Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Baada ya kukosa Penalti Okwi amwaga machozi

$
0
0


STRAIKA wa Simba, Mganda, Emmanuel Okwi aliangua kilio mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli baada ya kukosa penalti iliyopanguliwa na kipa wa Kagera Sugar, Juma Kaseja.

Simba ilijikuta ikilala bao 1-0 Kagera Sugar kwenye mchezo huo uliopigwa jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kuzima ndoto yao ya kumaliza Ligi Kuu Bara bila ya kupoteza mechi baada ya kufungwa kwa mara ya kwanza msimu huu.

Simba ilipata penalti baada ya Okwi kuchezewa rafu na George Kavila wa Kagera Sugar ambayo aliipiga lakini ilipanguliwa na Kaseja, ambaye ni kipa wa zamani wa timu hiyo.

Hatua hiyo ilikuwa pigo kwa Okwi kwani aliipotezea nafasi timu yake ya kusawazisha baada ya Kagera Sugar kuongoza kwa bao lililopachikwa na Edward Christopher katika dakika ya 85.

Mganda huyo alitoka uwanjani huku akilia na wenzake wakimbembeleza kutokana na kupoteza penalti hiyo.

Okwi pia alikuwa na hisia kali za kumbukumbu kiungo wa zamani wa Simba, Patrick Mafisango, ambaye alizikwa siku kama ya leo Mei 20, 2012 nchini Congo baada ya kufariki kwa ajali ya gari jijini Dar es Salaam.

Straika huyo baada ya mechi alivalia fulana iliyonadikwa `For you Brother Mafisango’ (Hii ni kwa ajili yako Kaka Mafisango).

Kwa upande mwingine, shabiki mmoja wa Simba ambaye jina lake halikufahamika alipoteza fahamu mara baada ya Okwi kukosa penalti.

Manara ashangiliwa
Tukio jingine la kuvutia ilikuwa pale mashabiki wa Simba, walimpomzingira kwa furaha msemaji wa klabu hiyo, Haji Manara baada ya kupokea kombe.

Manara, ambaye alikuwa na furaha kubwa baada ya timu kukabidhiwa kombe pia aliungana na wachezaji na kuzunguka uwanja huku akicheza muziki wa singeli uliokuwa unapigwa uwanjani hapo.

Sugu kutinga bungeni kesho May 21

$
0
0

Siku 11 baada ya mbunge wa Mbeya, (Chadema) Joseph Mbilinyi maarufu ‘Sugu’ kuachiwa huru, kesho Mei 21, 2018 ataingia bungeni.


Sugu ataingia bungeni kuwawakilisha wananchi wa Mbeya baada ya kulikosa bunge hilo la bajeti tangu lilipoanza Aprili mwaka huu.


 Sugu amesema: “Nipo Dodoma tayari, nimekuja baada ya hali ya mama yangu kuendelea kuimarika na kesho (Mei 21,2018) nitaanza kuwawakilisha wana Mbeya walionituma.”


“Wana Mbeya walikosa mwakilishi, walikosa wa kuwasemea mambo yao, kwani kilichotokea juu yangu ilikuwa kuwanyima fursa Mbeya kusikika ndani ya mjengo, sasa nimerudi kuwatumikia kwa nguvu zangu zote.”


Amesema kile kilichomtokea kimemwongezea umaarufu zaidi ya aliokuwa nao, “unajua mimi nilikuwa maarufu lakini kwa hiki kilichonitokea, nimekuwa mashuhuri na si maarufu tena.”


“Nikiwa njiani, Makambako wananchi wamenipa pole na wengine pongezi, sawa na Iringa na hapa Dodoma na kila mahali ninapopita, watu wanapiga picha na mimi, sasa utasema ni maarufu, mimi ni mashuhuri,” ameongeza:


Sugu na Katibu wa Chadema, Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga walihukumiwa Februari 26, 2018 kwenda jela miezi mitano na Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mbeya baada ya kuwakuta na hatia ya kutoa lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.


Mei 10, Sugu na Masonga waliachiwa huru kwa msamaha wa Rais Magufuli alioutoa Aprili 26, 2018 wakati wa sherehe za Muungano

Watuhumiwa wa ujambazi wapigwa mawe hadi kufa

$
0
0

Watu watatu wanaotuhumiwa kuwa majambazi wamepigwa mawe hadi kufa na wananchi wa Kijiji cha Bubare Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera.


Watuhumiwa hao waliuawa baada ya kuwekewa mtego kutokana na kuwapo taarifa za wao kutaka kuvamia nyumba ya mmoja wa wakazi wa kijiji hicho kwa nia ya kupora fedha za mauzo ya mifugo.


Baadhi ya viongozi wa Serikali ya kijiji waliojaribu kuwazuia wananchi kuwashambulia watuhumiwa hao, walilazimika kutimua mbio kuokoa maisha yao baada ya kugeuziwa kibao na kuanza kushambuliwa.


Mkuu wa Wilaya ya Missenyi, Denis Mwila alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi wanapowakamata watuhumiwa, badala yake wawafikishe kwenye mikono ya vyombo vya dola kwa hatua za kisheria.


Akizungumzia namna njama za watuhumiwa hao zilivyojulikana na kuwanasa, Mkuu huyo wa wilaya alisema uongozi wa kijiji na jeshi la polisi walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu watu kutaka kuvamia nyumba ya mkazi huyo aliyeuza mifugo yake Mei 16. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi alisema uchunguzi kuhusu tukio hilo unaendelea na kuahidi kutoa taarifa baadaye

Wastara Thomas Afunguka Tena Kuhusu Utapeli

$
0
0



 Msanii wa kike wa filamu Bongo Wastara Juma amefunguka juu ya picha aliyopost instagram na kuzua mjadala kwa baadhi ya watu, huku wakimtuhumu kupanga njama za kutapeli kwa kutumia ugonjwa wake, ambao ulikuwa unamsumbua muda mrefu na kusababisha kupelekwa India kwa matibabu.

Akizungumza na www.eatv.tv Wastara amesema kwamba kitendo cha watu kumfikiria vibaya  kinamtia uchungu na kinamvunja moyo, kwani ukizingatia hakuomba kupata matatizo aliyopata, na kwamba picha aliyopost ni ya muda mrefu akiwa nchini India.

“Kwa kweli inasikitisha na inavunja moyo sana kama Mtanzania, na kama mtu ambaye nina haki zote kama wengine, hii ni picha ambayo niliipiga wakati nipo India,  na nafikiri nilieleza pia nilikuwa na matatizo ya kichwa, kwa hiyo ni moja ya kipimo na matibabu pia, kwa hiyo hiyo picha ni ya zamani wakati nipo India”, amesema Wastara.

Wastara amesema kwa sasa anaendelea vizuri na matibabu na hakuna tatizo linalomsumbua, hivyo watu wasitilie maanani maneno ya watu wanaomsema mabaya ili aonekane mbaya kwa jamii.

Mwanamuziki Beyonce Anunua Kanisa na Kuanzisha Dini yake

$
0
0

Msanii maarufu wa muziki duniani, Beyonce amenunua jengo la kanisa kongwe mjini New Orleans nchini Marekani.

Kanisa hilo ambalo limejengwa kwa mawe miaka ya 1900’s limemgharimu Beyonce kiasi cha dola $850,000 sawa na tsh bilioni 1.9 .

Kwa mujibu wa taarifa kutoka mitandao mbalimbali ya burudani duniani ikiwemo TMZ na Shaderoom zinaeleza kuwa lengo la kununua kanisa hilo ni kueneza dini yake ya Beyism.

Beyism ni dini ambayo wafuasi wake wanamsujudu Beyonce kama mungu wao na tayari imeshapata maelfu ya wafuasi nchini Marekani.

Mwaka 2014, waumini wa dini ya Beyism walianzisha kanisa lao rasmi la Beyonce walilolipa jina la ‘The National Church of Bey’ huko mjini Atlanta nchini Marekani.

Waumini wa Kanisa hilo wanaimba nyimbo za Beyonce na kusoma biblia maalumu zinazoitwa beyble.

Kanisa hilo la Beyonce limepambwa na picha nzuri za Beyonce akiwa amevalia mavazi ya nguo kama za viongozi wengine wa makanisa ya kikristo.

Anachotarajia Shaffih Dauda baada ya mabadiliko Simba

$
0
0
Jumapili Mei 20, 2018 klabu ya Simba imefanya mkutano mkuu wa dharura kwa ajili ya mabailiko ya katiba yao ili kuendana na mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu hiyo.

Wanachama wa Simba kwa pamoja wamepiga kura ya ndio kupitisha mabadiliko ya katiba yao ili kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa klabu ambapo kuanzia sasa klabu hiyo itaendeshwa kwa mfumo wa hisa.

Mwekezaji Mohammed Dewji amechukua hisa asilimia 49 na wanachama wengine wamebaki na hisa 51%.

Baada ya mabadiliko hayo ya mfumo na katiba ndani ya Simba, Shaffih Dauda amesema tatizo la vilabu vya Simba na Yanga sio mfumo tatizo ni watekelezaji wa mfumo husika.

“Tatizo la Simba na Yanga siamini kama ilikuwa ni mfumo uliokuwepo, mfumo si tatizo wanaoingia kwenye mfumo kwa ajili ya utekelezaji ni akina nani?

“Mfumo unaweza ukabadilishwa lakini inapokuja suala la utekelezaji hapo ndio kwenye tatizo. Ukifuatilia vizuri sio tatizo kwenye mpira peke yake, ‘human capital’ ni tatizo kubwa la nchi.”

“Tunachotarajia kuona ni Simba mpya yenye vitega uchumi, viwanja, hostels, academies, uongozi unaoeleweka, ili hayo yote yawezekane wanahitajika watu wenye taaluma na uwezo wa kutekeleza hivyo vitu.”

“Hongera kwa wanasimba kwa kukubali kufanya mabadiliko ya mfumo.”

Kwaninj Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA,

Wastara Amlipua Mange Kimambi........ Asema Ndiye Mbaya Wake Anayemchafua

$
0
0
Wastara Amlipua Mange Kimambi........ Asema Ndiye Mbaya Wake Anayemchafua
Msanii wa muziki wa filamu bongo Wastara Juma amemtaja mtu ambaye yeye amemuita mbaya wake, anayemchafua kwenye mitandao ya kijamii kwa kumtuhumu masuala ambayo hayana ukweli.


Akizungumza na www.eatv.tv, Wastara amesema anajua mtu anayeleta habari za uongo dhidi yake ni Mtanzania anayeishi nchini Marekani Mange Kimambi, na kusema kwamba huenda yeye ana uhakika kuwa hatapata matatizo kama binadamu wengine.

“Hii yote tangu ilipotokea upinzani, mimi nasema mpinzani wangu mkubwa alikuwa Mange, na yeye ndiye ambaye alikuwa anacomnt vibaya na wale waliokuwa wanasuport kwenye acount yake, nadhani hawa hawajahi kupitia matatizo, na siku wakifa watapaa mbinguni, familia zao zikiugua hawata pata matatizo, ndio maana wanakuwa hawana huruma”, amesema Wastara.

Wastara ameendelea kwa kusema kwamba anashangazwa na kitendo cha mwanamke huyo kumuonyesha chuki ilhali hajawahi kumkosea kitu, na kuwataka Watzania kuwa na huruma kwani lichaya kuwa yeye ni binadamu pia ni mama ambaye anahitaji kulea watoto wake.

Msuva Kukosa Ligi ya Mabingwa

$
0
0
Msuva Kukosa Ligi ya Mabingwa
Nyota wa kimataifa wa Tanzania Simon Msuva usiku wa jana, amecheza mchezo wa mwisho kwenye ligi kuu ya soka nchini Morocco na kuifungia bao timu yake ya Difaa Hassan El Jadida dhidi ya Olympic Safi.

Msuva alifunga bao hilo dakika ya 43 katika mchezo huo wa ligi hiyo maarufu kama Botola Pro uliofanyika Uwanja wa Ben Ahmed El Abdi, El Jadida mjini Mazghan.

Pamoja na ushindi huo wa bao 1-0 lakini haujaisadia timu hiyo kucheza michuano ya kimataifa msimu ujao, baada ya kumaliza katika nafasi ya 5 kwenye msimamo wa ligi ya nchini humo.

Difaa Hassan El Jadida imefikisha pointi 48 baada ya kucheza mechi 30 na ipo nyuma ya FUS Rabat yenye pointi  49, Hassania Agadir pointi 51 sawa na Wydad Casablanca.

Difaa msimu huu inashiriki hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Africa na ilitoka sare ya 1-1 na MC Alger nchini Algeria na kufungwa 2-0 nyumbani na TP Mazembe. Timu hiyo itakamilisha mechi zake za mzunguko wa kwanza wa kundi  B kwa kumenyana na ES Setif nchini Algeria Julai 17

Rais wa Palestina Mahmoud Abbas Alazwa Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Rais wa Palestina Mahmoud Abbas Alazwa Kisa Hiki Hapa
Leo May 21, 2018 Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amelazwa katika hospitali moja kwenye Ukingo wa Magharibi kutokana na matatizo yaliyotokea baada ya upasuaji mdogo wa sikio aliofanyiwa wiki iliyopita.

Hii ni mara ya tatu, Abbas analazwa katika kipindi cha wiki moja.

Abbas aliwasili hospitalini baada ya kiwango chake cha joto mwilini kuenda juu.

Hata hivyo, shirika la habari la WAFA limesema kwamba uchunguzi wa kimatibabu aliofanyiwa rais huyo umeonesha kwamba hali yake ni nzuri.

Siri Yavuja Baada ya Harusi ya Mwanamfalme Kufanyia ‘Honey Moon’ Afrika, Nchi Mbili Zatajwa

$
0
0
Siri Yavuja Baada ya Harusi ya Mwanamfalme Kufanyia ‘Honey Moon’ Afrika, Nchi Mbili Zatajwa
Ikiwa ni siku moja imepita tangu harusi ya kihistoria ya kifalme ifanyike nchini Uingereza, kati ya Prince Harry na Meghan Markle sasa maswali mengi yanakuja ni wapi wanandoa hao watakwenda kwa ajili ya fungate (Honey Moon).

Kwa mujibu wa mtandao wa Travel + Leisure umeeleza kuwa wawili hao huenda wakaja Afrika kwa ajili ya fungate na nchi zilizotajwa ni Namibia na Botswana.

Hata hivyo, vyanzo vingi vya habari vinaitaja nchi ya Namibia kuwa ndiyo itakuwa sehemu ya kwanza kwa wawili hao kupumzika kwa ajili ya fungate.

Mwaka 2017 kwenye birthday ya Meghan, wawili hao walienda nchini Botswana kwa ajili ya kusherehekea siku hiyo ya mfanano wa kuzaliwa.

Kwa mujibu wa mtandao wa jarida la Vogue, bajeti ya Honey Moon kwa wawili hao ni Dola $221,175 sawa na tsh milioni 505.

Wawili hao kabla ya kuanza fungate wanatarajiwa kwenda nchini Mexico kumuona baba mzazi wa Meghan, Thomas Markle (75) ambaye hakuhudhuria kwenye harusi kutokana na maradhi ya moyo yanayomsumbua kwa muda mrefu.


Hamisa Mobeto Apewa Kichapo na Mama Daimond Afunguka Mazito.... Hata Vikombe Kabatini Vinagongana

$
0
0
Hamisa Mobeto Apewa Kichapo na Mama Daimond Afunguka Mazito.... Hata Vikombe Kabatini Vinagongana
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amefunguka kuhusu taarifa zilizodai kuwa amepigwa na mama mzazi wa Diamond Platnumz, Sanura Kassim ‘Sandra’.

Hapo jana katika uzinduzi wa kipindi cha Nyumba ya Imani cha Wasafi TV, Hamisa alipata time ya kuzungumza na waandishi wa habari na kusema jambo hilo ni binafsi zaidi ila kugombana kwa binadamu ni kitu cha kawaida.

“Hilo siwezi kuliongelea, yeah!. is too person, is too private, is too family. Hata vikombe kwenye kabati vinagong’ana, so sisi binadamu vinaweza kutokea,” amesema.

Alipoulizwa iwapo kwa sasa yeye na mama Diamond wana maelewano mazuri, alijibu; ‘Sina kinyongo na mtu, sina bifu na mtu, mimi am just fine, may be yeye mwenyewe sio upande wangu wa kuweza kuelezea,’.

Taarifa za Hamisa kupigwa na mama Diamond zilianza kusambaa Jumatatu ya wiki iliyopita, May 14, 2018 ambapo usiku ya jana yake Hamisa na Diamond walihudhuria katika uzinduzi wa filamu ya Aunt Ezekiel ‘Mama’ na baada ya hapo anadaiwa waliongozana hadi Madale kwa kina Diamond ambapo ndipo kisa hicho kinadaiwa kutokea.

Sugu: Viongozi Mnatakiwa Kutumia Mwezi Mtukufu Kujitathimini

$
0
0
Sugu: Viongozi Mnatakiwa Kutumia Mwezi Mtukufu Kujitathimini
Mbunge wa Mbeya, Joseph Mbilinyi (Sugu) kwa tiketi ya CHADEMA amewataka viongozi nchini kuutumia mwezi mtukufu kujitathmini.


Akizungumza leo Mei 21, kwa mara ya kwanza Bungeni tangu atoke gerezani kwa msamaha wa Rais wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amewatakia Waislam wote mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhan.

“Naomba niwatakie ndugu zangu Waislam mfungo mwema, Kwa wale viongozi naomba muutumie Mwezi Mtukufu kujitathmini, sheria hii pamoja sheria mbovu za habari zinazowabana wananchi kupata habari pia zinatumika kufunga watu jela kisiasa kwa mfano mimi nilifungwa kwa kujadiliana na wananchi wangu kuhusiana na watu kupigwa risasi, watu kutekwa, maiti kuokotwa kwenye viroba watu kutokuwa na uhru wa kuongea n.k,Ni lini sheria hizi zitafutwa ili kulinda Katiba ya nchi hususani ibara ya 18? alihoji Sugu.

Mbunge Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ aliachiwa huru gereza la Ruanda, Mbeya Mei 10 alipokuwa akitumikia kifungo cha miezi mitano.


Askofu Mkuu wa Angikana Akutana na Rais Magufuli na Kufanya Mazungumzo

$
0
0
Askofu Mkuu wa Angikana Akutana na Rais Magufuli na Kufanya Mazungumzo
Askofu wa Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Maimbo Mndolwa jana alikutana na kufanya mazungumzo ya faragha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam kabla ya kusimikwa rasmi kuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglican Tanzania.

Akifanya mazungumzo na Rais Magufuli, Askofu Mndolwa alisema kuwa, Tanzania inayokuja inaonekana anaiona yenye kuwa na neema ya kipekee licha ya changamoto zilizopo.

Chanjo ya Majaribio ya Ebola Yaanza Kutolewa Leo DRC

$
0
0
Chanjo ya Majaribio ya Ebola Yaanza Kutolewa Leo DRC
Shirika la afya Duniani (WHO) na Serikali ya Jamhuri ya Kidemkrasi ya Congo leo wameanzisha mpango wa kutoa chanjo ya majaribio dhidi ya ugonjwa wa Ebola ili kudhibiti kusambaa zaidi kwa virusi vya ugonjwa huo.

WHO linasema limewatambua zaidi ya watu 500 ambao huenda wamkaribiana na waathiriwa wa ugonjwa wa Ebola nchini Congo.

Huenda watakuwa miongoni mwa watu wa kwanza leo watakaopewa chanjo hiyo ya majiribio.

Kumekuwa na milipuko mitatu ya Ebola nchini DRC tangu janga la mwaka 2014-2016 katika Afrika ya magharibi.

Serikali Yatangaza Vita na Wanaowapeleka Wasichana Nje Kufanya Biashara ya Ngono

$
0
0
Serikali Yatangaza Vita na Wanaowapeleka Wasichana Nje Kufanya Biashara ya Ngono
Serikali imesema wajibu wake kuhakikisha Watanzania wanaopata fursa ya kufanya kazi nje ya mipaka ya Tanzania wanafanya kazi katika Mazingira mazuri na yanayolinda staha na utu wao.

Serikali imesema kama kuna wasichana wanapelekwa nje ya nchi yakufanya biashara ya ngono ikijulikana haitasita kuchukua hatua kali dhidi ya wanaofanya hivyo.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba ametoa ufafanuzi huo, leo Mei 21 Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge, Hawa Mchafu aliyeuliza,

Je ni hatua gani kali zinazochukuliwa dhidi ya wafanya biashara wanaosafirisha vijana wa Kitanzania hususani vijana wa kike kwenda nje ya nchi kwaajili ya kufanya biashara isiyo rasmi ikiwemo kuuza miili yao.? Ni ipi sasa kauli ya serikali dhidi ya madai ya kusikitisha sana kuwa baadhi ya Watanzania wanasafirishwa kwenda nje wanaenda kuuzwa figo zao?

“Kuhusu hatua gani kali zimechukuliwa kuhusu wafanya biashara ambao wamewapeleka wasichana nje kwenda kufanya biashara ya kuuza miili yao kwa kweli niseme kwamba hiyo ikijulikana hatua kali za nchi yetu zitachukuliwa lakini so far mimi sina data za aina hiyo,” amesema Dkt. Kolimba.

“Lakini kuhusu kwamba kuna Watanzania ambao wamepelekwa nje na kwamba wanapopelekwa nje figo zinachukuliwa hilo pia sisi tutafuatilia kama kuna ukweli hatua kali zitachukuliwa kwenye nchi husika.”

Haji Manara Afunguka Kuhusu Picha Zake Zinazosambaa Mitandaoni

$
0
0
Haji Manara Afunguka Kuhusu Picha Zake Zinazosambaa Mitandaoni
Baada ya kusambaa kwa video na picha zinazomwonesha msemaji wa Simba Haji Manara, akihuzunika uwanjani huku akiwa ameshika eneo la moyo amemtaja (Ankal Michuzi) ambaye ni mpiga picha wa Ikulu na alimruhusu kuzisambaza.


Manara ameeleza kuwa lengo la kuzisambaza video hizo ni kuwaonesha mashabiki nguvu ya mchezo wa soka ilivyo kubwa na wao kama viongozi huwa wanaumia pia pindi mambo yanapokuwa hayaendi vizuri.

''Anko Michuzi (mpiga picha wa Ikulu) ndiye ambae alipiga picha na video zote 'zinazotrend' mitandaoni bila mm kujijua, aliniuliza kabla ya kuziachia nikamruhusu ili Watanzania waone tunavyopagawa na hizi timu'', amesema.

Picha na Video hizo zilipigwa kwenye uwanja wa taifa juzi kwenye mchezo wa ligi kuu ambao ulikuwa maalum kwa Simba kukabidhiwa ubingwa lakini furaha yao ilitibuliwa na Kagera Sugar kwa kufungwa bao 1-0. Okwi alikosa penati ambayo ilidakwa na Juma Kaseja.

Ubingwa wa ligi kuu msimu huu ni wa kwanza kwa Simba tangu Haji Manara awe msemaji wa timu hiyo, na amekuwa akiusubiri kwa hamu huku akiwa ni miongoni mwa wanasimba ambao waliokuwa wanajivunia rekodi ya kutopoteza mchezo msimu huu.

Simba Kutumia Uwanja wake Msimu ujao

$
0
0
Kaimu Rais ya wa klabu ya Simba Salum Abdallah amethibitisaha kwamba kuanzia msimu ujao wa ligi kuu Tanzania Bara 2018/209 klabu hiyo itaanza kutumia uwanja wake wa mazoezi.


Kaimu Rais huyo amesema hayo leo Mei 20, 2018 katika mkutanao mkuu wa dharura wa klabu hiyo katika ukumbi wa mikutano wa mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa kwa msimu ujao Simba itakuwa ni timu isiyokamatika kwa maendeleo

“Msimu ujao Simba haitashikika, mnaweza kuona mambo haya yamechelewa kidogo lakini tulikuwa tunajua kiu ya wanasimba ilikuwa ni ubingwa, sasa ubingwa tumeshapata, tunaenda kuleta maendeleo katika klabu yetu, msimu ujao timu itafanya mazoezi katika uwanja wetu” amesema Abdallah

Mgeni rasmi katika mkutano huo alikua waziri wa habari, utamadunu sanaa na michezo Dkt Harrison Mwakyembe ambaye aliunga mkono mabadirko hayo kwa niaba ya serikali  na kuipongeza timu ya simba na kuomba klabu nyingine kufuata mfano kwasababu mabadiriko hayazuiliki.

Katika mabadiriko hayo wanachama wa Simba sasa watakuwa na uwezo wa kumiliki hisa 51% na mmiliki mwenye hisa nyingi ambaye ni Mohamed Dewji atamiliki 49% ya hisa katika jina la kampuni litakalojulikana kama Simba Sports Club Company Limited.

Mfumo Mpya Utavyonufaisha Wanachama Simba

$
0
0
Mwaasheria wa Simba Evodius Mtawala ametoa ufafanuzi kwa wanachama waliojitokeza kwenye mkutano baada ya wanachama kupiga kura ya kupitisha katiba mpya.

Mtawala ameelezea namna ambavyo wanachama wanaweza kunufaika na mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu ambapo mwekezaji Mohammed Dewji ‘Mo’ atamiliki hisa 49% na nyingine 51% zikibaki kwa wanachama.

“Tunapokuwa na reja ya wanachama 50,000 tukifanya uhakiki wa wanachama tutakuta tuna wanachama labda 10,000. Ili mwanachama ujue thamani yako kwenye klabu ya Simba sasa hivi katika wanachama 10,000, ukichukua bilioni 4 ambayo ndiyo fedha iliyopo ukaigawanya kwa 10,000 utakuta kila mwanachama anathamani ya shilingi 400,000.

“Tunapofungua wanachama wengine 50,000 ina maana tunahitaji wanachama wengine 40,000 ambao hawapo, ili wapate uanachama haitakuwa kama ilivyokuwa utaratibu wa zamani ulivyokuwa unatumika.

“Uanachama wao hautakuwa wa kulipia kadi shilingi 10,000 na shilingi 12,000 kwa ajili ya ada ya uanachama wa mwaka mzima. Watapata uanachama kwa kulipa sawa na stahiki yetu tutakayokuwa nayo, kwa hiyo mtu akija kuingia atanunua hisa atalipa 400,000.

“Ina maana kwamba unaposema unataka kuuza uanachama wako huyu mtu akishapata masharti ile ada anayolipa inayoendana na thani ya hisa zake kwetu kama ni 400,000 akishalipa hapa ile hela haiingii kwenye kampuni hela hiyo unapewa wews yeye nachukua nafasi yako.

“Sasa hivi unaweza kuuza uanachama wako na ukapata stahiki zako.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images