Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Vitu Vikubwa Ambavyo Huwaumiza Sana Kichwa Masupa Staa wa Bongo Mpaka Wengine Kufikia Kuaibika

$
0
0
Kati ya vitu ambavyo kwa msanii wa hapa bongo anavyojali most,miongoni mwao ni ku-maintain status yao ya u-superstar,na moja kati ya vitu anavyotakiwa kufanya mtu kama star ni kufanya vitu tofauti kabisa na mtu wa kawaida . Kwa bongo muziki umekua ukianza kulipa na pale msanii anapopata pesa hivi ndio vitu ambayo msanii wa kibongo hupata stress from:-
usafiri ,Wasanii wa bongo huumiza vichwa wanunue gari gani ili wawe kama msanii fulani au waongeze status yao. Kwa wale wasanii wadogo  stress zikizidi baadhi Yao hudiriki hata kukodisha magari ya Watu na kulipa kila mwisho wa mwezi,ili tu wasionekane wakipanda daladala,tu naweza kukubaliana kuwa si kila msanii hapa bongo anauwezo wakumiliki gari kutokana tu na mauzo ya Kazi zake,cause hata underground aliyetoka na ku-hit na nyimbo moja redioni utakuta naye anahangaika na Mishe za kutaka ku-maintain status

Mavazi , Usishangae kuona hata Nguo Watu wanagongea katika harakati tu za kuonekana unique,cause am sure si kila celeb hapa town anauwezo waku-change dress code kila siku,and Kati ya vitu ambavyo vinaongeza stress zaidi ni ujio wa instagram,social network ambayo kila celeb huwa anajitahidi ku-update Picha Yake bila ya kuonekana Kama Amerudia Nguo,cause fans lazima waliongelee Hilo, hivyo kutengeneza story mpya ya town ambayo is nzuri kWa mtu maarufu.

Nyumba, Siku za karibuni tumeona wasanii kibao wakionesha nyumba zao walizojenga na hili swala linatokana na stress wanazozipata pale wanapoona wasanii wengine wanajenga nyumba na wengine sio moja tu bali zaidi ya moja. Kwa siku za kaaribuni wasanii wengi wameonesha nyumba zao walizojenga kwa mfano linah , young D , Barnaba na Diamond. Muziki kwa sasa unalipa na hii stress ya nyumba itazidi kuongeneza kadiri siku zinavyoendelea.

Miili Mizuri , Hiki ni kitu kikubwa na kigumu kwa wasanii wengi. Msanii ni kioo na hamna msanii anayependa kuonekana akiwa na umbo baya kwahiyo wengi siku hizi hutumia muda wao kwenda gym kuweka miili yao sawa huku wengine wakiwa na personal trainers kabisa.

Ukweli kuhusu Maisha ya Watanzania Walioko Ughaibuni

$
0
0


Naona kumekua na maneno meengi kuhusu watanzania waishio ughaibuni.
Mimi nimeishi Scandnavia kwa muda mrefu ila baada ya kutimiza malengo yangu nilirudi nyumbani for good.Kwa sasa huwa ninakwenda mara kwa mara kwa sababu ya kibiashara kisha ninarudi nyumbani.

Kusema ule ukweli wa Mungu,kwa watoto wa maskini kama mimi ulaya ni bora kuliko bongo.Hapa nitaiongelea ulaya kama ninavyoifahamu mimi.Mimi mzee wangu hakua tajiri kama mzee wa Le mutuz,Tanzania niliyozaliwa mimi na kukulia ni tofauti sana na Tanzania aliyozaliwa na kukulia kaka yangu Le Mutuz.Mim Mungu alinijalia sana akili za darasani lakini kutokana na umaskini wa wazee nilishindwa kuendelea na chuo.

Ikatokea zali nikaenda scandinavia,nilienda kule nikiwa na malengo mawili,kusoma na kutafuta mtaji wa maana wa kijiajiri.Mungu alinisaidia,nimesoma,nina masters yangu,nina nyumba sita nimepangisha,nyumba moja ninafanyia biashara zangu na moja ninaishi na wadogo zangu na moja iko mkoani wazee wamejisitiri.Nina viwanja na mashamba.Vyote hivi nisingekuwa navyo leo kama nisingeenda ughaibuni.

Pia Mungu alinisaidia nikakusanya pesa ambazo nilitumia kujiajiri.

Mimi niliajiriwa kwenye kampuni ya kutengeneza magari.Huko nilikua na waafrika wengine wengi tu.

Sio kweli kwamba sehemu pekee wabongo waliyo nayo ni kwenye birthday za sebuleni tu LOL.Ulaya kuna viwanja vya maana bana za kula bata bongo itasubiri sana tu.Kitu kinachofanya wabongo wakusanyike kwenye hivyo vipati hadi nadhani ni ile hali ya kufurahia kukutana na wabongo wengine.Pia sio kila mtu anapenda kuwa kwenye hiyo mikusanyiko ya wabongo,mimi ni mmoja wa watu ambao nilikua sipendi kujimix na wabongo wenzangu.

Suala la kwamba wabongo walioko ughaibuni wana maisha magumu sikubaliani nalo.Kwanza kabisa idadi ya watanzania walioko tanzania wenye access ya internet inayowawezesha kusema wabongo wa ughaibuni wanateseka ni ndogo sana ukilinganisha na watanzania walioko bongo wasiojua hata internet ni nini.

Mimi kwa sasa ninaishi Tanzania na ninafurahia maisha ya hapa sababu ughaibuni imenisaidia leo hii sihitaji kwenda kujambiana kwenye madaladala,leo hii nikipata ugonjwa usio na tiba ya kueleweka bongo naenda zangu kutibiwa Scandinavia,mm nina uraia wa scandinavia tayari.

Hakuna binadamu yeyote awe muafrika au mzungu au muarabu hata awe amechoka vipi financialy aliyeko scandinavia anayelala njaa eti kisa hana hela ya chakula.Kwa Tanzania kila jua linapokuchwa kuna mamilioni ya watoto na watu wazima wanalala njaa.

Scndinavia inaongoza kwa uchache wa vifo vya watoto na wazazi,kwa Tanzania hebu tuchukue sekunde tano kuwaombea R.I.P dada na mama zetu watakaokufa wakati wakijifungua usiku wa leo.Tanzania mama zetu wanajifungua huku wakitzabwa makofi na manesi.Dada zetu waliko ughaibuni wanajifungualia katika mazingira kama mtu yuko hotelini,hata wanaojifungulia Aghakhan watasubiri sana compare na wanaojifungulia hospitali za serikalini ughaibuni.

Tokea nimeishi ughaibuni sijawahi shuhudia umeme ukikatika wala maji.Huwa wanayafunga tu kwa masaa au kuukata umeme kwa masaa na hapo mnapewa taarifa kuwa saa fulani mpaka saa fulani maji au umeme utazimwa.Sijawahi kuona watoto wanaotembea peku na kaptura zimechanika kwenye masaburi.Sijawahi ona mtoto akishindwa kusoma kwa sababu mzazi hana pesa,sijawahi ona mtu anakufa kwa kukosa elfu mbili ya kununua dawa,sijawahi ona watoto wenye utapiamlo,sijawahi ona watu wakitembea pekupeku,sijawahi ona ambulance za vibajaji LOL,sijawahi ona wakulima masikini kama hawa wa Tanzania.

Scandinavia maji huchemshi,unafungua bombani unakunywa,ukitaka ya baridi au ya moto kila wakati yapo.

Wkati naishi ughaibuni nilikua sina gari binafsi,japo magari ni bei chee sana kila mtu anaweza kuwa nalo cha muhimu tu uwe na vibali vya kukuwezesha kupata driving licence.Sikuhitaji gari binafsi kwa sababu usafiri wa public ni wa starehe.Baada ya kurudi bongo imenibidi tu niwe na usafiri sababu daladala kusema ukweli ni hiyo shida tu lakini ni mateso.

Wabongo walioko ughaibuni wanabezwa kwa kazi wanazofanywa,fine,hata mimi huko kwenye kampuni ya magari sikuwa nafanya kazi niliyosomea,ila ukweli ni kwamba nilikuwa nalipwa vizuri,wakati naanza nilikua nalipwa kama milioni sita za madafu kwa mwezi.Baadae waliniongeza,sasa kwa mtoto wa maskini kama mimi ukiniambia nilivokua ughaibuni nilikua nateseka nakuona unaongea kichini maana mdingi wangu angekua nazo hizo nisingeshindwa kwenda chuo bongo wakati kichwani kuko vizuri.

Hata wanaosafisha wazee hakuna anayepokea chini ya milioni nne za madafu kwa mwezi.Hapo nimetaja kima cha chini.

Kitu ambacho ambacho kwangu kilikua kinanipa stress enzi naishi ughaibuni ni kwamba sijawahi kufeel at home.Hii hali ndiyo ilinifanya kusave na kufanya kazi kwa bidii hadi nikatimiza malengo yangu nikarudi home.Kwa kifupi social life ya ughaibuni sucks(,huu ni mtizamo wangu).

Inshort kwa upande wangu mimi hata wale watanzania wanaoishi ughaibuni bila vibali mateso yao hayafikii hata theluthi ya mateso ya watanzania masikini walioko Tanzania.

Ughaibuni ni kweli kuna maisha ya ghali,ila ukiishi kwa malengo yako hakuna asiyefanikiwa.Pia ukiamua kuwa mtu wa bata ughaibuni utakula bata za maana kuliko wala bata wa bongo.

Ni kweli wahamiaji wengi(sio wabongo tu) wanafanya kazi za wazee,kusafisha na nyingine kama hizo ila ni ukweli pia kuwa wapo wapo wengi tu wenye kazi zao za maana.
Pia wewe secretary au mfanyakazi kwenye kampuni ya simu bongo na nyingine kama hizo hebu jiulize unapata shilingi ngapi kwa mwezi hadi umcheke mwenzio anayesafisha wazee na kupata milioni zake nne kwa mwezi?

Kitu ambacho wabongo wamewazidi walioko ughaibuni ni good social life tu.

Nimepiga Sana Punyeto Sasa Nina Matatizo, Nifanyeje?

$
0
0
Shida Na Tatizo Linaambatana Na Dalili Hizi...
-High Nerve Pain Hasa Mgongo ,Kifua Na Kiuno
-Kukosa Hamu Ya Sex
-Mwili Na Viungo Vyote Kukosa Nguvu
- Maumivu Ya Ubongo Hii Upelekea Ubongo Kuchoka Na Kusahau Haraka Sana
-Usingizi Mara Kwa Mara
-Macho Kukosa Uwezo Wa Kuona

Wakuu Msaada Kwani Utendaji Wa Kazi Na Shughuri Za Maendeleo Kwa Ujumla Zimesimama

Lunch Time inavyotumiwa na Wafanyakazi Wanandoa Kuchepuka

$
0
0
Usije ukajidanganya kumuona mumeo au mkeo eti anarudi nyumbani mapema na weekend hatoki ukadhani uko salama.

Sasa hivi ile lunch time kuanzia saa saba mpaka nane huko maofisini ibilisi anakuwa ameshika usukani, ikizingatiwa sasa kuna mahotel mazuri pande kariakoo, manzese, magomeni zile zinakuwa zimejaa ikifika muda huo, wake za watu na waume za watu wanakuwa wanacheza mechi za kirafiki watch out.

Hili halina ubishi

Hamu ya Kufanya Mapenzi na Walionizidi Umri Majibaba

$
0
0
Naombeni msaada wenu wakuu kuhusu hii hali inayonisumbua.
Wavulana wa umri Wangu sina hamu nao kabisa na Siwataki kabisa, Napendelea Wale kuanzia Miaka 30 naona ndo wananifikisha, Vijana Wanajisifu sana ila hakuna kitu Kwenye Tukifika Uwanjani ..Ama mie ndo Natatizo ? Naombeni Ushauri.
By Flora

Video:Kundi la ISIS Lamkata Kichwa Mwandishi Mwingine wa Marekani Angalia Video Hapa

$
0
0
Kundi La Wapiganaji wa Kiislamu la Iraq na Syria (ISIS) limetekeleza mauaji mengine ya Kutisha kwa kumkata Kichwa Mwandishi Mwingine wa Habari wa Marekani.
Mwandishi huyo aliyetajwa kwa jina la Steven Sotloff mwenye umri wa miaka 31 alitekwa na wapiganaji hao mwezi August Mwaka Jana , Mwezi uliopita Sotloff alionekana mwishoni katika picha za Video zilizoonyeshwa Kuhusiana na Kuchinjwa kwa Mwandishi mwingine wa Marekani James Foley.

Angalia Video ya Kutisha Hapa:

Mrema Amwomba Rais Kikwete Amfukuze Mbatia Ubunge

$
0
0
MBUNGE wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP), amemwomba Rais Jakaya Kikwete amnyang’anye ubunge Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia.

Mrema alitoa ombi hilo juzi mjini Dodoma, alipokuwa akizungumza katika kikao kilichowakutanisha wanachama wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na Rais Kikwete kwa ajili ya kutafuta mwafaka wa Bunge Maalumu la Katiba.

Chanzo chetu cha habari kilichokuwa katika kikao hicho kilichofanyika Ikulu ndogo eneo la Kilimani, kilisema Mrema alisema kuwa Mbatia ni mtu hatari kisiasa na anatakiwa kuchukuliwa hatua na Rais Kikwete kwa kuwa ameanza kampeni kabla ya wakati.

“Mrema jana (juzi) alikuwa mbogo kwa sababu alipopewa nafasi ya kuzungumza, alimwambia Rais Kikwete amfukuze Mbatia katika ubunge kwa sababu anafanya kampeni katika jimbo lake la Vunjo.

“Mrema alisema Mbatia ni hatari sana, akasema pamoja na kwamba anafanya kampeni kabla ya wakati, anayemlaumu zaidi ni Rais Kikwete kwa sababu ndiye amempa jeuri baada ya kumteua.

“Alipokuwa akisema hayo, Rais alicheka hadi akanyanyua miguu juu, yaani ilikuwa ni burudani kwa sababu alikuwa akizungumza kwa msisitizo akionyesha kukerwa na Mbatia,” kilisema chanzo chetu.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, Rais Kikwete alipokuwa akijibu malalamiko hayo, alimtaka Mrema asiwe na wasiwasi kwa sababu wananchi wa Vunjo wanamjua mbunge wao ni nani kati yake na Mbatia.

British Ebola patient, William Pooley, Has been discharged..Mwee Mbona Waafrika Hatuponi?

$
0
0
William Pooley, the first British National who tested positive to the deadly Ebola virus in Sierra Leone on August 23rd has been discharged from the Royal Free Hospital in London. He was discharged today September 3rd after being successfully treated with the experimental drug, ZMapp
The 29 year old volunteer nurse was transported from Sierra Leone to England on August 24th, a day after he tested positive.

Wanafunzi Shule za Msingi Wakithiri Kwa Ngono ya Kinyume na Maumbile

$
0
0
UTAFITI uliofanywa na mradi wa PREPARE uliokuwa na lengo la kuangalia uwezekano wa vijana kupunguza ngono, umebainisha elimu ya afya ya uzazi bado inahitajika ili kuwakinga na tabia hatarishi.

Akitoa matokeo ya awali ya utafiti huo, mmoja wa watafiti wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili, kitengo cha magonjwa na afya ya akili, Lusajo Kajula, alisema kuwa asilimia 10 ya vijana wenye umri wa miaka 12 hadi 14 ambao ni wanafunzi wa darasa la tano na sita wameshawahi kufanya ngono.

Alisema ngono hiyo kwa asilimia kubwa hufanywa na wanafunzi hao kinyume na maumbile.

Kajula alisema vijana wengi wamebainika kufanya ngono ya kawaida na ya mdomo, ikifuatiwa na ngono ya kinyume na maumbile.
Alisema kwa wale ambao wameshawahi kufanya ngono, asilimia 6.3 wamefanya kinyume na maumbile wakati asilimia 93.7 hawajawahi kufanya.

Alisema utumiaji wa kondomu umebainika kuwa mdogo kwa vijana wadogo ambao wameanza kufanya ngono.

“Asilimia 68 ya wale walioanza kufanya ngono hawajawahi kutumia kondomu kabisa, wakati asilimia 32 wamewahi kutumia,” alisema.

Alisema hiyo ni sehemu ya utafiti wa miaka minne ulioshirikisha Chuo Kikuu cha Makerere cha Uganda, Cape Town na Limpopo vya Afrika Kusini, Bergen na Oslo vya Norway, Maastricht cha Uholanzi na Sussex cha Uingereza.

Babu Tale aeleza Ujumbe Waliotumiwa na Promota wa Ujerumani kuhusu Diamond na Walichoamua Baada ya Vurugu

$
0
0
Kufuatia tukio la vurugu kubwa zilizotokea wakati wa show ya Diamond Platinum huko Stuttgart, Ujerumani, promota wa kampuni ya Britts event ameutumia ujumbe uongozi wa Diamond.

Akiongea na The Jump Off ya 100.5 Times Fm, Babu Tale ameeleza kuwa promota huyo amewatumia barua pepe kuwaomba radhi na wao wamemuelewa na kumsamehe.

“Promota ametupigia simu kuapologize ametuma na email, sisi kama binadamu tumemuelewa na tumemsamehe.” Amesema Babu Tale. 

Akieleza jinsi alivyolichukulia tatizo hilo, amesema kuwa yeye anaona kama sio hasara na analichukulia kama sehemu ya exposure. 

“Matatizo ni sehemu ya maisha ya binadamu. Kwa hiyo ukichukulia matatizo kama hasara utakuja kujuta bure. Unachukua kama xposure, unajifunza. Mwisho wa siku sisi tulikuwa tumelipwa hela yetu yote ya kazi na kila kitu. Athari kubwa aliipata yeye kwa sababu watu walikuja, ukumbi unamdai na nini. Na sisi kama binadamu tumeishia tu kumuonea huruma na kusema aaah ngoja turudi kwetu.” Babu Tale ameiambia The Jump Off. 

Akizungumzia ahadi ya kampuni ya Britts kumrudisha tena Diamond Ujerumani na kufanya show itayoshuhudiwa na mashabiki bure, Babu Tale wanasubiri kutoka kwa promota huyo na kwamba watakapopata uhakika wataeleza.

Gari La Rais Lililoibwa Kenya Lapatikana Uganda

$
0
0
Jumatano ya wiki iliyopita ndio liliibwa hili gari aina ya BMW lisilopenya risasi ambalo huwa linakuwepo kwenye msafara wa Rais Kenyatta, na taarifa ya Ikulu ilisema liliibwa wakati dereva wake ambae ni askari alikua akielekea kwenye makazi ya Polisi Nairobi, njiani akasimamishwa na watu waliokuwa na AK 47 wakamtupa mtaroni baada ya kumvua nguo na kukimbia nalo.

Taarifa mpya ambayo inaripotiwa na Julius Kepkoich toka Kenya inasema gari hili limepatikana kwenye mji wa Tororo Uganda na tayari limepelekwa Kampala baada ya msako uliofanywa na Polisi na kumkamata mshukiwa mmoja hotelini mjini Bungoma.

Kikosi cha Polisi wa Flying squard kikishirikiana na Interpol walivuka boda na kuingia mji wa Tororo Uganda walikohisi kwamba ndiko kulikopelekwa gari hilo.

Polisi wanamshikilia Nelson Topicho aliyekamatwa Bungoma na anatarajiwa kurejeshwa Nairobi ili kuhojiwa zaidi ambapo kikosi kingine cha Nakuru Kenya kinamshikilia Agrey Odhiambo anaetuhumiwa kukarabati gari lililoibwa na kumiliki bunduki huku Nairobi wakitarajiwa kumuhoji upya dereva wa Ikulu David Muchui.

Mainda Afunguka Kuhusu Mume Wake Mtarajiwa Alionyeshwa na Mungu Katika Maono

$
0
0
Na Mayasa Mariwata
STAA wa filamu Bongo ambaye amejikita kumtumikia Bwana kwenye wokovu, Ruth Suka ‘Mainda’ amesema kamwe hawezi kuainisha sifa za mwanaume anayehitaji aolewe naye kama ilivyo kwa mastaa wengine kwa kuwa jukumu hilo ni la Mungu.

Akipiga stori na paparazi wetu, Mainda alisema japo umri wake unaruhusu kuolewa hawezi kuweka wazi sifa za mwanaume anayehitaji awe wake kwa kuwa huenda sifa anazozihitaji Mungu hajampangia kuolewa na mtu wa aina hiyo.

“Kwenye maono naona kabisa mume wangu yupo karibu ambaye Mungu ameniandikia, sasa siwezi kusema nahitaji mwanaume mwenye sifa zipi sababu nikisema nahitaji awe hivi kumbe Mungu hajanipangia huyo,” alisema Mainda.
GPL

Shilole Afunguka 'Mpenzi Wangu Nuhu Ndio Anayenitibu Vizuri Wengine Big Noo'

$
0
0
Na Imelda Mtema
STAA wa Mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefungua kinywa chake na kusema mpenzi wake wa sasa, Nuh Mziwanda ndiye anayemtibu vizuri kunako ‘sita kwa sita’ japokuwa watu wengi wamekuwa wakiudharau mwili wake.

Akizungumza na gazeti hili bila kung’ata maneno, Shilole alisema wengi wanashindwa kujua kwamba mtu anaweza kuwa na mwanaume mwenye umbo kubwa lakini akawa hayajui mapenzi lakini mwenye umbo dogo kama Nuh, akawa ni bingwa wa mapenzi.

Akiendelea kumwaga data mbele ya kinasa sauti cha Amani, msanii huyo anayetamba na wimbo wa Nakomaa na Jiji alisema kuwa katika mapenzi, umri wala ukubwa wa umbo hauna maana yoyote.

“Yaani kwa kweli Nuh ananimudu na tunaenda sawa katika suala zima la mapenzi, kwa hiyo sioni udogo wake kwangu, kwa upande wangu Nuh ni mkubwa sana watu wasiangalie mwili,” alisema Shilole pasipo kutaja umri wa mpenzi wake huyo.

Shilole aliongeza kuwa, kutokana na mahaba ya nguvu anayoyapata kutoka kwa mpenzi wake huyo, anapata nguvu ya kufanya kazi vizuri siku hadi siku hivyo hapati tamaa.
“Sina stress za mapenzi na mara nyingi nafanya kazi zangu zinaenda sawa kabisa,” alimalizia Shilole.
GPL

Sintah Afurahia Diva Kupewa Makavu Live Instagram Kwa Kulinganishwa Uzuri na Yeye

$
0
0

"Nashukuru sana wanajamii kwa kuiona hii thou I dn care mtu akonitukana kitu ambacho sivyo but mmenifurahisha
 Binafsi sio kiraru raru tuu but yeyote ambaye ni msanii yaan mtu anayefahamika na jamii akiandika utumbo tutaandika na akiandika mema pia tutaandika
Hiki ni chombo cha habari kama vingine eg magazeti,umeshawah kuona binafsi ktk insta,twitter,fb namuandika mtu??ama natoa habari ya mtu?? Anyway tynashukuru kwa kuwa we get paid for whatever we write here,na tunashukuru kiraru raru kwa kutuongezea viewers Mungu akujaalieeeee
 Lastly but not least pole kwa kufungiwa acc twitter keep on writting bulshit watafunga na IG,kwakuwa watu wamechoka na tabia zako ndo maana wameku report so kaa tafakari
Thanks msamaria mwema kwa kumpa makavu live" Says Sintah

Mke wa Rafiki yangu Katolewa Mimba na Rafiki Yangu

$
0
0

Yaani kwa kweli mambo ya hii dunia ni ya ajabu na siku zote umdhaniae ndie kumbe sie kwa kweli, kuna rafiki yangu ambaye kwa kweli si kama tuna urafiki sana lakini ni rafiki maana tunaheshimiana nae sana na familia zetu zinafahamiana kwa kuwa tumejuana kibiashara na si mambo mengine.

Mme ndiye ambae ninafanya nae kazi ingawa mkewe namfahamu kwa kuwa ni sehemu pia ya msimamizi wa biashara za huyo mwanaume. Jana nilikua na appointment na rafiki yangu ambae ni daktari na ana hospitali yake.

Sasa wakati hiyo jana naingia nikakutana na huyo mdada ambae ni shemeji yangu, tuka salimiana nikamuuliza vipi hospital akasema ameenda kumcheki rafiki yake basi nikampotezea. 

Sasa kumbe yule rafiki yangu dokta alituona nikiongea nae, nlipofika kuzungumza na dokta maana namjua tabia zake si za kistaarabu maana ni mdhaifu sana kwa wanawake, katika story akaniambia amemtoa mimba ya wiki3.

Jamani mimi nimempokea Yesu na nilimueleza dokta swala alilofanya ingawa ni rafiki yangu, lakini kitu kingine ni kwamba mume wa huyu dada yuko nje ya nchi tangu july 21 na atarudi mwishoni mwa mwezi huu kama mambo yataenda sawa ila hii inamaanisha mkewe si mwaminifu kwa ujauzito wa wiki3. 

je, nina haja ya kumwambia awe makini na mke wake kwakua si mwaminifu?
By bomouwa

Sikiliza Wema Sepetu Akizungumzia Yote Yanayosemwa ikiwemo Issue ya Kuajiriwa na Kajala.

$
0
0
Kupitia mitandao na magazeti siku chache zilizopita ilitoka stori ambayo ilidai Kajala anaelekea kumuajiri Wema Sepetu,leo Wema kapatikana na kakubali kuongelea isue hizo zote ikiwemo hiyo ya Kajala.
Kupitia You heard ya  XXL ya Clouds Fm Soudy Brown alianza kwa kutaka kufahamu kama kweli Kajala anaweza kumuajiri yeyeWema,Wema Sepetu akamjibu’Inawezekana,kila kitu kinawezekana Soudy’
Kuhusu mshahara ambao anataka kulipwa na Kajala,Wema Sepetu amejibu ’Kwa Kajala mi sihitaji mshahara hata bure nitafanya kazi kwa Kajala,shughuli yoyote nitafanya Soudy’
Soudy Brown alipomuuliza kuhusu fununu za Meninah kutoka na Diamond,Wema amejibu ’Mimi sijui Soudy bwana na wala sijali’.

Sikiliza Yote Hapa:

Diamond Platnumz Azungumza Kwa Mara ya Kwanza Mambo Sita Kuhusu Fujo Zilizotokea Ujerumani

$
0
0
Kuanzia siku tatu zilizopita stori kubwa kwenye kiwanda cha burudani Tanzania imehusu fujo zilizotokea Ujerumani kwenye show aliyokwenda kufanya Diamond Platnumz huko Stuttgart.
Kilichotokea ni kwamba saa kumi alfajiri ndio promota alimpeleka Diamond kwenye ukumbi kunakofanyika show. Kwa nini ilitokea akamchelewesha? nini kilitokea baadae? hizi hapa chini ni kauli za Diamond mwenyewe kwenye exclusive na millardayo.com

1. ‘Mpaka sasa hivi nashindwa kuelewa tatizo lilikua nini, siamini kama tatizo lilikua ni hela, balance iliyokua imebaki ni balance ndogo kama EURO 3500 hivi ambazo ni zaidi ya milioni 7 za Tanzania, ninavyojua Mapromoter wengi wa nje wakifanya show huwa wanauza na vinywaji wenyewe na wanapata hela nyingi sana kwenye vinywaji kuliko hata viingilio so nahisi labda walivuta muda ili waendelee kuuza vinywaji zaidi’

2. ‘Walichelewa kunipeleka kwenye show, walinifata kwenye mida ya saa tisa usiku na wakawa hawana hela yangu iliyobaki, nikawaambia siendi kokote mpaka wamalize kunilipa, walikua na EURO 1500 wakati nilikua nawadai 3500 nikawaambia lazima wanipe hela yote, wakaifata ndio tukaenda kwenye show’

3. ‘Tukafika kwenye show saa10 kasoro, kweli hata ningekua mimi shabiki ningekasirika ningefanya vurugu, wengine walilipa zaidi ya laki moja na wametoka kwenye miji na nchi jirani, niliwaambia wanipeleke nikafanye show ndani ya ukumbi japo tulikuta watu wengi sana nje lakini Mapromota walikua waogawaoga kunipeleka ndani’

4. ‘Nikakuta watu wengi na vurugu nje, nikamwambia promota atupeleke ndani tungefika kwenye stage ingetulia baada ya sisi kuimba manake ni vitu tunakutana navyo kwenye muziki lakini promota walikua waogawaoga, askari wa Ujerumani karibu gari 7 wakaja pale lakini mtiti ukawa mkubwa’

5. ‘So dakika ya mwisho tukaona hapashukiki ndio wakaturudisha hotelini, kiukweli nimesikitishwa sana manake nilikua nimejipanga vizuri na ilikua ni mara yangu ya kwenda kuperform pale Stuttgart, imenisikitisha manake watu walikua kuniona alafu mwisho ikashindikana kuwafikishia walichokitarajia’

6. ‘Nafikiri October tutakua na show nyingine na itafanyika kulekule, nilikua nazungumza na uongozi wangu kwamba wanataka show nyingine na tayari wameshatuma hiyo hela ya show nyingine’
Unaweza kumsikiliza Diamond mwenyewe kwa kubonyeza play hapa chini.

Boko Haram Wazuia Watu Kuzika Maiti za Ndugu Zao, Miili ya Mait Yatapakaa Njiani

$
0
0
Taarifa za kutisha zimeibuka kutoka mjini Bama moja ya miji ambayo ilitekwa na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram Kaskazini Mashariki ya Nigeria
Seneta mmoja wa eneo hilo,Ahmed Zanna, aliambia BBC kwamba wakazi hawaruhusiwi kuwazika jamaa wao waliouawa na wapiganaji hao.

Inaarifiwa miili imetapakaa katika barabara za mji huo ambao Boko Haram imeuteka.
Kundi hilo linasemekana kuuteka mji huo huku wapiganaji wa kundi hilo wakishika doria katika barabara zake.
Maelfu ya watu wametoroka huku idadi kubwa ya wengine wakiuawa.
Seneta huyo ameitaka serikali ya Nigeria kupeleka wanajeshi mjini Maiduguri ambao ni mji mkuu wa jimbo hilo ili kuulinda dhidi ya wapiganaji hao.
Mnamo siku ya Jumatano serikali ya jimbo hilo ilikanusha madai kuwa jimbo hilo limetekwa na wapiganaji hao.
Maafisa wakuu wanakisia kuwa watu 26,000 wameachwa bila makao kutfuatia mapigano katika mji wa Bama.
Bwana Zanna anasema kuwa barabara za mji huo zimejaa miili ya watu na Boko Harama imewakata wakazi kuwazika jamaa wao. ''Kwa hivyo hali ni mbaya na inaendelea kuzorota,'' asema bwana zANNA
Boko Haram wameteka miji kadhaa Kaskazini Mashariki ya Nigeria, katika miezi ya hivi karibuni na kusababisha hofu kuwa huenda wakaufikia mji mkuu Maiduguri.
Bwana Zanna amesema kuwa itakuwa janga kubwa ikiwa Boko Haram wataushambulia mji wa Maidiguri ambao una watu zaidi ya milioni mbili.

Heka Heka Waongea na Jamaa Aliyefumaniwa na Mke wa Mtu na Kisha Kulawitiwa, Sikiliza Hapa

$
0
0
Miongoni mwa stori ambazo licha ya kuonekana sehemu mbalimbali za mitandao ya kijamii lakini zilivuta hisia za watu wengi baada ya kusemekana kuwa kuna mume wa mtu alifumaniwa na mke wa mtu.
Idara ya Hekaheka imefanikiwa kumpata mhusika ambaye walimuingilia kisha kumpiga picha za kumdharirisha,kaongea jumla ya tukio zima lilivyokuwa,ungana na Leo Tena ya Clouds Fm kusikiliza zaidi Hapa:

Nyerere Alikumbuka Shuka Wakati Kumekucha Juu ya Umuhimu wa Mfumo wa Vyama Vingi Nchini

$
0
0
Kuua mfumo wa vyama vingi miaka ya 60 na baadae kuiacha ya CCM itawale bila uwepo wa vyama vya upinzani lilikuwa ni kosa kubwa sana la utawala wa awamu ya kwanza na matokeo yake watanzania wengi walizoea mfumo wa vyama vingi na ndio sababu kubwa ya watanzania wengi kuukataa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.

Pamoja na Nyrere kushauri mfumo wa vyama vingi uanzishwe licha ya zaidi ya asilimia 80 ya watanzania kukataa mfumo huo,ilikuwa ni hatua iliyochelewa mno kwani teyari mfumo wa chama kimoja ulishaota mizizi na ulishatutia hasara kubwa mno watanzania kwani chama tawala kilikuwa hakina mpinzani na hivyo walifanya waliyotaka bila ya hofu yoyote tofauti na sasa ambapo "pressure" ya upinzani inasaidia kui-shape serikali iliyoko madarakani.

Hivi umewahi kujiuliza maendeleo ya nchi yetu yangekuwaje leo kama tungeendelea kuwa na mfumo wa vyama vingi tangu uhuru.Ule utaratibu wa kupiga kura kuchagua kati ya picha ya mtu na kivuli hukupaswa kuwepo kwa muda wote ule.

Maswali ambayo huwa najiuliza ni kuwa Mwalimu Nyere allitaka atawale pasipo upinzani(misukosuko) au aliona upinzani hauna umuhimu kwa wakati ule au alikuja kujua umuhimu wa upinzani baada ya yeye kutoka madarakani na kuona mambo yanaenda hovyo?Je,ni kweli mfumo huu ulipata msukumo kwasababu ya shinikizo la kimataifa?Na kama ndio,je shinikizo hilo halikuwepo kabla ya hiyo miaka ya 90 na kama lilikuwepo mbona lilipuuzwa na iweje lipate nguvu mwaka 1992?

Nimalize kwa kusema umasikini wa mtanzania na maendeleo duni ya nchi hii kwa kiasi kikubwa ni matokeo ya kuwa na mfumo wa chama kimoja kwa miaka mingi siku za nyum
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images