Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Magereza yamjibu Sugu Kuhusu Sare za Jela.."Sugu Anachanganya Mambo"

$
0
0
Jeshi la Magereza nchini limekanusha taarifa zilizoibuliwa na Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi kuhusu kukosekana kwa sare za wafungwa zaidi ya 600, katika gereza la Ruanda alipokuwa amefungwa.


Akizungumza na www.eatv.tv, msemaji wa Jeshi hilo Lucas Mboje, amesema kwamba sio kweli kwamba wafungwa hawana sare na hakuna kitu kama hiko, isipokuwa kuna mahabusu ambao wapo mule wakiendelea kusubiri kesi zao, na ndio huenda ambao aliwaona bila sare.

“Hiko kitu hakipo, halafu asichanganye mambo, kuna mahabusu ambao wao wanajulikana kwa mujibu wa sheria hawavai sare, sasa asichanganye, mtu akishafungwa inajulikana lazima avae sare, sasa kuna mahabusu pia, sio kweli kama kuna tatizo la sare hakuna mtu anakosa sare, hebu fikiria wafungwa karibia 600 kwenye gereza moja wakose sare ni kitu ambacho hakiwezekani, hiyo itakuwa ni issue nyingine”, amesema Lucas Mboje.

Mbunge Joseph Mbilinyi (Sugu) alipotoka jela kwa msamaha wa Rais alisema kwamba alilazimishwa kuvaa sare za jela wakati kuna watu amewakuta gerezani zaidi ya mia 6 wamekosa sare na wapo mule ndani.


"Naogopa Kufilisika Ndio Maana Sitoi Nyimbo Mara Kwa Mara" - Alikiba

$
0
0
Msanii wa Muziki wa kizazi kipya anayefanya vizuri kwa sasa na ngoma yake ya 'Mvumo wa radi', Alikiba amesema ana uwezo wa kutoa nyimbo kila siku lakini anaogopa kufirisika.


Kiba amesema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio ambapo amesema kuwa anauwezo wa kutoa nyimbo kila siku lakini anahofia kufirisika kwakuwa muziki unatumia pesa.

“Sio kama siwezi kuachia ngoma mfululizo naweza achia ngoma mwezi mzima yaani kila siku lakini naogopa kufirisika muziki unatumia pesa nyingi”. Amesema Kiba

Kiba ameongeza kuwa pia kukaa kutoa wimbo na kuupa muda mashabiki wanakuwa wanamuona mpya kwani kutoa kila siku unaweza chokwa mapema.

Sugu Mzuri, Niko Tayari Kumpa Tena- Faiza Ally

$
0
0

Faiza Ally ambaye ni muigizaji wa Bongo movie na mama watoto wa Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi 'Sugu’ amesema kuwa hayuko tayari kuolewa na mzazi mwenzake huyo bali anaweza mzalia mtoto mwingine.


Faiza amefunga hayo katika mazungumzo yake na eatv.tv ambapo amesema kuwa hana ndoto za kuolewa na Sugu bali anaweza mpatia mtoto mwingine kwakuwa ana mbegu nzuri na kujivunia kuwa binti yake ni mzuri kama baba yake.

“Sugu naweza mzalia mtoto mwingine maana ana mbegu nzuri kanipatia mtoto mzuri sana lakini sio kuolewa nae maana tulishindwana awali sidhani kama tunawezana tena”, amesema Faiza.

Mwana dada huyo mwenye watoto wawili hivi sasa ameendelea kusema kuwa ataongeza mtoto mwingine endapo atapata kipato zaidi lakini kwa sasa hali yake inamruhusu watoto wake hao wawili.

Wasiliana na Dr Mabula Anatibu Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha na Matatizo ya Maumbile Madogo kwa Mwanaume

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO
Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?

MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja 1hitakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uhimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio hasirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate amu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona? zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Mwigizaji Rammy Galis Adaiwa Kuringa na ni Mwenye Dharau Kwa Wenzake

$
0
0
MUGIZAJI wa kiume Bongo, Rammy Galis amefunguka kuwa anachukizwa na minon’gono ya watu wanaombeza kuwa anaringa kitu ambacho kinamkera sana kwa sababu hayuko hivyo.

Akizungumza na Amani juzikati, Rammy alisema kuwa kawaida yake yeye ni mkimya sana na hupenda kuzungumza pale anapokutana na mtu ambaye wamezoeana ambapo ana uhuru wa kuzungumza naye chochote lakini kinyume na hivyo anamheshimu kila mmoja.

“Mara nyingi nilishasikia watu wakisema mimi naringa au nina dharau kitendo ambacho kinanikera sana kwa sababu mimi siko hivyo kabisa labda ukimya wangu wanaona ndiyo niko hivyo lakini sivyo alisema Rammy.

Faiza afunguka tuhuma za kukwapua mume wa mtu

$
0
0
Msanii wa Filamu Bongo, Faiza Ally amefunguka sababu ya kutomuweka hadharani mzazi mwenzie wa sasa.

Muigizaji huyo amesema analazimika kutomuonyesha kwa sababu hawana malengo yoyote ila si kwamba ni mume wa mtu.

“Sipendi kumuonyesha sio sababu ni mume wa mtu, ni sababu hatuna malengo, hatutegemei kuoana wala kuishi pamoja kwa hiyo i take my time, when time come kuonyesha kwenye media nitafanya hivyo,” Faiza ameiambia Bongo5.

Ameongeza kuwa aliamua kuzaa mtoto wa pili kwa sababu umri unaenda na malengo yake yalikuwa akifikisha miaka 35 tayari awe na watoto na hao alionao wanamtosha.

Faiza ni mama wa watoto wawili, Sasha na Li Junior.

Kijana Mwingine wa Kitanzania Auawa Nchini London Kwa Visu

$
0
0
KIJANA wa Kitanzania kutoka Zanzibar mwenye umri wa miaka 24 (jina bado halijafahamikia) aliyekuwa nchini Uingereza, anadaiwa kuuawa kwa kuchomwa visu na watu wasiojuliakana jana Alhamisi Mei 17, 2018 jioni huko Barking London.

Polisi jijini London wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema walipewa taarifa na mtu wa karibu wa kijana huyo, walipofika walijitahidi kumpatia huduma ya kwanza lakini alipoteza maisha kabla akiwa njiani kupelekewa Hospitali kutokana na majeraha makubwa na kuvuja damu nyingi kufuatia kuchomwa visu sehemu mbalimbali za mwili wake.

Aidha, Polisi wamesema bado hawajamkamata mtuhumiwa yeyote wa mauaji hayo, lakini wanaendelea na uchunguzi wa mauaji hayo ya kinyama na mengine ambayo yameshamiri kwa siku za hivi karibuni yakihusisha kuchomwa visu, milipuko na kupigwa risasi kwa raia.

Kwa mujibu wa chanzo cha www.globalpublishers.co.tz kilichopo London Uingereza, inasemekana kijana huyo ni mtoto wa Mzee Nassor Juma kaka wa Nassra Juma anayefanya kazi katika Idara ya Uhamiaji Zanzibar.
Imearifiwa kuwa, kwa mwaka huu pekee, polisi wamepokea kesi za matukio zaidi ya 60 ya mauaji ambapo 39 ni ya kuchomwa visu na 10 ni ya kupigwa risasi.


Meya wa London, Sadiq Khan amelielezea tukio hilo kuwa ni la kinyama zaidi na limeacha pengo kubwa kwa ndugu na familia huku Mbunge wa Barking, Dame Margaret Hodge kupitia mtandao wa Twitter akitoa salam za rambirambi kwa familia ya marehemu.

CREDIT: BBC NEWS

Mama Diamond Afunguka Kumshushia Kipigo cha Nguvu Hamisa Mobetto...Kisa Kizima Hichi Hapa

$
0
0
BAADA ya kuvuma kwa taarifa mitandaoni kuwa mama wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’ amempa ‘vitasa’ mwanamitindo Hamisa Mobeto, Ijumaa limemtafuta bi mkubwa huyo na kufanya naye mahojiano maalum (exclusive) ambapo amefungukia sakata hilo kwa kirefu.

Mama Diamond alifungukia hilo la kumpiga Mobeto ambaye amezaa mtoto mmoja na mwanaye, Jumanne iliyopita katika mahojiano maalum yaliyofanyika katika duka la bintiye, Esma Khan ‘Esma Platnumz’ lililopo maeneo ya Afrika Sana jijini Dar.

 ISHU ILIPOANZIA

Mama Diamond alisema ishu hiyo ilianzia Mei 13, mwaka huu mara baada ya yeye pamoja na Diamond kutoka kwenye shoo ya msanii wa Kundi la Wasafi Classic Baby (WCB), Mbosso.

Alisema, kwa kuwa walirudi nyumbani kwao Madale usiku, yeye alilala katika chumba chake bila kujua Diamond amelala na Mobeto chumbani kwake.



KULIPOPAMBAZUKA

Bi mkubwa huyo alisema, kulipopambazuka, alikwenda kwenye mishemishe zake na aliporejea ndipo alipoliamsha dude baada ya kushtukia mrembo huyo amelala nyumbani hapo.



MAHOJAINO KAMILI YALIVYOKUWA

Ijumaa: Hivi hizi tetesi za kumpiga Hamisa, mpaka kumvua wigi ni za kweli au uzushi tu?

Mama Diamond: Uzushi wa kivipi? Ni kweli.

Ijumaa: Kwa hiyo ni kweli ulimpiga?



Mama Diamond: Ndiyo na wigi nikamvua.

Ijumaa: Kwa nini sasa ulimpiga na ni mzazi mwenzie na mwanao?

Mama Diamond: Hayo mambo ya mzazi mwenzie ni huko, pale Madale ni kwangu na simtaki nyumbani kwangu kabisa.

 Ijumaa: Kuna kosa lolote alishawahi kufanya kwako labda?

Mama Diamond: Kitendo cha kuniitia mimi Shilawadu (kipindi cha udaku cha Televisheni ya Clouds) kilinikera sana halafu nikaanza kutukanwa kwenye mitandao ya kijamii.

 KWA NINI KILIMUUMA?

Kwa muda mrefu mashabiki wa ubuyu Bongo walikuwa hawajui kiini cha ugomvi wa mama Diamond na Mobeto lakini sasa ameweka bayana.

Iko hivi, mapema mwaka jana, wakati Hamisa alipokuwa amenasa ujauzito wa Diamond ambaye wakati huo alikuwa kwenye uhusiano mzito na Zari, walikubaliana kufanya siri jambo hilo ili Zari asiusome mchezo.

 Mama Diamond inaonekana alikuwa kwenye huo ‘mpango mkakati’ wa kuficha ujauzito wa Mobeto hivyo kitendo cha kuwaita Shilawadu wamshuti alipokwenda kumuona hospitalini wakati Mobeto alipojifungua ndicho kilichomkera zaidi mzazi huyo.

Baada ya habari za Diamond kutembea na Mobeto kuvuma chini kwa chini kwa muda mrefu, kupitia vipande video vilivyorushwa na Shilawadu, vilimfanya Zari athibitishie pasi na shaka kwamba kweli Mobeto amezaa na Diamond.



TUENDELEE NA MAHOJIANO…

Ijumaa: Sasa inawezekana alishajua kosa lake ameamua kujirudi mama, huoni kama unapaswa kumsamehe?

Mama Diamond: Yaani kiufupi simpendi na simtaki na kila akikanyaga hapa kwangu ni kipigo tu.

Ijumaa: Kuna mtu yeyote alikutonya kuwa Mobeto yuko ndani siku ya tukio?

 Mama Diamond: Ni kama zari tu. Mimi nafikiri kama mganga wake kamtuma aje anijaribu afike tena kwangu aone kama sitomfanya kitu kibaya.

Ijumaa: Kwa sababu gani lakini umfanyie kitu mbaya kwani kulala na Diamond ni kosa?

Mama Diamond: Alipokuja kiwizi usiku ule na kulala nyumbani kwangu, alipaswa kuondoka kabla sijamuona kwa nini alisubiri mimi nimkute maana siku hiyo asubuhi yake nilitoka na nilivyorudi ndipo nikamkuta.

 Ijumaa: Ulivyomkuta ikawaje?

Mama Diamond: Mimi nilimsubiri tu getini na nilishajiapiza lazima nimpige.

Ijumaa: Sasa varangati lote Diamond alikuwa wapi?

Mama Diamond: Yupo na yeye ndiyo alimsaidia kumuamulia mimi nikabaki na wigi la sivyo ingekuwa shida.

 Ijumaa: Kwa hiyo baada ya kubaki na wigi yeye alifanyaje?

Mama Diamond: Alikimbia na viatu mkononi, maana nilikuwa nimeshavitupa nje ya nyumba yangu.

Ijumaa: Kuna sababu nyingine kubwa ya kumchukia Mobeto?

Mama Diamond: Kwanza tu siyo mwanamke wa kuoa (wife material) hajui kutandika hata kitanda wala kufanya tu usafi ni shida.

 Stori:IMELDA MTEMA, DAR

Bashe Aibua Mazito Bungeni..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya May 19

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya May 19

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0


Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Kubenea Acheza Kamari Bungeni "Mbunge CCM Akikwamisha Bajeti Hii Nisilipwe Mshahara"

$
0
0
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema), amesema kama atatokea Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi CCM) akakwamisha bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ataruhusu mshahara wake asilipwe.

Amesema pamoja na kwamba baadhi ya wabunge wa CCM wanaonyesha kutoridhishwa na baadhi ya bajeti za wizara lakini hawana uwezo wa kuzuia bajeti kwa kuwa wanazuiwa na chama chao kufanya hivyo.

Kubenea ameyasema hayo bungeni leo alipokuwa akichangia bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2018/19.

Katika hatua nyingine kubenea ameliambia bunge kwamba anatarajia kuwasilisha hoja binafsi bungeni akitaka bunge liunde kamati maalumu kuchunguza operesheni sangara inavyotekekezwa katika Ziwa Victoria.

“Operesheni hiyo lazima ichunguzwe kwa sababu imeumiza wavuvi na wananchi kwa ujumla,” amesema.

Naye Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa (CCM) amesema matatizo yaliyoko nchini yamesababishwa na baadhi ya wataalamu ikiwamo kupiga chapa mifugo huku wakijua wanaharibu ngozi.

Mgombea CCM Akamatwa Akigawa Rushwa

$
0
0
Mgombea wa nafasi ya Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Kilangala, Halmashauri ya Wilaya ya Lindi, Jenga Mohamedi  na wajumbe saba wa Mkutano Mkuu wa kata wa chama hicho wamekamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wakidaiwa kupokea na kutoa rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 18, Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Lindi, Steven Chami amesema watu nane wamekamatwa akiwamo Mgombea ukatibu aliyekutwa akitoa rushwa kwa wajumbe ili achaguliwe.

Kwa mujibu wa Chami, tukio hilo limetokea jana saa mbili asubuhi kwenye eneo la uchaguzi huku watuhumiwa wakiwa  na fedha Sh 2,000  kila mmoja huku mpambe wa mgombea huyo alikutwa na bulungutu kiasi hicho cha fedha zenye thamani ya Sh 50,000 na orodha ya majina ya wajumbe wa mkutano huo.

Alisema watuhumiwa wanashikiliwa  na Taasisi hiyo hadi mahojiano yatakapo kamilika na hatua zingine za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Maskini, Mwanafunzi Afariki kwa Mlipuko wa Simu ya Mkononi

$
0
0
Mwanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Sabasaba jijini Mwanza, Dotto Baraka (13) amefariki dunia baada ya kulipukiwa na betri ya simu aliyokuwa akiiunganisha na radio chakavu.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amethibitisha tukio hilo ambapo amesema limetokea Mei 17, mtaa wa Igoma Mashariki jijini Mwanza.

“Baada ya kutoka shuleni, marehemu akiwa na watoto wenzake alianza kutengeneza radio chakavu kwa kuchukua betri ya simu na kuunganisha kwenye nyanya za radio hiyo akitumia mdomo ndipo mlipuko ulipotokea na kusababisha kifo chake," amesema Kamanda Msangi.

Aidha Kamanda Msangi ameongeza kuwa wakati tukio hilo linatokea, wazazi wa watoto hao walikuwa safarini huko wilayani Kahama mkoani Shinyanga. Hata hivyo katika tukio hilo hakuna mtoto mwingine aliyejeruhiwa.

PICHA: Lowassa na RC Gambo katika mazishi ya DC Mstaafu Molloimet

$
0
0
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Monduli na Mkuu wa wilaya Mstaafu Luteni Mstaafu Lepilal Ole Molloimet aliyefariki dunia Jumapili iliyopita amezikwa leo wilayani Longido.

Luten Molloimet amefariki dunia kwa ugonjwa wa shinikizo la damu, moja ya viongozi waliohudhuria mazishi hayo ni mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA, Edward Lowasa pamoja na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.

Bashe "Ukisema Ukweli Unaambiwa Unamchukia Magufuli

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussen Bashe (CCM), amesema kwamba Bungeni kumekuwa na siasa mbaya za kuamini kila anayesema ukweli anamchukua Rais Magufulii ilihali anaisaidia serikali kuikumbusha mapungufu yake na kuyafanyia kazi ili kuboresha utendaji na kupeleka maendeleo kwa wananchi.
Bashe amesema hayo Bungeni jijini Dodoma leo Ijumaa, Mei 18, 2018 wakati akichangia hoja kuhusu Bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliyowasilishwa bungeni na waziri wake, Luhaga Mpina.

 ” Sisi hatuna nia mbaya na mawaziri, humu ndani kumekuwa na siasa mbaya sana, kila anayejaribu kusema ukweli anapewa jina kwamba anamchukia Rais Magufuli. Mimi simchukii Rais, nilimchagua kwa kumpigia kura, nilimpigia kampeni kwa siku 60, ninafahamu atakuwa mgombea wangu wa urais mwaka 2020 ndiyo maana nayasema haya.

 “Kama ningejua Rais Magufuli siyo mgombea wangu mwaka 2010 wala nisingejali kusema haya ninayoyasema ndani ya bunge, mimi nitaendelea kusema ilihali nipo ndani ya bunge hili. Naomba hii bajeti irudi, wala siyo kwa nia mbaya….. Bajeti ya Maendeleo iliyotengwa katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi mwaka jana ni asilimia sifuri, tunaenda wapi?

 “Mvuvi amekataliwa kuvua, option yake ni nini? Tunamtia umaskini mkulima…. Nchi yetu leo mkulima ananyanyasika, mfugaji ananyanyasika, mvuvi ananyanyasika, machinga ananyanyasika, mfanyabiashara ananyanyasika, nataka nikwambie Mhe. Spika, unda kamati, mimi siyo mtaalam wa kanuni,” alisema Bashe.

Paul Makonda Ayakana Makontena Yaliyoko Bandarini

$
0
0
Utata umeendelea kuandama umiliki wa makontena 20 yaliyotajwa na Mamlaka ya Mapato (TRA), kuwa miongoni mwa yale yatakayopigwa mnada kwa kukaa bandarini muda mrefu, baada ya mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kukana kuwa sio ya kwake.

Awali, TRA ilitoa tangazo katika gazeti la Daily News, ikisema mtu aitwaye Paul Makonda bila kubainisha kama mtajwa ni mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam au la, anamiliki makontena 20 yenye bidhaa mbalimbali zikiwamo samani katika bandari kavu ya DICD.

Hata hivyo, akizungumza jana wakati akizindua kamati ya mapendekezo kuhusu wanawake waliotelekezwa na wenza wao, Makonda alisema hajui chochote na amesikia habari hizo kwenye magazeti kama walivyozisikia watu wengine.

“Sidhani kama nahusika na jambo lolote lile na sijui chochote, hilo unalolisema hata mimi nimesoma kwenye magazeti kama ulivyosoma wewe. Nafikiri zilikuwa ni habari za jana na leo nimesoma nyingine,” alisema.

Makonda alisema Serikali hufanya kazi zake kwa maandishi na yeye hana nakala yoyote inayohusiana na mzigo huo.

“Sio suala la kwangu kabisa, nimekusikia wewe kama mimi nilivyosikia jana (juzi) na ninafikiri tutaendelea kusikia hivyo hivyo na ndio maana katika hizo habari hakuna sehemu yoyote umeona nimenukuliwa kusema kama ni mali zangu,” alisema Makonda.

Hata hivyo, Februari 16, Makonda alikaririwa na  gazeti la Serikali la HabariLeo kuwa alipokea makontena 20 yenye samani zitakazotumika katika ofisi za walimu zinazoendelea kujengwa ukiwa ni sehemu ya shehena ya makontena 36.

Ilielezwa kuwa samani hizo za ofisini zilizokuwa na thamani ya Sh2 bilioni, zilitolewa na Watanzania wanaoishi Marekani wanaojulikana kama Six Region Diaspora Council.

Mei, 12 kaimu kamishna wa Forodha na Ushuru wa TRA, Ben Asubisye alisema wamiliki wa mizigo hiyo wanatakiwa kuikomboa ndani ya siku 30 kuanzia siku hiyo. Katika tangazo hilo lenye orodha ya makontena zaidi ya 800, jina la Paul Makonda limejitokeza mara 20 akiwa mpokeaji wa makontena 20 yakiwa na bidhaa kadhaa, zikiwamo samani.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo alisema juzi kuwa mamlaka hiyo imetoa notisi ya siku 30 kwa waagizaji wa mizigo ambayo imekaa bandarini kwa zaidi ya siku 90.

“Tangazo lililotolewa ni notice (taarifa) kwa wahusika ili wakomboe mizigo yao ndani ya siku 30. Isipokombolewa itanadiwa. Mizigo hiyo inaweza kuwa ni ile ambayo haijalipiwa kodi au hata ile iliyolipiwa lakini haijaondolewa,” alisema.

Alipoulizwa kama shehena hiyo ni mali binafsi ya Makonda au ya ofisi yake, Kayombo alisema: “Majina yaliyoandikwa kwenye magazeti ndiyo taarifa za consignees (wapokeaji) zilizopo kwenye nyaraka.”

Ushauri: Mama Mkwe na Ndugu zake Wamepanga Waje Kwangu Kunihoji Kwanini Sifungi ndoa

$
0
0
Habari wakubwa;
Mimi naishi na mwanamke miaka 5 sasa sijafunga nae ndoa, Tumebahatika kupata mtoto mmoja ambaye kwa sasa ana miaka 4, mimba ambayo nilimtia punde tu baada ya kumaliza chuo;
bahati mbaya nilipomaliza chuo sikubahatika kupata ajira, nikawa naishi kwa kufanya vibarua elfu 50 kwa week, wakati nikifanya vibarua hivyo nikiwa naishi nae, aliniambia japo nikajitambulishe kwao, sikuwa na kipingamizi nikaapeleka barua ya uchumba, nikajibiwa pamoja na kupewa kiwango cha posa ambacho sijafanikiwa kukilipa hadi Leo.

SABABU ZINAZONIKWAMISHA NISIFUNGE NDOA
Katika history nakumbuka Wakati tukiwa chuo, Mimi nikiwa dar na yeye akiwa mkoani, yeye alikuwa anapokea bumu kubwa kuriko Mimi, lakini kila changamoto aliyopata kwa kidogo nilichonacho nilimrushie yeye punde tu aliponililia shida,
Mimi kila nilipokumbana na shida nilipokuwa nampigia kusema ukweli alikuwa mgumu sana, na hata anapofikia kutoa alinipa huku akisema sema maneno, nilivumilia, lakini ilikuwa inaniuma sana vile nilivyotumia nguvu kubwa kupata msaada wake, wakati Mimi akipatwa na shida nilikuwa tayar kushinda njaa ili nimtumie yeye!..

Nakumbuka siku moja nilimuomba aniazime elfu 10 ya kula, akaniambia hana, Mungu si athumani jioni yake akanipigia simu kwamba yuko polisi kuriport kaibiwa laki mbili mchana, aliniambia hivyo huku tayari akiwa amesahau kwamba nilimuomba hela ya kula anitumie akaniambia hana hela.........Nyway HAYO YOTE YA NYAKATI ZA CHUO NILISAMEHE NIKAJUA NI DHIKI ZA CHUONI TU ATABADILIKA.

Tukiwa tunaishi nae, kuna kikazi kilipatikana nikamuunganishia akapata, bahati mbaya wakati akiwa anaendelea na kazi Mimi kibarua kikasimama,
akiwa na ile kazi kiila nikimpgia simu alikuwa busy sana, yaan hata akisema subiri kidogo nitakupigia, wala hakupiga, na kwangu akahama akaenda kuishi kwa mama yake,
hata kodi ya nyumba ilivyoisha alinijibu majibu ya ajabu sana....anyway nisiseme sana lakini mwisho Wa siku nilihangaikaa wee nikafanikiwa kuendeleza maisha kivingine lakini mamamkwe wala hakunitetea,

Baada ya kupata kazi , niliendesha maisha yangu vizuri, aliposikia nimepata kazi akaanza kuja kunisalimia kwa kisingizio cha kufuata hela ya matumizi ya mtoto, Mara anakuja analala, Mara akasema kule anapokaa kwa mama yake pamebana kwahiyo akaamua kurudi, akawa anapika na kupakua; Baada ya Muda akaanza kuniuliza ndoa tunafunga lini! Nikamjibu sipo tayari kwa sasa,
Hali hii imeendelea hivohivo, Akaniuliza kwanini tunaishi pamoja? nimekuwa nikimjibu Arudi kwao hadi nitakapokuwa tayari nitamfuata,

Kwanza kabisa akipanga lake au kuondoka hata usipompa ruhusa yeye huwa anatoka, kiufupi huwa ananipa taarifa siyo kuomba ruhusa; Siku alikwenda kwa mama yake nikampigia simu mama yake kumuuliza kwanini binti yake kaondoka bila kuaga? Mama Mkwe alinijibu kwamba wewe si unamkataza asije kusalimia kwao!...nikamjibu mamamkwe Basi akae huko huko asirudi;
Baada ya siku mbili akawa karudi, sikumfukuza nikamuacha;
Kiila siku ananiuliza ndoa lini? na Mimi namjibu, Unataka Hayo matatizo yako niyafungie ndoa? Nikamwambia waambie hao ndugu zako wanaokutuma kwamba; Tabia yako haijanivutia kufunga ndoa;

Tangu nimjibu hivo Mama yake anataka twende anataka tuongee, kutokana na hasira zangu, nilimwambia binti yake amwambie sitaenda,
Baada ya kuambiwa hivo, MAMAMKWE KESHO JUMAPILI WAMEKUBALIANA KUVIZIA MIMI NISIPOTOKA WAJE KUZUNGUMZIA SUALA LA NDOA!

Je; Niwaambie laivu kwamba tabia ya binti yao haijanivutia? au nitumie lugha ya kistaarabu niseme bado najipanga?
maana hadi napata hofu maana ndo kwanza nimemaliza kujenga nyumba mbona wanaforce ndoa?

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Chin Bees afunguka ishu ya cover ya album yake kufanana na cover ya ‘A Boy From Tandale’ ya Diamond

$
0
0
Kama wewe ni mfuatiliaji wa muziki wa Bongo Fleva ukiangalia kwa makini utaona Cover ya album ya ‘LADHA’ ya Chin Bees imefanana kawa kiasi kikubwa na cover ya ‘A Boy From Tandale’ ya Diamond Platnumz.

Sasa Chin Bees amefunguka kwa mara ya kwanza kupitia Bongo5 kuhusu kufanana huko kwa cover za album mbili ambapo amesema yeye hakujua chochote kwani alihitaji picha ya nyoka kwenye cover yake lakini mwisho wa siku alishangaa kuona cover imewekwa picha yake.

Album ya A Boy From Tandale ya Diamond Platnumz imeachiwa rasmi mtandaoni Machi 14, 2018 huku Chin Bees album yake ya Ladha ambayo alitoa bure kwa mashabiki wake imeachiwa siku mbili mbele Machi 18, 2018.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images