Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Mambo ni Hivi Casto Dickson Awakata Vilimilimi Wanaomponda Tunda Atanga Ndoa

$
0
0

Mambo ni Hivi Casto Dickson Awakata Vilimilimi  Wanaomponda Tunda Atanga Ndoa
Mtangazaji wa kipindi cha Siz Kitaa cha Clouds TV, Casto Dickson, anatarajia kufunga ndoa na video queen, Anna Kimario 'Tunda' kabla ya mwaka kwisha.

Akizungumza na MCL Digital, Dickson amesema atafanya hivyo kwa kuwa ndio mwanamke anayeona anafaa kuwa mke.

"Unajua nimekuwa na mahusiano na wanawake wengi, lakini kwa Tunda nimekuta vitu tofauti sana, kwangu namuona anafaa kuwa mke wa mtu tofauti na watu wa nje mnavyomuona na nitamuoa kabla huu mwaka haujaisha," amesema mtangazaji huyo.

Amesema watu wamekuwa wakihoji iweje niwe na mwanamke ambaye ameshawahi kuwa na mahusiano na wanaume wengine, nawaambia wanamuona hivyo kwa kuwa ni maarufu lakini ukweli ni kwamba kuna watu wa kawaida wameshawahi kuwa na idadi ya wanaume wengi kuliko hata Tunda.

"Halafu kila unapoanza mahusiano na mtu ukataka kujua historia ya wanaume aliowahi kuwa nao, yatakushinda. Unachopaswa kuangalia kuanzia hapo mlipokutana na namna ya kwenda mbele kwani hata mimi nilishakuwa nao wengi kabla ya kukutana na Tunda," ameeleza Dickson.


"Hatutashirikiana na Wewe" - Jaji Mkuu

$
0
0
"Hatutashirikiana na wewe" - Jaji Mkuu
Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma amefunguka na kuweka wazi kuwa endapo viongozi wa Chama Cha Wanasheria Nchini (TLS) watajiingiza kwenye masuala ya siasa na haraka hivyo wao hawataweza kushirikiana nao kwa kuwa sheria zinataka kutojihusisha na siasa.


Jaji Mkuu amesema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari na kuwataka viongozi wa chama hicho kuendesha shughuli zao kwa manufaa ya Umma kwani ikiwa vinginevyo watakosa ushirikiano na vyombo vingine vilivyopo chini yake.

"Viongozi wanaoendesha chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) waendeshe gari lao kwa manufaa ya Umma wasikubali kuingia kwenye harakati na siasa kwani wakifanya hivyo wale ambao wanatakiwa kushirikiana nao hawatawapa ushirikiano, hivyo ukiingia kwenye siasa wengine sisi tumekatazwa kuingia kwenye mambo ya siasa hivyo hatutashirikiana na wewe" alisisitiza

Hata hivyo Rais wa Tanganyika Law Society (TLS), Bi. Fatma Karume akiwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast cha East Africa Radio aliweka wazi kuwa hana mpango wa kuingia kwenye siasa lakini amedai hawezi kuacha kuikosoa serikali pale anapoona inavunja sheria na kufanya mambo kinyume na kudai kwa hilo hataogopa kusema hata kidogo. 

“I like my freedom, napenda kufanya vile ninavyoona mimi, kama serikali inafanya vitu kinyume na sheria nitasema kwamba hivi sio vizuri, si vizuri kuvunjia watu majumba yao wakati kuna court order, nitasema sitaogopa, ila sitaki kugombea, sitaki siasa, I like to be left alone”, amesema Fatma Karume.

Mechi Kubwa kama Simb, Yanga Uchawi Lazima

$
0
0
Mechi Kubwa kama Simb, Yanga Uchawi Lazima
Leo April 25, 2018 kuna hii ya kuifahamu kuhusu Imani za kishirikina (Uchawi) ambapo ni miongoni mwa vitu vinavyotawala katika mchezo wa soka katika nchi mbalimbali.

Ivo Mapunda ni miongoni mwa wachezaji wakongwe waliostaafu katika soka akichezea nafasi ya goli kipa, ambapo anasema katika mechi kubwa kama ya Simba na Yanga hapakosagi Uchawi.

Simba na Yanga wanatarajia kucheza mechi yao April 29,2018 katila Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam

Okoa Ndoa yako Sasa...Umepungukiwa na Nguvu za Kiume na Unashindwa Kupanda Mlima Vizuri

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA : JE UMEPUNGUKIWA NA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO AU MPENZI WAKO HAKUTIMIZII UTAKACHO:


Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sababu ya kutokuwa na nguvu za kiume au Uume wako mdogo

Dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa Kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA MWENZI WAKO BADO AJAKOJOA

KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA

UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE

KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

Dawa hii utumiwa ata na wazee wenye umri mkubwa na haina madhara yoyote

MAKAKANUA HII NI dawa ya maumbili madogo urefusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5 kwa mini huabiki kwa kuwa na UUME mdogo wai sasa upate tiba sahihi kabisa na ni tofauti na ulizowai kutumia :

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba dawa za uzazi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA p

Piga simu 0743362017 au 0789234653

DR AGU

Diamond tena; Youtube wampa zawadi ya ''Gold Play' Button'' kwa kufikisha subscribers milioni moja

$
0
0
Kuna jitihada kubwa sana Youtube hufanya ili kutambua bidii na ushawishi ambao wamiliki wa account za youtube wanao, Moja wapo za jitihana hizi ni kuwatunuku zawadi ya “gold play button” watu waliofikisha subsribers zaidi ya milioni moja kwenye channel zao, Kupata subscribers milioni moja sio shughuli ya lele mama na inahitaji uwe zaidi ya competent ili upewe hii gold play ya youtube


Kuna wengi waliodhani kijana hatoweza na bado wapo wap*mb*vu wengine wasiomtakia mema lakini kijana anaendelea kutia mchanga vitumbua vya hao watu, Kwakweli kijana anatuwakilisha vyema nchi yetu na wengi huwa hatushangai akipendekezwa kuwa rasilimali ya taifa.

Iwe kuchukiwa na wasiompenda, kuitwa majina mabaya, kubanwa na media ama habari za kumchafua huyu dogo hakati tama hadi wengi kumdhania sio mtu wa hii Tanzania, Pindi inapotokea akidhaniwa hawezi kufanya kitu fulani ama akikatazwa kukifanya kwake ni kama unatia mafuta kwenye petroli maana atapambana hadi atekeleze ambayo huwa tunaona hayawezekani kwa wasanii wengi wa Tanzania.

Achilia mbali umaarufu wake ambao nao umechangia kupata hio zawadi ya subscribers milioni 1, Huyu kijana ni mtu anaeweza kuchanganyika na na jamii kwa kutokua na dharau tulizozizoe pindi mtu akiwa star, Kijana kachangamka sana (haboi) na wala hana shobo za kudharau watu kama baadhi ya wapinzani wake.

Yote kwa yote kijana tunampongeza na aendelee kuchapa mzigo na asije kukata tamaa kwajili ya watu ama vitu visvyo na msingi (mfano kelele za teams)

" Wasanii wa Bongo Fleva msidanganywe na uwingi wa Folowazi Mitandaoni ", Ommy Dimpoz

$
0
0
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Msanii maarufu wa Bongo Fleva Ommy Dimpoz amewataka Wasanii wenzake kuacha tabia ya kuamini na kudhani kuwa wale Watu wote ( Followers ) wanaowafuatilia katika Mitandao yao ya Kijamii huwa ni kweli wapo nao karibu na wanawaunga mkono katika Kazi.

Msanii huyo alieleza Kisa kimoja ambacho anasema hatokuja kukisahau maishani mwake pale ambapo alikuwa akienda kufanya ' show ' yake Mkoani Mtwara hivyo kama kawaida yake akawatangazia ' Folowazi ' wake katika mitandao yake ya Kijamii na kuwataka waende wakamuunge mkono kwa kuingia kwa wingi.

Ommy Dimpoz amesema kwamba mara baada tu ya kutoa tangazo hilo alipata majibu mengi sana katika ' Kurasa ' zake za Mitandao huku wengi wa ' Folowazi ' wake wakimuhakikishia kabisa kwamba watajumuika nae Mkoani Mtwara na Yeye ( Ommy ) akawa tayari ameshapiga Hesabu zake za kimoyomoyo kwamba kwa ' mrejesho ' ule wa majibu ya ' Folowazi ' wake basi umasikini wake ungeishia pale Mkoani Mtwara.

Cha ajabu na kusikitisha Ommy Dimpoz anasema siku ya ' show ' yake hiyo pale Mkoani Mtwara Watu walioingia ukumbini hawakuzidi hata 70 lakini ambao walimuhakikishia kuja walikuwa kama 3000 hivi katika Mitandao yake yote ya Kijamii ambayo yupo kila siku.

Baada ya kuona vile Ommy Dimpoz anasema alirudi katika Kurasa zake za Kijamii na kukagua wale ' Folowazi ' wake wote waliomuhakikishia kwenda katika ' show ' yake ndipo alipochoka kwani wengi wao kumbe walikuwa hawatoki Mtwara na walikuwa mbali mno Kijiografia.

Kilichomkera zaidi Ommy Dimpoz anasema kuna ' Folowa ' wake mmoja anakumbuka alipoweka tu Tangazo lake kwamba atafanya ' show ' Mtwara yule ' Folowa ' pale pale akamjibu hivi namnukuu..." Usijali mwana Ijumaa natia maguu katika Show yako tena mapema sana na nitaingia na tiketi yangu ya VIP kwani nakukubali kuliko maelezo na hapa sasa naandaa Nguo ya kuvaa siku hiyo ili tujumuike pamoja na nisipotokea basi najikata Uume wangu mbele yako ".

Ndipo Ommy Dimpoz baada ya ile siku ya ' show ' yake kupita akaingia tena Mtandaoni na kumfuatilia huyu ' Folowa ' wake ambaye alimuhakikishia kabisa kuwa angehudhuria siku ile aliyoposti alikuwa wapi ndipo akagundua kwamba kumbe Jamaa ( Folowa ) yule aliyekuwa na ' majigambo ' yote yale aliposti akiwa Kijiji kimoja hivi cha Kyaka Nkunde kilichopo Mkoani Kagera na wala kumbe hakuwa pale Mkoani Mtwara wala Mikoa ya karibu ndipo toka siku hiyo akasema hajawahi tena na hatokuja kuwaamini tena kwa 100% ' Folowazi ' wake.

Nadhani hili litakuwa ni fundisho kama siyo funzo kwa wengine.

Nawasilisha.

Madonna Ashindwa Kesi ya Barua ya Kutemwa na Tupac Shakur

$
0
0
Malkia wa muziki wa Pop kutoka nchini Marekani na mshindi wa tuzo za Grammy, Madonna ameshindwa kesi ya haki ya kulinda kutotolewa kwenye jamii kwa mambo yake binafsi na marehemu Tupac Shakur.

Mwaka jana, mwana mama huyo alikwenda mahakamani kuzuia mnada uuzwaji wa barua ya kutemwa na Tupac. Hata hivyo, jitihada zake hizo zimegonga mwamba.

Barua hiyo ambayo iliandikwa na hayati Tupac ambaye alikuwa mpenzi wa Madonna katika kipindi ambacho hakikufahamika, inatarajiwa kuuzwa kwa mnada mwezi Julai mwaka huu.

Tupac aliandika barua hiyo kwenda kwa ex wake huyo Januari 15, 1995 ikiwa ni miezi 18 kabla ya kifo chake. Sasa barua hiyo inatarajiwa kuuzwa kwa kianzio cha dola 100,000 sawa na zaidi ya shilingi milioni 228 za Kitanzania.

Mchumba Wangu Ameanza Kuvaa ''SHANGA" Miguuni...Nahisi Ameanza Kamchezo....

$
0
0
Nimekuwa kwenye mahusiano ya takribani miaka mitatu(3) sasa na msichana ambaye awali alikuwa yupo chuoni ila kwa sasa ni mfanyakazi taasisi fulani hivi (jina kapuni). Amepangiwa nje ya MKOA wa DAR nilipo.

Tulipoanza mahusiano haya hakuwahi kunionyesha anayonionesha hivi sasa.

Amekuwa akipost pictures mbalimbali akiwa amevaa ''vimini'' na ''vishanga (vikuku)'' miguu yote Miwili....

Nimejaribu kumuuliza nini MANTIKI ya hizo picha, kanijibu eti "...mbona kawaida tu,..

NIPO SO FRUSTRATED; ISIJE IKAWA KAANZA KALE KATABIA... MAANA NILISHA MTAMBULISHA KWA BAADHI YA NDUGU.

Steve

Makaburi ya 'Tiles' si Salama – Wanasayansi

$
0
0

Imeelezwa kwamba matumizi ya maru maru (tiles, marble , terrazzo) kujengengea makaburi sio salama kwa ardhi, kwani yana kemikali ambayo inaathiri udongo.


Taarifa hiyo imetolewa na mtaalamu wa sayansi ya mazingira na kilimo, Prof. Julius Zake wa Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, kwenye ripoti yake ya udongo wa Uganda na njia sahihi ya kutumia mbolea, na kueleza kwamba ujenzi wa makaburi kwa tiles unaongeza hatari kubwa ya udongo kushindwa kuzalisha.

“Zamani watu walikuwa wanatumia nguo maalum (backcloth ) kuzikia wapendwa wao, sasa hivi watu wanakufa sana na wanazikwa kila mahali kwa wingi,tiles haziwezi kuharibika zinaingiliana na mizizi inayorutubisha udongo na kusaidia uzalishaji, hivyo udongo unaathirika na kemikali”, amesema mwanasayansi huyo.

Mtaalamu huyo amesema ardhi sasa hivi imekuwa na acid nyingi na kusabaisha kushindwa kuwa na rutuba, ya kuweza kustawisha mazao na kutunza mazingira.

Hivi Ndisho Alivyoandika Irene Uwoya Baada ya Kifo cha Masogange

$
0
0
Hivi Ndisho Alivyoandika Irene Uwoya Baada ya Kifo cha Masogange
Ni ukweli usiopingika muigizaji Irene Uwoya na marehemu Agness ‘Masoganga’ Gerald walikuwa ni mashosti wakubwa – Tena kwenye shida na kwenye raha.

Kifo cha Masogange kimewaumiza wengi lakini Uwoya kimemgusa kwa ukaribu zaidi ukichana na familia ya marehemu. Irene kwa mara ya kwanza ameandika ujumbe tangu Masogange alipofariki dunia April 20 kwenye Hospital ya Mama Ngoma, Mwenge.

Irene Uwoya ameandika ujumbe huo mzito na wakusikitisha kwenye mtandao wake wa Instagram huku akionyesha hisia zake kali pamoja na pengo la moyoni mwake lililokuwepo baada ya kifo cha rafiki yake huyo kipenzi.

Kupitia mtandao huo Irene ameandika:

Siku zitapita na miaka itapita ila ntakukumbuka Milele kama rafiki wa kweli na mwenye mapenz ya dhati moyoni …najua ata ningetangulia mim ungefanya kama nilivyofanya…ntaendelea kukulilia kwa machoz ya ukimya …lakin pia kwatabasamu lahuzuni kwakuweza kutimiza Ndoto yako Japo hukufanikiwa kuiona…wewe ni mwanamke shujaaa!!!pumzika mama…I will always love u!!!

Wanaofanya Kiki Waendelee na Kiki Zao Mimi Siwezi Kufanya Hadi Naingia Kaburini- Alikiba

$
0
0
Wanaofanya Kiki Waendelee na Kiki Zao Mimi Siwezi Kufanya Hadi Naingia Kaburini- Alikiba
Msanii wa bongo fleva Alikiba ambaye hivi karibuni amefunga ndoa na Binti wa Kimombasa ajulikanae kwa jina la Bi. Amina Khalef amefunguka na kusema kuwa katika maisha yake hawezi kuruhusu maisha ya kiki au kufanya jambo ili kutaka kuzungumziwa na watu.


Alikiba amesema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na mtangazaji wa kipindi cha Nirvana Deogratius Kithama na kusema watu ambao wanafanya kiki wacha waendelee na hizo kiki ila yeye hawezi kufanya hivyo kwa kuwa anatambua watu wake wengi na mashabiki walitokea kumkubali na kumpenda kutokana na heshima yake hiyo haoni sababu ya kuanza kuhangaika kuivunja heshima ambayo amejijengea kwa muda mrefu.

"Ni kweli wapo watu wanafanya sana kiki ila mimi siwezi hilo, wanaofanya hivyo wacha waendelee kufanya ila mimi sioni sababu kwa kuwa mimi watu wengi wametokea kunipenda na kupenda kazi zangu kutokana na heshima ambayo nimekuwa nayo, hivyo siwezi kuivunja heshima yangu kwa kiki na nitaendeleza haya maisha yangu mpaka siku nakufa" alisisitiza Alikiba

Alikiba April 29, 2018 anatarajia kufanya sherehe ya harusi yake jijini Dar es Salaam na tetesi zilizopo baada ya sherehe hiyo wawili hao wanatarajia kwenda nchini Italia kwa ajili ya fungate.

Chadema Yatoa Msimamo wao Juu ya Jambo Hili

$
0
0
Chadema Yatoa Msimamo wao Juu ya Jambo Hili
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimelitaka Jeshi la Polisi nchini kutoa taarifa rasmi juu ya matukio ya kuwakamata na kuwapekua viongozi wa kisiasa katika ngazi mbalimbali nyakati za usiku bila ya kuwepo na sababu zozote zenye misingi ya kisheria.

Hayo yameelezwa na taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Tumaini Makene leo Aprili 25, 2018 na kusema  jeshi hilo limeendelea kuwashikilia kinyume cha sheria kwa kuwanyima dhamana na kutowafikisha mahakamani 

Aidha,  Makene amesema baadhi ya maeneo ambayo hadi sasa viongozi wa CHADEMA wamekumbana na manyanyaso na ukiukwaji huo mkubwa wa haki za binadamu na sheria za nchi unaofanywa na polisi ni Dar es Salaam, Geita, Pwani, Njombe, Iringa, Arusha, Morogoro na Tanga.

"Tunapinga na kulaani vikali vitendo hivyo vya ukiukwaji wa haki za binadamu na sheria za nchi yetu na tunasisitiza kuwa havikubaliki katika jamii yeyote inayozingatia kuwa haki ni msingi muhimu wa amani na utulivu wa kweli.Tunatumia nafasi hii kulikumbusha Jeshi la Polisi nchini kuwa lina wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Katiba, Sheria za Nchi na weledi unaokubalika", amesema Makene.

Kwa upande mwingine, Makene amesema chama chake kimetoa maagizo kwa wanasheria wake kupitia Kurugenzi ya Katiba na Sheria, kufuatilia suala hilo kwa ukaribu na kuchukua hatua za haraka za kisheria.

Daimond Akoshwa na Jitihada za Vanesa Mdee "Unapambana Sana Vee"

$
0
0
Daimond Akoshwa na Jitihada za Vanesa Mdee "Unapambana Sana Vee"
Msanii Diamond Platnumz amemfagilia mrembo Vanessa Mdee kutokana na jitihada zake anazofanya kila kukicha za kuupambania muziki wake uzidi kufika mbali zaidi.

Mkali huyo wa WCB kupitia mtandao wake wa Instagram ameandika ujumbe huo wa kumsifia Vee Money huku akimtakia baraka tele kwenye safari yake hiyo.

“Unapambana Sana Vee.. Mwenyez Mungu azidi kukufungulia Kwenye kila la Kheri Uliombalo @vanessamdee 🔥🔥,” ameandika Diamond.

Diamond amewahi kufanya kazi na Vanessa kwa kumshirikisha kwenye ngoma yake inayoitwa ‘Far Away’ ambayo inapatikana kwenye albamu yake ya A Boy From Tandale.

Kiongozi wa Kidini Ahukumiwa Maisha Kisa Mamilioni ya Waumini

$
0
0
Kiongozi wa Kidini Ahukumiwa Maisha Kisa Mamilioni ya Waumini
Mwanaume mmoja ambaye anadaiwa kuwa kiongozi wa kidini nchini India na kudai kuwa na mamilioni ya waumini dunia nzima, amehukumiwa kifungo cha maisha jela.

Mwanaume huyo Asaram Bapu ambaye anatajwa kuwa na umri wa miaka 77 amehukumiwa kifungo cha maisha kwa kosa la kumbaka mtoto wa kike wa umri wa miaka 16.

Bapu anaripotiwa kufanya kitendo hicho mwaka 2013 na anatuhumiwa mara nyingi kufanya vitendo hivyo vya ubakaji.

Mbarawa Apangua Hoja za Wabunge....Asema Ndege Nyingine Kubwa ya 7 Itanunuliwa

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa jana amepangua hoja wa wabunge waliokuwa wakichangia hotuba ya bajeti ya wizara hiyo huku akithibitsha kuwa Serikali inatarajia kununua ndege nyingine kubwa ya saba ya masafa marefu.

Alisema Serikali haikurupuki kununua ndege hizo kwa kuwa inao mpango kazi unaobadilishwa kila mara kulingana na wakati.

“Serikali itaendelea kununua ndege na haitakodi kwa sababu kukodi ni gharama kubwa ikilinganishwa na kununua.

“Nia ya serikali ni nzuri kwani huwezi kuwa na viwanja vya ndege kama huna shirika lako la ndege, hivyo tumenunua ndege sita ambazo tatu zimetua na zinafanya kazi.

"Mwaka huu tunategemea ndege tatu zitawasilisha ambazo ni Boeng 787 ya masafa marefu yenye uwezo wa kuchukua abiria 262, nyingine mbili zenye uwezo wa kuchukua abiria 132 kila moja ni Bombardier CHCS 300 ambazo zitawasilia na kuanza kufanya kazi.

“Kikawaida huwezi kuwa na ndege moja ya masafa marefu ikafanya kazi vizuri hivyo kwenye bajeti hii tumeshapanga kununua ndege nyingine boeng 787 ili tuwe na ndege mbili za masafa marefu ambapo moja ikiwa inatoka Dar es Salaam kwenda Guangzhou na moja inatoka Guangzhou kuja Dar es Salaam. Ndio utaratibu unavyokwenda,” amesema.

Aidha, amesema kwamba Kampuni ya Ndege (ATCL), inao mpango kazi hivyo si kweli kwamba haina kama wabunge walivyodai ambapo kila baada ya muda inabadilishwa kwani si msahafu hivyo itabadilishwa kutokana na mahitaji ya soko.

Mange Pasua Kichwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya April 26

$
0
0


Mange Pasua Kichwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya April 26

CHADEMA yatoa Tamko

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimelitaka Jeshi la Polisi nchini kutoa taarifa rasmi juu ya matukio ya kuwakamata na kuwapekua viongozi wa kisiasa katika ngazi mbalimbali nyakati za usiku bila ya kuwepo na sababu zozote zenye misingi ya kisheria.

Hayo yameelezwa na taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Tumaini Makene leo Aprili 25, 2018 na kusema  jeshi hilo limeendelea kuwashikilia kinyume cha sheria kwa kuwanyima dhamana na kutowafikisha mahakamani

Aidha,  Makene amesema baadhi ya maeneo ambayo hadi sasa viongozi wa CHADEMA wamekumbana na manyanyaso na ukiukwaji huo mkubwa wa haki za binadamu na sheria za nchi unaofanywa na polisi ni Dar es Salaam, Geita, Pwani, Njombe, Iringa, Arusha, Morogoro na Tanga.

"Tunapinga na kulaani vikali vitendo hivyo vya ukiukwaji wa haki za binadamu na sheria za nchi yetu na tunasisitiza kuwa havikubaliki katika jamii yeyote inayozingatia kuwa haki ni msingi muhimu wa amani na utulivu wa kweli.Tunatumia nafasi hii kulikumbusha Jeshi la Polisi nchini kuwa lina wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Katiba, Sheria za Nchi na weledi unaokubalika", amesema Makene.

Kwa upande mwingine, Makene amesema chama chake kimetoa maagizo kwa wanasheria wake kupitia Kurugenzi ya Katiba na Sheria, kufuatilia suala hilo kwa ukaribu na kuchukua hatua za haraka za kisheria.

Puto Alilowekewa Tumboni Kigogo IPTL Hatarini Kupasuka

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa hali ya kigogo wa IPTL, Harbinder Sethi inazidi kudhoofika na puto alilowekwa tumboni linaweza kupasuka wakati wowote.

Hayo yamedaiwa leo mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na Wakili wa Sethi, Hajra Mungula ambapo amedai puto hilo linaweza kupasuka na kuhatarisha maisha yake.

Wakili Mungula aliutaka upande wa mashtaka kueleza upelelezi wa kesi hiyo umefikia katika hatua gani kwa sasa kwani Aprili 11,  ilitolewa amri ya mahakama Sethi apelekwe katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu.

“Nashukuru Aprili 18,2018 mshtakiwa alipelekwa Muhimbili, akafanyiwa kipimo cha CT-Scan ya tumboni na alipaswa kupelekwa hospitalini hapo siku inayofuata kwa ajili ya kupatiwa majibu lakini hadi leo hajapelekwa,” amedai.

Baada ya kusikilizwa hoja hizo, Hakimu Shaidi alisema amefurahishwa Sethi kupelekwa hospitali ili apatiwe matibabu na kuamuru apelekwe tena mapema kwa sababu ya afya yake.

Aliamuru upande wa mashtaka kufanya kadiri wawezavyo kukamilisha upelelezi. Kesi imeahirishwa hadi Mei 10,2018 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika au la.

Sethi na mfanyabiashara James Rugemarila, wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya Dola za Marekani 22, 198,544.60 na Sh bilioni  309.

Kandoro alazwa hospitali ya Benjamin Mkapa.....Waziri Mkuu Amjulia Hali

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemtembelea na kumpa pole Mkuu wa Mkoa Mstaafu, Bw. Abbas Kandoro ambaye amelazwa katika hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma akipatiwa matibabu.

Akiwa hospitalini hapo jana (Jumatano, Aprili 25, 2018), Waziri Mkuu amefarijika baada ya kumkuta Bw. Kandoro na wagonjwa wengine waliolazwa kwenye hospitali hiyo wakihudumiwa vizuri.

Pia Waziri Mkuu amemjulia hali Mbunge wa Viti Malumu (CUF) Bi. Shamsiha Azizi Mtambo ambaye amelazwa katika ya Wodi ya Uangalizi Maalumu (ICU)kwenye hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma akipatiwa matibabu.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwapa pole wagonjwa hao na kuwaeleza kwamba madaktari wataendelea kuwahudumia vizuri ili kuhakikishia afya zao zinaimarika na kurejea katika shughuli zao za kila siku.

Kwa upande wake, Bw. Kandoro alimshukuru Waziri Mkuu kwa kutenga muda wake na kwenda kumjulia hali, pia aliwashukuru madaktari na wauguzi wa hospitali hiyokwa huduma nzuri wanazompatia tangu alipofika hospitalini hapo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mkwasa Awatupia Kijembe cha Utani Simba..Adai Wameyumba Kiuchumi

$
0
0
Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga, Charles Boniface Mkwasa, amewapiga kijembe 'UTANI' watani zake wa jadi Simba kuhusiana na kambi waliyoweka Morogoro.

Akizungumza na Radio EFM kupitia kipindi cha Michezo 'E Sports', Mkwasa amesema kuwa inawezekana Simba wameweka kambi Morogoro kutokana na kuyumba kiuchumi.

Mkwasa vilevile ameeleza kuwa yawezekana Simba wameshindwa kwenda Zanzibar kuweka kambi huko kutokana na gharama kuwa kubwa, hivyo nao wamemua kuwa Morogoro.

Kijembe amewapiga Simba zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya mtangange dhidi yao kupigwa Uwanja wa Taifa, Jumapili ya Aprili 29 2018.

Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images