Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0

TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30. 

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri 

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788 

DR MAGISE

Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi Cha Jangwani Kuhamishiwa Stand ya Basi Ubungo

$
0
0

DAR: Halmashauri ya Jiji na Menejimenti ya Kampuni ya UDART zinafanya majadiliano ya kukihamisha kituo cha Mabasi ya Mwendokasi(UDART) kutoka Jangwani na kukipeleka katika kituo cha Mabasi ya Mikoani Ubungo(UBT)

Meya wa Jiji la Dar, Isaya Mwita, amesema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari ya Mwendokasi yasiendelee kuharibika katika kituo cha sasa cha Jangwani kutokana na kukubwa na mafuriko

Aidha, Halmashauri ya Jiji ipo kwenye mchakato wa kupanua Mto Msimbazi uweze kuwa na nafasi kubwa ya kusafirisha maji hadi baharini

Meya Mwita aliongeza kuwa Serikali Kuu imetoa Tsh. Bilioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi yaendayo mikoani, kitakachojengwa Mbezi Mwisho

Kituo cha Umoja wa Mataifa Kuhamishiwa Kenya Kutoka Uganda....Yoweri Museven Agoma

$
0
0

UGANDA: Bunge la nchi hiyo limepinga mpango wa Umoja wa Mataifa wa kuondoa kituo chake cha Kikanda kilichopo Entebbe na kukipeleka mjini Nairobi, Kenya
-
Spika wa bunge Bi. Rebecca Kadaga ameteuwa kamati ya bunge ya maswala ya mambo ya nchi za nje ikiongozwa na mbunge Theodore Sssekikubo kulifuatilia swala hilo
-
Aidha, Rais Yoweri Museveni amemuandikia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres barua kuelezea kutoridhia na kupinga pendekezo hilo la kuondolewa kwa kituo hicho
-
Nairobi ndiyo mji uliopendekezwa kuwa makao ya kituo kipya cha Umoja wa Mataifa Afrika katika ripoti ya Kamati ya Ushauri wa Utawala na Maswala ya Bajeti(ACABO). Mji wa Budapest nchini Hungary umependekezwa kwa ajili ya kituo cha Ulaya

Amber Lulu Apata Dili la Kutangaza Bidhaa za Kondomu.

$
0
0
Amber Lulu Apata Dili la Kutangaza Bidhaa za Kondomu.
Msanii wa muziki Bongo na video vixen, Amber Lulu amepata dili la kutangaza bidhaa za kondomu.

Muimbaji huyo wa ngoma ‘Jini Kisirani’ alisaini dili hilo hapo jana na kueleza kuwa linampatia fedha za kutosha.

“Nimepata mpunga mrefu nimshukuru Mungu, ni hatua moja ambayo nimepiga, so inabidi tushukuru Mungu wote,” amesema Amber Lulu.

Utakumbuka siku za nyuma kulikuwa na taarifa za ujio wa bidhaa za kondomu kutoka kwa rapper Joh Makini hata hivyo kumekuwa na ukimya wingi wa hilo.

Bilali Mashauzi Kuzikwa Leo Upanga, Dar

$
0
0
Bilali Mashauzi Kuzikwa Leo Upanga, Dar
MWIMBAJI wa muziki wa taarab wa kundi la  Mashauzi Classic, Bilal Mashauzi, amefariki  jana na atazikwa leo Upanga jijini Dar es Salaam.

Familia yao imeishi kwa miaka mingi, Upanga mtaa wa Wibu  hadi  na baadaye waliposhindwana na mwenye nyumba miezi ya karibuni na wakahamia Mwananyamala ambapo yeye ndiye alikuwa kichwa cha familia.

Bilal Mashauzi enzi za uhai wake alikumbwa na kashfa ya kujihusisha na vitendo vya ushoga.

Wakati Isha Mashauzi anaanzisha Mashauzi Classic alimuomba Bilal hilo jina la Mashauzi na marehemu akaridhia ndipo kundi hilo lilipotambulishwa kwa jina la Mashauzi Classic.

Bilal amezaliwa na kukulia mitaa ya Togo, Kinondoni na Wibu, Upanga.

Madaktari Kumuua Mwanasayansi Mwenye Miaka 140 Kesho kwa Sindano ya Sumu

$
0
0
Madaktari Kumuua Mwanasayansi Kesho kwa Sindano ya Sumu
Mwanasayansi aliyesafiri kutoka Australia mpaka Uswiss David Goodall,  kwa ajili ya kuukatisha uhai wake kesho inatarajiwa kuwa ndiyo siku ya kuhitimisha maisha yake ya duniani baada ya madaktari kuchomeka sindano ya sumu katika mshipa.


Kesho, madaktari wanatarajiwa kuweka sindano iliyojazwa dawa ya sodium pentobarbital katika mshipa wa Mwanasayansi huyo mkongwe duniani na kumuacha aisukume mwenyewe kwenda mwilini mwake.

Goodall amelazimika kusafiri kutoka Australia mpaka Basel, Uswisi kukifuata kifo baada ya sheria za kwao kutomruhusu kufanya hivyo.

Akihojiwa na shirika la utangazaji la Marekani CNN, Goodall amesema maisha yake hayana thamani tena ndio maana ameamua kuomba kujiua akiamini hadithi yake itakuwa mfano na kuhamasisha uamuzi kama huo kwa wengine waliochoka kuishi.

Katika mahojiano Goodall amenukuliwa akisema "Natamani ningekuwa na uwezo wa kutembea mashambani na kuona vitu vinavyonizunguka. "Katika umri huu naamka asubuhi, nakunywa chai. Nasubiri mchana nile halafu sina cha kufanya tena. Maisha ya aina hii ya kazi gani?

Goodall aliyezaliwa katika Jiji la London Aprili 1914, anatarajia kufa akiwa na miaka 104 ambapo ameweka wazi kuwa maisha yake yalisimama miaka 10 iliyopita baada ya kupoteza uoni na uwezo wa kutembea na alitamani kama kifo kingemchukua katika miaka hiyo.

Ommy Dimpozi Amuumbua Shabiki Aliyemwambia Hajui Kuimba

$
0
0
Ommy Dimpozi Amuumbua Shabiki Aliyemwambia Hajui Kuimba
Siku ya May 1,2018 staa wa Bongo Fleva Ommy Dimpoz aliachia ngoma yake ya “Yanje” aliyomshirikisha Seyi Shay kutokea Nigeria na baadhi ya mashabiki walikuwa wakitoa mrejesho kuhusiana na ngoma hiyo ya Yanje.

Kupitia instagram account ya Ommy Dimpoz ameonekana kumjibu shabiki ambaye hajaikubali ngoma hiyo kuwa ni hit na inapendwa na watu wengi kutokana tu na feedbacks za watu ambao wengine wameonekana kuikubali ngoma hiyo na wengine kuikataa.

Shabiki alicomment kwa kuandika “Bola uludi Kigoma tu, hujuhi kuimba” baada ya comment hiyo Ommy Dimpoz akamjibu kwa kuandika “bora mimi sijui kuimba kuliko wewe usiejua Kiswahili BOLA(BORA) ULUDI(URUDI) HUJUHI(HUJUI)”

Mchungaji Msigwa, Dk. Tulia Wapimana Nguvu Bungeni

$
0
0
Mchungaji Msigwa, Dk. Tulia Wapimana Nguvu Bungeni
Mvutano umeibuka bungeni kati ya mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson.

Mvutano huo umeibuka leo Mei 9, 2018 baada ya Mchungaji Msigwa kutakiwa kufuta maneno aliyoyazungumza kuhusu utendaji wa Rais John Magufuli  katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji mwaka 2018/19.

Mbunge huyo alianza kuzungumzia kero za maji majimboni, kueleza jinsi wabunge wengi wanavyolalamikia jambo hilo na kubainisha kuwa kama ni suala la uwajibikaji wa Serikali, inapaswa kuundwa tume.

Huku akitolea mfano kukosekana kwa maji ni sawa na wananchi kula uchafu, wakiwemo watalii na huenda wote wakapata ugonjwa wa kipindupindu, Mchungaji Msigwa aliingia katika mvutano huo baada ya kudai kuwa tatizo la maji ili litatuliwe ni mpaka Rais John Magufuli apige simu kwa Katibu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

“Yaani tatizo la maji hadi Rais apige simu kwa katibu wa wizara, aunganishwe na mtendaji wa kijiji, hii inaoyesha mfumo umekwama,” amesema.

Amesema katibu huyo wa wizara amejikita mitandaoni kujibizana na maaskofu badala ya kutafuta ufumbuzi wa maji.

Wakati akiendelea kuchangia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama alisimama na kusema kwa mujibu wa kanuni ya 64, mbunge hatozungumzia utendaji wa Rais ndani ya Bunge.

“Madaraka aliyopewa Rais ni ya kikatiba, anaweza kusimamia jambo lolote, kwa utaratibu wowote anaoona unafaa kwa muktadha wa Watanzania. Na kanuni zinatufunza tusizungumzie mienendo ya Rais,” amesema Mhagama.

“Tukiacha liendelee kama anavyofanya Mchungaji Msigwa si sawa na tunavunja Katiba, ninaomba aheshimu kanuni ya 64 (1)(e) ya Bunge na kama itakupendeza Naibu Spika hayo anayozungumza afute.”

Baada ya maelezo hayo, Naibu Spika alisimama na kumtaka Mchungaji Msigwa kufuta maneno hayo.

Hata hivyo, Mchungaji Msigwa amesema hajui afute maneno gani jambo ambalo lilimnyanyua tena Dk Tulia, “kama hujui ufute yapi, futa mchango wako wote uliochangia na uanze moja.”

Agizo hilo lilipigwa na Mchungaji Msigwa na kuendelea kuchangia kitendo ambacho Dk Tulia hakukubaliana nacho na kumtaka aketi huku akimuita mbunge mwingine kuendelea na mjadala wa bajeti ya wizara hiyo.




Mbunge Ataka Serikali Kutatua Tatizo Maji Kisa Kuepuka Michepuko

$
0
0
Mbunge Ataka Serikali Kutatua Tatizo Maji Kisa Kuepuka Michepuko
Mbunge wa Kibiti Ally Ungando ameitaka serikali kutatua suala la maji jimboni kwake kwani yeye kama Mbunge wa Jimbo hilo amechoka kusuluhisha migogoro ya ndoa inayotokana na uhaba wa maji.


Akichangia hoja Bungeni Mbunge amesema kwamba tatizo hilo la maji linawafanya kina mama wengi kuamka alfajiri na kwenda mbali kutafuta maji, huku wakichukua muda mrefu na kuwafanya waume zao kukosa imani nao wakiamini huenda wanachepuka kwa wengine, na kusabaisha migogoro ya mara kwa mara.

“Kule jimboni kwangu nimechoka kusuluhisha ndoa kwa sababu ya muda mwingi wanandoa wanakwenda kutafuta maji visimani, baba anashindwa kuwa na imani mkewe amekwenda kisimani au amekwenda kwa mchepuko, kwa sababu maji yanatoka mbali, na ukienda yanakuwa ya kulindia, kwa hiyo baba anakosa imani, kwa hiyo tumekuwa na migogoro mikubwa ya wanandoa kule kwangu Kibiti, kwa hiyo Mheshimiwa angalia na kule Kibiti kwa jicho la huruma tuweze kutatuliwa tatizo la maji”, amesema Mbunge huyo.

Sambamba na hilo Mbunge amesema kwamba jimboni kwake kuna miradi ambayo ilikuwa inatekelezwa licha ya kuwa karibu na mto Rufiji, lakini inashangaza kukosa maji kwa ajili ya wananchi wake mpaka sasa.

Wanasiasa watano Wajiuzulu Ubunge Australia

$
0
0
Wanasiasa watano Wajiuzulu Ubunge Australia
Wanasiasa watano nchini Australia wamelazimika kujiuzulu kutokana na kugundulika kuwa na uraia wa nchi mbili kipindi ambacho walichanguliwa kushika nafasi hizo.

Mwaka jana, wabunge 10 nchini humo pia walivuliwa ubunge kutokana na kuwa na uraia wa nchi mbili tofauti na katiba inavyohitaji kwa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi.

Suala la uraia wa nchi mbili linatajwa kuyumbisha Bunge na serikali ya Australia kwa ujumla tangu mwezi July, 2017 na limewahi kuhatarisha baraza la mawaziri.

Timu Zilizoshushwa Daraja Zatajwa na TFF

$
0
0
Timu Zilizoshushwa Daraja Zatajwa na TFF
Ikiwa zimebakia takribani siku 22 kumaliza kwa mashindano ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa mwaka 2017/18 kwa mujibu wa kalenda, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia Bodi ya Ligi imezitangaza rasmi timu tatu kuzishusha daraja kutokana na kufanya vibaya.


Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura hii leo Mei 09, 2018 wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari na kuzitaja klabu hizo kuwa ni Namungo FC ya Lindi,  Pepsi FC ya Dar es Salaam, na Boma FC ya Kyela, Mbeya.

Kwa upande mwingine, Wambura amezitaja na kuzipongeza klabu sita zilizoweza kupanda daraja moja kwenda jingine ambazo ni JKT Tanzania FC ya Dar es Salaam, African Lyon ya Dar es Salaam, Kinondoni Municipal Council FC ya Dar es Salaam, Coastal Union ya Tanga, Biashara United FC ya Musoma pamoja na Alliance Schools FC ya Mwanza.

Tume Ya Haki za Binadamu Yataka Serikali Imrejeshe Miguna Miguna

$
0
0
Tume Ya Haki za Binadamu Yataka Serikali Imrejeshe Miguna Miguna
Tume ya Taifa ya Haki za Binadamu (KNCHR) imeitaka Serikali kununua tiketi ya ndege kwa ajili ya mwanasheria aliyeondolewa nchini kwa nguvu Miguna Miguna, na kumpatia hati ya usafiri ili aweze kurejea nchini wiki ijayo.

Katika barua iliyoandikwa na mwenyekiti wa KNCHR Kagwiria Mbogori kwenda Idara ya Uhamiaji inasema ni jukumu la serikali kuirahisishia tume hiyo kusimamia kurejea nchini kwa mwanasheria huyo machachari.

Mbogori, katika barua yake, amenukuu amri ya mahakama iliyotolewa kwa manufaa ya Dk Miguna kwamba masharti hayo matatu lazima yatekelezwe kabla ya kurejea kwake.

“Miguna ameiarifu tume kwamba anatarajia kurudi Kenya Mei 16, 2018,” alisema Mbogori katika barua yake iliyoandikwa Mei 5.

“Ili kuisaidia tume iweze kutekeleza maagizo ya mahakama, tume inaihimiza ofisi yake kutii maagizo ya mahakama kwa kumpatia Miguna Miguna hati halali ya kusafiria ya Kenya, kumnunulia tiketi Miguna ya kutoka Toronto, Canada, hadi Nairobi.”

Tume hiyo imeipatia Idara ya Uhamiaji hadi Alhamisi ya Mei 10 kujibu barua hiyo ya kurasa mbili.

Hili litakuwa jaribio jingine kwa Miguna kutaka kurejea kwenye nchi aliyozaliwa. Machi 29, aliondolewa kwa nguvu na kuingizwa kwenye ndege iliyokuwa inakwenda Dubai.

Huyu Ndiye Muimbaji wa Injili Kenya Anayedaiwa Kupewa Ujauzito na Harmonize

$
0
0
Huyu Ndiye Muimbaji wa Injili Kenya Anayedaiwa Kupewa Ujauzito na Harmonize
Mrembo kutoka nchini Kenya ambaye pia ni msanii wa muziki wa Injili, Veronica Wanja ‘Nicah The Queen’ anadaiwa kupewa ujauzito na msanii Harmonize.

Hata hivyo Nicah The Queen amekanusha taarifa hizo kwa kueleza kuwa hazina ukweli wowote, awali Nicah alikuwa katika mahusiano na mchekeshaji Dr. Ofweneke’s.

Taarifa za ndani zaidi kutoka nchini Kenya zinaeleza kuwa kipindi cha nyuma Nicah The Queen na Harmonize walikuwa wakionekana pamoja.
Weekend iliyomalizika Harmonize alikuwa nchini Kenya ambapo alitumbuiza katika show ya 10 Over 10 inayoruka kupitia Citizen TV.

Nicah The Queen hapo awali alitamba na nyimbo kama Pagawisha na Ushuhuda ila kwa sasa anafanya vizuri na wimbo unaokwenda kwa jina la Naringa. Unaweza kuutazama hapa chini.

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Zitto Kabwe Amshauri Job Ndugai

$
0
0

Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Ruyagwa Kabwe amefunguka na kumshauri Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai kuwa anapaswa kuwa na msimamo katika kuisimamia serikali kama alivyofanya jana na kudai hii itamfanya aweke 'legacy'


Zitto Kabwe amesema hayo baada ya jana Mei 8, 2018 Spika wa Bunge kumtaka Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Charles Mwijage kuja na maelezo ya kutosha kuhusu tatizo la sukari na mafuta nchini baada ya kutoridhishwa na majibu ya waziri huyo bungeni na kusisitiza kuwa haiwezekani wananchi wakawa wanaumia kwa gharama kubwa ya bidhaa hizo.

"Namna ambavyo Spika Ndugai amesimamia suala la majibu ya Serikali kuhusu kadhia ya Sukari na Mafuta ya Uto (kula) inanikumbusha bunge la tisa. Ndugai sasa ameanza kuweka ‘legacy’ yake. Aendelee hivi hivi ila jambo la muhimu zaidi suala la mafuta litazamwe kwa muktadha wa Wakulima wa Mawese na Alizeti" alisisitiza Zitto Kabwe

Kutokana na Spika wa Bunge na bunge kiujumla kutoridhika na majibu ya Waziri Mwijage hivyo spika wa bunge Job Ndugai aliomba maelezo zaidi na kutaka swali hilo kuulizwa tena wiki ijayo ili serikali ije na majibu ya kueleweka na yenye tija.

Mwanasayansi Kuuliwa na Sindano ya Sumu Kesho

$
0
0
Mwanasayansi aliyesafiri kutoka Australia mpaka Uswiss David Goodall,  kwa ajili ya kuukatisha uhai wake kesho inatarajiwa kuwa ndiyo siku ya kuhitimisha maisha yake ya duniani baada ya madaktari kuchomeka sindano ya sumu katika mshipa.


Kesho, madaktari wanatarajiwa kuweka sindano iliyojazwa dawa ya sodium pentobarbital katika mshipa wa Mwanasayansi huyo mkongwe duniani na kumuacha aisukume mwenyewe kwenda mwilini mwake.

Goodall amelazimika kusafiri kutoka Australia mpaka Basel, Uswisi kukifuata kifo baada ya sheria za kwao kutomruhusu kufanya hivyo.

Akihojiwa na shirika la utangazaji la Marekani CNN, Goodall amesema maisha yake hayana thamani tena ndio maana ameamua kuomba kujiua akiamini hadithi yake itakuwa mfano na kuhamasisha uamuzi kama huo kwa wengine waliochoka kuishi.

David Goodall

Katika mahojiano Goodall amenukuliwa akisema "Natamani ningekuwa na uwezo wa kutembea mashambani na kuona vitu vinavyonizunguka. "Katika umri huu naamka asubuhi, nakunywa chai. Nasubiri mchana nile halafu sina cha kufanya tena. Maisha ya aina hii ya kazi gani?

Goodall aliyezaliwa katika Jiji la London Aprili 1914, anatarajia kufa akiwa na miaka 104 ambapo ameweka wazi kuwa maisha yake yalisimama miaka 10 iliyopita baada ya kupoteza uoni na uwezo wa kutembea na alitamani kama kifo kingemchukua katika miaka hiyo.

Michepuko yaibuka Bungeni Kisa Maji

$
0
0
Mbunge wa Kibiti Ally Ungando ameitaka serikali kutatua suala la maji jimboni kwake kwani yeye kama Mbunge wa Jimbo hilo amechoka kusuluhisha migogoro ya ndoa inayotokana na uhaba wa maji.


Akichangia hoja Bungeni Mbunge amesema kwamba tatizo hilo la maji linawafanya kina mama wengi kuamka alfajiri na kwenda mbali kutafuta maji, huku wakichukua muda mrefu na kuwafanya waume zao kukosa imani nao wakiamini huenda wanachepuka kwa wengine, na kusabaisha migogoro ya mara kwa mara.

“Kule jimboni kwangu nimechoka kusuluhisha ndoa kwa sababu ya muda mwingi wanandoa wanakwenda kutafuta maji visimani, baba anashindwa kuwa na imani mkewe amekwenda kisimani au amekwenda kwa mchepuko, kwa sababu maji yanatoka mbali, na ukienda yanakuwa ya kulindia, kwa hiyo baba anakosa imani, kwa hiyo tumekuwa na migogoro mikubwa ya wanandoa kule kwangu Kibiti, kwa hiyo Mheshimiwa angalia na kule Kibiti kwa jicho la huruma tuweze kutatuliwa tatizo la maji”, amesema Mbunge huyo.

Sambamba na hilo Mbunge amesema kwamba jimboni kwake kuna miradi ambayo ilikuwa inatekelezwa licha ya kuwa karibu na mto Rufiji, lakini inashangaza kukosa maji kwa ajili ya wananchi wake mpaka sasa.

Sijaumia bikira yangu kuondolewa, dunia ya kujivunia bikira imepita – Ebitoke

$
0
0

Mchekeshaji kutoka Timamu, Ebitoke amedai bikira yake kuondolewa na muimbaji Ben Pol sio ishu kwenye maisha yake kwani kipindi cha mwanamke kujivunia bikira kimeshapita.


Akiongea akiwa Kikaangoni ya EATV, Ebitoke amedai kilichotokea katika maisha yake juu ya mahusiano na Ben Pol sio kitu kibaya, kwani wakati yupo naye mapenzi yalikuwa moto moto hivyo aliitendea haki nafsi yake.

“Kweli bikira yangu imetoka lakini sijaumia hata kidogo, maisha ya sasa yamebadilika, sasa hivi sio kama zamani bila bikira hauolewi,” alisema Ebitoke “Yote niliyopitia nikiwa na Ben Pol ni sehemu ya maisha yangu, sijawahi kujuta kwa sababu najua nimpata mwanaume mwingine,”

Katika hatua nyingine amewataka mashabiki wa vichekesho vyake kukaa mkao wa kula kwaajili ya filamu yake mpya itakayotoka mwakani.

“Eti Nini Wamekula Tena Rambirambi?..... Wakina nani Walikua Wanachangisha Zile Hela Kwani”- Nay wa Mitego

$
0
0
“Eti Nini Wamekula Tena Rambirambi?..... Wakina nani Walikua Wanachangisha Zile Hela Kwani”- Nay wa Mitego
Tetesi ambazo zimekuwa zikiendelea kwenye mitandao ya kijamii ni kuhusiana na rambirambi zilizotolewa kwenye msiba wa Marehemu Agnes Gerald Waya “Masogange” kusemekana kuwa rambirambi hizo zilizotolewa hazijawafikia wanafamilia wa Marehemu Agnes Masogange.

Inasemekana kuwa waigizaji wa Bongo Movie wamekula hela hizo za rambirambi zilizotakiwa kuwafikia familia wa Marehemu.

Nay wa Mitego kupitia account yake ya instagram ameandika caption ambayo inasemekana imewalenga waliochukua rambirambi hizo “Eti Niniiii.?! Wamekula tena RambiRambiiiii😳😳😭😭…?! Nooo Hapana una uhakika? Wakina nani walikua wanachangisha zile hela kwani? naomba majina yao”


Nkamia: Ufisadi Uliopo Katika Miradi ya Maji ni Zaidi ya Makinikia

$
0
0
Nkamia: Ufisadi Uliopo Katika Miradi ya Maji ni Zaidi ya Makinikia
Mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia amesema ufisadi uliopo katika miradi ya maji nchini unazidi ule wa mchanga wa madini na kushauri Bunge kuunda kamati teule kuchunguza miradi ya maji,

Akichangia bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji mwaka 2018/19, naibu waziri huyo wa zamani wa habari amesema, “miradi mingi ya maji ni zaidi ya makinikia na wakati Bunge linaunda tume hiyo Wizara ya Mambo ya Ndani ijiandae kupanua magereza.”

Akitolea mfano jimboni kwake Nkamia amesema, “pale Goima alipewa ofisa wa Takukuru, halafu sisi tunaonekana kama watu wa hovyo hovyo, waziri (wa Maji, Isaack Kamwelwe) kama utazunguka nchi nzima bila kuunda tume hutoweza, utazunguka, utapanda katika matenki, hutoweza, miradi mikubwa na midogo inapigwa.”

Amesema wananchi hawana uelewa wa utunzaji wa maji, “mnatumia Sh500 milioni kisha mnawakabidhi wanakijiji ambao hawana utaalamu wowote, miezi miwili unaharibika, badilisheni sera, wananchi wanataka maji.”

Mwaka 2017 Rais John Magufuli aliunda kamati mbili kuchunguza biashara ya usafirishaji mchanga wa madini ambao ulizuiwa kusafirishwa nje ya nchi, kamati hizo zilikuja na ripoti ikiwemo iliyobaini kiwango kikubwa na aina nyingi za madini yaliyomo kwenye makinikia.
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images