Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104663 articles
Browse latest View live

Msanii Jebby Azikwa Wasanii Wamchangia Laki Tano

$
0
0
Msanii Jebby Azikwa Wasanii Wamchangia Laki Tano
Msanii wa Bongo Fleva, Jebby amezikwa katika makaburi ya Mailimbili mjini Dodoma.

Jebby ambaye amewahi kufanya vizuri na wimbo wake wa ‘Swahiba’ alifariki dunia hapo jana April 22, 2018 mji
ni Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.

Wapili kushoto ni msanii Suma G.
Kwa mujibu wa mdogo Jebby, Hamis Omary msanii huyo hakubahatika kuwa na mke wala mtoto, pia kuna nyimbo zaidi ya nne alirekodi ambazo zipo tayari ila hazijatoka.
Professor Jay ni miongoni mwa wasanii waliohudhuria katika msiba huo ambapo amekabidhi Tsh. 550,000 zilizochangwa na wasanii kwa ajili ya msiba huo, msanii mwingine aliyehudhuria ni pamoja na Suma G.

Mtoto wa Masogange Awaliza Waombolezaji

$
0
0
Mtoto wa Masogange Awaliza Waombolezaji
MZAZIi mwenzake na marehemu Agness Gerald ‘Masogange’ amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu uhusiano wake na marehemu, ambapo amesema mawasiliano ya mwisho na Agnes yalikuwa wiki iliyopita ambapo alimwambia kuwa hali yake ni Mbaya.

Mzazi huyo ambaye ni baba wa Sania amewashukuru Watanzania kwa kujitolea kumsomesha mtoto wao kwani wamemsaidia kumpunguzia majukumu.

Kwa upande mwingine, Sania amewaliza waombolezaji hasa wakati wa kuuzika mwili wa mama yake kipenzi ambapo alionekana mnyonge na mwenye huzuni hasa anapokumbuka mapenzi aliyokuwa akiyapata kutoka kwa mama yake enzi za uhai wake.

Masogange amezikwa leo katika Kijiji cha Utengule, Mbalizi Mkoani Mbeya, leo Aprili 23, 2018 ambapo mamia ya Watanzania wamejitokeza kumzika wakiwemo wasanii wenzake.
 

Wema Abanwa Kuhusu Mimba Ya Daimond Afunguka Mazito

$
0
0
Wema Abanwa Kuhusu Mimba Ya Daimond Afunguka Mazito
UKITAJA mastaa wakubwa Bongo wenye mashabiki wengi, kamwe huwezi kuacha kutaja jina la Wema Isaac Sepetu ambaye Ijumaa Wikienda limembana na kujikuta akilipuka juu ya ishu mbalimbali ambazo ni ‘hoti’.

Hivi karibuni Wema alibeba Tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike kupitia Tuzo za Sinema Zetu zilizotolewa Azam TV. Kumekuwa na minon’gono juu ya mambo mengi yaliyomhusisha Wema ikiwemo kurudiana na mpenzi wake wa zamani ambaye ni mwanamuziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.

Habari hizo zilieleza kwamba, Wema alirudiana na Diamond baada ya jamaa huyo kuachana na mzazi mwenzake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.Kufuatia mambo hayo kusemwa mno kwenye mitandao ya kijamii na kuibua sintofahamu, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Wema ambaye aliamua kuweka wazi kila kitu ambacho wengi walikuwa wakikizungumza bila kupata majibu sahihi;

KUCHOROPOKA KWA MIMBA
Ijumaa Wikienda: Mambo vipi Wema, pole na mkasa uliokupata wa kuchoropoka kwa ujauzito wako kwa mara nyingine!
Wema: Asante, lakini hiyo mimba imetoka karibia mwezi na nusu hivi umepita.
Ijumaa Wikienda: Imekuwaje sasa watu wanaizungumzia hivi sasa?
Wema: Mimi niliweka picha moja ya mwanamke mwenye tatizo kama langu la kushika mimba kisha inatoka ndipo nikaandika; ‘My Life Story’.

Hapo ndipo watu walichukulia kama nimepatwa na janga hilo kwa wakati huu, lakini ukweli ni jambo lililonipata mwezi na nusu uliopita.
Ijumaa Wikienda: Kumbe ni kweli ulikuwa na ujauzito…je, ulikuwa na muda gani?
Wema: Kama miezi miwili tu.
Ijumaa Wikienda: Najua wewe ni staa, unajuana na watu wengi sana, sasa imeshindikana kweli kupata mtalaam wa tatizo lako?

Wema: Nimeshahangaika sana, sina la kukwambia, nimefunga mara nyingi sana, nimeamka usiku wa manane na kukesha nikiomba, basi sasa hivi nimeamua kupenda tu watoto wa watu.
Ijumaa Wikienda: Au ndiyo umekata tamaa, unataka kufunga kizazi?
Wema: Nilisema hivyo na hilo nitalimiza baada ya siku ya kuzaliwa kwangu kupita.

MIMBA YA DIAMOND
Ijumaa Wikienda: Kuna minong’ono kuwa mimba ilikuwa ni ya Diamond, ukweli ni upi?
Wema: Hakuna ukweli wowote, ni ya mtu mwingine kabisa.
AMERUDIANA NA DIAMOND?
Ijumaa Wikienda: Mbona imesemekana umerudiana rasmi na Diamond?
Wema: Hakuna lolote ila ni mshkaji wangu ambaye si unajua tumezoeana sana!?

DIAMOND NYUMBANI KWAKE
Ijumaa Wikienda: Mbona kuna taarifa kuwa anakuja kwako mara kwa mara na wewe unaenda nyumbani kwa Diamond, Madale?
Wema: Nasibu hajawahi kukanyaga kwangu ila mimi ndiye niliwahi kwenda Madale mara moja tu.
Ijumaa Wikienda: Ulikwenda kufanya nini?

Wema: Alinialika, kulikuwa na swimming part (pati ya kuogelea), ndiyo siku hiyo tu.
Ijumaa Wikienda: Kwa hiyo Diamond akiamua leo kwenda moja kwa moja kwa Mama Wema kutoa mahari utalipokeaje?

Wema: Yaani Diamond, hata aache kila kitu akaniambia sasa Wema nataka kukuoa sitakubali kabisa.
Wikienda: Kwa nini na wakati inasemekana ndiye mwanaume aliyeko moyoni mwako?
Wema: Ilikuwa zamani, lakini siyo sasa kwa sababu Nasibu nimekaa naye miaka miwili. Najua alivyo na hatanisumbua sana kwa sababu mimi nilimwacha CK kwa ajili yake, matokeo yake akatoka na Meninah (msanii wa Bongo Fleva) na meseji nilizibamba. Kwa hiyo hata kwenye ndoa hawezi kubadilika.

Ijumaa Wikienda: Kwa nini uliamua kumwacha CK ukaenda kwake wakati ulikuwa unapata kila kitu hadi ukapewa jina la Madam?
Wema: Mimi hakuna kitu ninachokiangalia kama furaha yangu, niliporudi kwake nilikuwa nina furaha. Nilipokwenda Hong Kong na kuachia picha, nilikuwa nina furaha kwa hiyo sijutii kitu nilichokifanya ambacho mimi kilikuwa kinanipa furaha.
Ijumaa Wikienda: Diamond alipoachana na Zari, Zari alilalamika kuwa wewe ndiye ulikuwa chanzo cha kuachana na baba watoto wake, je unalizungumziaje?
Wema: Yaani itakuwa ni vituko sana maana mimi hakuna kitu nilichofanya cha ajabu hadi achukue hatua hiyo kwa sababu kuna matukio mengi amefanya baba mtoto wake huyo ambayo ni makubwa mno yanayofanya watu waweze kutengana, lakini siyo mimi.

MOBETO NA ZARI
Ijumaa Wikienda: Basi kama ni kuoa ungependa kumshauri Diamond amuoe nani kati ya Hamisa Mobeto na Zari?
Wema: Yeye mwenyewe tu achague anayeona anayemfaa hapo maana siwezi kumchagulia.
Ijumaa Wikienda: Mbona dada wa Diamond, Esma bado anakuita wifi na hata kwenye mtandao mlikuwa mnajinadi na ikaonekana umerudisha majeshi kwa kaka yake?
Wema: Esma ni rafiki yangu sana. Kwanza kwa ajili ya Petit Man, lakini pia tulijiachia kwa sababu ya timu za mitandaoni, lakini kulikuwa hakuna chochote cha zaidi.

BIFU NA MOBETO
Ijumaa Wikienda: Kuna tetesi wewe una bifu kubwa na Hamisa Mobeto, je, ni kweli?
Wema: Sina bifu naye ila siyo rafiki yangu kabisa.
Ijumaa Wikienda: Mbona kuna kipindi mlikuwa kama mna ukaribu hivi mpaka kwenye Instagram mlikuwa mnawekana?
Wema: Ni kweli, lakini kuna maneno aliniongelea mabaya sana, tena siyo kwa kuambiwa, kwa kusikiliza sauti, sasa nikaona huo ni unafiki kwa hiyo nikaona kila mtu achukue muda wake na hata tukikutana kila mtu na hamsini zake.

YEYE NA ZARI
Ijumaa Wikienda: Unamuongeleaje Zari?
Wema: Sina shida kabisa na yule dada na ninampenda.
VIPI KUOLEWA?

Ijumaa Wikienda: Kuna kipindi ilisikika unataka kuolewa, vipi hilo?
Wema: Walijitokeza karibu wanaume watano wanaenda, kwa mama kupeleka barua kinachotokea mama ananiita, ananiuliza mimi, sikubali kwa sababu siwezi kuolewa na mtu ambaye simjui au sijakaa naye.
Ijumaa Wikienda: Mbona hutaki sasa hivi kumweka mpenzi wako wazi?
Wema: Nimekua sasa hivi, mambo ya utoto nimeweka pembeni.

Ijumaa Wikienda: Unamzungumziaje Ali Kiba alivyoamua kuoa, tena mbali na siyo nyumbani?
Wema: Ninampongeza sana kwa mwanamuziki mkubwa kama yeye kufanya jambo hilo amejijengea heshima kubwa sana, lakini ninaamini mke yupo popote ni jinsi tu Mungu alivyokupangia wapi utampata.
Ijumaa Wikienda: Mastaa wengi sasa naona wamejiingiza kwenye mambo ya ujasiriamali, vipi kwa upande wako?
Wema: Kwa vile napenda sana watoto na bado sijapata sasa hivi, ninatarajia kufungua maduka makubwa mawili kwa ajili ya nguo za watoto litakaloitwa Little Sweetheart na hapa tayari niko kwenye hatua ya mwisho kabisa ya kumalizia lipstics zangu ambazo zitakwenda kwa jina langu.
Ijumaa Wikienda: Ni nani rafiki yako wa moyoni?
Wema: Aunt, yaani anaishi kwenye moyo wangu.

Ijumaa Wikienda: Kulikuwa na madai kuwa ulihamishwa nyumba ya Ununio kwa sababu mwenye nyumba alikuwa hapendi unavyoishi na wanaume tata, unalizumziaje hilo?
Wema: Siyo kweli, mwenye nyumba alikuwa anataka kuishi mwenyewe na mpaka leo tunawasiliana vizuri tu.
Ijumaa Wikienda: Watu wengi wanajiuliza kwa nini unapenda kuongozana na wanaume tata?
Wema: Yaani hata wakiangalia nyota yangu inazungumza kabisa, sisi wenye nyota hii tunapatana na watu hao na mimi ninawapenda sana kwa sababu ni binadamu kama walivyo wengine.

MAMA KANUMBA
Ijumaa Wikienda: Vipi kuhusu ishu ya Mama Kanumba kuja kwako kisha akadai kuchomeshwa mahindi getini?
Wema: Jamani…kwanza siku hiyo mimi sikuwepo kabisa, niliambiwa tu alikuja na kwa nini nifanye hivyo sasa.
Ijumaa Wikienda: Yeye naye anaigiza, je, unaonaje ukamshirikisha kwenye filamu yako hata moja?
Wema: Hapana, siwezi kwa sababu Kanumba alikuwa hataki mama yake aigize na hata mimi alishaniambia, sasa nitavunja makubaliano yetu mimi na Kanumba.

Bodi ya Ligi Kuchunguza Mechi ya Yanga na Mbeya City

$
0
0
Ikiwa imepita siku moja tokea kulipomalizika kuchezwa kwa mechi kati ya Mbeya City na Yanga hapo jana, Bodi ya ligi nchini (TPLB) imesema inasubiri kupokea ripoti ya mchezo huo ili waweze kupitia kwa makini matukio mbalimbali yaliyojitokeza ikiwemo suala la malalamiko waliyoyatoa kwa Yanga
Hayo yameelezwa na Mtendaji mkuu wa Bodi hiyo Boniface Wambura na kusema suala la Yanga wameshalisikia lakini wanachosubiri wao ni ripoti ambayo itaweza kutoa mwangaza wa kuona tukio zima la wachezaji kuwa wengi uwanjani wa Mbeya City kama walivyodai walalamikaji ambao ni Yanga na mwishowe waweze kukaa kikao kwa mujibu wa kanuni ili kuweza kufanya maamuzi.
"Mechi imechezwa na Ligi yetu bahati nzuri inaonekana. Waamuzi wataleta ripoti pamoja na kamishna wa mchezo na hata msimamizi wa kituo kwa hiyo baada ya kupokea ripoti kuna vikao tutakaa kupitia ripoti na kufanya maamuzi pale tutakapokuta kuna changamoto au matatizo. Lakini vile vile taratibu zipo za kwa watu wenye malalamiko au wenye kutaka kukata rufaa zipo taratibu za kikanuni na tunawaomba wale wote wenye malalamiko wayatume kwa kufuata kanuni", amesema Wambura.#
Kwa upande mwingine, Wambura amesema kwa kuwa yeye ni sehemu ya wenye kikao hicho hawezi kusema sheria inasema nini mpaka pale watakapopitia ili kuhakikisha wanaangalia kanuni zinaelekeza nini kwa suala linalodaiwa kutokea katika mchezo huo.

Rammy Gals: Sikuzimia Kama Watu Wanavyosema

$
0
0
Rammy Gals: Sikuzimia Kama Watu Wanavyosema
Msanii wa filamu nchini Rammy Gals amefunguka na kuweka wazi kuwa kitendo ambacho kilitokea wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa mpenzi wake Agnes Gerald si kwamba alikuwa amezimia kama ambavyo watu wanasema kwenye mitandao ya kijamii.
Rammy Gals amesema hayo akiwa jijini Mbeya baada ya kumzika Masogange na kudai kuwa alipokuwa amesimama kwa muda mrefu alianza kuona anatetemeka miguuu kwa kuishiwa nguvu hivyo aliwaomba wasanii wenzake Duma pamoja na Idris Sultan wamsaidie kuondoka katika eneo hilo.
Dumma amedai kuwa wasanii hao walipoanza kumuondoa kwenye eneo hilo ndipo walipokuja mabaunsa na kumchukua kwa kumbeba wakidhani kwamba alikuwa amezimia lakini anadai hakuwa amezia bali aliishiwa nguvu tu kwa kusimama muda mrefu.
"Nilipewa jukumu kubwa la kusimama muda mrefu sana na nilivyoona hali yangu inazidi kuwa tete natetemeka miguuni nikaomba msaada kwa Duma na Idris Sultan nikawaambia jamanii nishikeni mabega mnitoe hapa nadhani nguvu zinaniishia hivyo walipoanza kunitoa ndipo walipokuja mabaunsa na kunitengua miguu na kunibebe juu kwa juu wakidhani kwamba nimezimia, unajua mtu akivaa miwani haraka haraka huwezi kujua kama macho yako yamefumba au hayajafumba hivyo nisingeweza kukataa sababu tayari nilijikuta nipo juu kikubwa niliishiwa tu nguvu lakini nilikuwa nasikia kila kitu kilichokuwa kinaendelea"alisema Rammy Gals
Mbali na hilo Rammy Gals amesema kuwa yeye na Irene Paul ni watu ambao walikuwa na matatizo na chanzo cha ugomvi wao kilikuwa kuhusiana na Masongange huyo huyo anadai kuwa msanii huyo alishawahi kumuuliza kuwa anaishi na Masogange lakini anatambua mtu ambaye anamlipia kodi? na kusema hicho ndicho kilikuwa chanzo cha ugomvi wao hivyo anaamini amefanya hivyo kuandika ujumbe ule kwa lengo la kutaka kumuharibia siku yake.

Rais Magufuli: Najua Wapo Watakaotumika Kuleta Vikwazo vya Maendeleo

$
0
0
Rais Magufuli: Najua Wapo Watakaotumika Kuleta Vikwazo vya MaendeleoRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amesema anajua wapo watakaotumika kuleta vikwazo kwenye hatua anazopiga za kuiletea maendeleo nchi.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa jengo la PSPF mkoani Dodoma, Rais Magufuli amesema kwamba wapo ambao hawapen
di kuona Tanzania inapiga hatua kwenye uchumi, hivyo watu watatumika na mabeberu kuleta vipingamizi na vikwazo, lakini yeye ataendelea kuchapa kazi kwa ajili ya watanzania masikini.
“Katika juhudi hizi za kuleta maendeleo wapo wengine watasaliti njiani, wapo wengine watatumika na mbinu za mabeberu, na hasa katika masuala haya ya kujenga nchi yetu, na hasa kwa sababu nchi yetu inakwenda mbele, ni lazima itawakwaza wengine, katika jukumu lolote la kazi hata kwenye familia, lazima watapatikana wa kupinga pinga kidogo, lakini kikubwa ni kunyoosha mstari kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania masikini”, amesema Rais Magufuli.
Sambamba na hilko Rais Magufuli amemuhakikishia mtoto wa Baba wa Taifa Mwl. JK Nyerere, Makongoro Nyerere, kuwa nchi ipo salama na imara, na anaamini itafika ikiwa imara zaidi licha ya vikwazo vingi anavyokutana navyo.

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special, Imeboreshwa zaidi

Mbunge CHADEMA Aishangaa Serikali Kununua Ndege Mpya

$
0
0
Mbunge wa Viti Maluum (Chadema), Lucy Magereli amesema uamuzi wa Rais John Magufuli kununua ndege hauwezi kuwa sababu ya kulifufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).

Akizungumza katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano mwaka 2018/19, mbunge huyo amesema kuliko kununua ndege hizo, Serikali ingekodisha ndege na kuanza kujipanga taratibu kuliboresha shirika hilo.

“Nani aliyemshauri Rais kununua ndege? Tungeweza kuifufua ATCL kwa ndege za kukodi, hatuhitaji ndege kubwa. Hivi tunawezaje kushindana na mashirika makubwa ya ndege duniani ambayo yapo muda mrefu na yamejiimarisha,” amesema.

“Suala si kuhitaji ndege, suala tumezipata kwa utaratibu upi. Tuna ndege wakati viwanja vya ndege vya ndani havifai kwa matumizi yetu. Leo mtalii akitua Dar es Salaam akitaka kwenda maeneo mengine atafika kwa shida.”

Mbunge huyo alihoji sababu za Serikali kununua ndege kubwa wakati haijaimarisha miundombinu, vikiwemo viwanja vya ndege, “ndege tunazonunua ni mzigo kwa nchi hii, zinahitaji matengenezo, tutayaweza?”

“Kesho na keshokutwa Bunge litakaa tena na kusema tumetumia fedha nyingi kuifufua ATCL na kuliingiza Taifa katika matatizo. Nawaambieni tutakaa hapa kujadili tena jambo hili.”

“Tumetumia fedha nyingi kukomboa ndege zetu zilizozuiwa Canada je hizo fedha Bunge gani limezipitisha?” Amehoji.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumanne

$
0
0

Okoa Ndoa yako Sasa...Umepungukiwa na Nguvu za Kiume na Unashindwa Kupanda Mlima Vizuri

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA : JE UMEPUNGUKIWA NA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO AU MPENZI WAKO HAKUTIMIZII UTAKACHO:


Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sababu ya kutokuwa na nguvu za kiume au Uume wako mdogo

Dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa Kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA MWENZI WAKO BADO AJAKOJOA

KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA

UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE

KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

Dawa hii utumiwa ata na wazee wenye umri mkubwa na haina madhara yoyote

MAKAKANUA HII NI dawa ya maumbili madogo urefusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5 kwa mini huabiki kwa kuwa na UUME mdogo wai sasa upate tiba sahihi kabisa na ni tofauti na ulizowai kutumia :

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba dawa za uzazi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA p

Piga simu 0743362017 au 0789234653

DR AGU

Baba Mzazi Masogange: Mwanangu A gnes AliishiaKidato cha Pili Niligombana Naye Kisa Usanii

$
0
0
Baba Mzazi Masogange: Mwanangu A gnes AliishiaKidato cha Pili Niligombana Naye Kisa Usanii
BABA mzazi wa marehemu Agness Gerald ‘Masogange’, Mzee Gerald Waya amefunguka alivyokuwa akigombana na mwanaye huyo akimsihi aachane na mambo ya usanii, kwani mzee huyo alikuwa hayapendi.

Akizungumza mara baada ya mazishi ya mwanaye, Mzee Waya alisema; “Mwanangu alikomea kidato cha pili lakini hata kidato  cha pili hakumaliza kwa sababu ya matatizo. Kuna wakati nilikorofishana naye nikamwambia mimi mambo ya usanii sitaki, akanijibu, ‘sasa baba mimi nitafanya kazi gani wakati unafahamu tangu niko kanisani nilikuwa naimba kwaya?’ Baada ya muda tulikutana tena, tukalimaliza suala hilo, nikamruhusu,” alisema Mzee Gerald.

Masogange alifariki dunia Ijumaa iliyopita katika kituo cha Huduma za Afya cha Mama Ngoma kilichopo Mwenge jijini Dar ambapo jana aliagwa katika Viwanja vya Leaders na kusafirishwa kwenda kwao Mbeya ambako alizikwa jana Aprili 24, 2018 kijijini kwao Utengule, Mbalizi.

Fatuma Karume: Sina Mpango wa Kuingia Kwenye Siasa

$
0
0
Fatuma Karume: Sina Mpango wa Kuingia Kwenye Siasa Mwanasheria maarufu nchini ambaye kwa sasa ndiye rais wa Tanganyika Law Society (TLS), Bi. Fatma Karu
me, amesema kwamba hana mpango wa kuingia kwenye siasa, licha ya kuonekana akikosoa sana wanasiasa na baadhi ya vitu vinavyofanywa na serikali.
Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast cha East Africa Radio, Fatma Karume amesema hataki kuingia kwenye siasa kwa sababu anapenda kuwa huru, licha ya kwamba hatoacha kuendelea kukosoa serikali na wanasiasa pale wanapokosea.
“I like my freedom, napenda kufanya vile ninavyoona mimi, kama serikali inafanya vitu kinyume na sheria nitasema kwamba hivi sio vizuri, si vizuri kuvunjia watu majumba yao wakati kuna court order, nitasema sitaogopa, ila sitaki kugombea, sitaki siasa, I like to be left alone”, amesema Fatma Karume.
Fatma Karume ameendelea kusema kwamba kitendo cha kuonekana kuikosoa serikali mara kwa mara na kutetea baadhi ya vyama vya siasa, anafanya hivyo kwa sababu haungi mkono uvunjaji wa sheria kwa namna yoyote ile, iwe inafanywa na serikali au vyama vya siasa.
"Siungi mkono uvunjaji wa sheria hata ukiwa upande wowote, mimi ni mtu huru, kama kitu hakiendi kwa mujibu wa sheria nitasema, sio kwamba unakosoa vitu una ugomvi wa serikali, sijali", amesema Fatma Karume.

Faiza Ally Afunguka Kuhusu Bongo Movie

$
0
0
Faiza Ally Afunguka Kuhusu Tasnia ya Bongo Movie
Msanii wa filamu Bongo, Faiza Ally amesema tasnia hiyo ina vitu vikubwa ila hajui ni wapi inakwama kwa sababu ushirikiano na umoja wanao.

Muigizaji huyo ameeleza hayo kufuatia ushirikiano ulionyeshwa na waigizaji wenzake katika mazishi ya video vixen, Agness Gerald ‘Masogange’ ambaye alizikwa jana mkoani Mbeya. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Faiza ameandika;
“Tunaishi kwa kujifunza na mara nyingi mitazamo ya nje sio halisi, naomba nimpongeze IreneUwoya kwa kuwa rafiki mwema a special kipindi hiki, nimemuona akishiriki na kwenye utulivu sana yaani kasimama kama rafiki na hivi ndio inavyo takiwa, yaani jambo linapo kufika la mtu wa karibu sio kulia sana au kupoteza fahamu lazima usimame ujue hatma ya mwenzio kwanza,” amesema.
Aliendelea kwa kuwapongeza Zamaradi Mketema, Steve Nyerere, Aunty Ezekiel, Husna Maulid, Husna Sajent, Shilole kwa kusimamia vizuri tukio hilo vizuri.
“Nahisi Bongo Movie tuna vitu vikubwa sana wote kwa pamoja lakini sijui tunakosea wapi, maana kwa ushirikiano huo huo wa msibani, urudi kwenye kwenye kazi naamini kuna hatua kubwa sana tutapiga, nisema tu mpo vizuri sana, nyinyi ni wa maana sana,” ameongeza.
Hapo jana April 23, 2018 alizikwa Agness Gerald ‘Masogange’ ambaye alikuwa video vixen na muigizaji wa filamu, Masogange alifariki April 20, 2018 katika hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge, Dar es Salaam.

Binti wa Miaka 24 Anayetarajiwa Kuolewa na Jacob Zuma Alazimishwa Kujiuzulu

$
0
0
Binti wa Miaka 24 Anayetarajiwa Kuolewa na Zuma Alazimishwa Kujiuzulu
Mwanamke ambaye anatarajiwa kuwa mke wa saba wa aliyekuwa rais wa Afrika kusini,Jacob Zuma amelazimishwa kujiuzulu ajira yake ya ukuu wa asasi isiyokuwa ya kiserikali na chombo cha habari cha nchini humo.
Nonkanyiso Conco ambaye ana mahusiano ya kimapenzi na bwana Zuma ambaye amemzidi umri wa miaka 52. wakati huo yuko kwenye asasi inayohamasisha kampeni ya kuwawezesha mabinti wadogo katika maisha yao ya kila siku na kuacha kuwategemea wanaume wenye umri mkubwa.
Bi.Conco mwenye miaka 24 amejifungua mtoto wa Zuma katika hospitali ya binafsi iliyoko mjini Durban.
Zuma kwa sasa ana umri wa miaka 76,ana wake wanne na mwingine mmoja waliachana na mke wa sita alijiua mwaka 200 pamoja na watoto ishirini.
Conco analazimika kujiuzulu cheo chake akiwa ni afisa mawasiliano wa kampeni ya kukabaliana na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kwa wanawake wadogo, unyanyasaji wa kijinsia na ujauzito kwa watoto wadogo.Mpaka sasa Bi Conso hajazungumza chochote kuhusiana na tuhuma zinazomkabili lakini amewasilisha barua ya kujiuzulu kazi katika shirika analofanyika kazi,Daily Maverick limeripoti.
Habari za mahusiano ya Jacob Zuma na Bi Nonkanyiso Conco zilizagaa sana tangu siku ya ijumaa iliyopita

Liverpool Kupimana Nguvu na AS Roma Leo

$
0
0
Liverpool Kupimana Nguvu na AS Roma Leo 
Vita ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya inaendelea tena usiku wa leo ambapo Liverpool wata


kuwa wanaikaribisha AS Roma kwenye Dimba la Anfield.

Liverpool waliingia hatua ya nusu fainali baada ya kuing'oa Manchester City kwa jumla ya mabao 5-1 huku nyota wake Mohamed Salah aking'aa.

AS Roma nao walitinga hatua hiyo kufuatia kupindua matokeo dhidi ya vinara wa ligi nchini Spain, FC. Barcelona.

Mechi hiyo ambayo inasubiriwa kwa hamu na wadau wengi wa soka duniani, itaanza majira ya saa 3 na dakika 45 za usiku.

Baada ta mtanange huo, kesho pia ligi hiyo itaendelea kesho kwa Bayern Munich kuikaribisha Real Madrid kutoka Spain.

Yanga Waamua Kuifata Simba Morogoro

$
0
0
Yanga Waamua Kuifata Simba Morogoro 
Baada ya kwenda sare ya bao 1-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, kikosi cha Yanga nacho kimeamua kuweka kambi


mjini Morogoro.

Yanga imeweka kambi maalum Morogoro kwa ajili ya maandalizi ya mechi ya ligi dhidi ya watani wake wa jadi, Simba SC, itakayopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Aprili 29 2018.

Kikosi hicho kimeanza mazoezi yake jana kwenye Uwanja wa Jamhuri ikiwa ni takribani siku tano pekee zikiwa zimesalia kuelekea mechi hiyo inayoteka hisia za watu.

Mbali na Yanga, Simba nao walikuwa wa kwanza kutia miguu mjini humo baada ya mechi yake ya ligi na Lipuli, ambapo inafanyia mazoezi yake kwenye Uwanja wa Chuo Cha Biblia.

Hivyo timu zote hizo, Simba na Yanga, zipo Morogoro hivi sasa kabla hazijakutana kwenye mtanange wa Jumapili ya wiki hii.

Rais Magufuli Awataka Wastaafu Kuiga Mfano wa Mizengo Pinda

$
0
0
Rais Magufuli Awataka Wastaafu Kuiga Mfano wa Mizengo Pinda

Rais John Magufuli jana alimmwagia sifa Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda kwa kumwelezea ni kiongozi mkimya na asiyependa kuzungumza ovyo ovyo.

Rais Magufuli alisema Pinda, maarufu kama Mtoto wa Mkulima, ni kiongozi anayefaa kuigwa na viongozi wengine, na kwamba hata yeye siku akistaafu atamfuata ili kujifunza.

Aliyasema hayo jana mjini Dodoma wakati akifungua Tawi la Benki ya NMB la Kambarage na Jengo la Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF).

“Mzee Pinda anaishi maisha ya kawaida sana, hapigi kelele, hazungumzi chochote, Mzee Pinda ‘you are too special’ (wewe ni mtu wa kipeke),” alisema Rais Magufuli.

“Watu watakukumbuka (Pinda) kwa ukarimu wako, wewe ni mtu wa kawaida sana. Sasa hivi hatujui thamani yako lakini ipo siku tutaijua.

“Ndiyo maana bado unaonekana kijana, hujipi ‘pressure’ (hofu), unaamini kile unachofanya, na mimi nikistaafu nitakuja kuchukua ‘course’ (mafunzo) kwako.”

Sifa kwa Pinda zinakuja miezi saba tangu alipokosoa viongozi wastaafu wa "maeneo mengine" wanaosemasema kila wakati kuhusu uendeshaji wa serikali.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Septemba 11, mwaka jana Rais Magufuli alitoa mfano wa majaji wastaafu ambao alisema ni tofauti na wastaafu wengine na kwamba huenda kujua sheria ndiko kunakowasaidia kutokuwa waropokaji.

Rais Magufuli alisema hayo wakati wa kumuapisha Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma.

“Nawashuruku majaji wakuu wastaafu, Barnabas Samatta na Augustino Ramadhani, walifanya kazi kubwa ya kujenga misingi ya mahakama nchini," alisema.

“Bahati nzuri majaji hawa ni waadilifu sana huwezi kumsikia Jaji (Mkuu mstaafu Othman) Chande, (Barnabas) Samatta, Augustino (Ramadhani), (Damian) Lubuva au majaji walioko hapa... ukiangalia wastaafu wa maeneo mengine hawachoki kusema, wanawashwawashwa.

“Ndiyo maana nawapongeza sana mahakama...Ni safi mno, nina uhakika wanapotaka kutoa ‘advice’ (ushauri) yoyote (wowote) lazima wanakushirikisha (Jaji Mkuu); ndiyo faida ya kujua sheria.

“Sisi wengine huku ambao hatujajua sheria mahali popote, chochote unaweza ukazungumza.”

Watu 10 Wauawa kwa Kugongwa na Gari la Mizigo

$
0
0
Watu 10 Wauawa kwa Kugongwa na Gari la Mizigo
Watu tisa wameuawa mjini Toronto, nchini Canada baada kugongwa na gari la mizigo ambalo lilielekea katika mtaa wenye watu wengi. Wengine 16 wamejeruhiwa pia.
Mashuhuda wanasema kuwa dereva huyo aliendelea kuliendesha gari takribani umbali wa kilomita moja hivi.
Diego de Matos yeye alikuwa akiendesha gari lake karibu na eneo hilo,ameiambia BBC kuwa aliona watu wawili wakigongwa na gari hilo la mizigo.
"Lori hilo liliwagonga mwanamke na mwanaume.Hata hivyo baada ya kuwagonga watu hao dereva wa gari hilo aliendelea kuendesha gari hilo ambapo,mita chache mbele kulikuwa na miili mitano ama sita ikiwa chini.Na inavyoonekana dereva alikuwa akiyumbisha gari nje mara ndani ya mtaa huo,ilikuwa ni jambo la kutisha." Diego De Matos
Waziri wa usalama wa Canada Ralph Goodale amewaambia waandishi wa habari kwamba ni mapema kusema tukio hilo ni la kigaidi.
"Kuna ushirikiano wa kutosha kwa Polisi,katika kuchunguza jambo hilo,na tutatoa majibu ya hili kwa umma.Lakini kwa sasa hakuna taarifa zozote kwangu kuhusiana na chanzo ama lengo la tukio hili.'' Ralph Goodale
Kumekuwa na matukio ya magari makubwa kutumiwa na magaidi kusababisha vifo katika maeneo yenye mikusanyiko,baada ya mamlaka za usalama kudhibiti njia za magaidi hao zilizooeleka.
Matumizi ya magari makubwa ya mizigo,ni mfumo mpya ambao umekuwa ukitumiwa na magaidi kutekeleza azma yao kufuatia kubainika kwa njia zao zilizo mara zote.

ACT Wazalendo Wafunguka ishu ya 'Kufichwa Zitto Kabwe' Baada ya Kuikosoa Ripoti ya CAG

$
0
0
ACT Wazalendo kupita kwa Katibu wa Uenezi wa Chama hicho Ado Shaibu kimefunguka na kuweka wazi kuwa Kiongozi Mkuu wa chama hicho Mhe. Zitto Kabwe hajafichwa kama ambavyo watu wanasema bali sasa hivi ameongezewa ulinzi na mienendo yake inaangaliwa kwa kina na idara ya ulinzi na usalama.

Ado Shaibu amedai kuwa zipo taarifa zinaenea kwenye mitandao ya kijamii mbalimbali kuwa kiongozi huyo anaweza kuuawa na kusema ndiyo sababu kubwa ambayo imepelekea sasa kulindwa kwa daraja la juu kabisaa la ulinzi.

"Ukisikia kwamba kiongozi wenu anataka kushambuliwa, kudhuriwa au kuuwawa ni muhimu kuyapa uzito sana maneno hayo kwa hiyo sisi tumechukua hatua kadhaa kwanza ndugu Zitto alikuwa na mkutano wa hadhara Kigoma Ujiji alikuwa anataka kuzungumzia masuala yanayoendelea nchini kuhusu ripoti ya CAG lakini alitaka kuwaeleza watu wa Kigoma wapi amefikia kuhusu suala la watu wa Kigoma kunyanyaswa uhamiaji na kutaka maoni ya wananchi kwa hiyo mkutano wenyewe huo ulizuiwa na sisi tulikuwa na mkutano wa ndani wa chama kutokana na mambo haya yanayoendelea tukaamua ni bora tusimamishe kikao hicho" alisema Shaibu

Ado Shaibu aliendelea kusema kuwa

"La pili kiongozi wa chama ameongezewa ulinzi na idara ya ulinzi na usalama ya chama kuhakikisha kwamba anakuwa salama na kuchunga mienendo yake ndiyo maana utaona baadhi ya magazeti yanasema Zitto Kabwe amefichwa, ndugu Zitto ni kiongozi hawezi kufichwa lakini mienendo yake sasa inadhibitiwa na idara ya ulinzi na usalama ya chama awe wapi, muda gani na kwanini, awe ndani ya nchi, nje ya nchi hayo ndiyo mambo ambayo idara yetu ya ulinzi na usalama inayapa kipaumbele kikubwa, kwa hiyo kiongozi sasa analindwa kwa daraja ya juu" alisisitiza Ado Shaibu

Baada ya Zitto Kabwe kuonekena ameikomalia sana ripoti ya CAG hasa zaidi kuhusu 1.5 Trilioni ambayo haileweki imetumikaje zilianza kusambaa taarifa mbalimbali kuwa kiongozi huyo naye anaweza kushughulikiwa na watu wasiojulikana.

Polisi Wajaribu Kutumia Kidole cha Marehemu Kuchora ‘Password’

$
0
0
Kutoka Florida nchini Marekani, Jeshi la Polisi limeshukiwa na watu baada ya askari polisi wawili kuingia kwenye nyumba iliyokuwa na msiba na kushinikiza kufungua ‘unclock‘ simu ya marehemu.

Inaelezwa kuwa marehemu huyo Linus Phillip, 30, aliuawa pindi alipojaribu kuwatoroka polisi katika kituo cha mafuta eneo la Largo mnamo March 23, 2018.

‘Bila kujali Bifu zenu ila katika hili tuko Pamoja’ RC Makalla

Mpenzi wa marehemu Victoria Armstrong ameeleza kusikitishwa na kitendo hicho ambacho polisi wenyewe wamedai kuwa ni sehemu ya upelelezi wao.
Viewing all 104663 articles
Browse latest View live




Latest Images