Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Nyimbo Mbili Anazozikubali Ommy Dimpoz Kutoka WCB

0
0
Msanii wa muziki Bongo, Ommy Dimpoz ametaja nyimbo mbili kutoka label ya WCB ambazo anaona zinafanya vizuri.

Muimbaji huyo anayetamba na ngoma ‘Wanje’ ametaja ngoma ngoma hizo kuwa ni Kwa Ngwaru ya Harmonize na Pochi Nene ya Rayvanny.

“Moja wapo ni hiyo kama unavyosema Kwa Ngwaru ni wimbo ambao unafanya vizuri, yeah!, kuna mwingine nimesikia wa Rayvanny Pochi Nene, kwa hiyo kwa currently ni nyimbo ambazo naweza kusema zinafanya vizuri,” Dimpoz ameiambia Citizen Radio.

Katika hatua nyingine amefunguka ni lini hasa bifu lake na Diamond litaisha kwa kusema; “Kila jambo lina wakati wake kwa hiyo time itakapofika mambo yote yatakaa sawa, tuombe Mungu".

Madeni ya Jeshi yatua Bungeni...Spika Ndugai Atoa Maagizo

0
0
Bungeni
Spika wa Bunge Job Ndugai amewataka wabunge wote wanaodaiwa na Jeshi la Kujenga Taifa wahakikishe wanalipa madeni yao haraka iwezekanavyo kwani siku zilizotolewa zinaisha Juni 23 Mwaka huu.

Agizo hilo la Spika limekuja baada ya kusoma tangazo hilo la madeni jana ambapo alisema kuna orodha ndefu ya wabunge wanaodaiwa na kwamba baadhi yao hawana hata fedha za ziada katika posho zao wanazolipwa.

“Mtakumbuka mheshimiwa Rais alitoa agizo hilo Mei 17, aliagiza madeni yote kulipwa ndani ya siku 30 kuanzia siku hiyo, leo naomba wabunge mlipe haraka sana madeni hayo na mwisho ni Juni 23,” alisema Ndugai.

Spika alisema orodha ya wadaiwa ipo mezani kwake na kwamba angetamani kuwataja lakini alishapitia majina yao na amebaini baadhi yao wana mikopo ndani ya Bunge hivyo kwenye mfuko huo hawawezi kukatwa fedha za kulipia madeni

Mei 17 mwaka huu, Rais John Magufuli alitoa mwezi mmoja kwa taasisi za Serikali na watu binafsi wanaodaiwa na Jeshi kuhakikisha wanalipa fedha hizo  ili ziweze kutumika kujenga viwanda vingine ambapo alidai kutolilipa jeshi ni dharau kubwa.

Polisi Shinyanga Wakamata Silaha Za Kivita,waua Majambazi Wanne Makaburini Kahama

0
0

Na Kadama Malunde
Watu wanne wanaodaiwa kuwa ni majambazi wameuawa kwa kupigwa risasi na polisi eneo la makaburi  ya Kitwana kata ya Busoka tarafa ya Kahama Mjini wilayani Kahama wakati wakijaribu kuwatoroka askari waliokuwa kwenye msako mkali wa kuwatafuta majambazi wanaojihusisha na matukio ya uhalifu katika wilaya hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika makaburi ya Kitwana kata ya Busoka wilayani Kahama jana Jumatatu Juni 4,2018,Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule alisema tukio hilo limetokea Juni 3,2018 majira ya saa sita na dakika 40 mchana.

Amewataja waliouawa kuwa ni Minani Deo (33) mkazi wa Mabanda Burundi ambaye pia ni muagizaji wa silaha haramu kutoka nchi jirani na Masalamali Paulo (34) mkazi wa Geita ambaye aliachiwa kwa msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia Dkt. John Pombe Magufuli katika gereza la Butimba mkoani Mwanza mwezi Aprili 2018.

Wengine waliouawa ni Hussein Issa Jumanne maarufu kwa jina la Shehe (30) mkazi wa Nyasubi Kahama,Maduhuli Cheyo Maselegu (42) mkazi wa Kigoma Ujiji.

Akielezea zaidi kuhusu tukio hilo,Kamanda Haule alisema siku ya tukio watu hao walijeruhiwa kwa kupigwa risasi sehemu mbalimbali za miili yao na kufariki dunia wakiwa wanapelekwa hospitali ya Mji wa Kahama.

“Walikuwa wanaelekea kuwaonyesha askari polisi bastola na bomu moja la kutupwa kwa mkono ‘Hand Grenade) pamoja na washirika wenzao wa ujambazi,wakiwa tayari wameonesha bastola na bomu hilo lililokuwa limechimbiwa chini ya ardhi ndipo walipotaka kuwakimbia askari na askari wakawafyatulia risasi”,alifafanua Kamanda Haule.

“Chanzo cha tukio hilo ni kutaka kuwatoroka askari waliokuwa kwenye msako mkali wa kuwatafuta majambazi wanaojihusisha na matukio ya uhalifu hasa katika wilaya ya Kahama kwa kipindi cha mwezi Machi hadi Mei 2018”,aliongeza.

Aidha alisema takwimu zinaonesha majambazi hao walikimbilia mkoani Tabora na mara baada ya askari kufika mkoani Tabora wakapata taarifa kuwa majambazi hao wamekimbilia mkoani Kigoma na polisi kufanikiwa kumkamata Masalamali Paulo eneo la soko la Mwanga mkoani Kigoma.

“Baada ya kumkamata na kumhoji aliwataja washirika wenzake watatu wa ujambazi ambao walikimbilia Katumba mkoani Katavi na kufanikiwa kuwakamata wakiwa na silaha ya kivita aina ya AK47 yenye namba UA-2651-1997 iliyokuwa na risasi 30 ndani ya magazine moja ambayo ilipatikana karibu na uwanja wa ndege mkoani Katavi”,alieleza.

Aliongeza kuwa silaha hiyo pia ilikuwa imehifadhiwa pamoja na bastola moja aina ya Browning yenye namba 17569465 ikiwa na risasi 15 ndani ya magazine yake ndani ya shimo.

Alisema katika mahojiano na majambazi hao walikiri kufanya matukio ya uhalifu katika wilaya ya Kahama na mikoa ya Tabora,Geita,Morogoro,Kigoma na Katavi na kwamba miili yao imehifadhiwa katika hospitali ya Mji wa Kahama.

Wakati huo huo,Kamanda Haule alisema mnamo tarehe 28.5.2018 majira ya saa moja na nusu usiku katika mtaa na kata ya Mhungula wilayani Kahama ikipatikana silaha moja aina ya shortgun yenye namba B-15939 iliyokuwa imekatwa kitako na mtutu ikiwa imehifadhiwa kwenye mfuko wa sulphate ndani ya nyumba ya Malale Kalikisu Malale aliyekuwa anatafutwa na polisi kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha.

Alisema mtuhumiwa alikimbia kabla ya kukamatwa na juhudi za kumtafuta na kumkamata zinaendelea.

Kamanda Haule amewataka wahalifu wote kujisalimisha pamoja na silaha zao ndani ya mkoa au nje ya mkoa na wasipofanya hivyo wataendelea kuwafuatilia sehemu yoyote waliyojificha iwe chini ya ardhi,angani au ziwani ili wachukuliwe hatua za kisheria.

“Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Magufuli kwa mapenzi yake na wananchi wake,kwa huruma yake aliamua kuwaachia huru wahalifu waliokuwa wamefungwa gerezani akiwemo huyu Masalamali Paulo warudi uraiani,wajirekebishe na washiriki kwenye shughuli za uchumi,sasa baadhi ya hao wahalifu wanauchukulia huu msamaha katika njia ambazo siyo sahihi,hivyo wote walioachiwa kwa msamaha wa rais waendane na maadili mema katika jamii”,alieleza.

“Ndugu wananchi naomba turejee kauli ambayo inatolewa mara kwa mara na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Nyakoro Sirro kuwa uhalifu haulipi, uhalifu hauna nafasi nami pia naungana na kauli ya afande IGP kurudia maneno hayo hayo kuwa kwa sasa uhalifu mkoani Shinyanga hauna nafasi,tunataka wananchi wafurahie matunda ya uhuru,matunda ya uhuru ni amani na utulivu",

"Wananchi wafanye shughuli zao za kiuchumi bila ya kuwa na hofu yoyote ile ya matishio ya kiusalama ili kusudio la kuleta maendeleo katika jamii litimie,natoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili ziweze kufanyiwa kazi mapema”,alisema.
 
Credit :Malunde

Wabunge Wahoji Ahadi ya Milioni 50 Kwa Kila Kijiji Iliyotolewa Na Rais Magufuli

0
0
Ahadi ya Chama Cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa 2015 ya kutoa Sh. milioni 50 kwa kila kijiji na kila mtaa kwa sehemu za mijini, ambayo haijatekelezwa kwa miaka miwili mfululizo huenda ikaanza kutekelezwa baada ya jana Bunge kuitaka serikali kutoa taarifa bungeni kuhusu utekelezaji wake.

Akiwasilisha bungeni jijini Dodoma jana taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu makadirio ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka ujao wa fedha, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Jitu Soni, alisema pamoja na kwamba serikali iliahidi kutoa Sh. milioni 50 kwa kila kijiji, hadi sasa hakuna fedha yoyote iliyotolewa.

Alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2016/17, serikali ilitenga Sh. bilioni 60 (Fungu 21) na katika mwaka huu wa fedha ilitenga kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kufanya utafiti wa majaribio kwa baadhi ya mitaa, vijiji, kata na shehia kutekeleza mradi huo.

"Hata hivyo, fedha hizo zilizotengwa katika miaka yote, hakuna fedha yoyote iliyotolewa licha ya serikali kuahidi na kuweka utaratibu maalum kuhusu utoaji wa Sh. milioni 50 kwa kila kijiji kupitia Tamisemi," alisema.

"Kamati ingependa Bunge lako tukufu lipewe taarifa ya utekelezaji wa mradi huu ikiwamo 'Pilot Study' (utafiti wa majaribio) iliyofanyika," alisema.

Kiongozi huyo wa kamati pia alisema tathmini ya jumla ya mwenendo wa utoaji wa fedha za utekelezaji bajeti ya mwaka 2017/18 si wa kuridhisha kwa baadhi ya mafungu.

"Hadi kufikia Machi, mwaka huu, kati ya mafungu nane yaliyo chini ya wizara, ni miwili tu yaliyokuwa yamepokea fedha zaidi ya asilimia 60 ya bajeti zilizoidhinishwa na Bunge," alisema na kueleza zaidi:

"Kati ya mafungu 47 ya wizara mbalimbali yanayostahili kupata fedha za maendeleo ni mafungu 16 tu yamepata fedha zaidi ya asilimia 50."

Pia alisema mapato yatokanayo na ushuru wa usafirishaji wa fedha na bidhaa zinazotozwa ushuru wa bidhaa kama pombe kali yameshuka kwa asilimia 30.

"Kamati inaendelea kuishauri serikali kuhakikisha kwamba sera zake za kikodi kwa sekta zinazokua ziwe zina lengo la kulea na kuendeleza sekta hizo na si kukusanya kodi kiasi ambacho kinaathiri hata ukuaji wa sekta husika,"alisema.

Jitu pia alisema pamoja na michezo ya kubahatisha kukua kwa kasi na kuipatia serikali mapato, kamati yake inashauri kupanda kwa ada, tozo na kodi mbalimbali kwa kuwa kimsingi michezo hiyo si ya kiuzalishaji na imekuwa na madhara makubwa kwa jamii.

"Katika nchi za Afrika Mashariki, Tanzania inaongoza kwa kutoza kiwango cha chini kwenye mapato ghafi ya michezo ya kubahatisha kuliko nchi nyingine," alisema.

Alitolea mfano Kenya kuwa inatoza asilimia 35, Rwanda asilimia 13 na Uganda inatoza asilimia 20 ya mapato ghafi.

Alisema kamati inaitaka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha (GBT) kusimamia kikamilifu sheria ili kuhakikisha kwamba wanaoshiriki katika michezo hiyo wawe wanafikia umri wa miaka 18.

Jitu pia alisema kamati yake inaishauri serikali kuhakikisha inalipa madeni yote ya watumishi, makandarasi na wazabuni yaliyohakikiwa.

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

0
0

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja.

Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.

Mambo Yazidi Kuwanyookea Simba Sasa Yatinga Nusu Fainali

0
0
Mambo Yazidi Kuwanyookea Simba Sasa Yatinga Nusu Fainali
TIMU ya Simba imefanikiwa kusonga mbele hatua ya nusu fainali ya michuano ya SportPesa Super Cup, baada ya kuinyuka Kariobang Sharks ya Kenya kwa jumla ya mikwaju ya penati 3-2 baada ya dakika 90 kumalizika kwa suruhu ya bila kufungana.


Mchezo uliokuwa uanpigwa Uwanja wa Afraha, umeshuhudiwa ukimalizika ndani ya dakika 90 huku kila timu ikishindwa kuona lango la timu pinzani wakati timu zote zikishambuliana kwa zamu bila mafanikio ya kupata hata bao moja.




Baada ya dakika 90 kumalizika hatua ya upigaji wa matuta ulifuatia na Simba ikaweza kupata penati mbili zilizofungwa na Erasto Nyoni, Haruna Niyonzima na Jonas Mkude.


Matokeo hayo yanaifanya Simba kuwa timu ya kwanza kuingia nusu fainali baada ya Yanga na JKU zote kutolewa jana.

Baada ya Simba kuvuka robo fainali leo, Tanzania itawakilishwa tena na Singida United kesho katika Uwanja huohuo wa Afraha.

Tundu Lissu Akamilisha Operesheni yake ya Mwisho Salama

0
0
Tundu Lissu Akamilisha Operesheni yake ya Mwisho Salama
Operesheni ya mwisho ya Tundu Lissu imefanyika na kumalizika salama.

Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alifanyiwa operesheni jana, Juni 4,2018 ya kuunga mguu wa kulia.

Katika Operesheni hiyo iliyofanyika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven nchini Ubelgiji, Lissu aliizungumzia akisema itakuchukua takriabani saa 8 hivyo kuwaomba Watanzania kumwombea.

Saa 3 usiku jana Juni 4,2018, Mke wake, Alicia ameiambia Mwananchi kutoka Ubelgiji kuwa operesheni imemalizika salama.

"Namshukuru Mungu kwani operation ya 20 iliyokuwa ya masaa 8 imekwenda vizuri na amezinduka. As always he is stable. Asanteni sana," amesema Alicia

Burundi Kuitambulisha Katiba Mpya Alhamis

0
0
Burundi Kuitambulisha Katiba Mpya Alhamis
Hata hivyo wapinzani na baadhi ya nchi za kigeni wamekosoa mchakato huo mzima kwamba haukuzingatia sheria na katiba mpya inanuwia kumbakiza madarakani Rais Pierre Nkurunziza hadi mwaka 2034.

Taarifa ya Ikulu ya Burundi imethibitisha kuwa sherehe za utiaji sahihi kwenye katiba mpya na kuitambulisha kwa raia zitafanyika alhamisi saba katika mkoa wa kati wa Gitega eneo la Bugendana ambako huko ndiko kulikozinduliwa rasmi mchakato wa katiba, lakini pia kampeni ya chama madarakani CN DD/FDD ya kuipiga debe katiba hiyo.

Aidhaa taarifa hiyo ya Ikulu imetoa mwaliko kwa magavana wote na Wakuu wa tarafa za Burundi kushiriki kwenye sherehe hizo. Wamealikwa pia wawakilishi wa vyama vya kisiasa , asasi za kiraia pamoja na Viongozi wa kidini .

Itakuwa mara ya kwanza katika historia ya Burundi kuwa na sherehe za kuipokea katiba mpya. Wadadisi wa siasa za Burundi wanahisi utaratibu huo mpya ni ujumbe wa Rais Nkurunziza wa azama yake ya kukamilisha shughuli ya katiba ambayo yeye ameipigia debe kwamba inakuja kuipa Burundi hadhi na Uhuru wake kamili wa kujitawala .

Lakini pia ni ujumbe ambao kiongozi huyo anaupeleka kwa Jumuiya ya kimataifa hususan, mataifa ambayo yalitilia shaka na kukosoa mpango mzima wa marekebisho ya katiba wakitaja kwamba uliandaliwa kinyume cha sheria .

Ni hivi majuzi tu Umoja wa mataifa, na baadhi ya nchi za magharibi washirika wa zamani wa Burundi kama Ufaransa na Ubelgiji walikemea vikali mchakato mzima wa katiba kwamba uligubiikwa na dosari nyingi na kwamba katiba hiyo mpya inatishia hata maridhiano ya kitaifa na uwakilishi wa makabila kwa Mujibu wa Mkataba wa Aman iwa Arusha. Madai ambayo yamepingwa vikali na Wakuu wa Burundi.

Katiba hii mpya ambayo inaanza kutekelezwa siku ya Alhamis itageuza mambo mengi kwenye taasisi za maongozi ya taifa , lakini pia kutoa fursa kwa Rais Pierre Nkurunziza kuweza kuwania uongozi wa nchi hadi mwaka wa 2034.

Katiba pia inaanza kutekelezwa wakati mazungumzo ya amani yakiwa yamekwama baada ya serikali kukata kuketi meza moja na wapinzani. Kufuatia hali hiyo ya mkwamo,

Wajumbe wa Muungano wa Ulaya wamelichagiza Shirika la Muungano wa Afrikan kuchukua mikononi mazungumzo ya amani ya Burundi kwa madai kwamba Jumuiya ya kimataifa imeanza kupoteza imani kwa mchakato wa upatanishi unaosimamiwa na Jumuiya ya Afrika ya mashjariki na inayoongozwa na Rais Museveni pamoja na msuluhishi Benjamin Mkapa.

Spika Ndugai Aionya Serikali....Atishia Kuzuia Mkutano wa Bunge Mwezi Oktoba

0
0
Spika Ndugai Aionya Serikali....Atishia Kuzuia Mkutano wa Bunge Mwezi Oktoba
Spika wa Bunge, Job Ndugai, ameitaka serikali kuhakikisha inatekeleza agizo lake la mwishoni mwa mwaka jana kuhusu kuwasilisha bungeni muswada wa sheria ya kuitangaza Dodoma kuwa makao makuu ya nchi vinginevyo atazuia kufanyika kwa mkutano ujao wa Bunge.

Novemba 17, mwaka jana, Spika Ndugai aliitaka serikali kuhakikisha muswada huo unasomwa kwa mara ya kwanza katika mkutano uliofuata uliofanyika kwa wiki mbili kuanzia Januari 30, lakini haikufanya hivyo.

Muda mfupi kabla ya kusitisha kwa muda kikao cha Bunge jijini Dodoma jana mchana, Spika Ndugai alikumbusha kuhusu agizo lake hilo na kumuonya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama kwamba hakuna muswada wowote wa serikali ambao utasomwa bungeni kabla ya kuwasilishwa kwa muswada wa kuitambua Dodoma kuwa makao makuu ya nchi.

"Hakuna muswada utakaosomwa hapa kwa mara ya kwanza kabla ya muswada huo. Na kwa maana hiyo, mkutano wa mwezi Oktoba hautafanyika," Spika Ndugai alisema.

Kiongozi huyo wa Bunge alitoa kauli hiyo baada ya Mbunge wa Iringa Mjini, Mch. Peter Msigwa (Chadema) kueleza bungeni jana kuwa mpango wa serikali kuhamia Dodoma haumo kwenye Mpango wa Taifa wa Maendeleo ya Miaka mitano 2015/6-2020/21.

Akichangia mjadala wa makadirio ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka ujao wa fedha, mbunge huyo alisema kuna mipango mingi imekuwa ikiibuliwa na kutekelezwa kwa fedha ambazo hazikuidhinishwa na Bunge.

Alisema mpango wa serikali kuhamishia shughuli zake Dodoma ni mfano mzuri kwa mipango inayotekelezwa bila kuidhinishwa na Bunge na haumo kwenye mpango mkuu wa serikali.

"Ndiyo maana leo tunahangaika kupata ofisi hapa Dodoma. Hatupingi serikali kuhamia Dodoma, lakini mpango huu Mheshimiwa Spika, haumo kwenye mpango wa serikali wa miaka mitano," Mch. Msigwa alisema.

Kutokana na kauli hiyo ya mbunge huyo, Spika Ndugai alisimama na kueleza kuwa suala la serikali kuhamia Dodoma limekuwa likiwekwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mpainduzi (CCM) tangu mwaka 1973.

Alisema kuna haja suala hilo liwe la kisheria, hivyo akamtaka Waziri Mhagama kuhakikisha anatekeleza agizo lake la kuwasilisha muswada huo bungeni vingine hatakubali muswada mwingine wowote kusomwa kwa mara ya kwanza ndani ya chombo hicho cha kutunga sheria.

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

0
0
Usipitwe na Habari zetu za kila siku kwa kuzisoma kirahisi kupitia Application ya Udaku Special ambayo ipo Play Store kwa watumiaji wa Simu za Android

Bonyeza Hapa Chini Kuinstall/Kudownload :

==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>> 
    

Zari Atoboa Siri ya Maisha Yake Kwenye Jarida la True Love East Afrika

0
0
Nyota ya Zari Yazidi Atoboa Siri ya Maisha Yake Kwenye Jarida la True Love East Afrika
Baada ya kuonekana kwenye video ya wimbo mpya wa Iyena wa Diamond ambao umezua gumzo kubwa, Zari The Bosslady anazidi kung’ara.

Mrembo huyo ataonekana tena kwenye jarida la True Love East Africa ambapo amezungumzia mambo mengi yakiwemo maisha yake.

Naibu Mwenyekiti Yanga Clement Sanga Ayakumbuka ya Manji "Kipindi cha Manji Mishahara Ililipwa kwa Wakati na Timu Ilifanya Vizuri"

0
0
Naibu Mwenyekiti Yanga Clement Sanga Ayakumbuka ya Manji "Kipindi cha Manji Mishahara Ililipwa kwa Wakati na Timu Ilifanya Vizuri"
Naimu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga amedai wakati aliyekuwa mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji yupo madarakani klabu hiyo ilikuwa na mafanikio makubwa sana.


Sanga miongoni mwa mambo ambayo aliyadadavua kwa upana ni maisha ya Yanga kabla na baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji.

“Tunashukuru kwa alichofanya Manji katika kipindi chote ambacho alikuwa madarakani na kabla ya kuwa madarakani wakati huo akiwa mdhamini wa klabu, amekuwa ni msaada mkubwa. Kila mwanachama na mpenzi wa Yanga anajua maisha tuliyokuwa nayo wakati huo, Manji alikuwa mpiganaji na timu iliweza kufanya vizuri kwa kipindi chote ambacho alikuwepo.,” Sanga alikiambia kipindi cha SportXtra cha Clouds FM.

Aliongeza,”Katika kipindi cha hivi karibuni wakati Manji yupo Yanga tuliweza kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya kambi mbalimbali hakukuwa na tatizo la kulipa mishara, ilikuwa inalipwa kwa wakati. Aina ya wachezaji na benchi la ufundi lilikuwa ni zuri sana katika vipindi vyote ambavyo alikuwepo na hakukuwa na dosari.”

Klabu hiyo yenye makazi yake Jangwani jijini Dar es salaam imekuwa na matokeo mabaya toka Manji aondoke madarakani. Wiki hii katika michuano ya SportPesa Super Cup nchini Kenya klabu hiyo imeondoshwa kwa kipigo cha goli 3-1 dhidi ya timu inayoshika mkia katika ligi ya Kenya.

Mimi Sina Chuki Wala Tofauti Yoyote na Diamond- Mr Blue

0
0
Mimi Sina Chuki Wala Tofauti Yoyote  na Diamond- Mr Blue
Mr Blue ameamua kuweka wazi kuhusu taarifa za muda mrefu zilizosambaa kuwa hana maelewano mazuri na Diamond Platnumz.



Hit maker huyo wa Mbwa Koko, ameiambia Wasafi TV kuwa watu ndio wanataka kuwaingiza kwenye matatizo, ila yeye ndio ameanza kumsupport Diamond tangu chini kabisa akiwa hajulikani na mtu yoyote hata waandishi wa habari.

“Ukikaa na Diamond ukimuuliza atakujibu kwamba mimi nimeanza kumsupport since day one, tokea Diamond hajulikani na waandishi wa habari, hajulikani na mtu yoyote. Alinifuata kama brother wake nikamsupport kwenye muziki wake,” amesema Mr Blue.

“Kwa mfano huo rahisi unaonyesha mimi sina chuki na Diamond, wala sina tofauti yoyote. Kama ningekuwa na tofauti ningemzuia tokea awali hata nyinyi msingepata ajira, kama ningemzuia kule mwanzoni nisinge msupport. Amekuja amekuwa msanii mkubwa ametengeneza kama hii Wasafi TV,” ameongeza.

“Kinachonichekesha na kunishangaza pale watu wanapoona nimemsupport akiwa na mafanikio, wanatak nianze kumkandia kitu ambacho hakiwezekani. Mimi Diamond ni mdogo wangu, wakati anatoka sikuwahi kuwa na bifu naye wala sikuwahi kukaa chini kumwambia ninatofauti naye, ni watu ambao wanataka kutuingiza katika tatizo mimi na Diamond,” amesisitiza.

Umapepe Uliokuwa Unaniponza Nishatupa Kulee- Ruby

0
0
“Umapepe Nishatupa Kulee- Ruby
Hakuna asiyefahamu uwezo mkubwa wa muimbaji Ruby, lakini kila mmoja amekuwa akishangaa ni kwanini mrembo huyo anashindwa kwenda mbele zaidi kimuziki kutokana na kipaji chake cha asili kilichopo ndani yake.


Mrembo huyo ambaye ni zao la Serengeti Super Nyota 2014, aliwahi kufanya kazi na THT chini ya Ruge Mutahaba wa Clouds Media na kupata mafanikio makubwa sana kwa muda mfupi kupitia wimbo wake ‘Na Yule’ambao uliteka vyombo vya habari.

Hata hivyo hakukaa muda mrefu aliachana na uongozi huo kwa kashfa nyingi na kuamua kujisimamia mwenyewe lakini hakuweza kufanikiwa kwani kila siku zilivyozidi kwenda aliendelea kupotea taratibu huku mashabiki wakijiuliza kitu gani kinamsumbua binti hiyo.

Mwezi huu amerudi umpya na wimbo ‘Niwaze’ ambao unaonekana kuwavutia watu wengi huku wadau wakidai huwenda pia ni kutokana na ukimya wake wa muda mrefu.

Jumatatu hii mrembo huyo amedai ameachana na ‘umapepe’ kitu ambacho kilikuwa kikitajwa na watu wengi hasahasa wadau wa muziki kwamba ndio kinachomkwamisha mrembo huyo.

“Umapepe nishatupa kuleeekuleee..tangu enzi za…niambie na ww mstari upi unakubamba,” Ruby alitoa ujumbe huo kupitia Instagram.

Kwa sasa muimbaji huyo hajaweka wazi anafanya kazi chini ya label gani lakini aliahidi mambo yakikaa sawa ataweka wazi kila kitu.

Wewe kama shabiki wa muziki na mdau unadhani mrembo huyo alikuwa anasumbuliwa na ‘umapepe’ au ana kitu kingine cha ziada kinamsumbua?. Toa maoni yako hapa chini au kipitia mitandao yetu ya kijamii.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo


Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

0
0

TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGESA

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Mwanajeshi wa Kulinda Amani Kutoka Tanzania Ameuawa Katika Shambulio

0
0
Mwanajeshi  wa Kulinda Amani Kutoka Tanzania Ameuawa Katika Shambulio

Taarifa kutoka kwa msemaji wa Umoja wa Mataifa leo June 5, 2018 inasema Mwanajeshi mmoja wa kulinda amani kutoka Tanzania ameuawa, katika shambulio lililotokea Jamhuri ya Afrika ya Kati na walinda amani wengine 7 wamejeruhiwa.

Shambulio hilo limetekelezwa dhidi ya kikosi hicho cha Umoja wa Mataifa wakati kikiwa kwenye doria katika Kijiji cha Dilapoko kilichopo Kusini Magharibi mwa Mji wa Mambere-Kadei.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric amesema inaaminika kuwa shambulio hilo limetekelezwa na wapigani wa Kikundi cha Siriri.

Kati ya waliojeruhiwa mmoja yuko katika hali mbaya anaendelea kutibiwa katika hospitali ya Bangui huku wengine watatu wakiendelea na matibabu katika mji wa Berberati.

Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa Aachia Ngazi Rasmi Yanga

0
0
Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa Aachia Ngazi Rasmi Yanga
Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa ameachia rasmi ngazi katika klabu yake baada ya mkataba wake kumalizika.

Nsajigwa aliingia katika benchi la ufundi la klabu hiyo wakati George Lwandamina akiwa Kocha Mkuu wa kikosi hicho kabla ya ujio wa Mkongomani, Mwinyi Zahera.

Nsajigwa anaondoka Yanga ikiwa ni siku moja tu baada ya kuondolewa katika mashindano ya SportPesa Super Cup inayoendelea mjini Nakuru, huko Kenya.

Yanga iliondoshwa na Kakamega HomeBoys kwa mabao 3-1 Jumapili ya June 3 2018 uliopigwa kwenye Uwanja wa Afraha Stadium.

Kuondoka kwa Nsajigwa kutakuwa kunamfanya kocha Noel Mwandila kusalia kwenye benchi la ufundi la Yanga kama Msaidizi pekee

Ni Vigumu Msanii Kushindana na Producer- Mr T Touch

0
0
Ni Vigumu Msanii Kushindana na Producer- Mr T Touch
Producer kutoka Touch Sound, Mr. T Touch amesema ni vigumu kwa msanii kushindana na producer.

Kutokana na hilo Mr. T Touch amesema hawezi kushindana vita ambayo anajua atashinda.

“Wale ni wasanii wanaenda wanaonekana mbele ya macho ya watu wengi kuliko sisi ma-producer, watu wengine wameanza kuona sura ya T Touch hivi karibuni lakini kila kitu kinaenda kwa wakati,” amesema.

“Lakini ukisema kwamba tushindane, msanii hawezi kushindana na producer, mimi naweza kutoa ngoma za wasanii watatu kwa mpigo na zika-hit zote lakini msanii unapotoa wimbo unategemea utashindana na producer,” Touch ameiambia Bongo5.

Kauli ya Mr. T Touch inakuja mara baada kumchukua aliyekuwa msanii wa Nay wa Mitego, B Gway kutoka Free Nation ambapo awali alikuwa akifanya kazi Mr. T Touch. B Gway anafanya vizuri na ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Na Stay.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images