Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Kijana wa Miaka 20 Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela kwa Kosa la Kutaka Kumbaka Bibi wa Miaka 70

$
0
0
Kijana wa Miaka 20 Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela kwa Kosa la Kutaka Kumbaka Bibi wa Miaka 70
Mahakama ya Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, imemhukumu kifungo cha miaka 3 jela Immani Andongwisye (20), mkazi wa Kijiji cha Katumba Kata ya Kibisi wilayani Rungwe mkoani Mbeya kwa kosa ya kujaribu kumbaka bibi wa miaka 70.

Bibi aliyenusurika kufanyiwa kitendo hicho ametajwa kwa jina la Rahab Salesi, 70 mkazi wa kijiji na kata hiyo.

Akisoma shtaka hilo Jumatano, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama hiyo, Patrick Maliyabibi, alidai kwamba mstakiwa huyo alitenda kosa hilo Aprili 18 mwaka huu saa 2:00 usiku alipoingia ndani ya nyumba ya mama huyo.

Alidai mshtakiwa alipoingia ndani alimvua nguo bibi huyo kwa nguvu kisha kuanza kumtomasa tomasa maeneo mbalimbali ya mwili wake, akitaka kumwingilia kimwili, lakini bibi huyo alijiangusha chini kutoka kwenye kitanda.

Maliyabibi aliiambia mahakama kuwa baada ya kujiangusha chini, alichukua panga chini ya uvungu wa kitanda kisha kumkata kidole kijana huyo, ambaye alikimbia.

Baada ya Andongwisye kukimbia, bibi huyo alikwenda kwenye uongozi wa kijiji usiku huo kutoa taarifa ambapo alikamatwa na kupelekwa polisi mjini Tukuyu.

Aliongeza kuwa baada ya kuwekwa lumande alifunguliwa kesi namba 38 na kuanza kusikilizwa katika mahakama hiyo huku mashahidi wa upande wa mashtaka wakipeleka ushahidi.

Mwendesha Mashtaka huyo aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa huyo, ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaofanya vitendo hivyo kwa kuwa suala hilo linawadhalilisha wanawake ambao wengi wao ni wajane.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Aristrida Tarimo, alisema ameridhika na ushahidi iliotolewa na upande wa mashtaka, hivyo kumhukumu kutumikia kifungo cha miaka 3 jela, ili iwe fundisho kwa wengine.

Nje ya mahakama, baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Katumba, walisema mahakama imetenda haki kwa kuwa kitendo kilichofanywa na kijana huyo ni cha udhalilishaji.

Wanaowafukuza Walimu wa Kuu Kisa Matokeo Mabaya ya Shule Kushughulikiwa

$
0
0
Wanaowafukuza Walimu wa Kuu Kisa Matokeo Mabaya ya Shule Kushughulikiwa
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako, amewajia juu baadhi ya watumishi wa serikali ambao wanatabia ya kuwafukuza kazi walimu wakuu wa shule ambao hutoa matokeo mabaya katika mitihani ya Taifa.


Ndalichako amesema hayo wakati akijibu hoja za wabunge kuhusu bajeti ya wizara yake na kuongeza watumishi hao hasa maofisa elimu, wanajukumu la kusimamia elimu katika eneo husika na sio kuwatupia lawama walimu pindi matokeo yanapokua mabaya.

“Hiyo sio sawa ni uonevu kwa wakuu wa shule kwa sababu na wenyewe wana viongozi juu yao, kwa nini wao ambao wanatakiwa kuwasimamia wasiwajibishwe, ninaagiza maofisa elimu wafanye kazi yao vizuri, utakuta mtu ana shule tano unashindwaje kuzisimamia, kwa hiyo katika hili serikali itahakiksha tunaimarisha usimamizi ikiwa ni pamoja na kuondoa viongozi ambao ni mizigo” amesema Ndalichako

Ndalichako ameongeza kwamba kama serikali inachukua hatua kubwa ili kuimarisha ubora wa elimu lakini baadhi ya watendaji hao wamekua wakirudisha nyuma jitihada hizo na serikali haitasita kuchukua hatua kwa watendaji hao.

Kwa upande mwingine Waziri Ndalichako ameitaka Tume ya Elimu ya Vyuo Vikuu (TCU) pamoja na Baraza la Taifa la Mafunzo ya Ufundi (NACTE) kuhakikisha wanafuatilia ubora elimu ya juu ili kutoa wahitimu wenye sifa zinazostahili na kiwango cha elimu husika.

Ramadhani Malima Naye Asimamishwa Kuchezea Mbeya City

$
0
0
Ramadhani Malima Naye Asimamishwa Kuchezea Mbeya City
Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania kupitia Mtendaji Mkuu, Boniface Wambura, imetangaza kumsimamisha beki wa Mbeya City, Ramadhan Malima, kwa kosa la kurudi Uwanjani kushangilia wakati akiwa amepewa kadi nyekundu.

Tukio hilo lilitokea katika mchezo dhidi ya Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa Aprili 22 katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Bodi imetangaza kumsimamisha mchezaji huyo kuichezea Mbeya City mpaka pale shauri lake litakaposikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF kisha kutolewa maamuzi.

Mchezaji huyo alipewa kadi ya pili ya njano na nyekundu kufuatia kucheza madhambi dhidi ya mchezaji wa Yanga zikiwa zimesalia dakika chache mpira kumalizika.

Mchezo huo uliofanyika Mbeya, ulimalizika kwa matokeo ya sare ya bao 1-1

Mkutano Mkuu wa Dharura Waitishwa Simba Mo Dewji Kukabidhiwa Timu?

$
0
0
Mkutano Mkuu wa Dharura Waitishwa Simba Mo Dewji Kukabidhiwa Timu?
Baada ya Simba kufanya mkutano wa kubariki mabadiliko ya mfumo Desemba 11, 2016 na wanachama kukubali,  Desemba 3, 2017 pia wanachama kwa pamoja walimpitisha Mfanyabiashara Mo Dewji kwaajili ya kuwekeza klabuni hapo na sasa wanaelekea kumkabidhi timu.


Hatua hiyo imekuja baada ya klabu hiyo kuitisha mkutano wa wanachama utakaopitisha Katiba mpya ambayo itatoa baraka rasmi za mfumo mpya wa Hisa kuanza kutumika kuendesha timu.

''Uongozi wa klabu ya Simba unapenda kuwataarifu kwamba kutakuwa na mkutano wa mabadiliko ya Katiba utakaofanyika siku ya Jumapili tarehe 20/05/2018,'' imeeleza sehemu ya taarifa ya klabu.

Katika mfumo huo wa hisa wanachama ndio watakuwa wamiliki wa hisa nyingi wakiwa na asilimia 51, huku mwekezaji akimiliki kwa asilimia 49. Tayari Mo Dewji ameshaweka wazi uwekezaji wake utakuwa na thamani ya bilioni 20.

Baada ya kutangazwa kuwa ndiye mshindi wa zabuni ya kuwekeza, Mo Dewji alieleza vipaumbele vyake kuwa ni kuwekeza kwenye timu za vijana pamoja na miundombinu ikiwemo mabweni ya timu pamoja na uwanja.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Ijumaa

Breaking News: Mahakama Kuu Imetoa Zuio la Muda Dhidi ya Matumizi ya Kanuni za Maudhui ya Kimtandao

$
0
0

MTWARA: Mahakama Kuu leo imetoa zuio la muda(Temporary Injuction) dhidi ya matumizi ya Kanuni za Maudhui ya Kimtandao (Online Content Regulations)

Kanuni hizo matumizi yake yamekwishaanza na tarehe ya mwisho ya bloga na mitandao kuridhia ilikuwa kesho Mei 5, 2018

Maombi hayo yaliyowalishwa mahakamani na waombaji 6 wakiwemo Jamii Media, Legal and Human Rights Cente(LHRC), THRDC, MCT, TAMWA na TEF

Katika kesi ya msingi ya mapatio ya kanuni hizo(Judicial review) washitakiwa ni Waziri wa Habari, Tanzania Communication Authority (TCRA) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG)

Katika maombi ya msingi waombaji wameiomba Mahakama kufanya mapitio ya kanuni hizo kwa vigezo hivi:

i) Waziri ametumia nguvu ya kisheria nje ya mamlaka yake (Ultra vires)
ii) Zinakiuka kanuni za usawa (Natural justice)
iii) Kanuni hizo zinapingana na Uhuru wa kujieleza (Freedom of Exepression) Haki ya kusikilizwa(Rights to be heard) na haki ya usiri( Right to Privacy)

Kesi ya msingi imepangwa kusikilizwa Mei 10, 2018

Kutana na Mtaalam Sharif Hamad Kalala Mchambuzi wa Nyota za Binadamu na Tiba Asili

$
0
0
KUTANA NA SHARIF HAMAD KALALA NI
SHARIFU MCHAMBUZI WA
NYOTA ZA BINAADAMU NA NI MWENYE UPEO MKUBWA KUTAFITI MATATIZO YAKO KABLA YA KUTOA USHAURI WAKE WA TIBA AlJALISHI MBALI ULIKO TIBA YAKE UMFIKIA YEYOTE MWENYE UITAJI POPOTE
DUNIANI.

 SHARIF HAMAD KALALA NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA QUR-AN, DAWA ZA ASILI ZA MITI SHAMBA PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.
ANATIBU KWA NJIA YA SIMU KWA KUTOA
MAELEKEZO NAMNA YA MATUMIZI YA DAWA UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-

 KUFANIKISHA NDOA KWA UNAYE MPENDA KWA HARAKA. KUMRUDISHA MPEZI NDANI YA MASAA 12 TU.
 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME) NDANI YA /IKI MMOJA TU
MIGUU KUWAKA MOTO KUTAFSIRI NDOTO MFARAKANO WA WANANDOA MFARAKANO KAZINIKUPANDISHWA CHEO NDANI YA SIKU SABA 7 TU.
KUTOA PETE YA BAHATI KUTOA MAJINI MACHAFU IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA. KUPATA MAFANIKIO YA MALI BILA YA MASHARTI. KUPANDIKIZANYOTA YA KUBASHIRI KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA KWENYE BIASHARA. ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE. ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA
KWA NJIA YAMSUKULE
NAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA MPYA NDANI SIKU 7 TU.
MENGINEYO MENGI ZAID YALIYO KUWA SUGU PIGA KWA WALE WALIYO ANGAIKA SEHEMU MBALI MBALI SHARIF HAMAD KALALA NI SULUISHO. ENDAPO UTAMSIKILIZA KWA YALE ATAKAYO KUSHAURI NA KUKUPA
ELEKEZI.
 TIBA NI KWA DINI ZOTE POPOTE ULIPO NJE NA NDANI YA NCHI.

MOBILE +255 -673 025 376
WhatsApp +255-757 069 066

Mambo ni Hivi Mke wa P Funk Agoma Kumuachia Nyumba Kajala "Nitapambana Hadi Kieleweke"

$
0
0
Mambo ni Hivi Mke wa P Funk Agoma Kumuachia Nyumba Kajala "Nitapambana Hadi Kieleweke"
Mke wa Prodyuza maarufu na mkongwe kwenye mziki wa Bongo fleva P Funk majani, Samira ameibuka na kudai atapambana na Kajala na kamwe hatamuachia nyumba.

Kwa Miezi kadhaa Kumekuwa na tetesi kuwa PFunk na Ex wake ambaye pia ni mama watoto wake aliyezaa naye mtoto mmoja Kajala wamerudiana kitu kinachomuweka Pabaya mke wa Pfunk ambaye hivi sasa ni mjamzito.

Samira ambaye wiki iliyopita ilisemekana alikuwa tayari kumuacha Pfunk na kurudi kwa wazazi wake Arusha, inadaiwa ameamua kupambana na Kajala na kukataa kumuacha Kajala amchukue mumewe.

Kwenye mahojiano na GPL, Samira ameongea kwa uchungu huku akidai kila siku huwa anaumizwa pale anapokutana na kashfa kumuhusu mume wake na Kajala lakini ameamua kubaaki kupambana.

"Yaani mateso ninayokutana nayo kwenye ndoa yangu ni Mungu pekee ndio anajua tena kwenye hali hii ya ujauzito niliyo nayo, awali nilipanga niondoke nimuachie nyumba lakini nimeona nikomae hadi kieleweke“.

Mara nyingi Kajala alipokuwa akiulizwa kuhusiana na kuingilia ndoa hii ya mzazi mwenzie amekuwa akikana na kusema kuwa kuwa P Funk ni baba wa mtoto wake na si vinginevyo ingawa video mbalimbali zinavuja zikiashiria ni wapenzi.

Qeen Darleen Ampa Ujumbe Mzito Harmonize "Punguza Uhuni Unamtesa Mzungu wa Watu"

$
0
0
Qeen Darleen Ampa Ujumbe Mzito Harmonize "Punguza Uhuni Unamtesa Mzungu wa Watu"
First Lady kutoka Label ya WCB, Queen Darleen ametoa ushauri mzito kwa Harmonize kuhusu maisha yake ya kimuziki na mahusiano.

Muimbaji huyo amemshari Harmonize kutokata tamaa na muziki wake ingawa watu wa kumkatisha tamaa wapo, huku akimsisitiza kuwa kuepeka kuwa katika mahusiano na wanawake wengi.

“Apunguze uhuni, atulie, mtoto wa watu masikini ya Mungu, Mzungu (Sarah) anampenda, yeye muhuni. Mdogo wangu maisha ya uhuni siyo mazuri, unakuwa kama mfalme Sulemani, ache hizo,” Queen Darleen ameiambia Radio Five.

Harmonize na Queen Darleen wameshakutana katika ngoma inayokwenda kwa jina la Zilipendwa ambayo ilikutanisha wasanii kama Diamond, Lava Lava, Rayvanny, Rich Mavoko na Mbosso.

Mbunge Chadema Amvaa Waziri Ndalichako Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Mbunge Chadema Amvaa Waziri Ndalichako Kisa Hiki Hapa
Mbunge wa Mlimba kupitia CHADEMA Suzan Kiwanga ameitaka serikali kupitia waziri wa elimu Joyce Ndalichako, kuendelea na mfumo wa kukaririsha madarasa wanafunzi kwani bila kufanya hivyo inasababisha wanafunzi wengi kutohitimu na kukosa elimu.


Suzan Kiwanga ameyasema hayo Bungeni ambapo pia amemtaka Waziri wa Elimu Prof. Joyce Ndalichako kuliangalia hili kwa undani zaidi, kwani waathirika wakubwa ni watoto wa kike, pale wanaposhindwa kufaulu mtihani na kuendelea nakidato cha tatu, hivyo hulazimika kuolewa wakiwa na umri mdogo kwa kuwa wanakosa cha kufanya.

“Sasa kukariri hamna, watoto ni wasichana, Ndalichako na wewe mwenyewe ni mwanamke, watoto wasichana wasipokariri waende wakaolewe!? Wakiwa bado wadogo!? Mi naona acheni watoto waendelee kusoma wakue shuleni wapate elimu baadaye hata wakitupwa huko mbali kama ataolewa yeye au atalima yeye”, amesema Mheshimiwa Kiwanga.

Licha ya hilo Mbunge Kiwanga ameitaka seikali kuangalia na utungaji wa mitihani, kwani kuna utofauti mkubwa wa ubora wa elimu wanaopata wanafunzi wanaoishi mazingira ya mjini, na wale wanaoishi vijijini kwani wengi wao hawana walimu.

Mwanasiasa Mkongwe wa Chama cha Upinzani Alonso Dhlakama Afariki Dunia

$
0
0
Mwanasiasa Mkongwe wa Chama cha Upinzani Alonso Dhlakama Afariki Dunia
Mwanasiasa mkongwe na kiongozi wa chama cha upinzani nchini Msumbiji, Afonso Dhlakama anaripotiwa kufariki dunia akiwa na umri wa miaka 65.

Inaelezwa kuwa kiongozi huyu Dhlakama amefariki kufuatia maradhi ya moyo yaliyokuwa yakimsumbua kwa kipindi kirefu.

Kiongozi huyu aliongoza harakati za kupinga Ukomunisti zilizofahamiaka kama RENAMO kwa kipindi cha miaka 15 ya uasi dhidi ya serikali ya Msumbiji.

Waziri Mkuu Atoa Agizo kwa Ma RC, DC Awataka Kusimamia Bei ya Bidhaa Msimu wa Ramadhani

$
0
0
Waziri Mkuu Atoa Agizo kwa Ma RC, DC Awataka Kusimamia Bei ya Bidhaa Msimu wa Ramadhani
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewatoa hofu waumini wa dini ya Kiislamu akiwaeleza kuwa bei ya bidhaa haitapanda katika msimu wa Ramadhani.

Pia amewaagiza wakuu wa mikoa (RC) na wilaya (DC) kuhakikisha wanasimamia bidhaa ili zisipande bei katika kipindi hicho.

Tayari kumekuwa na hofu miongoni mwa wananchi kuhusu upandaji wa bidhaa za vyakula katika msimu wa Ramadhani, hususan vinavyotumiwa mara kwa mara.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana bungeni mjini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kilichoongozwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Kauli ya Waziri Mkuu ilikuja baada ya mbunge wa kuteuliwa (CCM), Abdallah Bulembo kuuliza kuhusu kupanda kwa bei ya bidhaa katika kipindi cha mfungo.

“Kwa kuwa sisi Waislamu mwezi huu tunakaribia kuingia katika Ramadhani, bado kama siku saba hivi lakini sukari imepanda imefika Sh2,800 hadi Sh3,000, Serikali ina mpango gani katika hili,” alihoji.

Akijibu swali hilo, Majaliwa alisema, “Niwaondolee shaka Watanzania na katika kipindi chote cha Ramadhani sukari itapatikana na (Serikali) itafuatilia mwenendo wa bei ili watu wasipandishe wakijua kuna mfungo kwani watakuwa wanawaadhibu Waislamu.”

Katika swali la nyongeza la Bulembo alimtaka Waziri Mkuu kuwaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kusimamia hilo.

Akijibu, Waziri Mkuu alisema, “Nawaagiza wakuu wa mikoa, wilaya na maofisa biashara kuhakikisha sukari na bidhaa nyingine zote hazipandi bei kwa sababu ya kutaka kuwakomoa Watanzania, kwani malengo ya Serikali ni mazuri.”

Kadhalika, Majaliwa aliionya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutumia lugha rafiki wanapokwenda kudai kodi kwa wafanyabishara huku akisema suala la kukwama kwa meli zilizobeba mafuta ya kula katika Bandari ya Dar es Salaam linashughulikiwa.

Majaliwa alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ambaye alisema kuna taarifa za kupanda kwa bei ya mafuta kutokana na kuzuiwa kwa meli mbili za mafuta ghafi bandarini.

“Bunge lako lilipitisha sheria ya kutoza mafuta ghafi kwa asilimia 10 na mafuta masafi kwa asilimia 25 ili kulinda viwanda vya nchini. Lakini hivi sasa mafuta ya kula yameanza kupanda wakati kuna meli mbili zimezuiwa bandarini. Ili bei isiendelee kupanda, Serikali ina mpango gani na uagizaji wa mafuta,” aliuliza Lema.

Waziri Mkuu alisema atatoa mrejesho kwa kuwa kuna timu ya ufuatiliaji inayofanya kazi hiyo.

Pia, Majaliwa alisisitiza kuwa Serikali itawachukulia hatua maofisa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wanaotumia lugha chafu kwa wafanyabiashara.

Waziri Mkuu alisema hayo akijibu swali la Mbunge wa Tunduma (Chadema), Frank Mwakajoka aliyetaka kujua Serikali inatoa kauli gani kuhusu matatizo wanayofanyiwa wafanyabishara na TRA hasa ya unyanyasaji na kuongezewa kodi.

Alisema hatua zilizochukuliwa mkoani Lindi kwa watumishi wa TRA zitachukuliwa pia kwa wengine. “Waziri (wa Fedha) mkutane na TRA kuwakumbusha wajibu wao, ili TRA wawe sehemu nzuri kwani kodi inayotolewa na wafanyabiashara inatusaidia kutekeleza miradi yetu hii,” alisema.

Twitter Yawataka Watumiaji Wake Kubadilisha Password Zao

$
0
0
Twitter Yawataka Watumiaji Wake Kubadilisha Password Zao
Kampuni ya mtandao wa Twitter imewaambia watumiaji wa mtandao huo ambao ni takriban milioni 330 duniani kote kubadilisha password zao baada ‘kirusi’ kuingia kwenye mfumo wa mtandao huo na kusababisha password za watumiaji kuonekana kwa maandishi.

Kampuni hiyo imeeleza kuwa hakuna madhara yaliyofanyika kwani hakuna taarifa za watu zilizoibwa kutokana na kuonekana kwa password hizo, lakini ni vyema wazibadilishe kwa tahadhari.

Taarifa hiyo imetolewa na Afisa Mkuu wa Twitter Jack Dorsey kwa kuandika kwenye account yake ya mtandao huo na kuomba radhi kwa kilichotokea.

Familia ya John Heche Yakataa Fidia ya Serikali

$
0
0
Familia ya John Heche Yakataa Fidia
Chacha Suguta (27), ndugu wa Mbunge wa Tarime Vijijini (Chadema), John Heche aliyefariki dunia akidaiwa kuchomwa kisu akiwa mikononi mwa polisi, alizikwa jana nyumbani kwao katika Kijiji cha Nyabitocho wilayani humo.

Ingawa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima aliyefika nyumbani kwa marehemu kuhani msiba aliahidi kuwa Serikali itashirikiana na familia katika msiba huo, hakuna kiongozi yeyote wa Serikali wala Jeshi la Polisi ngazi ya mkoa na wilaya aliyehudhuria mazishi.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Mara, Samuel Kiboye ndiye pekee aliyekuwa kiongozi wa chama tawala wa ngazi ya juu aliyehudhuria mazishi hayo.

Poul Kagame Awawakia Viongozi wa Arsenal .... Amkingia Kifua Wenger

$
0
0
Poul Kagame Awawakia Viongozi wa Arsenal .... Amkingia Kifua Wenger
Rais wa Rwanda Mh. Paul Kagame ameweka wazi kuwa kufanya vibaya kwa Arsenal ni tatizo la uongozi na sio kocha Arsene Wenger hivyo yeye kama shabiki wa timu hiyo ameumizwa na Wenger kuonbdoka bila taji.


Kagame ametumia mtandao wa 'Twitter' kuelezea mapenzi yake kwa klabu hiyo ambayo usiku wa kuamkia leo imeondolewa kwenye michuano ya Kombe la Europa.

''Kuhusu timu yangu ninayoipenda ya Arsenal, ni timu nzuri sana na imekuwa na kocha bora sana ambaye ni Wenger na hakupaswa kuwa na mwisho huu wa kuondoka bila kombe, lawama zote ziwaendee viongozi, lakini nitaendelea kuipenda Arsenal'' amendika Kagame.

Mapema mwezi April, Arsene Wenger alitamngaza kuondoka Arsenal mwishoni mwa msimu huu baada ya kuifundisha timu hiyo kwa miaka 22 huku akiipatia mafanikio kadhaa.



Kutolewa kwa Arsenal jana na Atletico Madrid kunamaanisha timu hiyo msimu ujao haitashiriki michuano ya klabu bingwa Ulaya msimu ujao. Arsenal sasa inashika nafasi ya 6 kwenye msimamo wa EPL na ikimalizia hapo itashiriki Europa msimu ujao.


Diwani na Msanii Baba Levo Apandishwa Kizimbani Kwa Kutoa Kichapo Kwa Muuguzi

$
0
0

Msanii wa Bongo Fleva Levocatus Chipando maarufu kwa jina la Baba Levo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mwanaga Kaskazini katika Manispaa ya Kigoma Ujiji amepandishwa kizimbani leo katika Mahakama ya Wilaya mkoani Kigoma kwa tuhuma za kumpiga muuguzi wa zahanati ya Msufini.
.
.
TOA MAONI YAKO HAPA

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI3 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

Barabara Yafungwa Jangwani... Mndokasi Wasitisha Huduma

$
0
0
 Barabara Yafungwa Jangwani... Mndokasi Wasitisha Huduma
Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 6:00 mchana kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha


Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa na kusema wamechukua maamuzi hayo kutokana na maji mengi ya mvua kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria pamoja na vyombo vya usafirishaji.

"Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi - Kimara, Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, Kivukoni - Muhimbili, Gerezani - Kvukoni, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa", amesema Bugaywa.

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewaomba radhi wananchi wanaotumia usafiri huo kwa usumbufu ambao utajitokeza kwa namna moja ama nyingine.

Nyumba ya Joti Yabomolewa Afunguka Kisa Kizima

$
0
0
Nyumba ya Joti Yabomolewa Afunguka Kisa Kizima
Hapo jana May 03, 2018 Mchekeshaji Lucas Mhavile ‘Joti’ aligonga vichwa vya habari mara baada ya kuwepo taarifa zilizodai kuwa nyumba yake iliyopo Kibada, Kigamboni imevunjwa ili kupisha upanuzi wa barabara, sasa Joti ameeleza kilichotokea.

Akiongea na Clouds FM amesema si kweli kwamba nyumba yake imevunja bali ni ukuta ndio umewekwa alama ya X ila amekiri kuwepo kwa zoezi hilo.

‘’Wanapanua barabara huku kwetu, lakini huo upanuzi wa barabara haujahusiana na ubomoaji wa nyumba, wengi wanajua nyumba yangu ndio inabomolewa lakini sivyo, kinachobomolewa ni ukuta tu,’’ amesema Joti.

Kwa mujibu wa Afisa Manispaa ya Kigamboni, Davidi Langa wakazi zaidi ya 100 wa Kibada na Kisarawe wilayani Kigamboni nyumba zao zimewekea alama ya X na kutakiwa kubomolewa ili kupisha ujenzi wa barabara.

Chanzo cha tatizo ni Wizara ya Ardhi, Nyumba Maendeleo ya Makazi iliyopima maeneo hayo, Tanroad walikuwa bado hawajaweka alama zao za barabarani na viwanja hivyo ni vya muda mrefu, hivyo wamekuja kuweka wakati vimeshaendelezwa, hata hivyo Mkuu wa wilaya hiyo, Hashim Mgandilwa ameingilia kati suala hilo.

Serikali ya Burund Yaipiga Marufuku BBC, VoA Kurusha Matangazo Nchini Humo

$
0
0
Serikali ya Burund Yaipiga Marufuku BBC, VoA Kurusha Matangazo Nchini Humo
Serikali nchini Burundi kupitia Baraza la taifa la Mawasiliano (Conseil National de la Communation- CNC) imeyapiga marufuku mashirika mawili ya kimataifa ya utangazaji ya BBC na VoA .

Taarifa ya kufungiwa kwa mashirika hayo imetolewa leo Mei 04, 2018 na Rais wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini humo, Karenga Ramadhan ambapo imesema kuwa mashirika mwisho wa kurusha matangazo yao nchini Burundi ni Mei 07 mwaka huu.

Sababu za mashirika hayo kufungiwa ni kufanya mahojiano na watu walioiasi Burundi wanaoishi ughaibuni na kuyarusha nchini humo kitu ambacho ni kinyume na sheria za mawasiliano na ni uchochezi.

Sambamba na adhabu hiyo, vituo vingine vitatu vya redio RFI, Isanganiro na CCIB FM vimepigwa onyo kali huku gazeti Le Renouveau la nchini humo likifungiwa miezi mitatu.

Sababu za kufungiwa kwa gazeti hilo ni kuandika habari ya kuandika makala zenye uchochezi zilizolenga kuikosoa serikali ya Rais Pierre Nkurunziza.
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images