Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Mwakyembe awapa changamoto wateule wake

0
0

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, amewapa changamoto wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Michezo Malya, ambao amewateua hivi karibuni ya kuhakikisha wanawasaidia vijana wenye ari ya michezo.


Mwakayembe ametoa changamoto hiyo kwenye uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanyika mapema leo Mei 15, kwenye chuo hicho huko Malya, Kwimba, Mwanza. Amesisitiza kuwa wanatakiwa kujitoa kwaajli ya kuhakikisha taifa linapiga hatua katika michezo.

"Nataka niwaambie wajumbe wa Bodi hii changamoto ya kwanza inayowakabili ni kuhakikisha taasisi hii yenye wajibu adhimu katika maendeleo ya michezo mnaitangaza na kuiongezea thamani ili iweze kuhudumia Vijana wenye ari ya kupata ujuzi katika michezo", amesema.

Aidha Waziri Mwakyembe ameeleza kuwa ndoto yake ni kukiona chuo cha Malya kinakabiliwa na mafuriko ya wanachuo kuliko uwezo wake ili waweze kuingia makubaliano yenye tija na taasisi za kifedha na wadau wa michezo kuwekeza kwenye viwanja vya michezo na walimu zaidi.

Chuo cha Malya ndio chuo pekee nchini kilicho chini ya serikali amabcho kinatoa elimu ya michezo kwenye maeneo tofauti ikiwemo Uongozi kwenye taasisi za michezo pamoja mafunzo ya waamuzi.

Msinione Hivi Mimi Nimewahi Kuwa Chawa wa Barnaba - Benpol Afichua Siri

0
0
Msanii wa Muziki wa 'RNB' Benpol anayefanya vizuri na wimbo wake wa 'Natuliza boli' amesema amewahi kuwa chawa wa Barnaba kipindi anaanza safari yake ya muziki.


Benpol amesema hayo katika kipindi cha E-news kinachorushwa na EATV ambapo amemtaja Barnaba kuwa ni msanii ambaye amekuwa msaada kwake wakati anaanza harakati za kuimba muziki na amemsindikiza sehemu nyingi ikiwemo studio.

“Kitu ambacho hamjui mimi na Barnaba urafiki wetu umeanza muda mrefu kwani kupitia yeye nimejifunza vingi na nilikuwa naongozana nae sehemu nyingi kama ambavyo vijana wa leo wanaita ‘chawa’ basi mimi nimewahi kuwa chawa wa Barnaba”. Amesema Benpol

Hivi Karibuni Benpol kupitia ukurasa wake wa Instagram alipost picha ikionesha mazungumzo yake na Barnaba kwa njia ya ‘Videocall’ na kuandika “Was on a video call with my Blood, alikuwa ananiambia kuwa wimbo wetu tulioufanya umekamilika na umekuwa noma sana!!! Love you Bro, Asante sana!! always nice to talk to you”. Aliandika Benpol

Serikali yakanusha Tuhuma za Ubaguzi Mikopo vyuoni

0
0
Serikali imekanusha kuhusu tuhuma za kwenye sera ya elimu ya mwaka 2014 kuwa ni ya kibaguzi kwa wanafunzi nchini hasa kwa wale wanaosoma kwenye shule za binafsi na kusema kuwa yote wanayofanya ikiwepo kutotoa mikopo kwa wanafunzi wote ni kutokana na ufinyu wa bajeti.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha, wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea kuhusu vigezo vinavyotumika na serikali kuwanyima mkopo wanafunzi waliosoma shule za binafsi, huku akieleza kuwa sera ya elimu imefanya ubaguzi.

"Tunachoangalia ni nani mwenye uhitaji zaidi, sio suala la kibaguzi, bajeti ni iliyopo ndogo wahitaji ni wengi. Kwa wanafunzi waliopata bahati ya kusomeshwa na wafadhili shule binafsi serikali haiwanyimi mikopo tutahitaji ushahidi kweli walifadhiliwa". - William Ole Nash

Aidha Mhe. Ole Nasha ameongeza "Kuhusu watoto ambao wamesoma shule binafsi kutoruhusiwa kupata mikopo ni suala la kuangalia kati ya mtu ambaye ameweza kulipa milioni 3 au 4 ya shule ya msingi na sekondari na yule ambaye hakuweza, ni yupi utampa kipaumbele kupata mkopo, sio tunabagua".- William Ole Nasha

Sheria Yawabana Wanandoa Kenya, Hakuna Kugawana 50/50 Mkiachana

0
0
Nchini Kenya kumekuwa na mjadala mkubwa juu ya ugavi wa mali pindi wanafamilia wanapopeana talaka, jambo kubwa likiwa ni iwapo wanandoa wanatakiwa kugawana mali nusu kwa nusu wanapoachana kwa talaka au la?.

Jaji wa mahakama kuu nchini humo John Mativo amepinga wanandoa kugawana mali nusu kwa nusu wanapo achana kwa talaka uamuzi ambao wengi wameuchukulia kama pigo kwa haki za wanawake.

Uamuzi huo umetokana na sheria ya ndoa nchini humo ambayo hata hivyo imekuwa ikipingwa na shirikisho la mawakili wanawake Kenya FIDA wakidai kuwa sheria hiyo inawanyanyasa wanawake.

Ombi la FIDA limekataliwa na mahakama kwa madai kuwa kuruhusu kugawana mali nusu kwa nusu kutatoa mwanya kwa watu kuingia katika ndoa kwa lengo la kujinufaisha.

Mahakama imesema sheria haiwanyanyasi wanawake kwasababu umauzi huu pia utakuwa na manufaa na kuwalinda wale wanaofanya kazi kwa bidii katika familia.

Yaliyonikuta Jana Siwezi Rudia Kumpigia Simu Mwanamke Yoyote Usiku

0
0

Yaliyonikuta jana siwezi rudia kumpigia simu mwanamke yoyote usiku

Kuna msichana nilikuwa namchukulia kama dada kwa sababu ni dada wa rafiki yangu na tumekuwa tukipigiana simu ata usiku yeye pia amekuwa akinitumia ujumbe ata usiku ikawa mazoea.

Jana usiku wa saa nne nikampigia simu nimwambie wikend njema,akapokea simu mwanaume anaongea kama watu wa Arusha.

Alivyosikia sauti ya kiume tu bila kuuliza mi ni nani alinifulumishia matusi ya nguoni sana na kuniambia yeye anaenjoy kifuani mimi naangaika kupigia simu wake za wengine.

Akanitukania mama yangu,na matusi mengine makali, nilijitahidi kumwambia siwez rudia kupiga simu sababu sikujua kama ana mwanaume.Na pia nikamwambia uyo ni kama dada yangu lakin hakunielewa .uyo rafik yangu amekuwa akiniambia yuko single hana mtu.

Siwezi rudia kumpigia simu rafik yangu yoyote wa kike usiku.mwisho itakuwa saa 12 jioni.Matusi niliyotukanwa ni makubwa.

Viwanja vinauzwa Bunju

0
0

VIWANJA VIKUBWA vinauzwa: BUNJU
Viwanja viko Kimele, km 5 kutoka Bunju sokoni. Vipo viwanja vya ukubwa huu: Eka 1 (64/64) bei mil 40, Nusu eka (32/64) bei mil 20, Robo eka (32/32) bei mil 10, sqm 800 (20/40) bei mil 8, sqm 600 (20/30) bei mil 6
Viwanja vinafaa kujenga (kuishi) na kufuga pia.
call/watsap 0757489709

Wasiliana na Mtaalam wa Dua na Dawa za Kiarabu na Asili Dr Sharifu Lukumani

0
0
YULE MTAHALAM WA DUA NA DAWA ZA KIARABU NA ZA KIASILI YANI MITI SHAMBA SHARIFU LUKUMANI SASA YUPO HEWANI WENYE SHIDA ZITUATAZO CHEO KAZINI,KUONGEZEWA MSHAHARA KAZINI,MWENYE TATIZO LA NGUVU ZA KIUME,ALIEPOTELEWA NA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA, MWENYE KIFAFA,KISUKARI,FANGASI SEHEMU ZA SIRI KWA WALE WENYE MIILI MINENE MTOTO WA JICHO PAMOJA NA WALE WAKINA MAMA WANAOSUMBULIA NA CHANGO LA UZAZI PUMU YA MUDA MREFU WANAWAKE KUJAA MAJI SEHEMU ZA SIRI MWANAUME KUWAI KUFIKA KILELENI AU KUTOA MANII MFANO WA MAJIMAJI YAKIWA MEPESI AUTOWEZA KUMPA MKEO UJAUZITO JAMBO HILI LINAWASUMBUA WANAUME WALIO WENGI DUNIANI KWA KAWAIDA WANAUME ASIE NA TATIZO HILI UTOA MANII MAZITO NDIO YENYEUWEZO WA KUMPA MWANAMKE MIMBA.MWANAUME KUPATA MPENZI KWA ULAISI PASIPO NA GHARAMA YOYOTE YANI KWA WALE MADOMO ZEGE KUWA NA UWEZO WA KUSIKILIZWA HATAKAMA RAIA WA INCHI GANI NA UWEZO WA KURUDISHA MPENZI ALIE POTEA NA KUMFANYA AWE WAKO KWA WALE WASIO TAKA MITALA PIA UFANYA KAZI YA KUNG'ALISHA NYOTA SASA MATATIZO YAKO YAMEPATA SULUHISHO ANAPATIKA KWA MASAA ISHIRINI NA NNE

WASILIANA NAE KWA NAMBA 0762899488-0656145170

WhatsApp namba +255620665635

Kiongozi wa Kundi la Kigaidi la ADF Uganga Aliyekamatwa Tanzania Afikishwa Mahakamani

0
0
Kiongozi wa kundi la waasi la Allied democratic forces Jamil Mukulu, amefikishwa Mahakamani Kuu inayohusika na uhalifu wa kimataifa mjini Kampala, Uganda, Jumatatu miaka 3 baada ya kukamatwa nchini Tanzania.

Kikao cha mahakama cha jana Jumatatu  kilikuwa cha kushauriana jinsi kesi dhidi ya Mukulu na wenzake 38 itaendeshwa.

Akiwa amefungwa pingu mikononi na minyororo miguuni, Jamil Mukulu na wenzake 38 walifikishwa mahakamani chini ya ulinzi mkali wa kikosi cha polisi cha kupambana na ugaidi.

Washukiwa hao waliendelea kufungwa pingu na minyororo hata baada ya kuwa tayari wako ndani ya mahakama hiyo.

Kwa mwongozo wa Jaji Eva Luswata, kikao cha jana  Jumatatu kilikuwa cha kutoa fursa kwa wasimamizi wa mashtaka kuishawishi mahakama kwamba Jamil Mukulu na wenzake, wana kesi ya kujibu kuhusiana na ugaidi ndani ya Uganda.

Upande wa mashtaka umeieleza mahakama kwamba kwa mda mrefu, tangu mwaka 1986, Mukulu, akiwa kiongozi wa kundi la allied democratic forces – ADF, alikuwa akisajili wapiganaji, kutekeleza mauaji, wizi wa kimabavu, kutoa mafunzo ya ugaidi na kutekeleza ugaidi, kujaribu kuua, kuteka nyara na kushirikiana na makundi mengine ya kigaidi kutekeleza mauaji katika nchi za Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Washukiwa wamefuatilia kikao cha mahakama kwa msaada wa wakalimani katika lugha ya Kiswahili na lugha zingine asili kama lusoga, lugisu na Luganda.

Jamil Mukulu, anaripotiwa kupokea mafunzo ya moja kwa moja na aliyekuwa kiongozi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda Osama Bin Laden, upande wa mashtaka umeeleza.

Pia wamesema kuwa , mshukiwa huyu aliwahi kushiriki katika vita nchini Afghanistan. Video iliyotolewa na jeshi la Uganda UPDF inaonyesha kundi la ADF likiwa linafanya mazoezi katika misitu ya DRC kwa kutumia silaha nzito.

Mukulu alikamatwa mnamo mwaka 2015 akiwa nchini Tanzania kabla ya kurejeshwa nchini Uganda, ambako alikuwa akitafutwa kwa mda mrefu na kukwepa mitego ya maafisa wa usalama. Alifanikiwa kuhepa mitego ya maafisa wa usalama kwa kutumia majina bandia Zaidi ya 11 kwenye stakabadhi zake.

Alipokamatwa alipatikana na zaidi ya pasi za kusafiria 10 za nchi tofauti ikiwemo Uganda, Tanzania, Kenya na Uingereza.

Zifahamu Faida 5 za Kununiana na Mpenzi Wako Ndani ya Mahusiano ya Ndoa au Uchumba

0
0
Mapenzi yana wigo mpana mno ambao mtu anapaswa kuuangalia kwa jicho pana na akili pembuzi kabla ya kuingia, namaanisha kwamba ni lazima kuchunguza kina cha maji kabla ya kuzamia. Sasa basi, zifuatazo ni faida tano utakazozipata ukiwa umenuniana na mpenzi wako.

HUSAIDIA KUPUNGUZA MIGOGORO
Ni ukweli usiopingika kuwa, katika hali ya kawaida, ukiwa mbali na mtu fulani katika jamii unayoishi ni vigumu sana kujikuta umekwaruzana naye. Hii ni kwasababu utakuwa hauingiliani naye katika mizunguko yako, vivyo hivyo kwa wapenzi walionuniana.

Hali hii hupunguza kabisa migogoro ya hapa na pale, kwani hiki ni kipindi ambacho mtakuwa mbalimbali jambo ambalo huepusha maudhi ya kibinadamu.

Mfano, yawezakana katika kipindi mlichonuniana na mpenzi wako, uliingia ujumbe wa mapenzi kwenye simu yake kutoka kwa mtu aliyekosea namba. Kwa kuwa hauko naye karibu jambo hili halitakuumiza maana hutaelewa nini kimeendelea tofauti na kama ungelikuwa naye karibu.

Kwa hiyo kuna baadhi ya maumivu na maudhi ambayo utaepukana nayo kwa kipindi cha kununiana kwenu. Ni kweli kabisa kwamba hupunguza migogoro na mitafaruku ya hapa na pale, umeelewa mpenzi msomaji wangu? Haya twende kwenye faida ya pili.

KUBAINI TABIA X ZA MWENZAKO
Hiki ni kipindi ambacho sasa kitakusaidia wewe kubaini tabia na mienendo mibaya ya mwenzi wako. Hii ni kwa kuwa utakuwa mbali naye hivyo naye hujiona kuwa yuko huru kufanya jambo lolote analoona kuwa linafaa bila kujali uwepo wako kwani kila mtu hana ‘time’ na mwenzake.

Kama kuna asili ya maisha yake ambayo aliiacha baada ya kuingia katika uhusiano na wewe, ambayo ni mbaya zaidi sasa hapa ataanza kuirudia kwa kujiona kuwa hana mtu wa kumzuia na kumbana.

Kama ni mlevi kupindukia, mchafu, muongo na tabia nyingine mbaya za kufanana na hizi basi ataanza kuzionesha katika kipindi ambacho mmenuniana.

KUPATA MUDA WA KUTAFAKARI ZAIDI
Hapa naomba nieleweke vizuri kabisa kwamba, ninapoongelea suala la kutafakari zaidi katika kipindi ambacho wewe hauna maelewano mazuri na mwenzi wako, namaanisha kuwa utapata muda mzuri zaidi wa kutafakari penzi lenu kwa ujumla.

Ni kipindi kitachokuongoza wewe kuwa na uelewa wa ni aina gani ya mpenzi uliyenaye. Kivipi? Ni kwamba, katika muda huu mara nyingi utataka kupata suluhu ya kununiana kwenu, lakini pia katika kutafuta suluhu hiyo utapata fursa ya kutafakari kwa kina juu ya penzi lenu huku ukimpima mwezi wako kwa mtazamo chanya.

KUFAHAMU AINA YA MARAFIKI ZAKE
Si kila rafiki wa mwenza wako ana nia nzuri na uhusiano wenu au anafurahia penzi lenu. Mathalani, labda wewe ni msichana na pengine miongoni mwa rafiki zake kuna mmoja au wawili ambao hutamani sana kupata penzi lako.

Sasa katika kipindi ambacho utakuwa umenuniana na mpenzi wako basi itakuwa ni nafasi nzuri kwao kuitumia kunyunyizia sumu ya kumponda huku wakikutamkia maneno ya kukushawishi, hivyo utakuwa umeelewa ni aina gani ya marafiki alionao mwenzi wako.

Hii si kwa msichana tu, hata kwa wanamume kwani huenda kati ya rafiki wa ‘girlfriend’ wako, kuna wanaokutamani, sasa wakiona huna uhusiano mzuri na mpenzi wako, watatumia nafasi hii kukuambia maneno ya uongo juu yake na kukuonesha kila dalili za kukutaka.

Hivyo utakuwa umefahamu ni aina gani ya rafiki ambao mpenzi wako anao. Tambua kwamba, marafiki wengi wana tabia zinazofanana.

KUBAINI AINA YA PENZI ALILONALO KWAKO
Katika kipindi hiki, utaweza kuelewa ni aina gani ya penzi alilonalo huyo mtu wako juu yako. Kwa mpenzi aliye na hisia za dhati kabisa kwako, katika kipindi hiki atakuwa ni mtu wa kutafuta njia ya kupata suluhu ya tatizo lenu.

Pamoja na kwamba wewe utakuwa umenuna, bado yeye ataonesha kukujali kama kawaida, atakupigia simu za hapa na pale yaani ilimradi tu asikie angalau sauti yako, lengo lake likiwa ni kutaka kurejesha ukaribu ambao sasa anaona kama akiupoteza itakuwa ni maumivu kwake.

Kwa mantiki hiyo basi, utagundua ni kwa jinsi gani anathamini penzi lenu na ni aina gani ya penzi alilonalo kwako. Yote haya utabahatika kuyajua kupitia kipindi cha kununiana kwenu.

Hata hivyo, niwatahadharishe kwamba, kuandika haya isiwe ni tiketi ya wewe sasa kuanza kununiana na mpenzi wako eti kwa kigezo kwamba utapata nafasi ya kumfahamu, la hasha!
Siku zote katika uhusiano wako epuka maudhi na migogoro isiyokuwa ya lazima.

Kesi ya Kina Mbowe na Wenzake yasikilizwa leo...Hicho ndio Kinaendelea

0
0

KISUTU, DAR: Kesi ya kufanya mikusanyiko isiyo halali inayowakabili viongozi 9 wa CHADEMA, imeendelea tena leo Mei 15, 2018 Mahakamani hapo
-
Katika kesi hiyo Mahakama imetupilia mbali ombi la upande wa utetezi la kutaka kesi hiyo kupelekwa Mahakama kuu
-
Hakimu anayeendesha kesi hiyo, Wilbard Mashauri amesema usikilizaji wa awali utaanza rasmi kesho Mei 16, 2018 saa nane mchana
-
Wakati kesi hiyo ya jinai namba 112 ya mwaka 2018 ikisomwa leo, mshtakiwa wa 7, Halima Mdee na mshtakiwa wa 9 Ester Bulaya hawapo mahakamani
-
Wakili wa utetezi, Peter Kibatala ameieleza Mahakama kuwa sababu ya washtakiwa hao kutokuwapo imetokana na usafiri waliokuwa wanatumia kutoka bungeni kuelekea Dar kuwa na tatizo

Muigizaji wa Filamu Bongo Rammy Galis Kumpa Mtoto wa Masogange Fungu la Pesa

0
0

Muigizaji wa filamu bongo Rammy Galis ambaye aliwahi kuwa kwenye mahusiano na video vixen Agness Gerald aliyefariki hivi karibuni, amekusudia kumpa fungu la pesa Sania mabye ni mtoto wa Agness aliyemuacha, mara baada ya kuzindua filamu yake aliyoigiza naye.

Akizungumza na Big Chawa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Rammy amesema kiasi hiko cha pesa atahakikisha anakamkabidhi mwenyewe mtoto Sania, ambayo ni stahiki yake kutokana na kazi aliyoifanya marehemu mama yake kwenye filamu ya 'Hukumu' waliyoigiza. “Kwanza nisingependa kutangaza rasmi kiasi ambacho kitamfikia kwa sababu sijui filamu mauzi yake yatakuwaje, lakini mimi kama Ramy Galis nitatoa kile ambacho Mungu atanibariki kupitia filamu hii, kutakuwa na asilimia kadhaa ambazo nitaziweka kwa niaba ya mtoto, na nitakaa chini na famlia ya mtoto wa pande zote mbili watakapokubaliana na sio nibaki nazo mimi, ni haki ya yule mtoto”, amesema Rammy Galis.

Sambamba na hilo Rammy Galis amesema filamu hiyo anakusudia kufanya uzinduzi wake mkoani Mbeya ambako Agness ametokea, na anasubiri msiba upite kabisa ili watu wasije wakasema amefuata kiki ya msiba kufanya kazi zake.

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya May 16

0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya May 16

Mbunge "Ampa Makavu" Waziri wa Kilimo Bungeni

0
0
Mbunge wa Viti MaalumuCCM), Mariamu Ditopile amesemaa Waziri wa Kilimo,  Dk Charles Tizeba amemdanganya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuhusu ununuzi wa tumbaku.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka wa fedha 2018/19 bungeni leo Mei 15, 2018, amesema Dk Tizeba amemdanganya Majaliwa kwamba wanunuzi wa zao hilo walitaka kununua chini ya dola za kimarekani  0.8.

“Haujatusisimua (kwa bajeti yake) nothing (hakuna kitu),  utashi wako upelekee kukua kwa uchumi wa viwanda lakini  wewe ndiyo unavuruga.

Wanunuzi wanataka kununua Tumbaku kwa dola 1.3 (za kimarekani) lakini wewe unakataa, ukamlisha tango pori waziri mkuu,”amesema.

Amesema ukweli ni kwamba wanunuzi hao walitaka kununua  tumbaku kwa Dola 1.3 ya Marekani lakini waziri wa kilimo alikataa bei hiyo na matokeo yake akasababisha hasara kwa wakulima.

“Wale wakulima hawana vihenge, mvua iliponyesha tumbaku yao ilinyeshewa na mvua matokeo yake wamekuja kuuza chini ya dola 0.8 ya Marekani walichokipata walitumia kulipa madeni,”amesema.

Akizungumzia zuio la kuuza mahindi nje ya nchi, Mariamu amesema: “Mheshimiwa waziri wewe ni swahiba wangu lakini uswahiba wangu hauuzidi wa wakulima. Najua wakulima wanavyotoa jasho na machungu wanayoyapata. Mahindi tunalima kwa ajili ya chakula na biashara. Tumezalisha kwa zaidi ya asilimia 120.”

Hata hivyo, amesema wakulima hao wamekosa soko la mahindi baada ya Serikali kuzuia uuzaji wa mahindi nje ya nchi na kwamba yeye ni mmoja wa waadhirika ambaye amelazimika kuyatupa mahindi baada ya kukosa soko.

Mariamu amesema kuwa wizara hiyo imeleta miche ya mikorosho mkoani Dodoma lakini hakuna mafunzo yaliyotolewa kwa maofisa ugani wala wakulima na kushauri ni vyema Serikali ikawa na mpango wa mazao wa kikanda.

Amesema pia, waziri huyo amekuwa akiwachanganga wakulima kwa kusema kuwa dawa ya kuulia wadudu ya sulpher itatolewa bure kwa wakulima wa korosho lakini baadaye anawataka kulipia.

“Mliombwa mtoe bure? Waliwaambia shida yao ni sulpher? Ghana wameweka mpango baada ya miaka 10 watakuwa wakizalisha korosho ya kutosha. Sisi tunampango wa kulifanya zao hili kuwa endelevu?”amehoji.

Amesema iwapo zao hilo la korosho mkoani Dodoma litastawi kwa asilimia 10 atajiuzulu ubunge.

Mbunge CCM amwaga Machozi bungeni

0
0
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Jacqueline Ngonyani  ‘Msongozi’ ametoa chozi bungeni akiitaka Serikali kuwalipa mawakala wa pembejeo na kuacha kutumia kivuli cha uhakiki wa madeni hayo kutoyalipa.

Akichangia bajeti ya kilimo, leo Mei 15, 2018 bungeni, Msongozi amesema madai hayo yamedumu kwa zaidi ya miaka minne huku baadhi wakifariki kabla hawajalipwa.

“Nashangaa sana mawakala wa pembejeo wanadai miaka minne, walihudumia wakulima wetu na walikwenda kukopa fedha katika taasisi, ambazo sasa zinawadai,” amesema Msongozi.

Huku akishangiliwa na wabunge, Msongozi amesema, “Serikali imekuwa inajificha katika kichaka cha uhakiki, kwa nini hawawalipi? Serikali imekwenda kujificha katika uhakiki, ni uhakiki wa aina gani? Kuna watu wanakufa bila kupewa fedha zao.”

Msongozi akizungumza kwa sauti yenye kuashiria kulia huku mkono wake akiupeleka kufuta uso wake, amesema, “katika nchi hii watu wanatafuta haki zao, kama wameiba kwa nini wasipelekwe mahakamani, kwa nini hawapewi fedha zao, uhakiki gani, mbona watumishi siku mbili walihakikiwa? Kwa nini huku katika mawakala hawalipwi fedha zao.”

Amesema kuna kijana alitaka kujinyonga kwa kudaiwa na taasisi jambo ambalo amesema Serikali ichukue hatua ya kulipa madai kwani wako mawakala saba wamepoteza maisha.”

Msongozi amekuwa mbunge wa tatu kutoka CCM kutokuunga mkono bajeti hiyo akitanguliwa na Richard Ndassa (Sumve) na Mashimba Ndaki (Maswa Magharibi).

Mbunge CHADEMA Aishambulia CCM Bungeni

0
0
Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Cecilia Paresso amesema wakulima wanatakiwa kutambua kuwa adui yao namba moja ni chama tawala, CCM akisema haiwezekani asilimia 75 ya Watanzania wanaotegemea kilimo, lakini imeshindwa kuwasaidia.

Amesema  Serikali imeshindwa kuwekeza fedha za kutosha katika kilimo huku kwa upande wa asilimia tano ya Watanzania wanaotumia usafiri wa anga ndege zimenunuliwa.

Paresso ametoa kauli hiyo leo Mei 15, 2018 katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Kilimo mwaka 2018/19 ambapo wizara hiyo imeomba kuidhinishiwa Sh170.2bilioni.

Amesema  kwa mujibu wa taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zinaonyesha ukuaji wa sekta ya kilimo mwaka 2011 ilikuwa asilimia 1.9, mwaka 2012 (3.2), mwaka 2013 (4), mwaka 2014 (3.4), mwaka 2015 (3.2), mwaka 2016 (1.9) na mwaka 2017 kwa asilimia 1.3.

“Sekta hii kama itawekeza vizuri itatoa ajira, kuondoa umasikini na tutafikia hicho mnachosema uchumi wa viwanda, lakini sekta hii imekuwa haipewi fedha kama inavyotakiwa na fedha tunazozitenga hazifiki,” amesema Paresso.

“Serikali ya Awamu ya Nne inaondoka madarakani iliacha kilimo kinakua kwa asilimia 3.2, ila hii Serikali ya Awamu ya Tano inayojiita uchumi wa viwanda, kimeendelea kushuka na kufikia asilimia1.9.”

Amesisitiza, “wakulima wa nchi hii wanapaswa kujua adui yao ni Serikali, asilimia 75 wanategema kilimo lakini asilimia tano ya Watanzania wanaotegemea usafiri wa anga wanawepa ndege. Huku ni kuwahadaa wakulima ambao wanapaswa kujua Serikali ya CCM ndio adui yao.”

Mizengo Pinda Atoa Ushauri Kuhusu Tanzania ya Viwanda

0
0
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda amezitaka taasisi za elimu na mafunzo kuhakikisha mageuzi ya kiuchumi yanafanyika nchini kwa kutoa elimu.

Mhe. Pinda ametoa ushauri huo jijini Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Taaluma kuhusu nchi ya China kijulikanacho kama Centre for Chinese Studies yaani CCS, kituo ambacho ni sehemu ya taasisi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mh. Pinda amesema mageuzi ya kiuchumi hususani kupitia ukuaji wa sekta ya viwanda, yanahitaji kuwa na jamii inayopenda kufanya kazi kwa bidii na iliyo tayari kubadilika kifikra.

Uzinduzi wa kituo hicho umefanywa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt Augustine Mahiga, ambaye amesema Tanzania ina uhusiano mzuri na nchi ya China lakini inasikitisha kuona kwamba bado kama nchi haijatumia ipasavyo fursa ambazo taifa la China imezitoa kwa Tanzania.

Aidha kituo hicho kilichozinduliwa kimeelezewa kuwa  jukumu lake ni kukuza uhusiano kati ya China na Tanzania pamoja na kutumia mafanikio iliyoyapata nchi ya China kwa ajili ya kuharakisha mageuzi ya kiuchumi.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Ukiuza sukari zaidi ya 2600 Arusha Jiandae Kulala Selo

0
0
Msako wa kamati ya ulinzi na usalama katika maghala ya wafanyabiashara wakubwa umebaini kuwa jijini Arusha kuna mafuta na sukari ya kutosha hivyo ni marufuku kupandisha bei.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 15, 2018 baada ya msako huo jana, Mkuu wa wilaya ya Arusha, Gabriel Daqarro amesema maghala yote ambayo wametembelea licha ya kuwapo uzalishaji mdogo wamebaini bado kuna mafuta na sukari.

"Kamati ya ulinzi na usalama wilaya imetembelea maghala na kuona bado kuna bidhaa na kwa sukari bado bei ya jumla mfuko wa kilo 50 ni kati ya Sh102,000 na Sh110,000,” amesema.

Amesema kutokana  na bei hizo bei ya kilo moja haipaswi kuuzwa zaidi ya Sh2,600 hivyo ambao watauza zaidi watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Daqarro amesema kuhusiana na sukari iliyofungwa bei pia haipaswi kuzidi Sh2,800 na taratibu zinafanywa kuhakikisha bei haiongezeki.

Kuhusiana na mafuta pia amesema yapo ya kutosha ikiwapo ya alizeti licha ya uzalishaji kupungua.

Baadhi ya wakazi  wa Arusha waliomba Serikali kuendelea kudhibiti kupanda bei ya mafuta na sukari hasa kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Jasmin Ally mkazi wa makao mapya amesema katika maduka mengi kati kati ya jiji sukari inauzwa kilo kati ya Sh2,700 na Sh2,800.

Hillal Kusena amesema bei ya mafuta na sukari inaendelea kupanda licha ya matamko ya Serikali.

"Serikali ingefatilia kujua tatizo ni nini kama ni kodi kubwa basi wapunguze lakini kutoa matamko tu hakutoshi," amesema Kusena.

Amesema bei ya mafuta ya kupikia bei ya jumla imepanda kutoka Sh 61,000 hadi Sh 70,000 kwa lita 20 huku lita 10 imepanda kutoka Sh 30,000 hadi Sh35,000.

Maalim Seif Aitaka Serikali Isamehe Baadhi ya Kodi Katika Kipindi Hiki cha Ramadhani

0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ameitaka serikali iliyopo madarakani visiwani Zanzibar inayoongozwa na Dkt. Ali Mohamed Shein iwahurumie wananchi hasa katika kipindi cha mfungo wa mwezi wa Ramadhani.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za CUF Vuga mjini Zanzibar, amesema kuwa waliopo madarakani wasiwe hodari kuwataka wafanyabiashara wasipandishe bei za bidhaa wanazouza lakini na wao kodi ambazo hazina tija, zinawakamuwa wananchi waweze kuzipunguza.

"Ni vyema kujifunza kwa serikali ya Kenya ambayo imeweza kuondoa kodi kwa wafanyabiashara wale wote ambao watafanya biashara ya tende katika Mwezi wa Ramadhani", amesema Maalim Seif.

Aidha, Maalim Seif amewataka wananchi kufanya mambo ya kheri katika mwezi huo na kuacha kulumbana, kutoleana maneno yasiyofaa kwani mwezi huo ni mwezi wa rehema hivyo ni vyema kufanya mambo ya kheri yanayompendeza Mungu.

"Ni vyema kupendana,kusaidiana, kuhurumiana,kuacha kugombana na kutohasimiana ili kupata fadhila za Mwezi Mungu", amesisitiza Maalim Seif.

Kwa upande mwingine, Maalim Seif amewataka wafanyabiashara wasiuchukulie kwamba mwezi wa Ramadhani kama ni msimu wa kupata faida ya kupindukia na badala yake wauchukulie ni mwezi wa kuchuma thawabu kwa lengo la kuwasaidia wananchi hasa masikini.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images