Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Kikao cha Mazishi ya Maria na Consolata Kinafanyika

0
0
Kikao cha Mazishi ya Maria na Consolata Kinafanyika
Kikao baina ya Serikali, Kanisa la Roman Katoliki na Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Ruaha (Ruco) bado kinaendelea ili kupata muafaka wapi mazishi ya mapacha walioungana Maria na Consolata yatafanyika.

Hadi leo Juni 4, saa nne asubuhi bado hakuna ratiba wala mahali ambako msiba huo umewekwa.

Akizungumza na Mwananchi kaimu mkuu wa mkoa wa Iringa Richard Kasesela amesema taratibu zote zitawekwa hadharani baada ya kumalizika kikao hicho kinachofanyika Kanisa Katoliki, Jimbo la Iringa.

"Bado kikao kinaendelea, taratibu zote zitawekwa wazi tukishakubaliana," amesema.

Mapacha hao walifariki Juni 2, 2018 wakati wakiendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Iringa baada ya kurejeshwa toka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam.

Utility

1996-Mwaka waliozaliwa

2018-Wamefariki

Udzungwa Sekondari- Elimu ya Kidato cha tano na sita

Gari za Mwendokasi Zapata Hitilafu Katika Mfumo wa Tiketi Abiria Wasafiri Bure

0
0
Gari za Mwendokasi Zapata Hitilafu Katika Mfumo wa Tiketi Abiria Wasafiri Bure
Leo imekuwa ni asubuhi njema kwa abiria wa mabasi yaendayo haraka (Udart), baada ya kupanda usafiri huo bure.

Abiria wa mabasi hayo, wamejikuta wakipanda bure kutokana na kudaiwa kuwepo kwa hitilafu katika mfumo wa tiketi.

Madirisha ya vyumba vinavyotumika kukatia tiketi yalikuwa yamefungwa huku mabasi yakiendelea kubeba abiria kama kawaida.

Abiria wengi walionekana kufurahia kusafiri bure, hata hivyo baadhi ya wanaotumia kadi wamejikuta wakilipia usafiri huo kwa kuwa wanatumia mashine maalum za kugonga.

"Kumbe ni bure, sikujua inaniuma kama nikadai vile,"amesema abiria mmoja baada ya kugonga kadi yake.

Alipoulizwa kuhusu hali hiyo, ofisa mawasiliano wa Udart, Deus Buganywa amesema atatoa taarifa kwa vyombo vya habari baadaye.

Abiria mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Daudi Joshua amesema kupanda usafiri bure kumemfurahisha kwa kuwa anaona ni fidia ya usumbufu wa kusubiri magari hayo kwa muda mrefu.

"Huduma ya usafiri huu haitabiriki, tumekuwa tukipata usumbufu mkubwa, sasa leo sijui wanatoa ofa kusafisha makosa yao," amesema Joshua, mkazi wa  Luguruni Mbezi.

Mwananchi ilishuhudia wafanyakazi wa Udart wakiwa wamesimama vikundi wakijadiliana.

Tangu jana asubuhi, huduma za usafiri huo ziliendelea bila wananchi kukata tiketi.

Zari, Daimond Kimeeleweka.... Babu Tale Afanya Kweli SA

0
0
Zari, Daimond Kimeeleweka.... Babu Tale Afanya Kweli SA
KIMEELEWEKA asilimia 90! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya meneja wa msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Hamis Taletale ‘Babu Tale’ kutua pande za Afrika Kusini kwa lengo la kusaka suluhu ya msanii wake huyo na mama watoto wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.

KWA NINI ASILIMIA 90?

Kwa wafuatiliaji wa magazeti Pendwa, hakuna asiyejua kuwa familia inayomzunguka Diamond inavyomkubali Zari kuliko mwanamke mwingine yeyote hivyo kilichokuwa kimebaki ni mtu tu anayeheshimika na Zari kwenda kumuombea radhi Diamond.

“Sisi wote tulikuwa tunaomba tu mtu kama Babu Tale (Hamis Taletale) aamue kujitoa kwenda maana Zari licha ya kuwa na msimamo, anamheshimu sana Tale na ndiyo maana alivyoamua tu kwenda, tuna uhakika asilimia 90, Zari anarudi Madale,” mmoja wa wanafamilia ya Diamond aliling’ata sikio Ijumaa Wikienda.

AZIDI KUSHUSHA UBUYU

Mwanafamilia huyo alienda mbali zaidi kwa kusema kuwa kitendo cha Tale kutua Sauz ni kwenda kumaliza biashara kwani, kama familia, wote walikuwa wanamhitaji Zari na walikuwa wakimchombeza kila uchwao.

“Wewe angalia mama Diamond kila siku anawasiliana na Zari, Zari anamtumia picha za watoto kila wakati. Anamuweka karibu kiasi kwamba Diamond mwenyewe na ubishi wake anakuwa mpole,” alisema mwanafamilia huyo.

IYENA IMECHOCHEA MOTO ‘Fujo’ za kumrejesha Zari Madale zilichochewa zaidi na picha mpya za Zari na Diamond zilizovuja Ijumaa iliyopita mara baada ya msanii huyo kuachia wimbo wake mpya uitwao Iyena.


Katika picha hizo za ‘behind the scene’ ya wimbo huo, Zari alionekana alishaini kwa raha zake katika mavazi yanayoashiria si tu kwamba ni mzazi mwenzake bali ni mke halali wa ndoa wa Diamond.

FAMILIA YAZIDI KUVUTIWA Mara baada ya picha hizo kusambaa, mwanafamilia ya Diamond aliyezungumza na Ijumaa Wikienda, alisema picha hizo ziliongeza kasi ya kampeni ya kumrudisha Zari katika familia yao kwa kuvutiwa na muonekano wao.

“Kila mtu akasema yes, huyu ndiye mke halali wa Diamond na si mwingine yeyote,” alisema mwanafamilia huyo na kuongeza: “Yaani kwa sasa mama Diamond, Esma na sisi wote tunamsubiri kwa hamu maana Tale kwenda kule tunajua ni uhakika.”

MITANDAO YASHADADIA

Mbali na familia, baada ya kuvuja kwa picha hizo, mitandaoni kulichafuka ambapo watu mbalimbali walitupia maneno wakiiunga mkono kurudi kwa penzi la Diamond na Zari huku wakimrushia madongo makali Hamisa Mobeto, mrembo aliyechepuka na Diamond kisha kuzalishwa mtoto mmoja.

MSIKIE MAMA D

Katika harakati za kukushibisha ubuyu huu wa motomoto, Ijumaa Wikienda lilimtafuta mama mzazi wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ ambapo yeye alijikita zaidi kumsifia Zari kuwa ndiye mama Madale, na kitu kinachomvutia kwake ni mwanamke ambaye anajua jinsi gani anaweza kumjali mumewe kwa kila kitu na mambo mengi ya usafi wa ndani.

“Ninachojua mpaka sasa Zari ndiye mama mjengo, anajua jinsi gani ya kumfanya mume akajisikia yuko na mke na kwa upande wa kuweka nyumba poa huyu mwanamke ni hatari halafu kingine ananikosha kuhusu wajukuu zangu,” alisema mama huyo.

ESMA SASA…

Kwa upande wa dada wa mwanamuziki huyo Esma Khan ‘Esma Platnumz’, alisema kuwa Madale iko wazi na wanamkaribisha Zari, kwani kwa kipindi ambacho alikuwa hayupo, wametambua umuhimu wake.

“Jamani Zari ni mwanamke sijui hata nisemeje kwa sababu kwanza anajua kuweka nyumba safi mpaka ukiingia ndani unakubali kila kitu, kingine tunamkumbuka sana na umuhimu wake sasa unaonekana yeye aje tu Madale inamsubiri,” alisema Esma.


TUJIUNGE NA TALE

Tale alipotafutwa na Ijumaa Wikienda ili aweze kuweka bayana mafanikio ya safari yake hiyo aliyoifanya mwishoni mwa wiki iliyopita, alisema kama mtu ambaye Zari anamheshimu, hakuna kitakachoshindikana.

“Kwangu ni kazi ndogo sana kuyarudisha mapenzi ya Zari na Diamond na kwa vile mashabiki wote walikuwa wakinilaumu mimi nimeshindwa kuweka mambo sawa lakini naamini kabisa familia hiyo itarudi kama zamani,” alisema Tale.

MOBETO KAMA ULIVYOSIKIA

Baada ya kusikia familia ya Diamond imeweka msimamo wake kuhusu kumhitaji Zari arudi Madale, Mobeto alitupia ujumbe mzito kwenye ukurasa wa Diamond Instagram alipoweka picha na kuhoji mahojiano (ya kumponda Mobeto kuwa ni mchafu), aliyoyafanya dada yake Esma alikuwa mzima au alikunywa ndipo Mobeto alipolipuka na kumtaka mwanamuziki huyo aoe mke anayehitajika na familia hiyo.

“Inabidi umuoe mwanamke ambaye anatakiwa na ndugu zako…na mameneja zako bila kusahau mashabiki… siyo kutwa miye mtoto wa watu naandamwa na kukaliwa miye kooni.

Sijakuita wala kukufunga kamba…kila siku maneno kwani alishindwa kukufata kukushauri mpaka akimbilie kwenye Matv na mitandao? Unapokaa hapajui? Namba ya simu pia hana? Kwani miye hayo Matv hayaombi kunihoji mbona nakaa kimya? Tena saa ingine (nyingine) nakaa kimya kuwasitiri kwa mengi na pia @ deedaylan (mwanaye) akikua asione hii migogoro lakini ndugu zako hawabebeki its too much, talk to your familia maana wewe ni mwanaume na una uwezo wa kuyamaliza…na pia uwaambie unahitaji mke na siyo house girl wa nyumba…” alitoa povu Mobeto.

TUMEFIKAJE HAPA?

Februari 14, mwaka huu, Zari alitangaza kumpiga chini Diamond kwa kile alichosema kuwa staa huyo amezidi ‘mambo mengi’ hivyo ameamua kujiweka pembeni kuepusha msongamano kama si maradhi.

Licha ya Diamond kuonesha kukubaliana na matokeo, familia yake imekuwa ikijitahidi kurudisha uhusiano huo kwa nguvu huku ikielezwa kuwa Diamond amekuwa akijishusha na kuomba radhi lakini alipozungumza na gazeti hili wiki iliyopita, alikanusha taarifa hizo.

Polepole Awasikitikia Mbowe, Zitto Kabwe "Mmeanza Siasa Msibani CCM Tunasema Wembe ni Ule Ule''

0
0
Polepole Awasikitikia Mbowe, Zitto Kabwe "Mmeanza Siasa Msibani CCM Tunasema Wembe ni Ule Ule''
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Ndg. Humphrey Polepole ameonyesha Vongozi wa vyama vya Upinzani nchini, Mbowe pamoja na Zitto Kabwe baada ya kukubaliana kushirikiana kumpata Mbunge jimbo la Buyungu lililoachwa wazi na Mwl. Kasuku Bilago kwa kuwaambia wembe wa CCM ni ule ule.


Polepole amesema hayo ikiwa zimepita siku kadhaa baada ya mazishi ya Mwl. Kasuku Bilago kuzikwa huko Kakonko mkoani Geita baada ya kuugua kwa muda mfupi na kisha kwenda kuzikwa huko kijijini kwao.

Polepole amesema kuwa "Nimesikia jamaa palepale msibani walianza kugawana ubunge na kuanza kujihadaa, ni bahati mbaya sana. Utamaduni wa kiafrika ni kumaliza msiba ambapo lengo ni kufariji wafiwa".

Ameongeza kuwa "Nimekaa Kakonko kwa muda wa kutosha, kwakuwa mmeanza siasa msibani, CCM tunasema wembe ni uleule".

Wakiwa kwenye mazishi ya Mwalimu Bilago ambaye alikuwa Mbunge kupitia CHADEMA, Zitto Kabwe pamoja na Mbiowe walikubaliana kuweka umoja ambao utamsimamisha mgombea mmoja anayekubalika kutoka upinzani na kuhakikishia wanampigani hadi anashinda ili kumuenzi mwalimu Bilago.

Bunge Latoa Rambirambi Vifo vya Pacha Maria na Consolata

0
0
Bunge Latoa Rambirambi Vifo vya Pacha Maria na Consolata
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema Bunge limepokea kwa masikitiko makubwa vifo vya pacha Maria na Consolata.

Akitoa salamu hizo za rambirambi leo bungeni Juni 4, 2018, Spika Ndugai amemwomba Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako kufikisha salamu kwa ndugu, jamaa na marafiki.

Huku ukumbi wa Bunge ukiwa kimya kumsikiliza akitoa salamu hizo, Spika Ndugai amesema:  “Kwa niaba ya Bunge nitoe salamu za rambirambi kifo cha Maria na Consolata.”

“Walikuwa ni watoto wa ajabu na wenye upendo. Kifo chao kimetupa masikitiko makubwa sana. Waziri wa Elimu (Profesa Ndalichako) tufikishie salamu huko,” ameongeza

Diamond Platnumz: Mwanamke Sura Kwanza.... Tabia Baadae

0
0
Diamond Platnumz: Mwanamke Sura Kwanza.... Tabia Baadae
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amesema kuwa yeye kigezo kikubwa anachotumia kumpata mwanamke mwema wa kuoa ni kuangalia sura na sio tabia kama wengi wanavyosema.

Diamond akitetea msimamo wake kwenye kipindi cha Kaa Hapa kinachorushwa TBC 1, amesema kuwa mwanamke huwezi kumbadilisha sura kwa namna yoyote ile lakini tabia ni rahisi kumbadilisha.

Akielezea kuhusu kigezo hicho, Diamond amesema kama angetoa asilimia kwa vigezo vya sura na tabia basi asilimia 70 angetoa kwa upande wa sura na asilimia 30 zilizobaki ndio angeangalia tabia.

“Kiukweli tabia tunapenda lakini wakati mwingine sura nazo zina uzito wake, Kiukweli tabia mnaweza kuelekezana ila sura kuelekezwa mtaelekezana vipi?. Tabia tunajifunza kama alijifunza kuchukia atajifunza kupenda, sura atajifunza vipi?, Kwa mwanamke mimi naangalia sura kwanza , tabia tutaelekezana.“amesema Diamond Platnumz.

Hata hivyo, kupitia kipindi hicho Diamond Platnumz amefunguka kuhusu zile picha za faragha zilizovuja akiwa na Hamissa Mobetto kwa kusema kuwa walikuwa location wakirekodi kipindi cha TV.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGESA

Mke wa Bilionea Erasto Msuya Ataka Iundwe Tume Kuchunguza Kesi Yake

0
0
Mke wa Bilionea Erasto Msuya ataka iundwe Tume kuchunguza kesi yake
Mke wa marehemu Bilionea, Erasto Msuya, Miriam Mrita ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa iundwe tume ya kuichunguza kesi ya mauaji inayomkabili kwa sababu kuna uonevu unaendelea.

Miriam amewasilisha ombi hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba mara baada ya wakili wa serikali, Patrick Mwita kudai kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa, jalada halisi lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Baada kueleza hayo, Miriam alinyoosha mkono ambapo hakimu Simba alimruhusu kuongea.

Miriam alisimama na kuiambia mahakama kuwa huu ni mwaka wa pili sasa wanaendelea kusota mahabusu.

“Mimi ni mama mjane, mume wangu ameuawa, mimi nipo mahabusu gerezani kwa miaka miwili, kama mama sijui watoto wangu wanaendeĺeaje huko nje.” alionge Miriam.

Aliongeza kuwa amechoshwa na wimbo wa upande wa mashtaka kuwa upelelezi bado haujakamilika.

“Mtu ukishafiwa na mume kuna vurugu mechi zinaendelea huko nje, naomba iundwe tume ya uchunguzi wa kina ya kuichunguza kesi hii kwa sababu kuna uonevu ambao unaendelea.”alieleza Miriam.

Katika kesi hiyo namba 5 ya 2017 mbali na Miriam mwingine anayekabiliwa na kesi hiyo ni Revocatus Muyela.

Kwa pamoja washtakiwa hao, wanadaiwa kumuua kwa makusudi Dada wa marehemu Bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya May 25,2016 huko Kibada Kigamboni Jijini Dar es Salaam.

Msemaji wa Rais Magufuli, Kuchukuliwa Hatua

0
0
Msemaji wa Rais Magufuli, kuchukuliwa hatua
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kinalaani na kupinga ukiukwaji wa Katiba, Sheria na Kanuni mbalimbali zilizofanywa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Gerson Msigwa Mnamo Mei 21 na 25 mwaka huu kwa kujihusisha na shughuli za chama jambo ambalo ni kinyume na taratibu -

hivyo kama chama watachukua hatua dhidi yake

Hayo yamewekwa bayana na taarifu zilizotolewa na Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje- CHADEMA, John Mrema mchana wa leo Juni 04, 2018 baada ya kupita siku kadhaa tokea kulipomalizika vikao vya Halmashauri Kuu Taifa ya CCM vilivyofanyikia ndani ya kumbi za mikutano zilizopo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

"Tarehe 21 Mei, 2018 ilitolewa taarifa ya Ofisi ya Rais Ikulu ikiwa imesainiwa na Gerson Msigwa kuhusu tukio la Mwenyekiti wa CCM Taifa, John Pombe Magufuli kupokea taarifa ya ukaguzi wa mali za CCM katika Makao Makuu ya Chama hicho Lumumba Jijini Dar es Salaam.

Kwa mara nyingine tena tarehe 25 Mei, 2018 Msigwa kwa kujua au kutojua au kwa kiburi cha malamka alitoa taarifa kwa vyombo vya habari kwa nafasi yake kama Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu kuhusu uteuzi wa Wajumbe wawili wa Halmashauri Kuu ya CCM uliofanywa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa John Pombe Magufuli", amesema Mrema.

Aidha, Mrema amesema kwa mujibu wa Katiba ya nchi Ibara ya 3(1) imetamka wazi kuwa Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya demokrasia na ni nchi ya mfumo wa vyama vingi vya siasa huku Kanuni maadili ya vyama vya siasa za mwaka 2007, Kanuni ya 5(1) inakataza chama chochote cha siasa kutumia mamlaka, rasilimali za serikali kwa kujinufaisha kisiasa.

"Gerson Msigwa kama Mtumishi wa Umma mwenye wadhfa wa Mkurugenzi kwa mujibu wa kifungu cha 4 cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995 anatakiwa na anapaswa kuzingatia masharti ya Viongozi wa umma. Kifungu cha 21 cha sheria hiyo kinakataza kiongozi wa umma kutumia mali za serikali isivyoruhusiwa..

Kwa kuwa Msigwa ameendelea kunukuliwa akisisitiza kuwa yeye ni Msemaji wa Rais na ambaye ni Mwenyekiti wa CCM huku akijua kufanya hivyo ni kukiuka masharti kama tulivyoeleza, sisi kama Chama cha siasa tutachukua hatua kwa hilo", amesisitiza Mrema.

Pamoja na hayo, Mrema ameendelea kwa kusema "tunamtaka Msajili wa Vyama vya Siasa kutumia mamlaka yake kupitia Kanuni ya 6(1)(d) ya Kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa kutoa tamko dhidi ya ukiukwaji wa Kanuni hizo uliofanywa na CCM kwa kutumia mali za umma kwa maslahi yao ya kisiasa. Msajili akishindwa kufanya hivyo tutawasilisha malalamiko rasmi kwake kwa mujibu wa Kanuni ya 6(1)(a) kuhusu ukiukwaji huo.

Tunamtaka Katibu Mkuu Kiongozi au Tume ya Utumishi wa Umma kama mamlaka za nidhamu kumchukulia hatua Gerson Msigwa kwa kukiuka masharti ya Utumishi wa Umma kwa kufanya siasa wakati wa masaa ya kazi na pia kujipa nafasi ya kuwa Msemaji wa CCM huku akijua Chama hicho kina Msemaji wake".

Kwa upande mwingine, Mrema amesema endapo hayo yote hayatofanywa na mamlaka husika zilizotajwa basi wao watachukua hatua zaidi juu ya jambo hilo ambalo linatendwa kinyuma na taratibu.

Young Dee Afunguka Mpango wa Kumsaini Young Killer

0
0
Young Dee Afunguka Mpango wa Kumsaini Young Killer
Msanii wa muziki wa hip hip, Young Dee amefunguka kuzungumzia post ambayo aliiweka mitandaoni inayohusiana na kutaka kumsaini rapa Young Killer Msodoki ambaye kwa sasa anafanya kazi chini ya label ya Wanene Entertainment.

Dee ambaye kwasasa anafanya kazi na label ya King Cash, kupitia instagram aliandika “Hahaha siku ya kwanza ofisini wakati nataka kumsign mdogo wangu #youngkillermsodokii 😀😀 ni kweli anachana sana kijana ana kipaji!,”

Baada ya kauli hiyo Bongo5 ilimtafuta na kuzungumza naye kuhusiana na kauli ambapo alidai hakuna kitu ambacho kinashindikana kwenye hii dunia.

“Young Killer ni rapa mzuri sana, namkubali sana lakini ishu za kumsaini ni mapema sana pale niliandika kama masihara lakini mimi nadhani ni jambo ambalo linawezekana kama nikiamua kwa sasabu ana kila kitu,” alisema Young Dee.

Young Dee na Young Killer wote kwa pamoja watashiriki katika tamasha kubwa la muziki la Sports Muziki Festival linalotarajiwa kufanyika Mwanza, Geita na Kahama katika ya mwezi huu.

Ommy Dimpozi Akoshwa na Nyimbo Hizi Kutoka WCB

0
0
Ommy Dimpozi Akoshwa na Nyimbo Hizi Kutoka WCB
Msanii wa muziki Bongo, Ommy Dimpoz ametaja nyimbo mbili kutoka label ya WCB ambazo anaona zinafanya vizuri.

Mumbaji huyo anayetamba na ngoma ‘Wanje’ ametaja ngoma ngoma hizo kuwa ni Kwa Ngwaru ya Harmonize na Pochi Nene ya Rayvanny.

“Moja wapo ni hiyo kama unavyosema Kwa Ngwaru ni wimbo ambao unafanya vizuri, yeah!, kuna mwingine nimesikia wa Rayvanny Pochi Nene, kwa hiyo kwa currently ni nyimbo ambazo naweza kusema zinafanya vizuri,” Dimpoz ameiambia Citizen Radio.

Katika hatua nyingine amefunguka ni lini hasa bifu lake na Diamond litaisha kwa kusema; “Kila jambo lina wakati wake kwa hiyo time itakapofika mambo yote yatakaa sawa, tuombe Mungu’.

Rais Magufuli Asema Haridhishwi na Uendeshaji Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB)

0
0
Rais Magufuli Asema Haridhishwi na Uendeshaji Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB)
Rais John Magufuli amesema haridhishwi na utendaji kazi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) , kutokana na kushindwa kutoa mikopo kwa wakulima hali inayosababisha sekta ya kilimo kusuasua.

Rais Magufuli amesema hayo leo Juni 4, jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa Programu ya kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP2), uliofanyika.

“Sijaridhishwa na utendaji kazi wa Benki ya Kilimo, utoaji wa mikopo kwa wakulima umekuwa wa kusuasua badala yake wamejikita katika kufanya biashara na benki nyingine.

“Nawasihi mbadilishe mwelekeo na kupunguza gharama za uendeshaji ili wakulima anufaike.

“Wakati mwingine Benki ya Kilimo ikitaka kukopesha inawatafuta matajiri wakubwa sasa nikisema siridhiki na utendaji wa benki hii mtanikatalia, kwani nimesikia pia mmekuwa mahodari katika kupeana mikopo wenyewe kwa wenyewe,” amesema Rais Magufuli

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewataka mabalozi walioko nje ya nchi kufahamu kuwa moja ya majukumu yao ni kutafuta masoko kwa ajili ya mazao yanayopatikana nchini.

TFF Yafuata Nyayo za FIFA

0
0
TFF Yafuata Nyayo za FIFA
Shirikisho la soka nchini (TFF), limefuata utaratibu ambao Shirikisho la soka la Kimataifa (FIFA), hutumia ili kusikiliza vyama wanachama wa shirikisho hilo kupata maoni kwaajili ya kuboresha utendaji kazi kwa maendeleo ya soka.


Kamati ya Utendaji ya TFF, ambayo ilikuwa jijini Arusha kwaajili ya fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho (ASFC), imefanya kongamano kubwa la (TFF Executive Football Summit 2018) lililowakutanisha viongozi wa soka kutoka mikoa 6 nchini.

Kongamano hilo lililoongozwa na Rais wa TFF Wallace Karia jana Juni 3, Mkoani Arusha, limejadili mambo mbalimbali ikiwemo kuboresha miundo mbinu ya michezo pamoja na vyama vya mikoa kuwekeza nguvu kwenye soka la vijana.

Wajumbe waliohudhuria 'TFF Executive Football Summit 2018', ni kutoka mikoa ya Singida, Dodoma, Manyara, Kilimanjaro, Tanga na wenyeji ambao ni Mkoa wa Arusha.

Mapema Mwaka huu FIFA ilifanya Kongamano kubwa kwa nchini wanachama zaidi ya 17 barani Africa na lilifanyika jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na Rais wa FIFA Gianni Infantino pamoja na Rais wa CAF Ahmed Ahmed.

Maria na Consolata Kuzikwa Mkoani Iringa Jumatano

0
0
Maria na Consolata Kuzikwa Jumatano Mkoani Iringa
Pacha walioungana Maria na Consolata wanatarajiwa kuzikwa Jumatano katika makaburi ya viongozi wa dini ya Roman Katoliki, Tosamaganga Mkoani Iringa.

Pacha hao wanaandaliwa jeneza moja lenye mfumo wa watu wawili huku misalaba ikiwa miwili na kaburi moja.

Akizungumzia ratiba ya maziko ya pacha hao, leo Juni 4, Muwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Richard Kasesela alisema wapo katika hatua za mwisho za maandalizi ya mazishi hayo.

Amesema ibada ya kuaga mapacha hao itafanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha  Ruaha (Rucu) kuanzia saa mbili asubuhi kabla ya safari ya Tosamaga kwa ajili ya mazishi.

"Taratibu zinaendelea na tumekubaliana kutengeneza jeneza moja lenye mfumo wa watu wawili, tutakuwa na misalaba miwil lakini watazikwa kaburi moja," amesema.

Kasesela amesema kuwa tayari ndugu wa pacha hao kwa pande zote mbili wamewasili na kwamba saa kumi jioni watakutana tena kupanga bajeti ya msiba.

Simba Kweli Vidume...Watinga Nusu Fainali Kenya

0
0

Timu ya Simba imefanikiwa kutinga hatua ya Nusu Fainali ya Michuano ya SportpesaSuperCup baada ya kuifunga Timu ga Kariobangi Sharks kwa Penati 3-2.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo na Mafupi ya Kiume na Hawana Nguvu ?

0
0

KWA NINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MADOGO NA MAFUPI YA KIUME NA HAWANA NGUVU ZA KIUME NINI HUCHANGIA?

🌸 kama una Ngiri, au umejichua kwa muda mrefu, punyeto, una stres nyingi Sana, lishe duni, kisukari, presha, kutopata choo vizuri, tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu, kaswende, gono,haya yote husababisha kuwa na maumbile madogo na mafupi ya kiume na kukosa nguvu za kiume.MATIBABU

🌸tumia dawa ya asili itwayo (MASUNZU POWER MIX) inatibu tatizo la nguvu za kiume maradufu inatibu uume mdogo na mfupi na kuimalisha mishipa iliyolegea inarefusha Nchi(4-8) na kunenepesha maumbile na upana (cm3-4) dawa hii haina madhala hata kwa wazee walio na umri wa miaka (70-85) pia inaongea hamu ya kufanya tendo la ndoa Mara (3-5) bila hamu kuisha dawa hii inatibu siku 6 na kupona kabisa

🌸MASUNZU POWER MIX. ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo kunyoosha mishipa ya askari aliyesinyaa kutokana na kujichua kwa muda mrefu au Ngiri, nk 🌸pia tuna dawa ya kutibu busha bila opresheni

🌸 SOSOMA DX ni dawa ya kumvuta mme au mke mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyoanza mwanzo baada ya Masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba

🌸GINDU EXTRA ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda 350 itashuka haraka tunatibu presha, vidonda vya tumbo nk:

🌸 OFISI IPO DAR ES SALAAM BUGURUNI CHAMA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO AU SIMU 0673552294 / +255784552299 TABIBU ATHUMAN.

Shabiki wa Chelsea Akubali Kuishabikia Manchester UTD ili Aongezewe Damu

0
0
Shabiki wa Chelsea Akubali Kuishabikia Manchester UTD ili Aongezewe Damu
Leo June 4, 2018 nakusogezea stori toka nchini Uingereza ambapo shabiki mmoja wa Chelsea aliyekuwa akihitaji kuongezewa damu amejikuta akibadili timu ya kushabikia baada ya kupewa sharti la kuanza kuishabikia Manchester United ili apewe damu hiyo na kaka yake.

Martin Warbuton ambaye ni shabiki ndakindaki wa mashetani wekundu alimpa sharti ndugu yake Paul ambaye ni mshabiki wa Chelsea la kuhama timu ya kushabikia huku wakitia saini kabisa ili mmojawapo asije akamgeuka mwenzake.

Paul aligundulika kuwa ana kansa ya damu hivyo alihitaji damu hiyo ya ndugu yake kusaidia kutatua tatizo lake la afya.

Aidha ndugu hao kwa miaka mingi wamekuwa wakibishana kuhusiana na timu wanazoshabikia huku kila mmoja akiona timu yake ni nzuri zaidi ya mwenzake na ndio maana Martin aliamua kumfanyia ndugu yake huyo ili kumaliza ubishi wa nani anashabikia timu bora.

Kuna Baadhi ya Makundi Hayapewi Nafasi Kwenye Media – Roma

0
0
Kuna Baadhi ya Makundi Hayapewi Nafasi Kwenye Media – Roma
Msanii wa muziki Bongo, Roma amesema sababu ya baadhi ya wasanii wakongwe kutopenda kuitwa hivyo ni kutokana na kutopewa nafasi katika vyombo vya habari na kuonekana wakati wao umepita.

Roma katika mahojiano na FNL ya EATV ameeleza kutokana na hilo wasanii hao wana haki ya kukataa kuitwa wakongwe.

“Unafikiri ishu ni ukongwe, wala si hivyo, ishu ni kuna baadhi ya makundi hayapewi nafasi kwenye media house, mchongo ndio upo hapo, hizo nyingine zote mchongoma tu,” amesema.

“Snoop Dog ni mzee anafanya mchongo na Wiz Khalifa, kwanini Mox asifanye mchongo na Country Boy halafu ukawa kweli mchongo lakini sisi tunakuja kuitafsiri mkongwe hana nafasi kwenye generation ya sasa hivi which is total wrong,” ameongeza.

Ameendelea kwa kusema ikiwa msanii ataitwa mkongwe lakini anapata kile ambacho anastahili wala hakuna ambaye angelaumu ila kwa namna inavyotafsiriwa na watu wa vyombo vya habari sivyo.

Rais Magufuli Awataka Mabalozi Wake Kutafuta Masoko

0
0
Rais Magufuli Awataka Mabalozi Wake Kutafuta Masoko
Rais John Pombe Magufuli amewataka mabalozi wa Tanzania nje ya nchi kuhakikisha wanatafuta masoko ya mazao ya kilimo katika nchi wanazoziwakilisha.


Rais Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizindua Program ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

"Moja ya jukumu kubwa la mabalozi wetu huko waliko ni kutafuta fursa zitazoisaidia Tanzania kukua kiuchumi, na hili la kutafuta masoko ya mazao pia linawahusu." Magufuli.

Katika uzinduzi huo Rais Magufuli amewaonya wale wanaorudisha nyuma sekta ya kilimo na kuwataka viongozi wenye dhamana ya kuhakikisha kilimo kinawakomboa wananchi wawe wabunifu katika kuhakikisha wakulima wananufaika na kilimo, uvuvi na ufugaji.

Aidha amesema, ukosefu wa masoko wa bidhaa zinazozalishwa nchini, unarudisha nyuma maendeleo na kueleza kushangazwa kwake na uwepo wa tozo nyingi zinazosababishwa na Bodi ambazo hazina msaada wa moja kwa moja kwa wakulima.

Pamoja na hayo Rais Magufuli amewashukuru wadau wa maendeleo wakiwemo wabia wa maendeleo wa kimataifa kwa kufanikisha mradi huo, na kusisitiza kuwa iwapo kila mdau atasimamia jukumu lake kwa uadilifu na kujituma, Tanzania ya Uchumi wa kati ifikapo 2025 litafanikiwa.

Programu hii iliyozinduliwa leo ni ya miaka mitano na itagharimu shilingi trilioni 13.8.

Uwoya Afunguka Ishu ya Kuifuta Tatuu ya Masogange

0
0
Uwoya afunguka Ishu ya kuifuta Tatuu ya Masogange
MKALI wa sinema za Kibongo, Irene Uwoya ameeleza juu ya madai ya watu wanaosema kuwa ameifuta tatuu ya aliyekuwa video queen maarufu Bongo, marehemu Agness Gerald ‘Masogange’ na kusema kuwa ni kitu gani kinachoweza kumfanya aifute tatuu hiyo?

Uwoya aliiambia Over Ze Weekend kuwa, aliichora tatuu hiyo kwa kuwa ni jambo lililotoka moyoni mwake na lilitokana na uchungu aliokuwa nao wa kupitiliza kwa rafiki yake huyo hivyo hawezi kuifuta.

“Nitaanzaje kuifuta? Ni kitu ambacho nime-kichora mwen-yewe, tena cha kumbukumbu muhi-mu kwenye maisha yangu, jamani itaendelea kudumu kwenye mkono wangu daima,” alisema Uwoya ikiwa ni zaidi ya siku 40 tangu Masogange afariki dunia.

Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images