Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

0
0
Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja. Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.


Thomas Ulimwengu Amesaini Sudan

0
0
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars aliyewahi kuvichezea vilabu vya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na club ya AFC Eskilstuna ya Sweden Thomas Ulimwengu baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu leo amepata timu.

Thomas Ulimwengu alikuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akiuguza jereha lake la goti na baada ya kupona alijiunga na AFC Eskilstuna ya Sweden na kupata jeraha tena la goti liloendelea kumuweka nje ya uwanja tena kwa muda mrefu.

Leo Thomas Ulimwengu ameripotiwa kusaini mkataba wa mwaka mmoja na club ya Al Hilal ya Sudan, hiyo inakuja ikiwa zimepita siku chache toka zimalizike tetesi za kuwa alitaka kusaini club ya nchini Bosnia.

Benki Kuu Wamezungumza Mapya Kuwasili Mabilioni ya Dr. Shika

0
0
Jana May 24, 2018 nakusogezea Stori iliyoshika headlines katika mitandao ya kijamii inayomhusu  Dr. Louis Shika ambaye kasema fedha zake na vipande vya dhahabu vimewasili kutoka Urusi na ameonesha Document za kupokelewa kwa mali hizo hapa nchini.

Kaimu Meneja Mawasiliano wa B.O.T, Vicky Msina ambaye ameelezea kile kilichopo kwa upande wa Benki Kuu ya Tanzania.


Huzuni ya Baba Billnass Baada ya Kukanwa Kwenye Wimbo wa ‘Tag Ubavu’

0
0
Mkali wa Bongo Fleva Bill Nas katika wimbo wake wa ‘Tag Ubavu’ ameimba mashairi yanayoonesha amemkana baba yake mzazi “hata dingi simjui na story zake hazinisumbui”

Mdogo wake Billnas ambaye anaitwa Steve ameongea kuhusiana na ishu hiyo pamoja na ilivyomfikia baba yao.

Ndege ya Malaysia iliyopotea na watu 298 mwaka 2014 ilipigwa na Kombora

0
0
Taarifa mpya ya kuifahamu leo May 24, 2018 ni kuhusu Wapelelezi wa Uholanzi waliokuwa wakichunguza ajali ya ndege ya Malaysia MH17, wamekamilisha uchunguzi na kuonyesha kuwa ndege hiyo ilipigwa kombora na Jeshi la Urusi.

Katika shambulizi hilo la July 17 2014 kwenye anga la Ukraine watu wote 298 waliokuwa ndani ya ndege ya Boeng 777 waliuawa wakati ikivunjika vipande ikiwa safarini kutoka Amsterdam kwenda Kuala Lumpur.

Ilipigwa na kombora aina ya BUK lililofyatuliwa kutoka eneo lililodhibitiwa na waasi nchini Ukraine. Urusi inasema hakuna silaha zake zilizotumika.

Kisa hicho kilitokea wakati wa mzozo kati ya serikali na waasia wanaoungwa mkono na Urusi.

October, 2015 kamati ya Uholanzi ilisema kuwa ndege hiyo iligongwa na kombora lililotengenezwa nchini Urusi la BUK.

Usichokijua Kuhusu Wimbo wa Kwanza wa Diamond Platnumz "Nenda Kamwambie"

0
0
Fahamu kwamba video queen wa wimbo wa kwanza wa Diamond platnumz alikuwa dada yake Esma Platnumz,kwa nini Esma? ni kwamba wadada ambao aliwaalika Diamond kufanya hiyo scene hawakutokea kutokana na dharau kwa kuwa jamaa hakuwa staa wala Handsome

Ndipo Dada mtu akaombwa kucheza hiyo part na akaimudu sana (halafu Esma alikuaga mzuri kishenzi)...naamini hao wadada waliomtosa D leo hii wanatamani hata kushikana nae mkono tu,Maisha safari ndefu sana tusidharauliane.

Najua ulikuwa hujui ila mimi nakujuza kidogo tu..
Angalia hii kuanzia dakika ya 3:10

VIDEO:


TAZAMA KAMWAMBIE..

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Mayweather Afanya Kufuru Ampa Mwanaye Pete ya Bilioni 11 Kwenye Siku yake ya Kuzaliwa

0
0
Mayweather Afanya Kufuru Ampa Mwanaye Pete ya Bilioni 11 Kwenye Siku yake ya Kuzaliwa
BONDIA maarufu duniani, Floyd Mayweather amemfanyia kufuru mtoto wake, Iyanna ‘Yaya’ baada ya kumnunulia pete ya almasi yenye thamani ya dola za Kimarekani milioni 5 (zaidi ya shilingi bilioni 11 za Kibongo) katika siku yake ya kuzaliwa ‘bethidei’.



Kwa mujibu wa Mtandao wa TMZ, Mayweather amekuwa akimpenda Yaya kuliko pesa na marafiki. Mayweather alimkabidhi Yaya pete hiyo katika bethidei ambapo alikuwa akitimiza miaka 18. Hata hivyo, baada ya kutupia mtandaoni aliandika kuwa amekuwa akipenda kuiangalia mara kwa mara na wala hachoki.


Hii si mara ya kwanza kwa Mayweather ‘kumsapraizi’ Yaya katika siku yake ya kuzaliwa kwani alipotimiza umri wa miaka 16, aliwaalika wakali wa Hip Hop, Drake na Future kwa ajili ya kumuimbia huku pia Justin Bieber naye akialikwa kumtungia Yaya wimbo maalum.

Inakumbukwa kwamba, Yaya alipotimiza umri wa miaka 14, Mayweather alimzawadia gari aina ya Mercedes 550 S-Class

Aunt Ezekiel Awapa Makavu Wanaomsema Kuhusu Kuvaa Nguo Aliyoshonewa na Hamisa Mobetto

0
0
Aunt Ezekiel Awapa Makavu Wanaomsema Kuhusu Kuvaa Nguo Aliyoshonewa na Hamisa Mobetto
MKALI wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel amefungukia kuhusiana na ishu ya kushonewa nguo na mwanamitindo Hamisa Mobeto, ambayo aliiva siku ya uzinduzi wa filamu yake na kusema kuwa kwa upande wake haoni shida yoyote kwani akivaa nguo aliyoshonewa na mwanamitindo huyo si jambo la ajabu.

Aunt aliliambia Amani kuwa, anawashangaa wanaoshangaa ishu hiyo kwa sababu yeye na Mobeto hawana ugomvi wowote na wala hajawahi kukosana naye, sasa kitakachomfanya ashindwe kuvaa nguo aliyomshonea ni kitu gani?

“Mimi ninawashangaa sana wanaoongea kuhusiana na kuvaa nguo ambayo nimeshonewa na Hamisa. Sioni tatizo kwani tofauti zake na mtu mwingine mimi hazinihusu,” alisema Aunt.

Watu wamekuwa wakimsema Aunt mitandaoni wakihoji kuwa, anakuwaje karibu na Mobeto anayedaiwa kutembea na Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwa sasa wakati yeye ni ‘Team’ Zari (Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’, mpenzi wa zamani wa Diamond)!

Spika Ndugai: Wabunge 363 Hawatasafiri Nje ya Nchi Kwa Miaka Yote Mitano

0
0
Spika Ndugai: Wabunge 363 Hawatasafiri Nje ya Nchi Kwa Miaka Yote Mitano
Bunge  limesema wabunge 363 hawatasafiri kwenda popote nje ya nchi kwa kipindi cha miaka mitano kutokana na sera ya kupunguza safari za kimataifa.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Spika wa Bunge Job Ndugai bungeni alipokuwa akijibu mwongozo wa Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari.

Katika kauli yake, Nassari aliomba mwongozo wa Spika kutokana na uwakilishi wa Bunge kuwa hafifu "kidogo" kwenye majukwaa ya kimataifa.

"Ushiriki wao majukwaa mbalimbali wabunge wamekuwa wakienda kwa gharama zao... wanajilipia ndege, kampeni kwa gharama zao, wakati mataifa mengine kama Cameroon na wapi wametuma ujumbe wa watu kabisa kwenda kutafuta nafasi, naomba muongozo wako kwenye hili," alisema Nassari.

Nassari alisema juzi Bunge limewapongeza Mbunge wa Handeni Vijijini (CCM), Mboni Mhita ambaye amechaguliwa kuwa Rais wa Umoja wa Vijana wa Bunge la Afrika na Mbunge wa Shinyanga mjini (CCM), Steven Masele ambaye amechaguliwa kuwa Makamu wa Kwanza na Rais wa Bunge la Afrika (PAP), lakini ushiriki wa bunge ni hafifu kwa wabunge wanaotakiwa kushiriki kwenye majukwaa ya kimataifa.

Akijibu mwongozo huo, Ndugai alisema sera ya kupunguza safari za nje, imepunguza safari za wabunge kwa zaidi ya asilimia 90.

"Zimeelezwa mara kwa mara sababu za safari kupungua ndio mtazamo wa nchi na uelekeo wa nchi, hata mkuu wa nchi yeye mwenyewe ni mfano wa kutosafiri nje," alijibu Spika Ndugai.

"Sasa kundi linalobakia la kusafiri nje ya nchi angalau ni IPU (Bunge la Muungano wa Mabunge) ambalo lina wabunge sita, SADC yenye wabunge watano, PAP (Bunge la Afrika) yenye wabunge wanne, ACP (Bunge la Afrika, Caribean na Pacific) ambayo ina wabunge watatu, CPA (Madola) yenye wabunge watano... Ukiwajumlisha wote hawa ni takriban 30 na bunge lina wabunge 393. Ukiondoa hawa 30 wanabaki wabunge 363 ambapo kwa miaka mitano hawatasafiri kwenda popote," alisisitiza.

Ndugai alisema wabunge hao labda watasafiri kwa safari ambazo hazina gharama yote kwa mlipa kodi.

"Labda vile visafari ambavyo huwa havina chochote ambavyo huwa tunawauliza kuna safari hapa unaweza kutembea kidogo," alisema Ndugai.

"Vile ambavyo havihusishi serikali, tumekuwa tukiokota mmoja mmoja... wengine wanakataa."

Alieleza kuwa kuna wakati ilipatikana safari ya kwenda China wabunge 20 lakini walipofika Uwanja wa Ndege, wabunge sita au saba hawakuwapo.

"Wanasema aaah, Spika bwana hizo safari zao za njaa njaa hatuendi sisi, sasa panapokuwa na wabunge 30 kati ya 393 halafu hawa 30 kila wakati wanatushughulisha kujibu kwanini wao hawasafiri hapo ndio naonaga ni 'very unfair' (si haki kabisa)... tunashughulika nao ofisini tunaelezana ikiwezekana wanaenda na kadhalika."

Spika alifafanua wabunge hao wasifanye kuwa wanastahili sana kusafiri.

"Inategemeana na mambo kadhaa, bajeti yetu na mambo mengine kwa hiyo bajeti yetu ikiruhusu wataenda inapokuwa imebana na mambo mengine kidogo haijakaa sawa kikao hiki mnakosa kikao kinachokuja mnaenda," alisema spika huyo.

"Hivyo hivyo tunavyoenda. Ukiwa katika kundi ambalo wenzako hawaendi popote, lakini wewe angalau unasafiri kidogo halafu nyie ndio wakuuliza maswali kila kukicha haipendezi."

Aliagiza mambo ya aina hiyo yamalizwe kiutawala na kwamba wataendelea kusafiri hao wachache kutegemeana na hali halisi na mambo yalivyo mezani.

Korea Kasikazini Yasikitishwa Hatua ya Trump Kujitoa Katika Mazungumzo....... Yasema Ipotayari Kukutana Naye Wakati Wowote

0
0
Korea Kasikazini Yasikitishwa Hatua ya Trump  Kujitoa Katika Mazungumzo....... Yasema Ipotayari Kukutana Naye Wakati Wowote
Korea Kaskazini imeelezea kusikitishwa kwake na hatua ya rais Donald Trump kujitoa katika mazungumzo yaliyopangwa kufanyika juni 12 huko Singapore.

Kwa mujibu wa mashirika ya habari nchini humo, uamuzi huu umekuwa kinyume na matarajio ya dunia.

Inadaiwa kuwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un alikuwa amefanya jitihada zote katika maandalizi ya mkutano huo na kwamba Pyongyang ilikuwa tayari kuhakikisha tofauti zilizopo kati ya taifa lake na Marekani zinasuluhishwa kwa namna yoyote na popote, lakini Trump mwenyewe amesema uwezekano wa kufanyika mazungumzo hayo bado upo.

Taarifa hizo pia zimeleta mshtuko kwa jumuiya ya kimataifa, ambapo katibu mkuu wa umoja wa mataifa Antonio Guterres, ameelezea kuguswa kwake na hatua hiyo ya Marekani huku naye rais wa Korea Kusini Moon Jae-In akitoa wito kuwepo kwa mkutano wa dharura wa viongozi wa juu wa usalama kuhusiana na suala hilo.

Marekani imeghadhabishwa na hatua ya Korea kaskazini kufanya mazoezi juu ya rasi hiyo katika siku za nyuma
Mkutano huu ungejadili namna ya uondoaji wa silaha za nyuklia katika rasi ya Korea kufuatia mkutano wa Korea zote mbili uliofanyika mwezi April mwaka huu.

Hata hivyo yapo baadhi ya mambo yanayotajwa kama dosari zilizo jionyesha kuelekea mazungumzo hayo na hasa kauli za kushinikiza msimamo wake ndani ya barua aliyomuandikia kiongozi wa Korea Kaskazini baada ya kuwa na mazungumzo na rais wa Korea kusini Moon.

Washington pia inailaumu Pyongyang kwamba haikuwa imara katika maandalizi na kwamba pale maofisa wa Marekani walipopanga kukutana na wanadiplomasia wa Korea kaskazini hawakutokea, dalili zilizokuwa mbaya kuelekea mazungumzo haya.

Hatima ya Waliotajwa Mali za CCM Kuanza Jumatatu

0
0
Hatima ya Waliotajwa Mali za CCM Kuanza Jumatatu
Hatima ya wana CCM waliotajwa katika ripoti ya ubadhirifu, utapeli na wizi wa mali za chama hicho huenda ikajulikana wiki ijayo baada ya vikao vya juu vilivyopangwa kufanyika Jumatatu na Jumanne.

Hatua hiyo ni baada ya mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli kuahidi kupeleka ripoti ya uchunguzi wa mali hizo kwenye vikao hivyo ndani ya mwezi huu ili kuijadili na viongozi kutoa maelekezo.

Taarifa ya chama hicho kwa vyombo vya habari ilisema jana kuwa, kutakuwa na vikao vya Kamati Kuu (CC) pamoja na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) vitakavyofanyika kwa siku mbili, Mei 28 na 29.

Hata hivyo, taarifa hiyo iliyosainiwa na katibu wa NEC- Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole ilisema kuwa vikao hivyo ni vya kawaida na kwamba vinaketi kwa mujibu wa ibara ya 102(2) ya katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo la mwaka 2017.

Katika vikao hivyo, Polepole alisema NEC pia itashughulika na kazi zake zingine, ikiwamo kujaza nafasi zilizo wazi za wajumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu ya Taifa. Kujazwa kwa nafasi hizo kunafuatia uchaguzi wa wajumbe wa NEC uliomalizika Desemba 2017 ambapo wajumbe wanaoingia CC moja kwa moja kupitia nafasi zao walishapatikana.

Wajumbe hao ni mwenyekiti, makamu wenyeviti, wenyeviti wa jumuiya za chama (vijana, wazazi na wanawake), wajumbe wa sekretarieti (katibu mkuu, naibu makatibu wakuu na makatibu wa itikadi na uenezi; fedha na uchumi; mipango na oganaizesheni na mambo ya nje), maspika wa bunge, baraza la wawakilishi na waziri mkuu.

Kutokana na uamuzi wa chama hicho kupunguza idadi ya wajumbe kutoka 34 hadi 24, hivyo wajumbe wanaosalia kukamilisha idadi ni wanane.

Waliotajwa na kamati ya Bashiru

Wakati ikiwa ni wazi kuwa hatima ya watu waliotajwa kwenye kamati iliyochunguza wizi, utapeli na ubadhirifu wa mali za chama hicho huenda ikajulikana, wachunguzi wa masuala wa siasa wanasema uwezekano wake ni mdogo kutokana na muda mfupi wa vikao hivyo.

Hatua hiyo inafuatia ripoti ya kamati ya kuhakiki mali za chama hicho iliyoundwa na Rais Magufuli chini ya Dk Bashiru Ally kubaini upotevu mkubwa wa mali za chama uliosababishwa na mikataba mibaya, ubadhirifu, wizi, usimamizi mbaya wa mali, utapeli na ukosefu wa maadili katika uendeshaji wa miradi ya chama.

Akizungumza wakati wa kupokea ripoti hiyo mapema wiki hii, Rais Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM alisema haiwezekani kupiga vita rushwa na ufisadi ndani ya Serikali wakati chama kina rushwa na ufisadi.

Alisema anataka pia chama kisafishwe ili mambo ya rushwa na ufisadi yaishe na Tanzania iende vizuri.

Rais Magufuli alienda mbali zaidi na kuwaagiza wajumbe wa sekretarieti ya CCM waliohudhuria hafla ya uwasilishwaji wa ripoti hiyo kuanza kufanyia kazi baadhi ya mambo yaliyo ndani ya uwezo wao na kwamba, masuala mengine yataamuliwa na vikao vya juu vya chama.

Akihutubia Mkutano Mkuu wa CCM jijini Dodoma mwanzoni mwa mwaka jana, Rais Magufuli aliwaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa anataka kusimamia mali za chama na chini ya uongozi wake chama hicho hakitakuwa ombaomba tena.

Alisema kwa miaka yote CCM imekuwa ikiomba hata kwa watu ambao hawastahili wakati ina mali nyingi ambazo zinatumiwa vibaya na baadhi ya wanachama ambao sio waaminifu.

Kamati ya Dk Bashiru ilitangazwa Desemba 20 mwaka jana ikiwa na wajumbe tisa.

Akikabidhi ripoti hiyo, Dk Bashiru alisema uhakiki huo umefanywa kwa mali za chama hicho, jumuiya na kampuni zake.

Alisema wakati wa utekelezaji wa kazi hiyo, walitembelea maeneo yenye mali za chama hicho na kuwahoji watu mbalimbali wakiwamo viongozi waliohusishwa na mali zilizokuwa zikihakikiwa.

Dk Bashiru alisema kuwa, kamati imepitia nyaraka na kufuatilia uhalisia katika ofisi za mamlaka husika, kufanya uchambuzi wa taarifa na kutoa mapendekezo.

Maoni ya wachambuzi

Akizungumzia vikao hivyo, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Beson Bana alisema hatua ya kufikisha ripoti hiyo katika vikao vya juu vya chama hicho ni sawa, ingawa haoni hatua kubwa itakayofikiwa kwa sasa kutokana na muda wa vikao kuwa mdogo.

“Huwezi kumhukumu mtu bila kumpa nafasi, vikao hivi vinakutana kwa siku mojamoja sidhani kama watapata nafasi ya kuisoma ripoti hiyo yenye volume nyingi vile nilivyoviona na wakati huohuo itoe haki sawa ya kuwasikiliza watuhumiwa kisha kutoa maamuzi,” alisema.

Hata hivyo, Dk Bana alisema dhamira ya Rais imeonekana wazi kwamba ana nia ya dhati ya kupinga ufisadi na hata katika matukio mengine kama vile ya makinikia, wafanyakazi hewa na walioghushi vyeti hakuchukua hatua mpaka pale alipounda tume kuchunguza masuala hayo.

“Nia ya dhati ipo ila wanahitaji muda zaidi. Kwanza wajumbe wenyewe wanapaswa waisome ripoti ile kwa uangalifu mkubwa kisha waliotuhumiwa wapate haki ya kujitetea kabla ya kuwachukulia hatua, kwani naamini hilo limefanyika katika tume hiyo vivyo hivyo inapaswa kufanywa na chama pia,” alisema Dk Bana.

Hatua zaidi

Mwishoni mwa mwaka jana chama hicho kilitangaza ‘kiama’ kwa wanachama wake waliojimilikisha mali za chama hicho.

Katika mahojiano maalumu na Mwananchi, Polepole alisema kwa muda mrefu mali za chama hicho zilikuwa zikimilikiwa na vikundi au watu binafsi jambo lililosababisha kukikosesha mapato.

“Nawaambia wajiandae kuanzia wiki ijayo tutaanza kubomoa nyumba za watu, yakiwamo maghorofa ambayo yalijengwa katika viwanja vya chama kwani mpaka sasa tumeshinda kesi kadhaa ambazo zinatutaka tuyarejeshe maeneo yetu.

“Kuna watu walidhani hatutawafikia katika zoezi hili ukweli ni kwamba hakuna jiwe litakalobaki bila kugeuzwa. Na huu ni mwanzo tu maafa zaidi yanakuja,” alisisitiza Polepole.

Alisema katika uhakiki huo pia wameweza kurudisha jumla ya viwanja vya michezo 22 kati ya 33 na hatua zaidi zinaendelea ili kuhakikisha mali zote za chama hicho zinarudishwa.

Picha: Maalim Seif Apokelewa Vizuri na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza

0
0
Picha: Maalim Seif Apokelewa Vizuri na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amepokea ugeni wa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) na Makamu wa Kwanza wa Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dkt. Maalim Seif Sharif Hammad aliyefika Ofisini kwake akiwa ziara ya kikazi Mkoani humo jana Alhamisi, Mei 24, 2018.

IGP Sirro Awapa Onyo Kali Wafungwa Walioachiwa kwa Msamaha wa Rais Magufuli

0
0
IGP Sirro Awapa Onyo Kali Wafungwa Walioachiwa kwa Msamaha wa Rais Magufuli
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro amewaonya watu waliopata msamaha wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli wa Aprili 26, 2018 wajichunge tabia na matendo yao.


IGP Sirro ametoa onyo hilo leo Mei 24, 2018 mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akitoa taarifa ya ujenzi wa vituo vya polisi vya kisasa vya Mburahati, Kiluvya-Gogoni na Mbweni ambavyo vimezinduliwa leo.

"Nia ya Mheshimiwa Rais Magufuli kuwapa msamaha ilikuwa njema lakini kuna baadhi ya watu wameitumia vibaya fursa hiyo na hadi sasa watu watano wamekwishauawa na wananchi. Natoa onyo kwa wote waliopata msamaha na wana nia ya kurejea kwenye matendo yao maovu, ukitoka gerezani kwa msamaha, maana yake umerekebisha mwenendo wako na wananchi wanatarajia uwe hivyo, lakini kama ukifanya vinginevyo, aerikali isilaumiwe", amesema IGP Sirro.

Akielezea kuhusu utendaji wa Jeshi la Polisi, Kamanda Sirro amesema tangu ashike madaraka hayo, jeshi hilo limewapeleka askari 1,267 kwenye mafunzo ya medani za kivita na kwamba jeshi hilo liko imara.

"Pia tumepeleka askari wa upelelezi zaidi ya 1,000 kwenye mafunzo ya ujuzi na ustadi (skills and knowledge) wa kupeleleza kesi mbalimbali. Baada ya kuwapa mafunzo haya, tunataka kesi za kawaida upelelezi wake uwe umekamilika ndani ya miezi sita na zile kesi kubwa kubwa upelelezi wake uwe umekamilika ndani ya miezi 12. Tunataka kuhakikisha haki za watanzania zinapatikana kwa wakati," amesisitiza Sirro.

Kwa upande mwingine, Kamanda Sirro alitumia fursa hiyo kumshukuru pia Rais Magufuli kwa kuwapatia sh. bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za askari, kutoa kibali cha ajira kwa askari wapya 1,500 na kuwaruhusu wawapandishe vyeo askari wenye kustahili kuanzia cheo cha Koplo hadi Naibu Kamishna wa Polisi (DCP).

Kiss Daniel Aamua Kumaliza Mgogoro na Lebo ya G- Worldwide Aamua Kubadilisha Jina

0
0
Kiss Daniel Aamua Kumaliza Mgogoro na Lebo ya  G- Worldwide Aamua Kubadilisha Jina
MKALI wa Ngoma ya No Do na Sofa, Oluwatobiloba Daniel Anidugbe ‘Kiss Daniel’ amebadilisha jina na kuanza kujiita Kizz Daniel.

Ishu hiyo imekuja kutokana na mgogoro wa muda mrefu wa kibiashara kati yake na lebo ya muziki ya zamani ya G-Worldwide iliyokuwa ikisimamia kazi zake ambapo ilifikia hatua ya kumburuza mahakamani kwa madai kuwa amekiuka na kushindwa kutimika vigezo na msharti ya mkataba wa kibiashara waliokuwa wamesaini kisha wakamtaka asitumie jina la Kiss Daniel kwa kuwa ni mali yao.

Kiss Daniel, baada ya kuvunjika kwa mkataba wake na G-Worldwide alianzisha lebo yake iitwayo FLY BOY I.N.C ambapo ameshabadili jina na kuwa Kizz Daniel.

Hata katika mitandao yake ya kijamii, tayari ameshaanza kupatikana kwa jina hilo jipy

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA,

Dhuluma Waliotufanyia Yanga Kupitia Malinzi Inawatafuna Mpaka Leo Hata Nipewe Hela Zote na BoT Siwezi Kuwa Msemaji wao - Haji Manara

0
0
 Dhuluma Waliotufanyia Yanga  Kupitia Malinzi Wao Dhuluma Hiyo Inawatafuna Mpaka Leo Hata Nipewe Hela Zote na BoT Siwezi Kuwa Msemaji wao  - Haji Manara
Afisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara amedai kuwa kamwe haitatokea yeye kuihama klabu yake na kujiunga  Yanga SC.

Manara amesema kuwa hata kama angepewa fedha zote nchini na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kamwe hawezi kuwa msemaji wa klabu ya Yanga au hata kuwa mwanachama wa klabu hiyo.

“Hata kama nipewe hela zote na Benki kuu ya Tanzania (BoT) siwezi kuwa msemaji wa Yanga“. amesema Haji Manara kwenye kipindi cha Maisha Mseto cha Times FM.

Kwa upande mwingine, Manara amesema kuwa kipindi kigumu wanachopitia Yanga kwa sasa ni laana ya dhuluma waliyokuwa wanafanya miaka ya nyuma wakati wa enzi za aliyekuwa Rais wa TFF, Jamal Malinzi.

“Yanga walitufanyia dhuluma msimu uliopita kupitia kwa malinzi wao. Dhuluma hiyo inawatafuna mpaka leo. Mafuriko yako kwao, njaa iko kwao, dhuluma hiyo inawatafuna tu.“amesema Manara.

Waziri Jafo Amtaka Mkandarasi Kuvunja Jengo la Shule na Kujenga Upya

0
0
Waziri Jafo Amtaka Mkandarasi Kuvunja Jengo la Shule na Kujenga Upya
Waziri Ofisi Nchi Ya Rais Tamisemi Suleiman Jafo amewataka Wakandalasi wa Suma JKT wanaojenga Shule ya Sekondari Hombolo Kurudia kujenga Shule hiyo baada ya Kuijenga Chini ya Kiwango.

Jafo ametoa agizo madarasa hayo yaiwekewe madawati kwa milioni 20 hiyo ambayo ilitumika kwaajili ya kujenga shule hiyo kutokana ni ilikuwa ni mpango wa Serikali.

Hata hivyo Jafo amesema kuwa ujenzi huo ni mbovu na wanatakiwa kuvunja na kujenga upya katika kiwango cha fedha kilichotolewa.

Sakata la Kuzaa Nje ya Ndoa Lamvuruga Steve Nterere " Natamani Rais Magufuli Azime Data "

0
0
Sakata la Kuzaa Nje ya Ndoa Lamvuruga Steve Nterere " Natamani Rais Magufuli Azime Data "
Muigizaji na mchekeshaji maarufu bongo Steven Nyerere, amesema anatamani kukutana na Rais Magufuli ili amshauri azime data, ili watu wasitumie mitandao ya kijamii kwa kufanya umbea na kuongea habari za uongo za kuchafuana.


Akizungumza na www.eatv.tv, Steve Nyerere amesema iwapo atapata fursa hiyo atamsahuri Rais Magufuli kufuata wanachokifanya China, ambapo wao wamepiga marufuku utumiaji wa mitandao ya kijamii mbali mbali, na kutumia mitandao mingine ya kwao kwa ajili ya kukuza uchumi wao na sio kwa ajili ya kupiga umbea na kueneza habari za uongo.

“Bado tunahitaji kuwa na mwenendo wa China, nitafurahi sana siku Magufuli akizima data, na nadhani kuna haja ya kumshauri Mheshimiwa Rais, kwa sababu kama tunataka kujenga Tanzania ya viwanda, ni lazima siku moja tuzime data hata mwezi nadhani tutafikia malengo, tena andika kabisa Nyerere anatamani kuonana na Magufuli amnong'oneze kuhusu data, azime tu hata nwezi, ili watu wafanye kazi, amesema Steve Nyerere.

Steve ameendelea kwa kusema kwamba ….. “asilimia 90 wanaishi kwenye mitandao na kubuni vitu ambavyo haviingizi taifa hata pato, nia ni kuliongezea taifa pato, wenzetu China wameendelea kutokana kutoipa nafasi mitandao kuihairbu China yao, wameipa nafasi kwa ajili ya kutangaza biashara na utalii, sasa sisi tumeipa nafasi kwa jili ya umbea”,.

Steve Nyerere ametoa kauli hizo zote kutokana na watu kuzusha taarifa kuwa mke wake amemkimbia, baada ya kugundua amezaa nje ya ndoa na muigizaji Welu Sengo.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images