Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104688 articles
Browse latest View live

Skendo ya Kumtelekeza Mtoto, Mbasha Yamkuta ya Ali Kiba

$
0
0
DAR ES SALAAM: Mambo ni hivi! Achana na staa wa Bongo Fleva, Ally Salehe Kiba ‘Alikiba’ kuburuzwa mahakamani kwa kushindwa kutoa matunzo ya mtoto, mwimbaji wa Injili, Emmanuel Mbasha naye amekutwa na skendo kama hiyo baada ya kudaiwa kumtelekeza mwanaye mwenye umri wa miaka mitatu, Risasi Mchanganyiko linakuwa la kwanza kukuletea mkanda kamili.

 Chanzo makini kililieleza Risasi Mchanganyiko kwamba, hivi karibuni Mbasha aliburuzwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar na mama mtoto wake ambaye ni mjasiriamali anayejulikana kwa jina la Miriam Kawishe. Miriam alimlalamkia Mbasha kumtelekezea mtoto huyo waliyezaa pamoja aitwate Avantica kwa kutompa matunzo tangu azaliwe hadi hivi sasa ambapo ana umri wa miaka mitatu.

 “Unajua Mbasha naye ameburuzwa mahakamani kwa kesi ya kushindwa kutoa matunzo ya mtoto tangu alipozaliwa hadi sasa ana miaka mitatu na ilianza kutajwa wiki iliyopita huku ikitarajiwa kuendelea tena mwisho wa mwezi huu.“Ninyi mtafuteni huyo mzazi mwenzake atawaeleza vizuri,” kilisema chanzo hicho.

 Baada ya kupata habari hiyo, Risasi Mchanganyiko lilimtafuta mwanamama huyo aliyezaa na Mbasha, Miriam ambaye alikiri kwamba ni kweli, lakini hawezi kuzungumza sana kwani kwa sasa suala hilo liko mahakamani tayari pia ana wakili anayelisimamia.

 Wimbi la mastaa kudaiwa kutelekeza watoto na kushindwa kuwapatia matunzo limeendelea kuzidi kila kukicha ambapo lilianza kwa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kukataa kutoa matunzo kwa mtoto aliyezaa na mwanamitindo Hamisa Mobetto na kupelekeshana mahakamani.

Hivi karibuni Alikiba naye aliburuzwa mahakamani kwa skendo kama hiyo na mpaka sasa kesi yake inaendelea.

STORI: Mwandishi Wetu, Risasi Mchanganyiko

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0


Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Mwakyembe Noma, Afukua Utajiri wa Marehemu Kanumba

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk Harrison George Mwakyembe

SIFA anazomwagiwa Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk Harrison George Mwakyembe mitaani, zinatosha kusema kuwa waziri huyo ni noma katika uchapakazi wake.

Dawati la Ijumaa ambalo kila siku halipoi kusaka habari ziliokwenda shule limebaini kuwa Dk Mwakyembe amekuwa kiongozi anayetajwa na wananchi wengi hasa wasanii kuwa anamudu kuingoza wizara iliyo chini yake.

Ukaribu wake na wasanii wa muziki wa ladha tofauti, ufuatiliaji wa masuala ya michezo ukiwemo mpira wa miguu, ngumi, riadha na usimamiaji wa haki za wasanii kwa jumla ni miongoni mwa mambo yanayompandisha chati waziri huyo.

 HABARI ILIYOBAMBA

Hivi karibuni, Dk Mwakyembe, akiwa bungeni jijini Dodoma, aliliamsha dude kwa kuahidi kufuatilia kwa kina mikataba yote isiyokuwa na tija kwa wasanii ambayo hatimaye huyaacha maisha yao kwenye ufukara.

Ahadi ya ufuatiliaji huo wa mikataba feki ilichochewa na waziri huyo kuguswa na hali ya ugonjwa na changamoto za kimatibabu zinazomkabili mwigizaji mkongwe nchini, Amri Athuman ‘Mzee Mjuto’ ambaye kwa sasa yuko nchini India kwa matibabu.



“Leo hii Mzee Majuto anaumwa, anaomba pesa, ninachanga pesa kutoka mfukoni kwangu, lakini leo hii nusu ya mabango ya biashara, matangazo ya biashara kwenye TV ni Majuto, ninaomba sasa nitumie nafasi hii kusema nimeunda kamati ya wanasheria, tunaanza na kesi ya Majuto. Mashirika yote, kampuni zote zilizoingia mkataba na Majuto, tutapitia hiyo mikataba, kama ameonewa lazima ilipwe familia yake…tumechoka.



“Tukishamaliza na Majuto tunarudi na kwa Kanumba (marehemu Steven Kanumba) na msanii yeyote ambaye anaona ameingia mkataba wa kipumbavu, aje tuone. Mheshimiwa mwenyekiti inaudhi, lakini ndiyo hivyo.

“Leo hii Mzee Majuto yuko hospitalini, amekosa shilingi laki tano, nimtumie mimi wakati waziri pesa yenyewe ndiyo hiyo mnaelewa, eeh…maisha siyo…”

 IJUMAA NA DK MWAKYEMBE KATIKA MAZUNGUMZO

Baada ya tamko hilo la waziri huyo anayetaka kuuvunja mfupa uliowashinda mawaziri wenzake wengi wa kuwafanya wasanii wa Kibongo nao kula bata kupitia kazi zao za sanaa, gazeti hili lilizungumza katika mahojiano maalum na kutaka kujua amefikia wapi katika kushughulikia mikataba au naye amepoa?



Fasta bila kuchelewa, waziri huyo alipokea simu yake ya mkononi iliyopigwa na Mwandishi Wetu saa 7: 24 mchana wa Mei 9, mwaka huu na hapo ndipo alipofungua kabrasha la taarifa kamili juu ya kauli yake hiyo.

MSIKIE DK MWAKYEMBE

“Zoezi limeshaanza, kwa sababu suala la mikataba linahitaji umakini, weledi na kusimamia haki, nimeshaunda timu ya wanasheria watano ambao wanapitia hiyo mikataba.

“Lakini kwa sababu suala lenyewe ninahitaji liende haraka, ninakusudia kuongeza wanasheria wengine wanne ili wafikie tisa, lakini kwa sasa hao watano wameshaanza kuchambua baadhi ya mikataba inayolalamikiwa na wasanii wetu.

“Ninachoweza kukuambia ndugu yangu ni kwamba, katika hiyo mikataba tuliyopokea, tayari kuna mingine imeshachambuliwa na atumefikia hadi hatua za kuwakutanisha walalamikaji na wanaolalamikiwa, kwa hiyo zoezi linakwenda vizuri,” alisema Dk Mwakyembe wakati akijibu baadhi ya maswali aliyoulizwa na Mwandishi Wetu.

 ATOA WITO KWA WASANII

Aidha, Waziri Mwakyembe, mbali na kueleza kuwa atajitokeza hadharani hivi karibuni kuwaambia wananchi kile atakachovuna katika kazi yake hiyo aliyoianza amewataka wadau wa sanaa wenye mikataba yenye shaka wajitokeze ili matatizo yao yatafutiwe ufumbuzi.

Wito huo ulitolewa na waziri huyo baada ya gazeti hili kutaka kujua wizara yake iko ‘siriaz’ na mikataba ya Kanumba na Majuto peke yake au na wasanii wengine wanaweza kujiunga katika msafara huo aliouanzisha wa kuuangamizi unyonyaji.

MITAANI KWA WASANII KUKOJE?

Baada ya waziri kuliamsha dude, gazeti hili lilipita katika ulimwengu wa sanaa na kuwaangalia wasanii wenyewe wameipokeaje hatua hiyo ya waziri ambapo ilibainika kuwepo kwa vicheko na nderemo.

Mama mzazi wa msanii maarufu aliyega dunia miaka sita iliyopita, Steven Kanumba aitwaye Flora Mtegoa ni miongoni mwa watu waliofurahia hatua hiyo ya waziri.



“Mwanangu amefariki dunia, ameacha mikataba mingi kwenye makampuni, lakini hakuna nilichopata, kuna siku nilikwenda kwenye kampuni (anaitaja lakini tunahifadhi jina) kuulizia, nilipofika waliniambia Kanumba alishakufa na mikataba yake ilishakufa pia.

“Yaani sijui nikuambie nini, nimefurahi kusikia waziri anatafuta haki za mwanangu, najua kwa sasa yuko bungeni, akitoka huko nitakwenda kumuona,” alisema mama Kanumba.



Mbali na mama Kanumba, mwingine ambaye Ijumaa lilinasa habari za kulalamikia mkataba feki ni Wastara Juma ambaye mara kadhaa amekuwa akijitokeza na kudai kudhulumiwa kiasi cha shilingi milioni 80 na Kampuni ya KZG ya China.

Wastara anadai kuwa, KZG ilimpa mkataba wa kuwa balozi wa bidhaa za simu ya mkononi kwa makubaliano ya kiasi hicho cha fedha, lakini baadaye kampuni hiyo ilitimka nchini na kurejea China huku ikimwacha Wastara akilia.

 WANASHERIA WAFUKUA UTAJIRI WA KANUMBA, MAJUTO

Habari za chini ya kapeti zilizonaswa na gazeti hili zilidai kuwa, timu hiyo ya wanasheria walioteuliwa na Waziri Mwakyembe wameshaanza kufukua mikataba yote ya Kanumba na Majuto na endapo hali ikiwa upande wa wasanii hao, huenda utajiri ukawatembelea licha ya Kanumba kutokuwepo duniani na Majuto kuwa hospitalini huko India.

Kwa miaka kadhaa, kumekuwepo na kesi mbalimbali za wasanii wa Bongo kudhulumiwa haki zao, jambo ambalo kwa sasa linaonekana kuanza kupatiwa tiba na huenda likawatajirisha wasanii wengi.

 TUPEKUE KIDOGO HABARI HII

Pamoja na nia njema ya waziri ya kuwasaidia wasanii kupata haki katika mikataba feki, Timu ya Ijumaa inaungana na Waziri Mwakyembe na kumshauri kuwa jambo hilo linahitaji umakini mkubwa kulishughulikia kutokana na aina, maisha na uelewa wa wasanii wengi hapa nchini.

Kutokana na uzoefu na kuishi karibu na wasanii wa Bongo, gazeti hili limebaini kuwa maisha ya ‘njaanjaa za kujiendekeza’ yamekuwa yakisababisha baadhi ya wasanii kuingia mikataba feki ili kujipatia fedha hata kiduchu za kufanyia matanuzi mjini angalau kwa siku moja.

Kwa msingi huo, gazeti hili linawataka wasanii wa Bongo kutambua hadhi yao, kujielimisha kuhusu mikataba, kuacha tabia za kuingia mikataba kwa lengo la kukidhi shida ya siku moja.

Dalili kuu 7 zinazoonyesha mtu ambaye atachelewa sana kufanikiwa

$
0
0
1. Siku zote ana pesa za kununua vocha na kuweka vifurushi,ana pesa za kununua nguo  lakini hana PESA za kununua kitabu kitakachomuongezea maarifa.

2. Siku Zote ana muda wa kuchart watsapp, kuangalia Movie, kusoma magazeti na Kupiga stori za mpira ama za wasanii lakini hana MUDA wa Kusoma kuhusu taaluma yake ama mambo ya kumuongezea ujuzi.

3. Siku zote akiona waliofanikiwa anawatuhumu aidha wameiba, ni freemason ama wana bahati katika maisha. Huwachukia na hataki kujifunza Kwao.

4. Siku zote hupenda kuhalalisha kufeli kwake kwa kujitetea, kulaumu uchumi, wazazi, serikali au amerogwa.

5. Siku Zote Hujiona anajua Kuliko Mtu Yeyote Yule na hapendi Kujifunza kwa wengine. Huongea sana Kuliko Kusikiliza.

6. Kila anachoingiza anatumia, ukimwambia kusave ama kuwekeza anasema ngoja nipate cha ziada nitaanza kesho.

7. Anajua mambo mengi sana, anajua stori za mafanikio, anasoma vitabu lakini hafanyii kazi ama anafanyia kazi kidogo sana katika kile anachokijua.

Je Unayo dalili mojawapo kati ya hizo? Amua kubadilika ishi au fanya ukijua kesho ipo .... NDOTO YAKO INAWEZEKANA, CHUKUA HATUA.

Nimeshawishiwa Kuhamia CCM- Mwenyekiti wa BAVICHA

$
0
0

Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema (BAVICHA), Patrick Ole Sosopi, amesema amewahi kushawishiwa na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ili aweze kuhamia chama hicho tawala.


Ole Sosopi amesema hayo leo Mei 16 akiwa studio za EATV katika kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa kila siku ya Jumatano kuanzia saa 8:00 mchana hadi saa 10:00 za jioni na kuongeza kuwa yeye hana thamani ambayo itaweza kumnunua kwakuwa ni tegemeo la vijana wa CHADEMA nchi nzima.

“Ndiyo nimewahi kushawishiwa na kiukweli ukiwa bora watataka kukuonesha kwamba utakua bora zaidi, kumbe sio sahihi, ubora wa Ole Sosopi unaoonekana leo CHADEMA, kama ningekuwepo CCM inawezekana ninsingepata hata ubalozi wa nyumba kumi, naamini kule hawathamini uwezo bali ni nani anakujua na historia yako” amesema Ole Sosopi.

Kiongozi huyo wa BAVICHA Taifa ameongeza kuwa watu hao walikua wakimshawishi kwa kutumia njia ya kiurafiki kwa kumwambia kuwa kutokana na ubora wake alistahili awepo upande wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Novemba 21, 2017 aliyekuwa mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) Patrobasi Katambi alitangaza kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa madai ya kufurahishwa na utendaji kazi wa mwenyekiti wa chama hicho Rais Dkt. John Magufuli

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Nkurunziza Kutawala Burundi Mpaka 2034

$
0
0
Nchi ya Burundi leo inapiga kura ya maoni kufanya marekebisho ya katiba ambayo yanaweza kumuweka Rais wa sasa Pierre Nkurunziza madarakani mpaka mwaka 2034


Kwa mujibu wa BBC Kura hiyo itapigwa ya ndiyo au hapana ili kuongeza muda wa Rais kukaa madarakani kutoka miaka mitano mpaka saba katika awamu moja.

Katiba ya sasa imeweka ukomo kwa Rais aliyepo madarakani kuhudumu kwa kipindi cha awamu mbili, kwa mujibu wa mabadiriko yatakayofanywa yatampa uhuru Rais Nkurunziza kugombea tena katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 akiwa kama mgombea mpya na hivyo huenda akatawala mpaka mwaka 2034.

Chama tawala CNDD-FDD kinachoongozwa na Nkurunziza ndicho kinaendesha kampeni ya kuunga mkono upigwaji wa kura ya ndiyo huku kiongozi wa upinzani Agaton Rwasa chini ya mwamvuli wa muunganiko wa vyama vya upinzani ujulikanao kama Amizero y’Abarundi wakihamasisha kura ya hapana.

Alicholazimishwa Sugu kufanya akiwa gerezani

$
0
0

Mbunge wa Mbeya kupitia CHADEMA Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu, amesema alishangazwa na kitendo cha kusikia imepigwa simu kutoka juu, na kueleza kwamba ni lazima yeye na Masonga wavae sare za jela


Akizungumzia suala hilo Sugu amesema kwamba kitendo hicho kilimshangaza kwani kulikuwa kuna watu wengine wengi walikuwa hawana sare na wamefungwa mule muda mrefu lakini walikosa sare, hivyo kitendo cha kulazimishwa yeye ambaye yuko kwa muda mfupi kilikuwa kinamshangaza.

“ Nisiite kujisikia vibaya niite kushangaa, ni siku ambayo maagizo kutoka juu, ilipigwa simu kwamba lazima Sugu avae uniform na Masonga, unaweza ukaona kwamba zaidi ya wafungwa 600 hawana uniform, Sugu yuko pale mmemfunga kwa miezi mitano, anatakiwa kutumikia kama miezi mitatu, lakini unamlazimisha avae uniform, lakini kuna wafungwa pale wamefungwa maisha mamia kwa mamia hawana uniform, kwa nini usiangalie namna ya kuwapatia wale uniform unahangaika na mtu ambaye anapita tu!?”, amesema Sugu.

Sugu ameendelea kwa kusema kwamba kitendo cha yeye kulazimishwa kuvaa sare hakikumkwaza kwani aliona inamsaidia kuhifadhi nguo zake.

“Zilitafutwa siku hiyo hiyo uniform, wakaja wakatuletea uniform ambazo zimevaliwa tukagoma, tukakataa kwa sababu hatuwezi kuvaa nguo ambazo hatujui zimevaliwa na nani, wakaenda kuhangaika kila kona sijui walitoa Segerea, lakini walitumia nguvu kuhakikisha wanatuvalisha uniform, wao walidhani wakimvalisha Sugu uniform ataathirika kisaikolojia, lakini we umeshanifunga kuvaa nguo ni kitu gani, kwanza utanisaidia kutunza nguo zangu", amesema Sugu.

Sugu aliachiwa huru mapema wiki iliyopita kwa msamaha wa Rais baada ya kutumikia kwa muda mfupi kifungo chake cha miezi mitano katika gereza la Ruanda mkoani Mbeya, akiwa na mwenzake Emmanuel Masonga

Trump Afichua Mchepuko Wake

$
0
0

Rais wa Marekani Donald Trump amekiri kuwa alirejesha fedha kwa wakili wake baada ya kumlipa nyota wa filamu za ngono Stormy Daniels ili kumzuia kufichua uhusiano wao.


Ofisi ya Maadili ya Serikali ya Marekani imegundua kuwa Trump huenda alifichua malipo hayo akitangaza matumizi ya fedha awali.

Matumizi hayo ya fedha yanaonyesha kuwa alimlipa Michael Cohen kwa matumizi ya fedha ya mwaka 2016 kati ya dola 100,001 na 250,000.

Malipo kwa Stormy Daniels yanaweza kuwa tatizo la kisheria kwa Rais Trump kwa sababu yanaweza kuonekana ni matumizi mabaya ya pesa za kampeni.
Donald na Storm

Kibatala Aiomba Mahakama Ifute Mashtaka Kesi ya Mbowe na Wenzake

$
0
0

Upande wa utetezi katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, umeomba Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu kutupilia mbali mashtaka dhidi ya washtakiwa kwa kuwa yanamapungufu, kisheria.

Maombi hayo yamewasilishwa jana Mei 16, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilabard Mashauri na Wakili Peter Kibatala, ambaye aliwasilisha mapingamizi nane ya kisheria ‘yanayoshambulia’ uhalali wa hati ya mashtaka na mashtaka dhidi ya washtakiwa.

Katika Mapingamizi hayo, Kibatala alidai, kibali cha DPP kina mapungufu ya kisheria kwa sababu haioneshi imetolewa kwa mashtaka yapi na pia hati ya mashtaka imewataja majina washtakiwa wote bila ya kufafanua na pia imetaja tu kifungu cha sheria ambacho washtakiwa wameshtakiwa nacho huku akidai pia kwamba, hakuna kibali kilichowasilishwa mahakamani hapo kwa maana hiyo mashtaka dhidi ya washtakiwa yamepelekwa mahakamani hapo bila ridhaa ya DPP.

Aidha, Kibatala alitoa ombi mbadala na kuomba, iwapo mahakama itashindwa kuifuta hati nzima ya mashtaka yanayowakabili washtakiwa hao basi iyafutilie mbali mashtaka ambayo yanamapungufu kisheria, likiwamo shtaka la nne, latano, la sita na la saba.

Alidai, maelezo ya mashtaka hayo yanawachanganya washtakiwa na hawawezi kujitetea ipasavyo, pia mashtaka hayo kufunguliwa kwake kunahitaji ridhaa ya (DPP) ambayo haipo kutokana na mapungufu hayo, inaonesha hakuna ridhaa yake.

“Kwa kuwa mashtaka hayo tajwa kufunguliwa kwake kunahitaji ridhaa ya DPP, lakini kuwa haipo tunaomba yafutiliwe mbali. Hati ya mashtaka inamapungufu kwa sababu shtaka la pili na la tatu hayana maelezo ya kutosheleza ya kuwapa washtakiwa msingi na uwezo wa kuweza kujitetea kikamilifu katika kesi hiyo ya jinai.

“Katika shtaka la kufanya mkusanyiko bila kibali hati haijataja watu waliotishiwa na kwamba wametajwa kwa wingi hivyo haijulikani ni washtakiwa ama ni watu wengine. Mashtaka yanayowakabili washtakiwa yamejichanganya na hayaonyeshi walipelekeaje kifo cha Akwilina na hao majeruhi walijeruhiwa na nani na kwa kutumia nini,” alisema Kibatala.

Amedai maelezo katika hati ya mashtaka yamerundikana kiasi kwamba ni vigumu mtu kujitetea na kwamba unapomshtaki mtu kwa kisababisha kifo ni lazima utoe Maelezo ya kutosha kuonesha unamaanisha kitu Fulani ili mtu aweze kujitetea.

Alidai mapungufu mengine yaliyomo kwenye hati hiyo ni kuwa hayaoneshi dhumuni la pamoja ambalo washtakiwa walikutana kulitenda hivyo linawanyang’anya washtakiwa haki ya kujitetea. Kibatala alidai kuwa hati ya mashtaka inamapungufu kwa sababu vifungu vilivyotajwa katika shtaka la Tatu, tano na saba siyo sahihi.

Alidai kuwa katika shtaka la kumi, kumi na moja na kumi na mbili yanamapungufu kisheria kwa sababu hayaonyeshi watu waliochochewa kufanya makosa ni wakina nani waliohudhuria mkutano, wakazi wa Kinondoni ama wapiga kura bila kujali itikadi zao.

Akijibu mapingamizi hayo, Wakili wa serikali Mkuu, Paul Kadushi aliiomba mahakama kuyatupilia mbali mapingamizi yote hayo ya upande kwa kuwa hayana mashiko kisheria.

Kuhusu kibali cha DPP kinachoipa mahakama ridhaa ya kusikiliza kesi, Kadushi alidai kuwa hakuna uamuzi wowote ulioweka msingi kwamba ni lazima kiwepo na nini ama hakipaswi kuwepo.

Akiahirisha kesi hiyo, hakimu Mashauri alisema atatoa uamuzi kuhusu pingamizi hizo Juni 11, mwaka huu.

Mbali na Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa Chadema, washtakiwa wengine ni mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa; naibu katibu mkuu wa chama hicho Zanzibar, Salum Mwalimu; na wa Bara ambaye pia ni mbunge wa Kibamba, John Mnyika.

Wengine ni mbunge wa Tarime Mjini Esther Matiko; katibu mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji; mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche; mbunge wa Kawe, Halima Mdee na wa Bunda, Ester Bulaya.

TRA Yatishia Kuuza Makontena 20 ya Paul Makonda

$
0
0
Mamlaka ya Mapato (TRA), imetangaza kusudio la kupiga mnada kontena 20 za Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, ikiwa atashindwa kuzilipia ushuru na kuzichukua ndani ya siku 30 kuanzia Jumatatu.

Kontena hizo za Makonda ambazo zimesubiri utaratibu wa kuzitoa TRA kwa zaidi ya siku 90 zinazokubalika kwa mujibu wa sheria za kodi, zimesheheni samani za ndani na ofisini.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo, jana alisema kuwa kwa kawaida bidhaa zote zinapoagizwa na kufika bandarini zinatakiwa kuondolewa ndani ya siku 90.

Kayombo alisema inapotokea muda huo ukapita bila wahusika kuondoa mizigo yao, hujulishwa na mamlaka hiyo kwa kupewa notisi ya siku 30 ili waondoe.

Kwa mujibu wa tangazo la TRA lililotoka kwenye vyombo vya habari Jumatatu, Mamlaka hiyo imetoa notisi ya siku 30 kwa wateja nane akiwamo "Paul Makonda" ambao mizigo yao imekaa bandarini zaidi ya muda unaotakiwa.

Katika tangazo hilo, Kamishna wa Idara ya Kodi ya Ushuru wa Forodha na Bidhaa, ametoa siku 30 kwa wamiliki wa mali mbalimbali zilizopo katika ghala la TRA kwenda kuzichukua la sivyo baada ya muda huo zitapigwa mnada kwa mujibu wa sheria na utaratibu wa ushuru wa forodha.

Kayombo alisema kuwa, mzigo unapopitiliza muda wa kukaa bandarini, TRA huwakumbusha wahusika kwa kuwapa notisi kama ya siku hiyo.

"Tumetoa tangazo hili ili kontena ambazo ziko bandarini ambazo zimepitiliza siku 90 wahusika waende kuziondoa; wasipotekeleza ndani ya muda tuliowapa tutazipiga mnada kwa mujibu wa sheria," alisema.

Kayombo alisema nyaraka za bidhaa hizo ziko sawa tatizo ni muda wa kuziondoa bandarini hapo ndiyo haujafuatwa.

"Siwezi kusema kama wameshindwa kulipa kodi au la lakini hata ikitokea bidhaa ambazo zina msamaha wa kodi zimekaa zaidi ya siku zilizowekwa na wamiliki wakapewa notisi bila kutekeleza, muda wa notisi ukiisha bidhaa husika hupigwa mnada na kwenye hili hatuangalii bidhaa zimetoka wapi, ni msaada au sio msaada," alisema Kayombo.

"Bidhaa ikipitiliza siku za kukaa bandarini kwa mujibu wa taratibu, tunatangaza bila kuangalia zimeagizwa na nani, kuna nini ndani yake, zimelipiwa ama hazijalipiwa kama hazijaondolewa bandarini, tunatangaza, ndivyo tulivyofanya."

Hongera Hamisa Kwa Kumpendezesha Aunty Ezekiel

$
0
0
Kupitia mobetostyle kwa Mara ya kwanza mbongo muvi aunty Ezekiel alipendeza sana kwa vazi La heshima alilovaa kwenye uzinduzi wa film yake inayoitwa MAMA ktk ukumbi wa Mlimani City, kwa kweli umejitahidi mnoo!



Aunty alipendeza haswaa akanoga,akaonogeka katika siku yake adhimu.

Hongera sana kwa kufungua kiwanda cha ushonaji(Tanzania ya viwanda)naona unapiga hatua kubwa sanaa kimaendeleo na nimeona pia umevalisha mamiss ifm 2018,ni jambo zuri wadada wa wadogo kama wewe ambao mko chini ya miaka 30 mkifanya jitihada za kimaendeleo kama hizo.

hamisamobetto_BizPjA8HkzS.jpg

Hongera sana kwa wadada wa bongo movie pia kwa kuweza kuamua kujishughulisha na biashara tofauti tofauti na kusapotiana katika kazi zenu.

Nimekupenda bure we mdada na Mungu abariki kazi halali ya mikono yako!!
SIGNATURE
One step at a time!

Je, ni sahihi kufunika au kukiacha kidonda wazi?

$
0
0


Mara nyingi ukipata jeraha au kidonda utaambiwa ukiache wazi ili kipate hewa safi hasa kama kidonda ni kibichi na kuamini kuwa njia hiyo hukifanya kipone haraka. Lakini ukienda hospitali na kidonda kibichi, jambo la kwanza ambalo Muuguzi atafanya ni kukisafisha kidonda na kukifunika au kukifunga. Kwanini anafanya hivyo?

Mwili wa binadamu ni kama mashine, lakini utofauti wake ni kwamba umeumbwa kwa miunganiko ya biolojia. Ina njia mbalimbali za kukabiliana na majeraha lakini njia ambayo imezoeleka kukitibu kidonda ni utengenezaji wa gaga (scab).

Mchakato wa kutengeneza gaga unaanza muda mfupi baada ya kupata jeraha na damu zinapotoka. Chembechembe nyeupe damu ambazo ni mahususi kuzuia uvujaji wa damu hujikusanya pamoja kwenye eneo lenye jeraha (ulipojikata, mchubuko au alama ya kipigo) na kuganda juu ya ngozi.

Gaga ni ulinzi asilia dhidi ya vimelea vya wadudu lakini kiukweli sio njia nzuri ya kutibu kidonda. Gaga linahatarisha mchakato wa uponyaji kwa kuweka kizuizi cha ukavu na seli zilizokufa. Ngozi yenye afya inatakiwa ifanye mchakato yenyewe ndani kwa kuunda tishu mpya ili kuziondoa seli zilikufa na kuharakisha uponyaji. Kukiacha kidonda wazi eti kipate hewa, sio wazo zuri hasa kama kinavuja damu.

Ikiwa kidonda kibichi kikifungwa au kufunikwa, kinaepusha seli za ngozi kukauka na kutengeneza gaga, jambo linalopunguza uwezekano wa kupata kovu kwenye eneo la kidonda. Kukifunga kidonda kuna faida nyingi ikiwemo kutunza unyevunyevu ambao unasaidia uponyaji mzuri wa ngozi, kuzuia vimelea vya wadudu, vumbi, uchafu na maji kukutana na jeraha.

Zaidi, ni rahisi kwa gaga lililofunika kidonda kutoka na kupelekea kujitonesha na kuibua jeraha tena. Kinyume chake bendeji au kitambaa kinaongeza ulinzi kwenye kidonda. Pia inakukinga kujiumiza tena. Kwa vyovyote vile, ni muhimu kukifunika kidonda kwasababu inasaidia kukilinda na inaharakisha mchakato wa uponyaji.

Nafasi za Ajira zilizotangazwa Leo

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema afunguka kuhusu Tundu Lissu

$
0
0
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA, Patrick Ole Sosopi amesema kwamba hawataki Mwanasheria wa chama chao, Tundu Lissu  akirudi Tanzania  awe mtu wa kuhudhuria kliniki kwa ajili ya matibabu bali wanatarajia aingie kwenye 'struggle' moja kwa moja.

Ole Sosopi ameyasema hayo leo wakati akijibu swali kwenye Kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa kila siku ya Jumatano kupitia ukurasa wa Facebook EATV,  na kuongeza kwamba wanatarajia kiongozi wao atarudi nchini mara tu atakapomaliza matibabu yake anayoendelea nayo huko nchini Ubelgiji.

"Tundu Lissu tunataka akirudi asirudi ku-atend clinic, aje aingie kwenye mapambano moja kwa moja. Lissu ni kama kaka kwangu, alipopigwa risasi nilifadhaika sana, mpaka kesho nawaza hawa watu walikuwa na dhamira gani" Ole Sosopi.

Aidha Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa "Lissu ni 'asset' kwa Tanzania na Mungu amemponya kutuonyesha, na ndio maana yupo mpaka leo".

Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria wa Chadema alipigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 alipokuwa kwenye maeneo ya nyumbani kwake Area D Jijini Dodoma wakati alipokuwa akirejea kutoka katika majukumu yake.


Mwigizaji Dotnata Apata Pigo Kubwa

$
0
0
MASKINI! Mwanamama mkongwe wa filamu za Kibongo, Illuminata Poshi ‘Dotnata’, amepata pigo baada ya kufiwa na mama yake mzazi, Ildegalda Alphonce aliyefariki dunia juzi, Jumatatu, asubuhi katika Hospitali ya Boch, Dar baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akizungumza na Za Motomoto News, Dotnata alisema kuwa, kifo cha mama yake kimeacha pengo kubwa katika familia kwani kama mzazi, alikuwa na umuhimu mkubwa kwao, lakini ndiyo mapenzi ya Mungu hawawezi kuyapinga.

“Kufiwa na mama siyo jambo dogo, ni kubwa mno, mama yetu ametuachia pengo kubwa na tutamkumbuka sana kwa mengi, ameugua kansa (hakupenda kutaja ya nini) kwa muda mrefu na ameteseka sana kwa kweli ndipo Mungu akaamua kumpumzisha. Tunaumia sana, lakini inabidi tukubaliane na kilichotokea maana kila nafsi lazima itaonja mauti. Tulimpenda mama yetu, lakini Mungu amempenda zaidi,” alisema Dotnata huku akilia kwa uchungu.

Mwili wa mama wa Dotnata ulitarajiwa kusafirishwa kwenda Bukoba mkoani Kagera, lakini mpaka gazeti hili linakwenda mtamboni walikuwa hawajapanga siku ya kuusafirisha na msiba upo nyumbani kwa dada yake Dotnata, Segerea, Dar. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.  Amen!

Wanafunzi na wadau wailalamikia bodi ya Mikopo

$
0
0


Zikiwa zimepita takribani siku 6 tokea kulipofunguliwa dirisha la uombaji mikopo kwa njia ya mtandao nchini, wanafunzi na wadau mbalimbali wameendelea kuilalamikia Bodi ya Mikopo kwa kuweka vigezo vigumu bila ya kuwafikilia kwa undani watu wanaotaka kufaidika nayo.

Akizungumza kwenye kipindi cha EATV Saa1 Katibu Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP), Joseph Malecela amesema katika utoaji wa mikopo hiyo kumekuwa na ubaguzi wa upendeleo kwa baadhi ya michepuo ya wanafunzi hasa hasa wanaosomea sayansi huku wengine wakikosa kabisa.

Mbali na hilo, Malecela amesema ni vyema Bodi ya Mikopo itoe ufafanuzi zaidi juu ya kifungu cha muongozo wa kuomba Mkopo Na 1.0 (vii) ambacho kinasema 'waombaji ambao wazazi au walezi ni wamiliki wa biashara, mameneja wakubwa katika mamlaka zinazotambulika zenje usajili, hawaruhusiwi kuomba mkopo'.

"Sisi tunachojiuliza kama Mtandao wa wanafunzi Tanzania kwamba tuna mfumo gani wa mkopo ambao unaweza kupima kiwango cha uwezo wa mzazi katika kuweza kumudu hizo gharama, na madodoso gani yamewekwa ili kujua huyu mtu anafanya biashara kubwa hata kama si Meneja mkubwa", amesema Malecela.

Kwa upande wake Afisa Mawasiliano Mwandamizi kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Bi. Veneranda Malima amesema kifungu hicho kipo sawa na hawawezi kusema kwamba kitaondolewa.

Yanga mambo magumu vs Rayorn Sports uwanja wa Taifa

$
0
0
Jumatano ya May 16 2018 uwanja wa Taifa Dar es Salaam Yanga walikuwa wenyeji wa Rayon Sports ya Rwanda kucheza mchezo wao wa pili wa Kundi D wa kombe la shirikisho Afrika CAF.

Yanga wakiwa nyumbani wameshindwa kuutumia vyema uwanja wa nyumbani baada ya kujikuta wanalazimishwa sare tasa (0-0) hivyo wanakuwa na point moja na wakishika mkia katika Kundi D ambalo linaongozwa na USM Alger ambayr ana point nne.

Kwa upande wa game ya USM Alger dhidi ya Gor Mahia waliyopo Kundi moja na Yanga, mchezo wao umemalizika kwa sare tasa pia hivyo Gor Mahia na Rayon Sports wote wanabaki kuwa na point mbili mbili kila mmoja, Yanga sasa atahitaji kuutumia vizuri mchezo wake wa tatu dhidi ya Gor Mahia kama atakuwa ameweka dhamira ya kweli ya kusonga mbele michuano ya CAF.

Idris Sultan aomba michango kwa ajili ya Ben Pol

$
0
0
Mchekeshaji Idris Sultan ameamua kumtania Ben Pol kuhusu shati lake alilovaa siku ya May 14, 2018 katika uzinduzi wa ngoma yake mpya Clouds FM  na kuomba watu wamchangie fedha za kununua nguo mpya  kutokana na shati hilo kuchanika.

Idris ameandika utani huo kupitia ukurasa wake wa instagram na kusema kuwa tusimkumbuke mtu kwenye mazuri tu anapokufa bali katika uhai wake akipata shida tumsaidie.

“Wasanii huwa tunasubiri mpaka kuwe na msiba ndio tuungane kumsaidia mwenzetu kwani dalili kama hizi za kukosa nguo hatuzioni ? Kwanini tusimsaidie Ben angali hai ?”

“Kaka mpaka ananyoa kipara kubana sabuni tunakaa tu hatujiongezi ila tunajua kujifanya Dah RIP alikua noma sana Samboira aliambiwa ajichunge sijui kama kajichunga, shida yule demu ali touch phone yake naye nimemaindi.”

Habari Njema kwa Wanawake na Wanaume Wanaopenda Muonekano Bomba

$
0
0

PENDEZA_KESSY_ PRODUCT WEKA MUONEKANO WAKO NA UPENDEZE SASA,TUMIA BIDHAA HALISI NA UREMBO MAFUTA/DAW ZISIZO NA MADHARA ZIMETENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA MATOKEO NIMAZURI KUANZIA WEEK 2/4🍍🌾



1)-KUTOA MVI SUGU PIA ZAKUZALIWA_130,000/

2)-RUREFUSH NYWELE ZAKO NA KUZIJAZA -120,000/

3)-TENGENEZA MWILI WAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS KALIO NA MAPAJA (@) KUNYWA/VIDONGE/KUPAKA_130,000/

4)-ONDOA NYAM UZEMBE NA KUTOA MAFUTA_100,000/

5)-PUNGUZA NA KUKIMALIZA KITAMBI KABISA (@)KUPAKA 100,000/ (@)KUNYWA (VIDONGE)-130,000/

6)-PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO 15&20

@) KWADAW YAKUNYWA NA KUMEZA (VIDONGE)_130,000/

7)-PUNGUZA MAZIWA NA KUYASIMAMISHA _100,000/

8)-KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_100,000/

9)-ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/

10)-TOA MICHIRIZI SUGU NA MIPASUKO_90,000/

11)-TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/

13)-KUWA MWEUPE MWILI MZIMA (@)VIDONGE VYAKUMEZA_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAKA YASIO NAHARUFU YAKUKERA_100,000/

14)-TOA NDEVU NA VINYWELEO MWILINI _100,000/

15)-ONGEZA NGUVU KWA WANAUME (@)DW ZAKUPAK AINAZOTE -100,000/(B)VIDONGE VENYE

UHARAKA_100,000/

16)-REFUSH MAUMBILE NA UNENE SAIZI UNAYOTAKA

@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/

@) JELI/VIDONGE UREFUSHA NCH 5%6&_130,000/

17)-RUDISHA HAMU YA TENDO LA NDOA_100,000/

18)-DAW YA KURUDISH USCHANA (BIKRA)-100,000/

19)-TOA MAFUT USONI WEKA USO MKAVU_100,000/

20)-ONDOA MIKUNJO USON NGOZI YAKUZEEKA I00,000/(21)-ENGEZA MGUU (WABIA)_100,000/ 21)- PATA MIKANDA YAKUPUNGUZA TUMBON AINA ZOTE 22) DAW YA NGIRI_100,000/🍍🌾🍉🍌🍁



TUNAPATIKANA TZ NZIMA NA TUNATUM MIZIGO POPOTE ULIPO NCHI YOYOTE ILE WASILIANA NASI (+255)0719955528

(+255)0756259180

(+255)0785371237 @Pendeza_kessy_product @Pendeza_kessy_product

Delivery POPOTE ULIPO,


Viewing all 104688 articles
Browse latest View live


Latest Images