Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Kwaninj Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA,

Tunda Kanizidi Umri tu Ila si Mdogo Kama Anavyozani- Bob Junior

$
0
0
Tunda Kanizidi Umri tu Ila si Mdogo Kama Anavyozani- Bob Junior
Msanii na muandaaji wa muziki Bob Junior amesema kuwa Tunda Man amemzidi umri tu lakini kwenye kazi yeye ni mkubwa zaidi yake.


Bob Junior amesema hayo kupitia eNews ya EATV huku akisisitiza kuwa muziki ameanza muda mrefu lakini wazazi walikuwa wakimzuia na kusisitiza asome kwanza kwa kuwa alikuwa bado mdogo.

“Tunda ni kaka yangu na nina mheshimu kwakuwa kanizidi umri na baadhi ya vitu lakini kwenye kazi tuheshimiane mie sio mtoto kama anavyosema mbona nmemfanyia baadhi ya nyimbo zake tena bure wakati anaanza, sasa nani mdogo hapo kati yetu”,  amesema Bob Junior.

Hayo yamejiri baadaya msanii Tunda Man kutoa 'video' tatu za nyimbo zake mpya suala ambalo lilimuibua Bob Junior na kutoa ushauri kwa msanii huyo kuwa alitakiwa kutoa kwa awamu ili awape muda mashabiki wake.

Sugu Atoboa Hali ya Jeshi la Magereza "Magereza Kuna Hali mBaya Sana"

$
0
0
Sugu Atoboa Hali ya Jeshi la Magereza "Magereza Kuna Hali mBaya Sana"
Mbunge wa Mbunge Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) amesema kuwa Jeshi la magereza lina hali mbaya, halina magari na magari yaliyopo ni mabovu.

Leo, Mei 22 Bungeni jijini Dodoma, Sugu ameyasema hayo wakati akiuliza swali wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, lililojibiwa na Waziri wa wizara hiyo, Mwigulu Nchemba, ambapo amesema kuwa kutokana na changamoto hiyo inapelekea watuhumiwa kufungwa pingu kutembea kwa miguu mtaani hali inayopelekea kuhatarisha maisha ya mfungwa.

Sugu aliuliza “Pamoja na matatizo waliokuwa nayo Polisi, kwenye masuala ya vyombo vya usafiri lakini nikuhakikishie Jeshi la Magereza lina hali mbaya sana hawana magari sio tu magari mabovu kiasi kwamba wanafikia kupeleka kupeleka wafungwa ambao wana kesi au rufaa wanawafunga pingu wanawapeleka mahakamani kwa miguu sasa hii ni mbaya sana kwa usalama wao na wale Askari magereza lakini pia kwa wao kwa wale watuhumiwa ambao wamefungwa pingu na kutembezwa kwa miguu kwasababu madhalani anatuhumiwa ujambazi alafu anapita mtaani wale wanaomtuhumu wanamuona wanaweza wakamshambulia na kuhatarisha maisha ya yule mfungwa?, alihoji Sugu.

Spika Ndugai baada ya Sugu kuuliza amesema kuwa “Mfano mzuri sana huo Mh. Sugu anatetea Jeshi la Magereza, Mh. Waziri unasemaje,” alisema Spika Ndugai.

Kwa upande wake Waziri Mwigulu amesema kuwa “Nimpongeze Mh. Sugu kwa kuuliza swali kwa experience na niseme tu kwamba yeye ni mshauri mzuri tutazingatia hilo ili tuweke mgao kwenye upande wa Jeshi la Magereza ili kuepuka tahadhari hiyo aliyoisema.”

Unai Emery Kukabidiwa Mikoba ya Arsene Wenger

$
0
0
Unai Emery Kukabidiwa Mikoba ya Arsene Wenger
Klabu ya Arsenal inatarajia kumtangaza wiki hii aliyekuwa meneja wa Paris Saint-Germain, Unai Emery kurithi mikoba ya Arsene Wenger.

Emery ambaye ameachana na klabu ya PSG mwanzoni mwa mwezi huu ameonekana katika Jiji la London hapo jana siku ya Jumatatu akifanya mazungumzo na the Gunners.

Kocha huyo wa Hispania mwenye umri wa miaka 46, ameongoza klabu ya Ufaransa inayoshiriki na nafasi yake kuchukuliwa na Thomas Tuchel.

Chanzo kimoja kilichopo karibu na mazungumzo hayo kimeeleza kuwa Emery ndiye mgombea pekee aliyepewa nafasi ya kurchukua mikoba ya Arsene Wenger.

'Wanaowajambisha' Wenye Mabusha Kukiona..... Jeshi la Polisi Latoa Onyo Kali

$
0
0
'Wanaowajambisha' Wenye Mabusha Kukiona..... Jeshi la Polisi Latoa Onyo Kali
Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limewahatarisha wananchi wa Tanzania kiujumla kuachana na vitendo vya udhalilishaji kwa wanaume wenye mabusha kwa 'kuwajambisha' ama kuwapigia miruzi kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria.


Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi, Ahmed Msangi wakati akifanya mahojiano na eatv.tv baada ya kushamiri kwa matukio mengi ya udhalilishaji na unyanyasaji wa kijinsia licha baadhi ya watu kutofahamu kuwa wakifanya ni kosa kwa mujibu wa sheria za nchi.

"Vipo vifungu vya sheria vinavyoweza kumfikisha mtuhumiwa wa kitendo hicho Mahakamani pamoja kutozwa faini kulingana na mfungua mashtaka atakavyokuwa anataka kulipwa fidia kutokana na udhalilishaji aliyofanyiwa", amesema Kamanda Msangi.

Inasikitisha! Muuguzi Amefariki kwa Ugonjwa wa Ebola Wakati Chanjo Inatolewa

$
0
0
Inasikitisha! Muuguzi Amefariki kwa Ugonjwa wa Ebola Wakati Chanjo Inatolewa
Chanjo ya Ebola imeanza kutolewa nchini DRC huku muuguzi mmoja akiripotiwa kufariki dunia kutokana na ugonjwa huo katika mji wa Bikoro, kaskazini magharibi mwa taifa hilo na kuongeza idadi ya waliokufa kutokana na mlipuko wa Ebola kufikia 27.

Mkuu wa shirika la Afya Duniani, WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus, amesema mjini Geneva katika mkutano wa kila mwaka wa WHO unaohudhuriwa na nchi wanachama 190 kuwa anafurahi kwamba chanjo hiyo imeanza kutolewa na amefurahishwa na hatua za dharura za kimataifa zilizochukuliwa kuukabili.

Yanga Kukutana na Kibarua Kigumu Leo

$
0
0
Yanga Kukutana na Kibarua Kigumu Leo
Klabu ya soka ya Yanga leo itashuka dimbani kucheza na timu ngumu zaidi kuwahi kukutana nayo katika misimu ya hivi karibuni, Mbao FC ambayo haijawahi kuifunga tangu ipande daraja mwaka 2016.


Yanga ambayo haijaonja ushindi katika mechi zake 9 zilizopita katika mashindano yote, leo itakuwa wenyeji wa Mbao FC kwenye uwanja wa taifa huku ukiwa ni mchezo wa raundi ya 28 kwa Yanga na raundi ya 29 kwa Mbao FC.

Wakai Yanga inatafuta ushindi wake wa kwanza katika mechi 9 zilizopita pia itakuwa inatafuta kuishusha Azam FC katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi hivyo inahitaji ushindi ili kurudisha imani kwa mashabiki na morali kwa wachezaji.



Kwa upande wa Mbao FC ambao wao wanapigana kuhakikisha wanakwepa kushuka daraja pia watakuwa wanajitahidi kulinda heshima yao ya kutofungwa na Yanga tangu wapande ligi kuu msimu wa 2016/17.

Kwasasa Yanga inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 48, nyuma ya Azam FC yenye alama 52 na Simba yenye alama 68. Mbao FC ina alama 30 katika nafasi ya 13 ambapo inahitaji kushinda ili kuendelea kujihakikishia kusalia kwenye ligi kuu.

Madee Atofautiana na Diamond Kuhusu Mwanae Kufanya Muziki

$
0
0
Madee Atofautiana na Diamond Kuhusu Mwanae Kufanya Muziki
Msanii wa muziki Bongo kutoka Tip Top Connection, Madee amesema iwapo wanae wa kike, Aimal Hamad  atachagua kuwa msanii kama yeye hatokataa kwa sababu na yeye pia amefuata nyayo za baba yake.

Mtazamo wa Madee unatofautinaa na ule wa Diamond Platnumz pale alipoulizwa kuhusu mwanae Tiffah kuja kufanya muziki. Katika mahojiano na KTN, May 2017 alisema anaogopa iwapo Tiffah ataingia katika muziki ataweza atembea kimapenzi na wanaume wengi.


Sasa Madee katika mahojiano na Bongo5 hivi karibuni alisema licha ya mara nyingi kuwa na wanae hata studio hajui iwapo atapenda muziki lakini yeye kama mzazi hawezi kumuwekea mipaka.

“Tunashauriwa tuwaangalie watoto wafanye kile ambacho wanapenda kwa sababu anaweza kuwa anapenda mpira mimi nikamzuia nikamwambia afanye kitu kingine na asifanikiwe, nitakuwa nimepata lawama,” amesema.

“So akielekea huko mimi sina tatizo kwa sababu hata mimi mwenyewe nimemfuata baba yangu alikuwa ni mwanamuziki wa Western Tabora Jahazi Band wala hakutegemea nitakuwa mwanamuziki, so sitaona maajabu sana kwa sababu Waswahili wanasema maji hufuata mkondo,” Madee ameiambia Bongo5.

Mtoto wa Madee, Aimal Hamad ni miongoni mwa watoto wa wasanii ambapo pia wanapatikana katika mtandao wa Instagram.

Diamond Kuja na Wasafi Festival Mwaka Huu

$
0
0
Diamond Kuja na Wasafi Festival Mwaka Huu
Diamond Platnumz ni mfanyabiashara ambaye anatumia kila fursa inayopita mbele yake bila ya kuogopa chochote. Msanii huyo ametangaza ujio wa tamasha kubwa jipya la Wasafi Festival ambalo litafanyika mwaka huu.



Mashabiki wengi wa muziki wamekuwa wakitamani kuona tamasha kama hilo kutoka kwa wasanii hao wa WCB, lakini bahati nzuri kupitia mtandao wa Instagram, Diamond amethibitisha ujio wa tamasha.

“Kama Naiona hiyo #WasafiFestival Huu Mwaka Sijui hata tuanzie Mkoa gani???🙆‍♂️,” ameandika hit maker huyo wa African Beauty.

Hata hivyo Disemba 2016, WCB walifanya matamasha mawili makubwa likiwemo la Wasafi Beach Party lililofanyika Jangwani Sea Breezy jijini Dar es Salaam, na jingine mkoani Iringa.

Hivi Ndivyo Sugu Alivyotinga Bungeni na Namba Yake ya Gerezani

$
0
0
Hivi Ndivyo Sugu Alivyotinga Bungeni na Namba Yake ya Gerezani
Siku 12 tangu Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alipoachiwa huru, jana aliingia bungeni na kusimamisha shughuli za Bunge kwa dakika kadhaa.

Sugu, ambaye ni mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), alihudhuria kikao cha 33 cha Bunge la Bajeti lililoanza Aprili 3 likitarajiwa kuhitimishwa Juni 29 akiwa amevaa suti ya bluu bahari ikiwa na nembo ya namba yake ya mfungwa 219/2018.

Akiwa ameongozana na mbunge wa viti maalumu (Chadema), Kunti Yusuph, Sugu alikanyaga lango la kuingia bungeni saa 3:16 asubuhi kabla ya kuingia ukumbini saa 3:20.

Wakati akiingia, mbunge huyo alipita katikati ya ukumbi na wabunge wa upinzani walianza kumshangilia kwa kugonga meza. Awali alikosa vikao vya Bunge tangu Novemba, mwaka jana.

Wa kwanza kusalimiana na mbunge huyo alikuwa mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye kisha akapokewa na mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini kwa upande wa upinzani.


Wakati Sugu akiingia bungeni, naibu waziri wa Tamisemi, Josephat Kandege alikuwa akijibu maswali ya wabunge lakini alilazimika kusubiri kwa muda kabla ya Sugu kuhamia upande wanapokaa wabunge wa CCM na mawaziri.

Kisha baada ya salamu hizo, Sugu alisalimiana na waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama; mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Adelardus Kilangi na waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), George Mkuchika.

Wakati anarudi upande wake wa upinzani, Sugu alimpigia saluti mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kisha akakumbatiana na Selasini na kwenda kukaa sehemu yake karibu na mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), Esther Matiko ambaye alimpa vitabu vya hotuba za wizara zilizopita.

Kutokana na shangwe, mwenyekiti wa Bunge, Chenge alisema hatawapa wabunge nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza jambo lililozidisha shangwe ukumbini.

Kwa kuwa kipindi cha maswali na majibu kilikuwa kikiendelea, Chenge alimpa nafasi Sugu ya kuuliza swali la nyongeza ndipo alipoitaka Serikali kuangalia upya baadhi ya sheria akisema ni mbovu na hazifai kutumika kwa sasa.

Mbunge huyo aliitaja Sheria ya Huduma ya Habari akisema inakwenda kinyume cha Katiba ya nchi ibara ya 18.

“Mfano mimi nilifungwa kutokana na kuzungumza na wananchi wangu kuhusu watu kupigwa risasi, kuokota maiti kwenye viroba na demokrasia ya nchi,” alisema Sugu.

Akijibu swali hilo, naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa alisema sheria zote hutungwa na Bunge, hivyo kwa kuwa mbunge huyo amerudi bungeni ipo haja ya kukutana na kujadiliana kuona namna ya kufanya.

Kabla ya kujibu swali hilo, Kwandikwa alimkaribisha Sugu akisema, “Kwanza nikukaribishe sana hapa bungeni, karibu sana mheshimiwa Mbilinyi.”

Mapema, mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea alitaka kujua ni lini Serikali itapeleka bungeni muswada wa kuifanyia marekebisho sheria inayobana uhuru wa mwananchi wa kupata habari.

Kwandikwa alisema Sheria ya Makosa ya Mtandao namba 13 ya mwaka 2015 ni adhimu kwa kuwa inaainisha makosa na adhabu dhidi ya uhalifu unaotendeka mtandaoni.

Alisema sheria hiyo inaweza kuimarika kwa matumizi salama ya mtandao kama vile Serikali mtandao, elimu mtandao, biashara mtandao na hivyo kuleta maendeleo.

Alipokuwa amekaa Sugu, wabunge wa upinzani hawakukatika kwenda kuzungumza naye na kuitazama nembo iliyokuwa upande wa kushoto wa kifua chake.

Azungumzia namba yake

Akizungumza na Mwananchi kuhusu nembo hiyo baada ya kikao cha Bunge, Sugu alisema, “Hii ni namba yangu (219/2018) halisi ya mfungwa niliyokuwa naivaa gerezani.”

Alisema ataendelea kuivaa na baadaye ataiweka kwenye maktaba yake nyumbani.

Akizungumzia mapokezi ndani ya Bunge alisema, “Nimefarijika sana. Imeonyesha wabunge wenzangu pia hawakufurahishwa na walisikitishwa na kufungwa kwangu. Tena wabunge hata wa CCM.”

Baada ya kutoka ukumbini alisalimiana na kuteta na wabunge akiwamo waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi.

Magereza wafafanua

Akizungumzia uamuzi wa Sugu kuivaa namba hiyo uraiani, ofisa habari wa Jeshi la Magereza, Lucas Mboje alisema huo ni uamuzi na utashi wa mhusika na haihusiani na jeshi hilo.

“Sisi tumemalizana naye, kwa sasa sio mteja wetu. Huo ni utashi wake mwenyewe Sugu,” alisema Mboje

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Wadada Tubadilike Tabia ya Kuomba omba Kwa Wanaume si Nzuri inatuzalilisha

$
0
0
Wadada tubadilike jamani kuomba omba sana utazoeleka hata siku ukipata shida ya serious mtu atashindwa kukusaidia coz ni kawaida yako, Hii tabia ndio inafanya mnamegwa ovyo ovyo

Wengine sasa sio hata kwa boyfriend tuu yaani yeye asikuzoee kidogo tu kosa kesho yake ataomba hela. Ombaomba Siku Hizi Hawapo Barabarani tu Hata Kwenye Simu zetu Wapo Jamani ..

Hii ni tabia mbaya jamani tubadilikeni hata siku ikitokea umeomba hela mtu anashangaa anajua kweli umebanwa coz sio kawaida yako.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

IGP Sirro, Fatuma Karume Wakutana Kwaajii ya Mazungumzo

$
0
0
IGP Sirro, Fatuma Karume Wakutana Kwaajii ya Mazungumzo
MKUU wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro leo amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Fatma Karume aliyefika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kwa lengo la kujitambulisha tangu alipochaguliwa kuongoza Chama hicho ambapo pia walijadiliana masuala kadhaa ya kisheria.


Haji Manara Awaomba Radhi Mashabiki wa Simba

$
0
0
Haji Manara Awaomba Radhi Mashabiki wa Simba
Afisa habari wa  Simba, Haji Manara amewaomba radhi mashabiki wa klabu hiyo kwa kitendo cha kikosi chao kupoteza kwenye mchezo wao dhidi ya Kagera Sugar mbele ya Rais Magufuli akiwa mgeni rasmi na aliyewakabidhi kombe la ligi kuu soka Tanzania Bara msimu huu wa mwaka 2017/18.

Kupitia mahojiano na chombo cha habari cha Azam Tv, Manara amesema kuwa anawaomba radhi kwakuumizwa na matokeo ya wikiendi hii.

Nitumie fursa hii kuwaomba radhi mashabiki wetu wa Simba ambao waliumizwa na matokeo ya juzi, najua iliumiza sana kufungwa katika ligi kwakuwa watu walitarajia tungemaliza ‘Unbeaten’ lakini ilikera zaidi kufungwa mbele ya Rais Magufuli.

Hata mimi iliniuma sana sijarudi bado katika hali yangu ya kawaida lakini lazima tuchukulie mpira ni mchezo wa matokeo matatu, ilipanwa ligi hii lazima tufungwe tumechukua ubingwa bila kufungwa ila tunamaliza ligi kwa kufungwa kwahiyo tuchukulie ni changamoto tu.

Mchezo wetu wa mwisho dhidi ya Maji Maji tunaupa uzito kwasababu hatukubali tena kufungwa mechi mbili ijapokuwa tunajua ni timu nzuri, tutakwenda full timu wala hatwendi kidhaifu na tunatarajia mchezo utakuwa mzuri sana na hatwendi kumnusuru mtu kushuka daraja hatuwezi kuuchezea mchezo wa mpira wa miguu.

Mabingwa wapya Simba wanatarajia kucheza mchezo wake wa mwisho wa ligi kuu Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Maji Maji huku ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mechi iliyopita dhidi ya Kagera Sugar kwa bao 1 – 0 dimba la Taifa jijini Dar es salaam.

Vitendo vya Uharamia Viliongezeka Mwaka 2017

$
0
0
Vitendo vya Uharamia Viliongezeka Mwaka 2017
Idadi ya vitendo vya uharamia pwani ya Afrika mashariki iliongezeka mara mbili mwaka 2017 ukilinganisha na mwaka 2016, Vyombo vya kimataifa vinavyoshughulikia usalama wa majini vimeeleza.

Ilioyesha kuwa mtandao wa uhalifu nchini Somalia ulikuwa bado una uwezo wa utekeleza mashambulizi.

Vitendo vya uharamia mwaka 2017 vinaonyesha wazi kuwa makundi haya yameendelea kuwa na uwezo wa kuratibu na kutekeleza mashambulizi dhidi ya Meli zinazosafiri kwenye eneo la Afrika .

Phil Belcher kutoka kwenye taasisi ya Intertanko amesema mgogoro nchini Yemen pia ulikuwa ukitishia usafirishaji wa majini karibu na eneo la pembe ya Afrika

''Tunawashauri washirika wetu kuja na mbinu madhubuti za kiusalama ili kudhibiti vitisho vingine.

Maharamia waiteka meli huko Somalia

Uharamia umeendelea kuwa tishio katika rasi ya Guinea ingawa hatua mbalimbali zimechukuliwa katika maeneo ya pwani na makampuni ya ulinzi wa majini, imeeleza ripoti hiyo

Meli ya Korea Kusini Munmu ili tumwa tena katika eneo la rasi ya Guinea baada ya wavuvi watatu wa Korea Kusini kutekwa mwezi Machi.Utekaji nyara kwa ajili ya kujipatia pesa umeendeleza kukumba eneo hili, ambapo imezoeleka kuwa hivyo kwa bahari mbaya kuanzia mwaka 2016, alieleza Maisie Pigeon,mwandishi wa ripoti hiyo.

.Marekani Wamuonya Kim Jong-un Watakapokutana na Trump

$
0
0
.Marekani Wamuonya Kim Jong-un Watakapokutana na Trump
Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence amemuonya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un kuwa asimchezee Rais Donald Trump ikiwa watakutana mwezi ujao.

Pence pia alisema kuwa Trump ana nia ya kuondoka kwenye mkutano huo ambao unapangwa kufanyiwa nchini Singapore.

Kim Jong-un atishia kufuta mkutano wake na Trump baada ya matamshi ya mshauri wa masuala ya ulinzi nchini Marekani John Bolton aliyesema kuwa Marekani itafuata mfumo wa Libya kuondoa zana za nyuklia.

Kingozi wa zamani wa Libya Muammar Gaddafi alikubaliana na mataifa ya Magharibi mwaka 2003 kuharibu mpango wake ili apate kuondolewa vikwazo. Miaka minane baadaye aliuawa na waasi walioungwa mkono na nchi za Magharibi.

Ndugai Awapa Makavu Wahifadhi.... "Mmekuwa Walafi Mno"

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema wahifadhi wamekuwa ni walafi mno wa ardhi kwa kutaka maeneo makubwa nchini.

Amesema hayo bungeni leo Jumanne Mei 22, 2018 baada ya mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Profesa Anna Tibaijuka kuchangia katika bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2018/19.

 Ndugai amesema wanapokwenda watu wa hifadhi wanakuwa na wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambao hupima ardhi baada ya kukubaliana na wananchi.

 Hata hivyo, Ndugai amesema wakati wanaporudi ofisini  wanaongeza eneo bila kuwataarifu wananchi na baada ya  miaka 10 hupita maeneo husika na kuwaeleza kuwa mpaka upo maeneo mengine.

 “Si waseme (wawambie wananchi) mimi mwenyewe ni mhifadhi tatizo sisi wahifadhi ni walafi mno wa ardhi,” amesema.

 Awali, Profesa Tibaijuka akichangia amemweleza Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla kuwa yeye (Kigwangalla) ni daktari wa binadamu na kwake ni kulinda maisha ya watu, lakini kwenye masuala ya hifadhi kunamuangusha kutekeleza umuhimu huo.

 “Rais wetu anawalinda wanyonge lakini majirani wa hifadhi si wanyonge. Kusema ukweli hali ilivyo si hivyo,” amesema.

 Amemshauri Dk Kigwangalla kuachana na misitu ya akiba na mapori ya akiba, kwa sababu yamepitwa na wakati badala yake atangaze Hifadhi ya Taifa ambayo ina manufaa makubwa.

 Amesema wizara hiyo haina mamlaka ya kupima ardhi,

bali jukumu lipo kwa Wizara ya Ardhi lakini katika uwekezaji wa mipaka wameenda bila kuwa na watalaamu wa wizara hiyo.

 Ametoa mfano wa Msitu wa Kazimzumbwi ambao Wizara ya Maliasili ilibadilisha mipaka na kusababisha mgogoro.

 Pia, Profesa Tibaijuka ameshauri wizara hiyo kuachana na operesheni kwa sababu ni mambo ya haraka na ya kushtukiza.

Kamati ya Bunge Kumuhoji Mugabe Jumatano

$
0
0
Kamati ya Bunge Kumuhoji Mugabe Jumatano
Kamati ya Bunge imepanga kumhoji Rais wa zamani Robert Mugabe Jumatano kuhusiana na upotevu wa dola za Marekani 15 bilioni katika operesheni za madini ya almasi mnano mwaka 2016.

Awali, Mugabe alitarajiwa kuhojiwa na Kamati ya Kudumu ya Madini Mei 9 siku iliyotarajiwa ya kwanza kwa kiongozi huyo mkongwe kuonekana hadharani tangu alipoondolewa Novemba 2017 lakini hakuwa amepelekewa barua ya kuitwa bungeni.

Bunge linamhitaji mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 94 kutoa maelezo juu ya tangazo lake kwamba Serikali ilikoseshwa na kampuni za madini kiasi cha dola za Marekani 15 bilioni katika mapato ya almasi.

Taarifa ya Bunge inasema Mugabe atajibu maswali Jumatano ikiwa itakuwa imethibitishwa. Hakukuwa na maelezo zaidi.

Lakini ofisa mmoja wa Bunge mwenye uelewa wa suala hilo alisema upo uwezekano mdogo kwa Mugabe kufika kwenye kamati kwa sababu ya upinzani kutoka kwa maofisa kadhaa na wanasiasa wenye ushawishi ndani ya Zanu-PF.

“Wanasema hawataki mzee wao asumbuliwe na wabunge wa upinzani. Kamwe haitatokea,” alisema huku akikataa asitajwe jina kwa vile si msemaji.

Mwenyekiti wa Kamati ya Madini Temba Mliswa alisema Bunge lilimwandikia barua Mugabe na aliipokea. Hata hivyo, hakuthibitisha ikiwa atafika kwenye mahojiano.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images