Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Polisi Yafunguka Chanzo cha Ajal Iliyowaua Maofisa Watatu wa TIC

$
0
0
Polisi Yafunguka Chanzo cha Ajal Iliyowaua Maofisa Watatu wa TIC
Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani limesema uzembe wa dereva aliyekuwa akiendesha gari aina ya LandCruiser mali ya Serikali ya Tanzania ndiyo chanzo cha ajali ya gari hilo kugongana na lori na kusababisha vifo vya watu watatu, wawili kujeruhiwa.

Ajali hiyo imetokea jana Mei 21, 2018 katika Kijiji cha Msoga Chalinze Mkoa wa Pwani.

Akizungumza leo Jumanne Mei 22, 2018 Kamanda wa Polisi mkoani humo, Jonathan Shanna amesema watakuwa wakali kwa madereva watakaokiuka sheria za usalama barabara bila kujali wadhifa wao.

Amesema dereva wa gari hilo alihamia upande mwingine wa barabara wakati anayapita magari mengine bila kutazama mbele, hivyo kuligonga lori hilo.

"Sheria za usalama barabarani hazina watu maalumu wa kuzitii, sio kwamba ukiwa dereva wa ofisa wa Serikali basi wewe uende tu hovyo au ukiwa muajiriwa wa Serikali napo ujione mwamba, hata kama ni dereva wangu tutakushughulikia tu,” amesema.

Akisimulia ajali hiyo, amesema watu watatu ambao ni watumishi wa Serikali wakiwa safarini kwenda Dodoma kikazi  walifariki dunia katika ajali hiyo.

Amewataja waliofariki dunia kuwa ni Martin Laurence (39), Zacharia Nalinga (49) na Said Moshi, miili yao  imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Tumbi, Kibaha.


Mbunge Ataka Wafungwa wa Makosa ya Ubakaji Watengwe

$
0
0
Mbunge Ataka Wafungwa wa Makosa ya Ubakaji Watengwe
Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Saada Ramadhan Mwandwa ameitaka serikali kuweka utaratibu wa kuwatenganisha wafungwa wa makosa ya ubakaji wakiwa gerezani ili kuwanusuru watu hao kutoendelea na tabia hizo wakiwa kwenye kifungo.


Mjumbe huyo ameyasema hayo wakati akiuliza swali lake la msingi katika kikao hicho na kuhoji kuwa serikali haioni kwamba kuwachanganya wafungwa wa makosa mengine kunaweza kuwafanya kuendelea na tabia ya ubakaji wakiwa kifungoni.

Akijibu swali la mwakilishi huyo wa nafasi za wanawake, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum, Shamata Shaame Khamis amesema kuwa hakuna maeneo maalum gerezani yanayotengwa kwa ajili ya kuwekwa makundi fulani ya wahalifu wanaotumikia adhabu zao.

"Wanaotumikia adhabu wakiwa gerezani wanaweza kuhukumiwa kutokana na makosa tofauti yakiwemo uhaini, wizi, ugaidi, unyang'anyi pamoja na hayo ya ubakaji na udhalilishaji wa wanawake pamoja na Watoto. Ni kweli kila kosa linaathari zake kisailolojia kwa mkosaji na kwa wale wanaomzunguka", amesema Shaame.

Kwa upande mwingine, Shaame amesema chuo cha mafunzo kina-program ya ushauri nasaha kwa wafungwa hasa wale wafungwa wenye hulka za kipekee kama wa makosa ya ubakaji.

Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume, Maumbile Madogo, Mvuto wa Mapenzi na Magonjwa Sugu

$
0
0
KIBOKO YA MATATIZO YA NGUVU ZA KIUME,MAUMBILE MADOGO, MVUTO WA MAPENZI ,MAGONJWA SUGU

Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

SUPER CHAN :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

LUGINI 3 POWER:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

MANUS :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

TULIZA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR GALIMBO NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO
PIGA SIMU 0759208637

Mpiga Picha wa Diamond ‘Lukamba’Afunguka Ishu ya Hamisa na Zari

$
0
0
Mpiga Picha wa Diamond ‘Lukamba’Afunguka Ishu ya Hamisa na Zari
Kuna kipindi Mpiga picha wa Diamond, Lukamba alioneka katika picha moja na mwanamitindo Hamisa Mobetto wakati huo Diamond na Zari bado walikuwa na mahusiano kitu ambacho kilileta maneno.

Sasa Lukamba amefunguka kile kilichotokea kwa kueleza kuwa alikutana na Hamisa kwa ajili ya ku-shoot kipindi cha Wasafi TV na hakukuwa na zaidi ya hapo kama ilivyokuwa ikienezwa.

“Japokuwa watu walinitukana mtandaoni lakini mimi nafanya kazi, boss wangu ana TV kwa hiyo akiniambia Lukamba kam-shoot na si sikum-shoot Hamisa pekee yake na nilivyomaliza picha ni kitu cha kawaida lakini watu walivyoipokea ilikuwa tofauti,” Lukamba ameiambia Bongo5.

Kilichofanya ishu hiyo kuwa kubwa ni kutokana Hamisa Mobetto na Zari The Boss Lady hawaelewani baada ya Hamisa kuzaa na Diamond huku akifahamu fika muimbaji huyo bado alikuwa na mahusiano na Zari.

Waziri Majaliwa Amaliza Tatizo la Umeme Lindi na Mtwara

$
0
0
Waziri  Majaliwa Amaliza Tatizo la Umeme Lindi na Mtwara
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema shida ya umeme iliyokuwa inaikabili mikoa ya Lindi na Mtwara hivi sasa imekwisha.



“Kuunganishwa kwa mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye gridi ya Taifa, kumeondoa tatizo la umeme lililokuwa likiikabili mikoa hii, na mitambo ya jenerata iliyokuwepo, itabakia kuwa ya akiba endapo dharura yoyote itatokea,” alisema.



Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumatatu, Mei 21, 2018) wakati akizungumza na wakazi wa mji wa Mtwara kwenye viwanja vya bandarini mjini humo.



Alisema pengo lililokuwepo la kukatikakatika kwa umeme, limezibwa kwa kupata umeme wa kutoka Somanga hadi Lindi. “Umeme huu umeanzia kituo chetu cha Mbagala, umekuja Mkuranga, Muhoro, Lindi na hatimaye umefika pale Mahumbika. Na mchana wakati nikiwa Mahumbika, niliwasha kwa kompyuta kuashiria umeme wa gridi kuingia mikoa yetu ya Lindi na Mtwara,” alisema.



Akiwa Mtwara mjini, Waziri Mkuu alikagua na kisha kuzindua mradi wa upanuzi wa kituo cha kufua umeme wa gesi asilia wenye uwezo wa kuzalisha megawati nne.



Kabla ya kuzindua mradi huo, alipita bandarini kukagua ukarabati wa mitambo ya kupokelea mafuta ya dizeli na petroli ambako alielezwa kuwa kampuni mbili za GM na OILCOM zimeanza ukarabati na kwamba mwezi ujao, bandari hiyo itaanza kupokea meli za kubeba mafuta.



“Bandari ya Mtwara hivi sasa itaanza kupokea meli kubwa za mafuta, jambo ambalo halijafanyika tangu mwaka 2014. Mwezi ujao, wakati wowote, wataanza kupakua mafuta. Kwa hiyo mji utaanza kuchangamka.”



“Kuanza kupakuliwa kwa mafuta katika bandari hii, kutasaidia kushusha bei ya mafuta kwenye mikoa hii na pia kiasi kitakachobakia, tutakipeleka nchi za jirani za Msumbiji na Malawi,” alisema.



Alisema matengenezo hayo yakikamilika yatafanya bandari za Dar es Salaam, Mtwara na Tanga zote ziwe na uwezo wa kupokea mafuta. Pia aliitaka Mamlaka ya Bandari (TPA) iondoe urasimu na Mkurugenzi Mkuu wake awatumie vizuri watendaji waliopo chini yake.



Mapema, walipopewa nafasi ya kusalimia wananchi, wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF) walitumia fursa hiyo kuelezea kufurahishwa kwao na hatua za maendeleo zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano.



Zuberi Mohammed Kuchauka (Liwale) aliwataka wananchi wa mikoa ya Kusini wachangamkie fursa zinazopatikana kutokana na maendeleo yanayofanywa na Serikali ya awamu ya tano. “Kusini hivi sasa imeamka na imetoka gizani, sasa wananchi tuchangamkie fursa,” alisema.



Naye Mbunge wa Nachingwea, Bw. Hassan Elias Masala, alitumia fursa hiyo kuomba barabara ya kutoka Nachingwea iwekewe lami ili wakazi wake waweze kutumia fursa ya kusafirisha korosho zao hadi kwenye bandari ya Mtwara.



Naye Bw. Maftaha Abdallah Nachuma (Mtwara Mjini) pia aliomba barabara ya kutoka Mtwara hadi Mingoyo ikamilishwe matengenezo yake kwani kwa hali ya sasa siyo rahisi kusafirisha mizigo. Pia aliomba apelekewe umeme maeneo ya Mbawalachini na Mkunjanguo. “Maendeleo hayana chama, kabila wala itikadi,” alisema.



Wabunge wengine waliofuatana na Waziri Mkuu kwenye ziara hiyo ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti na Mbunge wa Mtwara Vijijini, Bibi Hawa Ghasia na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Bi. Hamida Mohammed Abdallah (Viti Maalum).

Mwanamke wa Kitanzana Achaguliwa Kuongoza UN

$
0
0
Mwanamke wa Kitanzana Achaguliwa Kuongoza UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amemteua Mtanzania Joyce Msuya kuwa Kaimu Mkurugenzi wa program ya Mazingira ya Umoja huo, ambapo ofisi zake zipo nchini Kenya.

Kabla ya uteuzi wake Joyce Msuya alikuwa Mshauri wa Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kwa Asia ya Mashariki na maeneo ya Pacific huko Washington DC.

Ms. Msuya ambaye ameolewa na mama wa watoto wawili, ana elimu ngazi ya uzamili ya Sayansi ya Microbiology na Immunology kutoka chuo kikuu cha Ottawa Canada, na shahada ya Sayansi ya Biochemistry na Immunology kutoka chuo kikuu cha Strathclyde, Scotland.

Joyce Msuya atachukua nafasi ya Ibrahim Thiaw wa Mauritania ambaye alitumikia nafasi hiyo tangu mwaka 2013 na aliyekuwa Katibu Mkuu wa UN Ban Ki-moon.

Mtandao wa Wanafunzi Tanzania Waijia Juu Bodi ya Mkopo Kuhusiana na Masharti ya Mkopo Elimu ya Juu

$
0
0
Mtandao wa Wanafunzi Tanzania Waijia Juu Bodi ya Mkopo Kuhusiana na Masharti ya Mkopo Elimu ya Juu
Mtandao wa Wanafunzi Tanzania(TSN) wameiomba Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kushughulikia baadhi ya vipengele vinavyozungumzia sifa za mwanafunzi anayepaswa kupata mikopo, kwa maelezo ni kandamizi na vinawanyima fursa wanafunzi.

 Moja ya kipengele hicho  ni kile cha mwanafunzi  ambaye ana mzazi au mlezi ayemiliki biashara au kampuni inayotambulika na mamlaka za usajili, kutoruhusiwa kuomba mkopo.

 Akizungumza leo Jumanne Mei 22, 2018 Mkuu wa Idara ya Haki ya Wanafunzi wa mtandao huo, Gibson Eliaform amesema, “Meneja ni cheo tu hakitambulishi uwezo wa mtu hata mwenye kibanda cha huduma za fedha kwa mitandao ya simu na kampuni ndogo iliyosajiliwa anaweza kuwa meneja wa biashara.”

 “Anaweza kuwa amesajili biashara yake Brela (Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni ) au TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) na ana mtaji wa Sh500,000 je huyu ni tajiri?” amehoji.

 Amesema kipengele kingine ni kinachozuia wanafunzi waliotajwa katika sheria ya utumishi wa umma kutoomba mikopo, ikiwamo madiwani, maofisa watendaji wa kata na mtaa ambapo kimsingi kazi yao haina mshahara.

 Eliaform amesema kigezo hicho hakipo kisheria na huenda kimewekwa makusudi ili kupunguza wanufaika wa mikopo kulingana na bajeti.

 Amesema kipengele kingine kinachotakiwa kufanyia marekebisho ni kuzuiwa wanafunzi waliosoma shule binafsi, kubainisha kusoma shule binafsi siyo kigezo kinachotambulisha uwezo wa mzazi kuhimili gharama za masomo Chuo Kikuu.

 “Hali hubadilika kuna kufilisika, magonjwa na pia wanaolipa ada ndogo chini ya Sh1 milioni kuwanyima mikopo ni kukatisha ndoto zao,” amesema.

Joto Kali Laua Watu 65 Pakistani

$
0
0
Joto Kali Laua Watu 65 Pakistani
Zaidi ya watu 65 wamefariki kwa Joto kali la nyuzi joto 44 lililotanda mjini Karachi nchini Pakistan. wengi wakiishiwa nguvu haswa kipindi hiki cha Ramadhan ambapo wengi huwa hawali wala kunywa nyakati za mchana.

Faisal Edhi, mkuu wa Shirika la Edhi ambalo linafanya kazi za maadili na huduma ya wagonjwa nchini humo, ameviambia vyombo vya habari kwamba miili ya watu 114 waliletwa kwenye nyumba ya kuhifadhia maiti mjini Karachi katika siku tatu zilizopita na watu 65 kati ya walioletwa walifariki kutokana na kiharusi cha joto.

Mamlaka nchini Pakistan imewasihi watu wapunguze kutembea juani.

JE ? Una Maumbile Madogo ya Uume? Unakosa Hamu au Kushindwa Kurudia Tendo?

$
0
0

JE, UNA MAUMBILE MADOGO YA UUME? UNAKOSA HAMU AU KUSHINDWA KURUDIA TENDO?
SOMA HAPA👇👇.
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea na matunda bila kemikali 🍇🍍🍓🌿🍉🍒🍎🍑 @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
#NguvuZaKiume
#OngezaMaumbile
#BidhaaTz

Joshua Nassari: Serikali Inawarudisha Watanzania Enzi za Ukoloni

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema) Joshua Nassari amesema Serikali imewarudisha Watanzania katika kipindi cha ukoloni ambako waliporwa ardhi yao bila sababu za msingi.

Nasari amesema kitendo cha kuwachomea nyumba wananchi wa Meru kinawakumbusha miaka ya 1950, ambapo walilazimika kuchanga fedha na kumtuma Japhet Kilila Nguro kwenda Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kutetea ardhi yao.

Akichangia katika hotuba ya Wizara ya Maliasili na Utalii, jana Mei 21, mbunge huyo alizungumza kwa hisia kali kuwa jambo kama hilo linawakumbusha mbali Watanzania na kuona kuwa bado wako katika kipindi cha ukoloni walipokuwa wakiporwa ardhi bila hata kusikilizwa.

“Mimi sijui tunawasaidia akina nani Tanzania yetu hii, wafanyabiashara wanalia, wavuvi wanalia, wananchi wanalia na mnawapora ardhi hivi mnataka kutawala nani lakini?” Alihoji Nasari

Alisema mali walizoachiwa Watanzania na Mungu zimeshindwa kuwa baraka tena na badala yake zimegeuka kuwa laana kwa Watanzania na kuwafarakanisha.

“Mnatutonesha kidonda sisi watu wa Meru, angalia picha hizi zinaonyesha haya ni maganda ya risasi na hizi ni picha za mifugo ambayo imedhoofu sana iliyosababisha wananchi kubaki maskini kabisa,” alisema Nasari

Wabunge Wa CUF Wamfagilia Rais Magufuli ....Wasifu Kasi Yake Na Waziri Mkuu Ya Uletaji Maendeleo

$
0
0
WABUNGE watatu kutoka Chama cha Wananchi (CUF) mikoa ya Lindi na Mtwara wamepongeza kasi ya utendaji kazi ya Rais John Pombe Magufuli katika kutatua kero za wananchi wa mikoa hiyo.

Wabunge hao Bw. Selemani Said Bungara (Kilwa Kusini), Bw. Zuberi Mohammed Kuchauka (Liwale) na Bw. Maftaha Abdallah Nachuma (Mtwara Mjini) walitoa pongezi hizo jana, (Jumatatu, Mei 21, 2018) wakati walipopewa nafasi ya kusalimia wananchi kwenye mikutano ya hadhara ambayo Waziri Mkuu alihutubia.

Akiwa wilayani Lindi, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kuzindua kituo cha kuunganisha umeme wa gridi ya Taifa katika kijiji cha Mahumbika, aliwapa fursa wabunge wote alioambatana nao katika ziara hiyo maalum kwa ajili ya uzinduzi wa miundombinu ya nishati kwa mikoa ya Kusini.

Akizungumza na wananchi na viongozi wa taasisi mbalimbali mkoani humo waliohudhuria uzinduzi huo, Mbunge wa Kilwa Kusini, Bw. Bungara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wabunge wanaotoka Mkoa wa Lindi alisema analishukuru Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuisimamia vizuri Serikali ya CCM.

“Faida ya demokrasia ya vyama vingi ni kwamba CCM bila CUF, CCM hakuna na CUF bila CCM, kama ambavyo hakuna Simba bila Yanga wala hakuna Yanga bila Simba. Tuwe kitu kimoja tu, Kusini kwanza, vyama baadaye!” alisisitiza.

Alitumia fursa hiyo kumpongeza Waziri Mkuu kwa juhudi zake za kuwaunganisha wabunge wa mikoa ya Kusini bila kuwabagua au kujali itikadi zao.

Naye Mbunge wa Liwale, Bw. Kuchauka alisema: “Niwapongeze wewe Waziri Mkuu pamoja na Mheshimiwa Rais Magufuli kwa yale ambayo mnayasimamia na mnaamini kwamba yataleta ukombozi kwa wananchi wa Tanzania. Lazima nikiri kwamba wakati mnazindua sera ya uchumi wa viwanda, nilikuwa siamini katika hiyo sera yenu kwa sababu niliona ni moja ya mbinu zenu za kututenga sisi watu wa mikoa ya Kusini.”

“Niliona hivyo kwa sababu nilijiuliza unawezaje kuwa na uchumi wa viwanda wakati huna nishati ya uhakika ya umeme? Sasa nimeona mwanga kwamba mikoa ya Kusini nayo inaweza kushiriki kwenye uchumi wa viwanda,” alisema huku akishangiliwa.

Alisema hivi sasa hakuna asiyeona mambo yanayotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano kwani dunia yote imekuwa kama kijiji na lolote linalofanywa na Mhe. Rais au Waziri Mkuu hakuna asiyejua. “Lolote analolifanya Mheshimiwa Rais au wewe Waziri Mkuu Watanzania wote watalijua, hakuna asiyeliona. Hivi sasa hakuna haja ya kubishana nani kafanya nini, jambo kubwa ni kuungana na tuangalie Tanzania yetu. Vyama vyote baadaye, Kusini kwanza,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Mbunge wa Mtwara Mjini, Bw. Maftaha alisema mwaka 2006 baada ya kuhitimu kidato cha sita, alipangiwa afanye mafunzo ya ualimu kwa vitendo katika shule ya sekondari Mingoyo, eneo la Mnazi Mmoja lakini alitafuta nyumba ya kuishi yenye umeme hakupata.

“Wakati ule nyumba zenye umeme zilikuwa hazizidi hata 10, na kulikuwa na simba na wadudu wa kila aina. Leo nafarijika kuona kwa kasi ya ajabu, ninyi viongozi tuliowapa dhamana, mnatumia rasilmali za nchi hii, mnasambaza umeme kwa wananchi wa mikoa ya Kusini, na pale Mnazi Mmoja leo hii, umeme siyo tatizo tena.”

Wabunge wengine waliofuatana na Waziri Mkuu ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti na Mbunge wa Mtwara Vijijini, Bibi Hawa Ghasia; Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Bi. Hamida Mohammed Abdallah (Viti Maalum). Mbunge wa Nachingwea, Bw. Hassan Elias Masala, Mbunge wa Nanyamba, Bw. Abdallah Dadi Chikota.

Waziri Mkuu alizuru pia mkoa wa Mtwara na kukagua ujenzi wa bandari, ukarabati wa mabomba ya kupokelea mafuta, matenki ya kuhifadhi mafuta, kuzindua upanuzi wa kituo cha kufua umeme kwa kutumia gesi asilia na kuzungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa bandari.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Maskini Q Chief Adai Mziki Umemkataa, Aachwa na Mke, Ataka Kujiua..Mtazame Hapa Akifunguka

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki, Q Chief ameahidi ataachia wimbo wake wa mwisho uitwao ‘Saratani’ kueleza namna muziki ulivyomtafuna na kumwaribia maisha yake.


Muimbaji huyo amesema hayo wiki hii wakati akizungumza na Bongo5 kuhusu kauli yake ya kuachana na muziki na kufanya shughuli nyingine nje ya muiziki.

“Siwezi kuwaacha watu hivi hivi, ngoma yangu mpya inaitwa Saratani, nadhani watu wanajua maana ya Saratani kitu ambacho kinakula ndani kwa ndani,” alisema Q Chief.

Aliongeza, “Huu ni mwimbo ambao nautoa, utakuwa wimbo wa mwisho, watu wajaribu kutofautisha kiki na maisha halisi ya mtu, kiki ni ile unanunua magari unapost na kuonyesha ufahari, halafu maisha ya mtu ni haya. kwahiyo huu utakuwa ni wimbo wangu wa mwisho”

Muimbaji huyo alidai anaacha muziki baada ya kufanya kazi nyingi bila kuwa na mafanikio yoyote katika maisha yake

VIDEO:

Neema yawaangukia Barack Obama na mkewe, wasaini dili nono na kampuni ya Netflix

$
0
0
Rais wa zamani wa Marekani, Barack Obama na mkewe Michelle Obama wamesaini dili nono na kampuni ya Netflix inayojihusisha na masuala ya burudani kwa kurusha vipindi vya TV, Series, filamu na Documentary mitandaoni.

Obama na mkewe kwenye dili hilo wamesaini kama Mameneja wazalishaji ambapo kazi yao kubwa itakuwa ni kusimamia na kuhariri scripts za Filamu, tamthiliya na Documentary kabla ya kuruka. Hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na NETFLIX




By @netflix
 President Barack Obama and Michelle Obama have entered into a multi-year agreement to produce films and series for Netflix, potentially including scripted series, unscripted series, docu-series, documentaries, and features.

Hata hivyo, Obama naye baada ya kutangazwa kwa dili amesema kuwa furaha yake ni kuona anaitumikia jamii na kukutana na watu wa kila aina ili kujionea utofauti.

“One of the simple joys of our time in public service was getting to meet so many fascinating people from all walks of life, and to help them share their experiences with a wider audience. That’s why Michelle and I are so excited to partner with Netflix — we hope to cultivate and curate the talented, inspiring, creative voices who are able to promote greater empathy and understanding between peoples, and help them share their stories with the entire world.”

Licha ya Netflix kutangaza dili hilo mpaka sasa hawajaweka wazi ni kiasi gani watawalipa wawili hao, kampuni hiyo imekuwa ikiwalipa watu maarufu mamilioni ya dola kwenye mikataba yake.

Kampuni ya Netflix mwaka 2014 ilitangaza rasmi kuingia barani Afrika lakini hata hivyo haijapata umaarufu zaidi ukilinganisha na mabara mengine.

Zitto Kabwe Amkosoa Kigwangalla

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo), amemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla kukubali amekosea na kurejea katika utaratibu wa awali wa utoaji wa vibali vya vitalu vya uwindaji.

Akichangia bajeti ya wizara hiyo ya mwaka 2018/19 ambayo ni Sh115.8bilioni, Zitto amesema:, “Waziri kwa kuwa umeona kuna tatizo la kisheria na maagizo uliyoyatoa ni kinyume na sheria turejee katika utaratibu wa awali.”

Zitto katika hatua nyingine ametoa wito kwa wizara husika kutafakari upya suala la kuondoa miti katika hifadhi ya Sealou kwani kwa kufanya hivyo kutaathiri mazingira kwa kiasi kikubwa.

“Hakuna anayekataa maendeleo ya taifa letu lakini kwa kuondoa miti ile kutaathiri mazingira pamoja na kupoteza watalii, tunaomba zoezi hili lisimame kwanza tutafakari athari zake ndio uamuzi ufanyike”. Amesema Zitto.

Watu 45 wamevuta hewa yenye sumu Dar es salaam

$
0
0
Watu 45 wameathirika baada ya kuvuta hewa yenye sumu kutoka kiwanda cha kutengeneza sabuni cha ROYAL kilichopo Mabibo external Jijini Dar es Salaam.


Akitibitisha kutoka kwa tukio hilo, Mkuu wa wilaya ya Ubungo  Bw. Kisare  Makori amesema tatizo hilo limetokea baada ya kuwepo kwa hitilafu katika moja ya mtambo wa kuchuja tindikali lakini mpaka sasa, wamiliki wa kiwanda hicho wameshadhibiti na zoezi la uzalishaji linaendelea kama kawaida.

"Kuna watu watatu ambao walipata madhara zaidi yaani walikuwa wanatapika na kuumwa vichwa lakini wameshapatiwa matibabu na wengine 42 walienda katika kituo cha afya kupatiwa huduma kutokana na kuhisi kuathirika na hewa hiyo waliyoivuta wakati wakiwa kiwandani", amesema Makori.

Umri sahihi wa kufunga ndoa ni huu hapa

$
0
0
Kwa mujibu wa utafiti wa Chuo Kikuu cha Utah kilichopo nchini Marekani imebainisha kwamba watu ambao wamefunga ndoa kati ya umri wa miaka 28 mpaka 32 wamekuwa na ndoa yenye mafanikio zaidi.


Utafiti huo umebainisha kwamba ndoa ambazo zipo katika hatari ya kuvunjika ni zile ambazo mmoja wa wanandoa ana umri wa chini ya miaka 20 na wale waliofunga ndoa wakiwa na umri wa miaka zaidi ya 45 na kuongeza kuwa ndoa hizo hazijadumu zaidi ya miaka mitano.

Taarifa za utafiti huo umeongeza kuwa kwa watu ambao wanasubiri kufika umri wa miaka 30 ili kufunga ndoa wanahatari ya kupata shida sana katika miaka mitano ya mwanzo ya ndoa yao

Awali ilijulikana kwamba watu wanaofunga ndoa katika umri mkubwa ndiyo wananafasi ndogo ya kuachana, lakini utafiti huu umeonesha kwamba watu wanaofunga ndoa katika umri wa miaka 45 uwezekano wa kupeana taraka unaongezeka kwa asilimia 5 kila baada ya mwaka mmoja.

Sababu kubwa inayosababisha watu walio katika umri mkubwa kupeana taraka ni historia za nyuma za kila mmoja wao, imani za kidini, miji wanayotoka, kiwango cha elimu, mahusiano ya kimapenzi waliyopitia awali.

Watu Wanaochelewa Kulala Wana Awezekano Mkubwa wa Kufa Mapema

$
0
0

UTAFITI: Watu wanaochelewa kulala wana uwezekano mkubwa wa kufa mapema kuliko wale wanaowahi kulala

Msingi wa utafiti huo ni kwamba watu wanaolala muda mzuri na kuamka mapema wanaweza kuishi muda mrefu ukilinganisha na wale ambao wanachelewa kulala ambao wakati mwingine wanaamka mapema wakiwa na uchovu mwingi

Matokeo ya utafiti huo yamechambua sampuli ya watu laki 5 wenye umri wa miaka 30 hadi 73 ambao walifuatiliwa tabia za ulalaji wao kwa zaidi ya miaka 6 na nusu

Watafiti walibaini kuwa watu ambao walikuwa wanachelewa kulala walikuwa na hatari kwa asilimia 10 kufa mapema katika kipindi cha utafiti kuliko wale ambao wanalala mapema na kuamka mapema

Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume, Maumbile Madogo, Mvuto wa Mapenzi na Magonjwa Sugu

$
0
0
KIBOKO YA MATATIZO YA NGUVU ZA KIUME,MAUMBILE MADOGO, MVUTO WA MAPENZI ,MAGONJWA SUGU

Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

SUPER CHAN :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

LUGINI 3 POWER:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

MANUS :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

TULIZA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR GALIMBO NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO
PIGA SIMU 0759208637

Shilole Achekelea Mfungo Ndani ya Ndoa "Huu ni mfungo wa Kipekee Kwangu"

$
0
0
Shilole Achekelea Mfungo Ndani ya Ndoa "Huu ni mfungo wa Kipekee Kwangu"
WAKATI waumini wa Dini ya Kiislam wakiendelea na Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, staa wa muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amechekelea mfungo huo ulivyo wa tofauti na miaka mingine kwake kwani yupo ndani ya ndoa.

Shilole aliiambia Za Motomoto News kwamba, katika mfungo wa mwaka huu, anaona raha mno kwani ndiyo kwa mara ya kwanza umemkuta ndani ya ndoa na amekuwa akifunga na kufanya dua na mumewe, Ashraf Uchebe tofauti na miaka mingine ambayo alikuwa hajaolewa, alikuwa akilegalega kufanya sala na kufunga.

“Huu ni mfungo wa kipekee kwangu kwani ndiyo kwanza umenikuta ndani ya ndoa, kiukweli ninajisikia raha mno ambayo sikuwahi kuipata awali,” alisema Shilole au Shishi Baby

Shilole aliwataka mastaa wa kike ambao hawajaolewa wajitahidi waolewe na waachane na kuzini kwa sababu dua zao ndipo zitakapopokelewa pia anawaombea ili wapate waume wema kama yeye alivyopata mume mwema anayemuongoza katika njia nzuri ya kumjua zaidi Mwenyezi Mungu.

Aunty Lulu Ampongeza RPC kwa Tamko la Wanaume Wanaokohoa Wanawake Wenye Makalio Makubwa

$
0
0
Aunty Lulu Ampongeza RPC kwa Tamko la Wanaume Wanaokohoa Wanawake Wenye Makalio Makubwa
BAADA ya hivi karibuni aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Magharibi ambaye kwa sasa amehamishiwa Mkoa wa Kaskazini Pemba visiwani Zanzibar, RPC Hassan Nassir kutoa tamko la wanaume wanaokohoa wanawake wenye makalio makubwa wanapokatiza kuwa ni kosa kisheria, mwanadada kutoka Bongo Muvi, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ amempa tano kamanda huyo kwa hatua hiyo.

Akichonga na Za Motomoto News, Aunty Lulu alisema kuwa, anampongeza RPC Nassir kwa hatua hiyo kwa kuwa yeye ni miongoni mwa wanawake ambao wamekuwa wakikutana na kero kubwa kutokana na umbo lake kwani kila akikatiza kwenye kundi la wanaume, humpigia miluzi, kumzomea na kujikohoza hovyo hivyo sheria kwamba wanaofanya hivyo ni shambulio la aibu na kwamba watapandishwa mahakamani itasaidia kutokomeza tabia hiyo.



“Kiukweli ninampongeza sana Kamanda Nassir maana wanaume wamezidi, wamekuwa wakizomeazomea tu na kuguna kila mwanamke aliyefungashia anapopita mbele ya macho yao, sasa wakipandishwa mahakamani naamini watakuwa wanawaheshimu wanawake,” alisema Aunty Lulu.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images