Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104416 articles
Browse latest View live

Serikali Kuhakiki Mikataba ya Wasanii

0
0
Serikali Kuhakiki Mikataba ya Wasanii
Serikali imesema kuwa, kamati maalumu iliyoundwa inaendelea na zoezi la uhakiki wa kupitia mikataba yote ya wasanii nchini, ili kusaidia wasanii waweze kunufaika na kazi zao kutokana na makubaliano ya kibiashara waliyoingia.


Hayo yamesemwa Bungeni leo Juni 18, 2018, Jijini Dodoma, na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa viti maalum Bi Martha Mlata aliyetaka kujua ni kwa namna gani serikali inasaidia wasanii kunufaika na kazi zao.

“Sasa hivi tumeunda kamati ambayo inapitia mikataba yote ya wasanii, sasahivi tumefikia hatua nzuri tunaamini kwamba kamati hiyo itakapokamilisha kupitia mikataba yote nchini, tunaamini kabisa kwamba wasanii wataweza kunufaika na kazi zao” amesema Shonza.

Naibu Waziri Shonza ameongeza kuwa serikali imekuwa ikitoa elimu ya mara kwa mara kwa wasanii nchini ili wafahamu umuhimu na namna ya kuhifadhi kazi zao pamoja na kusimamia haki za kisanii ili kuepuka changamoto ya kuingia katika mikataba ambayo haizingatii maslahi yao kama wasanii.

Kwa upande mwingine Naibu Waziri huyo amedai kwamba serikali inafanya mazungumzo na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuirudisha Idara ya Chama cha Hakimiliki nchini (COSOTA) katika usimamizi wa Wizara ya Habari, Utamadiuni Sanaa na Michezo ili kuwezesha masuala yote ya wasanii kuwa chini ya mwamvuli mmoja.

Alichoandika Vanessa Juu ya Tour INLOVE & MONEY Itakayofanywa Mwanza

0
0
Alichoandika Vanessa Juu ya Tour INLOVE & MONEY Itakayofanywa Mwanza
Wakali kutokea kwenye Bongo Fleva Vanessa Mdee pamoja na Juma Jux ambao pia ni wapenzi wanakuja na tour yao ya Inlove & Money ikiwa inahusisha album ya Juma Jux inayoitwa Inlove na album ya Vanessa Mdee ambayo ndio Money Mondays (Inlove &Money).

Tour hii itahusisha mikoa mbalimbali na pia wasanii ambao wapo chini ya record label ya Mdee Music watapewa nafasi ya kuperform katika mikoa hiyo, mkoa wa kwanza kuhusishwa ni Rock City Mwanza ambapo Vanessa Mdee pamoja Juma Jux watawasili na kutoa burudani June 30,2018.

“Kwanza Kabisa Thanks To The Lord najiona kabisa nikitua #Mwanza#Fimbo ake mtu #ILAM #MapenziNaPesaThe Vanessa Mdee and Jux Tour. Leo tutaanza kutambulisha wasanii watakao ungana nasi Mwanza. Wewe unataka kumuona nani pale kati? #InLoveAndMoneyTour“

Mkoa wa Mwanza ndio utafungua tour hiyo ya Inlove & Money ikiwa ndio itakua mara ya pili kwa Vanessa Mdee pamoja Juma Jux kufanya performance katika mkoa huo ambapo mara ya kwanza ilikuwa kwenye Fiesta 2017.

Jeshi la Polisi Lamshikilia Mwanaume Aliyemuua Mhadhiri wa UDOM

0
0
Jeshi la Polisi Lamshikilia Mwanaume Aliyemuua Mhadhiri wa UDOM
JESHI la Polisi Mkoani Dodoma linamshikilia mtuhumiwa wa mauaji a;liyekuwa mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Rose Manfredy Mndenye ( 31) aliyedaiwa kuuawa na mume wake kwa kile kinachosemekana kuwa ni sababu za wivu wa mapenzi.



Akizungumza na wanahabari jijini Dodoma, leo Jumatatu, Juni 18, 2018, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amesema Jeshi hilo limefanya uchunguzi na kubaini mtuhumiwa huyo alikuwa amejificjha mkoani Morogoro, hivyo likafanya jitihada za kumnasa na kumtia mikononi mwa dola.






“Baada ya uchunguzi tuliofanya, tumemkamata mtuhumiwa wa mauaji ya Mhadhiri wa (UDOM), marehemu Rose Manlfred Mdenye aliyeawa kwa kukatwa katwa na visu na mtu anayedaiwa kuwa ni mume wake eneo la Swaswa mtaa wa Sarungai.



“Tumemkamata akiwa amejificha katika Kijiji cha Chiwachiwa, Kata ya Mbingu wilayani Ifakara mkoani Morogoro, na sasa mtuhumiwa yupo sero, tunaendelea na uchunguzi zaidi na tukikamilisha tu tutamfikisha mahakamani.



Tukio la kuuawa kwa Rose liliyokea Maei 25, mwaka huu majira ya usiku baada ya mumewe huyo kudaiwa kumcharanga visu sehemu mbalimbali za mwili kisha kutokomea kusikojulikana.

Wafikishwa Mahakamani Baada ya Kukutwa na Ngozi ya Chui

0
0
Wafikishwa Mahakamani Baada ya Kukutwa na Ngozi ya Chui
Wakazi wawili wa Mburahati Kisiwani, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu shtaka la kukutwa na ngozi ya chui.

Akizungumza leo Juni 18 Wakili wa Serikali, Kandidi Nasua aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Vicent Mteleka(75) na Christopher Kipilili( 51).

Wakili Nasua, amedai mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Hamisi Ally, kuwa washtakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na shtaka moja la uhujumu uchumi.

Nasua alidai kuwa, Mei 9, 2018 katika eneo la Mburahati Kisiwani , wilaya ya Kinondoni, washtakiwa walikutwa na ngozi ya chui yenye thamani ya Sh 8milioni bila kuwa na leseni kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyama Pori nchini, huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Washtakiwa baada ya kusomewa shtaka linalowakabili,  hawakutakiwa kusema chochote kwa kuwa Mahakama hiyo haina  uwezo wa kusikiliza shauri hilo.



Hata hivyo, Wakili anayewatetea washtakiwa hao, Amon Ndunguru ameiomba Mahakama iwapatie dhamana wateja wake kwa sababu wamekaa mahabusu kwa muda mrefu kabla ya kufikishwa mahakamani.

“Kuzuia dhamana bila kuwa na hati kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini ni kwenda kinyume na sheria, hivyo naiomba mahakama yako iwapatie dhamana wateja wangu”amedai Wakili Ndunguru.

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote, Hakimu Ally amesema kwa mujibu wa thamani ya nyara zilizokamatwa ni chini ya Sh 10milioni, hivyo mahakama hiyo inayo mamlaka ya kutoa dhamana.

Hakimu Ally aliyataja masharti ya dhamana kuwa ni kila mshtakiwa kuwa na mdhamini mmoja wa kuaminika, anayetambulika kisheria atakayesaini bondi ya Sh9 milioni.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 2, mwaka huu itakapotajwa na mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, amerudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Hamisa Mobetto atoa kali, awaonea huruma wabongo

0
0

Mwanamitindo Hamisa Mobetto bado anachukua headlines zake za kiburudani Bongo. 

Time hii Hamisa amesema anatamani kuondoka Tanzania ila anawaza wale wanaomzunguka wataishi vipi. Kupitia Instagram ameandika; 

" Sometimes, Natamani Kuondoka Tanzania nafika hadi airport ila najiuliza Watanzania Wenzangu Wataishije Bila Mimi," 

Hamisa Mobetto amekuwa hakauki kwenye vyombo vya habari hasa mitandaoni hasa pale alipoweka wazi kuwa baba wa mtoto wake wa pili ni Diamond Platnumz. 

Si mtu wa kusafiri sana nje ya Tanzania, mara ya mwisho kuweka wazi kuwa yupo nje ya nchi ni pale alipoenda nchini Uganda kwa ajili ya party yake, Gal Power iliyofanyika December 21, 2017.

Tanzania Inaongoza Kwa Uchumi Kusini Mwa Jangwa La Sahara-majaliwa

0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema taarifa ya Kongamano la Uchumi la Dunia la mwaka 2018 inaonesha kuwa Tanzania inaongoza kwa kuwa na uchumi jumuishi miongoni mwa nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.


Amesema hali hiyo, imetokana na Tanzania kufungua fursa za ujasiriamali ambapo kuna zaidi ya biashara milioni tatu zinazokuwepo kila mwaka, lengo la nchi ni kuhakikisha kuwa uchumi unakua na unamgusa kila Mtanzania hususan mwananchi wa kawaida.


Waziri Mkuu ameyasena hayo leo (Jumatatu, Juni 18, 2018) wakati akifunguaKongamano la Tatu la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa LAPF, jijini dodoma.


“Pia, huduma za fedha jumuishi ni kigezo ambacho kimeiweka Tanzania mahala pazuri kwenye uchumi jumuishi ambapo zaidi ya Watanzania milioni 30 wamekuwa wakifanya miamala mbalimbali ya fedha kupitia simu za mkononi na hivyo kuongeza huduma za fedha kufikia asilimia 65,” amesema.


Amesema huduma za msingi za kijamii kama vile elimu, afya na kupungua kwa rushwa katika utoaji huduma za umma pamoja namtandao wa miundombinu ya barabara ambayo huwezesha wananchi wengi kujishughulisha na shughuli za kiuchumi ni kigezo kingine kilichozingatiwa katika kuipatia Tanzania nafasi hiyo.


Waziri Mkuu ameongeza kwamba Serikali inaamini kuwa uchumi wa viwanda ukiimarika uchumi utakuwa kwa kasi kubwa na matokeo yake yataonekana wazi kwa kupanua wigo wa ajira, soko la huduma na shughuli nyingine za kiuchumi.


Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema suala la uchumi wa viwanda kuelekea uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 ni moja ya ajenda muhimu ya Serikali ya Awamu ya Tano, hivyo amezitaka sekta zote zihakikishe zinatoa mchango mkubwa kwenye uchumi wa viwanda.


Pia amesema suala la uwezeshaji wananchi kiuchumi lazima liende sambamba na uwezeshaji vijana kujiajiri kama inavyoelekeza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015. “Ilani inatambua kwamba kuwawezesha wananchi kiuchumi ni hatua ya msingi katika kujenga Taifa lililoimarika kiuchumi na lenye lengo la kujitegemea,”.


Aidha, Ilani pia, inasisitiza kuhusu umuhimu wa kuhamasisha ushiriki wa Sekta binafsi katika kuwezesha wananchi kiuchumi, hivyo ni muhimu kukamilisha taarifa ya uwezeshaji kutoka kwa wadau wa sekta binafsi, ili Serikali iweze kuona mchango wa sekta binafsi katika kuwawezesha wananchi kiuchumi.


Waziri Mkuu amesema utekelezaji wa malengo hayo ya uwezeshaji wananchi katika maeneo ya fursa za mafunzo ya ujasiriamali na mikopo ya masharti nafuu ni muhimu sana katika kupambana na umaskini wa kipato.


Amesema kwa kutambua umuhimu wa ajenda ya uchumi wa viwanda, ndiyo maana makongamano ya uwezeshaji yamekuwa yakiweka mkazo kwenye masuala ya viwanda. Hali hiyo pia, inajidhihirisha katika kaulimbiu ya Kongamano la Tatu ambayo ni: “Viwanda: Nguzo ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi”.


Hivyo Waziri Mkuu ameongeza kwa kusema, “tuendelee kuhimiza kuhusu kutekeleza uchumi wa viwanda kwa lengo la kuwawezesha wananchi wetu kiuchumi na kuhakikisha kuwa tunafikia lengo la kuwa na  uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025,”.


Kongamano hilo lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) limehudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bibi Jenista Mhagama, Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba, Waziri Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage na Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Bw. Suleiman Jafo.


Wengine ni Wakuu wa Mikoa mbalimbali, Makatibu Wakuu wa Wizara, Wakuu wa Wilaya ya Mkoa wa Dodoma, Makatibu Tawala wa Mikoa, Mwenyekiti na Wajumbe wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi,Wakurugenzi wa Halmashauri za Mamlaka za Serikali za Mitaa,


Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bibi Beng’ Issa, wadhamini wa Kongamano hilo na Wawakilishi kutoka katika taasisi mbalimbali za Serikali na Sekta binafsi.


IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

0
0

Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Huyu Ndiye Mwanamume Aliyeanzisha Kombe la Dunia

0
0
Huku mashindano maarufu zaidi ulimwenguni yakiendelea Urusi, ni wapenzi wachache sana wa kandanda wanaojua chanzo cha mashindano ya Kombe la Dunia.

Mashindano hayo yalianzishwa na mtu mmoja mbunifu kutoka Ufaransa. Jules Rimet, aliyezaliwa Oktoba 14, 1873, Theuley, Mashariki mwa Ufaransa, na Mkatoliki alianzisha Red Star Sports Club 1897.

 Mfaransa huyo alihusika katikauzinduzi wa shirikisho la kusimamia kandanda ulimwenguni(FIFA) mwaka wa 1904. Lakini juhudi zake za kuanzisha jamii ya kandanda ya kimataifa zilitatizwa na vita vya kwanza vya dunia mwaka wa 1914

Baada ya vita hivyo kuisha, ambapo alikuwa mwanajeshi wa Ufaransa, Rimet alichaguliwa kama rais wa FFF(French Football Federation) mwaka wa 1919. Machi 1, 1921, Rimet alifanywa kuwa rais wa FIFA ambapo alilenga kuanzisha mashindano ya ulimwengu wote.

 Mipango yake ya Kombe la Dunia hata hivyo ilipata changamoto kubwa kutoka kwa vyama vidogo vya kandanda na Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki(IOC) chini ya Pierre de Coubertin.

Tuzo la mashindano hayo lilipewa jina la raia huyo wa Ufaransa, 1930, ambapo mataifa kadhaa ya Amerika Kusini yalizuru Uruguay kwa mashindano hayo.

Baada ya kufaulu kwa mashindano hayo, Rimet alisalia rais wa muda mrefu zaidi wa FIFA-kwa miaka 33. Alianzisha mashindano hayo na wanachama 12, lakini alipoondoka, yalikuwa na wanachama 85. Aliaga dunia 1956, akiwa na miaka 83.
Kombe la Dunia la Kwanza


“Pesa Haiishi Utamu” - Kitwanga

0
0
“Pesa haiishi utamu” - Kitwanga
Mbunge wa Misungwi (CCM) Charles Kitwanga, amewataka wananchi na wabunge kutoshangaa serikali kudaiwa madeni, kwasababu pesa inatabia ya kutotosheleza mahitaji yote  na vilevile pesa haiwezi kuisha matumizi yake.


Kitwanga amesema hayo leo Juni 18, 2018 Bungeni Jijini Dodoma, alipokuwa akichangia hoja mjadala wa mapendekezo ya Bajeti kuu ya Serikali katika mwaka wa fedha 2018/2019 na kusema kuwa Bajeti hiyo imetimiza viwango vya kuiwezesha Tanzania kufikia uchumi wa viwanda.

“Tabia ya pesa zipo mbili, kwanza pesa huwa hazitoshi, pili pesa huwa haiishi utamu kwahiyo ndugu zangu wa mkono wangu wa kulia, kilasiku wanapokuwa wanalalamika kwamba tuna madeni ni kwasababu pesa siku zote huwa haitoshi na utamu hauishi” amesema Kitwanga

Kitwanga ameongeza kuwa, mapendekezo hayo ya Bajeti yamelenga katika mpango wa maendeleo 2025 kwa kufikia uchumi wa kati na kuitaka Serikali kuondoa vikwazo, ikiwemo kutumia muda mrefu wa kupewa leseni kwa watu wenye lengo la kuanzisha viwanda nchini.

Bunge kwasasa linajadili mapendekezo ya mapato na matumizi ya Serikali kuu katika mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo Serikali imepanga kukusanya na kutumia jumla ya shilingi trilioni 32.4 ya kugharamia miradi ya maendeleo na mahitaji ya kawaida.

Rais Magufuli amemteua Jaji Mstaafu Lubuva kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

0
0
Rais Magufuli amemteua Jaji Mstaafu  Lubuva kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais John Pombe Magufuli amemteua Jaji Mstaafu Damian Zefrin Lubuva kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.



Soma taarifa kamili:

Niyonzima Aondolewa Kikosini

0
0
Kiungo wa Simba, Haruna Niyonzima amepumzika kucheza soka na sasa atakuwa akipata matibabu kuhakikisha anarejea vizuri dimbani na hatakuwa katika kikosi kitakachocheza michuano ya Kagame.


Niyonzima alirejea uwanjani baada ya kupata matibabu nchini India ambako alipata matibabu kabla ya kurejea nchini na kuanza mazoezi taratibu, aliumia wakati wa michuano ya SportPesa Super Cup ingawa mechi ya mwisho ya fainali hakucheza kwa kuwa alikuwa na kadi mbili za njano.

Habari kutoka Simba zimeeleza, Niyonzima aliumia licha ya kwamba alikosa mechi ya mwisho kutokana na kadi, hivyo atalazimika kukosa michuano ya Kagame, ndiyo maana ni kati ya wachezaji watakaopumzishwa katika michuano ya Kagame.

Kiungo huyo Mnyarwanda amekuwa na wakati mgumu tokea ametua Simba kutokana na kuandamwa na majeraha.



Basi la SABCO Lapata Ajali na Kuua Mtu Mmoja

0
0
Basi la SABCO Lapata Ajali na Kuua Mtu Mmoja
Mnamo tarehe 18/06/2018 majira ya saa 13:15hrs mchana katika barabara ya Usagara   – Kigongo Ferry maeneo ya Kingongo Ferry kijiji cha kigongo Ferry kata ya Bukumbi  tarafa ya usagara wilaya ya misungwi mkoa wa mwanza, gari no. T.581 ARL  aina ya scania bus kampuni ya SABCO  iliyokuwa inatokea Mwanza kuelekea Msalala wilaya ya Nyan’gwale mkoa wa Geita likiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la Idd Omary miaka 40, Mnyamwezi, mkazi wa Mkuyuni- Mwanza, liiligonga ofisi ya Ferry na kusababisja kifo kwa Zabroni Malando, miaka 37, Msukuma, mfanyabiashara na mkazi wa Sengerema, aliyefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya bukumbi.

 Aidha pia ajali hiyo ilisababisha majeruhi kwa watu kumi (10), wanaume sita (6) na wanawake wa nne (4), wote wapo katika hospitali ya Bukumbi wakiendelea kupatiwa matibabu.

Aidha kati ya hao majeruhi mahututi wapo watatu ambao ni Idd Omary, miaka 40, dereva wa gari lililopata ajali, Ibula  Raphael, miaka 34, msukuma, mkulima na mkazi wa Busolwa na Sophia Lugihila miaka 45, msukuma, mkulima na mkazi wa msalala na wote wamepelekwa hospitali ya Sekouture iliyoko Mwanza kwa matibabu zaidi.

Chanzo cha ajali ni kuferi kwa breki za gari hali iliyopelekea gari hilo kugonga ofisi za ferry na kusababisha kifo na majeruhi.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Bukumbi kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi pindi uchunguzi ukikamilika utakabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Kamishina msaidizi wa polisi Mkadamu Khamisi Mkadamu anatoa pole kwa wote hususani kwa  ndugu na jamaa wa marehemu wa ajali hiyo, tunawaombea kwa mwenyezi mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu. Aidha pia tunawaombea majeruhi wapone haraka ili waweze kuendelea na kazi.

Polisi Yamkamata Aliyesababisha Ofisi Ya Ridhiwani Kuteketea Kwa Moto Akamatwa

0
0
Polisi Yamkamata Aliyesababisha Ofisi Ya Ridhiwani Kuteketea Kwa Moto Akamatwa
JESHI la polisi mkoani Pwani, lina mshikilia Mariam Joakim mwenye miaka (52),kwa kosa la kudaiwa kusababisha kuteketeza kwa moto ofisi ya mbunge wa jimbo la Chalinze ,Bagamoyo Ridhiwani Kikwete .

Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Jonathan Shanna ,alithibitisha juu ya taarifa hiyo .

Alisema tukio hilo limetokea June 17 majira ya saa ya 18:00 ambapo jeshi hilo lilipokea taarifa kutoka kwa raia mwema kwa njia ya simu ,kuwa jengo la ofisi ya mbunge huyo linawaka moto.

“Katika tukio hilo ofisi yote imeteketea kwa moto na kuokolewa vitu vichache” alisema kamanda Shanna.

Kwa mujibu wa kamanda hiyo chanzo cha moto kimesababishwa na mtuhumiwa Mariam,ambae anaeleza aliwasha moto eneo la nyuma ya jengo hilo kwa lengo la kuchoma majani kisha moto ukamzidi na kushika majani na mabomba yaliyokuwa kando ya jengo hilo.

Anasema hatimaye moto uliunguza jengo lote.Thamani ya uharibifu na vitu vilivyoungua haijajulikana na mtuhumiwa yupo mbaroni kwa mahojiano zaidi.

Nae mbunge wa jimbo hilo ,Ridhiwani aliwashukuru wote walioguswa na mtihani alioupata.

“Mtihani unapita, asubuhi saa tano june 19 ,mungu akipenda nitakwenda angalia athari ya moto, na kueleza kwa ujumla tukio hili na hasara iliyotokea” alielezea Ridhiwani.

Mwanamume Afumaniwa Akijifanya Mwanamke Kuwanyemelea Wanaume Wenzake (Picha)

0
0
Mwanamume wa umri mdogo ambaye alijifanya mwanamke ili kuwanyemelea wanaume wenzake kimapenzi amekamatwa Uganda.

Wakati wa mahojiano, alisema alikuwa na mpango wa kupata pesa kutoka kwa wanaume hao. Kulingana na ripoti, alikamatwa alipokuwa akimchezea mwanamume mmoja kwa lengo la kumpora. Iliripotiwa pia kuwa mshukiwa huyo alikamatwa na maafisa wa polisi.

Kwa kutazama picha, mwanamume huyo alikuwa amejimwaya mavazi ya kike pamoja na herini na ‘wig’.

Alikuwa pia amejipaka vipodozi ili aonekane mwanamke kamili. 

Lukaku Afanya Kweli Apiga Magoli Mawili Michuano Kombe la dunia

0
0
Lukaku Afanya Kweli Apiga Magoli Mawili Michuano Kombe la dunia
Straika wa Ubelgiji na klabu ya Manchester United, Romelu Lukaku amefanikiwa kufunga magoli mawili na kuisadi timu yake ya taifa kuchomoza na ushindi wa jumla ya mabao 3 – 0 dhidi ya Panama mchezo wa kundi G wa michuano ya kombe la Dunia inayo endelea kutimua vumbi huko nchini Urusi.



Bao la kwanza la Ubelgiji likifungwa na Dries Mertens dakika 47 ya kipindi cha pili kisha Lukaku kutupia mawili kimyani dakik ya 69 na 75 na hivyo kuufanya mchezo huo kumalizika kwa jumla ya mabao 3 – 0.

Kikosi cha Ubelgiji: Courtois, Alderweireld, Boyata, Vertonghen, Meunier, Witsel, De Bruyne, Carrasco, Mertens, E. Hazard, R. Lukaku.

Wachezaji wa akiba wa Ubelgiji: Mignolet, Casteels, Kompany, Dendoncker, Hazard, Tielemans, Dembele, Fellaini, Chadli, Januzaj, Batshuayi.

Kikosi cha Panama: Penedo, Murillo, Escobar, R Torres, Davis, Gomez, Godoy, Cooper, J Rodriguez, Barcenas, Perez.

Wachezaji wa akiba: Claderon, A Rodriguez, Cummings, G Torres, Diaz, Machado, Pimentel, Arroyo, Ovalle, Tejada, Avila, Baloy.

Download Hapa Application ya Udaku Special Kwenye Simu Yako Kushuhudia Vimbwanga Mtaani na Stori za Mapenzi

Zifahamu Faida 5 za Kununiana na Mpenzi Wako Ndani ya Mahusiano yawe ya Ndoa au Uchumba

0
0
Mapenzi yana wigo mpana mno ambao mtu anapaswa kuuangalia kwa jicho pana na akili pembuzi kabla ya kuingia, namaanisha kwamba ni lazima kuchunguza kina cha maji kabla ya kuzamia. Sasa basi, zifuatazo ni faida tano utakazozipata ukiwa umenuniana na mpenzi wako.

HUSAIDIA KUPUNGUZA MIGOGORO
Ni ukweli usiopingika kuwa, katika hali ya kawaida, ukiwa mbali na mtu fulani katika jamii unayoishi ni vigumu sana kujikuta umekwaruzana naye. Hii ni kwasababu utakuwa hauingiliani naye katika mizunguko yako, vivyo hivyo kwa wapenzi walionuniana.

Hali hii hupunguza kabisa migogoro ya hapa na pale, kwani hiki ni kipindi ambacho mtakuwa mbalimbali jambo ambalo huepusha maudhi ya kibinadamu.

Mfano, yawezakana katika kipindi mlichonuniana na mpenzi wako, uliingia ujumbe wa mapenzi kwenye simu yake kutoka kwa mtu aliyekosea namba. Kwa kuwa hauko naye karibu jambo hili halitakuumiza maana hutaelewa nini kimeendelea tofauti na kama ungelikuwa naye karibu.

Kwa hiyo kuna baadhi ya maumivu na maudhi ambayo utaepukana nayo kwa kipindi cha kununiana kwenu. Ni kweli kabisa kwamba hupunguza migogoro na mitafaruku ya hapa na pale, umeelewa mpenzi msomaji wangu? Haya twende kwenye faida ya pili.

KUBAINI TABIA X ZA MWENZAKO
Hiki ni kipindi ambacho sasa kitakusaidia wewe kubaini tabia na mienendo mibaya ya mwenzi wako. Hii ni kwa kuwa utakuwa mbali naye hivyo naye hujiona kuwa yuko huru kufanya jambo lolote analoona kuwa linafaa bila kujali uwepo wako kwani kila mtu hana ‘time’ na mwenzake.

Kama kuna asili ya maisha yake ambayo aliiacha baada ya kuingia katika uhusiano na wewe, ambayo ni mbaya zaidi sasa hapa ataanza kuirudia kwa kujiona kuwa hana mtu wa kumzuia na kumbana.

Kama ni mlevi kupindukia, mchafu, muongo na tabia nyingine mbaya za kufanana na hizi basi ataanza kuzionesha katika kipindi ambacho mmenuniana.

KUPATA MUDA WA KUTAFAKARI ZAIDI
Hapa naomba nieleweke vizuri kabisa kwamba, ninapoongelea suala la kutafakari zaidi katika kipindi ambacho wewe hauna maelewano mazuri na mwenzi wako, namaanisha kuwa utapata muda mzuri zaidi wa kutafakari penzi lenu kwa ujumla.

Ni kipindi kitachokuongoza wewe kuwa na uelewa wa ni aina gani ya mpenzi uliyenaye. Kivipi? Ni kwamba, katika muda huu mara nyingi utataka kupata suluhu ya kununiana kwenu, lakini pia katika kutafuta suluhu hiyo utapata fursa ya kutafakari kwa kina juu ya penzi lenu huku ukimpima mwezi wako kwa mtazamo chanya.

KUFAHAMU AINA YA MARAFIKI ZAKE
Si kila rafiki wa mwenza wako ana nia nzuri na uhusiano wenu au anafurahia penzi lenu. Mathalani, labda wewe ni msichana na pengine miongoni mwa rafiki zake kuna mmoja au wawili ambao hutamani sana kupata penzi lako.

Sasa katika kipindi ambacho utakuwa umenuniana na mpenzi wako basi itakuwa ni nafasi nzuri kwao kuitumia kunyunyizia sumu ya kumponda huku wakikutamkia maneno ya kukushawishi, hivyo utakuwa umeelewa ni aina gani ya marafiki alionao mwenzi wako.

Hii si kwa msichana tu, hata kwa wanamume kwani huenda kati ya rafiki wa ‘girlfriend’ wako, kuna wanaokutamani, sasa wakiona huna uhusiano mzuri na mpenzi wako, watatumia nafasi hii kukuambia maneno ya uongo juu yake na kukuonesha kila dalili za kukutaka.

Hivyo utakuwa umefahamu ni aina gani ya rafiki ambao mpenzi wako anao. Tambua kwamba, marafiki wengi wana tabia zinazofanana.

KUBAINI AINA YA PENZI ALILONALO KWAKO
Katika kipindi hiki, utaweza kuelewa ni aina gani ya penzi alilonalo huyo mtu wako juu yako. Kwa mpenzi aliye na hisia za dhati kabisa kwako, katika kipindi hiki atakuwa ni mtu wa kutafuta njia ya kupata suluhu ya tatizo lenu.

Pamoja na kwamba wewe utakuwa umenuna, bado yeye ataonesha kukujali kama kawaida, atakupigia simu za hapa na pale yaani ilimradi tu asikie angalau sauti yako, lengo lake likiwa ni kutaka kurejesha ukaribu ambao sasa anaona kama akiupoteza itakuwa ni maumivu kwake.

Kwa mantiki hiyo basi, utagundua ni kwa jinsi gani anathamini penzi lenu na ni aina gani ya penzi alilonalo kwako. Yote haya utabahatika kuyajua kupitia kipindi cha kununiana kwenu.

Hata hivyo, niwatahadharishe kwamba, kuandika haya isiwe ni tiketi ya wewe sasa kuanza kununiana na mpenzi wako eti kwa kigezo kwamba utapata nafasi ya kumfahamu, la hasha!
Siku zote katika uhusiano wako epuka maudhi na migogoro isiyokuwa ya lazima.

Sio Kila EX Wako Anayeomba Mrudiane Anamaanisha! Wengine Huomba Kurudi Ili Wakutesti Tu

0
0
Sio Kila EX Wako Anayeomba Mrudiane Anamaanisha! Wengine Huomba Kurudi Ili Wakutesti Tu Jinsi Ulivyo Mbulula,Jinsi Usivyo Na Msimamo Na Jinsi Ulivyo CHEAP Na Huna Misimamo Wala Future.
.
Jitu Mmeachana Miezi 6,Leo Linakutesti Lirudishe Majeshi,Na Wewe Ulivyo Kiazi,Upo-Upo Tu,Ina Maana Miezi Yote Hii Ulikuwa Umeganda Unasubiria Rehema Zake Ama?? Kurudia Matapishi Ya EX Ukitegemea Amebadilika Ni Sawa Na Kupika Sufuria La Makande Kwa Mshumaa,Utaambulia Masizi Tu..
.
Kipi Kipya Kakiona Kwako Hadi Arudi??Nini Kilimshinda Huko Nyuma Ambacho Leo Anakiweza Anataka Kurudi??Akafie Mbele Huko.
.
KUWA NA MSIMAMO,Ukisema Its Over Umaanishe,Sio Unakuwa Na Hisia Zinapepea Tu Kama Bendera Ya Katibu Kata Wa Kishumundu... Mtu Kama Hajielewi Achana Nae,Siku Akijirudisha Mwambie Kwanza Akapimwe Minyoo Ya Kinyarwanda.
.
Umekazana Kuwaambia Marafiki Zako 'Siku Hizi Hakuna Mapenzi Ya Dhati Watu Wote Majanga Tu',Nani Amekwambia Hayapo?? Yapo Sana Ila Wewe Unatumia Mbinu Tofauti..
.
Huwezi Kusoma Degree Ya Law Halafu U-Apply Kazi Ya Chief Accountant Wa Bodi Ya Tumbaku...Kila Siku Utasingizia Balance Sheet Haina Jurisprudence..Lawyersl

Mmenielewa! Acha Kudate Watu Wasiojielewa,Usidate Kwa Sababu Uko Lonely,Usiwe Desperate Kuingia Mahusiano Kwa Sababu Shosti Zako Wanakusimulia Walivyopelekwa Ruwenzori Waterfalls..
.
Ingia Kwenye Mahusiano Pale Moyo Wako Ukiwa Tayari Na Mtu Uliyemfia Kihisia Na Amekuwa Approved Na Veins,Auricles,Na Aorta Za Moyo Wako Kwamba He/She Is Really The One.. Unadate Na Mtu Ambaye Mustakabali Wake Mwenyewe Haujui,Ukimuuliza Anataka Kuwa Wapi Ndani Ya Miaka 5 Ijayo Anakwambia Mungu Anajua Dont Worry,Halafu BBM Na Instagram Unajiita Baby Ake Mie Iam In Love..

Utaishia Kufua Boxer Hadi Kucha Zinukie Gololi! Mbwa Kamwe Hashughuliki Na Kesi Za Paka Kufungiwa Kabatini.Date The Right Person,With Right Reasons,In A Right Time Uone Kama Mapenzi Hayapo...
.
Nikipanic tena nitarudi

Huyu Hapa Binti Mrembo Kuliko Wema Sepetu Lakini Anafanya Kazi Chafu Kujinasua Kimaisha

0
0
Bila shaka, kila mtu hutia bidii awe mwanaume au mwanamke ili kujikimu kimaisha. Zaidi ni kwamba, kwa wengi haitajalisha aina ya kazi bora tu kipato kinakidhi mahitaji yake.

Wasomi wengi huzikwepa kazi nyingi kwa madai kuwa ni chafu, za kishamba na zisizowafaa watu walio na shahada, ila wengine huzichukulia kama kazi rasmi na bila shaka kipato chao cha kila siku huwa ndiyo furaha yao.

Binti huyo, Ogechukwu Kate, ambaye alifuzu kwa shahada ya kwanza katika chuo kikuu cha Ebonyi aliamua kuasi daraja lake na kujichafua kwa kazi ya makaa ili kujipa kipato chake 

Ni kazi ambayo humpa kipato kikubwa na anayoifurahia kama alivyochapisha katika ukurasa wa Facebook.

Alidai kuwa makaa ni dawa zuri sana kwa ngozi hivyo watu hawafai kuhofia kuhusu ngozi.
"...Usijali kuhusu ngozi kuharibika kwani kwa makaa ni tofauti kwani husaidia kusafisha. Husawazisha mafuta ya ngozi. Kwani huoni vile huwa mchafu na mweusi sana nikiwa kazini lakini safi sana baada ya kuoga," Alisema Kate.  

Hamisa Mobetto Atoa Mpya 'Kuna Muda Natamani Kuondoka Tanzania ila....."

0
0
Muigizaji wa Bongo movie na mzazi  mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto amedai kuwa kuna muda anatamani kuondoka Tanzania.

Hamisa ambaye ameendelea kushika headlines kwani tangu alivyotangaza kuwa ana ujauzito wa Diamond mwaka jana basi hajatoka midomoni kwa watu tena.

Hamisa siku ya jana alizuahgumzo baada ya kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa anatamani kuondoka Tanzania lakini kila akifika airport anajuuliza Watanzania wataishije bila yeye.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Hamisa aliandika:

Sometimes, Natamani Kuondoka Tanzania nafika hadi airport ila najiuliza Watanzania Wenzangu Wataishije Bila Mimi“.

Hamisa amekuwa akiongelewa sana Kwenye mitandao ya kijamii siku hizi tangu arudiane na Diamond na kiukweli imekuwa burudani kwa mashabiki zao hasa ukimuweka Diamond huku Zari pale na Hamisa huku.
Viewing all 104416 articles
Browse latest View live




Latest Images