Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Ummy Mwalimu apewa tuzo ya heshima

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM), amepewa tuzo ya heshima na klabu ya soka ya Coastal Union ya jijini Tanga.

Coastal Union wametoa tuzo hiyo kwa Ummy, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake ambao ulifanikisha harakati zao za kurejea ligi kuu kuanzia msimu ujao baada ya kufanikiwa kuwa miongoni mwa timu sita zilizopanda msimu huu.

Tuzo hizo ambazo zimetolewa na baraza la wazee wa timu hiyo chini ya Mwenyekiti Salimu Bawaziri pia amekabidhiwa Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani pamoja na wadau wengine.

Ummy alijitolea kugharamia kambi za timu hiyo wakati wa michezo ya ligi daraja la kwanza pamoja na kulipa mishahara na posho za viongozi na wachezaji jambo ambalo liliongeza hamasa kwa wachezaji.

Coastal Union ni miongoni mwa timu sita zilizopnda ligi kuu msimu ujao. Nyingine ni Alliance Schools, Biashara Mara, KMC, African Lyon na JKT Tanzania ambazo zitachukua nafasi za Ndanda FC na Majimaji FC huku zingine zikiongeza idadi ya timu kutoka 16 hadi 20.


Ukiona Mpenzi Wako Anaomba Kuruka Ukuta na Ukampa..Basi Ndoa Kwako Utaisikia kwa Wenzio

$
0
0
Juzi kati nilijumuika na watu wa on transit to Marriage....

Moja ya agenda ilikuwa ni wimbi la mapenzi kinyume na maumbile, nini sababu kama vijana, Tumefikaje hapa? Uzoefu wa wanaotumia hii kitu nk.

Hatimaye overview ikaja na mtizamo wa kila mwanaume ukaonesha iwe mvua au masika hakuna mwanaume anayekusudia kuingia ndoani na mwanamke anayeruhusu huo mchezo.

Hivyo ukiombwa na mtu wako hiyo huduma kuna 2 au laa, mosi anataka kujua kama ni muumini wa hiyo habari, Ukijifanya unampenda sana so unampa basi atakula huo mzigo na utakuwa umefuzu kuto kuiona ndoa kwenye miaka ya hivi karibuni.

Kila mwanaume anataka mwanamke mwenye staa ya hali ya juu kuja kuwa mama wa wanae. Ila ukimpa anaipuliza tu na utajijua mwenyewe ukimnyima unakuwa umefuzu hatua ya makundi kuelekea kwenye ndoa.........

Alikiba Amfananisha Diamond na "Mwanamke"

$
0
0
Jana ilikuwa siku maalumu kwa ajili ya mahojiano ya Kiba pale mawingu (Clouds) media, wenyewe wanakwambia ALIKIBA DAY. Baadhi ya maswali aliyoulizwa ni jinsi alivosalimiana na hasimu wake mkubwa Diamond Platnumz kwa kumgeuzia kiganja cha mkono, hakusita kusema kila mtu anasalimiwa kwa style yake, hata Wanawake wanakuwa na Salamu zao jinsi ya Kuwapa mkono , Akimanisha utofauti uliopo pindi unaposalimiana na mwanamke au mwanaume.

Mwanafunzi aliyejinyonga aagwa, wenzie wasimulia mazito

$
0
0
Leo May 12, 2018 Luciana Olutu alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo cha Makumira Arusha na amefariki dunia May 7 mwaka huu baada yakujinyonga kwa kile kinachodaiwa ni msongo wa mawazo baada ya mtoto wake kufariki.

Wanafunzi ambao wamesoma naye wameelzea jinsi Marehemu Luciana alivyojaribu kujiua zaidi ya mara mbili na kilichoandikwa katika barau.

VIDEO:

Source:Millard

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Mwanaume Ajiua Kisa ‘Bili Kubwa’ ya Umeme

$
0
0
Mwanaume mmoja, raia wa India ambaye anafanya biashara ya mboga za majani ameripotiwa kujiua jana May 10, 2018 baada ya kupokea bili ya umeme ya gharama ya Dola za Marekani 13,000 sawa na Shilingi za Kitanzania milioni 31.2.

Mwanaume huyo anayefahamika kwa jina la Jagannath Shelke, 36, alikuwa ni mkazi wa kusini mwa Maharashtra nchini humo.

Familia yake imeliambia Shirika la Utangazaji BBC kuwa Jagannath aliacha ujumbe kuwa amejiua kutokana na bili hiyo ya umeme kuwa kubwa sana.

Hatahivyo inaelezwa kuwa bili hiyo ilikuwa imekosewa, bili sahihi ilikuwa ni Dola za Marekani 41.6 sawa na takriban Shilingi za Kitanzania 98,000.

Hii ndio sababu ya Rihanna kuvamiwa nyumbani kwake

$
0
0
Hii ni nyingine ya kuifahamu kutoka kwa staa maarufu  Marekani Rihanna ambapo inaripotiwa kuwa siku ya May 11,2018 alivamiwa katika nyumba yake iliyopo Holly Wood Hills na kijana aliyefahamika kwa jina la Eduardo Leon.

Mashuhuda waliwaambia polisi waliofika nyumbani kwa Rihanna kuwa kijana huyo alifanya hivyo kwa dhumuni la kumuona Rihanna na kukutana naye kimwili kutokana na hisia alizonazo kwa mwanamuziki huyo.

Eduardo Leon mwenye umri wa miaka 26 alifanikiwa kuzima alarm kwenye nyumba hiyo na kufanya uvamizi na pia inasemekana kuwa hii sio mara ya kwanza kwa Eduardo kufanya uvamizi katika nyumba mbalimbali na kuripotiwa kuwa May 4,2018 alifanya uvamizi.

Idris Sultan amkingia kifua mke wa Ali Kiba mtandaoni

$
0
0
Leo May 11,2018 staa mkongwe katika game ya Bongo Fleva Ali Kiba amefanya ziara katika kituo cha redio cha Clouds Media akiongelea ishu mbalimbali kuhusiana na maisha mapya  ya ndoa na katika ziara hiyo aliongozana na mke wake Amina.

Baadhi ya mashabiki wamechukilia hii ishu kuwa sio kitu kizuri kwa mwanamke aliyeolewa kufanya ziara katika vyombo vya habari na kuandika comments tofautitofauti kupitia mitandao ya kijamii hasahasa mtandao wa instagram.

Mchekeshaji Idris Sultan ameamua kuwajibu mashabiki wote ambao wanahisi kuwa kitendo cha mke wa Ali Kiba kufanya ziara “AliKibaDay” na mume wake  ni kitendo kibaya .


Katarina Amvaa Ebitoke

$
0
0
Mchekeshaji wa kike Bongo aliyejizolea umaarufu mpaka nje ya nchi Katarina Karatu, amesema kauli ya Ebitoke kwamba Tanzania hakuna wachekeshaji wa kike, amekosea kwani wako wengi sana.

Katarina amesema licha ya kwamba hajisikii kumuongelea Ebitoke, lakini kauli aliyoitoa haileti maana na inavunja moyo, kwani wachekeshaji wapo wengi isipokuwa mashabiki ndio wanaamua nani ni mkali zaidi.

“Yule ni mtu mzima anajua anachofanya kwa hiyo kuanza kumuongelea sijisikii kwanza, nahisi sifanyi kitu sahihi, kuhusu wachekeshaji wa kike kwanza anakosea, wapo wengi tu kuna watu wanafanya vizuri, ni mashabiki wanaamua nani ni bora na nani anavamia fani, ila kuhusu yeye sihitaji kumuongelea sana kwa sababu zangu binafsi”, amesema Katarina.

Mchekeshaji huyo ameendelea kwa kusema kwamba ili kuthibitisha kuwa wachekeshaji wazuri Tanzania wapo, hivi karibuni amepata mwaliko nchini Kenya ambapo atapanda jukwaa moja na wachekeshaji kutoka nchi nyingine za Afrika Mashariki, Anne Kansiime wa Uganda, Idirs Sultan wa Tanzania na wengine wa Kenya.

Wema Sepetu Akanusha kuhusu lipstick zake

$
0
0
Mrembo Wema Sepetu amekanushaa taarifa zilidodai kuwa bidhaa zake mpya za lipstick zinafanana na zile za mwanzo.

Wema amesema hilo halina ukweli wowote zaidi ya watu walioamua kuzusha hilo.

“Kiss by Wema sio Wema Sepetu Liquid Matte, Kiss by Wema ilikuwa na mafuta, hii ya pili ni kavu, hazina mafuta and zipo kwenye package tofauti na zina ubora zaidi kuliko zile za mwanzo,” Amesema Wema Sepetu.

September 2017 Meneja wa Wema Sepetu, Happy Shame alikanusha taarifa zilizodai kuwa lipstick za ‘Kiss by Wema’ zilipigwa maarufu na Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA) kwa kueleza kuwa bidhaa hizo hazikuwepo tena sokoni kwa wakati huo.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

DR MAGISE

Aina 7 Za Juisi Zenye Kuondoa Sumu Mwilini

$
0
0
Sumu mwilini hutokana na vile vitu au vyakula ambavyo binadamu hutumia huenda kwa kujua au kutokujua. Sumu hizo pia huweza kuchangiwa na matumizi ya yasiyosahihi ya dawa mbalimbali.

Miongoni mwa mbinu bora na nzuri ya kuondoasumu hizo ndani ya mwili ni pamoja na kutumia vyakula halisi mara kwa mara.

Hapa nanayo orodha ya vinywaji ambavyo huweza kuondoa sumu ndani ya mwili:-

1. Juisi ya mchanaganyiko wa tango na spinachi.
2.Jusi ya mchanganyiko wa tangawizi na spinachi.
3. Juisi ya mchanganyiko wa chungwa na tango.
4. Juisi ya komamanga pamoja na mapera
5. Juisi ya changanyiko wa passion na tango
6. Juisi ya mchanganyiko wa apple na parachichi
7. Juisi ya mchanganyiko wa mbegu za maboga na strawberry

Zijue Dalili za awali za Ugonjwa wa Kisukari

$
0
0


Ili kuweza kutambua kama umeugua ugonjwa wa kisukari unatakiwa kujua dalili za awali za ugonjwa huo ambazo ni;

1. Kukojoa mara kwa mara.
Ugonjwa wa Kisukari unasababisha sukari kutolewa kwenye njia ya mkojo. Sukari inapotolewa  huambatana na maji hivyo  kukufanya upate mkojo kila mara.

2. Kuhisi Kiu mara kwa mara.
Unapokuwa na kisukari unapoteza maji mengi kwenye mkojo hali hii husababisha kupata koi mara kwa mara.

3. Kusikia njaa kali kila mara.
Mwili unapoteza uwezo wa kutumia sukari katika kazi zake. Hali hii hufanya mwili wako kuhisi kuwa hakuna chakula cha kutosha. Hii ndio sababu inakufanya  kuhisi njaa kila mara na hata baada ya kula unaendelea kuhisi njaa.

4. Uchovu wa mwili
Hii hutokana na mwili kushindwa kutumia  sukari  kutengeneza nishati ya kuwezesha mwili kufanya  kazi zake.

5. Kupoteza uzito/Kukonda
Ugonjwa wa Kisukari hupunguza uwezo  wa mwili kuhifadhi sukari kwenye misuli. Hivyo mwili wako utaanza  kupoteza uzito na kuanza kukonda.

Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic)

$
0
0
Kitunguu swaumu ni jamii ya vitunguu ambayo kwa kitaalamu huitwa Allium sativum. Jamii hii ilianza kutumika katika mabara mbalimbali duniani hususani Asia, Afrika na Ulaya takribani miaka 6000 iliyopita. Matumizi makuu nyakati hizo yakiwa viungo katika mboga na tiba.

Kitunguu swaumu kimetajwa kwenye vitabu mbalimbali vya dini vikielezea faida zake katika kutibu maradhi mbalimbali yasababishwayo na bakteria, matatizo katika mapafu, matatizo katika mfumo wa umen'genyaji chakula, na matatizo ya kuishiwa nguvu.

Historia inaonesha kuwa, vitunguu swaumu vilianza kutumika China mwaka 510 K.K na pia vilitumiwa na wanajeshi wa Ugiriki na Roma. Aidha wasafiri wa vyombo vya baharini na vijijini pamoja na wakulima barani Afrika walivitumia sana.

Mwaka 1858, mtafiti na mwanasayansi wa nyakati hizo, Louis Pasteur aligundua uwezo wa kitunguu swaumu katika kuua vimelea mbalimbali vinavyosababisha magonjwa, na hivyo vikaanza kutumika kama dawa ya kusafishia vidonda na kuzuia kidonda ndugu hasa zama za vita ya kwanza na pili ya dunia. Isitoshe, mpaka sasa zipo dawa kadhaa zilizotengenewa kwa kutumia jamii hii ya vitunguu swaumu ikiwemo dawa ya kusafisha mdomo (mouth wash) ingawa watumaiji wake wengi huilalamikia dawa hiyo kwa sababu ya harufu mbaya ya dawa hiyo inayowasababishia kunuka kwa mdomo.

Faida za vitunguu swaumu

Katika tafiti mbalimbali vitunguu swaumu vimeonekana kuwa na uwezo wa kutibu maambukizi ya bakteria, fangasi na virusi vya aina mbalimbali. Aidha husaidia kuzuia magonjwa ya moyo ikiwemo kuondoa lijamu katika mishipa ya damu na hivyo kusaidia katika kurekebisha shinikizo la damu. Faida nyingine za vitunguu swaumu ni pamoja na
Kutibu saratani ikiwemo saratani ya tumbo na utumbo mkubwa. Tafiti zinaonesha idadi ndogo ya wagonjwa wa saratani katika nchi ambazo wakazi wake wana utamaduni wa kutumia vitunguu swaumu kwa wingi.
Vitunguu swaumu husaidia kudhibiti kiwango cha sukari katika damu. Hata hivyo inashauriwa kwamba wagonjwa wa kisukari wanaotumia sindano za insulin wasitumie kitunguu swaumu kwa wingi mpaka watakaposhauriwa na daktari.
Huzuia kusanyiko la chembe sahani zinazosaidia kuganda kwa damu (platelet aggregation)
Husaidia ufyozwaji wa thiamin, hivyo kusaidia kuepusha mwili na ugonjwa wa beriberi
Ina kiasi kikubwa cha vitamini C ambayo husaidia kuzuia ugonjwa wa kiseyeye
Hutumika kutibu magonjwa nyemelezi kama toxoplasmosis, hasa kwa watu wenye upungufu wa kinga mwilini.

Ushahidi wa Kitafiti
Katika utafiti uliofanyika nchini Czech ilionekana kuwa matumizi ya vitunguu swaumu yalisaidia sana katika kupunguza kusanyiko la lijamu (cholesterol) pamoja na mafuta yasiyofaa mwilini (low density lipoproteins) katika mishipa ya damu. Aidha, mwaka 2007 BBC iliripoti matumizi ya vitunguu swaumu katika kusaidia kumkinga mtumiaji dhidi ya aina fulani ya mafua iliyosababishwa na virusi.

Mwaka 2010, ulifanyika utafiti mwingine ambao ulijumuisha wagonjwa 50 wenye shinikizo la damu sugu ambalo lilikuwa ni vigumu kudhibitiwa hata kwa matibabu yaliyozoeleka ya dawa na njia nyingine. Kama njia ya kuchunguza ufanisi wa vitunguu swaumu katika kutibu shinikizo la damu, baadhi ya wagonjwa hao walipewa vitunguu swaumu wakati wengine walipewa dawa isiyohusika na matibabu ya shinikizo la damu (au placebo).

Ilionekana kuwa wale waliopewa vitunguu swaumu kama dawa ya shinikizo la damu walionesha maendeleo mazuri kwa vitunguu swaumu kuweza kushusha vizuri kiwango cha shinikizo la damu, hususani systolic pressure, tofauti na wale waliopewa placebo.

Nini siri ya kitunguu swaumu?
Sifa kuu zinazokifanya kitunguu swaumu kuwa na uwezo na faida zilizoainishwa hapo juu ni kule kuwa kwake na viasili kadhaa (ingredients) ambavyo vinafanya kazi tofauti tofauti. Uwezo wake wa kiutendaji unatokana na mambo yafuatayo;

Vina uwezo wa kusababisha kutanuka kwa mishipa ya damu (vasodilation) kwa kubadilisha polysulfides zilizopo ndani yake kuwa hydrogen sulfides kwenye seli nyekundu za damu.
Husaidia uthibiti wa kiwango cha sukari mwilini kwa kushusha kiwango cha kemikali ya homocystine na kupunguza madhara ya kisukari.
Iwapo vitapondwa pondwa vizuri, vitunguu swaumu hutoa kemikali iitwayo Allicin ambayo ni dawa dhidi ya bateria, na phytoncide ambayo huua fangasi wa aina mbalimbali.
Harufu mbaya ya kitunguuu swaumu hutokana na gesi aina ya hydrogen sulfide ambayo inayotolewa baada ya kuvila.


Nini Madhara ya vitunguu swaumu?

Ukiacha faida zake, vitunguu swaumu pia vina hasara na madhara mbalimbali kwa mtumiaji. Madhara hayo ni pamoja na;

Harufu mbaya mdomoni ambayo hutokana na kemikali ya AMS (allyl methyl sulfide). Harufu mbaya hii, hata hivyo, yaweza kupunguzwa kwa kunywa maziwa au kunywa maji mengi.
Kwa baadhi ya watumiaji, vinaweza kuwaletea mzio au mcharuko mwili (allergies au inflammatory reactions)
Kichefuchefu, Kutapika na kuharisha.
Huweza kusababisha hatari ya kuvuja damu, kwa sababu huzuia kazi ya seli sahani (platelets) zenye kusaidia kuganda kwa damu kushindwa kufanya kazi yake vizuri, na hususani kwa mama wajawazito, baada ya upasuaji au mara baada ya kujifungua.
Huingiliana katika utendaji kazi wake na dawa kadhaa kama vile warfarin, antiplatelets, saquinavir, dawa za shinikizo la damu kwa ujumla hasa calcium channel blockers, na antibiotiki za jamii ya quinolone kama vile ciproflaxacillin.
Aidha, vinaelezwa pia kuwa na madhara kwa wanyama jamii ya paka na mbwa.

Usikubali Kuogopa Kumuonyesha Mke au Girlfriend Wako Unampenda Kisa Unaogopa Washkaji Watakuona Bwege

$
0
0
Usikubali kuogopa kumuonyesha mke wako au girlfriend wako unampenda kisa unaogopa washkaji au ndugu watakusema umekaliwa naye.

Ni tabia mbaya sana unakuta mtu mzima eti anajitamba mbele za wanaume eti "mimi bwana mwanamke hawezi niuliza niko wapi" sasa ndugu yangu wewe ndio ulimtongoza mwenyewe tena ulimsumbua hasa msichana wa watu leo hii anakupigia simu anakuuliza uko wapi unaanza kupanic.

Tusifanye vitu ili kuwaridhisha washkaji huko viringeni...tufanye vitu kuwaridhisha wake zetu.... imefikia wakati mwanaume usipokaa bar mpaka saa nane au saa saba usiku unaonekana bwege na ukiangalia ligi ya ulaya sebleni kwako na mke wako unaonekana bwege pia...au usipokua na demu wa nje eti wewe sio mjanja. huu ni upuuzu tubadilikeni jamani. ndio sikatai usikae na washkaji lakini usipitilize sasa.

Naona huruma sana unakuta mtu kavaa lipete likuuubwa la ndoa amekaa bar kwenye kiti anasinzia..jamani ?

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Mbunge Lema Alichambua Bunge Kama Karanga...Adai Limeshindwa Kusimamia Serikali

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA) amesema kazi ya Bunge ni kuisimamia serikai.

Lema, Jana Mei 12 amedai kuwa Tanzania kazi ya Bunge ni kusimamiwa na serikali huku akiwata wananchi kuelewa hivyo.

“Kazi ya Bunge ni kuisimamia Serikali,Tanzania kazi ya Bunge ni kusimamiwa na Serikali,hivi ndivyo wananchi wanapaswa kuelewa,Bunge ambalo haliwezi kusimamia haki ya Mbunge aliyepigwa risasi kupata haki yake,bunge hilo halitaweza kujua shida zenu za maji hata kama mnakufa na kiu,” ameandika Lema kupitia mtandao wake wa Kijamii.

Romy Jones Anogewa...Afunguka Kutoa Album Kabisa

$
0
0
Official Dj wa msanii Diamond Platnumz, Romy Jones amesema baada ya kuachia ngoma nne itafuata albamu.

Akiongea na BBC Swahili amesema kuwa albamu itajumuisha wasanii kadhaa ambao hakuwataja majina pamoja na Diamond Platnumz.

“Nadhani nitaitambulisha hivi karibuni, baada ya miezi miwili inayokuja nitaachia ngoma ya pili, ya tatu, ya nne na albamu, ” amesema.

Romy Jons/Rj The Dj kwa sasa anatamba na ngoma yake ya kwanza kutoa inayokwenda kwa la Bora Iwe ambayo amefanya na Barakah The Prince.

Simba ya Leo sio Ile ya Mwaka Jana..Waweka Rekodi ya Kutopoteza Mchezo Hata Mmoja

$
0
0
Kikosi cha Simba kimefanikiwa kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1 – 0 ugenini dhidi ya Singida United uwanja wa Namfua na kuendeleza ubabe wake wakutokupoteza.

Mabingwa wapya wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara Simba wanaifunga Singida United kwa mara ya pili sasa baada ya mchezo wa kwanza uliyopigwa jijini Dar es Salaam kuibuka na ushindi wa mabao 4 – 0.

Mfungaji pekee wa bao la leo la klabu ya Simba ni Shomari Kapombe dakika ya 24 kipindi cha kwanza na hivyo kuwafanya mabingwa hao wapya kutopoteza hata mchezo mmoja mpaka sasa huku wakijikusanyia jumla ya pointi 68.

Kwenye mchezo mwingine uliyopigwa hii leo timu ya Kagera Sugar imeibuka na ushindi wa jumla ya mabao 3 – 1 dhidi ya Njombe Mji na kufikisha jumla ya pointi 31 wakiwa nafasi ya 10 wakati vijana wa njombe wakiburuza mkia kwakuwa na alama 22 nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi.

Ray C "Nikipost Picha za Nusu Utupu Nitapelekwa Jela na Magufuli"

$
0
0

Mwanamuziki wa kike bongo ambaye aliwahi kutikisa Afrika Mashariki kwa sauti yake na kiuno chake laini, Rehema Chalamila au Ray C, amesema anaogopa kupost picha za utupu kama wengine, akihofia kufungwa na serikali.


Ray C ametoa kauli hiyo akiwa nchini Kenya na kuulizwa juu ya wasanii wanaopost  picha za utupu na kwa nini yeye hapost, na kusema kwamba serikali imeona hali ilikuwa mbaya na kuamua kupiga marufuku tabia hiyo, hivyo iwapo atafanya hivyo huenda akafungwa jela.

“Inakuwa too much ndio maana Rais Magufuli kakataza, si unajua baba yetu mkali kidogo!! It was too much, ilikuwa inaanza kwenda mbali, unajua watoto wanaangalia, ingawa watu wanaendelea, nitapelekwa jela na Magufuli nikifanya hivyo”, amesema Ray C.

Msanii huyo yupo nchini Kenya kwa ajili ya kazi zake za muziki, ambapo pia amepata fursa ya kufanya collabo na msanii wa muziki wa injili Papa Denis.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images