Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Aliyekuwa Kocha wa Yanga Afariki Dunia

0
0
Aliyekuwa Kocha wa Yanga Afariki Dunia
Aliyekuwa Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga, Jack Chamangwana amefariki dunia hapo jana siku ya Jumapili majira ya jioni kwenye Hospitali ya Queen Elizabeth (QECH) nchini Malawi.

Ripoti zinaeleza kuwa chanzo cha kifo chake ni kutokana na shinikizo la Moyo hii ikiwa ni Mwezi mmoja umepita toka kumzika mpwa wake, George Chamangwana.

Wakati wa uhai wake Chamangwana maarufu kwajina la ‘Africa’ alikuwa Mkurugenzi wa ufundi ndani ya klabu ya Be Forward Wanderers ya nchini Malawi.

Nahodha huyo wazamani aliyekuwa na umri wa miaka 61, aliwahi kuifundisha timu ya Yanga mwaka 2006 kabla kutimka zake kwao.

Chamangwana ameanza kuitumikia timu yake ya Taifa ya Malawi kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Kenya Julai 10 mwaka 1975 akiwa na umri wa miaka 18 huku goli lake la kwanza akifunga dhidi ya Botswana.


Penzi la David, Chioma Lazidi Kushika Kasi ni Bata tu

0
0
Penzi la David, Chioma  Lazidi Kushika Kasi
Msanii Davido na mpenzi wake Chioma wamezidi kuonyesha mapenzi yao ni kama njiwa baada ya kuyafanya siri kwa muda mrefu.

Davido ameweka picha kwenye mtandao wake wa Instagram akiwa na mrembo wake huyo huku wakionekana wenye furaha kubwa na kuandika kwenye moja yapicha ujumbe unaosomeka, “Happy people 😁.”

Msanii huyo wiki iliyopita alimzawadia mrembo wake huyo gari aina ya Porsche SUV yenye thamani ya kiasi cha dola 125k ambapo ni zaidi ya shilingi milioni 285 za Kitanzania kwenye birthday yake.



Kigwangalla Aagiza Kuandaliwa kwa Mkataba wa Makubaliano

0
0
Kigwangalla Aagiza Kuandaliwa kwa Mkataba wa Makubaliano
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, ameagiza uandaliwe mkataba wa makubaliano ya awali (MoU) ya utekelezaji wa mradi wa kuendeleza utalii wa picha katika Pori la Akiba Selous.

Mkataba huo wa makubaliano utahusisha wawekezaji kutoka Jiji la London nchini Uingereza na Serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA na utakapokamilika utasainiwa na pande zote mbili.

Dk. Kigwangalla ametoa agizo hilo akiwa ofisini kwake Jijini Dodoma kufuatia maombi yaliyowasilishwa kwake na wawekezaji hao, Eva Sanchez na Nicholas Negre.

Akiwasilisha maombi hayo, Sanchez amesema mradi huo utakuwa wa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA ambao ndiyo wasimamizi wakuu wa Pori la Akiba Selous utakapoanzishwa mradi huo.

Dk. Kigwangalla amewataka wawekezaji hao kuwasilisha andiko la mradi huo, kufanya utafiti wa kina na tathmini ya athari za kimazingira zitakazoweza kujitokeza kutokana na uanzishwaji wa mradi huo.

Kwangwaru ya Harmonize Yakimbiza Chati za BBC Radio

0
0
Kwangwaru ya Harmonize Yakimbiza Chati za BBC Radio
Harmonize amefanikiwa kuingiza ngoma yake ya Kwa Ngwaru kwenye Top 5 za Afro Boss Airline DNA za kipindi cha Destination Africa kinachoendeshwa na DJ Edu kupitia BBC Radio One Xtra.

Wimbo huo umefanikiwa kushika namba mbili kwenye chati hizo wakati namba moja ikishikiliwa na Davido kupitia wimbo wake mpya wa Assurance.

Wiki iliyopita wimbo huo ulishika namba tano kwenye chati hizo.

Wasanii wengine walioingia kwenye chati hizo ni Shado Chris (Kitadi), Bils na Giggz (Loudah) na Da Capo (Take It All).

Barua Ya Kumnusuru Malasusa Yasomwa Makanisani

0
0
Barua Ya Kumnusuru Malasusa Yasomwa Makanisani
Waumini  wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),  Dayosisi ya Mashariki na Pwani(DMP),  walisomewa barua maalumu kuhusiana na suala  la Askofu wao, Dk. Alex Malasusa.

Kusomwa kwa barua hiyo jana kunatokana na kikao cha Halmashauri Kuu ya Dayosisi ya Mashariki na Pwani kilichokutana Jumatano iliyopita.

Barua hiyo iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa Dayosisi hiyo, Godfrey Nkini, ilisomwa katika usharika mbalimbali za dayosisi hiyo wakati wa matangazo.

Kwa mujibu wa barua hiyo, washarika wametakiwa kufahamu kwamba Dk. Malasusa ni Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani na dayosisi itaendelea na umoja na mshikamano na askofu huyo katika kuongoza na kuihubiri injili ya Yesu Kristo.

“Halmashauri kuu inaendelea kulifuatilia jambo hili kwa makini. Washarika mnaombwa kuwa watulivu na kuliombea kanisa.

“Tunaombwa kutunza amani na umoja wa kanisa kama neno la Mungu linavyosema,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo.

Askofu Malasusa, Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini na Kati, Solomon Massangwa na Askofu wa Dayosisi ya Kusini Mashariki, Dk. Lucas Mbedule, wanatuhumiwa kwa usaliti kutokana na uamuzi wao wa kuzuia waraka wa Pasaka ulioandaliwa na maaskofu 27 wa kanisa hilo usisomwe katika dayosisi wanazoziongoza.

Jumapili iliyopita Askofu Mbedule alilazimika kuomba radhi kutii maagizo ya Baraza la Maaskofu wa KKKT.

Waraka huo ulioandaliwa mwishoni mwa Machi mwaka huu, wiki moja kabla ya maadhimisho ya Sikukuu ya Pasaka, ulichambua masuala ya jamii, uchumi, maisha ya siasa, umuhimu wa katiba mpya na matukio yaliyo kinyume na kile walichokiita tunu na misingi ya taifa.

Licha ya barua hiyo ya kanisa kusomwa baadhi ya waumini walihoji hatua hiyo kutokana na kutosomwa na waraka wa kanisa wa Pasaka na badala yake wamesomewa barua ya kumkingia kifua Askofu Malasusa.

Hatua ya halmashauri kuu ya dayosisi hiyo imeonyesha kumkingia kifua kutokana na barua iliyoandaliwa na chombo hicho na ilisomwa jana.

Kwa mujibu wa nakala ya barua hiyo , Halmashauri Kuu ya Dayosisi hiyo, imesema haikuwa na lengo la kupingana na maazimio ya Mkutano Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa  KKKT juu ya kusomwa kwa Waraka wa Pasaka.

Barua hiyo imesema maelekezo yote yaliyotolewa yamezingatiwa na imesisitiza kuwa umoja na mshikamano kwa Askofu Dk. Malasusa utaendelea katika kuongoza na kuihubiri Injili ya Yesu Kristo.

Barua hiyo ilieleza kuwa halmashauri hiyo ilikaa kikao Mei 2, mwaka huu na ilijadili na kujiridhisha kuhusu barua aliyoandikiwa Askofu Malasusa kuwa alikiuka mapatano yaliyotolewa na mkutano wa maaskofu wa KKKT.

“Halmashauri Kuu imetafakari kwa kina jambo hili na kujiridhisha kwamba: Haikuwa lengo la DMP kupingana na maazimio ya Mkutano wa Maaskofu daima. Maelekezo yote yaliyotolewa na KKKT Makao Makuu yamezingatiwa.

“Hata hivyo, Halmashauri Kuu imesikitishwa kwa jinsi suala zima lilivyotunzwa hadi kufikia vyombo vya habari na baadhi yao kupotosha ukweli wa suala zima,” ilieleza sehemu ya barua hiyo.

Kuhusu Askofu Malasusa barua hiyo ilisisitiza: “Washirika mfahamu kwamba Malasusa ni Askofu wa DMP. Halmashauri inatoa pole nyingi kwa Baba Askofu na familia yake kwa usumbufu uliojitokeza. DMP itaendelea na umoja na mshikamano na Askofu Malasusa katika kuongoza na kuhubiri Injili ya Yesu Kristo.”

Pamoja na barua hiyo kutoa pole kwa washirika wote kutokana na kuumizwa kwao na taarifa za kuandikiwa barua Askofu Malasusa za kukiuka mapatano ya Baraza la Maaskofu, ilizodai haikuwa lengo la KKKT Makao Makuu kuwaumiza waumini wake, pia ilieleza inaendelea kulifuatilia jambo hilo kwa makini.

Pia barua hiyo iliwaelekeza washirika hao kuwa watulivu na kuliombea kanisa na kutunza amani na umoja.

Uamuzi wa kumtenga Askofu Malasusa ulifikiwa na kikao cha Baraza la Maaskofu wapatao 25, lililoketi mjini Arusha, chini ya kiongozi wake ambaye ndiye mkuu wa kanisa hilo, Askofu Dk. Fredrick Shoo.

Huu Ndio Mnara wa Kumbukumbu ya Wanafunzi wa Lucky Vincent

0
0
Huu Ndio Mnara wa Kumbukumbu ya Wanafunzi wa Lucky Vincent
Mnamo May 6, 2017 Tanzania ilizizima kwa taarifa za ajali iliyohusisha basi la wanafunzi wa shule ya Lucky Vincent ambayo iliua wanafunzi 29, dereva na walimu wawili huko katika mlima Rhotia wilayani Karatu Mkoani Arusha.

Jana May 6 ilikuwa ni kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kutokea kwa ajali hiyo iliyobakiza wanafunzi watatu tu waliokuwa kwenye basi hilo.

Katika kumbukumbu hiyo shule ya Lucky Vincent imefanya ibada maalumu ya kuwakumbuka wanafunzi pamoja na waalimu waliofariki kwenye ajali hiyo.

Umejengwa mnara katika eneo la mlima huo wa Rhotia ambapo ndipo gari hilo lilipopata ajali. Mnara huo una majina ya watoto wote waliofariki kwenye ajali hiyo.

Mafuta ya Kula Yaanza Kuhadimika Viwanda Vyasitisha Uzalishaji

0
0
Mafuta ya Kula Yaanza Kuhadimika Viwanda Vyasitisha Uzalishaji
Sakata la kuzuiwa kwa meli mbili zenye tani 62,000 za mafuta ya kula katika Bandari ya Dar es Salaam, linatishia kuadimika kwa bidhaa hiyo baada ya viwanda vingi kusitisha uzalishaji.

Tayari bei ya mafuta ya kula imeanza kupanda kutokana na kuadimika kwake sokoni baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuzizuia meli hizo tangu mwezi uliopita kushusha mzigo mpaka wamiliki wake watakapolipa kodi husika.

Utata wa kulipa kodi inayodaiwa na TRA, unatokana na madai ya mamlaka hiyo inayosema mafuta yaliyoingizwa ni safi ilhali wamiliki wakieleza ni ghafi.

Kwa utaratibu uliopo, mafuta safi ya kula yanayoingizwa kutoka nje ya nchi hulipiwa kodi ya asilimia 25 wakati ghafi yanatozwa asilimia 10.

Licha ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuahidi kulifuatilia suala hilo, mkurugenzi wa Elimu ya Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo aliliambia Mwananchi kuwa hakuna namna zaidi ya wamiliki hao kulipa kodi husika badala ya kuendelea kulalamika.

“Ni kweli tunazishikilia meli mbili zenye mafuta ya kupikia. Wanachotakiwa ni kulipa kodi tu. Kama wanaona wameonewa wafuate utaratibu wa kukata rufaa, siyo kulalamika kwenye vyombo vya habari,” alisema Kayombo.

Hivi karibuni, alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Kuteuliwa, Abdallah Bulembo bungeni jijini Dodoma, Majaliwa aliwahakikishia Watanzania kuwa bei ya sukari na mafuta ya kula hazitapanda kuelekea mfungo wa Ramadhan unaotarajiwa kuanza Mei 15 kulingana na mwandamo wa mwezi.

Bei zinapanda

Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwapo ongezeko la bei ya mafuta ya kupikia kuanzia mwishoni mwa Aprili. Mwananchi limeangalia bei hizo mpaka juzi jioni.

Jijini Arusha, lita moja imepanda kutoka Sh3,500 hadi 4,000 huku ndoo yenye ujazo wa lita 10 ikiuzwa Sh35,000 kutoka Sh31,000 za awali.

Jijini Dodoma, ndoo ya lita 20 ya mafuta hayo sasa inauzwa Sh70,000 kutoka Sh56,000.

Mkoani Geita, kibaba kilichokuwa kikiuzwa Sh100 sasa kinauzwa Sh300, wakati kibaba kimoja kinauzwa Sh500 kikiwa kimepanda kutoka Sh300 ya Januari jijini Mwanza.

Kwenye baadhi ya maduka jijini Dar es Salaam, robo lita imepanda kutoka Sh600 hadi Sh1,000, wakati nusu lita ikitoka Sh1,600 mpaka Sh2,000.

Lita moja iliyokuwa inauzwa Sh3,200 sasa ni Sh4,000 wakati ndoo ya lita 20 ikiuzwa Sh70,000 kutoka Sh55,000.

Kupanda kwa bei hiyo kunatokana na uwezo mdogo wa Tanzania kuzalisha mafuta ya kula. Takwimu za Chama cha Wasindikaji wa Mbegu za Alizeti (Tasupa), zinaonyesha mahitaji ya bidhaa hiyo nchini ni tani 570,000 kwa mwaka na wazalishaji wa ndani husindika tani 210,000.

Mwenyekiti wa Tasupa, Ringo Iringo anasema kati ya kiasi hicho kinachozalishwa nchini, tani 180,000 zinatokana na alizeti wakati vyanzo vingine ikiwamo pamba zikichangia tani 30,000 zilizobaki hivyo kulazimika kuagiza tani 200,000.

Tofauti na takwimu za mwenyekiti huyo, taarifa nyingine zinaonyesha mahitaji ya mafuta hayo ni tani 400,000, huku uzalishaji wa ndani ukiwa haufiki hata robo.

Mmoja wa wazalishaji wa alizeti anasema mbegu zote za alizeti zinazozalishwa nchini ni tani 100,000, zikikamuliwa hutoa tani 25,000 tu za mafuta ya kula.

Kati ya tani 80,000 za mbegu za pamba inayolimwa zaidi mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa mwaka, zikikamuliwa hutoa tani 10,000 za mafuta.

“Kwa takwimu hizi, uzalishaji wa ndani ni tani 35,000 za mafuta lakini bado Serikali inatoa kibali cha kuuzwa nje kiasi cha tani 10,000 kila mwaka. Kuzuiwa kwa mafuta hayo kunazidisha upungufu nchini,” kilisema chanzo kingine.

Mzozo

Wakati TRA ikiwataka waagizaji husika kulipa kodi inayodaiwa, kiongozi wa Chama cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA), Hussein Kamote alisema mabadiliko yanayoleta mkanganyiko unatokana na kanuni mpya za kodi zilizotungwa na mamlaka hiyo Februari, lakini zikitakiwa kutumika kuanzia mwishoni mwa mwaka jana.

“TRA wametunga kanuni Februari, lakini wanataka zianze kutumika kwa mizigo iliyoingizwa tangu Novemba mwaka jana. Pia, wanawataka wafanyabiashara walete nyaraka ambazo awali hawakuzidai,” alisema Kamote.

Kutokana na ugumu wa kupata nyaraka zinazohitajika, Kamote alisema itakuwa rahisi kwa TRA wakiziomba kutoka Serikali za nchi husika kwa sababu ni rahisi mamlaka za umma kubadilishana taarifa.

“Tunashangaa wanaposema ni mafuta safi wakati (Shirika la Viwango Tanzania) TBS, ofisi ya mkemia mkuu wa Serikali na (Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania) TFDA wameshakagua na kuthibitisha kuwa ni ghafi,” alisema Kamote.

Licha ya taasisi hizo kuthibitisha kuwa mafuta hayo ni ghafi, TRA imezitaka kampuni zilizoyaagiza kupeleka nyaraka kutoka Indonesia na Malaysia walikonunua ili kuthibitisha kama ni ghafi.

Kutokana na zuio la mafuta hayo ambayo ni malighafi kwa viwanda vya mafuta nchini vinavyojumuisha Bidco, East Coast, Azania na Murza Oil, vimelazimika kusitisha uzalishaji.

Mmoja wa wamiliki wa mafuta yaliyozuiwa bandarini alisema: “Hilo suala lina siasa ndani yake.”

Ofisa mmoja wa TBS ambaye aliomba kutotajwa, alisema suala hilo lipo ngazi za juu lakini tayari shirika hilo lilishayapima na kujiridhisha ni ghafi.

“TBS inatumia wataalamu, hatupimi kwa macho. Hilo suala tumeziachia Wizara za Fedha, Afya na Viwanda watalizungumzia wenyewe. Sisi tumepima na kuona ni mafuta ghafi, mkemia mkuu wa Serikali naye amekuta ni crude oil (ghafi), basi tumeziachia ngazi za juu,” alisema ofisa huyo.

Kaimu meneja masoko, mawasiliano na huduma kwa wateja wa ofisi ya mkemia mkuu wa Serikali, Cletus Mnzava alitaka taarifa zitafutwe mamlaka nyingine.

“Ni vyema ukawauliza watu bandari kwa sababu wao wanajua nani aliyapima hayo mafuta. Kama ni vyakula kuna taasisi yake, kama ni kemikali kuna taasisi yake, ukiwauliza hao ndiyo wanajua,” alisema Mnzava.

Naye meneja mawasiliano wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Janet Ruzangi alisema mamlaka hiyo haihusiki na upimaji wa mizigo bali wenye jukumu hilo ni TRA.

“Kazi ya kupima ni ya TRA kwa sababu mizigo yote ikishafika bandarini huwa ni yao. Wakisema tupakue tunapakua, wakisema tuache tunaacha. Sisi tunatoa mizigo baada ya kuhakikisha nyaraka zote zimekamilika,” alisema Ruzangi.

Mkakati

Mwenyekiti wa Tasupa, Ringo Iringo alisema japo hawawezi kuziba pengo la mahitaji nchini, lakini wanaendelea kuongeza uzalishaji kuanzia kwenye kilimo hadi viwandani.

“Kwa Dodoma, mafuta ya Korie yamefikia Sh70,000 kwa ndoo ya lita 20 ila tunajitahidi kukamua mafuta ya kutosha ili kukidhi mahitaji. Mwaka huu wakulima wamevuna alizeti nyingi na ukamuaji umeongezeka, kwa hiyo tutapunguza tofauti ya mahitaji na uzalishaji uliopo,” alisema Ringo.

Vilevile, alisema Serikali imeimarisha uzalishaji wa pamba kwa kupeleka mbegu bora kuongeza uzalishaji wa mafuta.

Wiki iliyopita suala hilo liliibuka katika Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira mjini Dodoma, mwenyekiti wake Sadiq Murad alisema meli hizo zimekaa bandarini kwa zaidi ya wiki mbili kutokana na ubishani kati ya Shirika la Viwango (TBS) linalosema mafuta hayo ni ghafi huku TRA ikipinga.

Baada ya Kutandikwa Bao Nne Yanga Kurejea Dar Leo

0
0
Baada ya Kutandikwa Bao Nne Yanga Kurejea Dar Leo
Baada ya kupoteza mchezo wa jana ukiwa ni wa kwanza katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, kikosi cha Yanga kinatarajia kuanza safari ya kurejea nchini leo.

Yanga ilikubali kuanza vibaya dhidi ya USM Alger kwa kufungwa idadi ya mabao 4-0, mechi ikipigwa majira ya saa 4 usiku wa jana.

Yanga itaanza safari yake kwa kupitia nchini Dubai kisha kuanza tena safari ya kuendelea kurejea Tanzania.

Matokeo hayo ni mwanzo mbaya kwa Yana kutokana na kipigo hicho kikali ambapo sasa inahitaji kuweka nguvu nyingi katika michezo mingine itakayofuata kwenye kundi hilo.

Ukiachana na USM Alger, ikumbukwe Yanga ipo na timu za Rayon Sports ya Rwanda na Gor Mahia FC ya Kenya.

Serikali Kufanya Ukaguzi za Sehemu za Kazi Nchi Nzima

0
0
Serikali Kufanya Ukaguzi za Sehemu za Kazi  Nchi Nzima
Serikali ya awamu ya tano kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imesema itafanya zoezi la ukaguzi nchini nzima katika sehemu za kazi ikiwemo kampuni ya ACACIA ili iweze kuwabaini waajiri ambao hawazingatii vigezo na masharti wanayopaswa kuwafanyia wafanyakazi wao.


Kauli hiyo imetolewa leo Mei 07, 2018 na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde Bungeni Jijini Dodoma kwenye kikao cha 23 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akijibu la Mbunge wa viti maalum Jocye B. Sokombi aliyetaka kusikia kauli ya serikali juu ya tatizo la wafanyakazi wa mgodi wa Nyamongo kutolipwa mshahara wala posho pindi wafanyapo kazi zao.

"Mgodi wa dhahabu wa Nyamongo unamilikiwa na kampuni ya ACACIA na kwenye mgodi huo kuna makundi mawili ya wafanyakazi ambapo moja ni wale walioajiriwa na ACACIA na pili wafanyakazi waliajiriwa na makampuni yanayopewa kazi na ACACIA 'sub contractors'. Hivyo kwa wafanyakazi walioajiriwa na ACACIA wao hawalipwi posho bali hulipwa mshahara kwa mwezi", amesema Mavunde.

Pamoja na hayo, Mavunde ameendelea kwa kusema "makampuni mengine huwa wanalipwa mishahara kutokana na aina ya mikataba ya ajira na asili ya kazi anayoifanya mfanyakazi kwa kuzingatia sheria. Ofisi yangu kupitia idara ya kazi itaendelea kufanya kaguzi za kazi katika sehemu za kazi mbalimbali nchini ikiwepo kampuni ya ACACIA kwa lengo la kuwatambua waajiri ambao hawazin gatii matakwa ya sheria za kazi yanayotakiwa".

Kwa upande mwingine, Naibu Waziri Antony Mavunde amesema idara ya kazi imekuwa na taratibu za kufanya ukaguzi katika makampuni yote kwa lengo la kujua changamoto mbalimbali zinazojitokeza kwa wafanyakazi.

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

0
0

TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Tazama Picha Jinsi Volacano Hai ilivyolipuka huko Hawii

0
0

HAWAII: Moja kati ya Volkano hai Ulimwenguni yalipuka na kuharibu nyumba 26. Lava yaruka zaidi ya mita 100 hewani

Takribani watu 1,700 wamelazimika kuondoka katika eneo hilo na wanapaswa kukaa mbali na eneo hilo lililokuwa makazi yao kwa muda

Kilauea ni Volkano iliyo hai ambayo tangu mwaka 1983 imekuwa ikilipuka mara kwa mara

Hatimaye Nchi ya Saudi Arabia yaruhusu Ujenzi wa Makanisa Baada ya Katazo la Muda Mrefu

0
0

Nchi ya Saudi Arabia imeamua kuruhusu ujenzi wa makanisa baada ya kusainiwa kwa makubaliano kati ya viongozi wa Wahhabi na Kadinali wa Vatican.

Makubaliano hayo kati ya Rais wa Baraza la Kipontifiki ya midahalo ya dini mbalimbali, Kadinali Jean-Louis Tauran na Sheikh Mohammed bin Abdel Karim Al-Issa, ambaye ni Katibu Mkuu wa NGO kubwa ya Wahhabi yanalenga kuruhusu ujenzi wa makanisa pamoja na mikutano ya Waislamu na Wakristo mara moja kila baada ya miaka miwili.

Saudi Arabia ni moja ya nchi zisizo na uvumilivu kwa dini nyingine zaidi ya Uislamu. Wasio waislamu wanaadhibiwa kwa kuonesha matendo ya dini yao nje ya nyumba zao huku Muislamu yeyote anayeamua kubadili dini akihukumiwa kifo. Sheria za kiislamu zinawahusu wote wanaoishi nchini humo bila kuzingatia imani zao huku Jeshi la Polisi likisimamia ufuatwaji wake.

Hadi sasa inakadiriwa kuwa kuna Wakristo zaidi ya Milioni 1.5 nchini humo ambao ni wahamiaji wanaofanya kazi hususani kutoka nchi ya Ufilipino.

Uwezekano wa ufanikiwa kwa harakati hizi za Vatican zilizoanza mwaka 2008 ulianza kuonekana baada ya Mwanamfalme Mohammed bin Salman kuingia madarakani ambapo amedhamiria kubadili muonekano wa nchi hiyo kimataifa kwa kubadili mambo kadhaa.

Katika kipindi chake tayari ameshabadili taratibu kadhaa zilizokuwepo kwa miaka mingi kama wanawake kutoruhusiwa kuendesha magari na kutakiwa kuwa na mwangalizi muda wote.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

0
0

Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu
kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI

0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR Magise

Rais Magufuli Ahamisha Bilioni 2 za UDSM Azipeleka SUA

0
0
Rais Magufuli Ahamisha Bilioni 2za UDSM Azipeleka SUA
Rais Magufuli ametoa agizo hilo kwa Waziri anayehusika na wizara hiyo, Prof. Joyce Ndalichako, leo Mei 7, 2018 wakati akihutubia Jumuia ya Chuo hicho alipokitembelea na kupata fursa ya kusikiliza kero za wanafunzi, wahadhiri na wafanyakazi wengine wa chuo hicho ambapo alizitolea ufafanuzi na nyingine kuagiza uongozi wa chuo kuzitatua.


“Mimi ninaamini Chuo Kikuu hiki cha SUA kinaweza kikawa chanzo kikubwa cha kubadilisha maisha ya Watanzania wengi, ninakipenda chuo hiki, si kwa sababu ya jina la Sokoine, ni kwa sababu ya jinsi kinavyofanya kazi.



“Ninafahamu kuwa mna changamoto nyingi, Waziri wa Elimu (Prof. Ndalichako) amesema ametenga Shilingi Bilioni 2 kwa ajili ya kuongeza majengo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mimi ninasema hizo bilioni mbili haziendi UDSM, nazihamishia hapa ili zianze kujenga mabweni.



“Tatizo langu mimi ni moja tu, ni usimamizi, nimeenda Chuo cha Mkwawa, Iringa, nilikuwa discouraged, ninapotoa pesa ninafuatilia, mimi siyo ‘kilaza’ kwa kufuatilia, ninafuatilia kila senti, na ninafahamu thamani ya pesa.



“Sipendi nitakapokuja hapa SUA halafu nikute hizo pesa zimetumika vibaya. Niwaambie tu ukweli sitaki kuonekana mnafiki, mzitumie vizuri. Mimi ninataka dhamira ile ya Baba wa Taifa aliyeanzisha chuo hiki cha SUA tuienzi kwa dhati na kwa vitendo katika awamu hii ya tano.



“Serikali inatamani hata kujenga mabweni ya wanafunzi wote elfu tisa hapa SUA, lakini wapo tu watakaotoka na kukaa huko (nje ya chuo), unakuta mwingine labda ameoa au ameolewa, lakini nitajenga tu,” alisema Magufuli.

Hiki Ndicho Kilichosababisha Abiria wa Mwendokasi Kugoma na Kuandamana Kimara

0
0
Hiki Ndicho Kilichosababisha Abiria wa Mwendokasi  Kugoma na Kuandamana Kimara
Leo May 7, 2017 katika kituo cha mabasi ya mwendokasi cha Kimara Mwisho, abiria wa mabasi hayo wamefanya vurugu ikiwa ni pamoja na kuandamana kwenye njia ya mwendokasi.

Shuhuda aliyekuwa eneo hilo Alexander Wencelaus ameeleza kuwa magari yote yaliyokuwa yanapita kituoni hapo yalikuwa yamejaa kiasi cha kutoweza kuchukua abiria wengine kwenye kituo hicho.

Baada ya changamoto hiyo kudumu kwa saa kadhaa ndipo abiria walipoanza kupita kwenye njia ya mwendokasi kwa ‘kuandamana’ wakishinikiza magari yaongezwe ili kutatua changamoto hiyo.

Hata hivyo baada ya muda changamoto hiyo ilitatuliwa kwa magari ya ‘Express’ kuanza kuchukua abiria kituoni hapo na hatimaye shughuli nyingine katika eneo hilo kuendelea kama kawaida.

Rais Magufuli Atembelea Chuo cha SUA Morogoro.....Wanafunzi Wafunguka na Kueleza Kero Zao

0
0
Rais Magufuli Atembelea Chuo cha SUA Morogoro.....Wanafunzi Wafunguka na Kueleza Kero Zao
Wanafunzi wa Chuo cha Kilimo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) wametoa ya moyoni mbele ya Rais John Magufuli kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo chuoni hapo ikiwamo uhaba wa mabweni ya wanafunzi na fedha za mikopo.

Wametoa ya moyoni baada ya kiongozi huyo mkuu wa nchi kutoa nafasi kwa wanafunzi na watumishi wa chuo hicho kueleza mambo mbalimbali wanayokabiliana nayo baada ya kufanya ziara katika chuo hicho kilichopo mjini Morogoro.

Kabla ya Rais kutoa nafasi hiyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alieleza mafanikio na juhudi zinazoendelea kufanywa na wizara yake ikiwa ni pamoja na kufanikisha utoaji wa mikopo.

Hata hivyo, Emmanuel Gwalaje, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza kozi ya wanyama amesema wapo wanafunzi wa mwaka wa kwanza chuoni hapo hawajalipwa fedha katika muhula wa kwanza na wanaishi maisha magumu hadi sasa.

Mhadhiri wa chuo hicho, God Swai amesema wanafunzi wanaporwa mitaani na kukabwa kutokana na uhaba wa majengo ya bweni, huku akiomba kujengwa kwa ofisi za wahadhiri chuoni hapo.

Mbali na maombi ya wanafunzi, pia kulikuwa na maombi ya watumishi, huku Amina Juma akiomba Rais Magufuli kuwafikiria watumishi wa darasa la saba waliofukuzwa kazi.

Amesema yeye ni mtumishi chuoni hapo tangu mwaka 1994, aliyeathirika na kuondolewa kwa watumishi wa darasa la saba, akiomba wafikiliwe upya kutokana na hali ngumu ya maisha mtaani.

Siku Nikki wa Pili Akipewa Uwaziri Atafanya Jambo Hili

0
0
Siku Nikki wa Pili Akipewa Uwaziri Atafanya Jambo Hili
Msanii wa muziki wa hip hop Bongo, Nikki wa Pili amesema ili wasanii watambulike kama wafanyakazi ni lazima serikali itambue wasanii wanafaje kazi na iwapo wanataka kuilinda ijue inalinda kitu gani.

Amesema baada hapo kinaweza kuanzishwa chama cha wasanii wafanyakazi ambacho kinasimama na kutengeneza kanuni na taratibu za mfanyakazi huyo na kitu hicho kutafsiriwa kama sheria.

“Kubadilisha sanaa kuwa biashara hicho ni kitu kingine, so niwajibu wa msanii kujifunza misingi ya biashara, hiki nilichonacho mkononi ninawezaje kukiuza? . Ukinipa uwaziri kitu cha kwanza ni kufanya utafiti mkubwa wa biashara ya muziki,” amesema.

“Kujua hii biashara inafanyikaje, uhalisia wake ni upi na huo uhalisia wake umetengeneza picha gani, then kutoka hapo tunawezaje kwenda mbele, bila kutafiti kwa facts utapiga bla! bla!,” Nikki wa Pili amesema hayo katika mahojiano na JJ wa Jembe FM.

Nikki wa Pili kutoka kundi la Weusi kwa sasa anatamba na ngoma Hesabu ambayo amemshirikisha producer, S2kizzy.

TFF Yapangua Ratiba ya Ligi Kuu

0
0
TFF Yapangua Ratiba ya Ligi Kuu
Shirikisho la soka nchini kupitia kwa Bodi ya ligi (TPLB), limepangua mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara kati ya Mbao FC na Ndanda FC uliokuwa unatarajiwa kucheza Ijumaa ijayo.

Taarifa ya TFF leo, imeeleza kuwa mchezo huo umerudishwa nyuma kwa siku moja ambapo badala ya kuchezwa Ijumaa sasa utachezwa Alhamisi ya wiki hii sababu kubwa ikiwa ni uwanja kuwa na shughuli nyingine.

''Mchezo wa Ligi Kuu kati ya Mbao FC ya Mwanza na Ndanda FC ya Mtwara uliokua uchezwe Mei 11, 2018 umerudishwa nyuma utachezwa Mei 10, 2018 Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, kufuatia Uwanja huo kuwa na matumizi mengine ya kijamii'', imeeleza taarifa hiyo.

Mbao FC inashika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi kuu kwenye mechi 26 ilizocheza huku ikiendelea kuwa kwenye mstari wa kushuka daraja. Ndanda nayo ipo nafasi ya 15 ikiwa na alama 22 baada ya mechi 27.

Harmonize Afunguka Mazito Kuhusu Kuibiwa Sarah na Baunsa wa Diamond

0
0
Harmonize Afunguka Kuhusu Kuibiwa Sarah na Baunsa wa Diamond
Kwa habari za chini ya kapeti ni kwamba yule mzungu wa Harmonize (Konde boy) Sarah kwa sasa haambiwi wala hasikii kitu kuhusu mwarabu fighter yaani anampenda mpaka kapitiliza ,zile pesa alizokuwa ana muhonga Harmonize kwa sasa kwa kiasi kikubwa amezihamishia kwa mwarabu fighter na gharama za gym kwa kiasi kikubwa yeye ndiye anazisimamia.

Sarah amepunguza mapenzi kwa kiasi kikubwa na Harmonize kilichobaki anahangaikia tu penzi la mwarabu fighter ili aweze kutuliza roho yake.

Kitu ambacho mpaka sasa kinachofanya ugumu wa couple hiyo kusimama ni kutokana na Harmonize kuwa mtu wa karibu saana na Diamond Platnumz ambaye pia ndiye anayemuweka mjini mwarabu fighter na siku zote ukitaka kumkwaza Diamond au ukitaka kumkwaza Harmonize basi mtu amkwaze mmoja wapo yani Diamond wanapendana sana kama mtu na kaka yake.

Kwa hiyo mwarabu fighter anaogopa kibarua kuota nyasi kama akifanikiwa kumpindua Harmonize .

Rais JPM Awapa Onyo Kali Wanachuo wa SUA "Sitosita Kuwafukuza Wote''

0
0
Rais JPM Awapa Onyo Kali Wanachuo wa SUA "Sitosita Kuwafukuza Wote''
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amesema hatosita kufukuza wanafunzi wa chuo watakaobainika kufanya vurugu shuleni na kuacha kuzingatia masomo, na suala hilo sio vitisho bali ni ukweli mtupu.


Rais Magufuli ameyasema hayo leo alipokuwa kwenye ziara yake Chuo Kikuu cha Kilimo cha SOkoine (SUA) mkoani Morogoro, na kuwataka wanafunzi wote vyuoni kuzingatia masomo yao, na sio kujihusisha na vurugu hasa za kisiasa, kwani akigundua hilo atafukuza wote hata kama ni chuo kizima, na iwapo atafanya hivyo, hajui kama atawarudisha tena chuoni.

"Niwaombe ndugu zangu, mmekuja hapa kwa ajili ya shule, msipoteze muda wenu kwenye masuala yasiyo na tija, tumieni muda wenu kwenye masuala ya shule, msigeuze vyuo kuwa sehemu za siasa, siasa mtazikuta tu, pigeni shule msiingie kwenye mikumbo, kila moja ana maisha yake na baba yake na mama yake, someni, pasua, kazingatieni hilo, nataka niwaeleze kiukweli, kama kutatokea chuo chochote kinafanya fujo, mimi wala sitasita kufukuza, na nikifukuza sifahamu ntawarudisha lini, hili siwatishi nawaeleza ukweli", amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameendelea kwa kusema kwamba serikali kupitia wizara ya elimu itahakikisha inkilinda chuo cha Sokoine kama mboni ya jicho, kutokana na upekee ulionacho chuo hiko.

Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images