Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu

 Bonyeza Hapa Chini Kuinstall Upya:


==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>  

“Serikali Mnatufikisha Mahali Pagumu Sana Kwa Mambo Madogo ”-Spika Ndugai

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai ameieleza Serikali kwamba inaenda kulifikisha taifa mahali pagumu sana kwa kushindwa kumaliza tatizo la ongezeko la bei ya mafuta ya kula nchini na wakati huo amemuagiza Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage kuja na majibu ya tatizo hilo Bungeni haraka iwezekanavyo.

Kauli hiyo ya Spika imekuja baada ya Mbunge wa Nzega mjini Hussein Bashe aliyetaka kupata majibu ya Serikali kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta hayo ambapo Waziri Charles Mwijage  alimjibu kwamba jambo hilo linashugulikiwa ingawa kwa sasa kuna mvutano umeibuka baada ya meli mbili zenye mafuta kuzuiwa bandarini. VIDEO:

Toka Nijue Mapenzi Sijawahi Kuiba Mume wa Mtu- Thea

$
0
0
Toka Nijue Mapenzi Sijawahi Kuiba Mume wa Mtu- Thea
WAKATI mastaa wengi wa kike Bongo wakizungukana na kuchukuliana mabwana, mkongwe wa maigizo Bongo, Salome Urassa ‘Thea’ amevunja ukimya kuwa, tangu ajue mapenzi ni kitu gani, hajawahi kuiba mwanaume wa mwanamke mwenzake.



Akizungumza na Za Motomoto News, Thea alifunguka kuwa, suala la kuibiana mabwana halipo kwa wasanii tu, bali ni kwa jamii nzima, lakini kwa upande wake hajawahi  kumzunguka mtu kwa kuwa hiyo ni tabia ya mtu na kwake haipo.



“Kiukweli tangu niyajue mapenzi, sijawahi kuiba bwana wa mtu kwa sababu siyo tabia yangu na siwezi kufanya hivyo, wanaochukua mabwana za watu ni tabia zao ambazo huwezi kuzibadilisha na hii haipo kwa wasanii tu, bali ni kwa jamii kwa jumla kwani tumekuwa tukisikia sana ila kwa wasanii wanaonekana zaidi kutokana na majina waliyonayo,” alisema Thea.

Shahidi: Gari ya Lucky Vicent Haikuwa na Kibali cha Kusafirisha Wanafunzi 32

$
0
0
Shahidi: Gari ya Lucky Vicent Haikuwa na Kibali cha Kusafirisha Wanafunzi 32
Shahidi wa nne upande wa mashtaka katika kesi inayomkabili Mmiliki wa Shule ya Lucky Vicent, Innocent Mushi pamoja na Makamu Mkuu wa shule hiyo, Longino Nkana ameeleza kuwa gari lililotumika kusafirisha wanafunzi halikuwa na kibali cha kusafirisha wanafunzi hao.

Shahidi huyo, Allen Mwanri ambaye ni Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Usafirishaji wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) ameieleza mahakama hiyo kwamba gari hilo lilipewa leseni ya kusafirisha abiria kutoka wilayani Arusha kuelekea Mirerani mnamo Mei 16,  2016 na iliisha Mei 15, 2017.

Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Arusha, Desdery Kamugisha, shahidi huyo ameieleza mahakama kwamba kwa mujibu wa kumbukumbu za ofisi gari hiyo yenye nambari T871 BYS aina ya Mitsubishi Rosa inamilikiwa na Swalehe Kiluvia.

Shahidi huyo ameeleza kwamba ofisi yake haijawahi kupokea maombi yoyote ya kubadilisha matumizi ya gari hilo tangu leseni iishe muda wake na uhalali wa leseni iliyotolewa ilikuwa ni kusafirisha abiria kutoka wilayani Arusha kuelekea Mirerani.

Shahidi huyo ameeleza kuwa kanuni hizo zimeyataja magari ya abiria lakini sio magari ya kubeba wanafunzi kwa kuwa kanuni za kubeba wanafunzi zimetajwa katika kanuni za SUMATRA za mwaka 2007.

Hakimu Kamugisha ameahirisha kesi hiyo hadi ambapo shahidi mwingine upande wa mashtaka atafika mahakamani hapo kuwasilisha utetezi wake.

Baadhi ya wazazi wa wanafunzi waliofariki katika ajali hiyo walifurika nje na ndani ya mahakama hiyo kwa mara ya kwanza kusikiliza kesi hiyo ambayo imeibua hisia kwa baadhi ya wakazi wa jiji la Arusha.

Rais Trump Ajitoa Katika Mkataba wa Nyuklia wa Iran

$
0
0
Rais Trump Ajitoa Katika Mkataba wa Nyuklia wa Iran
Rais Donald Trump ametangaza kujitoa katika mkataba wa kimataifa wa Nyuklia wa Iran. Ameuita mpango huo kuwa umeoza na ni kero kwa raia wote wa Marekani.

Amesema mpango huo hauwezi kuleta amani hata kama Iran ikikubaliana na kila kitu kama sehemu ya utekelezaji wa mpango huo uliosainiwa mwaka 2015 chini ya utawala wa aliyekuwa rais taifa hilo Barack Obama.

Rais wa Iran amekosoa hatua ya Marekani kujitoa na kudai kuwa haiheshimu makubaliano yake. Akienda kinyume na mataifa ya Ulaya yaliyofikia makubaliano hayo,Trump amesema kuwa watarejhesha vikwazo vya kiuchumi vilivyoondolewa dhidi ya Iran kupitia makubaliano hayo ya mwaka 2015.

Israel na Saudi Arabia kwa pamoja wamepongeza.Viwazo vya vinatarajiwa kuanza dhidi ya Iran ndani miezi mitatu hadi mitatu.

Trump awali alilalamikia mkataba huo kwamba ulikuwa unaiwekea Iran vikwazo kwa muda tu na kwamba ilishindwa kusitisha mpango wake wa makombora na kwamba Iran ilipewa kiasi cha dola bilioni 100 kwaajili ya kutokomeza silaha na ugaidi huko mashariki mwa kati.

Baby J Afunguka Kilichomfanya Kuwa Kimya Kwenye Game

$
0
0
Baby J Afunguka Kilichomfanya Kuwa Kimya Kwenye Game
WASWAHILI tuna msemo unasema, kila zama na mvua zake si, ndiyo? Sasa zama fulani hivi za nyuma, mwishoni kwa miaka ya 2000, mwanadada kutoka Zanzibar, anayejulikana zaidi kwa jina la Baby J alikuwa ni miongoni mwa mvua kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva.

Wengi watakumbuka ngoma zake nzuri za kuimbika na zenye maudhui ya mahaba. Zaidi zinaweza kuwa zinawakumbusha baadhi ya watu wakati ‘zinahiti’ walikuwa wanaziimba na kina nani!

Ngoja nikukumbushe chache. Unakumbuka ngoma ya Bwashee Bwashee ambayo mwanadada huyu aliimba na Ali Kiba? Vipi kuhusu Moyo Wangu alioimba na Pasha? Mpenzi Wangu je alioimba na Banana Zorro unaukumbuka? Huu hata mimi ninaupenda zaidi!

Ukweli ni kwamba mwanadada huyu aliuteka muziki na alikuwa anafanya vizuri kwa nyimbo tamu. Lakini kwa sasa hatumsikii tena, kiufupi kapotea na bila shaka wengi wangependa kufahamu ni wapi alipo na anafanya nini? Si ndiyo?

Haya huyu hapa Risasi limekuletea.

Risasi: Baby J mambo vipi, umepotelea wapi?

Baby J: Mbona nipo jamani.

Risasi: Tunafahamu upo lakini kimuziki hatukusikii kabisa.

Baby J: Ni kweli nilikuwa nimepotea kidogo kutokana na mambo ya maisha ya hapa na pale lakini hivi karibuni narudi maana nimefanya kazi na MwanaFA, ninatarajia kuiachia baada ya mfungo unaokwenda kuanza ‘soon.’






Risasi: Kabla ya kuzungumzia ujio wako huo mpya, hebu tuzungumzie kilichokupoteza ni nini hasa, hayo mambo ya maisha ndiyo yapi?

Baby J: Ni mambo ya maisha tu ambayo sidhani kama naweza kuweka wazi, lakini inaweza kumtokea mtu yeyote yule akarudi nyuma, si unajua tena maisha.

Risasi: Au uliolewa?

Baby J: Hahahaa (anacheka), hapana. Sijaolewa jamani, ni mambo tu ya maisha ya hapa na pale, niseme tu changamoto za kimuziki na maisha mengine ya nje ya muziki.

Risasi: Kwa hiyo kwa sasa vyote hivyo vimekwisha ndiyo maana unarudi kwenye gemu upya?

Baby J: Yah! Kwa kiasi kikubwa baadhi ya mambo nimeshayaweka sawa na ndiyo maana nimeamua kurudi.

Risasi: Kwani huko Zanzibar zaidi unajishughulisha na nini hasa mbali na muziki?

Baby J: Kwanza huku ni nyumbani. Lakini pia kuna biashara zangu ambazo nashughulika nazo na mambo mengine ya kimaisha.

Risasi: Biashara gani hizo unafanya?

Baby J: Hahahaaa (anacheka tena), za kawaida tu. Si unajua maisha ni kupambana.

Risasi: Unaonekana wewe ni msiri sana, haya bwana. Lakini nini unamisi kwenye ‘mainstream’?

Baby J: Kiukweli ile kutrend kwenye media mara kwa mara lakini pia kampani kutoka kwa wasanii wenzangu. Unajua kampani ya wasanii si kama ya watu wa kawaida. Kuna vingi mnakuwa mnashare.

Risasi: Hummis mpenzi wako ambaye kwa sasa ni mwanamuziki mkubwa?

Baby J: Hahahaaa (anacheka), nani huyo?

Risasi: Kwani hujawahi kutoka na staa?

Baby J: Niliwahi kutoka naye lakini wengi hawamfahamu na siwezi kumuweka wazi.

Risasi: Kwa nini?

Baby J: Aaaa nikimtaja kwa sasa itakuwa balaa.

Risasi: Au ni huyu aliyeoa hivi karibuni na hutaki kuvunja ndoa yake?

Baby J: Hahahaaa (anacheka), kiukweli sifahamu na sihitaji kulizungumzia hili zaidi.

Risasi: Haya basi zungumzia ujio wako zaidi, kwa nini umeamua kurudi na MwanaFA?

Baby J: Kwa sababu ni mwanamuziki mzuri na wimbo ulikuwa unamhitaji yeye. Lakini jambo lingine ni kwamba nimekaa kimya muda mrefu kwa hiyo kwa kurudi na MwanaFA ambaye ni mwanamuziki mwenye heshima na ana mashabiki wengi kwangu nahisi ni jambo zuri.

Risasi: Asante sana Baby J, bila shaka mashabiki wako angalau wamefahamu upo wapi kwa sasa.

Baby J: Asante sana na kwa mashabiki wangu, kiukweli nawapenda na tupo pamoja.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo..

anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.


Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto.

Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Piga simu +255 622588038 au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Sababu 5 Kwanini Wanawake Wenye Akili Nyingi Hupata Tabu ya Kupata Mapenzi ya Kweli

$
0
0
Akili nyingi ni zawadi na laana. Wanapojiangalia kwenye kioo, wanawake wenye akili nyingi huona picha ya mtu mwenye nguvu mwenye malengo, anayejua anachotaka. Kuwa na akili nyingi ni kitu muhimu kuwa nacho, lakini wakati mwingine kinaweza kuwatisha wengine.

Pengine ndio maana watu wenye akili nyingi hupata shida ya kupata pendo. Kama unajiuliza kwanini bado upo single, hizi ni sababu tano kwanini unaweza ukawa unapata shida kupendwa.

1. Unakuwa mchambuzi mno

Wasichana wenye akili mara nyingi huchambua sana vitu. Huwa na shaka na kesho yao, njia nzuri za kuimarisha mahaba, na wanataka sana kumpata mtu sahihi. Hiki hata hivyo sio kitu kibaya.

2. Unajua ni bora kuwa peke yako kuliko kuwa na mwenza asiye sahihi

Na hakuna tatizo katika hilo pia. Watu wenye akili wako makini katika kumpata mwenza sahihi ambapo wanaweza kuamua kubaki wenyewe kama asipopatikana.

3. Unajua kuwa mahusiano mara nyingi hufa

Hawa hujua ukweli unaouma kuwa mahusiano mengi hayafiki popote. Matokeo yake, wakati mwingine hufanya mambo pole pole na kuwa na shida katika kuingia miguu miwili. Lakini mwenza sahihi ataelewa hilo.

4. Unaweza kuwa unaogopesha

Sio kwamba watu wenye akili huwatisha mambumbu lakini hata wenye akili pia. Wanaweza wasiwe comfortable na ukweli kuwa unafanya vizuri katika eneo la maisha ambayo hawapo.

5. Unajua kujilinda mwenyewe

Watu wenye akili katika dunia hii wanaelewa sana hatari katika hali yoyote na hiyo inahusisha pia dating. Huwa makini, waangalifu na huweka vikwazo kujilinda wenyewe.


Chanzo: Life Box Today


Imethibitisha visa vipya vya Ebora Vimeibuka DR Congo

$
0
0
 Imethibitisha visa vipya vya Ebora Vimeibuka DR Congo
Kumetangazwa visa vipya vya ugonjwa wa Ebola kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Kuna visa viwili vilivyothibitishwa na watu 17 waliofariki, wizara ya afya imesema.

Wataalam wa maradhi ya Ebola kutoka wizara ya afya nchini Congo leo Jumatano wanatarajiwa kuambatana na wale wa shirika la afya duniani WHO kwenda jimboni Equateur baada ya kuthibitishwa kuwepo kwa visa hivyo.

Kisa kilichotokea katika mji wa Bikoro kinajiri zaidi ya mwaka baada ya mlipuko wa ugonjwa huo kusababisha vifo vya watu wanne nchini humo.

Tangazo la kuzuka kwa visa hivyo vipya limetolewa baada ya matokeo ya uchunguzi wa maabara kuthibitisha visa viwili vya Ebola kati ya sampuli za wagonjwa watano waliokuwa wanahsukiwa, Shirika la afya duniani (WHO) limesema.

"Leng letu kuu ni kuushirikisha mji wa Bikoro na serikali,"Msemaji wa WHO Peter Salam alisema katika taarifa yake.

"Kushirikiana na washirika na kukabiliana na visa mapema katika namna iliyoratibiwaitakuwa ni muhimu katika kuudhibiti ugonjwa huuu hatari."


Hii ni mara ya tisa kunazuka ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Virusi vya ugonjwa huo viligunduliwa kwa mara ya kwanza katika nchi hiyo iliyokuwa ikijulikana kama Zaire, mnamo 1976 na jina lake linatokana na mto Ebola.

Inadhaniwa kwamba Ebola husambazwa katika maeneo ya mbali kupitia popo na husambazwa miongoni mwa binaadamu kutokana na kula nyama za mwituni.

Polisi Mkoani Iringa Yatekeleza Agizo la Rais Yamkamata Mkandasi

$
0
0
Polisi Mkoani Iringa Yatekeleza Agizo la Rais Yamkamata Mkandasi
Wiki moja baada ya Rais John Magufuli kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi wa thamani ya fedha iliyotumika kujenga ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu cha Elimu cha Mkwawa (Muce), polisi mkoani hapa imemkamata mkandarasi wa ujenzi huo.

Mei 2, akizungumza na wafanyakazi na wanafunzi wa Muce mjini Iringa, Rais Magufuli aliagiza vyombo hivyo ikiwamo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kufuatilia ujenzi huo uliogharimu Sh8 bilioni.

Sambamba na agizo hilo, pia aliagiza aliyekuwa mkuu wa chuo hicho, Profesa Phillemon Mushi kuhojiwa na mkandarasi kukamatwa.

Akizungumza na wanahabari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire alisema wanamshikilia mkurugenzi mtendaji wa kampuni iliyojenga mradi huo ya MNM Engineering Service, Godwin Mshana (62) akituhumiwa kujenga ukumbi huo chini ya kiwango. Bwire alisema mkandarasi huyo amekamatwa kutokana na agizo la Rais.

“Mei 3 tulimkamata mtuhumiwa na kumuweka chini ya ulinzi,” alisema Kamanda Bwire.

Aliongeza kuwa wameunda kikosi kazi kinachowahusisha wao na Takukuru kwa ajili ya kufanya uchunguzi na utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Kamanda Bwire alisema msako unaoendelea hivi sasa unawalenga waliohusika na mradi huo wakiwamo waliotoa zabuni.

Akizungumzia suala hilo, Kamanda wa Takukuru mkoani Iringa, Aidan Ndomba alisema, “Kama vyombo vya sheria tumeshirikiana kufanya msako na kuhakikisha tunamkamata mkandarasi baada ya kufuatilia kwa kina juu ya ujenzi huo.”

Alisema Takukuru imefanya kazi kubaini thamani iliyotajwa ambayo alieleza ni kubwa ikilinganishwa na ubora wa jengo.

Ndomba alisema kwa sasa hawawezi kusema ni watu wangapi wanahusika kwa sababu uchunguzi unaendelea.

“Kwa hiyo tutaweza kuona ni uchunguzi unaohusisha watu wengi na fedha nyingi, hivyo baada ya uchunguzi tutaweza kujua ni mtu yupi anahusika na upotevu wa fedha,” alisema.

Okwi Amwagia Sifa Amisi Tambwe

$
0
0
Okwi Amwagia Sifa Amisi Tambwe
WAKATI kikosi cha Simba kikikaribia kutangaza ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu, mshambuliaji wa timu hiyo, Mganda, Emmanuel Okwi ametoa kauli ya kummwagia sifa mshambuliaji wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe.



Okwi ambaye anaongoza msimu huu katika michuano ya Ligi Kuu Bara kwa kuzifumania nyavu akiwa na mabao 20, amemmwagia sifa Tambwe kutokana na kazi kubwa aliyoifanyia Yanga msimu wa 2015/16.



Katika msimu huo, Tambwe alifanikiwa kuifungia timu yake hiyo ya Yanga mabao 21, huku pia akifanikiwa kuwa mfungaji bora.



Akizungumza na Championi Jumatano, Okwi alisema kuwa amefikia hatua hiyo ya kumpongeza Tambwe kutokana na kuitambua kazi kubwa aliyoifanyia Yanga msimu huo lakini pia heshima ambayo alitoa hivi karibuni dhidi yake baada ya kufanikiwa kuzivunja baadhi ya rekodi zake za kuzifumania nyavu pamoja na za wachezaji wengine.



“Siku zote unapofanikiwa kufunga unakuwa umeisaidia timu yako kufanya vizuri, lakini pia unapofanikiwa kuvunja rekodi za waliokutangulia ni jambo zuri.



“Namshukuru sana Tambwe kwa heshima ambayo amenipatia baada ya kuvunja baadhi ya rekodi zake, lakini pia na mimi napongeza sana kwa kazi kubwa aliyoifanyia Yanga msimu wa 2015/16.



“Kuhusiana na kuivunja rekodi yake hiyo ya mabao 21 hakika anayejua hilo ni Mungu kwani lolote linaweza kutokea katika mechi hizi zilizobakia ila jambo kubwa ambalo naweza kusema ni kwamba nitaendelea kupambana kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu ili kuhakikisha tunapata matokeo mazuri katika mechi zetu zilizobakia.

“Ikitokea nikaivunja rekodi hiyo basi nitamshukuru Mungu pia,” alisema Okwi

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Mataifa ya Magharibi Kunusuru Makubaliano ya Nyuklia Iran

$
0
0
Mataifa ya Magharibi Kunusuru Makubaliano ya Nyuklia Iran
Viongozi wa mataifa ya magharibi wanasema kuwa wataendelea kuuunga mkono makubaliano ya kinyuklia ya Iran muda mfupi baada ya Marekani kutangaza kuwa inajiondoa katika makubaliano hayo.

Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zinasema kuwa watafanya kazi pamoja na matiafa yote yaliosalia katika mkataba huo huku ikiitaka Marekani kutovuruga utekelezwaji wake.

Mataifa mengine yalioweka mkataba huo wa 2015- Urusi na China pia yamesema yataendelea kuunga mkono makubaliano hayo.


Ridhiwani Kikwete Ahusishwa Kugombea Nafasi ya Manji Yanga Mwenyewe Afunguka Haya

$
0
0
Ridhiwani Kikwete Ahusishwa Kugombea Nafasi ya Manji Yanga Mwenyewe Afunguka Haya
Shabiki wa Yanga, Ridhiwani Kikwete, amehusishwa kugombea nafasi ya uongozi wa Uenyekiti ndani ya klabu hiyo ambao umeagizwa kufanyika na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Baada ya taarifa hizo kuenea, Ridhiwani amesema kuwa yeye hana mpango wa kuchukua nafasi hiyo kutokana na majukumu mengine ya kiserikali yanayomkabili.

Akizungumza na radio EFM asubuhi hii, Ridhiwani ameeleza kuwa yeye si Mwanachama wa Yanga hivyo anakosa kigezo hicho cha kuwania nafasi hiyo ya juu katika uongozi ndani ya klabu hiyo.

Mbali na majukumu ya kiserikali, Ridhiwani ameeleza pia kuwa aliwahi kusemwa na mmoja wa kiongozi wa Yanga miaka kadhaa nyuma akielezwa kuwa hana mamlaka ya kuzungumza chochote kuhusiana na klabu hiyo.

Kitendo cha kuambiwa kuwa hana mamlaka ya kuongea chochote, huku akitajwa kuwa hajalipia kadi ya uanachama ndani ya Yanga, kinamfanya asipate nguvu ya kugombea nafasi hiyo.

Kiongozi huyo amesema ni wanachama na mashabiki ndiyo wamekuwa wakipendekeza agombee na si yeye kuwa amehitaji kufanya hivyo.

Diamond Aingia Location na Miri Ben-Ari UK Kutengeneza Video ya Baila

$
0
0
Diamond Aingia Location na Miri Ben-Ari UK Kutengeneza Video ya Baila
Safari ya Diamond nchini Uingereza haijakuwa kwaajili ya kufanya show bali ameitumia kuteneneza video ya wimbo wake wa Baila ambapo mrembo Miri Ben-Ari amesikika akilicharaza vizuri Violini.

Diamond ameonekana kwenye baadhi ya picha na video akiwa location nchini humo akitengeneza video hiyo ambapo inaweza ikawa ndio kichupa kinachofuata baada ya African Beauty.

Lakini kubwa zaidi Miri Ben-Ari na yeye ameonekana location baada ya kusafiri kutoka mjini New York, Marekani mpaka London ambapo inadaiwa ndio video hiyo inatengenezwa.




Uganda Yapinga Ofisi za Umoja wa Mataifa Kuhamishwa Nairobi Kutoka Entebbe

$
0
0
Uganda Yapinga Ofisi za Umoja wa Mataifa Kuhamishwa Nairobi Kutoka Entebbe
Bunge la Uganda limepinga mpango wa Umoja wa mataifa wa kuondowa kituo chake cha kikanda Entebbe kukipeleka mjini Nairobi Kenya.

Spika wa bunge Bi Rebecca Kadaga ameteuwa kamati ya bunge ya maswala ya mambo ya nchi za nje pamoja na mbunge Theodore Sssekikubo kulifuatilia swala hilo.

Tayari inaaripotiwa kuwa Rais Yoweri Museveni amemuandikia katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres barua kuelezea kutoridhia na kupinga pendekezo hilo la kuondolewa kwa kituo hicho.

Zaidi ya wafanyakazi 420 wakiwemo 134 kutoka nje ya nchi na raia wa Uganda 285 na wafanyakazi wanane wa Umoja wa mataifa wa kujitolea watakosa kazi kama kituo hicho mjini Entebbe kitaondolewa na kupelekwa mjini Nairobi Kenya mwezi ujao.

Steve Nyerere Ajibu Tuhuma ya Michango ya Masogange "Michango Haipewi Familia"

$
0
0
Steve Nyerere Ajibu Tuhuma ya Michango ya Masogange "Michango Haipewi Familia"
Msanii wa filamu bongo ambaye pia ni mchekeshaji maarufu Steve Nyerere, amefunguka juu ya tuhuma za kutofikisha fedha za michango zilizobaki kwenye msiba wa Agness Masogange, na kusema kuwa pesa hizo haziwezi kupewa familia.


Akizungumza na www.eatv.tv Steve Nyerere amesema kwamba pesa hizo ambazo zimetajwa kuwa milioni mbili zimekusudiwa kumsaidia mtoto wa marehemu Sania, atakapoanza kidato cha kwanza hapo mwakani,

Steve Nyerere ameendelea kwa kusema kwamba familia ya Agness inapaswa kushukuru kwa mchango wao walioutoa kumzika ndugu yao, na sio kuanza kuulizia masuala ya pesa, kwani pesa hizo si kwa ajili yao bali ni kwa ajili ya mtoto.

Harmorapa Afunguka Sababu ya Kutohudhuria Harusi ya Alikiba "Nilialikwa Ila Nilikua Afrika Kusini"

$
0
0
Harmorapa Afunguka Sababu ya Kutohudhuria Harusi ya Alikiba "Nilialikwa Ila Nilikua Afrika Kusini"
Baada ya ukimya mrefu msanii Harmorapa ameibuka na kueleza sababu ya kilichopelekea kupotea ghafla.

Harmorapa amesema kwa kipindi kirefu alikuwa nje ya Dar es Salaam kwa kuandaa kazi zake mpya ambazo alikuwa akizifanyia nchini Afrika Kusini.

Pia Harmorapa amedai kuwa yeye ni miongoni mwa wasanii waliohalikwa katika harusi ya msanii Alikiba ila alishindwa kuhudhuria kutokana na safari yake hiyo.

“Uongo dhambi, kualikwa nilialikwa sema nilikuwa sipo Dar es Salaam, kwa hiyo ile kuwa mbali ilisababisha kutohudhuria kwenye harusi, nilikuwa bize nasafiri sana,” Harmorapa ameiambia TV E.

Katika hatua nyingine amedai kuwa nia yake ya kumuoa Wema Sepetu ipo pale pale kwani ni kitu ambacho anaamini kipo ndani ya uwezo wake, huku akieleza kama Dogo Janja ameweza kumuoa Irene Uwoya haoni sababu ya yeye kushindwa.

Mlinda Mlango wa Azam Anyakua Tuzo ya Mchezaji Bora

$
0
0
Mlinda Mlango wa Azam Anyakua Tuzo ya Mchezaji Bora
Mlinda mlango wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Mwadini Ally amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa timu hiyo mwezi Machi baada ya kupata kura nyingi zaidi alizopigiwa na mashabiki wa timu hiyo.


Mwadini ametwaa tuzo hiyo baada ya kuwa na kiwango kizuri mwezi huo akicheza jumla ya mechi nne sawa na dakika 360 huku akiruhusu wavu wake kutikiswa mara moja tu.

Kipa huyo amevuna asilimia 52 za kura 1,000 zilizopigwa na mashabiki wa soka kupitia ukurasa maalum wa kijamii wa Azam FC, kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’ amevuna asilimia 25 huku Frank Domayo ‘Chumvi’ naye akivuna asilimia 23 ya kura hizo.



Yanga Yaogopa Kuvunja Mikataba na Wachezaji Wake Kuhofia Hasara

$
0
0
Yanga Yaogopa Kuvunja Mikataba na Wachezaji Wake Kuhofia Hasara
Baada ya wachezaji baadhi wa Yanga kutoonekana dimbani kwa muda mrefu, uongozi wa Yanga umesema unahofia kuvunja nao mikataba kwa hofu ya kupata hasara.


Donald Ngoma na Amis Tambwe ni miongoni mwa wachezaji walioshindwa kuichezea timu hiyo kwa muda mrefu kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

Katibu Mkuu wa Yanga, Boniface Mkwasa, amesema kuwa wana hofu ya kuvunja nao mikataba kwasababu itawalazimu kuwalipa fedha za uvunjaji.

Kauli ya Mkwasa imekuja kutokana na klabu hiyo kutokuwa vizuri kiuchumi kwa sasa tangu Mwenyekiti wao Yusuph Manji kutangaza kujiuzulu nafasi yake.

Kutokuwepo kwa wachezaji hao kumechangia kikosi hicho kushindwa kupata matokeo yasiyo mazuri kwenye ligi msimu huu kwani huduma yao ina muhimu mkubwa ndani ya timu.

Viewing all 104667 articles
Browse latest View live




Latest Images