Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

JWTZ yazungumza kuhusu askari wake aliyeuawa

$
0
0
Msemaji Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kanali Ramadhani Dogoli leo June 6 2018 amethibitisha kuwa June 3, 2018 Kikosi cha kulinda amani cha Askari wa Tanzania huko Jamhuri ya Afrika ya Kati kimeshambuliwa na kundi la waasi lijulikanalo kama Siriri .

 Akizungumza na waandishi wa habari Kanali Dogoli amesema waasi hao waliwashambulia Askari wa Tanzania ambapo askari mmoja amefariki, 18 wamejeruhiwa na wengine watano hali zao sio nzuri.



Mama ashiriki kumteka Mwanae ili apate fedha toka kwa Mumewe

$
0
0
Mama Rose Nantongo anatuhumiwa na Polisi nchini Uganda kushirikiana na mfanyakazi wake wa zamani Edward Matovu kufeki tukio la kutekwa kwa mtoto wake Vianney Ssebulime ili ajipatie fedha kutoka kwa mume wake.

Polisi wamesema kuwa walipokuwa wakimhoji Matovu kuhusiana na utekwaji wa mtoto huyo aliiambia Polisi kuwa aliagizwa na mama wa mtoto huyo kumteka mwanae.

Kwa mujibu wa msemaji wa jeshi la Polisi mkoa wa Kusini Lameck Kigozi amesema kuwa Matovu aliwapeleka Polisi katika kijiji cha Kananjiri nyumbani kwa Yuniya Komukama na kumkuta mtoto huyo akiwa salama.

Kwa upande mwingine John Mukisa mkazi wa kijiji cha Nabirizi alipokamatiwa Matovu amemshutumu Nantongo kwa kupenda fedha sana kuliko mwanae.

Aidha watuhumiwa hao watafunguliwa mashtaka  ya utekaji wa mtoto mara tu upelelezi utakapokamilika.

Mwasiti asimulia alivyoporwa na vibaka kwenye foleni Ubungo

$
0
0
Muimbaji Mwasiti amethibitisha kuporwa na kibaka kwenye foleni alipokuwa mataa ya Ubungo DSM, ambapo amesema ni kweli ameibiwa kibegi ambacho kilikuwa na baadhi ya vitu vyake. Msikilize hapa Mwasiti akielezea

Bonyeza PLAY hapa chini.


Exclusive: Diamond Ndani ya Mjengo na Wanae Ndani ya South Afrika

$
0
0

Wasafi TV kupitia instagram account yao wamepost picha ya kwanza ikumuonesha Diamond Platinumz akiwa South Africa na wanae. Bila shaka hii ni habari njema mno kwa team Diamond na team Zari, na wale wote ambao walikuwa wanaiombea hii couple imalize tofauti zao.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo na Mafupi ya Kiume na Hawana Nguvu ?

$
0
0

KWA NINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MADOGO NA MAFUPI YA KIUME NA HAWANA NGUVU ZA KIUME NINI HUCHANGIA?


Kama una Ngiri, au umejichua kwa muda mrefu, punyeto, una stres nyingi Sana, lishe duni, kisukari, presha, kutopata choo vizuri, tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu, kaswende, gono,haya yote husababisha kuwa na maumbile madogo na mafupi ya kiume na kukosa nguvu za kiume.MATIBABU

Tumia dawa ya asili itwayo (MASUNZU POWER MIX) inatibu tatizo la nguvu za kiume maradufu inatibu uume mdogo na mfupi na kuimalisha mishipa iliyolegea inarefusha Nchi(4-8) na kunenepesha maumbile na upana (cm3-4) dawa hii haina madhala hata kwa wazee walio na umri wa miaka (70-85) pia inaongea hamu ya kufanya tendo la ndoa Mara (3-5) bila hamu kuisha dawa hii inatibu siku 6 na kupona kabisa

MASUNZU POWER MIX. ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo kunyoosha mishipa ya askari aliyesinyaa kutokana na kujichua kwa muda mrefu au Ngiri, nk 🌸pia tuna dawa ya kutibu busha bila opresheni
SOSOMA DX ni dawa ya kumvuta mme au mke mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyoanza mwanzo baada ya Masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba
GINDU EXTRA ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda 350 itashuka haraka tunatibu presha, vidonda vya tumbo nk:

OFISI IPO DAR ES SALAAM BUGURUNI CHAMA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO AU SIMU 0673552294 / +255784552299 TABIBU ATHUMAN.

Simba Ipo Vizuri Sasa Kuja na Tuzo Zake Maalum Mo Dewji Simba Awards

$
0
0
Simba Ipo Vizuri Sasa Kuja na Tuzo Zake Maalum  Mo Dewji Simba Awards
Mfanyabiashara maarufu Tanzania ambaye pia ni muwekezaji kwenye klabu ya Simba, leo ametangaza rasmi kuwa ameanzisha tuzo maalumu kwa klabu hiyo.


Tuzo hizo ambazo amezipa jina la MO Simba Awards zitatolewa Juni 11, 2018 katika hoteli ya Hyatt Regency na zitakuwa na vipengele 16 ambavyo vimelenga mashabiki, wachezaji na viongozi wa klabu hiyo.

Kwenye Taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari akizungumzia lengo hasa la tuzo hizo, MO Dewji amesema kuwa “Simba ni timu kubwa inastahili kuwa na tuzo zake ambazo zitakuwa zinatolewa kwa kutambua mchango wa wenzetu ambao umetuwezesha kupata mafanikio haya ikiwepo kushinda taji la Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Ni jambo ambalo litawatia moyo kuendelea kujituma lakini hata kwa ambao watakosa itawatia hamasa na hivyo kuongeza juhudi”.

Vipengele vitakavyogombaniwa ni Mhamasishaji Bora wa Mwaka na Tawi Bora la Mwaka, Kiongozi Bora wa Mwaka, Tuzo ya Wasimamizi wa Mchakato wa Mabadiliko, Mhamasishaji Bora wa Mwaka kwenye Mitandao ya Kijamii na washindi watapatikana kwa kupiga kura kwenye website ya mosimbaawards.co.tz .

TANZIA: Mwanamuziki Sam wa Ukweli afariki dunia, Mtu wake wa Karibu Afunguka Ukimwi

$
0
0
.Msanii Sam wa Ukweli Afariki Dunia
Msanii wa Bongo Fleva, Sam wa Ukweli amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Juni 7, 2018 baada ya kuugua na mwili wake kupelekwa katika hospital ya Mwananyamala.

Taarifa hiyo imethibitishwa na msambazaji wa nyimbo zake na Meneja wa ‘Team Mtaa kwa Mtaa’, Amri the Business ambaye aneeleza kwa masikitiko makubwa kuwa Sam amefariki dunia na kumtakia kupumzika kwa amani.

“Siamini kilichotokea muda huu ila sina jinsi, kwani woote safari ni moja, pumzika kwa amani Sam wa Ukweli, hakika nilikupenda kama ndugu yangu wakuzaliwa tumbo moja, #rip” amesema Amri the Business.

Pia, aliyekuwa mtayarishaji wa nyimbo za Sam wa Ukweli, Steve amesema Sam alikuwa akiumwa na walipomuuliza alisema ni UKIMWI wa kulogwa.


Boyfrend Wangu Kanikataza Kumzungumzia Bill Nass- Nandy

$
0
0
Boyfrend Wangu Kanikataza Kumzungumzia Bill Nass- Nandy
Msanii wa muziki Bongo, Nandy amedai kuwa amekatazwa na Boyfriend wake kuzungumzia kile kilichotokea kati yake na Bill Nass.

Muimbaji huyo ameiambia U-Head, Clouds FM kuwa hata alipokuwa katika media tour nchini Kenya ni kitu ambacho alikuwa anaulizwa mara kwa mara na kukiri kuwa kilikuwa kinamsumbua.

“Kawaida nimefanya interview hayo maswali yalikuwepo, hakikuwa kitu kidogo kilienda mbali sana na kilinisumbua kiukweli lakini yameshapita,” amesema.

“Unavyoniuliza maswali sijui ya Bill Nass nimeshakatazwa na Boyfrind wangu kuyaongelea mambo hayo,” amesisitiza Nandy.

Utakumbuka April 12, 2018 Nandy na Bill Nass walikamata headlines za kiburudani Bongo hasa katika upande wa udaku kufuatia kuvuja kwa video yao ikiwaonesha wakiwa faragha. Suala hilo lilifika hadi bungeni na polisi waliweza kuwahoji wahusika.

Wastara Akosolewa Kujianika Adharani Kipindi Hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

$
0
0
Wastara Akosolewa Kujianika Adharani Kipindi Hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
MREMBO mkongwe wa Bongo Movies, Wastara Juma, amekosolewa kwa kitendo chake cha kujianika mitandaoni akiwa ameshikilia tasbii anaswali.



Licha ya kuweka picha hiyo kwa nia njema ndani ya mwezi mtukufu wa Ramadhani katika ukurasa wake wa Instagram, baadhi ya watu walimkosoa kwa kumtaka afanye jambo hilo bila kujionesha lakini pia wengine walimpongeza.



“Sasa wewe unaswali ama unaonyesha watu kama mcha Mungu ama kuna matangazo ya kuswali hapo umechemsha… kila kitu Instagram hee unacheza  wewe,” aliandika jamaa mwenye akaunti iitwayo Mbwenitegg.



Hata hivyo, wachangiaji wengine katika picha hiyo walionekana kumsifia kwa kumcha Mungu wake kwani amefanya hivyo ili ikiwezekana na wengine wajifunze kuswali kupitia yeye. Alipotafutwa Wastara kuhusu hilo, simu yake haikupatikana.

Rais Magufuli Amteua Athumani Mbuttuka Kuwa Msajili wa Hazina

$
0
0
Rais Magufuli Amteua Athumani Mbuttuka Kuwa Msajili wa Hazina
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Athumani Selemani Mbuttuka  kuwa wa Msajili wa Hazina.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema kuwa uteuzi wa. Mbuttuka utaanza  Juni 6, 2018.

Aidha, kabla ya uteuzi huo, Mbuttuka alikuwa Naibu Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Taifa (DAG) katika Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali  (NAOT).

Mbuttuka anachukua nafasi ya Dkt. Oswald Mashindano ambaye tayari amekwisha staaafu.

Serikali ya Rwanda na Arsenal Kufanyiwa Uchunguzi

$
0
0
Serikali ya Rwanda na Arsenal  Kufanyiwa Uchunguzi
Wanasiasa nchini Uholanzi na baadhi ya Wabunge wa Uingereza na Ujerumani, wametaka kufanyika kwa uchunguzi kuhusiana makubaliano ya hivi karibuni yaliyofikiwa na Serikali ya Rwanda kuidhamini klabu ya soka ya Arsenal ya nchini Uingereza.


Uamuzi huo umejitokeza baada ya kuwepo kwa wasiwasi kuhusiana na mkataba huo wa mamilioni wakati mataifa hayo yakitoa msaada mkubwa kwa Rwanda.

Mkataba huo wa udhamini wa miaka mitatu unaojulikana kama Visit Rwanda, unahusu nembo ya Rwanda kuonekana kwenye jezi za timu ya Arsenal ambapo lengo likiwa ni kutangaza vivutio vya utalii vya taifa hilo la Afrika Mashariki.

Wakosoaji wamehoji kwanini serikali ya Rwanda imetumia Paundi za Kiingereza milioni 30 kusaini makubaliano hayo na kudai ni fedha nyingi ambazo zingesaidia kuboresha miundombinu na masuala mengine ya maendeleo na kuhakikisha Wanyarwanda wanajikwamua kutoka kwenye umasikini.

Hata hivyo serikali ya Rwanda imesisitiza kwamba fedha hizo za udhamini zimetokana na mapato ya sekta ya utalii yenyewe na inaamini uamuzi huo utachangia pakubwa kuinua sekta hiyo.

Utalii ndio sekta inayoongoza kwa kuingiza fedha za kigeni nchini Rwanda kiasi cha Dola milioni 400 kwa mwaka ambapo nchi hiyo imepanga kuongeza mapato hayo maradufu na kufikia Dola milioni 800 ifikapo mwaka 2024.

Aliyejitosa kwa Zari Afunguka ‘Tunajua Huwezi Kurudiana na Diamond’

$
0
0
Aliyejitosa kwa Zari afunguka ‘Tunajua huwezi kurudiana na Diamond’
Msanii wa muziki wa Injili kutoka nchini Kenya, Ringtone Apoko ameonyesha kuchukizwa na tetesi za Zari kurudiana na Diamond.

Utakumbuka hivi karibuni Ringtone alieleza hisia zake kuwa anataka kumuoa Zari, alienda mbali zaidi kwa kueleza kuwa alishanunua gari aina ya Range Rover Sport ya mwaka 2017 kwa ajili ya mrembo huyo.

Soma Pia; Aliyetangaza kumnunulia Zari Range Rover Sport 2017 ala za uso

Sasa Rington Apoko amesema atashangaa ikiwa Zari atarudi kwa Diamond ingawa anajua hawezi kufanya hivyo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

Mpendwa Zari huwezi ukaendelea kusoma kurasa za kitabu kile kile kila siku ilihali unajua kitakavyoishia, ulioandoka Misri ukaenda Kanani itasikitisha kama utarudi tena.

Nini kitatokea kwa wasichana kibao uliowaambia sasa unamjenga Zari? Ushauri wangu ni kuwa hivi sasa mtafute Mungu kwa kufunga na maombi ili Mwenyezi Mungu akupe mwelekeo. Lakini hivi sasa hatuna wasiwasi maana wote tunajua huwezi kurudiana na Diamond.

Muimbaj huyo amekuwa akituma jumbe mbali mbali kwa Zari kupitia mtandao, hata hivyo Zari akiwa nchini Kenya May mwaka huu alisema hamjui Ringtone kwani ana followers zaidi ya milioni 3.9 katika mtandao wa Instagram. Kumekuwa na taarifa zinazodai kuwa huenda Diamond na Zari wamerudiana au kufanya hivyo hivi karibuni.

Walichoandika Wolper, Snura na Prof. Jay Kuhusu Kifo cha Sam wa Ukweli

$
0
0
Walichoandika Wolper, Snura na Prof. Jay Kuhusu Kifo cha Sam wa Ukweli
Usiku wa June 6, 2018 Muimbaji Sam wa Ukweli amefariki dunia baada ya kuugua na mwili wake kupelekwa katika hospital ya Mwananyamala huku Producer wake Steve aliekua akifanya kazi na Msanii huyo kuthibitisha kuwa Sam wa Ukweli alikuwa akiumwa UKIMWI wa kulogwa..

..>>> “Sam alianza kuzidiwa toka J’mosi, tulipomuuliza anaumwa nini alisema UKIMWI lakini sio UKIMWI wa kawaida bali wa kulogwa” – Steve

Sasa baadhi ya mastaa mbalimbali wameguswa na tukio hilo na kupost kwenye ukura zao za Instagram…>>>“Dah!!!😢😢😢😢nitasema nini sasa mimi 😢😢tangulia tu mdogo wangu harakati ndio zimeishia hapa kweli????😢😢😢😢😢” – SNURA
…>>>”Poleni Ndugu wafiwa wote na Mashabiki kwa ujumla jamani🙌 R.i.p Sam Tangulia mwaya 🙏” – WOLPER
……>>>“Whaaaat? R.I.P SAM WA UKWELI🙏” Prof. Jay

Polisi Waanza Uchunguzi Matapeli wa Meseji za Simu

$
0
0
Polisi Waanza Uchunguzi Matapeli wa Meseji za Simu
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kupitia kitengo cha upelelezi wa makosa ya mtandaoni, (Cybercrime investigation unit) kimesema kuwa kinafanya uchunguzi kuwabaini wanaotuma ujumbe mfupi wa simu za mkononi kwa nia ya kuwatapeli wananchi.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Makao makuu, Barnabas Mwakalukwa, leo imesema yeyote aliyetapeliwa anatakiwa kutoa taarifa katika kituo cha polisi alichokaribu nacho.

“Tunawataka wananchi kuacha kutumia simu na mitandao ya kijamii vibaya na badala yake itumike kuhabarisha na kuelimisha jamii juu ya mambo mbalimbali ya maendeleo,” imesema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imesema, baadhi ya jumbe hizo ni zile zinazosema. ‘Ile hela tuma kwa namba hii’ au ‘usipige kwa sasa, spika imeharibika, tuma ujumbe,’ au ‘Mjukuu wangu ile ndagu niliyokutumia imefanya kazi na sasa unapata wateja wengi... sasa njoo uchukue ndagu nyingine ya mvuto na nyingine kama hizo.’

Pamoja na hayo Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi kutumia mitandao pamoja na simu katika kuelimisha na kuhabarisha na si vinginevyo ikiwa ni pamoja na kuwataka wananchi kupuuzia  jumbe hizo zenye lengo la kitapeli.

Dk Tulia Amzuia Waziri Mkuu Kujibu Swali Waraka wa KKKT

$
0
0
Dk Tulia Azuia Waziri Mkuu Kujibu Swali Waraka wa KKKT
Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amemkingia kifua Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kujibu swali kuhusu Serikali kulipa siku 10 Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kufuta waraka wake wa Pasaka uliotolewa Machi 24, 2018, ambao mbali na masuala ya kiroho, ulitaja changamoto tatu za kijamii.

Swali kuhusu KKKT iliyoandikiwa barua ya kutakiwa kufuta waraka huo na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, limeulizwa leo Alhamisi Juni 7, 2018 katika kipindi cha Maswali ya papo hapo kwa Waziri Mkuu na mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia.

Katika swali lake, Mbatia ametaka kujua ukweli kuhusu barua hizo lakini baada ya kumaliza kuuliza swali hilo, Dk Tulia amesema haliwezi kujibiwa na kiongozi huyo wa shughuli za Serikali bungeni.

“Kuna barua wamepewa KKKT na TEC (Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania ) wakitakiwa kufuta nyaraka zao za Kwaresima,” amesema Mbatia na kuitaka Serikali kueleza uamuzi huo una lengo gani.

Mara baada ya swali hilo, naibu spika huyo amesema, “mtakumbuka mheshimiwa Kubenea (Saed-mbunge wa Ubungo-Chadema) alimuuliza waziri Mkuu swali linalohusu dini na mheshimiwa Spika alizuia suali hilo lisijibiwe.”

Baada ya maelezo hayo, Dk Tulia alimuita mbunge mwingine kuuliza swali huku Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi akiketi na kuzungumza na na wabunge wengine wa vyama vya upinzani chini kwa chini.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa leo

$
0
0

Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

$
0
0
Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja.

Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.

Producer Steve Joniso Afunguka A-Z Kuumwa Ghafla kwa Sam wa Ukweli Mpaka Kifo Chake

$
0
0
 Producer Steve Joniso Afunguka A-Z Kuumwa Ghafla kwa Sam wa Ukweli Mpaka Kifo Chake
Usiku wa kuamkia Alhamisi hii zilianza kuzagaa taarifa za majonzi za kifo cha msanii wa muziki, Sam Waukweli baada ya kuugua kwa muda mfupi.



Kwa mujibu wa taarifa za awali muimbaji huyo alianza kuugua ghafla akiwa studio na baadaye kukimbizwa hospitali ya Palestina iliyopo Sinza Kinondoni jijini Dar es salaam kwaajili ya matibabu lakini muda mchache alifariki dunia.

Akiongea na Millardayo usiku huo producer Steve Joniso ambaye alikuwa mara ya mwisho na marehumu, alisema wakati yupo studio akiandaa beat kwaajili ya wimbo wa Sam, muimbaji huyo alikuwa akilalamika kuumwa tumbo na baadaye alizidiwa na kukosa nguvu kabisa hali ambayo ilipelekea hata ashindwe kwenda chooni mwenyewe.

“Ikabidi tumpeleke chooni huwezi amini chooni tulimtenga hawezi kukaa kwenyewe, sisi tukaona hii sio kawaida, tukamwambia Sam ngoja tutoe taarifa kwa ndugu zako, yeye anakataa msiwataarifu, hiyo inaenda saa moja usiku, mida ya saa mbili usiku tukaamua kuwapigia simu ndugu zake tukawataarifu mbwana Sam yupo kwenye hali hii lakini amesema tusiwaambie kama mnaona vipi njooeni. Lakini baada muda mchache tukapigiwa simu ya yule ndugu yake, bwanaee nimeongea na mke wake lakini amesema hana nauli kesho atakuja hapo kumuona, hata mimi nitakuja muda huo huo,” alisema producer huyo.

“Tumekaa mpaka saa nne usiku hali yake ikawa mbaya zaidi, akaomba akupumzike, sisi tukamwambia tukupe dawa yeye akaomba apumzike ila kwa kunisaidia ili nisiwasumbue naomba nifunge pempasi, sisi kama vijana wa kiume tukamchukua tukamfunga pempasi, sisi tukarudi studio kuendelea na kazi,” aliongeza.

Kifo Chake

“Tumekaa dakika tano tu tukagongea kwamba Sam anawaita, kwenda kutamuuliza vipi Sam akasema siwezi kupumua vizuri, nasikia kama nashindwa kupumua, sisi kwa upande wetu tukaona hii imekaa vibaya, tulichokifanya ni moja kwa moja kumpeleka hospitali, tukampeleka mahabara ndogo pale Mabibo, kumpeleka pale wakatuambia huyu jamaa anaumwa sana mpelekeni Palestina. Tumefika Palestina tumefanya process zote baadaye tukaambiwa tumpeleke kwenye emergency wakawa wanamuekea vifaa vya kupumulia baadaye kama dakika 10 tukaitwa bwana nani anahusika nikasema mimi nahusika, wakaniambia njoo tukupe majibu, wakiambia nijikaze huyu ndugu yako hatuko naye tena, sikuamini kwa sababu tulikuwa naye muda mchache uliopita na jana yake tulishinda naye,” alifafanua Steve.

Kajala Afungukia Kuvunja Ndoa ya P Funk "Si Kosa Mimi Kupiga Picha na Mzazi Mwenzangu Nimeishi Naye Miaka 9"

$
0
0
Kajala Afungukia Kuvunja Ndoa ya P Funk "Si Kosa Mimi Kupiga Picha na Mzazi Mwenzangu Nimeishi Naye Miaka 9"
MKALI wa filamu za Kibongo, Kajala Masaja ‘Kay’amefungukia madai ya kuvunja ndoa ya mzazi mwenzake ambaye pia ni prodyuza maarufu wa Bongo Records, Paul Matthyasse ‘P Funk’.

Akipiga Stori na global TV Online, Kajala amekanusha kuvunja ndoa ya P Funk na mkewe Samira huku akidai kuwa hayo ni mambo ya mitandaoni tu wala hayana ukweli wowote.

“Mimi sijavunja ndoa ya P Funk, yule ni mzazi mwenzangu, nimeishi naye miaka tisa, nimezaa naye mtoto (Paula) ambaye sasa hivi yupo kidato cha nne na ana miaka 16, si kosa mimi kupiga picha na mzazi mwenzangu,” alisema Kajala.

Minon’gono ya Kajala kuvunja ndoa ya P Funk na Samira iliibuka baada ya ukaribu wa wawili hao wa hivi karibuni.

Ridhwan Kikwete Amlilia Sam wa Ukweli “Tangulia Rafiki Yangu ‘Mwana wa Ukae”

$
0
0
Ridhwan Kikwete Amlilia Sam wa Ukweli “Tangulia Rafiki Yangu ‘Mwana wa Ukae”
Mbunge wa Chalinze Ridhwan Kikwete amezipata taarifa za kifo cha hitmaker wa ‘Hata kwetu wapo’ Sam wa Ukweli na ameamua kuandika katika ukurasa wake wa Twitter.

Ridhwan ameandika “Innallillah Wainnaillah Rajuun, Nadhani sihitaji kusema mengi ila kumshukuru Mungu Mwenyezi kwa mapenzi yake kwetu Binadamu na hasa kwako rafiki yangu Sam “Mwana Wa Ukae, Mzukulu wa Mwali Bonele Wa Kiwangwa”.Tangulia Rafiki Yangu, Pumzika kwa Amani Sam Wa Ukweli.”
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live


Latest Images