Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Yanga Yakabidhiwa Uwanja Dodoma

$
0
0
Yanga Yakabidhiwa Uwanja Dodoma
Klabu ya Mabingwa watetezi Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imefunguka na kudai wamekabidhiwa kiwanja chenye takribani hekari 50 Mkoa Dodoma kwa lengo la ujenzi wa 'academy' itakayokuwa inakuza vipaji vya vijana wadogo nchini Tanzania.


Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na uongozi huo kupitia ukurasa wao maalum wa kijamii asubuhi ya baada ya kumaliza shughuli za ufunguzi wa tawi la jipya la Yanga katika makao makuu ya nchi, mkoani Dodoma. 

"Wanachama wa Yanga tawi la Dodoma Makao Makuu kupitia mlezi, Naibu waziri wa kazi, vijana na Ajira , Antony Mavunde, wametoa eneo la hekari 50 kwa Yanga SC kwa ajili ya ujenzi wa 'academy' ya klabu itakayokuwa na jukumu la kutafuta, kukuza na kendeleza vipaji kwa vijana wadogo ili waje kuwa wachezaji wakubwa wa Yanga katika siku za usoni", imesema taarifa hiyo.

Kwa upande mwingine, matumaini ya Yanga SC kutetea ubingwa wake wa Ligi kuu Tanzania Bara yamezidi kuonekana kuwa hafifu baada ya jana Aprili 22, 2018 kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na wenyeji, Mbeya City uwanja wa Sokoine na kusababisha kuwa na alama 48 katika mechi 23 huku wakiwa wamezidiwa alama 11 na watani wao wa jadi Simba SC wenye pointi 59 za mechi 25 na wababe hao watakutana Jumapili uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Rais Uganda Aonya Wanaotumia Ulimi Kufanya Mpenzi na Wanawake

$
0
0
Rais Uganda aonya wanaotumia ulimi kufanya mapenzi na WanawakeRais Yoweri Museveni amewaonya wananchi wa Uganda dhidi ya vitendo vya kutumia mdomo katika kufanya mapenzi, akisema "mdomo uliumbwa kwa ajili ya kula na si mapenzi".
Rais huyo wa muda mrefu nchini Uganda amesema utamaduni huo wa kutumia mdomo katika mapenzi uliletwa na wageni.

“Nichukue nafasi hii kuonya watu wetu hadharani dhidi ya vitendo visivyo sahihi vilivyoletwa na vinavyoendelezwa na wageni. Mojawapo ni mapenzi ya kutumia mdomo. Mdomo ni kwa ajili ya kula si mapenzi.” Museveni alisema hayo wiki iliyopita wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliorushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni.

Vyombo vya habari vya Uganda vimeripoti onyo hilo na kuzua mijadala kwenye mitandao ya kijamii, ambako baadhi ya watu wanapingana naye na wengine kumpongeza.

Kauli yake ilitoka siku chache baada ya kusambaa kwa picha zinazomuonyesha ofisa mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Makerere akimnyonya sehemu za siri  mwanafunzi wake ofisini kwake.

Ofisa huyo, anayehusika na utawala, ameshasimamishwa kazi na analipwa nusu mshahara, wakati tukio hilo likichunguzwa.

Tukio hilo lilijulikana baada ya mwanafunzi huyo kusambaza picha alizojipiga wakati ofisa huyo akimfanyia kitendo hicho.

Mwanafunzi huyo alisema ofisa huyo wa Makerere alimbusu sehemu zake za siri kwa nguvu na alipiga picha hizo ili apate ushahidi kwa kuwa ofisi hiyo haikuwa na kamera za usalama.

Mwanaume wa Miaka 69 Akutwa Amekufa Kanisani

$
0
0
Mwanaume wa Miaka 69 Akutwa Amekufa Kanisani
Mwanaume mmoja anayetajwa kuwa na umri wa miaka 69 siku za hivi karibuni amekutwa akiwa amefariki katika Kanisa la Anglicana huki Ngerwe, katika jimbo la Embu nchini Kenya.

Inaelezwa kuwa marehemu Jason Nyaga Njiru alikuwa akifanya kazi kama mlinzi kwenye kanisa hilo. Mwili wake ulikutwa kwenye nyumba ya mbao ambayo iko katika eneo hilo la kanisa ambapo alikuwa akijikinga na mvua zinazoendelea.

Familia iliyomfanya mtoto wao wa kike kuwa ‘wa kiume’

Askari Polisi wa jimbo hilo Mark Wanjala ameeleza kuwa walitaarifiwa na mtoto wa marehemu kuwa baba yake hajarudi nyumbani tangu alipokwenda kazini jana yake usiku.

Hata hivyo mwili wa marehemu haujakutwa na majeraha yeyote na tayari umekwenda kuhifadhiwa hospitali.

Mke wa Mwana wa Mfalme wa Uingereza Amejifungua Mtoto wa Kiume

$
0
0
Mke wa Mwana wa Mfalme wa Uingereza Amejifungua Mtoto wa Kiume
Mtoto huyo ambaye atakuwa kitukuu wa sita wa malkia, amezaliwa katika hospitali ya St.Mary iliyopo Lindo Wing huko mjini London .

Hali ya afya ya mama na mtoto inaendelea vizuri .

Ujio wa mtoto wa tatu wa mwana wa Mfalme na mke wake Catherine amezaliwa saa saa saba majira ya Afrika mashariki.

Image caption
Ukoo wa Malkia wa Uingereza
Familia zote wamepata taarifa ya ujio wa mtoto huyo na wanafuraha kwa habari hizo njema.

Wenger Awatupia Lawama Mashabiki kwa Kukosa Umoja

$
0
0
Wenger Awatupia Lawama Mashabiki kwa Kukosa Umoja
Mara baada ya meneja wa Arsenal, Arsene Wenger siku ya Ijumaa kutangaza kuondoka ndani ya klabu hiyo mwishoni mwa msimu, Jumapili hii amewatupia lawama mashabiki kwakukosa umoja hali inayopelekea kuaribu taswira ya timu hiyo.





Kwa mara ya kwanza jana siku ya Jumapili, Wenger ameeleza sababu ya maamuzi yake ya kuachia ngazi ambapo amesema kuwa hakuchoka kuifundisha timu hiyo bali aliamua kufanya hivyo baada ya kuona baadhi ya mashabiki wakiandamana wakimuhitaji aondoke jambo ambalo limekuwa likimuumiza na kuvuruga taswira ya klabu.

Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 68 hapo jana aliamua kuweka wazi sababu zilizomfanya kumaliza ukomo wa utawala wake wa miaka 22 ndani ya klabu ya Arsenal.

Sikuchoka kuifundisha Arsenal, wenga ameyasema hayo mara baada ya kupata ushindi wa jumla ya mabao 4 – 1 dhidi ya West Ham.

Sikuchoka kuifundisha Arsenal, binafsi ninaamini hii klabu inaheshima dunia nzima, ni zaidi hata ya Uingereza. Mashabiki wetu hawana umoja na hivyo kujenga taswira mbaya kwa klabu jambo ambalo linaniuma, taswira hii tunayo ijengea timu yetu siyo kitu ambacho mimi nakipenda.

Sifanyi hivi kwa kutengeneza vichwa vya habari vya kijinga, nahitaji kile ninachokifikiria kwenye klabu yangu kifanikiwe na hicho ndiyo kitu muhimu pekee  kwangu.

Nimesafiri sana na klabu hii na kujionea namna inavyoheshimika duniani, tunaangushwa kwa namna tunavyocheza, kwa namna ya tabia zetu zilivyo kwa sasa na vile tunavyo wafanya watu watuchukulie hivyo nahitaji kuondoka na kuiacha taswira ya timu ikiwa kwenye muonekano mzuri. Ijapokuwa kuna fedha nyingi kwenye mchezo zaidi hata ya matokeo ya uwanjani.

Wenger amejiunga na Arsenal mwaka 1996  akiwa ni meneja wa pili kutoka nje ya Uingereza au Ireland kupata nafasi ya kuzinoa timu za nchi hiyo na kuisaidia kwa kiwango kikubwa mabadiliko ya soka Epl.

Akifanikiwa kutwaa taji la ligi akiwa na Arsenal mwaka 1998, 2002 na 2004 bila kufungwa ‘Invincibles’ msimu mzima huku ikifanikiwa kuvutia mashabiki.
Wenger amesema kuwa mchezo ni zaidi ya kushinda au kufungwa kiasi kwamba anadhani kubwa kwake ni kuhakikisha anatanua wigo kwa timu hiyo kwa watoto wanaopenda soka Afrika, China,  America. na lengo lake kubwa ni kuzalisha vipaji kwa vijana wadogo.

Mfaransa huyo amesema kuwa kuna Arsene Wenger mmoja tu uwanja wa Emirates. Ninajiskia furaha pale mashabiki wanapokuwa na furaha.

Najaribu kuvutia miundombinu ya klabu na maendeleo ya mchezaji mmoja mmoja na kuwekeza katika aina ya uchezaji wetu. Ninaamini nitaiyacha timu hii ikiwa na mipango imara na hiyo ilikuwa lengo langu lakini pia kumuachia nafasi mrithi wangu atakae kuja kuchukua nafasi hii na pengine kufanya vema zaidi yangu mimi kwa miaka 20 ijayo, hilo ndilo tarajio langu.

Nafasi kubwa ya Arsenal iliyopo kwa sasa ni michuano ya Europa League hatua ya nusu fainali dhidi ya Atletico Madrid siku ya Alhamisi. Kwa kuwa sasa Arsenal ipo nje ya ‘top four’ kwenye msimamo wa ligi ya Uingereza ikitwaa ubingwa huo itapata nmafasi ya kushiriki Champions League.

Nimetumia miaka yangu 22 ndani ya klabu na niliipatia miaka yenye mafanikio, nilikuja hapa nikiwa na miaka 46 na nilifanya kazi kwa siku saba bila hata kupumzika ni siyo sita bali siku saba kwa wiki nzima. Najua nitapitia wakati mgumu kwenye maisha yangu baada ya kuachana na timu hii lakini nawashukuru sana na nasema kwaherini.

Wenger mpaka sasa hajatangaza kama atakwenda kujiunga na klabu gani licha ya kuwa huwenda asifundishe Uingereza.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?

Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU.

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili, ZINDIKO za Nyumba.

MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA.

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.

Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

WASILIANA NAE:

+255 622588038
0679119679
+255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Ukweli Kuhusu Mapenzi ya Kweli na Pesa....

$
0
0

Siku hizi kumekuwepo na malalamiko sana kutoka kwa wanaume,wakidai kuwa wanawake
Wengi siku hizi wanapenda sana
Kuomba pesa,hali ambayo
Imewafanya wanaume wengi kuamini kuwa mapenzi ni pesa,
Kama hauna pesa huwezi kuwa
Na mwanamke jambo ambalo
Si kweli,leo nataka niwambie

Wanaume wenzangu ni kweli pesa
Ni muhimu katika mapenzi lakini
Mapenzi ya kweli hayana uhusiano
Wowote na pesa,"Mwanamke akikupenda kweli hawezi kuwa na Ujasiri wa kukuomba pesa hata siku moja",Huu ndio ukweli ukimuona Girlfriend wako hana aibu na mwepesi wa kukuomba hela jua
Hapo unaibiwa.


Mwanamke anayekupenda kweli anakuhitaji zaidi wewe katika maisha yake kuliko pesa yako
Lazima aogope kukuomba pesa
Kwa sababu anaogopa usije uka
Mtafsri vibaya na ukamuacha.
Lakini na wewe mwanaume
Unatakiwa ujiongeze kidogo
Umtunze mpenzi wako pale
Unapopata kidogo,mpatie pesa
Japo kuna wengine hujifanya kukataa we mbebeleze mpaka achukue huyo ndio mwanamke
Anaekupenda kweli.


Note:Mwanamke yoyote yule anaekupenda kweli hata awe changudoa hawezi kutanguliza pesa kwenye mapenzi yenu
wewe utapewa papuchi bure na pesa juu lakini wengine watalipia.

Nyaggad

KIMENUKA: Diva Atakiwa Kumlipa Michael Lukindo Milioni 50 Kwa Kumdhalilisha

$
0
0
Msanii wa Bongo fleva na mtangazaji wa Cloud Fm ,Diva Gissele Malinzi maarufu kama "Diva the bawse" ametakiwa kuomba radhi pamoja na kulipa faini ya Tsh.Milioni 50 kwa kosa la kumdhalilisha msanii mwenzake ambaye alikuwa mtangazaji mwenza wa Cloud Fm ,Michael Lukindo.

Diva amepewa agizo hilo na taasisi ya wanasheria ya "East Woods Attorney" ambako Michael Lukindo aliwasilisha madai yake ya kudhalilishwa.

Picha liko hivi
Siku chache zilizopita Michael Lukindo alifanya mahojiano na XXL ya Clouds Fm na alikuwa anatambulisha nyimbo yake mpya ya " Basi Iwe" lakini Kwenye mahojiano hayo alifunguka amewahi kuwa Kwenye Mahusiano na Diva.

Baada ya kusikia taarifa hizo Diva alitumia ukurasa wake wa Instagram na kumwaga povu zito na kukataa kata kata kama yupo Kwenye Mahusiano ya kimapenzi na Michael Lukindo.

Baada ya Tetesi hizo kusambaa Soudy Brown alimsaka Michael ambaye alikiri kuwa alikuwepo Kwenye Mahusiano na Diva lakini walifanya siri na mpaka sasa Diva hayupo tayari kuzungumzia hayo mahusiano.

Baada ya kusikia maneno hayo Diva ambaye kwa muda huo alikuwa studio alimtolea matusi mazito Michael Lukindo:


“Wewe mata** unikome shika adabu yako umeshawahi kuwa na Mahusiano na mimi lini na wapi?na nilikwambia kabisa kwamba nimekushtaki I have defamation letter for you utajifunza kufunga huo mdomo wako sitaki mambo ya kise*** k*** la mama ako umeenda umemzungumzia Jokate on the same same thing haukutosheka ukamuandika Miriam Odemba kuwa una Mahusiano naye sasahivi unataka kwangu mimi kunitafutia kiki sasa mimi ntakukomesha nimeshakushtaki”.

"East Woods Attorney" wamemwamndikia barua Diva ambapo wamemtaka amwombe msamaha mteja wao Michael Lukindo pia amlipe Tsh .Milioni 50 . Diva ametakiwa kufanya hayo ndani ya siku 14 kuanzia tarehe 19 April ,2018.Akishindwa kufanya hayo hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa

Hii hapa barua aliyoadnikiwa Diva na wanasheri wa Michael Lukindo.



Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special, Imeboreshwa zaidi

Watazamaji wa Wimbo wa Belle 9 'Masogange' Waongezeka Ghafla Youtube

$
0
0
Kwanza tupeane pole kwa Msiba wa ndugu yetu Agnes.
Kurudi kwenye mada nimepitia kwenye Youtube Channel na nimegundua watazamaji wengi sana wemeutazama huu wimbo kipindi hichi ili kumuona Agnes au Masogange kama alivyofahimika baada ya kushiriki kwenye wimbo wa video hii.

Kabla ya hapo watazamaji wa huu wimbo na wachangiaji walikuwa wachache wasiofikia hata laki moja. Hivi niandikapo kuna watazamaji zaidi ya laki mbili na nusu na watoa maoni zaidi ya mia nne.

Basi na wewe kama bado hukuwahi kuutazama wimbo huo wa Masogange uliompa umaarufu Marehemu Aggy mpaka akaitwa Masogange nimekuwekea hapa chini utazame

VIDEO:

Paul Makonda Agharamia Mazishi ya Masogange

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amegharamia gharama mbalimbali katika msiba wa Agnes Gerald alimaarufu kama Masogange ambaye amefariki April 20, 2018 na kuzikwa leo April 23, 2018 jijini Mbeya.


Akiongea mbele ya waombolezaji na Mkuu wa mkoa wa Mbeya mchekeshaji maarufu nchini, Emmanuel Matebe Mathias 'MC Pilipili' ambaye ndiye 'MC' wa shughuli za mazishi ya Agnes Masogange amesema kuwa wameona mkono wa serikali katika hilo na kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ndiye aliyefanikisha na kulipia magari ambayo yamewapeleka wasanii mbalimbali Mbeya.

"Mkuu wa mkoa wa Mbeya kuna upendo mkubwa ambao tumeuona kutoka kwenu kwani ulikuwa karibu na sisi muda mwingi, ulikuwa ukitupigia simu kujua tupo wapi hivyo naamini usiku wa leo hujalala kabisaa. Pia tunamshukuru Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwani yeye ndiye aliyelipia magari mawili, matatu ambayo yametuleta hapa Mbeya leo kutokea Dar es Salaam, hata kamati ambayo ilikuwa imeandaa kuanzia kutoa heshima ya mwisho pale Leaders Club ambayo ilikuwa chini ya Steve Nyerere ilipewa nguvu na watu wa serikali tumeona serikali mmetupa support vizuri" alisema MC Pilipili

Mbali na hilo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla aliweza kuwapokea na kutoa neno la shukrani kwa wasanii na watu mbalimbali ambao wameweka tofauti zao pembeni na kuungana kuwa kitu kimoja katika kuhakikisha wanampumzisha salama mwenzao katika nyumba ya milele.

"Mueendelee kuwa pamoja hivi hivi bila kujali tofauti zenu, mabifu yenu mzidi kuwa wamoja kwani hili jambo mmejenga heshima kubwa sana, naomba nitoe pole sana kwa familia kwa msiba huu" alisema Makalla 

Mzee Majuto Azidiwa Tena Na Kurejeshwa Kulazwa Hospitalin

$
0
0
Dar es Salaam. Muigizaji na mchekeshaji wa siku nyingi, Amri Athuman maarufu Mzee Majuto, amelazwa tena katika Hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam, baada ya kuzidiwa.

Mke wa mwigizaji huyo, Aisha Yusufu, ameiambia MCL Digital leo Aprili 23 kwamba mume wake walimpeleka hospitalini hapo leo saa 7:00 mchana.

Aisha amesema kidonda alichofanyiwa upasuaji kimeleta shida, hivyo kumpeleka kwa ajili ya uangalizi zaidi.

Majuto alilazwa hospitalini hapo Januari mwaka huu na kufanyiwa upasuaji wa tezi dume.

Source: Mwananchi

Kutana na Mtaalam wa Matabibu ya nyota za Binadam na Bingwa wa Tiba za Asili Afrika Mashariki.

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasi, Mfanyabiashara , Msani, ama mwanafunzi tunazo dawa na pete za bahati zenye uwezo mkubwa wakuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na SHABA WA SHABA kutoka Tanga,
Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki.
Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sasa amezianza ziyara zake za mikoani na atayatembeleye maeneo mbali mbali ndani na inje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nasiojulikana kwakutumia maji, Kioo na mitishamba.
Anazo dawa za mapenzi, kumrudisha alipoteya, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, kutoa ndagu , Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, Kuuza kwa haraka ( shamba, nyumba, Gari,...), Kesi mahakamani, Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na utajiri bila masharti na mengine mengi ya Siri...

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa nambari ya simu :
+255 785 358 267 ,
+255 785 358 267

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 2

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 2

Habari Mjema..Treni ya Kisasa Kuanza Novemba Mwakani

$
0
0
Serikali imesema treni inayotumia umeme inatarajiwa kuanza kutoa huduma Novemba mwakani kwa usafiri wa reli ya kati, kipande cha Dar es Salaam - Morogoro.

Vilevile, imesema mpaka sasa ujenzi wa reli hiyo kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) umepiga hatua saba.

Utekelezaji wa mradi huo unahusisha ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza ambao sasa unaendelea kwa Dar es Salaam-Morogoro (km 205) na Morogoro-Makutupora (km 422).

Akiwasilisha bungeni mjini hapa jana hotuba yake kuhusu makadirio ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka ujao wa fedha, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, alisema hadi sasa ujenzi wa kipande cha Dar es Salaam-Morogoro umefikia asilimia 10 na unatarajiwa kukamilika Novemba mwakani.

Akizungumzia hatua saba muhimu zilizofikiwa katika ujenzi wa reli hiyo, Prof. Mbarawa alisema hatua ya kwanza ya ujenzi wa kambi ya mkandarasi ya Dar es Salaam imekamilika kwa asilimia 99, Soga umekamilika kwa asilimia 89 na Ngerengere asilimia 67.

Alisema hatua ya upimaji wa ardhi itakakopita reli hiyo (topographical survey), umekamilika kwa asilimia 95.

Waziri huyo alisema hatua ya tatu iliyofikiwa ni njia ya kuhudumia mradi itakayotumika kupitishia watu, mitambo na vifaa vya ujenzi ambayo imekamilika kwa asilimia 83.

"Jumla ya vifaa kwa ajili ya ujenzi (mitambo na magari 755) vimeshawasili kwa ajili ya kazi. Kazi ya kusafisha eneo la mradi nayo imekamilika kwa asilimia 59.7," alisema.

Prof. Mbarawa alitaja hatua ya sita iliyofikiwa kuwa ni utafiti wa ardhi itakayobeba misingi ya madaraja pamoja na makalavati ya kuvukia watu, wanyama na baiskeli ambao umekamilika kwa asilimia 10.

Waziri huyo alisema hatua ya saba ni ujenzi wa tuta la reli ambayo imekamilika kwa asilimia 15.

Aliongeza kuwa utekelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa kwa sehemu ya pili inayoanzia Morogoro hadi Makutupora yenye jumla ya urefu wa kilometa 422 (km 336 njia kuu na km 86 njia za kupishana treni) unaendelea vizuri.

"Mkataba wa ujenzi kwa utaratibu sanifu na jenga, ulisainiwa Septemba mwaka jana kati ya iliyokuwa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) na kampuni ya Yapi Merkezi ya Uturuki," alisema na kusema zaidi:

"Mhandisi mshauri wa mradi huu ni muungano wa kampuni nane unaoongozwa na kampuni ya KORAIL ya Korea Kusini."

Alisema taratibu za kusaka fedha za ujenzi wa reli ya kisasa kwa maeneo ya Makutupora-Tabora (km 295), Tabora-Isaka (km 133), Isaka-Mwanza (km 250), Tabora-Uvinza-Kigoma na Kaliua-Mpanda-Karema zinaendelea.

"Nchi za China, Korea, Ujerumani, Ufaransa, India, Marekani, Nigeria, Ureno na Uingereza zimeonyesha nia ya kushiriki katika ujenzi huo," alisema.

"Zabuni kwa ajili ya kununua treni na mitambo itakayotumika kutoa huduma ya usafiri kwenye reli ya kisasa ilifungwa Februali, mwaka huu na tathmini inaendelea."

Jiwe la msingi la ujenzi wa sehemu ya reli hiyo liliwekwa na Rais John Magufuli, Machi 14, mwaka huu na ilielezwa kuwa unatarajiwa kukamilika Desemba 2020.

Prof. Mbarawa pia alisema serikali inatambua umuhimu wa reli ya kati iliyopo sasa kwa ajili ya kutoa huduma za mizigo na kuendelea kusafirisha mitambo na vifaa kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kisasa inayojengwa.

Kwa kutambua umuhimu huo, alisema maandalizi ya kukarabati miundombinu ya reli ya kati kupitia Mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Reli (TIRP) unaogharamiwa kwa fedha za mkopo kupitia Benki ya Dunia (WB), yanaendelea.

Katika hatua nyingine, Prof. Mbarawa alisema kuwa mwaka ujao wa fedha, Shirika la Ndege (ATCL) limetengewa Sh. bilioni 495.6 kwa ajili ya kununua ndege mbili; moja aina ya Q400 yenye uwezo wa kubeba abiria 76 na ndege kubwa ya masafa marefu aina ya Boeing 787-8 (Dreamliner) yenye uwezo wa kubeba abiria 262.

Prof. Mbarawa alisema fedha hizo pia zitatumika kulipia bima, gharama za uendeshaji wa ndege (start up cost), mafunzo ya marubani, wahandisi na wahudumu na ulipaji wa madeni.

Waziri huyo pia alisema kuwa katika mwaka ujao wa fedha, serikali itaendelea kuboresha huduma zinazotolewa na Shirika la Reli (TRC), Sh. trilioni 1.506 (fedha za ndani) zikitengwa.

Akifafanua kuhusu fungu hilo, Prof. Mbarawa alisema Sh. trilioni 1.4 zitatumika kuendelea na ujenzi wa reli ya kati (Dar - Morogoro km 300 na hadi Makutupora (km 422) kwa kiwango cha Standard Gauge.

Alisema Sh. bilioni 100 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa reli ya Isaka-Rusumo (km 371) kwa kushirikiana na Rwanda, Sh. bilioni tatu zimetengwa kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi ikiwa ni pamoja na kumwajiri mtaalamu atakayeandaa nyaraka na kusaidia kutafuta fedha za ujenzi wa reli ya Mtwara-Mbambabay na matawi ya Mchuchuma na Liganga.

Prof. Mbarawa pia alisema kuwa katika mwaka ujao wa fedha, Sh. bilioni 9.29 ili kutekeleza miradi ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) ambayo ni pamoja na ununuzi na usimikaji wa rada nne za kuongozea ndege za kiraia katika viwanja vya JNIA, KIA, Mwanza na Songwe.

Aliongeza kuwa serikali imetenga Sh. bilioni sita kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya sekta ya uchukuzi ikiwa ni pamoja na ununuzi wa magari ya zimamoto kwa viwanja vya ndege vya Mpanda, Shinyanga na Iringa.

Prof. Mbarawa aliliomba Bunge kuidhinisha jumla ya Sh. trilioni 4.271 ili kutekeleza majukumu yake kwa mwaka ujao wa fedha. Kati yake, Sh. trilioni 1.865 ni kwa ajili ya sekta ya ujenzi, Sh. trilioni 2.387 za sekya ya uchukuzi na Sh. bilioni 18.856 za sekta ya mawasiliano.


Rais Magufuli Ampongeza Mizengo Pinda.....Ataka Viongozi Wengine Wastaafu Waige Mfano Wake

$
0
0
Rais John Magufuli jana alimmwagia sifa Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda kwa kumwelezea ni kiongozi mkimya na asiyependa kuzungumza ovyo ovyo.

Rais Magufuli alisema Pinda, maarufu kama Mtoto wa Mkulima, ni kiongozi anayefaa kuigwa na viongozi wengine, na kwamba hata yeye siku akistaafu atamfuata ili kujifunza.

Aliyasema hayo jana mjini Dodoma wakati akifungua Tawi la Benki ya NMB la Kambarage na Jengo la Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF).

“Mzee Pinda anaishi maisha ya kawaida sana, hapigi kelele, hazungumzi chochote, Mzee Pinda ‘you are too special’ (wewe ni mtu wa kipeke),” alisema Rais Magufuli.

“Watu watakukumbuka (Pinda) kwa ukarimu wako, wewe ni mtu wa kawaida sana. Sasa hivi hatujui thamani yako lakini ipo siku tutaijua.

“Ndiyo maana bado unaonekana kijana, hujipi ‘pressure’ (hofu), unaamini kile unachofanya, na mimi nikistaafu nitakuja kuchukua ‘course’ (mafunzo) kwako.”

Sifa kwa Pinda zinakuja miezi saba tangu alipokosoa viongozi wastaafu wa "maeneo mengine" wanaosemasema kila wakati kuhusu uendeshaji wa serikali.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Septemba 11, mwaka jana Rais Magufuli alitoa mfano wa majaji wastaafu ambao alisema ni tofauti na wastaafu wengine na kwamba huenda kujua sheria ndiko kunakowasaidia kutokuwa waropokaji.

Rais Magufuli alisema hayo wakati wa kumuapisha Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma.

“Nawashuruku majaji wakuu wastaafu, Barnabas Samatta na Augustino Ramadhani, walifanya kazi kubwa ya kujenga misingi ya mahakama nchini," alisema.

“Bahati nzuri majaji hawa ni waadilifu sana huwezi kumsikia Jaji (Mkuu mstaafu Othman) Chande, (Barnabas) Samatta, Augustino (Ramadhani), (Damian) Lubuva au majaji walioko hapa... ukiangalia wastaafu wa maeneo mengine hawachoki kusema, wanawashwawashwa.

“Ndiyo maana nawapongeza sana mahakama...Ni safi mno, nina uhakika wanapotaka kutoa ‘advice’ (ushauri) yoyote (wowote) lazima wanakushirikisha (Jaji Mkuu); ndiyo faida ya kujua sheria.

“Sisi wengine huku ambao hatujajua sheria mahali popote, chochote unaweza ukazungumza.”

Rais Magufuli Abaini Mchezo Mchafu NMB.......Ashangazwa Gawio Kufanana Miaka Mitatu Mfululizo

$
0
0

Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Bodi ya National Microfinance Bank (NMB) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo kuangali kiasi cha gawiwo kinachotolewa na benki hiyo, kutokana na kiasi hicho kutoongeza ndani ya miaka mitatu mfululizo.

Rais Magufuli ameyasema hayo jana Mjini Dodoma wakati alipokuwa akifungua jengo jipya la Mfuko wa Pensheni wa Watumishi wa Umma (PSPF) pamoja na tawi jipya la NMB Kambarage lililoko katika jengo hilo.

“Kuna mambo mazuri mengi yaliyofanywa na NMB lakini tunahitaji uhakiki wa gawiwo linalotolewa kwa Serikali, kutokana na gawiwo hilo kutopanda kwa miaka mitatu mfululizo tangu mwaka 2014/2015 mpaka mwaka 2016/2017 ambapo benki hiyo imekuwa ikitoa shilingi Bilioni 16.525 kama gawiwo la hisa ya asilimia 32 iliyonayo katika Benki hiyo,” alisema Rais Magufuli.

Ameendelea kwa kusema, ni matumaini yake kuwa kiasi hicho cha fedha kitapanda kwa mwaka 2017/2018 kutokana na benki hiyo kutengeneza faida kila mwaka. 

Aidha, Rais Magufuli ameipongeza benki ya NMB kwa kuwa na matawi mpaka vijijini pamoja na kutoa ajira kwa zaidi ya Watanzania 3000 na kutoa misaada ya kijamii ikiwemo madawati 600, kompyuta 300 kwa shule za Sekondari na vitanda vya wagonjwa.

Vilevile Rais Magufuli ameupongeza mfuko wa PSPF kwa kuona fursa ya Serikali kuhamia Dodoma na kujenga jengo ambalo limeboresha na kupendezesha mandhari ya Dodoma ambapo pia ujenzi huo umetoa ajira kwa Watanzania takribani 250.

Pia amesema, mfuko huo umekuwa ukitoa mikopo kwa wanachama wake pamoja na kuwekeza katika ujenzi wa viwanda mbalimbali ikiwa ni pamoja na kiwanda cha cha Sukari Kagera, kiwanda cha nguo na turubai vilivyopo mkoani Morogoro.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amesema Rais Magufuli kupitia TAMISEMI ametoa shilingi bilioni 70 kwa ajili ya ujenzi mbalimbali wa miundombinu mkoani Dodoma.

Dkt. Mahenge ametaja miundombinu hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa stendi mpya ya kisasa yenye uwezo wa kuingia mabasi makubwa 250, magari madogo 600 pamoja na bajaji na bodaboda 300 kwa wakati mmoja.

Aidha, Dkt Mahenge ameitaja miundombinu mingine ambayo ni ujenzi wa soko la kisasa, sehemu ya kupaki malori, miundombinu ya majitaka, maeneo ya kupumzikia pamoja na kuboresha miundombinu ili kuondoa msongamano wa magari.

kwa upande wake, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji ameutaja mfuko wa PSPF kuwa ndio mfuko wa kwanza kuwekeza katika vitega uchumi Makao Makuu ya Nchi ukiondoa mfuko wa LAPF ambao Makao Makuu yake yapo Mkoani Dodoma.

Jengo la PSPF ni moja ya majengo marefu yaliyoko mkoani Dodoma ambapo ina jumla ya ghorofa 11 pamoja na eneo la maegesho ya magari 161 ambapo mpaka sasa jengo hilo limeshapata wapangaji kwa asilimia 100.

Mbunge CHADEMA Ahoji Bungeni sababu za ripoti za CAG kutokuwa na taarifa za Tanroads Shirika la Ndege (ATCL)

$
0
0
Mbunge wa Momba, David Silinde (Chadema), amehoji bungeni kuhusu taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutokuwa na taarifa za Shirika la Ndege (ATCL) na Wakala wa Barabara (Tanroads).

Akichangia bungeni jana mjadala wa makadirio ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka ujao wa fedha, mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Waziri Kivuli wa Fedha na Mipango, alisema hakutarajia kuona ripoti ya CAG ya mwaka 2016/17 ikikosa taarifa za taasisi hizo muhimu katika kipindi hiki ambacho zinatengewa fedha nyingi.

Alisema taarifa za fedha za taasisi hizo zilipaswa kuwamo kwenye ripoti ya CAG ili wahoji kama wanavyofanya sasa kuhusu kutoonekana kwa matumizi ya Sh. trilioni 1.51.

Silinde ambaye alihoji ni sababu za ripoti za CAG kutokuwa na taarifa za Tanroads ili wabunge waangalie barabara za Tanzania kama zinaendana na thamani ya fedha inayotolewa.

“Sisi kama wabunge tunatakiwa kuhoji kwanini katika ripoti ya CAG huwa hakuna Tanroads, tunatakiwa kuhoji; je, barabara inayojengwa inalingana na 'value for money' (thamani ya fedha)?” alisema Silinde.

Majonzi ya Belle 9 kwenye maziko ya Agness Masogange..Ashindwa Kuongea na Kuishia Kulia

$
0
0
Inafahamika kwamba Mwimbaji wa Bongofleva Belle 9 ndio alikua Msanii wa kwanza kumtambulisha Video Queen Agness Masogange kwenye bongofleva baada ya kufanya nae video na jina la Masogange ndio likaanzia hapo.

Belle 9 alikua miongoni mwa Mastaa waliosafiri mpaka Mbeya kumzika Agness Gerald maarufu kama Masogange ambapo alipewa nafasi ya kuongea msibani lakini majonzi yalichukua nafasi kubwa kuliko kuongea kwake, tazama zaidi kwenye hii video hapa chini:

VIDEO:

Irene Uwoya Aguswa na Kifo cha Agness Masogange, Aamua Kumuenzi kwa Njia Hii

$
0
0
Siku ya Ijumaa April 20,2018 Tanzania ilipokea taarifa za kifo cha video vixen maarufu nchini Marehemu Agnes Gerald Waya “Masogange” ambapo kila mtu alipokea taarifa hizo kwa style yake na wengine walizimia na vilio vilitanda kila sehemu kutokana na wengi kuwa karibu na Marehemu Agnes Masogange.

Muigizaji Irene Uwoya ni miongoni mwa watu waliokuwa karibu na Marehemu Agnes Masogange na kusikitishwa na taarifa hizo kutokana na ukaribu aliokua nao Irene na Marehemu Agnes na ameamua kumuenzi rafiki yake kipenzi kwa kuchora tattoo katika mkono wake na kuandika “R.I.P Agnes”

Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images