Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Maskini, Mjasirilia Mali Carol Ndosi Asimuli Jinsi Alivyopata Hasara Kubwa Mwaka 2017 Kwenye Matamasha ya Nyama Choma

$
0
0

Ameandika Carol Ndosi
-------------------------------

Barua kwako Mjasiriamali Unayeanza.

Salaam kwako, ni matumaini yangu kuwa Mwaka 2017 unaumaliza kwa kushukuru Mungu kwanza kwa uhai na afya uliyo nayo wewe, na uwapendao. Ni wengi walitarajia kufika, lakini mipango ya Mungu haina makosa.

Nitaongea kama ninavyoongeaga na vijana wengi tukikutana kubadilishana mawazo..Nitaongea kama Sister Carol.

2017 umekua ni mwaka ambao personally nimesikia vilio vingi sana katika fani yangu ya ujasiriamali. Ingawa wengine wameweza kutafuta upenyo wa kubadilisha ‘challenge into opportunity’, wengi wameishia kufunga biashara, kubadilisha biashara, kurudi kuajiriwa kwa wale waliokua wamejiajiri na wengine kukata tamaa kabisa ya maisha.

Mzunguko wa fedha haupo kama ulivyo kua miaka 2 iliyopita, na kwa wasomi ni kitu kinachoeleweka kabisa lazima nchi ipitie mtikisiko kukiwa na major reforms kwenye sekta za biashara na uchumi. Nilisoma mwezi wa 9 au 10 kuwa zaidi ya biashara 7000 zimefungwa ndani ya mwaka mmoja. Nilijiuliza sana ‘what became of all those who depended on these businesses all the way down to the value chain?’.

Nilijifunza siku nyingi kuwa ukitaka biashara iwe sustainable, uongeze value kwa kushirikisha watu wengi zaidi kwenye chain. Kwa mfano, kwenye biashara ya matamasha ambayo wengi ndio mnanifahamu kupitia Nyama Choma Festival, tunajivunia kuwa sio tu ni biashara lakini tumeweza kuunganisha supply chain kutoka kwa mfugaji, mkulima, wauza nyanya na tangawizi sokoni, wafanya usafi, watu wa maturubai, viti, meza, vyombo vya usalama, vya afya..the list goes on.

Ndio maana jukumu la kuendesha hili tamasha ni kubwa mno na tunaamini kwa miaka 6 hatujaweza wenyewe bali kwa kudra za mwenyezi Mungu na neema zake pamoja na support kutoka kwa wananchi na wadau wetu.

Nakuandikia wewe mjasiriamali leo, ambae ulianza kama mimi, kwa juhudi na bidiii na mtaji wako MWENYEWE, no offence kwa wale ambao wamekua spoon fed, tena kuna ambao nawafahamu ‘wameboostiwa’ lakini mafanikio yao ni kutokana na juhudi walizoweka baada ya ‘kuboostiwa’. But I honestly have issues with arrogant condescending pompous people who did not knock down their own doors.

Nataka nikusisitizie kuwa haijalishi mara ngapi utaanguka, au nani alianza safari na wewe akakuacha au umepoteza mali ngapi, cha msingi ni nafsi yako inakwambia nini kuhusu dhamira yako. Dhamira yangu ni kufanya kazi kwa bidii, kuleta maendeleo kwa wanaonitegemea na wanaonizunguka. Huwa najitahidi kama nina furaha, basi wanaonizunguka wawe hivyo pia. This pushes me everyday, together with what I believe is my purpose, which is to aspire to inspire.

Sasa nikueleze tu tuliyopitia sisi kama Nyama Choma Festival mwaka huu, ujaribu kuona kama unaweza kupata inspiration au motivation kutokana na hili. Kujenga brand si jambo dogo, tumejitahidi, 7 years in 2018 ; we are beyond grateful for the run that we have had. We have seen the best and the worst. Kama nilivyosema, miaka 2 kidogo kama nchi (false modesty) tumetikisika kwenye mzunguko wa fedha, hata wadhamini nao mtikisiko umewaathiri. Haya makampuni ya bia na telecomms ambao ni big spenders kwenye sponsorship wamecut down sana marketing budgets zao.

So kwa mfano, TNCF ilikua inaendeshwa kwa 65% ya sponsorship fee na 35% ya makusanyo toka kwenye kiingilio getini. 2016/17 imekua ikiendeshwa na operating capital ya kampuni, na mwenye tamasha pamoja na 25% sponsorship fee na chochote kinachopatikana getini.

Kwa wachumi mtakua mmeelewa kabisa ilihitaji turnout kubwa kuwa na turnover kubwa. Haisadii pia kama brand umeijenga kwa standard fulani kwahiyo scaling back itaathiri quality of the event. 2016 kwanza tukasema kwasababu hali sio nzuri, tunapunguza Dar editions from 4 to 3 maana purchasing power ya watu pia imeshuka..ma-buckets na ma-ndafu hayanunuliwi kama yalivyokua yananunuliwa 2015.

Anyways, tulipitia changamoto nyingine ya crack down ya mamlaka ya kodi, si kwetu bali kwa washiriki wetu. Wengi wa washiriki wetu ni wajasiriamali wadogo au ndio wanajaribu, chochote wanachokipata pale ndio kinampa nguvu ya kwenda kufanya kikubwa zaidi. Utekelezaji wa makusanyo ikabidi wajasiriamali na wafanyabiashara wote nyama choma kuwa na mashine za EFD, failure of which walichukuliwa hatua kwa kupigwa fine. Hii iliwanyong’onyeza wajasiriamali wengi na tukapoteza wachoma nyama na washiriki wetu mashuhuri katika kushiriki tena kwa kuogopa fine maana ilikua sio kukosa mashine tu, hata kama unayo, umejisahau kutoa wakakukuta hata kwa mteja mmoja ilikua ni fine not less than 2.5 Mil TZS. Iliwaathiri pia sponsors ambao walikua wakishiriki wanauza na bidhaa zao pia so guaranteed return on investment.

So 2017 tukabadilisha ratiba na kufanya tamasha la kwanza Dar es Salaam 29th April..siku mvua KUBWA sana iliponyesha in years. Ile mvua ilikua historical, na Leaders Grounds bahati mbaya tulikua hatujashuhudia mvua ikinyesha kama maji yakijaa panakuwaje. It was horrible. Palifurika! First event of the year in Dar,( shimo lenu la hela) and this happens.
On top of that media partner wa kipindi hicho alituangusha ilikua tufanye media campaign kabambe lakini hadi Jumatano kabla ya event bado tulikua tunatafutana na MOU…labda promo zaidi ingesaidia.We were devastated. Not just because sisi kama sisi tulipata hasara ya 68 Mil+ ( mind you hamna sponsorship funds tunabeba budget wenyewe hapo na mdhamini mmoja mkubwa), but sababu hamna kitu huwa kinatuumiza kama mabanda ya nyama choma yakibaki na chakula. Kwetu sisi hapo ndio tunaona tumeshindwa kudeliver, even if the rain was out of our hands contrary to what people used to say about us eti tunastopisha mvua..smh.

Anyways, dusted ourselves off, head held high and marched on….so fast forward the next event in Dar..again ndio shimo letu hili. Tumepiga loss in April, we have 3 events to do before the Dar one..tulifanya..ila kwa mbinde. Ikaja ya Dar ya August, it wasn’t bad but it wasn’t good either, ndio sheria ya matamasha ilikua imeanza kutekelezwa, ikabidi tuzime mziki saa 7…tofauti na saa 8 au 9 tuliyokua tunaendaga.

Tukapiga moyo konde na kusema let's keep pushing, na tuwaze namna gani tunaweza endelea kwenye fani aidha kwa kuscale back au kucome up na njia nyingine ya kuwafikia wateja wetu. Tabata BBQ Fever was born, tukasema sasa tunafanya nyama choma kwenye vitongoji. Tukafanya matayarisho yetu ya Tabata, ingawa tulitapeliwa uwanja at first (si kwa hela), watu tuliokua tunaongea nao kumbe sio wamiliki na baada ya mmiliki kujua kidogo ikawa problem..lol..anyway tuliisort tukafanya set up Friday, Saturday event.

Come Saturday, event is ongoing..tukafuatwa tuzime mziki na kusambaratisha wanachi saa 4 usiku. Kibali chetu kilisema Saa 6 usiku ndio mwisho. Hapo tukawa tumeingia loss ingine, because kwa wale kwenye event business 2 hours is a lot and can give you 10 Mil Tzs easily. So hadi hapo ikawa ni loss after loss.

Bado tukaendelea kupiga moyo konde, tukapambana na za mkoani, Mwanza, Arusha, Dodoma huku tunaendelea kurecover loss na tuko na sponsor wetu yule yule mmoja maskini hajawahi kututupa #TeamGreen. Tukawa tunajipa matumaini Dar 2nd of December walau tutapumua. Uwanja wa Leaders ukapigwa marufuku one week before our event, with non refundable expenses amounting to 23 Mil TZS. Tulitoa tamko na kuwafahamisha wateja wetu, tukaomba sana ushirikiano kutoka kwa washiriki na wahudhuriaji maana kama nilivyosema, nyama choma sio ya waandaji tu, kuna wengi mno wanaotegemea jukwaa hili na ndio maana ilibidi tuappeal to the masses to save this.

Tanganyika packers was the only option lakini kama ilivyo desturi ya Watanzania, huwapeleki tu venue mpya, we saw this tulivyohamishwa toka UDSM to Leaders the first time. Tukajitahidi kufanya matayarisho lakini siku ya siku, masupppliers kutoka wenye mabati, mobile toilets, tents walituangusha MNO.

Washiriki wetu walijaribu kupambana na MVUA kubwa tu na hata baada ya kunyeshewa mkaa na nyama waliamka tena mvua ilivyokata na kuendelea. Kuna wateja walikuja mvua inanyesha wanatembea kwenye mvua kuja kutusupport. Kuna wajasiriamali wadogo walifanya wawezalo kutokana na mazingira ili biashara iendelee.

9 Dec jambo la msingi nililo kuwa najiambia ni ‘ I just want this night to end’. Everything was just going WRONG. Mziki ukazimwa na DJ aliyekua anatake over sababu aliingia kwenye mfarakano na walinzi katika kujitambulisha wakakosana lugha. IT WAS A HORRIBLE DAY. So another loss incurred, brand suffered. Kesho yake bado uamke uwaze ‘what is the next step?’.

Nimetumia wiki moja kukaa na kupanga tena mawazo na ARI maana yataka ARI kuendelea. Bado naendelea kujipanga na team, lakini ninalofahamu ni QUITTING is NOT an option. Leo nimeamka, mdhamini wetu #TeamGreen amepledge tena for 2018, lakini yabidi kukaa chini na re-strategize. At least thats good news and we are hopeful. I want to insist on these things, choose your partners wisely..kuna ambao tuliwategemea lakini wametuangusha vibaya mno. Some support systems are just there for material things and when you have something, We are not friend-less for no reason. You might have better luck than some of us. If you are a woman, Some support systems because of their sexism and male chauvinistic behaviours will turn on you when you don’t agree with their shenanigans or do not accept defeat.. they will even go to the length of tarnishing your brand and when they fail claim you did not ‘appreciate’ them hence the retaliation. The other is resilience to keep going..kama hujazungukwa na ambao wanakwambia ‘unaweza’ inabidi ujiambie mwenyewe.
Some will just want to watch you drown because you were a good swimmer, so ‘kama alikua anajua kuogelea mbona leo anazama’ kind of mentality.

This happened to us 6 years down the line, and we were broken. You will fall, you will rise but you cannot STOP. Kama wewe unasoma hii sasa hivi na ulikua ndio kwanza unaanza au umekutana na misuko suko please, first know your purpose. My purpose is to use what I have to uplift others, and because of that I keep going…no matter what you throw at me, I will stand up and keep walking. GOD gave me a bullet proof vest that only HE can penetrate. Find your purpose and let it drive you! let it be the reason for you to keep going everyday no matter what.

Sympathy? why not for those filled with compassion and empathy will reciprocate. Only the evil spirited will mock. Tunaonewa? Hell YES! Walk in our shoes and tell us that is not true. It doesn’t stop us though! We keep pushing! Against all odds! Nilienda kuappeal decision ya leaders nikawa rejected na kuishia kuzimia mbele za watu..did I stop? No! Niliomba nionewe huruma? NDIO! Sababu this is bigger than me…way bigger.

I take my failures in what I do seriously because if I fail..Aunt Asia na Muhsin wa mabati amefeli, if I fail, Imani wa tents amefeli, If I fail, Abraham wa sound system amefeli, if I fail, G4S, JKT SUMA, POLICE wamefeli, if I fail, Aggreko amefeli, if I fail, Mabanda ya Nyama Zaidi ya 10 na wafanyakazi sio chini ya 7 wanaotegemea kipato hicho wamefeli, if I fail wote waliowauzia chochote hawa mabanda na hawakumaliziwa hela zao wamefeli, if I fail, watoa huduma wote wamefeli, if I fail, mamlaka ya kodi imefeli, if I fail my team imefeli, if I fail my family, my two beautiful daughters wamefeli, if I fail, my country has failed.

I CANNOT AFFORD TO FAIL, and when I do, I CANNOT NOT TRY AGAIN. That is my purpose. All the best with yours!

Rosa Ree Afunguka Sababu ya Kuhamia South Afrika Kwa Muda...

$
0
0

Msanii Rosa Ree amesema sababu za yeye kuwa South Africa kipindi hiki ni kufanya video ya ngoma yake mpya na msanii ambaye anafanya vizuri pande hizo za South Africa Emtee.

Licha ya kuwa mmoja kati ya wasanii ambao Rosa anawakubali pia jamaa tayari ametoa ngoma nyingi kama #RollUp #WeUp #CornerStore #Plug na kufanya kupata heshima kwa kazi zake tusubiri na tuone mkwaju mpya kutoka kwao.

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special, Imeboreshwa zaidi

Siri 6 za Ali Kiba kumuoa Mkenya na Kuachana na Wabongo hizi hapa

$
0
0
Alfajiri ya Aprili 19, mwaka huu, Kiba alifunga ndoa na mrembo Amina Khaleef katika Msikiti wa Ummul Kulthum uliopo mjini Mombasa, Kenya. Ndoa hiyo ilifungishwa na Sheikh Mohamed Kagera.
Hakika ilikuwa ni furaha, shangwe, nderemo na vifijo kwa maharusi hao, wanafamilia na mashabiki wa Kiba mjini Mombasa mara baada ya ndoa hiyo kufungwa.

Mara baada ya kufungwa kwa ndoa hiyo, mitandaoni kulichafuka ambapo baadhi ya mashabiki wa Kiba walikuwa wakihoji ni kwa nini mkali huyo wa Wimbo wa Seduce Me ameacha warembo kibao Bongo na kwenda kwa Amina wa Mombasa? Kufuatia wengi kutaka kujua Amina ni nani au ana nini cha tofauti kilichomteka Kiba, Risasi Jumamosi lilifanya uchunguzi wake wa kushiba na kuibuka na siri sita zilizomvutia Kiba kwa mrembo huyo na kuwasahau kabisa warembo wa Bongo;
[​IMG]​
1: SIFA YA KUWA MKE
Uchunguzi huo ulibaini kwamba, Amina ambaye aliingia kwenye uhusiano wa uchumba na Kiba mwaka 2016, ana sifa za kuwa mke (wife material) na pia anafaa kuwa mama bora kutokana na utulivu wake na kujua malezi kwa jumla. Ilibainika kwamba, Amina ni binti mwenye maadili na aliyekulia kwenye familia iliyoshika mno Dini ya Kiislam hivyo ‘amekwiva’ kwenye eneo hilo la kuwa mama bora wa familia ukilinganisha na warembo wengi wa Kibongo ambao ilisemekana, wengi hawajatulia na hawajashika dini kwa dhati zaidi ya kuigiza tu.



2: SIYO TEGEMEZI, NI MCHAPAKAZI
Uchunguzi huo uliotumia watu wa nyumbani kwa akina Amina ulibaini kwamba, mrembo huyo mwenye umri wa miaka 23, siyo mtu wa kukaa tu nyumbani na kusubiri kuletewa pizza au chipsi kuku na mwanaume, bali ni mchapakazi asiyependa kuwa tegemezi, tofauti na mabinti wengi wa Kibongo ambao hubweteka na kutegemea kila kitu kutoka kwa wanaume.

3: SHULE IPO KICHWANI
Ilifahamika kwamba, Amina hakukimbia umande kwani ni msomi mwenye shule yake kichwani, akiwa amehitimu masomo ya uhasibu kwa levo ya chuo kikuu na kuwa mfanyakazi wa serikalini katika Kaunti ya Mombasa. Hii ni tofauti na baadhi ya mabinti wa Kibongo ambao wengi walikimbia umande.


4: UZURI WAKE SIYO FEKI
Ukimtazama Amina hata kwenye picha zilizosambaa mitandaoni, utagundua kuwa uzuri wake ni wa asili na siyo wa kutengeneza yaani feki kama walivyo warembo wengi wa Kibongo. Ilielezwa kuwa, kutokana na mvuto wa kipekee alionao, basi Amina amebeba maana halisi ya uzuri wa mwanamke. Hana makalio feki ya kutengeneza wala nido zake kifuani siyo za kubusti na hategemei make-up ili aonekane mzuri bali kila kitu kwake ni cha asili.


5: HASHINDI NA KUKESHA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII
Uchunguzi wetu huo ulibaini pia kwamba, Amina siyo mtu wa kushinda na kukesha kwenye mitandao ya kijamii kama walivyo warembo wengi ambao kazi yao huwa ni kuposti picha na video za kuwatamanisha wanaume. Katika kuthibitisha hilo, tangu aingie kwenye uhusiano na staa huyo mkubwa ambaye kwa mrembo mwingine angefanya matangazo kwenye mitandao ya kijamii hadi dunia nzima ijue, lakini Amina yeye hakuwahi kufanya hivyo.


6: ANAJUA ATAKAVYODILI NA WALIOMZALIA KIBA
Ilifahamika kwamba, Kiba ana watoto watatu ambao kila mmoja ana mama yake, lakini ilisemekana Amina alimhakikishia atakavyodili na mama wa watoto hayo na yupo tayari kuwalea bila kusababisha drama au tafrani. Sifa nyingine aliyoelezwa kuwa nayo Amina ni pamoja na kujua kutunza siri za familia kama alivyofanya kwenye uhusiano wake na Kiba tangu mwaka 2016 bila kujali skendo zilizokuwa zikimuandana staa huyo.


MASKINI MASTAA HAWA, BAHATI HAIKUWA YAO

Kabla ya kumuoa Amina, Kiba aliwahi kutajwa kutoka na warembo mbalimbali wakiwemo wanawake watatu aliozaa nao, mastaa wa Kibongo, Jokate Mwegelo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Jacqueline Wolper na wengineo ambao mashabiki wao wengi waliwahurumia kwa kukosa bahati ya kuolewa na staa huyo anayejiita Pasua Kichwa

Bombardier Yazua Mtifuano Bungeni....Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 25

$
0
0







Bombardier Yazua Mtifuano Bungeni....Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 25

Maxcom yatoa Ufafanuzi Utata Tiketi za Mabasi ya Mwendokasi...Kumbe UDA-RT Hawajawalipa

$
0
0
Maxcom yatoa Ufafanuzi Utata Tiketi za Mabasi ya Mwendokasi...Kumbe U DART Hawajawalipa

Soma Hapa Chini:


Liverpool Noma Yamchapa Roma Magoli Matano

$
0
0

Liverpool wameibuka na Ushindi kwenye Dimba lao la Anfield, Shughuli inahamia Roma wiki ijayo kwenye Mchezo wa Marudiano Je Roma. Watafanya ‘Come Back’ kama walivyofanya kwa Barcelona au Liverpool watafanya kile walichomfanyia Man City?

John Heche: Waliniambia Watanipoteza na Kuna Kesi Inaandaliwa Dhidi yangu

$
0
0
Mbunge wa Tarime Vijijini (Chadema), John Heche amesema anatishiwa maisha kutokana na kauli zake za kuikosoa Serikali, likiwemo sakata la ufisadi wa mradi wa hati za kielektroniki ya kusafiria.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 24, bungeni mjini Dodoma, Heche amesema licha ya kutotishika na vitisho hivyo amebainisha kuwa kuna kesi inaandaliwa dhidi yake na muda wowote anaweza kukamatwa.

“Kuna njama za kutishia watu wanaohoji masuala mbalimbali ambayo tunayazungumza na kuonekana wazi kuigusa Serikali,” amesema.

Sakata la mradi huo lilitikisa katika mkutano wa Bunge uliofanyika Februari mwaka huu, ambapo mbunge wa Momba (Chadema), David Silinde pia aliligusia na kubainisha kuwa mradi huo umekuwa ikitekelezwa kwa gharama za Dola 40milioni za Marekani, wakati taarifa zilizopo ni kuwa mradi huo ulikuwa na thamani ya dola 16 milioni za Marekani, sawa na Paundi 11 milioni.

Mradi huo wa hati za kusafiria ulizinduliwa Januari 30, 2018 na Rais John Magufuli.

Msanii Diamond Diamond Aula...Kutoa Burudani Kombe La Dunia 2018 Nchini Urusi

$
0
0
Msanii nguli wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz, kwa kushirikiana na kampuni ya Coca-Cola ametangaza kuwa ameshiriki kuimba wimbo utakaosherehesha Kombe la Dunia 2018 uitwao Colours.

Wimbo huo uliotungwa na mwanamuziki Jason Derulo wa Florida, Marekani, Diamond ameshiriki kuweka maudhui ya lugha ya Kiswahili na umetayarishwa na prodyuza Nahreel kwa kushirikiana na maprodyuza kutoka nchi nyingine chini ya udhamini wa kampuni ya Coca-Cola.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, amesema anayo furaha kupata fursa ya kushiriki kuimba kuimba wimbo wa mashindano haya makubwa ya kidunia na kuitangaza Tanzania na lugha ya Afrika bila kusahau tasnia ya muziki kwa ujumla.

“Kwangu hii ni nafasi nyingine ambayo najivunia kuipata ya kutangaza muziki wa kitanzania sambamba na lugha ya Kiswahili kwa kuwa sehemu niliyoshiriki kuimba nimetumia lugha ya taifa la Tanzania ambayo inazidi kupata umaarufu mkubwa duniani”alisema Diamond

Kwa upande wake Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini, Sialouise Shayo, alisema kampuni ya Coca-Cola ambayo ni moja ya mdhamini wa mashindano haya makubwa ya soka duniani inayo furaha kwa msanii kutoka nchini Tanzania kushiriki kuimba wimbo maalum wa mashindano haya. “Tuna imani watanzania watapata mzuka wa soka dimbani na kujisikia sehemu ya mashindano haya”alisisitiza.

Prodyuza nguli wa muziki nchini na kanda ya Afrika Mashariki, Nahreel ,ambaye ameshiriki kutengeneza wimbo huu aliishukuru kampuni ya Coca-Cola kwa jitihada mbalimali ambazo imekuwa ikifanya kuwanyanyua wasanii wa hapa nchini ambapo mbali na Diamond naye ameshiriki kwenye tukio hili kubwa. “Ninayo furaha ya kufanya kazi na Diamond kwa mara nyingine katika tukio hili kubwa la mashindano ya Kombe la Dunia na najivunia heshima kubwa tuliyopewa”

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu

 Bonyeza Hapa Chini:

==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>   

Siri Wema Sepetu Kuutosa Msimba wa Masogange Yafichuka

$
0
0
BAADA ya kuwa gumzo msibani wakati wa kuagwa kwa mwili wa aliyekuwa video queen kwenye nyimbo mbalimbali za Bongo Fleva, Agness Gerald ‘Masogange’ kutokana na kutoonekana, siri imefichuka ya msanii wa filamu, Wema Sepetu kuutosa msiba huo.

 Awali habari zilidai kwamba Wema alishindwa kuhudhuria kwenye msiba huo kutokana na kwamba yeye na marehemu Masogange walikuwa na bifu kali na hawakuwahi kupatana.

“Unajua Wema na Masogange walikuwa hawaivi, sasa inawezekana ndiyo maana hajaonekana msibani. Au ana sababu nyingine? Mimi kwa kweli nimeshangaa kutomuona,” alisikika akisema mmoja wa waombolezaji aliyekuwa amefika katika Viwanja vya Leaders jijini Dar kuuaga mwili wa Masogange.

SIRI YAFICHUKA

Kutokana na gumzo la Wema kuutosa msiba huo, Risasi Mchanganyiko lilimtafuta kwa njia ya simu yake ya mkononi lakini iliita bila kupokelewa. Baada ya kutopokelewa, gazeti hili liliamua kumtafuta meneja wake, Neema Ndepanya ambaye alitoa siri ya Wema kutohudhuria msibani hapo ambapo alisema mwanadada huyo alipatwa na tumbo la ghafla ambalo lilimzuia kutoka kwenda popote.

“Wema alikuwa na nia ya kufika msibani kabisa na alikuwa ameshajiandaa lakini ilishindikana baada ya kuugua tumbo la ghafla ikabidi aahirishe tu, pia Mbeya alishindwa kusafiri maana Jumatatu ambayo ndiyo mazishi ya Masogange alikuwa anatakiwa kuhudhuria mahakamani kwenye kesi yake inayoendelea,” alisema Neema.

 Masogange alifariki dunia Aprili 20, mwaka huu katika Hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge jijini Dar na mwili wake kuagwa Aprili 22 katika Viwanja vya Leaders, Kinondoni na kusafirishwa nyumbani kwao Mbeya kwa mazishi yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.

STORI: Mwandishi Wetu, Risasi Mchanganyiko.

Kutana na Mtaalam wa Matabibu ya nyota za Binadam na Bingwa wa Tiba za Asili Afrika Mashariki.

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasi, Mfanyabiashara , Msani, ama mwanafunzi tunazo dawa na pete za bahati zenye uwezo mkubwa wakuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na SHABA WA SHABA kutoka Tanga,
Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki.
Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sasa amezianza ziyara zake za mikoani na atayatembeleye maeneo mbali mbali ndani na inje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nasiojulikana kwakutumia maji, Kioo na mitishamba.
Anazo dawa za mapenzi, kumrudisha alipoteya, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, kutoa ndagu , Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, Kuuza kwa haraka ( shamba, nyumba, Gari,...), Kesi mahakamani, Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na utajiri bila masharti na mengine mengi ya Siri...

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa nambari ya simu :
+255 785 358 267 ,
+255 785 358 267

Rais Magufuli awafunda Wabunge wa Afrika Mashariki

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutilia mkazo ajenda zitakazoimarisha zaidi umoja, upendo, ushirikiano na mshikamano baina ya nchi wanachama ili kufanikisha jukumu muhimu la kupambana na umasikini wa wananchi na kukuza uchumi.

Mhe. Rais Magufuli amesema hayo tarehe 24 Aprili, 2018 wakati akihutubia Bunge la Afrika Mashariki kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani, katika ukumbi wa Pius Msekwa uliopo ndani ya viwanja vya Bunge Mjini Dodoma ambako Bunge hilo linafanyia vikao vyake kwa mara ya kwanza katika mji huo.

Mhe. Rais Magufuli amesema Wabunge hao wanao wajibu wa kushughulikia migogoro ambayo imekuwa ikigharimu maisha ya wananchi, vikwazo vya biashara na uwekezaji, na kutilia mkazo ujenzi wa viwanda vitakavyochakata na kuzalisha bidhaa zitokanazo na rasilimali lukuki zilizopo ndani ya Afrika Mashariki ili manufaa ya rasilimali hizo yawanufaishe wananchi.

Ametaja miongoni mwa mambo yanayopaswa kutiliwa mkazo na nchi zote kuwa ni kuimarisha miundombinu ya usafirishaji na uzalishaji wa umeme wakutosha na wenye gharama nafuu, ambavyo ni muhimu katika ujenzi wa viwanda.

“Tafiti zinaonesha gharama za usafiri kwenye ukanda wetu ni mara 4 hadi 5 ukilinganisha na gharama za Asia Mashariki, Marekani na Ulaya na zinachangia kuongezeka kwa gharama za bidhaa kwa asilimia 40.

“Umeme pia umeonekana kuwa sio mwingi, utafiti uliofanywa na taasisi ya Power Africa mwaka 2015 umeonesha kuwa nchi zote 6 za Jumuiya ya Afrika Mashariki zina takribani megawati 6,500 tu za umeme, hiki ni kiwango kidogo mno kuweza kuhimili mahitaji ya uchumi wa kisasa” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Katika kutekeleza azma hiyo Mhe. Rais Magufuli ametoa wito kwa nchi wanachama kubadilishana uzoefu wa namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza na kutekeleza miradi muhimu ya maendeleo, na pia ameshauri nchi wanachama zisitegemee misaada pekee na badala yake zifikirie kutekeleza miradi kwa fedha zake zenyewe ili kuokoa muda na kupunguza gharama za miradi husika.

Mhe. Rais Magufuli amezungumzia juhudi zinazofanywa na Tanzania katika kufikia dhamira hiyo kuwa ni pamoja na kuanza ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) kuanzia Dar es Salaam hadi Dodoma ambayo itaunganisha hadi nchi za Burundi, Rwanda na Uganda, kujenga meli katika ziwa Victoria, kutekeleza mradi wa uzalishaji wa umeme katika mto Rufiji (Stieglers’ Gorge), kununua ndege 6, kujenga barabara, kupanua bandari ya Dar es Salaam, ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania, kuboresha viwanja vya ndege 11 na amepongeza juhudi mbalimbali zinazofanywa na nchi nyingine wanachama wa Afrika Mashariki.

“Nataka kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge wa Afrika Mashariki kuwa Serikali ninayoiongoza itaendelea kushirikiana na Bunge hili katika masuala mbalimbali ya kuiunganisha jumuiya yetu, na ninawaomba nanyi mtekeleze wajibu wenu wa kuwaunganisha na kuwaelimisha wananchi ili waone umuhimu wa jumuiya hii” amebainisha Mhe. Rais Magufuli.

Kwa upande wake Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Martin Ngoga amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kulihutubia Bunge hilo na amempongeza kwa jitihada zake za kujenga nidhamu ya utumishi wa umma, kuzidisha mapambano dhidi ya rushwa, kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, kukuza uwekezaji na biashara ikiwemo ujenzi wa viwanda na kuonesha uongozi mahiri, na ametoa wito kwa Watanzania kuunga mkono juhudi hizo.

Pamoja na Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, viongozi wengine waliohudhuria wakati Mhe. Rais Magufuli akihutubia bunge hilo ni Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Naibu wa Pili wa Waziri Mkuu wa Uganda Mhe. Kirunda Kivejinja, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi, Mawaziri, Mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali hapa nchini, viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dodoma
24 Aprili, 2018

Je Agness Masogange Ameuawa...Madai Yaibuka

$
0
0
WAKATI mwili wa ‘Video Queen’ maarufu Bongo, Agness Gerald ‘Masogange’ ukitarajiwa kuzikwa jana nyumbani kwao Utengula, Mbalizi-Mbeya, utata umeibuka juu ya kifo hicho kufuatia kuibuka kwa madai kuwa mrembo huyo ameuawa.

Masogange alipatwa na umauti huo, Ijumaa iliyopita katika Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar alipokuwa amelazwa kwa takriban siku nne ambapo taarifa za awali zilieleza kuwa, mrembo huyo amefariki kwa ugonjwa Pneunomia (nimonia) na tatizo la kupungua damu.

 MADAI YA KUUAWA YAIBUKA

Mara baada ya kifo hicho kutokea, taarifa mbalimbali zilibuka na kutawala kwenye mitandao ya kijamii zikieleza kuwa Masogange ameuawa kutokana na kifo hicho kuwa cha ghafla.

“Inabidi kwa kweli uchunguzi wa kina ufanyike. Kifo chake kimekuwa cha ghafla mno, hajaumwa kiivyo na watu wengi tulikuwa tunajua ni mzima wa afya,” waliandika watu tofauti mitandaoni.

 WENGINE WAHUSISHA NA SIASA

Wengine walienda mbali zaidi kwa kukihusisha kifo hicho na masuala ya kisiasa huku wengine wakihusisha kifo chake na vigogo wa madawa ya kulevya.

Uwazi lilizungumza na majirani mbalimbali waliokuwa wanaishi na Masogange, maeneo ya Makongo Juu jijini Dar ambao walionesha kushtushwa na taarifa hizo za kuuawa huku wengi wakiliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi ili kuondoa huo utata.

“Kwa kweli tumeshtuka sana maana haya madai yalianza taratibu lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda ndipo yanavyoongezeka nguvu, sasa ni vizuri polisi wakajiridhisha,” alisema Abdul, mkazi wa Makongo Juu.

POLISI WAINGILIA KATI Wakati mamia ya waombolezaji wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya kuuaga mwili wa Masogange juzi Jumapili katika Viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es Salaam, polisi walilazimika kufika kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kuufanyia uchunguzi kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kujiridhisha kutokana na madai hayo ya kuuawa.

 Wanahabari wetu waliofuatilia hatua kwa hatua kifo hadi mazishi ya video queen huyo, walishuhudia polisi wakizuia kwa muda mwili huo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili hali ambayo ilisababisha ratiba za ibada ya kuaga mwili huo kuchelewa kuanza. Awali, ratiba ilionesha kuwa mwili huo ungechukuliwa Muhimbili mishale ya saa 2 asubuhi ili ratiba ya kuagwa ianze saa 3 kamili lakini kutokana na uchunguzi huo wa polisi, ratiba ya kumuaga mrembo huyo ilianza saa 6 kamili viwanjani hapo.

SOMA PIA: Job Opportunities at Tanzania Posts Corporation, Regional Managers

MIKE SANGU ANENA

Uwazi lilizungumza na mmoja wa waigizaji ambao walienda kuuchukua mwili huo, Mike Sangu ambaye aliweka wazi kuwa walilazimika kuchelewa kuanza kwa ratiba ya kumuaga kama walivyokuwa wamepanga awali. “Tulipanga hapa tuwe tumeondoka kabla ya saa 3 ili pale Leaders ratiba ianze saa 3 kamili lakini ndio hivyo tena polisi wamesema hadi wakamilishe kwanza uchunguzi wao ndio tukabidhiwe mwili,” alisema Mike.

MSEMAJI WA MUHIMBILI AFUNGUKA

Uwazi lilizungumza na Msemaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha ambaye alithibitisha polisi kufika hospitalini hapo na kuuchunguza mwili huo kwa ajili ya kujiridhisha kabla ya kuuruhusu mwili huo kwenda kuzikwa.

“Ni kweli, walifika kwa ajili ya kuufanyia uchunguzi ili kujiridhisha sababu za kifo kama unavyojua ni kifo cha ghafla,” alisema Aminiel. Hata hivyo, baadhi ya watu waliofika msibani walionesha wasiwasi wao baada ya kujua kuwa polisi waliamua kuufanyia uchunguzi mwili wa msanii huyo na kujiuliza kulikoni?

POLISI WANASEMAJE?

Uwazi lilitafuta Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, ACP Salum Hamduni na ili kujua kama ana taarifa za uchunguzi huo uliofanywa na polisi lakini hata hivyo alisema hana taarifa za uchunguzi huo.

Uwazi halikuishia hapo, lilifanya jitihada za kumtafuta Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Murilo Jumanne Murilo lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda kufuatia simu yake ya mkononi kuita bila kupokelewa baada ya kupigiwa mara nyingi. Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,(ZPC) Lazaro Mambosasa alipotafutwa na gazeti hili, alisema yupo mkoani Mbeya, hivyo hana taarifa rasmi kuhusu suala hilo.


TUJIKUMBUSHE

Kabla ya kukutwa na umauti huo, Masogane aliyeuza sura kwenye video mbalimbali za wasani wa Bongo Fleva ikiwemo Magubegube (Barnaba Elias), Msambinungwa (Tunda Man), aliwahi kupata misukosuko ya kuhusishwa na madawa ya kulevya.

Mwaka 2013, Masogange alikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Oriver Tambo nchini Afrika Kusini akidaiwa kusafirisha madawa ya kulevya aina ya Crystal Methamhetamine.Hata hivyo, baada ya kesi kuunguruma nchini humo, ilibainika kuwa hayakuwa madawa ya kulevya bali ni malighafi za kutengenezea madawa hivyo Masongange aliachiwa baada ya kulipa faini.

 Mwaka jana, Masogange alitajwa na kuunganishwa kwenye kesi ya matumizi ya madawa ya kulevya baada ya kutajwa katika orodha ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipokuwa akiendesha oparesheni ya watumiaji na wauzaji wa madawa ya kulevya.

Kesi iliunguruma hadi Aprili 3, mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar ilipotolewa hukumu kwa mrembo huyo kutakiwa kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi milioni moja na nusu.Masogange alilipa faini hiyo na hivyo kuwa huru hadi alipopatwa na umauti Ijumaa iliyopita.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, amina!

STORI: GPL

TLS Ni Chama Cha Umma Kifanye Kazi Kwa Mujibu Wa Sheria

$
0
0

Na Lydia Churi, Magreth Kinabo-Mahakama
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amesema Chama cha Wanasheria cha Tanganyika (TLS) ni taasisi ya Umma na siyo binafsi hivyo amekitaka kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kisheria kwa kushirikiana na Mahakama na kuacha kujiingiza kwenye masuala ya uanaharakati na siasa.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam Jaji Mkuu amesema TLS ni chama huru cha kitaaluma kwa kuwa kilianzishwa kwa mujibu wa sheria kufanya kazi kwa manufaa mapana ya Umma.

“Hatuwezi kukubali chama hiki kikajisemea kuwa wao ni chama binafsi na tukakubali, dhana ya ubinafsi haipo”, alisisitiza Jaji Mkuu.

Alisema jukumu la TLS ni Kuisaidia Serikali na Mahakama kuhusu mambo yoyote yanayogusa sheria, utawala wa sheria na kazi za kisheria na akaongeza kuwa dhana hii ndiyo inayoiunganisha Taasisi hiyo na Mahakama ya Tanzania.

Aidha, Jaji Mkuu amewataka viongozi wa TLS kushirikiana na Mahakama pamoja na Mihimili mingine ya dola  na kuacha malumbano kwenye vyombo vya habari kwa kuwa hayawasaidii kuendeleza chama hiki muhimu kwa wanasheria nchini.

Jaji Mkuu pia amewashauri viongozi wa chama hicho kumuheshimu Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuwa Sheria na Kanuni zote ni lazima zipitie kwake.

SOMA PIA:Job Opportunities at Ilula Orphan Program, Youth Program Officer

Alisema Mamlaka ya Baraza la Uongozi la TLS katika Kutekeleza Majukumu ya Umma ni kusaidia kuboresha elimu ya sheria na taaluma ya Sheria Tanzania na kuwawezesha wanataaluma wa sheria kupata elimu ya ziada ya sheria kwa kadri mabadiliko yanayotokea nchini na duniani.

Majukumu mengine ya TLS ni pamoja na kuwawakilisha, kuwatetea na kuwasaidia wanasheria Tanzania kuhusu mazingira ya kufanya kazi za kisheria na kuwasaidia wananchi wa Tanzania katika masuala ya kisheria yanayogusa Sheria.

TLS ni Taasisi iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria za nchi kabla ya Uhuru na kukubalika kuendelea kuwepo kama Taasisi ya Kisheria kwa malengo ya kuanzishwa kwake kuelekezwa kwenye manufaa ya umma kwa kushirikiana na Mahakama, Bunge, pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Chama hiki kilianzishwa kwa Sheria ya Baraza la Kutunga Sheria (Legislative Council) Namba 30 ya 1954 na ni moja ya Sheria nyingi za iliyokuwa Tanganyika kabla ya Uhuru, ambazo kwa mujibu wa Kifungu cha 4 cha Katiba ya Tanganyika  ziliruhusiwa kuendelea kutumika Tanganyika ilipopata Uhuru Disemba 9 mwaka 1961 kama Sheria za Tanganyika huru.


Wanafunzi 23 Wamefukuzwa Chuo Kwa Kuwa na Mahusiano ya Kimapenzi

$
0
0
Chuo Kikuu cha Kiislamu nchini Uganda kimewafukuza wanafunzi wake 23 kwa madai ya kujihusisha na mahusiano ya kimapenzi jambo ambalo ni kinyume na kanuni za taasisi hiyo.

Mratibu wa chuo hicho, Dk. Sulait Kabali, ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya Nidhamu, aliliambia gazeti la Daily Monitor kuwa wanafunzi hao wamefukuzwa kwa kuwa na mahusiano na kufanya mapenzi kwenye eneo la chuo.

Maamuzi hayo ya kuwafukuza wanafunzi hao yalifanywa na Kamati ya Nidhamu ya chuo hicho.

SOMA Pia: Nafasi za Ajira Serikali 

Je Unajua Kwanini ni Muhimu Kwa Mwanaume Kufanyiwa Tohara? Hizi Hapa Faidi zake Tano

$
0
0
Tohara ni muhimu sana katika afya ya mvulana yeyote yule, na ndiyo maana hata wizara ya afya ikaona ni vyema kuanzisha hata huduma ambayo itawafanya watu waweze kupewa huduma hiyo bure kwenye baadhi ya mikoa.

Pasipo kupoteza muda naomba tukaangalie faida za tohara kiafya kama ifuatavyo;

1. Usafi, Kikawaida Ngozi ya uume ( govi) huficha uchafu na pia kuzalisha mafuta meupe meupe yanayojulikana kitaalamu kama smegma ambayo huweka mazingira ya wadudud (bacteria kuzaliana) hivyo kusababisha magonjwa. Hivyo pindi mtu anapofanyiwa tohara huondokana na hatari ya kupata magonjwa hayo ambayo mara nyingi huitwa ni magonjwa ya zinaa.

2. Hupunguza hatari ya kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Mtu anapotahili ngozi ya kichwa cha uume huwa ngumu na kuzuia kupata michubuko kiurahisi tofauti na ya mtu ambaye hajatahili hivyo kupunguza hatari ya kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa kiasi fulani. Japo ukweli ni kwamba ili upukane na ugonjwa wa huu hatari wa ukimwi unakiwa kuna makini sana kwa kuachana na ngono zembe.

3. Kufanyiwa tohara ni kinga tosha dhidi ya magonjwa ya saratani ya uume ( penis cancer)
utafitiu unaonesha kua saratani ya uume inawapata sana watu ambao hawajatahili

4. Hupunguza hatari ya kupata saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake.
Utafiti pia unaonesha kua mwanamke kujamiiana na mtu ambaye hajatahili inamweka kwenye hatari ( Risk ) ya kupata saratani ya shingo ya kizazi kutokana na uchafu unaotunzwa kwenye govi kuweza kua na Virusi aina ya Human Papilloma Virus (HPV) ambavyo husababisha saratani ya shingo ya kizazi.

5. Kufanyiwa tohara huleta heshima, hii ni kwa wakubwa wenzangu nadhani watakuwa wameelewa zaidi

Monalisa Afunguka Bifu la Wema na Riyama Kumbe Halikuanzia Kwenye Tuzo

$
0
0
Monalisa Afunguka Bifu la Wema na Riyama Kumbe Halikuanzia Kwenye Tuzo
Baada ya kumalizika drama za hapa na pale kati ya Wema Sepetu na Rihama Ally, msanii wa Filamu Bongo, Monalisa amesema malalamiko ya Riyama yalikuwa ni zaidi ya tuzo aliyoshinda Wema.

Awali Rihaya alikuwa akilalamika kuhusu kushindanishwa na Wema Sepetu katika tuzo za za Sinema Zetu International Film Festival Award (SZIFF) na Wema kushinda tuzo hiyo.

Hata hivyo wawili hao walionekana kupatana mara baada ya kukutana katika kumpokea Monalisa akitokea Nigeria ambapo alishinda tuzo ya The African Prestigious Awards (APA) 2017 kwenye kipengele cha Msanii Bora wa Kike barani Afrika..

“Kwanza niseme nilivyofika pale sikutegemea kuona watu lakini nilivyoshuka nikakutana na wasanii wenzangu, nilijisikia furaha sana,” amesema Monalisa.

“Nilifurahi kuawaona, sidhani kama Riyama kamlalamikia Wema nyie tu ndio mnachukulia vibaya, Riyama alikuwa na malalamiko yake na mimi ninayafahamu toka siku ya kwanza,” Monalisa ameiambia Times FM.

Ameongeza kuwa Riyama na Wema wote ni rafiki zake na anaongea nao vizuri na wote si watu wa vinyongo.

April Mosi mwaka huu Wema Sepetu aliibuka mshindi wa tuzo mbili za Sinema Zetu International Film Festival Awards (SZIFF),

Mbeya City Wamwendea Kumchongea Obrey Chirwa TFF

$
0
0
Mbeya City Wamwendea Kumchongea Obrey Chirwa TFF
MBEYA City imesema haikubaliani na namna ambavyo mchezo wao dhidi ya Yanga ulivyo­chezeshwa jijini hapa hivi karibuni na hivyo wana­kata rufaa kupinga upa­tikanaji wa bao la Yanga kwa kuwa haikuwa rafu.



Katibu Mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe amesisitiza mjini hapa kwamba wamekasirishwa na maamuzi mabovu ya mwamuzi Shomary Lawi ambaye alionekana kushindwa kuumudu mchezo huo uliokumbwa na vurugu za ndani na nje ya uwanja.



Kimbe alidai kuwa hiyo ni mara ya pili kwa mwamuzi huyo kutoa maamuzi mabovu huku akikumbushia mchezo wa mzunguko wa kwanza kati ya Mbeya City dhidi ya Stand United uliyochezwa mwaka jana mkoani Shinyanga.

“Tunakata rufaa kupinga maamuzi mabovu ambayo yalitolewa kwenye mchezo wetu dhidi ya Yanga ,faulo ile ambayo ilizaa bao la Yanga haikuwa halali lakini pia tunatoa malalamiko yetu juu ya faulo ambayo aliicheza Chirwa dhidi ya Ramadhan Malima,” alisema Kimbe.

Pia Kimbe alizungumzia sakata la mchezaji Eliud Ambokile ambaye alitolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Danny Joram mnamo dakika ya 96 kisha baadae kuingia tena.



“Eliud Ambokile ni kweli alifanyiwa mabadiliko lakini wakati yanafanyika alikuwa hajui kuwa nafasi yake imechukuliwa na mtu mwingine ,lakini cha ajabu mwamuzi namba mbili alimuuliza Eliud kama anaweza kuendelea na baadae Eliud akaruhusiwa kuingia,”alisema kiongozi huyo ambaye amehusika na mikataba yote ya udhamini wa Mbeya City.



“Wakati Eliud anarudi uwanjani mwalimu Ramadhani Nsanzurwimo aliinuka na kumfuata mwamuzi wa mezani kumtaka amjulishe mwamuzi kuwa kuna mtu ameingia wakati akiwa amefanyiwa mabadiliko na ndipo viongozi wa Yanga nao wakamfuata mwamuzi na kuanza kumlalamikia,” alisema Kimbe.

Mbeya City wanaendelea na maandalizi kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Singida United utakaochezwa siku ya Ijumaa.

Hali Yangu si Nzuri Ila Sitaki Kwenda Kutibiwa Nje ya Nchi- Mzee Majuto

$
0
0
Hali Yangu si Nzuri Ila Sitaki Kwenda Kutibiwa Nje ya Nchi
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Kilakala, amemtembelea muigizaji mkongwe nchini, King Majuto, aliyelazwa katika Hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam, kwa siku mbili akisumbuliwa na tatizo la Nyonga.


King Majuto amemuleza ndugu Kilakala kuwa hali yake si nzuri sana lakini ameshapatiwa tiba ambayo inamhitaji mgonjwa kuwa na subra kwani inachukua miezi mitano na kuendelea kuweza kupona na pia amesema haitaji matibabu nje ya nchi kwani ana imani na tiba inaayotolewa na hospitali za nyumbani.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images