Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Yatangaza Kuanza Kupokea Maombi ya Mikopo

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Yatangaza Kuanza Kupokea Maombi ya Mikopo
Leo May 10 2018 Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza kuanza kupokea maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa muda wa miezi miwili na kusisitiza kuwa maombi yote yatapokelewa kwa njia ya mtandao.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkururugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru amesema BILIONI 427 zimetengwa kwa mwaka huu na wanafunzi wapya zaidi ya 40,000 watanufaika.

Jeshi la Magereza: Sugu Ametoka kwa Msamaha wa Rais

$
0
0
Jeshi la Magereza: Sugu Ametoka kwa Msamaha wa Rais
Jeshi la Magereza limesema mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu ametoka kwa msamaha wa Rais John Magufuli alioutoa kwa wafungwa katika maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Aprili 26, 2018.

Akizungumza na MCL Digital leo Alhamisi Mei 10, 2018, ofisa habari wa jeshi hilo, Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Lucas Mboje amesema katika maadhimisho hayo,  Rais Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa 3,319, kati yao wafungwa 585 waliachiliwa huru Aprili 26, 2018.

“Wafungwa 2,734 walibakia gerezani akiwemo Sugu kumalizia sehemu ya kifungo kilichobakia baada ya kupewa msamaha huo na Rais Magufuli,” amesema.

Simba Yaanza Safari ya Singida Kuweka Kambi Dodoma Kupata Baraka ya Wabunge

$
0
0
Simba Yaanza Safari ya Singida Kuweka Kambi Dodoma Kupata Baraka ya Wabunge
Kikosi cha Simba kimeanza safari ya kuelekea Singida kwa ajili ya mtanange wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Singida United.

Simba itapitia katika Makao Makuu ya nchi, Dodoma, kuweka kambi fupi kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea mjini Singida.

Taarifa kwa mujibu wa Meneja wa kikosi hicho cha wekundu wa Msimbazi, Richard Robert, amesema kuwa kikosi kitapita jijini hapo ili kuweka kambi fupi kabla ya kuendelea na safari.

Inaelezwa kuwa Simba wamepanga kupitia Bungeni kwa ajili ya kupata baraka za kuelekea mechi yao na Singida itakayopigwa Mei 12 kwenye Uwanja wa Namfua.

Tayari kikosi hicho kipo njiani hivi sasa kuelekea jijini humo na kesho kitaanza tena safari ya Singida.

Yanga Kuvaana na Prisons Leo Ikiwa Pungufu

$
0
0
Yanga Kuvaana na Prisons Leo Ikiwa Pungufu
Kikosi cha Yanga kinateremka dimbani Sokoine jioni ya leo kuvaana na Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Uongozi wa Yanga umesema unataka kutengeneza heshima hata kama wataukosa ubingwa wa ligi kwa kushinda mechi zote zilizosalia.

Yanga inashuka dimbani ikiwa pungufu kufuatia nyota wake kadhaa kusalia jijini Dar es Salaam ikilelezwa kuwa ni madai ya mshahara.

Msafara wa Yanga haujaweka wazi orodha ya kikosi kilichosafiri kwa ajili ya mchezo dhidi yao na Prisons utakaoanza saa 10 leo.

Timu zote mbili zimejivuna kupigania alama tatu kuelekea mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka jijini Mbeya.

Mbunge Sugu: Nilifungwa Kiholela na Nimetoka Kiholela

$
0
0
Mbunge Sugu: Nilifungwa Kiholela na Nimetoka Kiholela
Saa chache baada ya kutoka jela, mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu amesema ni mfungwa wa kisiasa, “nilifungwa kiholela na nimetoka kiholela.”

Viongozi wa Chadema wakiongozwa na mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe leo Mei 10, 2018 walifika katika Gereza Kuu la Ruanda mkoani Mbeya kuwapokea Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga lakini walipigwa chenga ya mwili baada ya kuelezwa na askari magereza kwamba wameshatoka, hivyo kulazimika kuwafuata nyumbani.

Akizungumza na MCL Digital leo Sugu amesema, “Sikutaka kuhoji sababu za kutolewa, jana niliambiwa jiandae kesho (leo) tutatoka, basi nasi tukasema haina shida kwa sababu sikuwa na sababu ya kuwa ndani. Naamini sikutakiwa kuwa gerezani.”

Sugu akiwa na Masonga alifika nyumbani kwake na kumkuta mlinzi pekee kutokana na mkewe Happiness Msonge kwenda Gereza la Ruanda kuwapokea.

Dakika chache baadaye Happiness na mke wa Masonga, Grace Malya walifika nyumbani hapo na kuwalaki kwa furaha huku wakikumbatiana na kucheka.

Akizungumzia mazingira ya kuachiwa kwa wawili hao, Mbowe amesema, “inaonyesha hawakuwa na sababu ya kuwepo gerezani maana mazingira ya kutolewa kwao ni tata sana.”

Serikali Kutafuta Muwekezaji Mwingine Mradi wa Mabasi ya Mwendokasi

$
0
0

Serikali Kutafuta Muwekezaji Mwingine  Mradi wa Mabasi ya Mwendokasi
Serikali imesema ipo katika mchakato wa kutafuta muwekezaji mwingine katika awamu ya pili ya mradi wa mabasi ya mwendokasi ikiwa kama njia ya kujaribu kutatua changamoto za usafiri katika Jiji la Dar es salaam.


Hayo yamesemwa Bungeni leo Mei 10, 2018 na Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa katika kipindi cha maswali na majibu na kusema kuwa serikali ikiongeza muwekezaji mwingine katika mradi huo itasaidia kuleta ushindani wa kibiashara baina ya makampuni hayo na hatimaye wananchi watapata huduma bora ya usafiri.

"Tunaendelea kuondoa changamoto za muendeshaji aliyopo sasa, lakini tumeanza utaratibu wa kupata muendeshaji mwingine ili tupate kampuni nyingine iingize mabasi yake, kuimarisha usafiri wa Jijini Dar es salaam lakini suala la miundombinu tutaimalisha na tunajipanga vizuri ili kuhakikisha huduma hii inaendelea kuwanufaisha watanzania", amesema Majaliwa.

Waziri Mkuu Majaliwa aliongezea kuwa serikali itachukua hatua kwa muwekezaji wa sasa kama akishindwa kuendesha mradi huo.

"Pale ambapo itabainika muendeshaji wa sasa anamatatizo yaliyokithiri, hatuna shida tutamuondoa kwasababu waendeshaji wapo wengi, wapo watanzania na mataifa ya nje wanaweza kuendesha na kuleta mabasi", amesisitiza Majaliwa.

Kumekuwepo na changamoto mbalimbali katika uendeshaji wa maradi huo ikiwemo mgogogro kati ya UDART na kampuni ya ukatishaji tiketi ya za kielektroniki, ubovu wa miundombinu katika ofisi za kampuni hiyo hasa kipindi cha mvua na changamoto ya uchache wa mabasi kwa abiria wakati wa asubuhi na jioni.

Mradi wa mabasi ya mwendokasi kwasasa unasimamiwa na serikali kupitia shirika la usafiri UDA kwa kushirikiana na kampuni binafsi ya DART na kuunda kufanikiwa kuunda kampuni moja ya UDART.

Rammy Galis “Mungu Anisaidie Niweze Kutoa HUKUMU”

$
0
0
Rammy Galis “Mungu anisaidie niweze kutoa HUKUMU”
Muigizaji Rammy Galis ni miongoni mwa watu waliokuwa karibu na Marehemu Agnes Waya “Masogange” na pia alishawahi kuwa mapenzini na Marehemu, kupitia ukurasa wake wa instagram ameandika caption iliyotafsiriwa tofauti na mashabiki mbalimbali.

Hii ni kutokana na tetesi ambazo zimekuwa zikiendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na waigizaji wa Bongo Movie na kusemekana kuwa wamekula hela za rambirambi ambazo zilitakiwa kuwafikia ndugu wa Marehemu Agness Masogange.

Rammy Galis ameandika “Namuomba mungu anisaidie ili niweze kutoa kile kitacho barikiwa katika kazi ya mkono wangu na wako [HUKUMU] , SANIA yupo kwa niaba yako ❤😢 #PumzikaSalama  #RipAgness#HUKUMU”

Aunty Ezekiel alijibu kile alichokiandika Rammy Galis “Wewe ulitoa shillingi ngapi kwenye huo msiba, punguzeni drama basi kwa mambo ya familia za watu tena wenye majonzi bado”

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

DR MAGISE


Watu 27 Wafariki Kutokana na Mvua Zinazoendelea Kunyesha Kenya na Kuvunja Kuta za Bwawa

$
0
0
Watu 27 Wafariki Kutokana na Mvua Zinazoendelea Kunyesha Kenya na Kuvunja Kuta za Bwawa
Watu 32 wamefariki  dunia huku wengine wakikosa mahali pa kuishi baada ya  bwawa la Patel kubomoka kutokana na mvua kubwa iliyonyesha jana  usiku.

Taarifa kutoka nchini humo zinasema kwamba watu wengi hawafahamiki walipo mpaka sasa.

Bwawa la Patel mjini Nakuru katika mkoa wa bonde la ufa lilibomoboka jana usiku na kusomba mamia ya nyumba za wakazi waliokuwa karibu na eneo hilo.

Waziri wa Mambo ya Ndani Kenya, Fred Matiangi amewasili katika eneo hilo.

Mmoja ya walioshuhudia maafa ya kupasuka kwa bwawa hilo nchini Kenya anasema imeonekana miili iliyofukiwa katika matope.

“Tulipata miili 11 iliyokuwa imefukiwa na matope katika shamba moja la kahawa na hawa ni watu ambao huenda walikuwa wakijaribu kujiokoa  lakini hawakufanikiwa kutokana na nguvu na kasi ya maji ,’’amesema.

Kwa mujibu wa taarifa ya polisi wengi wao ni wawawake na watoto ambao hawakuweza kukimbia kwa kasi pamoja na wazee.

Hiki Hapa Kikosi cha Yanga Dhidi ya Tanzania Prisons

$
0
0
Hiki Hapa Kikosi cha Yanga Dhidi ya Tanzania Prisons
Kikosi cha Yanga kitakachoanza dhidi ya Tanzania Prisons, mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

1. Beno Kakolanya



2. Juma Abdul



3. Emmanuel Martin



4. Abdallah Shaibu



5. Pato Ngonyani



6. Maka Edward



7. Paul Godfrey



8. Thaban Kamusoko



9. Yohana Mkomola



10. Matheo Anthony



11. Baruan Akilimali







Kikosi cha akiba







12. Yusuph Suleiman



13. Amis Tambwe

Wakili Alalamika Mke wa Seth Kukataliwa Kumuona Mumewe Mahabusu

$
0
0
Wakili  Alalamika Mke wa  Seth Kukataliwa Kumuona Mumewe Mahabusu
Wakili wa Harbinder Seth, Dora Mallaba amelalamika kuwa, mke wa mteja wake, amezuiwa kumuona mume wake mahabusu.

Akizungumza leo Mei 10, mbele ya  Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Huruma Shahidi, Wakili  Mallaba amesema kibali cha mke wa Seth kumuona mume wake gerezani kiliombwa tangu Februari mwaka huu lakini hadi leo hakijatoka.

 Ameiomba Mahakama  kutoa maelekezo ili mke wa Seth, akamuone mume wake gerezani.

Pia wakili huyo, amelalamika kuwa Sethi alipelekwa hospitali ili apimwe na kupewa majibu ya vipimo kutokana na hali yake ya kiafya kuwa mbaya, lakini hajapewa majibu hayo mpaka sasa.

Baada ya Dora kueleza hayo, Shaidi alidai kuwa amri ya Mahakama imetekelezwa kwa kumpeleka Seth hospitali na kwamba suala la matibabu halipaswi kuingiliwa na mahakama liachwe baina ya mgonjwa na madaktari.

Kuhusu mke wa Seth kuzuiwa kumuona mumewe, Shaidi amedai kuwa sheria ya magereza ipo wazi na kwamba imetoa utaratibu wa kumuona mtu aliyekuwapo mahabusu.

Soma Zaidi: Hakimu akerwa bilionea IPTL kutopatiwa matibabu Muhimbili

“Ni rai yetu wafuate utaratibu za Magereza walizoelekezwa ili mke apate nafasi ya kumuona mumewe," ameeleza Shaidi.

Baada ya kusikilizwa hoja hizo, Hakimu Shaidi amesema suala la kuonana na mtu aliyekuwepo magereza ni la kibinadamu kwani hao ni mtu na mkewe na wanapendana hivyo alishauri wapewe nafasi ya kuonana.

Hakimu Shahidi ameiahirisha kesi hadi Mei 25, 2018 kwa ajili ya kutajwa.

Seth ni mmiliki wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independe Power Tanzania Ltd(IPTL) na James Rugemarila, Mmiliki wa kampuni ya VIP Engineering and Marketing.

 Wanakabiliwa na mashtaka  12 ya  uhujumu uchumi  kwa kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu , kughushi,  kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu,  kutakatisha fedha  na kuisababisha serikali hasara .

Mobetto ni Mdogo Wangu Kuna Wakati Mazoea Yanazidi- Wema Sepetu

$
0
0
Mobetto ni Mdogo Wangu Kuna Wakati  Mazoea Yanazidi- Wema Sepetu
BAADHI ya wasanii wa Bongo Muvi wamemuandalia hafla fupi msanii mwenzao, Wema Sepetu, wakimpongeza kutokana na tuzo alizoshinda kwenye tuzo za sinema zetu zilizoandaliwa na Azam TV mwezi uliopita.

Wema amewashukuru sana wasanii wenzake kwa hafla hiyo na pia amesema ameyasikia maneno maneno ya baadhi ya wasnii wengine walioponda yeye kupata tuzo hizo, lakini anazichukulia kama changamoto tu kwenye maisha kwani huwezi kupendwa na kila mtu.

Aidha, Wema amezungumzia uhusiano wake na Mwanamitindo, Hamisa Mobeto, ambaye awali alikuwa rafiki yake lakini baada ya kuzaa na X-wake Mbongo Fleva, Diamond Platnumz, urafiki umepungua kidogo.

“Hamisa ni kama Mdogo wangu, lakini kuna wakati sijui mazoea yakizidi sana kunaleta mushkeri kidogo, kwahiyo kila mtu anatakiwa kubaki kwenye mipaka yake,” amesema Wema.

Mhandisi Aliyetajwa na Rais Magufuli Asomewa Mashtaka na Kunyimwa Dhamana

$
0
0
Mhandisi Aliyetajwa na Rais Magufuli Asomewa Mashtaka na Kunyimwa Dhamana
Mahakama ya Hakimu Mkazi, Iringa, imemnyima dhamana Mkurugenzi wa Kampuni ya MNM, Engineering Service Ltd, Mhandisi Godwin Mshana, kwa tuhuma za kujenga ukumbi wa Chuo Kikuu Mkwawa, (MUCE) chini ya kiwango.

Mshana alifikishwa leo Mei 10, Mahakamani hapo na kusomewa mashtaka matatu mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa, Iringa, David Ngunyale.

Wakili wa Serikali, Blandina Mnyamba amemsomea mashtaka Mshana na kusema kuwa alitenda makosa hayo kati ya 2010 na 2012.

 Amesomewa mashtaka ya kughushi nyaraka za serikali, kujipatia fedha Sh 3 bilioni kinyume na utaratibu na shtaka la tatu ni kuhujumu uchumi katika matumizi ya Sh 2bilioni.

Dhamana ya Mshana imezuiwa na kesi hiyo itasikilizwa tena Mei 22 mwaka huu.

 Mei 2 mwaka huu, akiwa katika ziara Chuo Kikuu cha Muce, Iringa, Rais Magufuli aliagiza uchunguzi ufanyike katika ujenzi wa ukumbi wa mikutano wa chuo hicho, uliogharimu Sh 8 bilioni.

Pia, Rais Magufuli  aliagiza, aliyekuwa Mkuu wa chuo hicho, Profesa Philemon Mushi naye ahojiwe kuhusiana na ujenzi huo.

Zari Amnunuliwa Range Rover Sport ya Mwaka 2017 na Mkenya Aliyetangaza Kumuoa Kipindi cha Nyuma

$
0
0
Mkenya Aliyetangaza Kumuoa Zari Amnunulia  Range Rover Sport ya Mwaka 2017 Zari
Ringtone Apoko ni msanii wa muziki wa Injili kutoka nchini Kenya ambaye kipindi cha nyuma alitangaza ni yake ya kumuoa Zari The Boss Lady, sasa muimbaji huyo amerejea tena kwenye headlines zake.

Muimbaji huyo ametangaza kuwa amemnunulia Zari gari aina ya Range Rover Sport ya mwaka 2017, hii ni baada ya kupata taarifa kuwa Zari siku si nyingi atakuwa nchini Kenya.

Soma Pia; Baada ya kuachana na Diamond, msanii wa Kenya ajitosa kwa Zari

Pia ameeleza kufurahishwa mara baada ya kumuona Zari akiwa kanisani na kumtaka kuendelea hivyo hivyo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;.

Dear Zari,
I know you are coming to Kenya anytime from now. I take this opportunity to welcome you to my beloved country.

I checked and I realised that you were in church ⛪ on Sunday am happy because it’s only in Jesus that you won’t be hurt like Diamond did. Pleaaaase stay in church and in God. You recently posted on your IG that you wanted a Range Rover OK I took note and I want to let the world know today that I have bought you a brand new Range Rover sport 2017 model.

Am sorry I know you wanted white but I only managed a black one in color. Please arrange how to pick your key🔑 b4 you leave. While you in Kenya if you need anything let me know I will make sure it’s done for you.

Wiki iliyopitia Zari aliweka wazi kununua gari aina ya Range Rover Spor na kuibuka stori kuwa huenda mrembo huyo kapata mwanaume ambaye ameamua kumuhudumia vilivyo hata hivyo alikanusha hilo.


Zari kwa sasa anasema yupo single mara baada ya kuachana na mzazi mwenzie, Diamond Platnumz ambaye walijaliwa kupata watoto wawili, Tiffa na Nilan.

Serikali Yafunguka Sakata la Ugonjwa wa Ebola

$
0
0
Serikali Yafunguka Sakata la Ugonjwa wa Ebola
Serikali imesema hakuna mgonjwa yeyote aliyehisiwa au kuthibitishwa kuwa na virusi vya ugonjwa wa Ebola hapa nchini na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari kubwa dhidi ya ugonjwa huo ambao umeripotiwa hivi karibuni katika nchi jirani ya Demokarasia ya Kongo (DRC).


Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema kuwa hata hivyo taarifa hiyo haiizuii Tanzania kuchukua hatua thabiti dhidi ya kujikinga na ugonjwa wa Ebola kwa kuwa inapakana na nchi ya DRC ambapo kuna mipaka mingi ambayo watu huwa wanaingia na kutoka kwa njia zisizo za halali.

"Tanzania imepokea taarifa ya uwepo wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini DRC uliotangazwa na na shirika afya Duniani Mei 8 mwaka huu ambapo vipimo vya maabara vimethibitisha baada ya kupokea wagonjwa 21 ambapo kati yao 17 wamepoteza maisha", amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amewataka watu wanaoishi katika mikoa inayopakana na nchi ya DRC kuchukua tahadhari pale wanapohisi kupata magonjwa yenye dalili za Ebola kwa kuwahi kufika kwenye hospitali zinazotoa huduma ili wafanyiwe vipimo vya kina kuonyesha kama wameathirika au la.

Waziri Ummy ameitaja mikoa ambayo inapakana na nchi ya DRC kuwa ni Mwanza, Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa na Songwe na kuwataka wananchi wanaoishi katika mikoa hiyo kuchukua tahadhari kubwa ya kujikinga na ugonjwa wa Ebola.

“Nimeitaja mikoa hiyo kwa sababu ina njia nyingi ambazo siyo rasmi zinazowawezesha watu kuvuka kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine na hivyo kama kutakuwa na mtu ambaye ameambikizwa ugonjwa huo itakuwa ni rahisi kuusambaza tofauti na mtu nayeingia nchini kwa kutumia mipaka rasmi kama vile uwanja wa ndege”,  amesema Waziri Ummy.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amesema Wizara imechukua hatua mbalimbali ili kudhibiti ugonjwa huo ikiwemo kutoa taarifa ya tahadhari ya ugonjwa wa Ebola kupitia kwa makatibu tawala na waganga wakuu wote wa mikoa kwa kujumuisha na namna mgonjwa anavyoweza kutambuliwa, namna ya kuchukua sampuli na namna ya kuwahudumia wagonjwa.

Unalalamika Hela za Rambirambi Umechangia Nini?- Steve Nyerere

$
0
0
Unalalamika Hela za Rambirambi Umechangia Nini?- Steve Nyerere
Muigizaji wa Bongo Movie Steve Nyerere amezungumza kuhusu watu wanaolalamika kuwa yeye na baadhi ya watu waliokuwa kwenye kamati ya mazishi ya msiba wa Masogange wamekula za rambirambi ambapo Steve amedai kuwa anashangaa sana watu kwenda kulalamika mitandaoni kuhusu hela hizo wakati mtu huyo hajatoa kitu zaidi ya kuvaa sare na kulia.

Steve Nyerere amesema hela ya rambirambi ipo ambayo ni Milioni 2 na laki moja lakini kama kamati walikubaliana kumuwekea mtoto ije imsaidie kwenye masomo yake na watu wanao lalamika kuwa hela zimeliwa hawajatumia ustaarabu kwenda kulalamika kwenye mitandao wakati wao hawajajitoa chochote.

“Sizani kama mtu mwenye akili timamu tena kama wewe ni ndugu ambae hata arobaini ya marehemu haijafika unafikia muda unaanza kuongelea michango iliyobaki ndani akili yako yote ilitakiwa iende kwenye arobaini,”

Niulize unatokaje kwenda kuzungumza kwneye vyombo vya habari wewe umechangia nini zaidi ya kulia? umechangia jeneza?” – Steve Nyerere

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam  na mikoan wasiliana na DR Oshinda no 0755505099 au 0714126118  Karibuni kwa hunduma bora 

Chips Zenye Madawa ya Kulevya Nusura Zitoe Maisha ya Watu Watatu

$
0
0

CHATO, GEITA: Watu 3 wamenusurika kifo baada ya kula chips zinazoaminika kuwa na #DawaZaKulevya zilizosababisha wapoteze fahamu kwa saa 9 na kuibiwa mali mbalimbali

Watu hao walikirimiwa chakula hicho na mgeni mmoja aliyefika katika nyumba ya kulala wageni(Diana) wanakofanya kazi

Baada ya kula chips hizo walianza kuishiwa nguvu na hatimaye kupoteza fahamu kwa saa 9 hadi pale walipozinduka wakiwa katika hospitali ya Wilaya hiyo

Mpaka sasa watu hao wamelazwa katika Hospitali hiyo ingawa afya zao bado zimedhoofu huku dawa waliyowekewa kwenye chakula hicho ikiwa bado hakijafahamika

Bwawa la Kutengeneza Lapasuka na Kuuwa Watu 27 Kenya

$
0
0

NAKURU, KENYA: Watu 27 wamefariki huku wengi wakiwa hawajulikani walipo na wengine zaidi ya 2000 wakiachwa bila makazi baada ya bwawa la Patel kuvunja kuta zake jana Mei 09, usiku

Waliokiwa jirani na eneo la bwawa hilo wanasema walisikia mshindo mkubwa kabla ya maji mengi kuanza kusomba makazi na mashamba ya watu umbali wa kilometa mbili kutoka bwawani

Kuna hofu kwamba huenda idadi ya watu waliofariki ikaongezeka wakati jitihada za uokoaji zikiendelea

Bwawa hilo la Patel ni mojawapo ya mabwawa matatu yanayomilikiwa na mkulima mmoja mkubwa katika eneo hilo

Chanzo cha kuta za bwawa hilo kupasuka inaarifiwa kuwa ni maji mengi kujaa baada ya kukusanyika kufuatia mvua kubwa inayoendelea kunyesha nchini humo

Kuzuiwa Meli ya Mafuta ya Kupikia Bandarini..Viwanda Vikubwa Vinne vyasitisha Uzalishaji, Wafanyakazi 4000 Kuathirika

$
0
0

DAR: Viwanda vinne vikubwa vya kuzalisha mafuta ya kula vinadaiwa kusitisha uzalishaji kwa takribani mwezi mmoja sasa baada ya kuzuiwa kwa meli mbili zenye mafuta ghafi katika bandari ya dar

Mwenyekiti wa Chama cha Watengeneaji mafuta ya kupikia Tanzania, Hussein Kamote amesema viwanda hivyo vinatengeneza mafuta ya kula ya kutokana na mchikichi na kukidhi mahitaji ya zaidi ya 80% ya watanzania

Amesema mafuta hayo yanayoagizwa kutoka Indonesia na Malaysia yapo bandarini mpaka sasa kwa kuwa TRA imekataa kuyatoa

Aidha amesema kusitishwa kwa uzalishaji kumeathiri zaidi ya wafanya kazi 4000 ambao kwa sasa inabidi wasiende kazini kwa kuwa hakuna uzalishaji
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images