Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Harmonize Amkataa Diamond Amtaja Mrisho Mpoto Kama Nembo ya Taifa

$
0
0

Ameandika Harmonize Kupitia Ukurasa wake wa Instagram:

By @harmonize_tz "Binafsi nikiionaga sura yako naona inaashiria Amani, Upendo, Furaha, Hekima, na Busara....!!! Naamini tupo wengi sana...!!! wenye mtazamo kama wangu wewe ni kama Nembo ya Tanzania kwani hata viongozi hujivunia uwepo wako katika Sanaa nichukue fursa hii kusema Asante sana....!!! Kwa kuniamini na kunipa nafasi ya kushiriki katika kazi yako #Mjomba @mrishompoto M/mungu akubariki sana....!!! hii nikama ndoto kwangu 🙏🙏 kama wewe ni mzalendo na unamkubali"

Wachungaji Watatu Waliodai Wana Uwezo wa Kufufua Maiti Wanusurika Kichapo

$
0
0

MPANDA, KATAVI: Wachungaji watatu waliodai wana uwezo wa kufufua marehemu wamenusurika kupigwa na wananchi baada ya kushindwa kumfufua marehemu Raymond Mirambo katika kijiji cha Sitalike

Mwenyekiti wa kijiji, Christopher Angelo, alisema tukio hilo lilitokea Mei 7 ambapo wachungaji hao walifika katika ofisi ya Kijiji na kujitambulisha kuwa wao ni wachungaji kutoka Kijiji cha Nsimbo na wameitwa na ndugu wa marehemu

Baada ya kujitambulisha walienda nyumbani kwa marehemu na kuanza maombi yaliyofanyika kwa muda wa siku 7 usiku na mchana pasipo kuwa na mafanikio yoyote, hali ambayo iliwafanya ndugu wa marehemu washikwe na hasira

Wananchi, ndugu na jamaa walikasirika kutokana na kuona kuwa wachungaji hao wanawatapeli na kwa sababu waliwasababishia kuingia gharama kubwa ya kulisha watu waliokuwa wakishiriki maombi hayo

Angelo anaendelea na kusema baada ya kufika eneo la tukio walikuta vurugu za wananchi wakitaka kuwapiga wachungaji hao, walochokifanya ni kuwaondoa eneo la tukio

Ndugai afurahishwa Wabunge kuvaa Kanzu na Hijab

$
0
0

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amewapongeza Wabunge kwa kuvaa Kanzu kwa wingi na kwa Wabunge wa Kike kuvaa Hijab.


Spika ametoa pongezi hizo leo, Mei 18 mapema katikati ya kipindi cha maswali na Majibu kwa serikali  ambapo pia amemsifia Naibu Spika wa Bunge kwa kuvaa Baibui na Hijab.


“Wabunge kama hatujaendelea nimefanya utafiti wangu leo watu wengi sana wamependeza kwa kuvaa Kanzu na kofia hongereni sana, tukumbuke tu kanuni tunapo vaa tunatakiwa ivaliwe vilevile kama inavyovaliwa Pwani na miguu sio kuvaa kiatu cha kamba hapana unavaa kobazi,” amesema Spika Ndugai huku akicheka na Wabunge wakimpigia makofi.


“Lakini kwa upande wa kina mama leo Hijab zimekubali, lakini katika Hijab, Hijab namba moja leo hii ni ya Naibu wangu Mh. Naibu Spika, Mh. Naibu Spika ebu simama kidogo hapo ahsante sana, hiyo inaonyesha Utanzania wetu sisi ni wamoja,” ameongeza Spika.

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

$
0
0

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja. Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.

Sethi Agoma Kuvuliwa Madaraka IPTL

$
0
0

Siku chache baada ya kuondolewa katika Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL, mfanyabiashara Herbinder Sethi ameeleza kusikitishwa kwake na hatua hiyo, huku akisema hautambui uongozi mpya uliowekwa madarakani.


Uamuzi wa kumwondoa Sethi katika bodi ya wakurugenzi ambayo pia ilimvua uenyekiti wa IPTL, ulifikiwa baada ya kushindwa kushiriki na kuhudhuria mikutano ya bodi kwa miezi sita mfululizo bila ruhusa, tangu Juni 19, 2017 alipokamatwa na kushtakiwa.


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimsomea Sethi mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na kuisababishia Serikali hasara ya Dola 22.198 milioni za Marekani (Sh309.5 bilioni).


Hata hivyo, taarifa kutoka kwa wakili wake, Hajra Mungula iliyotolewa jana kupitia mitandao ya jamii ilisema Sethi hatambui mabadiliko ya uongozi uliowekwa na kwamba yeye ni mmiliki halali wa IPTL ambayo kimsingi inamilikiwa na kampuni anayoimiliki ya Pan African Power Solutions (PAP).


“Pamoja na kuagiza wanasheria wake kuchukua hatua za haraka za kisheria, Mwenyekiti Sethi pia hana taarifa zozote juu ya mabadiliko hivyo anapenda kuutaarifu umma wazipuuze taarifa hizo kwa kuwa hazitokani na mamlaka halali ya kisheria ya kampuni hiyo,” ilisema taarifa ya Mungula


Mungula alisema mabadiliko hayo yamekwenda kinyume na notisi ya katazo la Mwanasheria Mkuu wa Serikali la Februari 12, 2018 lenye kumbukumbu Na. AGS234 lililozuia aina yoyote ya uhamishaji wa mali na umiliki wa mali za IPTL.


“Kimsingi mabadiliko hayo batili yanaathiri na kwenda kinyume na maelekezo ya Serikali.


“Pamoja na kwamba Mwenyekiti bado yuko mahabusu akituhumiwa kwa mashtaka kadhaa ya jinai, hiyo haiondoi ukweli kuwa IPTL ni kampuni binafsi yenye wamiliki halali wenye hisa halali, hivyo haiwezekani kwa mtu asiyehusika na asiye mwanahisa kutangaza mabadiliko ya uongozi bila kufuata taratibu zilizopo kisheria,” alisema Mungula.


Alisisitiza kwamba licha ya Sethi kuwa na mashtaka ya jinai yanayomkabili, lakini Watanzania wajue bado kampuni hiyo iko chini ya usimamizi salama wa PAP na kwamba madeni yote, madai ya mali na stahiki zote zinazohusiana na kampuni hiyo zipo katika mikono salama.

Video Queen Agness Adakwa Kwa Wizi

$
0
0

MUUZA sura kwenye video za Kibongo ‘Video Queen’ aliyejipatia umaarufu kwa kutupia picha za utupu mitandaoni, Agness Mmasi, yamemkuta mazito, baada ya kuswekwa rumande kwa tuhuma za utapeli Ijumaa linakumegea ishu kamili.

Akipiga stori na Ijumaa, chanzo wa kuaminika kilieleza kwamba muuza sura huyo, mpaka juzi (Jumatano), alikuwa bado akisota rumande katika Kituo cha Polisi Mabatini Kijitonyama jijini Dar es Salaam kwa takribani siku nne.

“Mnahabari kamba Agness amedakwa kisa kutapeli nguo maeneo ya Kijitonyama? Kama hamjazidaka ni kamba alichukua kwa mkopo, baadaye akawa anamzungusha mwenye mzigo, mara amtukane hapo ndipo alipodakwa na mpaka sasa anasota nyuma ya nondo,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kuunyaka ubuyu huo, Ijumaa lilifanya jitihada za kumtafuta anayedaiwa kuwa ndiye mwenye mzigo huo wa nguo ambazo Agness alichikichia nazo, aliyefahamika kwa jina moja la Nyange na alipopatikana alikiri kutapeliwa na mwanadada huyo.

“Ni kweli alichukua mzigo wa nguo, jinsi sita zenye thamani ya shilingi 90,000. Alichukua akidai anakwenda kuzijaribu na siku iliyofuata angetoa pesa, lakini aliingia mitini. Nilipokuwa nikimtafuta baadaye alikuwa akitukana na kudai hakuna ambacho ninaweza kumfanya.

“Ndipo nilipomfungulia mashitaka kwenye Kituo cha Polisi Mabatini kwa jalada namba KJN/ RB/3851/I6L (matusi), akatafutwa na kutiwa mbaroni,” alisema Nyange.

Nyange aliongeza kuwa baada ya kumkamata ndugu wa mwanadada huyo waliomba wayamalize kwa kuzungumza namna watakavyomlipa pesa zake.

Hata hivyo mpaka gazeti hili linakwenda kitamboni Agness alikuwa nyuma ya nondo, kwa hiyo hakuweza kupatikana kuzungumzia sakata hili

Davina "Sijilaumu Kwanini Nimeachika Katika Ndoa zote Nilizoolewa"

$
0
0

MUIGIZAJI wa Bongo Muvi, Halima Yahaya ‘Davina’ amefunguka kuwa hata kama hajapata bahati ya kukaa na mume muda mrefu kama mke lakini kumemfunza kujua maisha mbalimbali na kuwa shupavu kwa mapito aliyopitia.

Akizungumza na Amani kwa njia ya simu, Davina alisema Mungu amemjalia kupitia kwenye ndoa mbili lakini hakubahatika kukaa kwa muda mrefu lakini kikubwa ni kwamba ndoa hizo zimemfunza mambo mengi sana ya kujituma ili aweze kuwalea watoto wake vizuri.

“Siwezi kujilaumu hata siku moja kwa nini sikai kwenye ndoa zote nilizozipitia bali ninachojua ni kwamba zimenifundisha mambo mengi sana hasa ya kujisimamia mimi kama mimi na kuendesha familia nikiwa kama mwanamke mwenyewe bila mtu mwingine pembeni,” alisema Davina.

Mimi Mars " Nilikuwa Siupendi Mwili Wangu Mnene...Nimepungua ila Kuna Watu Hawajapenda

$
0
0

Msanii wa muziki Bongo, Mimi Mars amesema baada ya kupunguza mwili wake kuna baadhi ya mashabiki wake hawakupendezwa na jambo hilo ila wanapaswa kusikiliza muziki wake na sio kujikita zaidi katika muonekano wake.

Mimi Mars amesema kuwa alilazimika kufanya hivyo ili kujiongezea kujiamini zaidi katika tasnia ya muziki na pia muonekano wa awali alikuwa hapendezwi nao.

“Nilikuwa sijafurahi na nilichokuwa nakiona, ilikuwa inaninyima confidence kidogo, so ikabidi nijitengeneze, nibadilishe hilo suala kwa sababu confidence ni kitu ambacho kinahitajika sana hasa kwenye hii industry ambayo tupo,” Mimi Mars ameiambia Bongo5.

“Najua wengi hawajafurahia, hawajapenda, wamelalamika lakini is me, ninachokipenda mimi ndio kinanifaa mimi. Waendelee kuupenda muziki wangu na kuendelea kuusikiliza, mwili wangu waniachie mimi,” amesisitiza.

Muimbaji huyo anayetamba na ngoma ‘Papara’ ameongeza kuwa alitumia muda wa miezi minne hadi mitano kupata muonekano alionao kwa sasa kwa kubadilisha mfumo wa kula na kufanya mazoezi.

Kesi ya Tido Mhando yapigwa kalenda Hadi June 8

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, itaendelea kusikiliza ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka Juni 8 huu katika kesi inayomkabili Mkurugenzi mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando.

Wakili wa Takukuru, Leonard Swai jana amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa  kesi  inayomkabili Tido leo ilipaswa kuendelea kusikilizwa kwa ushahidi wa  mashahidi wa upande wa mashtaka.

Lakini shahidi waliyemtarajia kutoa ushahidi katika kesi hiyo ana udhuru.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Shaidi ameiahirisha kesi hiyo hadi Juni 8 ili mashahidi wa upande wa mashtaka waendelee kutoa ushahidi.

Katika kesi hiyo tayari mashahidi watatu wa upande wa Jamhuri wamekwishatoa ushahidi .

 Mashahidi hao ni  Ofisa uchunguzi wa Takukuru, Victor Lesuya, Mwanasheria wa TBC, Gwakisa Mlawa na Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa TBC, Clement Mshana.

Tido anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh887.1 milioni.

Waziri: Wahitimu Elimu ya Juu ni wengi kuliko ajira

$
0
0
Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi, ajira na watu wenye ulemavu Mh. Antony Mavunde amesema kuwa Serikali inatambua kuwa wahitimu wa Elimu ya juu ni wengi kuliko mafasi za ajira.

Waziri Mavunde ametoa kauli hiyo bungeni leo wakati akijibu swali la Hadija Ally Mbunge viti maalum (CCM) lililohoji serikali imepanua fursa kwa kuongeza vyuo vikuu nchini, je ni kiasi gani mfuko wa vijana unaweza kuwanufaisha walengwa ikizingatiwa kuwa tatizo la ajira ni hali halisi inayowakabili vijana.

Mavunde amesema “Nafasi za ajira zinazotengenezwa kwa mwaka zimekuwa ni chache kuliko wingi wa vijana hivyo basi serikali imeanza kuwabadili mitazamo kuwa sio wote wanaoweza kukaa maofisini bali wanaweza kutumia uwezo wao na kujiajiri katika sekta za kilimo na shughuli nyingine halali zinazoweza wapatia kipato”.

Waziri mavunde ameongeza kuwa Mfuko wa Maendeleo ya vijana umeweza kufikia vikundi 397 ambapo zaidi ya Bilioni nne zimekwisha tumika kuwezesha vijana kiuchumi.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Mbunge CHADEMA Asema Wizara Ya Mifugo Ni Hewa.....Aahidi Kuifadhili Kama Serikali Imeshindwa

$
0
0
Mbunge wa Serengeti, Marwa Chacha (Chadema) amedai Wizara ya Mifugo na Uvuvi ni Wizara hewa ambapo pia amehoji ni kwanini Serikali imekuwa ikiwanyanyasa wavuvi kwa kuwanyang’anya nyavu zao.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi bungeni jijini Dodoma jana Mei 17, wizara hiyo ilitengewa fedha za maendeleo Sh bilioni nne lakini hakuna fedha waliyopewa.

“Najiuliza kwanini wameiweka hii wizara peke yake na kuitenganisha na Kilimo au ilikuwa kuwatafutia ‘washkaji’ ulaji, maana yake ni kwamba hamtaki kusikia biashara ya wavuvi nchi hii.

“Ng’ombe 300 wamepigwa mnada ila tembo akila shamba la ekari tano mhusika analipishwa faini ya Sh 100,000 kwa ng’ombe mmoja.

“Wafugaji wetu wanapata shida mtapata hela wapi Ulega (Abdallah, Naibu Waziri wa Kilimo) mwaka uliopita hamkupewa hata 100 afadhali mje hata mimi naweza kuwafadhili,” amesema Marwa.

Bashe: Bajeti Ya Mifugo Iondolewe, Imejaa Kasoro

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), ameitaka serikali iiondoe bungeni Bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya mwaka 2018/19, kwa sababu imejaa kasoro zinazotakiwa kurekebishwa kabla haijapitishwa.

Amesema bajeti hiyo inatakiwa kurekebishwa kabla haijapitishwa kama ilivyo kawaida ya wabunge kupitisha bajeti zenye kasoro kama ilivyofanyika juzi katika bajeti ya Wizara ya Kilimo iliyokuwa na kasoro mbalimbali.

Bashe ameyasema hayo bungeni leo Mei 18, alipokuwa akichangia bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya mwaka 2018/19 iliyowasilishwa juzi na Waziri wa Wizara hiyo, Luhaga Mpina.

Amesema hoja za baadhi ya wabunge zinazohusu maisha ya wananchi zinafia katika vikao vya vyama vya siasa.

“Naweza kuonekana mbaya kila ninapokuwa nikiikosoa serikali  lakini nitaendelea kusema ukweli kwa kuwa nilianza kuwa na kadi ya CCM kabla sijawa mbunge,” amesema Bashe.

Bashe alieleza jinsi Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye alivyowahi kuitwa na Kamati ya Bunge ya Uongozi baada ya kutaka kuwasilisha hoja ambayo haikuwafurahisha baadhi ya watu.

Ukifanya Haya Mambo Mapenzi Yatanoga Kwa Asilimia 90

$
0
0
Wanaume wengi hupuuzia hili, huona kama ni jambo lisilo na maana sana kwao na wenzi wao. Hali ni tofauti sana kwa wanawake ambao hupenda kuwasifia wanaume zao. Nitakupa mifano miwili ya namna wanandoa wa jinsia mbili tofauti wanavyotambulishana kwa jamaa zao. Kwa mafano manakutanata kwenye majumuiko ya harusi na sherehe kama hizo. Mme 1 akamtambulisha mkewe kwa jamaa zake, huyu ni mama Rick mke wangu. Mme wa 2 akamtambulisha mkewe, huyu ni my lovery sweetheart wife, nampenda sana kuliko wanawake wote duniani. Kama upo kwenye huu utambulisho umeona tofauti gani? hao wanawake wa pande mbili watajisikiaje? Nahisi umejifunza kitu hapo

MALENGO SHIRIKISHI
Wanaume wengi wana ulemavu mmoja; hawapendi kuwashirikisha wanawake katika mambo yao. Wanapenda kufanya mambo yao kwa siri na wakati mwingine ikilazimika kumwambia mkewe basi kwa mshtukizo baada ya kukamilisha jambo husika. Siku hizi dunia imebadilika, kuna mambo mengi. Kuna suala la hasara katika biashara, utapeli, kifo cha gafla, ajali n.k. Mkeo ndiye rafiki yako mkubwa kuliko wote, ndiye ndugu yako wa karibu zaidi kuliko yeyote. Mmeshirikiana kuzaa watoto na kujenga maisha pamoja. Yeye anapaswa kujua mambo yako, ndiye mtetezi wako nambari wani. Mweleze juu ya malengo yako, wakati mwingine anaweza kukusaidia sehemu ambayo hukutarajia. Hata hivyo, kumshirikisha katika malengo yako, kunampa nguvu na nafasi ya kujiona mama katika familia yenu. Lakini ngoja nitoe angalizo, kuna wanawake ambao huwezi kumshirikisha from A to Z ya malengo yako kutokaa na tabia na mienendo ya maisha, hope kila mtu anafahamu strength and weakness ya wake na waume zetu, so be careful in some extent.

KIPAUMBELE/CONCERN
Kuna wakati wanawake huwa na mambo yao binafsi. Kazini au kifamilia. Inawezekana akatatizika katika eneo fulani ambalo kwa namna moja ama nyingine atahitaji usaidizi wako. Ikitokea mkeo akawa katika hali hiyo, msikilize. Mathalani ana tatizo la kifamilia, amekuambia mmoja wa wazazi wake anaumwa, msaidie. Si lazima kifedha, lakini kuonesha kujali kwako tu, kutampa matumaini na faraja kwamba anaishi na mtu sahihi. Acha kupuuza mambo yake; hata yale madogo, kama ya ‘mtoto wa dada amerudishwa ada shuleni’. Msikilize, mshauri panapofaa kufanya hivyo na ukiweza msaidie hata kifedha. Katika upande wa pili ni hivyo hivyo. Labda una tatizo binafsi, kikazi au kifamilia, mshirikishe. Unaweza kushangaa jambo ambalo uliamini unaweza kulimaliza peke yako, kwa kumshirikisha likawa jepesi zaidi na mambo yakaenda vyema. Kipaumbele kwa namna yoyote ile, kunaongeza mapenzi zaidi kwa mwanamke.
"Together we swim in the same pool"

USAFI
Asilimia kubwa ya wanawake wanapenda sana usafi. Ni aghalabu kukutana na mwanamke asiyejipenda. Ndiyo maana wanaitwa mapambo ya nyumba au ua la nyumba! Ni kwa sababu ya hulka yao ya kupenda sana usafi. Mwanamke anavutiwa sana na mwanaume mtanashati. Usafi wako unamfanya ajiamini kuwa na wewe. Hata nyumbani kwako, lazima uishi katika nyumba safi. Hata anapokuja kukutembelea, anakuta mazingira masafi kuanzia sebeleni hadi chumbani. Anapokukuta katika hali ya usafi, inakuwa rahisi zaidi yeye kuanzia hapo alipokukuta na kuendelea mbele. Rafiki yangu, kama uko mbali na usafi, ujue kuwa itakuwa vigumu kupata mdada wa ukweli – yule wa ndoto zako. Wanaume wengine wanapanga kutoka outing na wapenzi wao, mkifika huko mwanamke anajuta WHY amekubali kukutana na wewe maana utamkuta mwanaume hajapasi Tshirt/shirt, kwapa linapumua, ukiongea mdomo unatoa harufu inakuwa tabu tupu. Mwanume ukijipenda unatakuwa mtanashati tu

KUJIAMINI
Mwanamke anajisikia salama zaidi akiwa na mwanaume ambaye anajiamini – mwenye uwezo wa kutetea hoja zake na kujieleza sawia. Siyo anayebabaika. Suala la msimamo binafsi, kwa mwanamke ni kubwa kuliko hata kumnunulia manukato mapya! Mathalani unakuwa naye katika mtoko, angependa kukuona ukiwa katika hali halisi ya maisha yako, usiyeyumbishwa na mwenye kutoa maamuzi yasiyoyumba. Wakati mwingine, mwanamke anaweza kukupima hata katika jambo ambalo amekosea yeye, ataangalia unavyotoa maamuzi yako, lakini pia atafuatilia kuona kama utakuwa mwepesi wa kuyabadilisha. Anataka kuona msimamo wako muda wote. Mwenye kujiamini na mawazo yasiyo na matege wala makengeza! Usiyebadilika kama kinyonga! "Men believe on your standing hills"

ANAYEJALI na KUFUATILIA
Wanawake wanapenda sana wanaume wanaowajali. Wanaowaona wao ni kila kitu na wanaotoa kipaumbele kwao. Kama huna tabia hiyo, ujue upo katika nafasi kubwa ya kumkwaza mpenzi wako. Mjali mpenzi wako kwa kila hali lakini pia uwe na kiasi. Kumjulia hali kila wakati na kutaka kujua maendeleo yake, kutakupa nafasi kubwa ya kuendelea kudumu katika uhusiano hai. Wanaume wengi ni wavivu, si tu kuwatumia hata SMS za “mambo dia?” wapenzi wao lakini hata kujibu tu, “niko poa, Si hulka ya wanaume kutumatuma SMS – inajulikana, lakini angalau ukiweza kulifanya hili hata kidogo tu hata mara moja kwa wiki, utakuwa unajiongezea pointi kwa mwenzi wako na kumpa courage ya kufurahia mapenzi ya ndoa.

MAANDALIZI YA TENDO LA NDOA
Tendo la ndoa halina maana ya kukomoana. Jenga mazoea ya kufanya maandalizi kamili kabla ya tendo. Sikiliza hisia za mwenzako. Ukiweza kumjulia mke wako katika eneo hili, ni wazi kwamba utazidisha upendo wake kwako, lakini pia atakuwa katika kuta za uaminifu. Unapokuwa kazini mchokoze "aisee nasikia hamu leo" hayo ndo maandalizi ya saikolojia. kupitia sms hiyo utasikia feeling zake, ataji-express. Kufikia jioni/usiku utashangaa unashikwa mkoni kupelekwa kitandani. Akatafute nini nje wakati wewe ndiye mganga wake unayeweza kumtibu barabara? Jiamini katika shughuli, fanya mazoezi ya viungo hata kukimbia ili uongeze pumzi ya kutoa dozi kitandani.
Epuka mapenzi ya kubakana, unafika tu bed unamvuta unamvua na kuanza kupanda kifuani......nooooooo hapo hakuna maandalizi ya kisaikolojia wala ya kimwili, hii itampekea kuchukia tendo because there is no any enjoyment

OUTING SOMETIMES
Kulingana na budget yako, si vibaya mara moja kumtoa mpenzi wako outing walau mara moja ndani ya miezi sita hata mwaka kama budget ni shida. Kwa wale wenye familia unaweza toka mkaspend 1 or 2 days outing na mkeo. Kuna mambo mmeo/mkeo anaogopa kukufanyia kulingana na mazingira ya hapo nyumbani na familia kwa ujumla. Lakini mkitoka nje LAZIMA mta-experience the difference for SURE. Pia ni njia mojawapo ya kuboresha na kupalilia penzi lenu na kuongeza uaminifu kati yenu

Naomba niishie hapo kwa leo

Manara awaomba Yanga kujitokeza, ajitolea kulipia viingilio kwa wasio na fedha hapo kesho

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kuwa yupo tayari kujitolea kiingilio kwa baadhi ya mashabiki watakao shindwa kufanya hivyo ili kuhakikisha mashabiki wanajitokeza kwa wingi.

Kupitia mahojiano yake na Radio EFM kipindi cha Sports HQ kinachoruka asubuhi, Manara ameeleza kuwa kwa wale baadhi watakaokuwa hawana fedha za kiingilio, atakuwepo getini na bunda le fedha kuwapatia Tshs 2000 kwa kila mmoja.
Licha ya kuwalipia kiingilio msemaji huyo mwenye mbwembwe zaidi kwenye klabu za soka hapa nchini, Manara amewaomba watani zake wa jadi Yanga kujitokeza kwa wingi Uwanjani hata kama watakuja kuzomea nakusema kuwa hiyo ndiyo burudani ya soka.

Kwenye mchezo huo wa hapo kesho wa Simba dhidi ya Kagera Sugar ambapo watakabiziwa taji mabingwa hao wapya wa ligi kuu Tanzania Bara itahudhuriwa pia na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Ali Kiba Namba na Technologia Aidanganyi Mzee Baba...We

$
0
0
ALI Saleh Kiba ndiyo ma­jina matatu yanayo­tambulika kiseri­kali. Mengine ni King Kiba au Ali Kiba. Mzee Baba ni swaga tu ya kumpamba mtu inayo­tumiwa na watoto wa mjini kuonesha kuwa unakubalika.

Kiba wewe ni bonge moja la mwanamuziki wa Bongo Fleva na Afro-Pop kwa jumla. Najua mbali na uimbaji pia wewe ni mtunzi mzuri wa nyimbo kali chini ya Lebo ya Rockstar4000 ambayo wewe ni mkurugenzi wake. Hongera! Sina shaka na kipaji chako chenye tofauti na wanamuziki wenzako. Unaweza kuwa miongoni mwa wa­namuziki watano bora kabisa kuwahi kutokea kwenye Bongo Fleva.

Tunajua na wewe mwenyewe unakumbuka mwaka 2011 ulichaguliwa kuwa Msanii Bora wa Kwanza wa Afrika Mashariki ukiwakilisha Tanzania, Kenya na Uganda. Mwaka 2015 ulishinda Tuzo Tano za Kili na kuthibiti­sha kuwa wewe ni bora ukilin­ganisha na mshindani wako, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’. Itoshe tu kusema kuwa, Kiba Mzee Baba dunia inakujua na inajua muz­iki wako.

Ushindani wako na Diamond ume­sababisha muziki huu kufika mbali zaidi. Bila ninyi, pen­gine leo tungekuwa tunazungumza anguko la muziki huu kama ilivyo kwa muziki wa dansi. Kwa bahati nzuri mmetengeneza aina ya ushindani unaoelekea kuwa kama uadui lakini ndani yake kuna biashara kubwa. Ni ushindani wa nani zaidi kati yenu! Ni ushindani ambao unahitajika kwenye muziki ili kuleta chachu kiroho safi.

Mara ya mwisho kwa wasanii wa Tanzania kuwa na ushindani wa namna hii ilikuwa yapata miaka saba iliyopita. Kulikuwa na waigi­zaji wawili maarufu wa filamu hapa Tanzania, Vincent Kigosi ‘Ray’ na marehemu Steven Kanumba.

 Ray na Kanumba walikuwa walikuwa na upinzani mkali katika wakati ambao ninaweza kusema ulikuwa wa dhahabu katika tasnia ya filamu hapa nchini. Kila baada ya miezi mitatu kulikuwa na filamu mpya kutoka kwa mmoja wao.

Kukaibuka vibanda vingi vya kuu­za filamu za Kibongo. Wakati wote huo, Ray na Kanumba walikuwa wakiishi kama maadui. Huyu ak­isema hili, huyu anasema lile.Tofauti ya ushindani wa Ray na Kanumba na huu wa Kiba na Diamond ni mitandao ya kijamii pekee, lakini upinzani huu yafaa kuwa wa jadi kwani unatia chachu kwa mashabiki wenu.

 Baada ya hapo tujadili kidogo kili­chojiri mara tu ulipoachia ngoma yako mpya ya Mvumo wa Radi na ikawa kama imesimama kiasi fulani ilipofiki­sha views laki saba na themanini, kabla ya kuiruhusu na sasa inakimbilia views milioni mbili. Kiba nilikusikiliza kwa umakini mkubwa ulipodai kuwa, kuna mchezo mchafu wa wasanii kununua views (watazamaji wa ngoma) katika Mtandao wa YouTube.

 Kama utakumbuka, wakati una­toa kauli ile, ilikuwa ni siku moja tu imepita tangu ngoma yako hiyo iingie YouTube na kupata tatizo. Tatizo lenyewe ilikuwa ni kwamba idadi ya views ilisima­ma na baadaye kushuka kabisa hivyo kuibua sintofahamu.

 Mzee baba ulionekana kama kupaniki fulani hivi. Ulisikika ukisema kwamba suala la ununuzi wa views lipo, tena sana ila kwako halina maana.Ulikiri kwamba, kuna suala la kuweka maro­boti kwenye YouTube ambao kazi yao ni kuongeza views. Ulimalizia kwa kusema kuwa, wewe hufanyi jambo kama hilo na kwamba kufanya hivyo ni utoto badala yake wewe unafanya muziki kwa ajili ya watu hivyo huwezi kuwadanganya.

 Pia ulidai kwamba, pamoja na tatizo hilo la kusimama kwa views na baadaye kushushwa hakukuathiri muziki wako.Katika ufafanuzi wa YouTube ni kwamba walibaini uwepo wa maroboti wa kununuliwa kwa ajili ya kuongeza views wapatao elfu the­lathini hivyo kuwaondoa na kubaki laki saba na nusu!


Tafsiri ni hii, kinachoonekana Kiba ndiye aliyedaiwa kununua views ndiyo maana Youtube wakaishikilia akaunti yake, wakati views wakiwa laki saba na themanini. Walipoi­fanyia ukaguzi iligundulika kuwa kulikuwa na maroboti elfu thelathini hivyo walipowaondoa akabakiwa na views laki saba na hamsini ndipo wakaiachia video hiyo.

 Kiukweli Kiba hapo ulipaswa kukubali kuwa namba hazidanganyi kuliko kuendelea kung’ang’ania tu kuwa kuna wasanii wananunua views bila kuwataja huku mwenyewe ukiwa umekamat­wa na maroboti elfu thelathini! Hata hivyo, tunajua kuwa hata ukinunua views huwezi kukiri.

 Ukweli Kiba ni kwamba namba hazidanganyi labda utoe ushahidi wa wasanii wanaonunua views. Lakini hadi sasa ushahidi unaonesha wewe ndiye unadaiwa kununua views na ndiyo maana YouTube walishikilia akaunti yako na kuondoa views feki za maroboti.

Kwa hiyo mimi naona wewe siyo mtu sahihi wa kukemea jambo hilo ilihali na wewe ni mtuhumiwa wa kununua views.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Nasubiri Kumfumania Mke Wangu, Naombeni Ushauri

$
0
0
Waku habari za mchana,kama nilivyojieleza hapo juu,ni kwamba nilibahatika kuoa miaka 10 iliyopita iliyopita,tulipata sakrament ya ndoa takatifu tar.7/5/2011.pia katika ndoa yetu tumejaliwa kupata watoto 2.sasa kilichonifanya nije hapa jukwaani ni taarifa nilizozipata toka kwa jirani yangu ambae amenithibitishia kuwa mke wangu anatembea na mtu ambae pia ni jirani yetu kabisa.mke wangu huwa anashinda nyumbani akijishughulisha biashara ya kiduka tulichokifungua karibia mwaka sasa.pia mimi huwa nashinda kibaruani kwangu ambapo mara nyingi huwa nachelewa kurudi nyumbani kutokana na kabiashara kangu kanakonipatia riziki.huyu jirangu kanijulisha huwa wanatoka majira ya saa 1 jioni na kurudi sa 2:30 jioni kabla mimi sijarudi.

Baada ya kupata tarifa hizi nilijaribu kufanya uchunguzi na nimeanza kuona kuna ukweli juu ya jambo hili.juzi ilipofika saa 1:30 jioni nilimpigia simu kumuulizia jambo fulani nikasikia anaongea taratibu tofauti na siku nyingine,nikamuuliza umeshafunga duka?akanijibu ndio,nikamuuliza mbona mapema akasema kuna mkanda nimeupenda nauangalia..nikakata simu nikampigia yule jirani kumuuliza kama mke wangu yupo nyumbani akasema hayupo na ametoka na jamaa kama kawaida yake,kama huamini uje uone.

Nilitamani kwenda lakini nilishindwa kujua ni uamuzi gani nichukue kwa sababu,kwanza sikujua wamekwenda guest gani,huyo jamaa anausafiri hivyo wanauwezekano wa kwenda nje ya mji kidogo.nilijikaza sikumuuliza wala kumwonyesha dalili zozote za kufahamu mambo hayo machafu anayoyafanya mke wangu.hivyo naombeni ushauri wenu pindi nikiwafumania au kuwahi kurudi home na kumkosa mke wangu wakati amenijulisha yupo home..naombeni ushauri wenu ni uamuzi gani naweza kuchukua ukawa sahihi.

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu 

 Bonyeza Hapa Chini Kuinstall Upya:


==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>  
    

Alikiba Avunja Ukimya Kuhusu Kutomtaja Baba yake Katika Mafanikio yake Kwenye Muziki

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva mwenye 'hit song' ya 'Mvumo wa Radi' Alikiba amefunguka na kudai sababu kubwa ya yeye kuwa anamtaja mama yake mzazi kila mara ni kutokana na kumpa ushirikiano mkubwa katika kukikuza kipaji chake cha kuimba kuliko baba yake mzazi kwasababu alikuwa mtu wa kusafiri sana.

 Alikiba ameeleza hayo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo ndani ya Heshima ya BongoFleva inayorushwa mubashara kupitia EATV baada ya kuulizwa swali na muongozaji wa kipindi hicho kuwa ni kwanini kila mara anapenda kumzungumzia mama na sio baba.

"Baba yangu kiukweli alikuwa ni international driver, alikuwa anasafiri mara kwa mara nchi tofauti tofauti yaani kachafua bara la Afrika zima. kwa hivyo alikuwa yupo busy sana muda mwingine alikuwa anaweza kukaa nje ya nchi hata mwezi mmoja au hata mitatu", amesema Alikiba.
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images