Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Tuache Kufananisha Nyumba na vitu vya Maana Kama Bia

$
0
0

Kila ukinywa bia *1* umekunywa tofali *2* za kujengea. Bia 1 kwa bei ya kawaida ni *Tsh.2500/=* na tofali *1* la inch *6* kwa maeneo mengi ya nchi ni bei isiyozidi *Tsh.1300/=.*

Kama unakunywa wastani wa bia *5* kwa siku (kipimo cha kawaida) it means unakunywa bia *1,825* kwa mwaka sawa na tofali *3,650.

Tofali *3,650* zinatosha kujenga nyumba *1* ya room *3* self contained ya kisasa

Hii inamaanisha kuwa kama wewe ni mnywaji basi kila mwaka unakunywa angalau nyumba *1 au 2.

Sasa hebu jiulize tangu umeanza bia hadi leo umeshakunywa nyumba ngapi?

Anyway.._
Tuache kufananisha nyumba na vitu vya maana kama Bia

*Muhudumu ongeza bia*

Meneja wa Dr. Shika Abanwa, Ni kweli Mabilioni ya Dkt. Shika yamefika..? Ashikwa Kigugumizi

$
0
0
Meneja wa Dr. Louis Shika ambaye anafahamika kwa jina la Catherine Kahabi amesema kuwa kwa taarifa zilizopo ni kweli fedha imefika lakini ipo namna ya kujiridhisha na hawezi kuongea in deep kwakua hajafuatilia sana kwani alikuwa busy ila atalifuatilia kujua zaidi.

Na alipoulizwa na mwandishi wa millardayo.com na Ayo Tv kama fedha zimeshaingia mpango ni kwenda kuchukua zile nyumba zilizokuwa zikipigwa mnada..? Majibu yake aliyatoa hapa Bonyeza PLAY kumsikiliza VIDEO:

Billnass Kazungumza ishu ya Kumkana Baba yake Kwenye wimbo

$
0
0
Baada ya kijana anayedaiwa kuwa ni mdogo wa Billnass kuzungumzia ishu ya baba mzazi wa Billnass kuhuzunishwa na ngoma ya “Tagi Ubavu” kutokana na mstari unaosema kuwa “dingi simjui na story zake hazinisumbui”

Tumempata Billnass kazungumza kuhusiana na ishu hiyo kwenye exclusive interview na Ayo Tv, bonyeza PLAY kusikiliza alichokizungumza.


Sakata la Shehena ya Korosho kuchanganywa na Kokoto lafika Patamu

$
0
0

DODOMA: Serikali kupitia Naibu Waziri wa Kilimo, Mary Mwanjelwa amesema uchunguzi dhidi ya maafisa walioruhusu kusafirishwa kwa shehena ya Korosho iliyochanganywa na kokoto
-
Mpaka sasa hatua zilizochukuliwa na Serikali ni pamoja na kuitaka Bodi ya Korosho Nchini, Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi Ghalani, Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Mamlaka ya Serikali za Mitaa kuanza kushirikiana
-
Mikakati iliyoafikiwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha usimamizi wa ubora wa Korosho katika mnyororo wake wote ili kudhibiti uhalifu kama huo yoyote
-
Serikali itatoa kauli mara moja pindi uchunguzi dhidi ya watu hao utakapokamilika.

Msichana ni Mzurii Lakini Haeleweki..Naombeni Ushauri

$
0
0
Kuna msichana ambaye ni Jirani yangu sana na kusema kweli ni mzuri sana. Nilipataga hofu ya kumtongoza kwa sababu ya uzuri wake na ni gate kali. Ila kila alipokuwa anapata upenyo anakuja getto kwangu tunacheki movies na kula kwangu.


Siku moja nikajisemea moyoni kuwa Jamii na masela wangu wataniona kama sitampa mtoto haki yake mbali na kumuoa. Basi kidume nikajipanga na alivyo kuja kwa mara ingine gheto nikampa makavu live bila kupepesa macho. msichana aliniangalia na hakuweza kusema kitu akang'oa nanga na kuondoka.

Sikuwa na haja ya kumsihi arudi kwani alikasirika,ila moyoni nilijua massege sent. Ikapita kama wiki mbili bila kumwona tena ila kwa bahati nilikuwa nakatiza mtaani nikakutana nae akitokea sokoni nikampa hi na akaipokea bila kusita.

Nilivyompita na kumwacha nyuma aliniita "Ras" Lete habari,naomba unisaidie haka kamfuko huku akinitazama kwa jicho la madaha akiashiria kukubalian na ile sms nliyomtumia.

Basi tukiwatunasonga na safari huku story za hapa na pale nikaona ni vyema kumuuliza vp juu ya ile sms. Cha ajabu alikasirika zaidi ya mwanzon na kuninyang'anya kale ka mfuko na kuniambia nimemboa na hataki kampan yangu wala swaga zangu.

Naommbeni ushauri wenu nimfanyie Suprise gani huyu msichana ili anielewe kuwa nampenda.

Heche Afunguka Suala la Ufisadi wa TANESCO

$
0
0


Mbunge wa Tarime Vijijini (CHADEMA) John Heche amesema Shirika la Umeme nchini TANESCO halitaweza kupata faida mpaka kuisha kwa dunia kutokana na mkataba wa kifisadi waliongia na kampuni ya uzalishaji umeme ya Songas.

Heche amesema hayo jana Mei 25, 2018 Bungeni Jijini Dodoma, alipokuwa akichangia hoja mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati katika mwaka wa fedha 2018/2019 na kuongeza kuwa kama mkataba huo utaendelea basi madeni ya TANESCO yatazidi kuongezeka maradufu.

“Mwenyekiti umesema hapa TANESCO wameanza kupata faida, kamwe mpaka dunia hii inaisha TANESCO hawatapata faida kwasababu mkataba walioingia na Songas ni mkataba wa kihuni na wizi ndiyo unasababisha shirika hili kuendelea kuwa na madeni na hata dunia hii inaisha kama mkataba na Songas utaendelea kuwepo madeni ya TANESCO yataendelea kuwa makubwa”, alisema Heche.

Mbunge huyo aliongeza kuwa kitendo cha TANESCO kuwa shirika pekee linalozalisha umeme nchini bila ya kuwa na mshindani imechangia kwa kiasi kikubwa kuwa na mzigo wa kutoa huduma pamoja na madeni ambapo mpaka kufikia sasa TANESCO inadaiwa zaidi ya bilioni 900.

Bunge limepitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo jumla ya shilingi trilioni 1.69 imeizinishwa kwa matumizi ya miradi ya maendeleo na matumizi ya kawaida.

Wanawake/Wasichana wa Aina Hii ni Hatari Sana Kuwa Nao Kimapenzi

$
0
0


1.Demu wako wa zamani
Ni vizuri kutorudia mahusiano ya zamani na zaidi kama kwenye mahusiano yenu ya mwanzo mambo hayakuishia kwa uzuri. Sababu kuu ya msingi, kiukweli ni kwamba hakika mwanzoni mlikuwa hamuendani na ndio sababu ya iliyopelekea kuvunjika kwa mahusiano yenu, ndani ya hizo sababu kuna vitu vilivyopolekea kutokea kwa hayo, ukichunguza na kuziangalia kwa makini utagundua ni za asili na ambazo si rahisi kwa mmoja wenu kuzibadilisha sababu ni vitu au mambo ambayo yatakuwa ni ya damuni.

2.Dada wa rafiki yako kipenzi
Epukana na kujiingiza kwenye mahusiano na dada wa rafiki yako. Si tu kwamba utaweza kujiingiza kwenye uhasama na chuki kama mambo hayatakwenda sawa, ila pia utaweza kujiweka kwenye mazingira ya kujikuta siku moja unapigwa hata ngumi za uso sababu tu ulimuumiza dada yake. Pia, utaweza kumkosa mtu ambaye ndie alikuwa ni kimbilio lako kwa mambo mbalimbali pale ambapo itatokea wewe na dada yake mambo kutokwenda sawa, sababu hapo patakuwa na mgongano wa kimaslahi kwa huyo rafiki yako.

3.Wanawake wenye mambo mengi
Kiukweli, kutoka na watu kama hawa kinaweza kuwa ni kitu cha kufurahisha, ila mwisho wa siku itakuingiza kwenye matatizo. Mara zote kumbuka ni vyema kuwa salama kuliko kujuta. Usijiingize kwenye majaribu ambayo utakuja kuyajutia kwa maisha yako yote.

4.Wanawake wanaopenda hela kupitiliza (Wachunaji)
Kuwa mbali nao, labda kama unataka salio lako limalizike pasipo wewe kujifahamu. Naamini hili kila mmoja analifahamu na halihitaji darasa zaidi.

5.Demu wa zamani wa rafiki yako
Kama unathamini urafiki wako na mshikaji wako achana na habari ya kutoka na aliyekuwa demu wake. Mambo yanaweza kubadilika na kuwa kama au zaidi ya yaliyotokea kwa rafiki yako na ikaja kula kwako zaidi. Wakati mwengine inaweza tengeneza chuki kati yako na rafiki yako, huku akiamini kwamba ulikuwa unatoka au kumnyemelea demu wake toka zamani.

Wadau mademu wapo wengi sana, fanya kutafuta wengine nje ya hawa….. ni ushauri tu.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Kama Unataka Kufurahia Mapenzi oa Mwanamke Asiye na Kazi

$
0
0

Wanawake wasio na Kazi wanakua hawana mambo mengi. Ukitoka kwenye mihangaiko yako anakupokea na kukukaribisha Nyumbani kwa furaha. Utakuta chakula kishaiva, utakuta Watoto wasafi kama mmebahatika kuwa nao, hata ukimuachia hela ya matumizi anatumia Vizuri tena unampa hela kwa furaha kabisa. Mkibahatika kupata Mtoto hutakuwa na mawazo ya Mtoto wako kupigwa na House girl. Ukitembelewa na Familia, hawataboreka kwani muda wote watakua na mwenyeji Mama mwenye Nyumba.

Jidanganye uoe Mwanamke mwenye Kazi. Asilimia kubwa wanarudi wamechoka kiasi kwamba hata mkilala hakugeukii wala hataki umguse. Atataka haki sawa eti akipika wewe ufue Nguo au umsaidie Kupika. Mara chache atakutengea Maji ya kuoga. Muda mwingi anatoka Kazini amenuna, hata akichelewa hataki umuulize alikua wapi.

Wana viburi sana, ukiwauliza kitu wanajibu kwa nyodo, hatakusikiliza. ukimsemesha kidogo tu ataenda kulala kwa marafiki zake au kwa ndugu zake. Haoni aibu kukukolomea Mwanaume hata mbele za watu. Anajifanya anawivu sana, atapiga Simu kila dakika kukuuliza ulipo as if wewe mtoto mdogo hujui pa kwenda.

Anapewa Mshahara lakini hautojua unaenda wapi kwani kila siku utaombwa hela ya Salon. Siku ukiishiwa ukamuomba hela ya Bia hatakupa bali atasema siwezi kukupa hela yangu ukahonge Malaya zako.

Siku akifurahi atakuletea zawadi ya Shati, mara moja kwa Miezi Mitano kana kwamba halipwi Mshahara. Dawasco wakimkuta hatawapa hela yake hata kama anayo, atawambia hayupo.

Ukioa Mwanamke mwenye kazi utamfaidi siku ukiumwa, ataomba ruhusa ili aje akuhudumie, atakununulia sana Socks na Matunda Matunda. akitaka kununua kitu atakua na kianzio sana sana ataomba umuongezee Hela.

Manara Asema Hawezi Kuishi Bila mke "Wanawake Wana Faida Kubwa Sana"

$
0
0
Ukitaka kumtesa msemaji wa Simba Haji Manara basi we mwambie aishi bila mke, amekiri mwenyewe kwamba hawezi kuishi bila mke.

Manara anasema tangu alivyooa ameshasahau kunyoosha nguo, kufua na mambo mengine kibao kwa sababu vitu vyote hivyo hufanywa na mama watoto wake.

Ukimuona Manara popote kama amependeza au ‘amepuyanga’ upande wa mitupio basi wa kusifiwa au kulaumiwa ni mke wake, jamaa anasema hadi nguo za kuvaa kwenye mitoko mbalimbali anapangiwa na baby wake.

“Wanawake wanafaida kubwa sana, kwa mfano ukizoea kuishi na mke, huwezi kuishi bila mke. Mimi siwezi kuishi bila mke, kwa sababu kuna baadhi ya mambo ya msingi kwa binadamu mimi siyamudu.”

“Siwezi kupiga pasi, kufua, sio kwamba sijui lakini nimeshasahu miaka nyingi sana. Sijawahi kufungua kabati langu la nguo kwa hiyo sijijui yani, hata nguo za kuvaa nachaguliwa na mke wangu, nikitaka kutoka ananiuliza mizunguko yangu halafu ananichagulia nguo za kuvaa.”

“Tangu nimeoa sijawahi kujichagulia nguo za kuvaa kwa hiyo kwangu kuishi bila mke ni shida. Namshukuru Mungu hata mtalaka wangu ambaye alikuwa mke wangu wa kwanza naye alikuwa hivyohivyo.”

“Namshukuru Mungu katika jambo ambalo sikukosea ni kuchagua mke, wa kwanza na wa pili pamoja na kwamba mke wa kwanza nimwacha lakini sikukosea, nimepata wake ambao dini zetu, kabila zetu, tamaduni zetu, wake wazuri ambao unaweza kutoka naye popote lakini na tabia zao nzuri.”

Alikiba Afunguka Kuhusu ujio wa Albamu yake

$
0
0
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma ‘Mvumo wa Radi’ ameiambia ITV kuwa kuna uwekano wa albamu kutoka mwaka huu na tayari maandalizi yameshafanyika.

“Albamu naweza nikaachia mwaka huu nipo katika kumalizia japokuwa tayari nipo na nyimbo ila nataka kila kitu kitoke kikiwa perfect,” amesema Alikiba.

Ameongeza kuwa albamu hiyo itauzwa kwa njia ya online na kawaida, yaani hard copy.

Utakumbuka kuwa wasanii wa Bongo Flava waliotoa albamu hivi karibuni ni pamoja na Vanessa Mdee, Diamond, Wakazi na Chin Bees.

Azam FC wamsajili Donald Ngoma

$
0
0
Uongozi wa Klabu ya Azam FC yenye makazi yake huko Chamazi jijini Dar es salaam, umethibitisha kuwa umeingia makubaliano ya usajili na mshambuliaji Donald Ngoma, kwa ajili ya msimu ujao 2018/2019.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu hiyo mapema leo, imeeleza kwamba muda wowote kuanzia sasa Azam FC inatarajia kumpeleka mchezaji huyo katika Hospitali ya Vincent Pallotti jijini Cape Town, Afrika Kusini kwa ajili ya kumfanyia vipimo vya afya ili kuona ni kwa kiasi gani majeraha yaliyokuwa yakimsumbua yamepona.

Azam FC inaamini ya kuwa ujio wa nyota huyo kutoka nchini Zimbabwe aliyewahi kuchezea FC Platinum ya huko kabla ya kuhamia Yanga, ni sehemu tu ya mikakati ya benchi la ufundi na uongozi katika kuboresha kikosi kwenye eneo la ushambuliaji kuelekea msimu ujao.

Pia uongozi wa Azam FC unaamini kuwa Ngoma atakuwa ni miongoni mwa nyota wapya wa timu hiyo watakaoonekana kwenye Kombe la Kagame (CECAFA Kagame Cup) linalotarajia kuanza hivi karibuni tukiwa kama mabingwa watetezi wa michuano hiyo.

Tayari mchezaji huyo ameandaliwa jezi namba 11 iliyokuwa ikitumiwa na mshambuliaji Yahaya Mohammed, aliyerejea Aduana Stars ya nchini kwao Ghana.

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

$
0
0
Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja. Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.

Wanawake Wengi Wanaoolewa ni Darasa la Saba na Form 4 Wenye Degree Hamfai na Degree Zenu.

$
0
0
Wengi Wenye degree hamfai na degree zenu.
Mwanaume ni kichwa cha nyumba. Wanawake wenye elimu ya darasa la saba na form 4 hawasumbui wanaume. wanajua wajibu wao kutii na kumjali Mume,ila wenye zaidi ya hapo,wachache .

Wengi hawajielewi baada ya kujiona wanajua,ila hawafai kuolewa hawana sifa ya kuwa wake,ni wanaume wenzetu. Mtazalishwa,mtalea watoto,mtadanganywa na hamtaolewa. Mtaongezewa watoto na majukumu ila wataolewa wa darasa la saba na form 4.

Na hata maprofesa wake zao ni la saba na form 4 au wanaojielewa,mnaojifanya mna figure, degree,mkoo wapi? mna familia za maana na mmeolewa?.......wife material ni anayemsikiliza mme wake, uwe na elimu au vipi bila kujinyenyekeza huna heshima.

Steve

Je Hii Kauli ya Mdau inaukweli Wowote?

Watu 19 Wamefariki Katika Ajali ya Basi na Lori

$
0
0
Watu wasiopungua 19 wamefariki na wengine kadhaa kujeruhiwa May 26, 2018 wakati basi walilokuwa wakisafiria kugongana na lori katika wilaya ya Kiryandongo magharibi mwa Uganda.

Miongoni mwa waliofariki kulikuwa na watoto watatu na watu wazima 16, taarifa kutoka kwa maafisa wa polisi ilisema.

“Timu ya uokoaji wanafanya kazi bila kuchoka ili kuwaokoa majeruhi na kuwapeleka katika hospitali ya Kiryandongo,” taarifa hiyo ambayo iliyotolewa na msemaji wa polisi, Emilian Kayima, ilisema.

Mashindano ya Kufanya Sura Kuwa Mbaya

$
0
0
Dunia ina vituko sana unaambiwa hivi huko nchini Uingereza kuna mashindano ya kufanya sura kuwa mbaya (Gurning Competitions) sasa leo May 26, 2018 nakusogezea mmoja wa washindi wa kihistoria  wa mashindano hayo anayejulikana kama Anne Woods ambaye ameshinda mashindano hayo mara 27 katikati ya miaka ya 1977 mpaka 2010.



Aidha duru zinasema kuwa familia yake ndio ilimuingiza Anne kwenye mashindano hayo mwaka 1977 na kwa sasa amestaafu kushiriki mashindano hayo.

Mashindano hayo yalianzishwa mwaka 1267 nchini Uingereza na hufanyika kila mwaka mwezi September huko Egremont,Cumbria nchini Uingereza.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?

Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.

Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME,

Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Amenisomesha, Kaninunulia Gari Lakini Sina Mapenzi Naye..Nifanyeje?

$
0
0

Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 28 Naishi Tabata jijini Dar nimejitokeza kwenu kuomba ushauri, Mimi na mpenzi wangu ambae amenisomesha toka form one hadi sasa nipo chuo kwani wazazi wangu walifariki wakati mimi nikiwa mtoto mdogo sana.

Sasa huyu mpenzi wangu amenigharamia sana yani kuanzia nguo zote hadi chakula nacho kula vyote ni msaada wake yeye na amejitolea kuninunulia gari la kutembelea na kanambia nitafute kiwanja ili tujenge nyumba ya kupangisha.

Ila mimi kwa sasa naona kama huyu mwanaume hatuendani kwani yeye hana elimu ila anafanya kazi kutumia akili ya kuzaliwa, Jamani mimi nataka kuishi na msomi mwenzangu ila huyu kaka mimi naona kama freemasson kwani kanisaidia sana asije akanitoa kafala, Mimi kwa sasa nimepata mpenzi mpya ambae anaelimu ya chuo sio mshamba kama huyu wa zamani.

Sasa please naombeni ushauri wenu jamani nimwambiaje kama sipo tayari kuishi na yeye huyu mpenzi wa zamani bila kuumiza moyo wake...?

Sijamaliza Ashasinzia au Ndo Nina Kibamia

$
0
0
Wakuu swali,

Nina msichana wangu nimekaa naye miaka miwili sasa, mwanzoni ilikuwa ngumu sana kufika kule kunako wakati wa ku do, nikajitahidi sana kuongeza maufundi sasa hali imebadilika sijamaliza ashamaliza na kusinzia kabisa usingizi wakati bado niko juu yake nashughulika.

yaani huwa inakuwa like nina do mtu ambaye hayuko duniani hadi baadaye kabisa baada ya nusu saa hivi ndo anashtuka, swali langu ni hiyo ni kawaida au ana shida manake ni mda hajaniona nikimaliza kwani alikwisha sinzia au ndo nina kibamia akimgusi kunako?

Dunia Kusimama kwa Dakika 90 Kuiona Real Madrid vs Liverpool hii leo

$
0
0
Real Madrid vs Liverpool hatimaye siku imefika, hii ni fainali ya 16 kwa Real Madrid maarufu kama Los Blancos katika michuano ya barani Ulaya, na hakuna klabu ambayo imewafikia wababe hawa wa Madrid katika rekodi hii.

Wakati Real Madrid wakiwa na rekodi hiyo, wapinzani wao siku ya leo Liverpool wenyewe wamekwenda fainali za barani Ulaya mara 7 na ni ya 8 na ndio klabu ya nchini Uingereza ambayo imekwenda fainali za Ulaya mara nyingi zaidi.

Ukiacha mwaka 1962 ambapo Real Madrid walifungwa na Benfica katika fainali hizi, 1964 walipofungwa na Inter Milan na 1981 walipofungwa na Liverpool, fainali zingine zote 12 zilizobaki Real Madrid waliibuka kidedea.

Wakati Real Madrid wenyewe wamepoteza katika fainali 3 kati ya fainali 15 ambazo wameshacheza, majogoo wa London Liverpool wenyewe wamepoteza fainali 2/7, Liverpool walipigwa na Juventus 1985 na wakafungwa na Ac Milan mwaka 2007.

Hii ya leo ni fainali ya tatu mfululizo kwa Real Madrid kucheza katika Champions League, lakini Real Madrid sio wa kwanza kufanya hivi kwani mwaka 1996-1998 klabu ya Juventus ya nchini Italia nao walifika fainali mara 3 mfululizo za Champions League.

Tangu Liverpool wawafunge Real Madrid katika fainali za UEFA mwaka 1981 Los Blancos hawajawahi kupoteza katika fainali sita zilizofuatia za michuano ya Champions League walishinda 1998, 2000, 2002, 2014, 2016 na 2017.

Tangu baada ya Liverpool kuifunga mabao 5-4 Alaves katika michuano ya UEFA Cup mwaka 2001, timu za kutoka nchini Hispania hazijawahi kupoteza fainali hata moja ya michuano mikubwa Ulaya dhidi ya timu za kutoka Uingereza.

Wakati karibia kikosi chote cha Real Madrid hii leo wamewahi kushiriki fainali ya Champions League, hali ni tofauti kwa Liverpool kwani kikosi chao kizima hii leo hakuna mchezaji aliyewahi kucheza fainali hizi.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images