Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Masau Bwire Awaandikia Waraka Mzito Singida United

0
0
Masau Bwire Awaandikia Waraka Mzito Singida United
Ofisa habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire ameandika waraka akiizungumzia Singida United na kutaja chanzo cha timu hiyo kukosa mataji katika msimu uliomalizika wa 2017/18 ni aliyekuwa kocha wake Hans Pluijm.


Msemaji huyo ameandika waraka uliionesha masikitiko yake kwa klabu ya singida united kwa kile alichodai ina pesa za kutosha hawana shida kama vilabu vingine lakini imekuwa na matokeo ya kawaida sana msimu huu.

“Sikutarajia kabisa kwamba, Singida United watasumbuliwa kiasi cha kufungwa na timu kama Lipuli, Prisons, wapapaswe na wapapasaji, na wengineo wenye usajili wa kawaida, ambao hawana hakika kesho kutakuchaje, jasho lao kufutwa mpaka wapige kelele kama vyula wakati wa mvua huku wamejificha matopeni,tafakarini, mpatengeneze mlipopaharibu ili msimu ujao hali yenu iendane na hadhi yenu”, ameandika Massau Bwire.

Bwire ameongeza kuwa “Kumaliza ligi nafasi ya tano, kupigwa 3-2 fainali FA na Mtibwa wakati Watanzania wengi waliwapa nafasi kubwa ya ushindi ni aibu, au Alizeti inawachanganya? Kama ndivyo badilisheni kilimo, limeni ufuta!”

Timu ya Singida United imetangaza kocha mpya atayekinoa kikosi hicho msimu ujao ambaye ni  Hemed Morocco aliyechukua mikoba ya Hans Van Pluijm ambaye ametimkia Azam FC.

Majambazi Wanne Watwangwa Risasi Wakijaribu Kuwatoroka Polisi

0
0

SHINYANGA: Watu wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wameuawa kwa kupigwa risasi na Askari wa Jeshi la Polisi wakati wakijaribu kutoroka

Imeelezwa kuwa majambazi hao walikuwa wakitafutwa kwa muda mrefu kwa tuhuma za kufanya uhalifu katika maeneo mengi ya kanda ya ziwa

Watu hao wamekutwa na bunduki 2 moja ikiwa ini AK 47 na Short Gun moja iliyokatwa kitako, Bastola 2, bomu la kutuoa 1 na risasi 45

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo amesema watu hao wamefariki dunia wakati wakipelekwa hospitali

Usizubutu Kufanya Mambo haya kwa Mpenzi Wako

0
0

Unapokuwa na mpenzi wako katika mahusiano, epuka sana kufanya vitu vya aina hii ambavyo vitasababisha mahusiano yenu kufa.

1. Kuanza kuchelewa kutoka kazini mara kwa mara.

Sio kwamba kila mtu anapochelewa kutoka kazini basi anakuwa sio mwaminifu, lakini zaidi ya asilimia 75 (kutoka kwenye tafiti) ya ambao wamekuwa na mahusiano nje wamekuwa wakitoa visingizio vinavyohusiana na kazi, vikao, mikutano na safari za kikazi, yamkini wewe ni shahidi wa hili.

2. Mazingira tatanishi ya simu :

Gafla simu zinaanza kumiminika mpaka mida ya usiku. Yamkini pia alikuwa yuko huru hata simu yake inapolia waweza ichukua na kumpatia lakini gafla anakuwa na hofu kubwa na kuificha simu yake, nimeongea na wengine ambao wanakwenda na simu hadi bafuni isije ikasikika.

Wengine wanaondoa milio katika simu zao wakati haikuwa kawaida yao, kuwe siri (password) ngumu hadi mwenyewe anashindwa kuikumbuka, wako ambao simu zao zikipigwa hawawezi kupokea na kuongea kwa uhuru kama kawaida, ataondoka na kujitenga pembeni akijifanya anaongea kiuaminifu kabisa.

3. Harufu ambazo hujazizoea

Kwa kuwa wapendanao huwa wamezoeana, maranyingi hata aina ya manukato mmoja anayotumia yanakuwa yanajulikana kwa mwenzake, Sasa hembu fikiri unamkuta mpenzi wako ametokea na ana harufu ya tofauti kabisa na uliyoizoea, umeisikia harufu hiyo akiwa amerudi toka kazini wakati asubuhi alipoondoka alikuwa na harufu ile uliyoizoea.

4.Tabia za kuanza kukufuatiliasana au hata kukuganda.

Wapo wanaotawapeleka wapenzi wao kila wanakotaka, nakutoruhusu mazingira ya wapenzi hawa wakike kuwa huru kufanya mambo yao wenyewe, wengine waliitafsiri hali hii kama penzi kubwa lakini baada ya muda unagundua kuwa ile ilikuwa ni ujanja wa kuficha uhalisi wake na kuzuia mazingira kwa mpenzi wake kugundua au kupewa taarifa ya tabia zake.

5. Kuzungumza sentensi za kutatanisha:

Unaweza kukuta katika mapenzi yenu mpenzi wako anaanza kuwa na sentensi ngumu na zisizo kuwa na msingi kwa mfano anasema “kwa jinsi hii sidhani kama tutafika” “mi siamini kama mapenzi yanadumu” “yani ndio maana watu wanashindwa kukaa na mpenzi mmoja” na maranyingine anaweza kukuuliza baadhi ya maswali moja kwa moja ili kukuona utajibuje. Sentensi hizi zina chanzo moyoni, kuwa macho.

6. Tabia za kuficha fedha:

Hii utaiona ghafla mpenzi wakeo anaanza kuwa na siri kuhusu fedha zake au matumizi yake, na wala hapendi kuulizwa ulizwa kuhusu suala hilo. Tabia hii ikidhihirika katika mapenzi yenu usichelewe kuchunguza maana kwa kukaa kimya unaweza kujikuta umechelea mwana na maji ya moto.

Hivi Ndivyo Mazoea Yanavyoharibu Mahusiano

0
0

Kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususani kwa upande wa mwanamke kwa kutojali usafi wake, mavazi anayovaa, chakula anchopika, nidhamu ya nyumba na mpangilio kwa ujumla.

Matatizo mengi ndani ya nyumba yanaweza kusababishwa na moja au baadhi ya tabia hizo, ambazo huenda ikawa hazitokani na dharau, bali kuzoeana, kwa mfano, siku za mwanzo wa ndoa mwanamke huwa anajali sana usafi wa mwili wake, umaridadi wa nguo anazovaa, usafi wa nyumba na nidhamu ya hali ya juu, upishi wa chakula unaozingatia vionjo na ubunifu, mapokezi yenye bashasha na wakati mwingine hata kumkumbatia mumewe arudipo kutoka kazini.

Lakini baada ya kuzoeana yote hayo hubadilika, mwanamke huhisi kuwa hana jipya la kumuonyesha mumewe, hujiona wameishakuwa watu wazima sasa, na mara nyingi utakuta mwanamke huyu anashinda na sare (uniform) moja kuanzia asubuhi hadi anapopanda kitandani usiku, mambo ya Hinna, nguo za fashion, salon, manukato, kujipamba na dhahabu huyafanya pale anapotoka kwenda harusini na sio nyumbani. Huku ndio kuzoena, na tafsiri sahihi ni kudharau.

Hivyo ili kulinda kibarua cha chako cha mahusiano ni vyema ukajifunza kila wakati kutofanya vitu ambavyo vimekuwa havijayajengi mahusiano yako.

Asante kwa kuwa msomaji wa muungwana blog.

Ushauri kwa Wasichana Single

0
0

Siku ya leo naomba nizungumze na wale wadada wote ambao hawajoelewa au kwa kibantu huitwa (single ladies).  Ewe mwanadada yapo mambo ya msingi ambayo unapaswa kuyafahamu kabla ya kuolewa na mambo hayo ni;
Usiharakishe kutoka nyumbani kwa wazazi wako kwa gia ya kwenda kuolewa.
Usimsubiri mwanaume mpaka aje ndio uanze kuishi. Unaweza kuishi maisha timilifu hata ukiwa huna mwanaume.
Achana na pombe zimewauwa wenzako wengi kwa kisingizio cha kuondoa stress na wewe unaweza kufa pia.
Usiwe mtu wa kuendekeza kuzipokea na kuzijibu namba ngeni za simu hasa nyakati za usiku.. sio njia sahihi ya kupatia mpenzi.
Tengeneza mazingira ya kuilinda afya. Jitahidi Kunywa maji mengi na Chakula kwa diet achana na viofa ofa vya bure, vimesha waponza wenzio wengi mpaka sasa.
Vaa vizuri na kiheshima. Watu watavutiwa na wewe ulivyo kabla ya kuongea nawe

Hizi Hapa Sifa za Wife Material, Kwa Vijana Wanaotafuta Kuoa

0
0

Je wewe ni single boy? Au bachela kama wengi ambavyo hupenda kujiita? Kama jibu ni ndio basi naomba utambue ya kwamba suala la kupata mke si kazi bali kupata wife material ndio kazi. Hivi hujawahi kusikia wahenga wa zamani wakisema ya kwamba ni heri ukosea njia utauliza kwa pita njia kuliko ukosee kuoa? Hii ina maana gani? Hii ina maana ya kwamba wakati unafanya mchakato wa kutafuta mke wa kuoa ni lazima uzingatie misngi na mchakato mzima wa kupata  mke bora na si ke bora.

Miongoni mwa misingi hiyo ni lazima uchagua mwanamke ambaye atakuwa na sifa hizi:

1. Mwanamke ambaye hana tamaa ya pesa.

Katika maisha ya sasa mwanamke anayependa sana pesa ukikubali awe mkeo mtasumbuana sana. Kwa maana hiyo mwanamke ambaye utagundua hana tamaa ya pesa, kwamba ikiwepo, ikikosekana anabaki kuwa yuleyule wa siku zote, huyu ni ‘wife material’.

2. Mwanamke anayependa watoto

Utajuaje kama mwanamke uliyenaye ana mapenzi na watoto? Iko hivi; katika uhusiano wenu ukiona ni mtu wa kupendapenda sana watoto wa marafiki zake, kuwanunulia zawadi, kuwashauri wenzake namna nzuri ya kuwalea watoto, hata akija kupata wa kwake itakuwa ni hivyohivyo, huyo ni wife material unatakiwa kumoa haraka.

3. Mwanamke ambaye ana heshima ya kweli. 

Msichana ambaye anaheshimu kila mtu, mdogo na mkubwa, anawapenda na kuwaheshimu ndugu, jamaa na marafiki zako, huyu ana sifa ya kuwa mkeo pia.

4. Mwenye uwezo wa kujishusha.

Ogopa sana mwanamke ambaye anataka usawa, yaani yeye hata akikosea anakuwa hayupo tayari kusema samahani msichana wa aina hii hafaai bali  Anayekufaa ni yule anayejua yeye ni mke, nawewe ni mume. Anayetambua kuwa, mwanaume ndiye kiongozi wa familia.

5. Mtu ambaye anakushauri kwenye mema.

Kama mpenzi wako ni wa kukutaka kila siku muende baa au mfanye madili hatari ili mpate pesa, huyu hana sifa ya kuwa mkeo. Mke ni yule ambaye atakuongoza kwenye kutenda mema na kuacha mabaya. Kwa mfano kama unakunywa pombe atakushauri uache, kama siyo mtu wa ibada, atakushawishi umjue Mungu wako na mambo mengine kama hayo.

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume? Unakosa Hamu ya Tendo au Maumbile Madogo?

0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea tiba na matunda bila kemikali sasa
@markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

"Nimetolewa Bikira na Watu Wawili ila sio Stereo" - Chemical

0
0

Rapa wa kike wa bongo Chemical 'mwana wa Lubao' amefunguka na kudai hawezi kujutia kutokuolewa na mwanaume ambae ametoa usichana wake 'bikra' kwa kuwa anawajua wanaume waliokuwa wengi hawana mapenzi ya kweli huwa wanabadilika muda wowote wakijisikia.


Chemical ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha eNewz kutoka EATV na kusisitiza kuwa licha ya kuwa yupo katika mahusiano lakini hana malengo ya aina yeyote kwa kipindi hiki kufunga pingu za maisha 'ndoa' mpaka pale atakapojihakikishia yeye mwenyewe ameweza kukamilisha kila alichokuwa anakihitaji kukipata.

"Sijasema kama ninaingia kwenye ndoa baada ya miaka mitano au 10, 'no' sijasema hivyo. Watu hubadilika sana anaweza mtu akakupenda leo halafu kesho asikupende na kwangu mimi hilo suala nipo fresh kabisa kwa hiyo sijaingia katika mahusiano kwa kusema huyo ndio atakuja kunioa leo wala kesho", amesema Chemical.

Mbali na hilo, Chemical amedai haikuwa jambo rahisi ya yeye kutolewa usichane wake na mwanaume mmoja kwa kuwa alikuwa amekomaa sana hivyo ikapelekea kutembea na wanaume wawili kwa wakati mmoja katika kutekeleza jambo hilo.

"Ujue nimekaa hiyo miaka 20 sio midogo, kwa hiyo ikabidi wasaidiane. Yote hayo yamefanyika nikiwa na akili zangu wala sijatumia pombe maana nilipanga kitolewe na kwa kuwa wa kwanza alishindwa ili bidi aje mwingine amalizie kuitoa", amesisitiza Chemical. 

Mtazame hapa chini Chemical akifunguka zaidi...

UDART yafunguka Sababu za Abiria Wa Mabasi ya Mwendo Kasi Kusafiri Bure Kwa Siku Mbili

0
0
Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imefunguka na kudai sababu kubwa iliyosababisha kutoa huduma kwa abiria kwenye mfumo wa bila ya kulipa nauli kwa siku mbili mfululizo ni kutokana na wahudumu wanaouza tiketi kugoma kufanya kazi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo baada ya watumiaji wa mabasi hayo kupata huduma ya bila malipo tangu Juni 3 hadi leo Juni 4, 2018 na kusema imefanya hivyo kwa lengo la kutoathiri shughuli za abiria hao.

"Tunatambua kusafirisha abiria bila ya kulipa nauli kuna sababisha hasara kubwa kwa kampuni  lakini kwa kuzingatia umuhimu wa abiria wetu kupata huduma na hadhi ya taifa, hasara iliyopatikana haiwezi kuzidi madhara ambayo yangetokea kwa kusimamisha huduma", amesema Bugaywa.

Pamoja na hayo, Bugaywa ameendelea kwa kusema "kutokufika kwa wahudumu kwenye vituo kwa siku mbili mfululizo kumetokana na kucheleweshewa mishahara ya mwezi Aprili na Mei ambayo awali ilikuwa inalipwa na UDART kupitia Maxcom. Lakini badala ya mkataba huo kuisha na wakati tukisubiri kamati zilizoundwa na wakala anayesimamia mradi DART Agency, kusimamia na kukabidhi mfumo kwa UDART.

Kampuni iliomba taarifa za benki za wafanyakazi hao ili waweze kulipwa mishahara moja kwa moja kutoka UDART, bahati mbaya hil halikuwezekana hadi sasa tumefikia hatua hii".

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewahakikishia abiria wa mfumo huo na wananchi kwa ujumla kuwa mradi huo ni muhimu kwa ustawi wa taifa na kwa namna yeyote hawapo tayari kuhatarisha uendelevu wake kwa manufaa mapana ya taifa.

Spika Ndugai Afunguka Kilichomfanya 'Asusie' Mazishi Mbunge CHADEMA

0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amelazimika kutoa ya moyoni baada ya kuwepo na taarifa za kususia mazishi ya Mbunge wa Buyungu, Mwl. Kasuku Bilago ambapo amesema kuwa kamwe asingeweza kwenda kwenye uwanja ulioandaliwa na vyama vya siasa kujadili Mbunge gani atafuata kuchukua jimbo hilo.

Akitoa ufafanuzi huo leo bungenii Spika Ndugai amesema kwamba asingeweza kufanya biashara hiyo ya kuanza kunadi siasa msibani kwani ni jambo ambalo hajawahi kufanya na hataweza kufanya kwani hata maspika waliopita hawakuweza kushiriki mazishi kwenye viwanja vya siasa.

Ndugai amesema utaratibu wa siku zote wa Bunge, marehemu huwa anapelekwa kwa familia na anaagwa kwa familia kisha kupelekwa makaburini kama utaratibu unakuwa umekamilika watu wote humaliza msiba eneo hilo lakini utamaduni wa kupelekwa viwanjani hata kama angekuwa kiongozi wa Chama gani Spika asingeweza kwenda viwanjani.

Mbali na hayo, amesema kuwa kutokana na utaratibu wa  Watanzania  watu huwa 'hatugombei msiba' ndiyo maana walikabidhi mwili wa marehemu Bilago kwa familia kwa kufuata utaratibu kwa kuwa Bunge kama Taasisi lilipanga kumaliza msiba Mei 30.

Hata hivyo Spika Ndugai amefafanua kuwa familia ndiyo yenye mamlaka na marehemu na wao ndiyo wenye maamuzi ya kubadilisha ratiba pindi wanapokuwa wanahitaji.

Pamoja na hayo Ndugai amemtaka Mh. Selasini pamoja na viongozi wengine (hawajatajwa majina) wanaoshiriki vikao na kupata maamuzi ya pamoja kisha wanaenda kutoa taarifa tofauti waache kwani ni jambo lisilo na maana hata kidogo.

Huyu Mrembo Diamond Hawezi Kumuacha Hivihivi..Ona Alichofanya

0
0
Wakuu, heshima kwenu! Katika pitapita yangu kwenye mitandao ya kijamii, nimekutana na huyu mrembo, jina lake anaitwa Precious Mary akiwa amefanya cover ya wimbo wa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz akiwa na Omarion, African Beauty.

Nikiri kwamba sijawahi kusikia habari zake mahali popote lakini baada ya kuiona cover hiyo, nimeshawishika kuamini kwamba endapo Simba naye ataiona, hawezi kumuacha mwanadada huyu hivihivi!

Ukiachilia mbali sauti yenye uwezo wa 'kumtoa nyoka pangoni', huyu msichana ni mrembo wa haja na anajua pozi za kucheza na kamera. Enyi wafuasi wa Simba, hebu muonesheni bosi wenu hii cover ili afanye mambo kwa huyu mrembo.

Ni matumaini yangu na natoa RAI kwamba mambo atakayoyafanya Simba, yatahusiana na kumnyanyua mrembo huyu kisanii ili kesho na keshokutwa naye aje kuwa icon mkubwa katika muziki huu wa Bongo Fleva na si vinginevyo.
Wasalaam!

 VIDEO:

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

0
0
Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja.

Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.

“Kigoma Mpo nje ya Tanzania Mpo Porini Sana Mmetengwa”- Msigwa

0
0
Mbunge wa Iringa mjini (CHADEMA) mchungaji Peter Msigwa, amesema kuwa wakazi wa Mkoa wa Kigoma wamesahaulika na Serikali ni kama wapo nje ya Tanzania kutokana na ubovu wa barabara ya Nyakanazi

Msigwa amesema hayo leo Juni 4, 2018 Bungeni Jijini Dodoma wakati wa kuchangia hoja mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango katika mwaka wa Fedha 2018/2019 na kudai kuwa wabunge wanapaswa kuungana pamoja kuishinikiza Serikali ijenge barabara hiyo.

“Kuhusiana na barabara ya Nyakanazi, tangu nimekuwa Mbunge kipindi cha kwanza nimekuwa nikisikia Kigoma Nyakanazi, kwakweli watu wa Kigoma mnaonewa inabidi tuwasaidie, mpigiwe debe kwakweli mpo porini sana mmetengwa, mimi ilikuwa mara ya kwanza kufika Kigoma kwakweli mpo nje ya Tanzania” amesema Msigwa.

Kwa upande mwingine Mbunge huyo amesema kuwa Wizara ya Fedha na Mipango imejikita zaidi katika masuala ya fedha na kusahau kujihusisha na mipango kwasababu mipango mingi inayotekelezwa ipo nje ya mpango wa miaka mitano wa Taifa hivyo kushindwa kutekeleza vipaumbele vya maendeleo ya nchi.

Leo Juni 4, 2018 Bunge linajadili Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango katika mwaka wa fedha 2018/2019 na Waziri husika Dkt. Philip Mpango ameomba Bunge kuizinisha jumla shilingi trilioni 12.5 ambapo trilioni 10.07 ni katika matumizi ya kawaida na shilingi trilioni 1.2 kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

Polepole Awafungukia Mbowe na Zitto Kabwe Baada ya Kutangaza Kuungana

0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Ndg. Humphrey Polepole amewaonya Vongozi wa vyama vya Upinzani nchini, Mbowe pamoja na Zitto Kabwe baada ya kukubaliana kushirikiana kumpata Mbunge jimbo la Buyungu lililoachwa wazi na Mwl. Kasuku Bilago kwa kuwaambia wembe wa CCM ni ule ule.

Polepole amesema hayo ikiwa zimepita siku kadhaa baada ya mazishi ya Mwl. Kasuku Bilago kuzikwa huko Kakonko mkoani Geita baada ya kuugua kwa muda mfupi na kisha kwenda kuzikwa huko kijijini kwao.

Polepole amesema kuwa "Nimesikia jamaa palepale msibani walianza kugawana ubunge na kuanza kujihadaa, ni bahati mbaya sana. Utamaduni wa kiafrika ni kumaliza msiba ambapo lengo ni kufariji wafiwa".

Ameongeza kuwa "Nimekaa Kakonko kwa muda wa kutosha, kwakuwa mmeanza siasa msibani, CCM tunasema wembe ni uleule".

Wakiwa kwenye mazishi ya Mwalimu Bilago ambaye alikuwa Mbunge kupitia CHADEMA, Zitto Kabwe pamoja na Mbowe walikubaliana kuweka umoja ambao utamsimamisha mgombea mmoja anayekubalika kutoka upinzani na kuhakikishia wanampigania hadi anashinda ili kumuenzi mwalimu

Muonekano wa Jeneza la Consolata na Maria

0
0
Pacha walioungana Maria na Consolata wanatarajiwa kuzikwa Jumatano katika makaburi ya viongozi wa dini ya Roman Katoliki, Tosamaganga Mkoani Iringa.


Pacha hao wanaandaliwa jeneza moja lenye mfumo wa watu wawili huku misalaba ikiwa miwili na kaburi moja, akizungumzia ratiba ya maziko ya pacha hao, Muwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Richard Kasesela amesema wapo katika hatua za mwisho za maandalizi ya mazishi hayo.

"Taratibu zinaendelea na tumekubaliana kutengeneza jeneza moja lenye mfumo wa watu wawili, tutakuwa na misalaba miwil lakini watazikwa kaburi moja," amesema. Kasesela.

Ibada ya kuaga mapacha hao itafanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Ruaha (Rucu) kuanzia saa mbili asubuhi kabla ya safari ya Tosamaga kwa ajili ya mazishi

“Wizara ya fedha ni adui namba moja wa taifa” –Mbunge Silinde

0
0
Mbunge wa Momba David Silinde ni miongoni mwa Wabunge waliosiamama Bungeni leo June 4, 2018 kuchangia mapendekezo yake katika makadirio ya mapato na matumizi ya wizara ya fedha na mipango kwa mwaka wa fedha 2018/19 ambapo amelieleza bunge kuwa Wizara hiyo ni adui namba moja wa taifa.

VIDEO:

Simulizi Chungu ya Maria na Consolata Muhimbili...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya June 5

0
0


Simulizi Chungu ya Maria na Consolata Muhimbili...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya June 5

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo na Mafupi ya Kiume na Hawana Nguvu ?

0
0
KWA NINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MADOGO NA MAFUPI YA KIUME NA HAWANA NGUVU ZA KIUME NINI HUCHANGIA?


  • Kama una Ngiri, au umejichua kwa muda mrefu, punyeto, una stres nyingi Sana, lishe duni, kisukari, presha, kutopata choo vizuri, tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu, kaswende, gono,haya yote husababisha kuwa na maumbile madogo na mafupi ya kiume na kukosa nguvu za kiume.MATIBABU
  • Tumia dawa ya asili itwayo (MASUNZU POWER MIX) inatibu tatizo la nguvu za kiume maradufu inatibu uume mdogo na mfupi na kuimalisha mishipa iliyolegea inarefusha Nchi(4-8) na kunenepesha maumbile na upana (cm3-4) dawa hii haina madhala hata kwa wazee walio na umri wa miaka (70-85) pia inaongea hamu ya kufanya tendo la ndoa Mara (3-5) bila hamu kuisha dawa hii inatibu siku 6 na kupona kabisa
  • MASUNZU POWER MIX. ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo kunyoosha mishipa ya askari aliyesinyaa kutokana na kujichua kwa muda mrefu au Ngiri, nk 🌸pia tuna dawa ya kutibu busha bila opresheni
  • SOSOMA DX ni dawa ya kumvuta mme au mke mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyoanza mwanzo baada ya Masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba
  • GINDU EXTRA ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda 350 itashuka haraka tunatibu presha, vidonda vya tumbo nk:
  • OFISI IPO DAR ES SALAAM BUGURUNI CHAMA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO AU SIMU 0673552294 / +255784552299 TABIBU ATHUMAN. 

Msajili wa Vyama: Sina Taarifa ya Mahakama ya Kutomtambua Lipumba

0
0
Msajili  wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi ametaka Watanzania kuepuka taarifa za upande mmoja zinazotolewa kwenye mitandao na badala yake watumie vyombo vya habari makini kupata taarifa zinazohusiana na ofisi yake.

Kauli hiyo aliitoa jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na gazeti la Mtanzania, ambapo alisema anashangazwa kuona jamii inakumbatia zaidi habari za mitandaoni ambazo baadhi hazina ukweli kuhusu yeye, kwa sababu kuna masuala yameelzwa bila kuzingatia mkisingi ya weledi.

“Kuna watu wamekuja ofisini kwangu wakijiita viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF), lakini kimsingi sitambui kama ni viongozi kwa sababu tayari nilishatoa taarifa za kutotambua uongozi wao, wanadai walileta taarifa ya Mahakama.

“Sikuwepo ofisini kwa sababu nilikua mgonjwa. Lakini nashangaa wamekwenda kwenye kitandao ya kijamii wamesema maneno mengi ya upotoshaji kuwa nimejifungia ofisini na kukataa kupokea taarifa yao,” alisema Jaji Mutungi

Alipoulizwa sababu za kutilia shaka ujio wa maofisa hao wa CUF Jaji Mutungi alisema utaratibu wa kufikisha taarifa za mahakama unajulikana.

“Hata kama ningekuwepo ofisini tayari nilishatoa salamu kwa maofisa wangu kuwa hao watu waandike barua kueleza malalamiko yao lakini si kuniletea taarifa ya mahakama.

“Siku hizi kila kitu kinaghushiwa hadi taarifa za Ikulu kuna watu wanaghushi, mimi nitaamini vipi kama kweli taarifa ile ilikua inatoka mahakamani? Mbaya zaidi wanaishia kueleza mambo kwa namna wanavyotaka wao kwenye mitandao ya kijamii, halafu ndugu zangu wanahabari mnazipokea kama zilivyo,” alisema.

Chama cha CUF kinakabiliwa na mgogoro wa ndani baina ya Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba ambaye anatambuliwa na msajili kama kiongozi halali pamoja na Katibu Mkuu wake Maalim Seif Sharif Hamad.

Baada ya kuripotiwa taarifa za uamuzi wa mahakama kuhusu kuzuia ruzuku kutopewa Lipumba, CUF upande wa Maalim Seif waliandika barua kwenda kwenye taasisi mbalimbali kuwafahamisha kuhusu hatua hiyo ya mahakama wakisisitiza kutotolewa kwa fedha hizo

Mbunge Amtaka Spika Arudishe Matangazo LIVE Ya Bunge

0
0
Mbunge wa Viti Maalum (CUF), Riziki Lulida amemwomba Spika wa Bunge, Job Ndugai kurejesha matangazo ya Bunge yaonekane moja kwa moja.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango ya mwaka 2018/19 jana  bungeni, Lulida alianza kwa kumpongeza Spika Ndugai jinsi alivyounda kamati za Bunge zilizoonyesha tija kwa Taifa.

“Hongera Spika, umeliamsha dude, tunataka Bunge live, wananchi wanataka kusikia, nini unazungumza na kujua wabunge wanasemaje,” alisema Lulida na kuongeza:

“Tukikaa humu ndani, wananchi hawaoni unayoyafanya na ukifanya hivyo itakuwa jambo zuri.”

Lulida ameiomba Wizara ya Fedha na Mipango kuangazia hujuma zinazofanywa katika mashine za kielektroniki (EFDs) kwa kuhakikisha kunakuwapo na mifumo imara ya usimamizi kwani baadhi ya watu wanaweza kuwa na njama za kuihujumu.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images