Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104743 articles
Browse latest View live

Polisi Waibua Balaa Ishu ya Wanawake Wenye Makalio Makubwa

$
0
0
POLISI WAIBUA BALAA ISHU YA WANAWAKE WENYE MAKALIO MAKUBWA!

DAR ES SALAAM: Huu mchezo wa baadhi ya wanaume kuona wanawake wenye makalio makubwa na kujifanya kurukwa na akili kwa kuwapigia miruzi, kujikohoza au kuzomeazomea umefikia mwisho.

Jeshi la polisi na hasa Visiwani Zanzibar liko ‘siriazi’ na ishu hii ambapo hivi karibuni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Magharibi ‘RPC’, Hassan Nassir (pichani), alitoa tamko ambalo limeibua balaa mitaani.

 SIKIA TAMKO LA RPC

Hebu kabla ya kuelezea balaa lilolopo kuhusu tamko hilo ni bora kujipa muda wa kumsikiliza RPC Nassir kile alichosema alipozungumza katika semina ya kulinda utu wa mwanamke na mtoto iliyofanyika hivi karibuni mkoani humo.

“Naomba wananchi wajue mwanamke kupita pengine maumbile yake yamejazajaza ukaanza kukohoa, mmh, mmmh, hilo ni shambulio la aibu tutakukamata tukupeleke mahakamani.

“Maana wengine wanafikiri ni mchezo tu ina maana mama zetu, dada zetu, watoto wetu wenye maumbile makubwa wasitembee mitaani; maana wakitembea watu wanaanza kukohoa mmh, kama una kihozi nenda kwako ukakohoe ndani huwezi kuwa mwanamke kupita hapo unaanza kukohoa hilo ni shambulio la aibu.


BALAA LILILOPO

Siku chache baada ya kutolewa kwa tamko hilo la RPC Nassir mitandao ya kijamii ilishiba hoja hiyo huku mawazo ya wengi yakitofautiana.

Wapo waliosema kwamba amri ya kuwakamata wanaowadhalilisha wanawake kwa kuwapigia miruzi itaishia Visiwani Zanzibar kwa sababu aliyeitoa si mkuu wa Jeshi la Polisi.

Mbali na agizo hilo kuleta mkanganyiko huo wa sura ya kitaifa baadhi ya wanaume walionekana kutishika na hali ya kutaniana kati ya mtu na mtu nayo haikubaki nyuma.

 AMANI LAMTAFUTA RPC

Pamoja na uwepo wa video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha RPC Nassir akitoa tamko hilo, Amani lilimtafuta mkuu huyo wa polisi mkoa ili kuomba ufafanuzi zaidi.

Amani: Tumeona kuna video inasambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikikuonesha ukikaripia vitendo vya baadhi ya wanaume kuwadhalilisha wanawake; tungependa kujua kama ni yako na nini msingi wake.



RPC Nassir: Ndiyo hiyo ni yangu, nimeitoa jana (Jumatatu, Mei 14 mwaka huu) msingi wangu ni kulinda utu wa mwanamke, haifai kuwafanya wenye makalio makubwa wajione kama vioja mitaani, waone aibu kutoka majumbani kwao kwa kuhofia watazomewa au kuchekwa, haiwezekani.

Amani: Wewe ni kamanda wa mkoa, watu wanasema huwakilishi jeshi lote la polisi, hii marufuku yako inahusu Zanzibar au na Tanzania Bara kwa ujumla?



RPC Nassir: Naweza nisijibu hili kwa ufasaha kwa sababu sijui sana sheria, lakini katika hali ya kawaida makosa ndani ya nchi yetu na sheria zake zinafanya kazi nchi nzima, huwezi kusema tutawalinda wananawake wa Zanzibar wasifanyiwe mashambulio ya aibu halafu tukaacha wanawake wa Tanzania Bara wakinyanyaswa.

Amani: Umesema utawakamata wote na kuwafikisha mahakamani, ninyi ni polisi mmepanga kuingia mitaani kusikiliza wanawake waopigiwa miruzi ndipo muwakamate watuhumiwa, au mtafanyaje?

RPC Nassir: Tutafanyia kazi malalamiko, ndiyo maana nawaomba wanawake wote nchi nzima wanaofanyiwa vitendo hivyo waripoti kwenye vituo vya polisi ili hatua zichukuliwe, lengo ni kujenga jamii inayoheshimiana, tusilifanyie mchezo jambo hili.



WENGI KUISHIA MAGEREZA

Uchunguzi unaonesha kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya wanaume na hasa vijana kuwapigia miruzi wanawake wenye makalio makubwa kama ishara ya kupagawishwa na maumbile yao.

Endapo hatua ya Polisi kulivalia njuga jambo hili itakuwa na meno kuna uwezekano wanaume wengi kuingia gerezani kutokana na kupenda kushabikia vitendo hivyo vibaya dhidi ya wanawake wenye makalio makubwa maarufu kama ‘wamejaaliwa.’

 WALIOJAALIWA WANASEMAJE

Miongoni mwa wanawake waliojaaliwa waliozungumza na Amani wameonesha kuipongeza hatua hiyo ya Jeshi la Polisi kwa madai kuwa itawasaidia kulinda heshima yao.

“Ile video niliiona nikadhani ni mambo ya mitandao, lakini kwa kuwa mmesema ni ya kweli nampongeza huyo polisi, wakati mwingine huwa najuta hata kuumbwa hivi, sina raha kila ninapopita mitaani nazomewa utafikiri nimebeba kinyesi,” alisema Joan James binti aliyejaliwa mkazi wa Sinza, Dar alipozungumza na Amani.

 MWANASAIKOLOJIA HUYU HAPA

Miaka ya hivi karibuni kumekuwepo na tabia ya wanaume wengi kuvutiwa na wanawake wenye makalio makubwa jambo ambalo wanasaikolojia wamekuwa wakilielezea kama ni la kisaikolojia zaidi.

“Hisia huleta hamasa haraka, wanaume wengi wanapowatazama wanawake wenye makalio makubwa huwa wanaamini kuwa wana kitu cha ziada kwenye mapenzi na mambo kama hayo, lakini si kweli.

“Ni mhemko tu ambao huwasukuma kuvutiwa nao haraka, lakini uchunguzi unaonesha kwamba wanaume wengi kati ya waliofanya mapenzi na wanawake wa aina hiyo hawakukatwa kiu yao kwa kiwango cha msukumo waliokuwa nao tangu awali,” alisema Chris Mauki mwanasaikolojia maarufu nchini.

STORI: Waandishi Wetu, Amani

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Wasichana Msiolewe na Wanaume Wanaoishi Mabondeni

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, amewasihi wasichana katika mkoa wa Dar es salaam kutokubali kuolewa na wanaume ambao wanaishi katika maeneo ya bondeni ambayo ni hatarishi hasa katika kipindi cha mvua za masika.


Makonda amesema hayo leo Mei 17, 2018 alipofanya ziara katika eneo la Mbagala Kiburugwa na kuona badhi ya nyumba za wananchi ambazo zimeathirka kutokana na kujengwa katika maeneo hatarishi na kuwataka wakazi hao kahama mara moja.

“Nitoe rai kwa wasichana ambao hawajaolewa, usikubali kuolewa na mwanaume ambaye atakuonesha ana kiwanja bondeni, kataa huyo sio wa kukuoa sasahivi angalieni akina mama mnavyotaabika na nyumba zimebomoka hujui watoto wako unawalaza wapi” amesema Makonda.

Makonda ameongeza kuwa serikali haitaweza kutoa msaada wa chakula na malazi kila mara kwa wananchi ambao wanakumbwa na majanga yanayotokana na wao kuamua kukaa katika maeneo hatarishi kwa kujitakia.

Mkuu wa mkoa huyo amedai kuwa katika maeneo hayo ni ngumu kwa mwananchi kupata msaada wa dharura ikiwemo gari la wagonjwa au huduma ya zima moto

Wizkid na Kashfa ya Kutelekeza Mtoto wake

$
0
0
Staa wa muziki kutokea Nigeria Wizkid “Starboy” amechukua headlines kupitia mitandao ya kijamii baada ya mwanamke aliyezaa nae mtoto wake wa pili Binta Diamond Diallo kutoa malalamiko kupitia ukurasa wake wa instagram kuwa staa huyo hatoi matunzo kwa mtoto wake.

Kupitia ukurasa wa instagram wa Binta ambaye ni mwanamke aliyezaa na Wizkid ameandika “Sijali ulipo, sijali upo na nani, kama una watoto hakikisha unawajali na unapata muda wa kuwa nao #usitoevisingizo”

Wizkid kwa sasa ana watoto watatu wakiume ambao amezaa na wanawake watatu tofauti akiwemo manager wake Jada Pollock.

"Baba yangu Alipigana vita ya Kagera" - Makonda

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, amebainisha kuwa baba yake ni moja kati askari kutoka Tanzania ambao wamepigana vita nyingi kwaajili ya kutetea taifa ikiwemo vita ya kagera mwaka 1978.


Mh. Paul Makonda amesema hayo leo Mei 17, 2018 wakati wa alipokuwa anatoa salamu kwa Rais Magufuli katika sherehe za ufunguzi wa kituo cha uwekezaji cha SUMA JKT Mgulani Jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa alizaliwa na kulelewa katika kambi za jeshi

“Nikunong’oneze mheshimiwa Rais, mimi nimezaliwa kambini na baba yangu ni miongoni mwa askari waliopigana vita nyingi ikiwemo vita ya Uganda na mpaka ulemavu wake wa mguu ni kutokana na kazi ya kuipigania Tanzania” amesema Makonda

Makonda aliongeza kuwa kutokana na kulelewa katika kambi za jeshi imemsaidia kupata ujasiri wa kuongoza mkoa wa Dar es salaam wenye changamoto nyingi na kuweza kufanya kuwa Jiji la raha Tanzania.

Katika tukio hilo, Rais Dkt Magufuli alizindua kituo cha uwekezaji cha SUMA-JKT ambacho ndani yake kuna kiwanda cha Ushonaji, Maji, Chuo cha Ufundi Stadi na Ukumbi wa Mikutano.

Trump Amgeuka Mshauri Wake Kuhusu Kuifanya Korea Kaskazini Kama Libya

$
0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump amepinga kauli ya mshauri wake mkuu wa masuala ya ulinzi, John Bolton aliyedai kuwa mfumo wa kuondoa silaha za kinyuklia nchini Korea Kaskazini utafanana na uliotumika Libya.

Tump amesisitiza kuwa makubaliano kati ya Marekani na Korea Kaskazini yanayotarajiwa kuanza katika mkutano kati ya viongozi wa nchi hizo mbili, uliopangwa kufanyika Juni 12 mwaka huu hayana mlengo wowote wa mfanano na aliyoyasema Bolton.

“Mfumo uliotumika Libya sio mfumo ambao tunaulenga tunapofikiria suala la Korea Kaskazini,” alisema Trump.

Rais Trump alifafanua kuwa anachofikiria ni kuhakikisha Korea Kaskazini inafuata mfumo wa Korea Kusini katika kuleta maendeleo baada ya kuondolewa vikwazo. Aliwasifu watu wa Korea Kaskazini kuwa ni watu wazuri na wachapakazi, hivyo anaamini baada ya makubaliano hayo yatakayoondoa vikwazo pia nchi hiyo itakuwa tajiri zaidi.

Korea Kaskazini ilitishia kuachana na mpango wa kiongozi wake, Kim Jong-un kufanya mazungumzo na rais Trump nchini Singapore baada ya kukasirishwa na kauli za Bolton pamoja na mazoezi ya pamoja kati ya Marekani na Korea Kusini ambayo waliyataja kuwa ni mazoezi ya kujiandaa kufanya uvamizi.

Mwaka 2003, Libya chini ya uongozi wa Muammar Gaddafi ilitangaza kuachana na mpango wake wa kutengeneza silaha za maangamizi za kinyuklia, hatua iliyoishtua dunia. Uamuzi huo ulisababisha kuondolewa vikwazo pamoja na kurejeshwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati yake na Marekani pamoja na washirika wake.

Hata hivyo, mwaka 2011, Libya ilivamiwa na waasi walioungwa mkono na Marekani chini ya mwamvuli wa NATO na mwisho wakamuua Gaddafi.

Historia hiyo imemshtua Kim Jong-un ambaye alitangaza kuteketeza vinu na eneo la majaribio la silaha za maangamizi za kinyuklia za nchi hiyo.

Hata hivyo, kuna mkanganyiko wa matakwa ya Marekani na inachofanya Korea Kaskazini, ambayo imesema kuwa katika makubaliano yake na Korea Kusini, walikubaliana kuharibu na kuachana na mpango wa silaha za nyuklia katika eneo lote la Rasi ya Korea, kwa pande mbili.

Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume, Maumbile Madogo, Mvuto wa Mapenzi na Magonjwa Sugu

$
0
0
KIBOKO YA MATATIZO YA NGUVU ZA KIUME,MAUMBILE MADOGO, MVUTO WA MAPENZI ,MAGONJWA SUGU

Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

SUPER CHAN :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

LUGINI 3 POWER:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

MANUS :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

TULIZA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR GALIMBO NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO
PIGA SIMU 0759208637

Nape Awatoa Jasho Mawaziri Sita Bungeni..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 18

$
0
0


Nape Awatoa Jasho Mawaziri Sita Bungeni..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 18

Mwakyembe Awataka Vijana kuiga Mfano Wa Flaviana Matata

$
0
0
Na Loretha Laurence-WHUSM,Dodoma
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amempongeza mwanamitindo wa kimataifa Bibi. Flaviana Matata kwa juhudi za kusaidia watoto wa kike kupata elimu kwa kuwawezesha  vifaa muhimu vya shule ikiwemo ada na madaftari.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini Dodoma Dkt. Mwakyembe amewataka vijana wa kitanzania kuiga mfano wa mwanamitindo huyo ili kuchangia katika ujenzi wa taifa.

“Nawasihi vijana wengine wenye fursa kama za Flaviana Matata kuzitumia vizuri  kwa kuhakikisha jamii inanufaika na mafanikio waliyoyapata” ameongeza Dkt. Mwakyembe

Aidha, aliongeza kwa kueleza kuwa, Mwanamitindo huyo amekuwa ni balozi mzuri katika kupeperusha bendera ya Taifa katika nchi mbalimbali za Ulaya.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza amempongeza Bibi. Flaviana kwa kuwa  mfano bora kwa watoto wa kike kwa jinsi ambavyo amekuwa akisaidia watoto wa kike nchini.

Naye Mwanamitindo wa Kimataifa Bibi. Flaviana Matata ameleza kuwa mbali na kujishughulisha na mitindo, ameweza kuanzisha kampuni ya Flaviana Matata Foundation ambayo inasaidia kutoa vifaa vya shule, ambapo hadi sasa amefanikiwa kutoa vifaa zaidi ya 5000 katika shule mbalimbali nchini.

Anazidi   kueleza kuwa, Taasisi hiyo imefanikiwa kurabati shule mbalimbali kwa kujenga madarasa na  kusomesha wasichana 15 ambao wanamaliza kidato cha sita mwaka huu na wengine watano bado wapo shule.

Hata hivyo, Mwanamitindo huyo ameushukuru uongozi wa Wizara kwa jitihada za wazi wanazozifanya katika kusimamia haki za wasanii na hivyo kurudisha hadhi ya tasnia hiyo nchini.

Huyu Mrembo Corazon Anachofanya Siyo Kabisa..Atupia Picha Chafu Mtandaoni...Mashabiki Wagoma

$
0
0
MWANAMITINDO mwenye shepu ‘tata’ Corazon Kwamboka amechafuka mtandaoni mara baada ya kutupia picha ya nusu utupu akiwa na Mzungu anayedaiwa kuwa ni mchumba wake.

Corazon ambaye pia ni mwanasheria nchini Kenya, aliweka picha hiyo ikimuonesha akiwa kifua wazi na Mzungu huyo huku akiwa ameshikiliwa kifua chake.

“Mwendo wa ufukweni,” aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Kutokana na picha hiyo mashabiki wake hawakupenda na alipokea matusi mfululizo huku wengine wakimsema vibaya Mzungu wake kwa kitendo cha kumshikilia vibaya kifuani tena hadharani.


Picha sio Nzuri ila Kama upo 18 years and above Click HAPA

Mahusiano na Mapenzi Yakifikia Ukomo; Kumbe Kuna Wanaume Wanaanguaga Kilio Hadharani Namna hii Kama Huyu MC Pili Pili

$
0
0
Kumbe mapemzi huwa yanakaba pabaya eeh! Wanaume nilidhani huwa hakuna maumivu pande zao kumbe siyo kabisa. Baada ya bwana RM wa radio ya mawingu aliyeangua kilio wakati bibiye ZM -  alipopata wa kumuweka na kumsitiri, Basi unaambiwa MC Pilipili naye kilio kutwa kucha kisa Demu wake aliyemchukulia poa kuolewa na Bwana Mwingine

Tazama Hapa chini kilio cha mwanaume mzima:

Wageni Wanaoingia Nchini Waanza Kupimwa Ebola

$
0
0
Serikali Kagera imeanza kuwapima watu wanaoingia kutoka nchi jirani kupitia mkoa huu, ili kubaini kama wana maambukizi ya ugonjwa wa ebola.

Hatua hiyo inafuatia kutangzwa kwa mlipuko wa ugonjwa huo kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Manispaa ya Bukoba jana, Kaimu Ofisa Afya Mkoa wa Kagera, Geraz Ishengoma alisema kuwa kila mgeni anayeingia nchini anapimwa na anayeonekana ana dalili zinazofanana na ugonjwa huo, hupelekwa kupimwa zaidi.

Ni mara ya pili katika mwaka mmoja kwa serikali kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya ebola. Mei 29, mwaka jana Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema wageni kutoka nchi hiyo wangesajiliwa na kufuatiliwa hadi wanakoishi ili kujiridhisha kama hawana virusi vya ebola.

Kaimu Ofisa Afya Mkoa wa Kagera, Ishengoma alisema jana: “Tumeweka kambi katika maeneo ya mpakani hasa Mutukula, Murongo, Kabanga na Rusumo, (na) kila mtu anayeingia anapimwa ikiwamo joto la mwili.

"Tunayekuwa na shaka naye, tunamtenga na kumchunguza zaidi.”

Alisema kuwa kambi hizo za mpakani ziliwekwa baada ya serikali kutangaza kuwapo kwa ugonjwa huo DRC Mei 8, mwaka huu, na kuwa hadi sasa hakuna mtu yeyote aliyebainika kuwa na maambukizi ya virusi vya ugonjwa huo.

Alisema virusi vya ugonjwa huo vinaambukizwa kwa kugusa damu au majimaji, kugusa maiti ya mtu aliyekufa kwa ugonjwa huo na kugusa wanyama wenye maambukizi, na kuwa dalili zake huanza kuonekana kuanzia siku mbili hadi 21 tangu mtu anapoambukizwa.

Ishengoma alitaja dalili za ugonjwa huo kuwa ni homa kali, kulegea mwili, kichwa kuuma kunakoambatana na kutapika na kutokwa na damu sehemu tofauti za mwili, ikiwamo puani.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu, alisema serikali imechukua kila tahadhari ili kuhakikisha ugonjwa huo hauingii nchini kupitia mkoa wa Kagera.

“Kumbukeni Kagera ni mkoa ambao unapakana na nchi nyingi, zikiwamo za Rwanda, Burundi na Uganda, lakini pia unapakana na mkoa wa Kigoma ambao watu kutoka Congo hupitia katika mkoa huo na kuingia Kagera hasa kupitia eneo la Murusagamba,” alisema.

Kijuu aliwataka wananchi kutoa taarifa haraka endapo watabaini kuwapo kwa mtu mwenye dalili kama za ebola katika maeneo yao, ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa.

“Lakini pia wananchi hawapaswi kugusana na mgonjwa mfano kugusa mate, majimaji na damu, kuepuka kugusa maiti, kutochelewa kupata huduma na kuzingatia usafi wa mwili,” alisema.

Alisema kuwa serikali inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali, ili kuhakikisha ugonjwa huo hauingii nchini.

VIDEO: Nandy Amekuletea Sabuni na Mafuta Yanayomfanya Aonekane Natural

$
0
0
Jana May 17,2018 tunayo story kutokea kwa Msanii wa muziki nchini, NANDY, ambapo ametangaza rasmi bidhaa zake mwenyewe zikiwa na jina lake ikiwemo Sabuni na Mafuta.

Nandy anatueleza imekuaje hadi na yeye ameamua kujitosa katika masuala ya kibiashara…licha ya kuwa bado ni msanii.

Bonyeza PLAY hapa chini kutazama

Pendeza kwa Kutumia Dr.Kessy Products, Mafuta na Dawa Zisizo na Madhara

$
0
0

PENDEZA_KESSY_ PRODUCT WEKA MUONEKANO WAKO NA UPENDEZE SASA,TUMIA BIDHAA HALISI NA UREMBO MAFUTA/DAW ZISIZO NA MADHARA ZIMETENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA MATOKEO NIMAZURI KUANZIA WEEK 2/4🍍🌾



1)-KUTOA MVI SUGU PIA ZAKUZALIWA_130,000/

2)-RUREFUSH NYWELE ZAKO NA KUZIJAZA -120,000/

3)-TENGENEZA MWILI WAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS KALIO NA MAPAJA (@) KUNYWA/VIDONGE/KUPAKA_130,000/

4)-ONDOA NYAM UZEMBE NA KUTOA MAFUTA_100,000/

5)-PUNGUZA NA KUKIMALIZA KITAMBI KABISA (@)KUPAKA 100,000/ (@)KUNYWA (VIDONGE)-130,000/

6)-PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO 15&20

@) KWADAW YAKUNYWA NA KUMEZA (VIDONGE)_130,000/

7)-PUNGUZA MAZIWA NA KUYASIMAMISHA _100,000/

8)-KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_100,000/

9)-ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/

10)-TOA MICHIRIZI SUGU NA MIPASUKO_90,000/

11)-TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/

13)-KUWA MWEUPE MWILI MZIMA (@)VIDONGE VYAKUMEZA_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAKA YASIO NAHARUFU YAKUKERA_100,000/

14)-TOA NDEVU NA VINYWELEO MWILINI _100,000/

15)-ONGEZA NGUVU KWA WANAUME (@)DW ZAKUPAK AINAZOTE -100,000/(B)VIDONGE VENYE

UHARAKA_100,000/

16)-REFUSH MAUMBILE NA UNENE SAIZI UNAYOTAKA

@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/

@) JELI/VIDONGE UREFUSHA NCH 5%6&_130,000/

17)-RUDISHA HAMU YA TENDO LA NDOA_100,000/

18)-DAW YA KURUDISH USCHANA (BIKRA)-100,000/

19)-TOA MAFUT USONI WEKA USO MKAVU_100,000/

20)-ONDOA MIKUNJO USON NGOZI YAKUZEEKA I00,000/(21)-ENGEZA MGUU (WABIA)_100,000/ 21)- PATA MIKANDA YAKUPUNGUZA TUMBON AINA ZOTE 22) DAW YA NGIRI_100,000/🍍🌾🍉🍌🍁



TUNAPATIKANA TZ NZIMA NA TUNATUM MIZIGO POPOTE ULIPO NCHI YOYOTE ILE WASILIANA NASI (+255)0719955528

(+255)0756259180

(+255)0785371237 @Pendeza_kessy_product @Pendeza_kessy_product

Delivery POPOTE ULIPO,



IGP Sirro amemuhamisha Rpc wa ‘Shambulio la Aibu’ na wengine

$
0
0
Jana May 17, 2018 Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Simon Sirro amefanya uteuzi na mabadiliko kwa baadhi ya Makamanda wa polisi wa mikoa katika Mikoa mbalimbali Tanzania Bara na Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji wa jeshi la polisi nchini Barnabas Mwakalukwa imesema IGP Sirro amemteua Naibu Kamishna wa Polisi Maulid Mabakila aliyekuwa kuwa Mkuu wa Kitengo cha kuzuia uhalifu Makao makuu ya Polisi DSM kuwa Naibu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Zanzibar.

IGP Sirro pia amefanya mabadiliko kwa Makamanda wa  Mikoa ambapo Naibu DCI Zanzibar Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ramadhan Ng’anzi ameteuliwa kuwa RPC wa Arusha huku RPC Arusha Charles Mkumbo akihamishiwa Makao Makuu.

Pia aliyekuwa Kamanda wa polisi mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Nassir Ali amehamishiwa Kaskazini Pemba na nafsi yake ikichukuliwa na Kamishna na msaidizi Thobias Sedoyeka.



Kamanda Hassan Nassir Ali alizishika headlines za vyombo vya habari Tanzania Baada ya kusambaa kwa video aliyokuwa  anazungumzia suala la kuwa kamata na kuwafikisha mahakamani wanaume wanao jikoolesha au hata kuwasumbua wanawake wenye maumbile makubwa haswa sehemu za nyuma

Volkano yarusha Mawe Makubwa Angani Hawaii, Marekani

$
0
0
Mlipuko mkubwa ulitokea katika volkano ya Kilauea katika jimbo la Hawaii nchini Marekani na kuzua wasiwasi zaidi eneo hilo.

Mlipuko huo ulirusha majivu futi 30,000 (9,100m) juu angani. Aidha, ulirusha juu mawe makubwa wa kilo kadha, na baadhi inakadiriwa kuwa yanaweza kuwa na uzani wa tani kadha.

Mlipuko huo ulitokea mwendo wa saa kumi na robo alfajiri saa za huko, Wanasayansi wanasema bado kuna uwezekano mlipuko mwingine unaweza kutokea.

Watu waliokuwa wakifanya kazi katika kituo cha kufuatilia volkano hiyo waliokuwa kwenye mbuga ya taifa ambapo kunapatikana volkano hiyo wamehamishwa.

Shirika la Jiolojia la Marekani linasema mawe ya ukubwa wa hadi 60cm (2ft) yalionekana hatua kadha kutoka kwenye shimo la mlipuko wa volkano hiyo.

Lakini walitahadharisha kwamba huenda mambo yakawa mabaya zaidi, "Wakati wa milipuko ambayo imesababishwa na mvuke, mawe ya ukubwa wa hadi 2m yanaweza kurushwa pande zote umbali wa 1km au zaidi," shirika hilo lilisema.

"Mawe hayo yanaweza kuwa na uzito wa kilo kadha hadi tani kadha. mawe madogo yanaweza kurushwa mbali, kilomita kadha."



Tangu milipuko ya volkano ilipoanza kutokea eneoi jipya Kilauea, matope yenye moto yamekuwa yakimwagika na kuharibu mamia ya nyumba eneo hilo na kulazimu maelfu ya watu kuhamishwa.

Tahadhari ya kiwango cha juu zaidi imetolewa, na marubani wa ndege wameonywa kuhusu hatari inayoweza kutokana na 'wingu' la majivu ya volkano hiyo.

Shirika la Jiolojia la Marekani lilikuwa limeonyesha kwamba kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kutokea mlipuko mkubwa eneo hilo.

Hii ni baada ya kina cha 'ziwa la matope moto' kwenye vilkano hiyo kuonekana kupungua na kuongeza uwezekano wa maji yanayopatiukana chini ya ardhi kukutana na matope hayo moto chini ya ardhi, maji yakijaribu kujaza mianya inaoachwa wazi na kupungua kwa matope hayo.

Shirika la huduma za dharura Hawaii liliwatahadharisha watu walio maeneo yaliyoathiriwa na majivu hayo kusalia ndani ya nyumba zao.

Kilauea ni moja ya volkano tano ambazo bado hulipuka katika kisiwa cha Hawaii, Ni moja ya milima inayolipuka sana duniani na imekuwa ikilipuka mara kwa mara ingawa hakujakuwa na mlipuko mkubwa kwa miaka zaidi ya 30.



Mlipuko wa mwisho mkubwa eneo hilo ulitokea 1924, Hata kabla ya mlipuko huo wa Alhamisi, majivu kutoka kwa volkano hiyo yalikuwa yanaweza kuonekana kutoka kituo cha kimataifa cha anga za juu (ISS).

Fahamu Jinsi ya Kujiokoa Katika Dharura ya Moto Nyumbani Mwako

$
0
0
Ajali  ya moto imekuwa ikitokea mara kwa mara, muda mwingine matatizo haya huja bila taarifa, inapotokea dharura ya moto ndani ya nyumba unatakiwa kujua mambo yafutayo:

Kitu cha muhimu ni kutoka nje salama haraka iwezekanavyo (as soon as possible).
Hakikisha  kila siku mlango wa dharura wa nyumba  umekaa kwa urahisi sehemu ambayo imekaa mahali ambapo ni karibu, na pia uwe ni malngo ambao unagumgukia nje. Lakini pia Kila mtu ajue funguo za milango ya kutokea zinapowekwa, sio zinafichwa.

Fahamu kwamba ktk matukio mengi ya moto kinachoua ni moshi kabla ya moto, hivyo ukiona dalili ya moshi hakikisha unakuwa na kitambaa kibichi cha kujifunika puani na mdomoni, na kama moshi umeanza kuingia ulipo tambaa chini (crawl down) sababu hewa ya uhai (oxygen) ina uzito (density) kubwa kuliko hewa ya kifo (carbon monoxide) hivyo inakuwa imekandamizwa chini sentimita chache kutoka kwenye sakafu (few centimeters from the floor). Hivyo tembea kwa kutambaa.
Hakikisha unawajulisha watu wote ambao wamelala ili kama wamelala ili waweze kutoka nje haraka.
Achana na fikra ya kuokoa vitu, katika hatua hii cha muhimu ni kuokoa uhai kwanza.
Kumbuka, muda ni kitu cha msingi, fanya haraka iwezekanavyo (quick as possible) katika kujiokoa na kuokoa wengine.

Ni muhimu nyumba zetu kuziwekea kiashiria moshi (smoke detectors) na pia kizima moto (fire extinguishers). Kugundua haraka (early detection) ya moto ni muhimu sana ili kuweza kuudhibiti kirahisi. Smoke detector ni mashine ya elektroniki ambayo inagundua moshi ktk hatua ya mwanzo kabisa na itapiga kelele (alarm) kwa sauti ya juu, itakusaidia kuamka hata kama upo usingizini na kuweza kujiokoa na kuokoa wengine na kuuzima moto kabla hujashika kasi.

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Wasichana 29 Tanga Wakamatwa Wakielekea Uarabuni Kuuza Figo

$
0
0

TANGA: Wasichana 29 ambao baadhi yao wamekutwa na hati feki za kusafiria wamekamatwa wakiwa wanaelekea Uarabuni kupitia nchi ya Kenya

Inadaiwa wasichana hao walikuwa wanaelekea katika nchi hizo za Uarabuni kuuza figo kwa gharama kubwa pamoja na kufanya kazi za ndani

Hivi karibuni Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkinga amewaonya wasichana hao juu ya vitendo viovu vinavyoweza kuwapata wakiwa huko ikiwa ni pamoja na kulawitiwa

JPM "Ningekuwa na Uwezo Ofisi zote za Serikali Wangekunywa Maji ya Uhuru Peak"

$
0
0

MGULANI, DAR: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli akinywa maji ya Uhuru Peak yaliyotengenezwa na kiwanda cha SUMA JKT, jana Mei 17, katika ufunguzi wa kituo cha uwekezaji cha Suma JKT
-
Rais Magufuli alisema "Mimi kuanzia leo nitakuwa mdau wa maji ya Uhuru Peak nitashangaa sana Waziri wa Ulinzi siku nikimtembelea ofisini kwake nikute anakunywa maji ya aina nyingine au Mkuu wa Majeshi au hata Wastaafu au Mkuu wa Magereza anakunywa maji mengine nitashtuka kidogo, lakini nitashangaa."
-
Aliongeza kuwa "Nayapongeza sana Majeshi yetu, ni bahati mbaya tu sina amri ya kusema sasa maji yote yanayonywewa Serikali yawe yameandikwa hii nembo(Uhuru Peak) kwa sababu huo uwezo sina. Lakini ningekuwa nao huo uwezo ningesema, lakini sisemi."
Viewing all 104743 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>