-1, na watavuna kiasi cha shilingi milioni 600 kama wakimaliza katika nafasi ya nne.
Aidha makundi ya michuano hiyo tayari yameshatangazwa juzi Jumamosi ambapo im­epangwa Kundi D ikiwa ni pamoja na Gor Mahia ya Kenya, Rayon Sport ya Rwanda na USM Alger ya Algeria.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ephraim August, amesema kuwa, Yanga haiwezi kukabidhiwa fedha zake sasa kwa kuwa haiju­likani itamaliza nafasi ya ngapi, kwani kadiri inavyomaliza nafasi za juu, ndivyo fedha zinavyoongezeka.
“Milioni 600 ambayo inatajwa Yanga kuzipata baada ya kuingia hatua ya makundi, iwapo watamaliza mi­chuano hiyo wakiwa wa mwisho kwenye kundi lao na iwapo watapanda na kumaliza wa pili kutoka chini, watapata milioni 750 na wakipiga hatua na kumaliza wa tatu kutoka chini watapewa milioni 850.

“Bingwa ka­tika michuano ya Caf anaibuka na kitita cha shilingi bilioni 2.8, mshindi wa pili bilioni 1.2 na nusu fainali atachukua bilioni 1,” alisema.
Aliongeza: “Caf ha­wawezi kutoa fedha sasa hivi kwa kuwa hakuna anayejua timu ipi itamaliza katika nafasi ya ngapi, na vilevile hawatoi kabla kwa kuhofia timu inaweza kutoshiriki michuano.”
Khadija Mngwai, Dar es Salaam.

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu

 Bonyeza Hapa Chini

==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>  

Mwigizaji Rammy Galis ajitetea kuzimia akiwa kashikilia kitambaa msibani kwa Masogange

$
0
0
Baada ya picha yake inayomuonyesha kazimia huku kashikilia kitambaa mkononi kuibua gumzo jana mitandaoni, msanii wa filamu, Rammy Galis ameeleza kuwa hakuwa amezimia ila alijisikia kuishiwa na nguvu.

Galis alikuwa mmojawapo wa watu waliobeba jeneza la marehemu Agnes Gerald 'Masogange’ katika shughuli za kuuga mwili zilizofanyika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam jana Jumapili, Aprili 22.

Galis amesema kutokana na kusimama muda mrefu wakati wa shughuli za kuuaga mwili alijikuta akiishiwa nguvu na kuomba msaada kwa wenzie wamuondoe eneo ilipokuwa inafanyikia shughuli hiyo.

"Unajua nilisimama sana tangu tunapofikisha mwili pale viwanjani mpaka watu wanaanza kuaga, nadhani kutokana na hilo nikajikuta naishiwa nguvu, hivyo niliwafahamisha wenzangu kwamba sijisikii vizuri na kuomba waniondoe eneo lile,”

“Hivyo pamoja na wao kuamua kunibeba sio kwamba nilikuwa eti nimepoteza fahamu na ndiyo maana hata kitambaa bado niliweza kukishikilia naomba watu waelewe hivyo na kuacha kunisema kuwa nilikuwa naigiza siwezi kufanya hivyo katika msiba," amesema msanii huyo aliyewahi kutamba kwenye filamu ya Chausiku.

Mbali ya kucheza filamu ya Hukumu na Masogange enzi ya uhai wake,Galis pia alishawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na marehemu  uliodumu kwa mwaka mmoja (2016-2017).

Masogange aliyefariki Machi 20 mwaka huu akiwa anapatiwa matibabu hospitali ya mama Ngoma, anatarajiwa kuzikwa leo Jumatatu, Aprili 23  jijini Mbeya.

Tetesi: Aliyewahi kuwa Beki wa Simba SC, Abdi Banda kumuoa dada yake Ali Kiba

$
0
0
Tetesi za Kitaa zinasema Abdi Banda anatarajia kufunga ndoa na dada ake Kiba, Zabibu baadae mwaka huu, hii ni baada ya kaka yake kufunga ndoa. Pongezi kwake Abdi Banda

Abdi Banda kwa sasa anachezea timu moja huko South Africa,ila aliwahi kuichezea simba sc

Viwanja vya Makazi Vinauzwa Bunju Bei Nafuu

$
0
0

Plots for sale: BUNJU
Viwanja vipo Kimele, km 5 kutoka Bunju sokoni na km 3 kutoka main Road (Bunju to Bagamoyo road).
vipo viwanja ukubwa wa 20/30, 20/40, 35/40 na 60/40 na bei zake ni mil 7, 9, 15 na 25 respectively. Bei zote ni negotiable.
call/watsap 0757489709

Kutana na Mtabibu Mongwa Mganga wa Waganga...Sasa Anapatikana Mikoa Yote...

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU MONGWA MGANGA WA WAGANGA SASA WAKO MIKOANI KARIBU YOTE NCHINI...
.
HIVYO WATATOA TIBA MAENEO YOTE YA MBEYA ,DODOMA, IRINGA , MOROGORO, MWANZA,ZANZIBAR

==>KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA

➖Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote

➖ tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .

➖natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
➖natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini

➖ kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa

➖kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri

Piga simu
+255 764291657
+255 764291657
+255 764291657
+255 764291657

Mbeya Yasimama Mamia Wajitokeza Kuupokea Mwili wa Masogange

$
0
0
MAMIA ya wananchi wakazi wa Utengule, Mbalizi na maeneo ya karibu wamejitokeza kuungana na familia, ndugu, jamaa, marafiki na wasanii kuupokea mwili wa msanii Agnes Gerald ‘Masogange’ ambao umewasili kijijini kwao kwa ajili ya mazishi.

Mwili wa marehemu umewasili kijijini hapo mapema leo baada ya jana kuagwa katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.

Masogange alifariki dunia Ijumaa iliyopita katika kituo cha Huduma za Afya cha Mama Ngomakilichopo Mwenge jijini Dar ambapo jana aliagwa katika Viwanja vya Leaders na kusafirishwa kwenda kwao kuzikwa.

Suala la Tsh. Trilioni 1.5 Professor Jay alipeleka kwa Mhe. Shonza

$
0
0
Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule ‘Professor Jay’ amehoji sababu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kumiliki viwanja vikubwa vya michezo wakati kuna uwaba wa viwanja hivyo kwa wanamichezo.

Akiuliza swali Bungeni leo April 23, 2018 amesema tatizo la wanamichezo wa Tanzania ni viwanja kukosa ubora na anafikiri Tsh. Trilioni 1. 5 (zinazodaiwa kupotea) zingeweza kupunguza changamoto hiyo.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amesema sera ya michezo ya mwaka 1995 inahamasishwa wadau, vyama, taasisi kumiliki viwanja vya michezo.

“Kwa hiyo viwanja vyote vinamilikiwa kwa uhalali, ni haki yao na hakuna kiwanja hata kimoja kimeporwa na Chama cha Mapinduzi,” amesemaMhe. Shonza.

Utakumbuka April 20, 2018 wakati Rais Magufuli akiwaapisha majaji Ikulu Dar es Salaam alisema katika ripoti aliyopokea kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad haikuwa na upotevu wa fedha Tsh. Trilioni 1.5 kama inavyodaiwa bali ni watu wanatumia uhuru wao vibaya na kupotosha kitu kilicholeta taharuki.

Bongo5

Wema Sepetu Afarajiwa, ‘Kuitwa Mama sio Lazima Uzae’

$
0
0
Msanii wa filamu Bongo, Wema Sepetu ameelezwa kitendo cha kutopata mtoto hadi sasa kisimkatishe tamaa kwani wakati wake utafika Mungu akipenda.

Hayo yamesemwa na Mjasiriamali, Maznat Bridal ambapo amemueleza Wema kuwa kuitwa mama sio lazima awe na mtoto. Kupitia ukurasa wake Instagram ameandika;

“Kuitwa mama siyo lazima uzae, ukifikia umri tu wa kuitwa aunt, mama mdogo, shangazi, mama mkubwa ina maana wewe tayari ni mama. Kuwa mama siyo lazima uingie labour, mimi namshukuru Mungu nimezaa na nimelea watoto wangu na wasio wangu na katika yote nimejifunza kupenda watoto kwa dhati pasipo kubagua,” amesema.

“Mungu ni msiri sana sana mdogo wangu Wema Sepetu anajua nini kinamstahili nani, kwa muda gani, muda wa Mungu ukifika ataku suprise, atakupa faraja ya ajabu, atakupa kile moyo wako unahitaji, atakutunuku zawadi ya kipekee…utabaki mdomo wazi, ukishangaa maajabu ya Muumba. Jipe moyo, it is well,” amesisitiza.

SOMA Pia: Nafasi za ajira zilizotangazwa Leo

September mwaka jana Wema Sepetu alieleza kuwa amekuwa akihitaji mtoto toka akiwa na umri wa miaka 24 hadi sasa ila hilo haliwezi kumkatisha tamaa. February 2016 wakati Wema akiwa katika mahusiano na muigizaji Idris aliweka wazi kubeba ujauzito wa watoto mapacha hata hivyo baadaye ujauzito huo uliripotiwa kuharibika.

Msuva Aendelea Kung’ara Morocco, Azidi Kuipa Ushindi Difaa El Jadid

$
0
0
Mshambuliaji wa Taifa Stars na klabu ya Difaa El Jadid, Simon Msuva ameendelea kung’ara kwenye ligi kuu ya Morocco.

Mshambuliaji huyo jana (Jumapili) amefanikiwa kuifungia timu yake hiyo bao moja kati ya ushindi wa mabao 2-1 walioupata katika ligi kuu dhidi ya Raja Casablanca.

SOMA Pia: 3 Job Opportunities at TANROADS Tanzania, Weigh bridge Operators

Msuva alifanikiwa kufunga bao hilo kwa kichwa dakika ya 76 ya mchezo huo huku goli la kwanza likifungwa na Ahaddad H dakika ya 45. Wakati huo huo bao la Raja Casablanca lilifungwa wa njia ya penalti na Iajour M dakika ya 41 ya mchezo huo.

Mchezo huo uliocheza kwenye uwanja wa Stade Ben Ahmed El Abdi (El Jadida (Mazghan)).

Mmiliki wa Shule ya St. Patrick Kumsomesha Mpaka Chuo Kikuu Mtoto wa Masogange

$
0
0

Mbeya. Mmiliki wa Shule ya Sekondary ya St. Patrick ya jijini Dar es Salaam, Ndele Mwaselela amejitolea kumsomesha mtoto wa marehemu Agnes Masogange, Sania(11) kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne na akifaulu hadi chuo kikuu.

Hii ni neema nyingine kwa mtoto huyo wa pekee wa Masogange aliyemuacha, baada ya jana kamati ya maandalizi ya mazishi kupitia mweka hazina wake, Zamaradi Mketema kueleza kuwa wamemwekea Sh2 milioni zilizobaki katika michango ya msiba huo kwenye akaunti yake.

Zamaradi amesema fedha hizo zimewekwa mahususi kwa ajili ya kumsaidia kianzio katika cha ada atakapoanza kidato cha kwanza mwakani kwa kuwa mwaka huu anatarajiwa kumaliza darasa la saba.

Akizungumza leo Jumatatu Aprili, 23 katika shughuli za mazishi, zilizofanyika nyumbani kwa baba wa Masogange, Kijiji cha Utengule, Wilaya ya Mbalizi, Mwalesela amesema mbali ya kumsomesha pia mtoto huyo atakaa hosteli kwa gharama zake kwa muda wote wa masomo yake.

“Akifaulu kidato cha nne pia atasomeshwa na mimi hadi kidato cha tano na sita lakini pia akifaulu atakwenda hadi chuo kikuu,” |amesema.

Kutokana na maamuzi hayo, alimtaka msanii Irene Uwoya ambaye mtoto wake naye anasoma katika shule hiyo, kuhakikisha anapokwenda kumsalimia mwanaye awe anakwenda kumsalimia na Sania.

“Hivyo wewe msanii Uwoya una mtoto wako pale shuleni kwangu naomba ukija kumuona hakikisha unamuona na mtoto huyo,” amesema Mwaselela.

Kupiga picha na wasanii kwachelewesha mazishi ya Masogange

Source: MCL

Julius Mtatiro: Kwa Heri Masogange Hatukukutendea Haki Kama Taifa

$
0
0
#Mtatiro J

Ndugu zangu, uvumilivu umenishinda na nikaona lazima niandike jambo. Ni kawaida yetu kwenye taifa letu kuandika kurasa nyingi za wasifu wa wanasiasa, watumishi wa umma "waliotukuka", matajiri na watu tunaodhani waligusa maisha ya jamii kwa njia sahihi kila wanapofariki.

Ni kawaida yetu pia kuwahukumu marehemu wengine, bila kuwajua, wakifa tunaishia kutangaza yale tuliyodhani ni maovu yao bila kujiuliza tuliweka mchango gani kwao.

Wapo watu wengine hufa, tukadhani hawana maana, ni wadhambi, hawana mchango kwenye jamii na hawapaswi kuigwa hata kidogo. Kumbe vifo vyao ni kioo kikubwa cha maisha yetu, ni funzo kubwa na ni tafakari halisi ya sisi ni nani.

Tangu dada yetu Agnes Gerald (Agnes Masogange) afariki, nimeona kwenye mitandao mingi watu wakimzungumzia vile watakavyo. Hiyo ni kawaida. Sehemu kubwa ya wanaomzungumzia wanaeleza namna ambavyo hakuishi maisha mema na hakuwa kioo cha jamii.

Mimi sikuwahi kukutana na Agnes zaidi ya kumuona mitandaoni, mara ya kwanza kupitia video ya mwanamuziki "Bele 9", tangu hapo nilimuona kama msichana mwenye vituko na visa vingi, tangu kuchezesha viungo vyake bila nguo hadi kuhusishwa na tuhuma za madawa ya kulevya.

Katika safari yote hiyo binafsi sikuwahi kumhukumu, maana nilijua chanzo cha yote hayo ni kukosa elimu bora (ya darasani), elimu bora ya uraia na elimu bora ya maadili. Chanzo cha kukosa vitu hivyo ni familia yake, ndugu zake, marafiki zake, serikali yake na wote tuliomzunguka.

Kwa kipaji cha Agnes, tangu kinachomozwa kwenye wimbo wa Bele 9, umbo lake na haiba yake - kama tungelikuwa na taifa lenye maandalizi na vijana walioandaliwa, Agnes tumuagaye na kuelekea kumzika labda angelikufa akiwa Agnes mshindi wa tuzo ya Oscar kwenye Muziki, Uigizaji, Uhamasishaji Jamii, Uburudishaji n.k.

Lakini tunaenda kumzika Agnes na vipaji vyake sahihi ambavyo aliwahi kuvichomoza, vikageuzwa kuwa faida kwa wengine kwa njia nyingine, vikaharibiwa, akavishwa taswira ya picha chafu mitandaoni na madawa ya kulevya.

Naamini, kipaji cha Agnes kilipochomoza tu, wajanja walimuwahi, wengine wakiwa watu wakubwa tu, wengine wakiwa na nyadhifa kubwa tu, wengine wakiwa na elimu kubwa tu, wengine wakiwa na fedha nyingi tu na wengine wakiwa na vipaji vikubwa zaidi.

Dada yetu huyu najua alikimbiliwa na kutumiwa na sisi sisi, kila mmoja wetu akimtumia kwa maslahi yake.

Agnes aliwahi kukutwa na kemikali ambazo haziruhusiwi kusafirishwa, alikamatiwa Afrika Kusini, baadaye aliachiwa. Zile kemikali zilikuwa ni za nani? Kwa alimpa Agnes? Je tulimfuatilia (maana naambiwa yuko hapa Tanzania) na ni mtu mkubwa tu, ana hela nyingi tu na ana elimu ya kutosha! Taifa zima likamhukumu Agnes, tukamuita muuza madawa; mtu mwenye mamlaka (mmiliki wa kemikali hizo) hadi leo anatembea barabarani akitamba, Agnes yuko kwenye jeneza na jamii ikihukumu matendo yake!

Kuna wakati video ya Agnes ilionekana mitandaoni akiwa anacheza na nguo za ndani tu. Aliyekuwa anarekodi video ile alikuwa anampa maelekezo "...bebi sogea hivi, cheza hivi, fanya vile..." Agnes anatekeleza!

Video ile ikazua gumzo, bila shaka aliyeilikisha mitandaoni kwa sababu zozote zile ni huyu mwanaume ambaye anaweza kuwa mpenzi wa wakati huo wa Agnes. Kwa kutojali na kutotambua umuhimu wa vijana wetu (serikali/taifa), hatukuwahi kusikia mwanaume huyo amehojiwa, hatukuwahi kusikia akihukumiwa na hatukuwahi kuona Agnes akilipwa fidia ya udhalilishaji ule uliomuonesha kama msichana mdhambi. Sana sana ambaye alitukanwa na kuhukumiwa na taifa ni Agnes, huyo mwanaume yuko "SALAMA!" na huenda anaendelea kurekodi wasichana wengine.

Tumo kwenye taifa ambalo halijui kulinda vijana wake kwa kutatua mizizi na vyanzo vya matatizo yao. Tumo kwenye taifa ambalo, vijana wanakamatwa kwa tuhuma za kutumia madawa ya kulevya huku wasambazaji na wenye mitaji ya uingizaji wa madawa hayo wakiwa ni wafadhili wakubwa wa vyama vyetu na kutusaidia kuingia serikalini. Sisi ni wapumbavu sana!

Upumbavu wetu ndiyo unafanya vijana wetu wanakufa na vipaji vyao huku sisi kama taifa tukiendelea kushindwa kuwanyanyua na kuwasaidia, sana sana tukiingilia vipaji vyao, tunavitumia kwa maslahi yetu, waje kuimba kwenye matamasha na wawe wanachama wa vyama vyetu, na huko tunawatumia tutakavyo, mwisho wa siku hawatambuliki.

Ndiyo maana kwa hawa wasanii wetu, ni wachache mno ndiyo wana mafanikio, wengi wamo kwenye sanaa kuwanufaisha watu wengine. Angalia wachezaji wetu, wengi hustaafu michezo yao wakiwa hawajui watakula nini. Sababu ya yote haya ni taifa letu kutokuwa na mpango unaotekelezeka wa kuwasaidia vijana kuinuka kutoka chini ni kung'arisha vipaji vyao.

Kifo cha Masogange kimeniumiza kwa sababu kinajenga taswira za maisha ya ndani ya vijana wengi wa taifa letu, taswira ya kutwishwa mizigo mizito wakiwa wadogo, kuharibiwa, kutelekezwa, kujitafutia maisha, kuonesha vipaji vyao na vipaji hivyo kutumiwa na watu wengine kwa manufaa ya watu hao huku vijana wetu wakibaki na taswira hasi na kuonekana ni wavunja maadili.

Namheshimu Binti Agnes kwa sababu naamini hakupaswa kufa akiwa Masogange huyu atafsiriwaye na watu wenye mitizano hasi. Naamini Agnes alinyimwa fursa na usimamizi wa kila mtu (familia, marafiki, ndugu na taifa).

Nimemuona Baba ya Agnes akisema alikosana na mwanaye tangu alipopata ujauzito na kuacha shule akiwa kidato cha 2. Baba ya Masogange alijua kuwa "...mtoto wako akipata mimba shuleni suluhisho ni kumfukuza nyumbani", ndivyo mababa wengi wa zamani waliamini na ndivyo hata baadhi ya viongozi wakubwa wa sasa wanaamini. (Yupo kiongozi amesema mwanafunzi akipata mimba asisomeshwe tena).

Pamoja na kuishia kidato cha pili na kutelekezwa na familia yake naambiwa ya kuwa, hata baba ya mwanaye alimtelekeza. Masogange akaanza kupambana kivyake.

Video ya Bele 9 ikamtambulisha kwa watanzania, alirudi na kusimama kwa msaada wa watu wema lakini tokea hapo akakosa usimamizi na menejimenti.

Kama kipaji cha Diamond kisingepata usimamizi, Diamond angelikuwa anaomba dua kupata nauli ya daladala, yeye mwenyewe Diamond mara kadhaa amesema kuna watu wamemnyanyua sana.

Lakini Agnes najua kuna watu wamemdidimiza sana, wamemuumiza sana, wamemtumia sana na wamempa matatizo makubwa sana - wengine kati ya watu waliomuumiza watakuwa msibani kwake wakishughulikia usafiri, chakula, matangazo....wengine watafika kuchangia maziko yake lakini walimuumiza sana na ama walifurahi sana wakati walidhani anazama alipokuwa hai. Ni kawaida yetu!

Wako watu wanaamini "wewe binafsi ndiye wa kulaumiwa kwa maisha yako", ni kweli kabisa, lakini wanasaikolojia wanajua "wewe ni wewe hivi sasa kwa sababu ya jinsi ulivyoathiriwa na mazingira uliyomo." Watu ulionao, familia uliyonayo, ndugu zako, taifa lako, marafiki zako n.k ni vyanzo vikubwa vya kukufanya wewe uwe nani.

Dada yetu Masogange ni matokeo ya yote niliyoyataja hapo juu. Yeye ni tunda letu, ni dada yetu, mtoto wetu, mwenzetu.

Agnes ni taswira yetu halisi. Kama tunadhani yu mdhambi, basi sisi ni wadhambi mara 100. Kama tunadhani hafai, basi sisi hatufai mara 100 - yeye ni zao letu sisi, ni zao la mazingira yetu, zao la mipango yetu kwa vijana wetu, zao la roho zetu.

Wakati tunamzika Agnes tukumbuke maisha aliyokuwa anaishi ndiyo wanaishi vijana wetu wengi kwenye taifa letu, mapito aliyopitia hadi mwisho ndiyo safari ya maisha ya vijana wetu wengi, tabu, mateso, usumbufu, shida, kutengwa, kutwezwa, kudhalilishwa, kuumizwa, kutumiwa na kulaumiwa kwa yote hayo - ndiyo maisha wanayopitia vijana wetu wengi na hasa wasichana wa taifa hili.

Nimemsikia baba ya Agnes akisema mwaka jana na hadi mwaka huu binti yake alimweleza kuwa anajipanga kumfanyia mambo makubwa. Agnes akamsisitiza baba yake kuwa siku hizi (yeye Agnes) amebadilika mno, ameachana na maisha ya hovyo na ana shabaha ya kulinda nidhamu na kutafuta mafanikio.

Kwa mtizamo wangu, Agnes amekufa kifo cha amani na matumaini makubwa kwake na kwa Mungu wake. Halafu naamini Agnes alikuwa mdhambi kama sisi woote, na labda sisi wengine tumewahi kufanya dhambi kubwa kumshinda, yeye anahukumiwa sana kwa sababu alikuwa maarufu kiasi chake, alikuwa socialite, video queen na msanii.

Wasanii wetu (hasa wa kike) wajifunze kupitia maisha ya Agnes, wajipange, wajenge nidhamu, wachague marafiki wenye faida, wakuze sanaa zao ndani ya menejimenti imara, wasikubali kutumiwa na watu wenye fedha, wanasiasa wenye mamlaka yoyote na hasa wanaume.

Familia zetu, ndugu, jamaa, marafiki, taifa zima..sote tujifunze na tusikimbie majukumu yetu, tusitose wajibu wetu.

Nawapa nukuu hii kutoka Yohana.8:7-9
“Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati. ”

Nawakumbusha ya kwamba, wale wanaodhani Agnes alikuwa mwovu wajichunguze mara 7 zaidi, watagundua wao ni wadhambi kuliko marehemu. Agnes ni tunda letu, na kama kuna makwazo aliipa jamii yetu basi hayo ni malezi yetu.

Binti huyu amemaliza safari yake, ametuachia mafunzo makubwa sana. Taswira yake ya ndani ya yeye na Mungu wake inaweza kuwa utukufu mkuu ambao binadamu hatuna jicho la kuuona. Kifo chake kimenigusa mno ndiyo maana nimempa heshima hii.

Mungu wa Mbinguni ampokee, amsamehe dhambi zake! Sisi tuliobaki tunajua wajibu wetu, tumsitiri, na kama hapo kabla ulisambaza picha zisizo na maadili, kama umemaliza kusoma andiko hili, zifute, maana Yesu angelikuuliza "Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe".

By Mtatiro J,
(+255787536759, juliusmtatiro@yahoo.com)

Masogange Azidi Kumtesa Rammy Galis Pale Anapoona Jeneza Lake

$
0
0
Masogange Azidi Kumtesa Rammy Galis Pale Anapoona Jeneza Lake
KUFUATIA msiba wa msanii Agnes Gerald ‘Masogange’, msanii mwenzake Rammy Galis amekuwa mtu wa huzini, kulia na majonzi mazito hasa wakati anapoona jeneza lenye mwili wa marehemu.



Baada ya mwili wa marehemu kufika nyumbani kwao maeneo ya Utengule, Mbalizi mkoani Mbeya, msanii huyo alionekana kukosa raha na huku wasanii wenzake wakimsihi apunguze mawazo na ajipe moyo hasa katika kipindi hiki cha majonzni.



Rammy ambaye aliwahi kuwa mpenzi wa Masogange, jana alianguka na kuishiwa nguvu wakati akiaga mwili wa marehemu katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.



Masogange alifariki dunia Ijumaa iliyopita katika kituo cha Huduma za Afya cha Mama Ngomakilichopo Mwenge jijini Dar ambapo jana aliagwa katika Viwanja vya Leaders na kusafirishwa kwenda kwao ambako amezikwa leo.

Bora Masogange Alishahukumiwa- Wema Sepetu

$
0
0
Image result for wema na masogange


Malkia wa Bongo Muvi, Wema Sepetu, amefika tena mahakamani leo kusikiliza kesi inayomkabili ya matumizi ya madawa ya kulevya, ambpo amesema upande wa mashtaka wameshawasilisha maelezo yao na umebaki upande wao kuweza kujitete ambapo kesi hiyo imesogezwa mbele mpaka mwezi Mei.

Akiwa mahakamani hapo Wema amesema hana matumaini yoyote juu ya kesi yake isipokuwa anasubiri sheria ifuate mkondo wake, huku akisema ni bora Marehemu Agness Masogange alifanikiwa kumaliza kesi yake na akatozwa faini, lakini kwa upande wake anasubiri tu sheria ifanye kazi yake.

Baada ya Ndoa ya Alikiba Mbasha Ajiweka kwa Jokate " Usihofu Yetu Inakuja"

$
0
0
Baada ya Ndoa ya Alikiba Mbasha Ajiweka kwa Jokate " Usihofu Yetu Inakuja"
Baada ya msanii Alikiba kuoa, maneno mengi na maswali yamekuwa yakielekezwa kwa mrembo Jokate Mwegelo.

Sababu ni kwamba mara kadhaa mrembo huyo alidaiwa kuwa katika mahusiano na Alikiba, hivyo kitendo cha Alikiba kuoa mwanamke mwingine kilizidi kuibua mijadala ya hapa na pale kuhusu Jokate.

Soma Pia; Jokate amuandikia Alikiba barua kutoka kwenye sakafu ya moyo wake

Sasa muimbaji wa nyimbo za Injili nchini, Emmanuel Mbasha amemuelezaJokate kuwa asijali kwa kuwa ndoa inakuja, hata hivyo haijafahamika iwapo ni yao wawili au laa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

“Usihofu Mungu hajakuacha Jokate Mwegelo yakwetu inakuja, tv zote zitakuwa live ukumbini hadi wasafi tv,” amesema Mbasha.

Soma Pia; Jokate mbioni kuolewa

Katika kuhadhimisha kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa March 20, 2018 Jokate aliweka wazi kuwa yupo mbioni kuolewa ingawa hakuweka wazi ni nani atahusika katika ndoa hiyo.

Utakumbuka pia muimbaji Mbasha kwa sasa hayupo katika ndoa na hii ni baada ya kuachana na aliyekuwa baby mama wake, Madam Flora ambaye aliolewa April 30, 2017 na Daudi Kusekwa.

Tazama Live Uzinduzi wa Jengo la Capital One na Tawi la NMB Unaofanywa na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanina

$
0
0
 Fuatilia LIVE uzinduzi wa jengo la Capital One na tawi la NMB unaofanywa na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanina, Mh. John Pombe Magufuli mjini Dodoma.
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images