Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu

 Bonyeza Hapa Chini Kuinstall Upya:


==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>  

Alikiba mwambie Diamond apatane kwanza na Baba yake ndio arudi kwako, Diamond ni mswahili na Mnafiki usimuamini

$
0
0
Mdau Kaamua Kufunguka:


Alikiba mimi kama shabiki yako naomba usimamie msimamo wako uleule usikubali kuyumbishwa na mtu mnafki kama Diamond, ambaye amekuwa akikupiga vijembe mara kwa mara huku akiigiza kuwa anataka kupatana na wewe na muwe kitu kimoja

Mwambie akapatane kwanza na baba yake mzazi ambaye anamchukia ndio arudi kwako, haiwezekani mtu ashindwe kumsamehe au kupatana na mzazi wake aliyemtoa kiunoni alafu aje kwako mtu baki tu ajifanye kuwa anataka mpatane

Hata kumpa mkono skuile ya msiba ulijishusha sana ,kwani ilibidi Diamond aanze kwanza kumpa mkono baba yake mzazi ndio aje kwako yule mtu ni mnafiki nakushauri kuwa nae makini

By Mtotomtamuu

"Hii ilikuwa Mara ya Kwanza Kumuibia" - Kijana Aliyenasiwa na Mzigo wa Wizi Afunguka

$
0
0
Kijana Frank Joseph mwenye umri wa miaka 23 ambaye anaishi Dar es Salaam, Mbezi Mwisho amefunguka na kusema kuwa ni kweli aliiba mzigo huo japo kwake ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kumuibia mama huyo.


Kijana Frank amesema kuwa baada ya kuiba mzigo Mlandizi mkoani Pwani baadae ulikataa kutoka kichwani mpaka pale alipopigiwa simu muhusika ndipo alikuja kutokea Dar es Salaam ambako anafanya kazi na kufika kituo cha polisi Mlandizi kisha alimshika zipu ndipo alipoweza kushusha mzigo huo wa mahindi kichwani.

"Ni kweli nimeiba na sasa nashikiriwa na serikali kwa wizi na mzigo ulikuwa hautaki kushuka mpaka mama huyo alipofika na kunishika zipu kwa msaada wake ndiyo mzigo huo uliweza kushuka, kwa mimi ni mara ya kwanza kumuibia huyo mama labda sijui kwa watu wengine, mimi nilikuwa napita tu nilipouona mzigo huu nikachukua na kuondoka nao" 

Aidha kijana huyo Frank Joseph kufuatia tukio ambalo limekuta leo amewaomba vijana wengine ambao wanajihusisha na wizi kuacha kufanya hivyo akisema ni si jambo zuri pia Kamanda Shana amewataka vijana wafanye kazi badala ya kutaka kufanya vitendo vya uharifu ambavyo vitawagharimu maisha yao.

Mtoto Akutwa na Sindano 7 Tumboni

$
0
0
Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu mkazi wa kijiji cha Keringet kaunti ya Pokot amekutwa na sindano 7 za kushonea kwa mkono tumboni mwake, baada ya kupigwa picha ya xray.


Mtoto huyo alipelekwa hospitali ya Kapenguria siku ya Jumanne kupata matibabu ya maumivu ya tumbo ambayo alikuwa akiyapata kwa muda mrefu bila kujua tatizo ni nini.

Bibi yake Bi. Emily Linga'a ambaye ndiye anayeishi naye, amesema mtoto huyo alikuwa akilalamika maumivu ya tumbo kwa zaidi ya miaka miwili, lakini hawakuweza kubaini mara moja chanzo cha maumivu hayo na kuendelea kumpatia dawa za kutuliza maumivu, lakini baada ya kuona anazidi kualalamika walimpeleka hospitali na kugundua ana tatizo hilo.

“Kwanza nilidhani mtoto alikuwa na minyoo, sikuwahi kufikiria kwamba ana sindano tumboni mwake, nilikuwa nahisi ni malaria siku zote na kumpa dawa za maumivu”, amesema bibi huyo ambaye anaishi naye, baada ya mama yake kumuacha alipoolewa na mwanaume mwengine.

Madaktari wa hospitali hiyo wamempa rufaa ya kwenda hospitali kubwa ya Moi ili kuwea kufanyiwa upasuaji wa tumbo, na kutolewa sindano hizo ambazo hazijajulikana zimeingiaje.

Mlinga ampa kazi IGP kuhusu kina Mange

$
0
0
Mbunge wa Ulanga (CCM), Goodluck Mlinga amemtaka Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro kutumia nguvu alizonazo kwa watu wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kuwatukana viongozi huku akimtaja Mange Kimambi na wengineo kama vinara.


Akichangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya ndani kwa 2018/19, Mlinga amemtaka IGP kutumia nguvu alizowekewa mabegani kuwawajibisha watu wanaotukana kwani wamevuka mipaka hadi kufikia hatua ya Rais kutukanwa.

“Matusi mitandaoni ni 'too much', kwenye mitandao hajulikani Rais ni nani, kiongozi ni nani, kuna akaunti nyingi zinatukana, wanatukanwa wananchi, mawaziri mpaka Rais. IGP uko hapa tumekuwekea hizo nyota mabegani ni nguvu, tumia nguvu zako wasikuchezee. Mfano natoa akaunti zinazomtukana rais ni kama Kwinyara, Malisa GJ, Yericko Nyerere na Dada yao Mange Kimambi wamekuwa wakimtukana rais". Mlinga

Aidha Mbunge huyo ameongeza "Jamani hakuna nchi ambayo rais anachezewa. Mfano nimtolee mfano Kagame, umeshawahi kusikia mtu anamtukana Kagame? Polisi tumieni nguvu zenu".

Jini Mahaba Linavyonitesa Linaniingilia Mpaka Kinyume na Maumbile..Msaada

$
0
0
Hi ni history ya kweli ya maisha yangu naomba mnishauri wadau.
Mimi ni mwanaume mwenye umri wa miaka 29 ni mkristu na ni mzaliwa wa morogoro mwenye asili ya mkoa wa kilimanjaro.Wakati wa utoto wangu nilikuwa ni mtu mwenye akili sana.Kuanzia la standard 1 mpaka form 4 nilikuwa naongoza nikishuka sana nakuwa mtu wa pili au wa tatu.Kifupi nilizaliwa nikiwa na akili sana pia nilikuwa na nyota ya kupendwa na watu na nililelewa kwenye mazingira mazuri nikiheshimu kila mtu.

Tatizo hili lilinianza nilipokuwa shule ya msingi yaani nilipofika std 7. Nilikuwa napita karibu na mto na kuna mti mkubwa.Nilihisi nywele kusisimka na nikawa kila nikipita hapo naokota pesa. Tabia hiyo iliendelea kila siku mpaka jamaa na wazazi wakawa wananiambia nawaibia na kusingizia naokota.Mpaka namaliza std7 nilikuwa sijawahi kutana na mwanamke.Nilipofika form 2 nikibalehe bt hapo ndipo nilipoanza hisi utofauti.Nilianza kupata wet dream ila nilijua ni kawaida kama mwalimu wa biology alivyotufundisha bt cha kushangaza ndoto hizo zilikuwa ni endelevu.Mwaka huo huo nilipata dada mmoja akawa mpz wangu ila nilipokuwa namdu sikuwa nahisi raha kama ambavyo naota.Pia nikaanza tabia ya uongo, uchonganishi, unafki, hasira pia nikawa nachukiwa na wanafunzi na hata walimu bila sababu.

Nilipomaliza form 4 nilifaulu kwenda A level pindi hko nilikuwa na mwanamke m1 ambae alikuwa na mimba yangu bt cha kushangaza ile mimba ilitoka kwa mazingira ya ajabu.

Nilipofika A level nikawa na tabia ya kujichua na kupenda wanawake kupitiliza.Nilikuwa natoroka shule na kutafuta wanawake kuanzia mabaamedi, mama guest mpaka wanaojiuza nikikosa napiga punyeto huku na zile tabia zingine zikiendelea.

Nilienda chuo kikuu k1 moro na kuendeleza hizo tabia mpaka nilipomaliza chuo na kuanza kazi arusha.Wakati nilipokuwa chuo nilimtia dada m1 mimba ila pia mtoto alifia tumboni bila sababu.
Nikiwa kazini arusha mabosi na wafanyakazi wenzangu wakawa wananichukia bila sababu mwisho nikafukuzwa.

Siku moja nikiwa arusha wakati nimefukuzwa kazi nikaenda kanisa la safina.Nilijishangaa nilipopandisha mashetani baada ya maombezi na kuanza ku confess na hayo mashetani yakasema yote tangu kuniingia mpaka walivyosababisha kuua watoto wangu pia kunisababishia UKIMWI, kuchukiwa, kutopata maendeleo mi na familia yangu yote.

Nilimshukuru mungu na kuanza maisha mapya ya maombi ila sasa kuna lingine limeibuka.Nikipitiwa na kulala bila kusali huwa naingiliwa sana kinyume na maumbile nikiamka najikuta nimechafuka. Nguo zangu za ndani zinachafuka sana.Nateswa na haya majini natamani kujiua husasani kwa vitendo ninavyofanyiwa pia mi ni muathirika bila kupenda. Nimechoka na maisha haya sijui nitafanyaje?
Mnanishaurije wadau?
Natamani nikipata pesa niende nigeria kwa tb joshua kwa ajili ya maombezi.

Naombeni ushauri wenu

Nilimfumania Mwanamke Wangu na Jamaa Mwingine Kitandani, Nikamsamehe..Baada ya Mwezi Ananiambia Ana Mimba yangu

$
0
0
Nilimfumania mwanamke wangu na jamaa mwingine chumbani kwetu kitandani kwetu. Nilimwacha kwa muda lakini alirudi na kuniomba msamaha tukarudiana. Ila sasa ananiambia ni mjamzito alivyoniambia tu ni mjamzito hasira zimenirudi. Sijui ni ujauzito wangu au sio. Na pia sina uhakika kama ameshaachana na yule jamaa niliyemfumania nae ama la.

Naombeni ushauri

Sina Hamu na Mwanamke Yoyote Hata Awe Mzuri Kiasi Gani

$
0
0
Najisikia sihitaji mwanamke yeyote yule hata akiwa mzuri kiaisi gani. Sina hamu naye na wala siwezi kumfanya chochote. Naogopa kusema i hate you women kwani ni kama neno lisilo sahihi.

Nina mke wa muda mrefu sasa na mtoto mmoja, tulioana kwa upendo sana hasa mimi nikiwa na furaha sana kwenye ndoa yangu, lakini cha ajabu mambo yalibadilika sana mara nyingi mke akawa ni wa kulalamika tu, mara nyingi anashinda amenuna, maongezi hakuna kabisa ndani,. Nilijitahidi sana kumuweka chini na kuzungumza naye nikijishusha na wakati mwingine kuomba anisamehe na aniambie makosa yangu yanayomfanya asiwe na furaha.

Mara nyingi nilidhani ni mambo ya "kitandani" labda sifanyi vizuri lakini cha ajabu amekataa sana juu ya hili na kusema anaridhika sana na tena kwa kiwango cha juu na mara nyingi tumekuwa tukifanya hilo tendo hubadilika na kuwa mpole sana na hata kusema ananipenda sana.

Nimemwambia kwa lolote analoona liko tofauti aniambie mara nyingi najishusha sana kwake na nina msikiliza san, lakini nimegundua hana nia ya dhati maana kila kukicha anakuwa vilevile tena wakati mwingine hufanya makusudi kabisa.

Sikutarajia maishani mwangu kuwa na ndoa ya hivi inaniuma sana, nilimuoa kwa taratibu zote za kikanisa na ndoa kubwa na yenye maana, najiuliza kumwacha inakuwa siyo solution maana moyo huwa unaniuma sana kiasi kwamba natoa machozi na kumbembeleza, ninavyoelewa nimefuata moyo wa mama yangu ni mpole saaana tena sana nadhani hata mimi nimerithi huko.

Umefika wakati sasa nimechoka machozi yananitoka kila wakati, ofisini kazi zimenishinda sasa, na siwezi chochote, najihisi sisitahili kuishi duniani lakini natakiwa kuwasaidia wanaonitegemea, nahisi wanawake wote wanaroho mbaya za kinyama kiasi kunitesa hivi, lakini mbona mama yangu ni mtaratibu kiasi hicho? Kuna kitu kimoja kimenijia nimelia sana, nilikuwa namchumba mpole sana ila alinikataa ghafla bila kosa na kwenda masomoni, kumbe hakunikataa ila alifanya hivyo ili tusisumbuane wakati anasoma amemaliza nikiwa nimeoa, aliposikia amelia sana, na mimi nimelia sana. Dunia haijanitendea haki.

Nimetulia chumbani nalia sana saivi sipati solution zaidi moyo wangu unawachukia wanawake zaidi. Wanawake hamna jema kabisa yaani hata mkipendwa na kulelewa kama watoto mnakuwa hivi?

By Frank

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 4

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 4

Waziri Mkuu: Wapangaji wa Muda Mrefu NHC Wapewe Fursa ya Kununua Nyumba

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim  Majaliwa ameiagiza Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kukaa pamoja na chama cha wapangaji wa nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ili kusikiliza changamoto zao pamoja na kutoa fursa kwa wapangaji wa muda mrefu kununua nyumba hizo.

Mhe. Majaliwa ametoa tamko hilo leo Bungeni, Jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ilala Mhe. Azzan Mussa Zungu juu ya lini Serikali itakutana na wanachama na wamiliki wa nyumba za NHC ili kutoa fursa kwa wapangaji wa muda mrefu kuzinunua nyumba hizo badala ya kuwaondoa.

“Shirika la nyumba inayo sera inayotoa muongozo namna nyumba hizo zinavyotakiwa kutumika ikiwemo na maamuzi kwa wale wanaokaa kwa muda mrefu kwenye nyumba hizo inapofikia thamani ya nyumba kushuka iweze kurasimishwa rasmi ili kutoa fursa kwa wapangaji hao kuweza kuzinunua kwa kulipa kiwango kidogo kidogo,” alisema Waziri Mkuu.

Aliendele kusema, asilimia kubwa ya wapangaji wa muda mrefu wa nyumba hizo ni wastaafu ambao hawana nyumba. Hivyo ameitaka NHC kuangalia jambo hilo na kuwapa fursa wapangaji hao kulipa kidogo kidogo kadiri ya uwezo wao.

Wakati huo huo Waziri Mkuu ameitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutotumia lugha ya kuudhi au kutumia nguvu pindi wanapokusanya kodi kwa wafanyabiashara. Badala yake wawaelimisha wafanyabiashara juu ya umuhimu wa kulipa kodi na kuwaeleza ni kwa kiasi gani kodi hiyo imefikia.

Amesema hayo, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Tunduma Mhe. Frank Mwakajoka kuhusu kauli ya Serikali juu ya usumbufu unaoletwa na TRA kwa wafanyabiashara wakati wa kukusanya kodi.

“Serikali imeunda chombo cha kusikiliza kero za wananchi ndani ya TRA lakini kama hawatasikilizwa wanauwezo wa kupeleka kero zao Wizara ya Fedha au kwa kiongozi yoyote mkubwa katika eneo lake kama vile Mkuu wa Mkoa au Wilaya,” alisema Waziri Mkuu.

Aidha ameitaka Mamlaka hiyo kufanya kazi kwa weledi na kuwa na mazungumzo na wafanyabiara. Pia tathmini ya kodi isiwe kiwango kikubwa kuliko mtaji wa mfanyabiashara.

Hata hivyo amesema hatua zitachukuliwa kwa yeyote ambaye hatatumia utaratibu mzuri wa kukusanya  kodi na amewataka wafanyabiashara kufanya biashara kwa amani.

CCM Mara Watoa Tamko Kuuawa Mdogo wake Heche

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Mara kimelaani madai ya askari polisi kumuua kwa kumchoma kisu Suguta Chacha ambaye ni ndugu wa mbunge wa Tarime vijijini (Chadema), John Heche.

Akizungumza leo Alhamisi Mei 3. 2018 mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Samuel Kiboye amesema haiwezekani raia anayekamatwa kwa tuhuma yoyote kufariki kwa kipigo au sababu yoyote isiyohusika na ugonjwa wa kawaida akiwa mikononi mwa polisi.

"Nikiwa kiongozi na rafiki wa familia nalaani kitendo kilichofanywa na askari aliyefanya tukio hili," amesema Kiboye alipotoa salaamu wakati wa ibada ya mazishi ya kijana huyo inayoendelea muda huu.

Amesema kwa nafasi yake ya uenyekiti wa mkoa, ataendelea kuwahimiza watendaji wa Serikali, vyombo na taasisi zake  kutekeleza wajibu na majukumu yao kwa weledi wakizingatia sheria, kanuni na taratibu.

Umaskini Utazidi Kukunyemelea Sana Kama Una Tabia Hizi za Pesa

$
0
0
Kushindwa katika maisha hakuji kwa bahati mbaya bali kuna kuja kutokana na tabia zetu ambazo tunazo kila siku kwenye maisha yetu. Tabia hizo kiuhalisia zinaturudisha nyuma sana kimafanikio kama tunazikumbatia.

Kupitia makala haya ya leo nataka nikukumbushe baadhi ya tabia chache tu, na kama tabia hizo utazikumbatia uwe na uhakika unazidi kuukaribisha umaskini ukunyemelee kwenye maisha yako na kukupoteza kabisa.

Inatakiwa kuwa makini sana na tabia hizi ambazo zinaweza zikaingilia uhuru wako wa kifedha na kuweza pengine kukuharibia karibu kila kitu kwenye maisha na kukuacha ukiwa mtupu hauna kitu.

Tabia hizi ni zipi, twende pamoja tuweze kujifunza;-

Tabia 1: Matumizi yako ni makubwa sana.
Kama una matumizi makubwa kwa namna yoyote ile huwezi kukwepa kuishiwa. Inatakiwa matumizi yako uweze kuyabana kiasi cha kwamba yapate nafasi ya kukupa pesa ya ziada. Ni vizuri kuwa na daftari la kumbukumbu litakalokusaidia kutunza kumbukumbu zako za matumizi ili kimatumizi usikengeuke kwa kutumia sana pesa zako hovyo.

Tabia 2: Pesa nyingi unatumia kwenye usafiri.
Iwe matumizi ya nauli za kawaida au matumizi ya gari lako binafsi ila kama pesa zako nyingi unazitumia hovyo kwenye usafiri tu, basi jiandae kuanguka pia kiuchumi. Haiwezekani ikawa karibu muda wako wote ni wewe wa kusafiri tu, halafu ukategemea mambo yako yakaenda sawa. Kuwa makini na matumizi ya pesa unazotumia kwenye usafiri, vinginevyo umaskini unakufuata.

Tabia 3: Unazungukwa na marafiki wabovu.
Marafiki zako wanaokuzunguka ikiwa tabia zao ni mbaya juu ya matumizi ya pesa, basi hata wewe utakuwa ni miongoni mwao. Haitawezekana kwako wewe uweze kukwepa kiunzi hicho hata siku moja ni lazima utakuwa kama rafiki zako tu na sio vinginevyo. Kukwepa hilo unatakiwa kuchagua marafiki makini zaidi kwenye matumizi ya pesa.

Tabia 4: Huweki akiba.
Pengine nikuulize unafikiri, ni kitu gani ambacho kitatokea ikiwa wewe kila aina ya pesa kwako unayoipata unaamua kuitumia. Jibu ni rahisi sana hapo ni utaendelea kushiwa na mwisho wa siku unaukaribisha mwenyewe umaskini. Usijaribu kujiingiza kwenye mtego huu, pesa yoyote unayoipata iwekee akiba hata kama ni kidogo sana, wewe weka akiba.

Tabia  5: Unatawaliwa na matumizi ya starehe.
Hapa utakuta badala ya mtu kuwaza maendeleo, lakini kila pesa unayoipata wewe unawaza ni kwa namna gani utakavyoweza kuifanyia matumizi tena matumizi ya starehe. Hakuna mafanikio yanayokuja kwa nama hiyo kwa kutafuta vitu vya starehe peke yake. Kama uko ‘siriazi’ na kutafuta pesa itafute, la sivyo tabia hii itakuachia janga kubwa sana la umaskini.

Okoa Ndoa yako Sasa...Umepungukiwa na Nguvu za Kiume na Unashindwa Kupanda Mlima Vizuri

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA : JE UMEPUNGUKIWA NA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO AU MPENZI WAKO HAKUTIMIZII UTAKACHO:


Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sababu ya kutokuwa na nguvu za kiume au Uume wako mdogo

Dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa Kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA MWENZI WAKO BADO AJAKOJOA

KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA

UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE

KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

Dawa hii utumiwa ata na wazee wenye umri mkubwa na haina madhara yoyote

MAKAKANUA HII NI dawa ya maumbili madogo urefusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5 kwa mini huabiki kwa kuwa na UUME mdogo wai sasa upate tiba sahihi kabisa na ni tofauti na ulizowai kutumia :

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba dawa za uzazi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA p

Piga simu 0743362017 au 0789234653

DR AGU

Nandy “Nimekataa Kuuza Nguo za ndani Baada ya Makampuni Mengi Kunifuata”

$
0
0
Mwimbaji staa wa Bongofleva Nandy ambae juzi kati alikaa kwenye headlines na ishu ya kusambaa kwa video yake ya chumbani na Billnass, ameongea kwa mara ya kwanza na AyoTV na millardayo.com kuhusu kutangaza nguo ya ndani, tazama hii video hapa chini uone kila alichosema

VIDEO:

Mchungaji Peter Msigwa Ajitetea Baada ya Video Akimsifia Rais Magufuli Kusambaa...Aishangaa Ikulu

$
0
0
Baada ya kuonekana akimsifia Rais Magufuli kwenye IKULU ndogo Iringa, Mbunge wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa amejitokeza na kuzungumza na wale ambao hawajapendezwa na kitendo hicho, bonyeza play hapa chini kumsikiliza mwanzo mwisho.

VIDEO:


Hatimaye Mwanasayansi Aanza Safari ya Kujitoa Uhai

$
0
0
Mwanasayansi mwenye umri wa miaka 104 David Goodall ameaga nyumbani Australia kuanza safari ya kimataifa kwenda kujitoa uhai.

Sio kwamba mwanaekoljia huyo anaugua mahututi, La, anatamanai kuharakisha kifo chake. Sababu kuu ya uamuzi wake anasema ni kupungua kwa uhuru wake.

"Najuta kufika umri huu," Dkt Goodall alisema mwezi uliopita katika sherehe ya kuzaliwa kwake, katika mahojiano na shirika la utangazaji la Australia.

"Sina raha. Nataka kufa. Sio jambo la kuhuzunisha, kinachohuzunisha ni kwamba mtu anazuiwa kufa."

Ni jimbo moja pekee Australia lililohalalisha kujitoa uhai mwaka jana kufuatia mjadala mkali uliozusha mgawanyiko, lakini ili mtu kuruhusiwa, ni sharti awe anaugua mahututi.

Dkt Goodall anasema atasafiri kwenda katika kliniki moja nchini Uswisi kujitoa uhai kwa hiari. hatahivyo anasema anachukizwana kwamba anaondoka nyumbani ili aweze kufanya hivyo.



  • Uswizi, ni nchi pekee iliyo na vituo vinavyotoa huduma hiyo kwa raia wa mataifa mengine.
  • Uholanzi, Ubelgiji na Luxembourg zinaruhusu, hata kwa watoto lakini katika hali maalum.
  • Colombia inaruhusu kujitoa uhai kwa hiari wakati mgonjwa akiwa hatibiki.
  • Majimbo sita ya Marekani - Oregon, Washington, Vermont, Montana, California na Colorado - zinaruhusu kwa wagonjwa mahututi wasio tibika.
  • Canada ililifuata jimbo la Quebec kuruhusu hilo mnamo 2016.


Katika nchi nyingi tu Afrika, njia zote za kujitoa uhai zinatizamwa kama mauaji.

Wataalamu barani Afrika wamepinga wito wa watu kutaka kujitoa uhai kwa hiari.

Mjadala mkubwa umezuka kuhusu kinachotajwa kuwa 'kuuawa kwa huruma' hususan kwa wagonjwa walio mahututi na wasioweza kutibika.

Lakini mkutano wa muungano wa wataalamu wa afya duniani katika mkutano mapema mwaka huu mjini Abuja NIgeria waliamua kwamba hatua hiyo inakwenda kinyume na kiapo cha matabibu na inakwenda kinyume na imani na maadili ya jamii za Kiafrika.

Badala yake viongozi katika muungano hao wameyaka kuboreshwa kwa huduma za kuwashughulukia wagonjwa mahututi wasioweza kutibika.

Masuala yaliozingaiwa katika kuptisha uamuzi huo ni sheria, dini, jamii na tamaduni, saikolojia na upana wa maadili kuhusu suala hilo.

Wataalamu wa mataifa kutoka Afrika kusini, Kenya, Botswana, Zambia na Cote D'ivore walipinga hoja hiyo ya kujitoa uhai kwa hiari wakisisitiza inakwenda kinyume na maadili ya utoaji matibabu.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0

TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788
-DR KUZENZA

Kisa Harusi Bongo Movie Wamtolea Uvivu Alikiba

$
0
0
Kisa Harusi Bongo Movie Wamtolea Uvivu Alikiba
Siku chache baada ya mkali wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘AliKiba’ kuangusha bonge la sherehe ya harusi katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena jijini Dar, wasanii wa Bongo Muvi wameibuka na kumtolea uvivu staa huyo.

NI KWA NINI?

Mastaa hao wa Bongo Muvi, wamedaiwa kumtolea uvivu AliKiba kwa kitendo chake cha kutowaalika katika sherehe yake hiyo iliyofanyika Jumapili iliyopita.



MSANII AVUJISHA MCHAPO

Mmoja wa wasanii wakubwa ambaye aliomba hifadhi ya jina lake, alivujisha mchapo kuwa, baada ya harusi ya Kiba kupita na kuona wasanii wa Bongo Muvi kama walitengwatengwa kwenye mnuso huo wa nguvu, ndipo walipoanika jamvini mjadala.

“Yaani harusi ilipopita, tukafanya tathimini na kuangalia idadi ya watu waliohudhuria. Tukagundua wengi ni mastaa wa Bongo Fleva, watangazaji na wadau wengine wasiohusiana na Bongo Muvi.

“Kwa kweli tukagundua jamaa ni mbaguzi. Hakuwa fair, alipaswa kuwaalika angalau mastaa wachache wa Bongo Muvi kuonesha ushirikiano, mbona sisi kwenye mambo yetu huwa tunaalika watu wote?” alihoji msanii huyo.





AMZUNGUMZIA ESHA

Kama hiyo haitoshi, msanii huyo alienda mbali zaidi kwa kusema, ameifanyia tathimini kwa kina zaidi harusi hiyo na kusema, hakuona Bongo Muvi aliyeenda katika harusi hiyo kwa kupewa mualiko.

“Wewe fuatilia, sanasana alienda Esha Buheti peke yake sababu kama unavyojua yule ana kaundugu fulani hivi na kina Kiba,” alisema.



WARAKA WANASWA

Wakati likiendelea kuichimba habari hiyo, Amani lilifanikiwa kuunasa waraka mzito ulioonesha masikitiko ya wasanii wa Bongo kwenda kwa AliKiba kwa kitendo chake cha kutowaalika.

Waraka huo ulisomeka hivi:

“Nimeshangazwa sana na AliKiba kwa alichowafanyia Bongo Movie, inashangaza kukosa kualikwa kwa wasanii angalau wachache wa Bongo Muvi, huu ni ubaguzi wa wazi.



“Sisi Bongo Muvi tumekuwa tukishiriki matukio mengi ya wasanii wa Bongo Fleva iwe harusi, misiba na hata maradhi, lakini kwa tukio la AliKiba tumejiuliza sana, wasanii kama Wema Sepetu, Irene Uwoya, Jacqueline Wolper, Aunt Ezekiel, JB, Dk. Cheni, Ray, Richie, Gabo nk. ambao hata wachache chini ya hapo walifaa kualikwa.

“Tulimuona Esha Buheti lakini najua yule ni mwana familia kwa upande flani, sijajua ni kipi kimetokea kiasi cha kutokualikwa sisi, lakini kwenye video zao wamekuwa wakitualika ili tupendezeshe video zao, na hata kututaja ndani ya nyimbo zao,” ulisomeka waraka huo ambao unadaiwa kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii na msanii Kulwa Kikumba ‘Dude.’



KIBA ATETEWA

Chanzo kingine kilichozungumza na Amani, kilieleza kuwa, Kiba alikuwa sawa kwani si lazima amualike kila mtu katika harusi yake kwani ni jambo lake binafsi na ukizingatia suala hilo lilitawaliwa na mambo ya timu za mjini.

“Unajua kuna watu hawakualikwa kwa sababu wapo timu Diamond (Nasibu Abdul), watu wa aina hiyo si rahisi kualikwa. Kwa hiyo waache kumlaumu Kiba,” kilisema chanzo hicho ambacho ni shabiki wa Kiba wa kindakindaki.



DUDE AJILIPUA

Amani lilimtafuta muigizaji Kulwa Kikuba ‘Dude’ ambaye alisema yeye pamoja na wenzake wa Bongo Muvi hawakufurahishwa na kitendo cha kutoalikwa.

“Kuhusu kuandika waraka mimi sina cha kukubali wala kukanusha ila tambua tu kuwa wasanii wengi wa Bongo Muvi hatukupenda kutengwa.


“Sisemi angenialika mimi au wasanii wote wa Bongo Muvi lakini hata baadhi tu kama kina Irene Uwoya, Wema Sepetu, Aunt Ezekiel, Steve Nyerere au JB basi angalau ingeonesha tuko pamoja,” alisema Dude.



Amani lilijaribu kuzungumza na baadhi ya wasanii ambao hawakuonekana kwenye harusi hiyo ambapo kila mmoja alitoa mawazo yake.

Aunt: Nisingependa kabisa kuongelea kuhusu hilo.

Wolper: Kwa kweli sikupewa mualiko lakini pia nilikuwa naumwa.



Steve Nyerere: Siwezi kulalamikia kutoalikwa kwenye harusi japo najua hayo mambo ya utimu yanaweza kuingia.

Amani lilimtafuta Alikiba bila mafanikio kutokana na simu yake kuita bila kupokelewa lengo lilikuwa ni kutaka kusikia kwa upande wake anasemaje kuhusu madai ya kuwatenga wasanii wa Bongo Muvi kwenye sherehe ya harusi yake ambayo viwango vyake vilikuwa ni vya kimataifa.

Lwandamina Atambulishwa Rasmi Zesco

$
0
0
Lwandamina Atambulishwa Rasmi Zesco
Kocha wa zamani wa Yanga, George Lwandamina, rasmi ametambulishwa na uongozi wa Zesco United ya Zambia kuwa Mwalimu Mkuu wa timu hiyo.



Lwandamina alirejea nchini kwao kimyakimya akiiacha Yanga kutokana na madai ya fedha za mishahara ambazo hajalipwa.



Zesco wameamua kumrejesha tena Lwandamina wakiwa na imani kuwa atakisaidia kikosi hicho kufanya vizuri katika mashindano ya ligi na kimataifa.



Lwandamina ametambulishwa jana wakati Yanga ikiwa tayari imeshaanza kazi na Mkongomani mpya, Mwinyi Zahera aliyekuja nchini hivi karibuni kuchukua mikoba yake.

Baada ya Kupewa Onyo na TTF Haji Manara Akubali Yaishe

$
0
0
Baada ya Kupewa Onyo na TTF Haji Manara Akubali Yaishe
Kikao cha kamati ya saa 72 kilikaa na kujadili mambo mbalimbali ya Ligi hiyo sambamba na matukio yaliojitokeza, baada ya kukaa leo afisa mtendaji mkuu wa bodi ya Ligi Boniface Wambura alijitokeza mbele ya waandishi wa habari na kuzungumza maamuzi yaliofikia ikiwemo kumpa onyo kali msemaji wa Simba Haji Manara kwa kuingia uwanjani kushangilia wakati wa mchezo huo.

Baada ya kupewa onyo  Haji Manara aliandika hivi katika ukurasa wake wa instagram “Muungwana akivuliwa nguo huchutama..naomba radhi bodi ya ligi,TFF na wadau wote..nilihemewa na furaha ndugu zangu..hakuna raha kwangu mm na kwa mshabiki kama kumgalagaza mtani…it will never happen again..ila sijui itakuwaje siku ya kukabidhiwa mwali😁😁😁 @tanfootball #bodiyaligi 🙏🙏“
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images