Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live

Sasha Atishiwa Kuuliwa Akimbilia Polisi

$
0
0
Sasha Atishiwa Kuuliwa Akimbilia Polisi
VIDEO Queen mwenye figa matata Bongo, Sasha Kassim amelazimika kukimbilia katika kituo cha polisi cha Mtongani jijini Dar akidai kuwa, mwanamke mmoja aliyemtaja kwa jina la Mama Aisha anatishia kumuua.

Akizungumza na gazeti hili, Sasha alisema kuwa, kuna wakati aliwahi kudaiwa kupora mume wa mama huyo na kuanzia kipindi hicho amekuwa akipokea vitisho vya hapa na pale.

“Huyu mama (mama Aisha) alipoachana na mumewe, akadai eti mimi ndiye nimemvunjia ndoa, nikashangaa sana lakini hivi karibuni nimepata taarifa kuwa anapanga kunimwagia tindikali. “Nilipata hofu sana lakini jamani labda leo niseme ukweli kwamba sikuwa na uhusiano na mume wa mama huyu, nilikuwa naenda pale nyumbani kwake maana dada yangu anaishi jirani.

“Yeye anashikilia kuwa mimi nilionekana nyumbani kwake kwenye kochi, ni kweli kabisa ila ulitokea msiba, nikawa naogopa kukaa kwa dada yangu, ndo’ nikaenda pale nyumbani kwa yule baba kama jirani tu lakini hakuna ishu ya mapenzi, aache kuniwazia mabaya kabisa,” alisema Sasha na kuongeza:

“Nimeona nisikae tu maana linaweza kunitokea lolote, nimeenda kufungua jalada kwenye kituo cha Polisi cha Mtongani lenye namba MT\ RB\1477\2018 KUTISHIA KUUA KWA MANENO.” Kufuatia malalamiko hayo ya Sasha, mwandishi wetu alimtafuta Mama Aisha kupitia simu yake ya mkononi na alipopatikana alifunguka hivi:

“Jamani huyo Sasha amejikosha kwani alichokifanya anakijua yeye, mimi sijawahi kusema kwa mtu eti nitamwagia tindikali.” Hivi karibuni Mama Aisha alimtuhumu Sasha kumpora mume wake na kudai kuwa ndiye aliyesababisha ndoa yake kuvunjika.

Nisha Afunguka Kuhusu Kibenteni Kilivyomgeuza ATM

$
0
0
Nisha Afunguka Kuhusu Kibenteni Kilivyomgeuza ATM
STAA wa filamu na muziki Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amefunguka jinsi alivyoteswa na penzi la mwanaume mwenye umri mdogo ‘kibenteni’ kutokana na kumgeuza ‘ATM’ kwa kumuhudumia kama mwanaye.

Nisha aliiambia Za Motomoto News kuwa wakati akiwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na kibenteni huyo ambaye hakutaka kumtaja jina alikuwa akimnunulia kila kitu na kumpa fedha na kumuhudumia kama mtoto wake lakini baadaye alikuja kushtuka kuwa anachunwa na kua­mua kuachana naye.

“Nimejifunza sana na nime­koma kuwa na uhusiano na mwanaume ninayemzidi umri na kipato maana nilijikuta nime­ingia kwenye uhusiano huo bila kujua kwamba kibenteni huyo ni tege­mezi ambaye alinifanya kama mashine yake ya ATM na kuniko­moa kuja kushtuka ameshanikwan­gua vya kutosha,” alisema Nisha.

Hata hivyo Nisha aliwataka mastaa wa kike kuwa makini wanapoing­ia kwenye uhusiano kwani kwa sasa kuna wanaume vibenteni ambao wanatafuta wanawake wanaowazidi kipato na umri wakiwa na dhu­muni la kuwachuna fedha zao.
Chanzo: Global Publishers

Mume Amuua Mkewe kwa Kumchoma Kisu naye Ajiua

$
0
0
Mume Amuua Mkewe kwa Kumchoma Kisu  naye Ajiua
Mwanaume mmoja amuua mkewe kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake kisha na yeye mwenyewe kujichoma kisu tumboni na kufariki dunia wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amesema tukio hilo limetokea katika nyumba za kulala wageni ya 'Angel Guest House' iliyopo kijiji cha Kanyara Wilayani Sengerema mkoani Mwanza ambapo wanandoa hao walifikia kwaajili ya mapumziko.

Aidha, Kamanda Msangi amesema inadaiwa kuwa wanandoa hao walikuwa na ugomvi wa muda mrefu katika familia yao, hali iliyopelekea mwanamke kuondoka nyumbani kwao kijiji cha Bukokwa kisha kwenda kupumzika kwa wakwe zake kijiji cha Kanyara.

Msikilize hapa chini Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishina wa Polisi Ahmed Msangi akielezea kiundani juu ya tukio hilo.

Canada Yaruhusu Kuvuta Bangi Hadharani

$
0
0
Canada Yaruhusu Kuvuta Bangi Hadharani
Canada imepitisha sheria rasmi kwa nchi nzima inayoruhusu matumizi ya bangi.

Sheria hiyo hatimaye ilishinda kwa kupata kura za ndiyo 52 zinazoruhusu matumizi ya bangi hadharani,huku kura 29 za maseneta zikisema hapana.


Raia wa Canada wataruhusiwa kununua na kutumia bangi kihalali kuanzia mapema mwezi Septemba
Kwa sheria hiyo sasa raia wa Canada wataruhusiwa kununua na kutumia bangi kihalali kuanzia mapema mwezi Septemba mwaka huu.

Kumiliki bangi ilikuwa ni kosa kisheria tangu mwaka 1923 lakini matumizi ya bangi kama dawa yaliruhusiwa kisheria tangu mwaka 2001.

Kutokana na kupitishwa kwa sharia hiyo sasa itawachukua majimbo,Manispaa na mamlaka takribani wiki kati ya nane hadi 12 kutengeneza masoko mapya ya kuuza bangi.

Lakini pia muda huu kabla ya kuanza kutumika kwa bangi rasmi,utatumika na Polisi kuandaa mifumo mipya ya kisheria.

Kwa mjibu wa sheria hii mpya mtu ataruhusiwa kuagiza bidhaa hii ya bangi kwa mfumo wa kimtandao kutoka kwa wasambazaji wanaotambulika kisheria.


Umri unaoruhusiwa kununua na kutumia bangi umepitishwa kwa mjibu wa sharia hiyo kwamba ni kuanzia miaka 18,lakini baadhi ya majimbo yamependekeza umri wa kuanzia miaka 19. Ni


Waziri huyo mkuu amesema kuwa sheria za miaka mingi za Canada zinazoharamisha matumizi ya bangi hazina maana kwa kuwa watu nchini Canada ni baadhi ya watumiaji wakubwa wa bangi duniani.

California yaidhinisha matumizi zaidi ya bangi
Kura za maoni zimekuwa zikionyesha kuwa watu wengi nchini Canada wanaunga mkono hatua hiyo.

Hatua ya kuhalalisha matumizi ya bangi kwa burudani nchini Canada yanakuja wakatoi nchi za dunia zinahalalisha bangi inayotumiwa kwa kiwango kikubwa duniani.

Shukuba na Wenzake Mambo Bado Magumu

$
0
0
Shukuba na Wenzake Mambo Bado Magumu
Wakati vita ya kupambana na madawa ya kulevya ikionekana kufanikiwa kwa kiasi flani hapa nchini, taarifa mpya iliyotua kwenye dawati la gazeti hili ni kwamba, hivi karibuni Watanzania watatu wamepandishwa kizimbani Texas, California nchini Marekani kwa tuhuma za kujihusisha na biashara hiyo haramu.



Akizungumza na UWAZI kwa njia ya simu, Kamishna wa Sheria wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya nchini, Edwin Kakolaki amewataja Watanzania hao kuwa ni Ally Haji ‘Shikuba’, Iddy Mfuru na Tiko Adam ‘Tikotiko’ ambao kesi yao imeshaanza kusikilizwa nchini humo.

“Katika uendeshwaji wa kesi hiyo tumekuwa tukishirikiana na Marekani kwa kupeana taarifa mbalimbali kwa kila kinachoendelea.






“Taarifa walizotuletea hivi karibuni ni kwamba wameshawapandisha kizimbani na kuwasomea mashitaka yao ya kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya,” alisema Kakolaki. Alisema watu hao wanashitakiwa kwa makosa ya kusambaza na kujihusisha na biashara hiyo haramu nchini Marekani.



Wakati watuhumiwa hao wakihenyeshwa kortini, hapa nchini mambo yanazidi kuwa moto kufuatia mamlaka ya kuzuia na kupambana na madawa ya kulevya kuonesha kujizatiti kuhakikisha wafanyabiashara wanaotumia njia za panja kuingiza madawa hayo hawafui dafu.



Akizungumzia hilo, Kamishna wa Intelijensia wa Mamlaka hiyo ya kuzuia madawa ya kulevya nchini, Frederick Kibuta alisema cocaine na heroine hazizalishwi hapa nchini, zinatoka nje ya nchi na kuingizwa kwa njia mbalimbali.



“Kwa upande wetu tunapambana kuhakikisha madawa hayo hayaingii nchini kwa namna yoyote, iwe kupitia mipakani au viwanja vya ndege, tumejizatiti vilivyo,” alisema.

TUJIKUMBUSHE YA AKINA SHKUBA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, chini ya Hakimu Mkazi, Cyprian Mkehe Aprili 12, 2017 ilikubali ombi la Wizara ya Sheria na Katiba la kuruhusu mtuhumiwa wa kusafirisha madawa ya kulevya, Shkuba na wenzake wawili, Mfuru na Tikotiko, wasafirishwe kwenda Marekani kujibu mashtaka ya kusafirisha madawa ya kulevya.
Chanzo: Global Publishers

Yanga Kukitangaza Kikosi Watakachobaki Nacho Wiki Hii

$
0
0
Yanga Kukitangaza Kikosi Watakachobaki Nacho Wiki Hii
Klabu ya Yanga wanatarajia kuweka bayana majina ya wachezaji watakaobaki katika kikosi hicho na wale watakaoachwa huku pia wakitangaza maingizo mapya ndani ya kikosi hicho.


Mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu hiyo Hussein Nyika ameeleza hayo huku akisisitiza kuwa staili yao ya kusajili ni ile ile ya kimya kimya na hawataki kuonesha tambo zozote.

 "Tunasajili kimya kimya na mambo yetu yote yatakuwa hadharani pindi kocha wetu atakaporejea kutoka Ufaransa, kila kitu kinaenda sawa na watu wawe watulivu", amesema Nyika.

Nyika ameongeza "Kuhusu wachezaji wetu waliomaliza mikataba tupo katika harakati za kuwaongeza kama kocha bado atakuwa na matumizi nao na akarudi tutatangaza wanaobaki na watakaopelekwa klabu zingine kwa mkopo".

Yanga wanajiandaa na mchezo wa hatua ya makundi katika kombe la Shirikisho barani Afrika huku wakitarajia kukipiga na Gor Mahia ya nchini Kenya Julai 18 mwaka huu.

Ruto Asambaratisha Ngome za Raila Odinga

$
0
0
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto anaendelea kuwakosesha usingizi wapinzani kwa kunyemelea ngome zake za kihistoria huku akijitayarisha kuchukua uongozi wa nchi kutoka kwa Rais Uhuru Kenyatta miaka minne kuanzia sasa.

Ruto amekuwa akizuru maeneo ya mwambao wa Pwani takriban kila mwisho wa wiki kusambaratisha ngome ya Kiongozi wa chama cha ODM na muungano wa Nasa, Raila Odiga.

Makamu wa Rais amefanikiwa kurusha ndoano na kuwanasa samaki wengi wakubwa kama vile nyangumi na papa.

Hatua ya Ruto haijapokelewa vyema na ODM ambayo sasa wanapanga mkutano wa dharura kujadili ziara za kiongozi huyo katika maeneo hayo na kutafuta suluhu ya kuzuia viongozi zaidi kumuunga mkono katika safari yake ya 2022.

Kamati kuu ya kitaifa ya chama hicho itakutana wiki hii ikiwa na ajenda ya kuziba nyufa zinazosababishwa na ziara za Ruto.

Raila anatarajiwa kuongoza kikao hicho baada ya shughuli nyingi za wiki jana za kujaribu kuwapatanisha viongozi wa Sudan Kusini wanaozozania uongozi.

Kiongozi huyo alirejea Juni 10 kutoka Afrika Kusini ambapo alikutana na aliyekuwa Makamu wa Rais wa Sudan Kusini, Riek Machar.

Mkutano huo utaamua jinsi ya kuwaadhibu wanasiasa wa ODM wanaokaidi kanuni za chama. Wanasiasa wanaolengwa kuadhibiwa ni wale ambao wamekuwa wakimlaki na kuongozana na Ruto katika ziara zake za Pwani ambazo zimezidi kwa miezi miwili iliyopita. Kamati ya adhabu itakuwa na kazi kwa sababu idadi ya wanasiasa (wabunge, maseneta na magavana) ambao wanamuunga mkono Ruto ni kubwa.

ODM ina kila sababu kupata tumbo joto kutokana na kampeni za mapema za makamu wa Rais. Miongoni wa wabunge 46 wa ODM katika Bunge la Kitaifa kutoka Pwani, 42 wameapa kumpigia debe Ruto hadi 2022.

Pwani ina magavana sita (mmoja wa Jubilee na waliosalia wakiwa wa ODM. Kwa sasa ni Gavana Hassan Joho pekee ambaye hajamfuata Ruto. Kwa ufupi, magavana watano wameingia katika kambi ya Ruto.

Raila ataambulia chochote?

Swali la kujiuliza sasa ni iwapo Raila ataponea chupuchupu katika mazingara haya na mawimbi ya Ruto katika eneo hili ambalo kwa miaka kadhaa limekuwa ngome yake.

“Kuna sintofahamu kwenye chama chake kwa sasa. Hakuna anayejua kama Raila atawania urais 2022 au la. Anahitaji kujitokeza na kusema kama atakuwa miongoni mwa wale watakaowania kiti hicho au la,” mwanachama mmoja wa Kamati Kuu ya ODM alisema.

Makamu wa Rais amekuwa akitumia nguvu zake na ushawishi wake wote kuwaweka mfukoni wanasiasa wa ODM katika maeneo ya Nyanza, Magharibi mwa Kenya na Pwani huku akijitayarisha kumrithi Uhuru.

Lakini, Ruto anakanusha madai yoyote yanayoonyesha ameanza kampeni. Anasema yeye yuko katika ziara rasmi za kuzindua miradi ya maendeleo na kumwakilisha Rais Uhuru. Lakini, wadadisi wa siasa hawakubaliani naye, wanasema ameanza kampeni za 2022 huku akipeana “zawadi” na ahadi kwa wale anaowalenga wamuunga mkono.

Kuna tofauti kati ya Ruto anayefanya kampeni na Ruto anayetekeleza majukumu ya kiserikali kama vile uzinduzi wa miradi mbalimbali.

Ruto ambaye Wakenya wanamuona sasa katika ziara, ni mtu ambaye yuko kwenye pilikapilika za kampeni rasmi. Lengo la Ruto ni kutayarisha na kuimarisha kampeni zake ili wengine watakapoanza zao miaka mitatu au minne kuanzia sasa, atakuwa amepiga hatua.

Madhara yake

Harakaharaka zake zinaweza kuhujumu ndoto zake kwa sababu 2022 bado ni mbali mno. Wakati wanasiasa wengine watakapokuwa wanaanza kampeni zao, Ruto na wafuasi wake watakuwa wamechoka. Wananchi wengine watakuwa wamebadilisha mawazo yao na kuanza kuegemea upande wa wanasiasa “wapya”.

Ruto alizindua mradi wa Ksh3.2 bilioni katika eneo la Shimoni katika Jimbo la Kwale. Hii ni moja ya miradi mingi ambayo amezindua katika eneo la Pwani. Bila shaka, hii itasaidia kuwavutia wananchi kumpigia kura 2022.

Kwa siku tatu mfululizo, Ruto aliweka kambi Pwani ambapo amemiminiwa sifa na wanasiasa wa upinzani. Vitisho vya Katibu wa ODM, Edwin Sifuna kuwa atawaadhibu wanasiasa hao vimepuuziwa huku wanasiasa wa ODM wakisisitiza kuwa wataendelea kumpigia debe Ruto hadi mwisho.

Tangu Rais Uhuru na Raila kukutana Machi 9 na kuzika tofauti zao, Ruto amefanya mikutano 46 ya hadhara kote nchini. Ruto hufanya mikutano mitatu kwa wiki moja.

Kama mwanafunzi kamili wa Rais mstaafu, Daniel arap Moi, Ruto anazingatia michakato ileile ya kukutana na wananchi kila siku na pia kuwaalika viongozi nyumbani kwake, Eldoret na Nairobi.

Kila wakati anapozindua miradi, Ruto pia hutumia fursa hiyo kukutana na viongozi wa maeneo ambayo miradi hiyo inazinduliwa.

Ziara hizo za Ruto hazijamfurahisha Rais Uhuru ambaye wiki mbili zilizopita alisema Ruto anafaa kuacha “kutangatanga katika vichochoro”.

Duru za kuaminika zinasema kwamba Ruto huwa anaahidi kuwatunza wanaomuunga mkono atakapokuwa rais.

Wabunge wa ODM wajitosa

Baadhi ya wabunge wa chama cha ODM waliomwacha Raila na kumfuata Ruto wanasema makamu wa rais ni mtu ambaye si mchoyo na ameendelea kuwaletea miradi ya maendeleo.

“Ruto sasa haongozi katika orodha ya wanasiasa wanaogombea urais. Yeye ni mgombea wa kipekee ambaye anatuletea suluhisho la matatizo yetu huku tukielekea 2022,” akasema Mbunge wa Malindi, Aisha Jumwa.

Jumwa ambaye sasa anajulikana kwa jina la Mama Radar kwa sababu ya machachari yake anapompigia debe Ruto, alikuwa mfuasi sugu wa Raila. Jumwa ni miongoni mwa wanasiasa wa kwanza kumfuata Ruto.

Ruto ameleta mawimbi makali katika ngome ya Raila katika eneo la Nyanza. Mnamo Aprili 8, Makamu wa Rais alikutana na wabunge watano kutoka Jimbo la Nyamira na kutangaza kwamba shule katika kanda hii zitafaidika kwa Ksh2.1 bilioni.

Mapema kabla ya mkutano huo, Ruto alikuwa amefanya mkutano na wabunge wote tisa kutoka Jimbo la Kisii na kuwashauri wajitenge na mizozo iliyosababishwa na uchaguzi mkuu wa mwaka jana na kushirikiana katika miradi ya maendeleo.

Katika nyumba yake mtaa wa kifahari wa Karen, Nairobi, Ruto amekutana na wabunge kutoka eneo la Magharibi. Mkutano huu ulichochea mawazo kwamba huenda Ruto anapanga kushirikiana na kiongozi wa chama cha Ford-Kenya, Moses Wetangula na mwenzake wa ANC, Musalia Mudavadi.

Kwa miaka 15 iliyopita, Raila amekuwa ana wafuasi kutoka Nyanza na Magharibi ambapo alipata asilimia 70 ya kura katika sehemu hizi mbili zenye wapiga kura wengi.

Naibu mwenyekiti wa ODM, Gavana Wycliffe Oparanya wa Jimbo la Kakamega amekutana na Ruto huku kukiwa na fununu kwamba anapania kuwa mgombea mwenza wake.

Kiranja wa Kundi la wachache katika Bunge la kitaifa, Junet Mohamed ameonya kwamba kampeni za mapema zimeng’oa nanga na kuna hatari ya kufungua mianya ya matumizi na uvujaji wa pesa za umma. Huku Ruto akiendelea kujenga ufuasi wake, washiriki wake wa kisiasa wanasema hawajafurahishwa na jinsi vita dhidi ya ufisadi vinavyotekelezwa.

Kiongozi wa walio wengi bungeni, Aden Duale na Seneta wa Jimbo la Nandi, Kiprotich Cherargei wanadai vita hivyo vilivyoanzishwa na Rais Uhuru wiki tatu zilizopita, vinalenga watu walio na uhusiano wa kisiasa na makamu wa Rais.

Nataka Kupenda Kama Mjinga, Nizame Nipotee! Kama limbwata ni Kweli Lipo Basi Nilishwe Hata Hilo

$
0
0

It may sound strange but this has been my major wish for a while,

Nataka kupenda kama mjinga, yaani niwe zombiee, nizame mapenzini nipotelee huko. Kila nachoambiwa nione sawa niwe mjinga mjinga no reasoning.

Yale mapenzi usipowasiliana ama kumwona mtu wako for a day unajisikia mgonjwa, mapenzi ambayo unaongea na mtu wako for two or three hrs and you feel like its just 5 minutes na haujui mlikuwa mnaongea nini.

Yaani mapenzi ambapo nikiachwa au nililazimika kuacha basi nichanganyikiwe, nishindwe kula, nikose usingizi, nipungue uzito, nione kama dunia imekwisha shughuli zangu nishindwe kufanya, kichwa kigome kufukiri

Kama limbwata ni kweli lipo basi nilishwe hata hilo, haya mapenzi ya kupenda robo robo with a lot of reasoning sio nayotaka.

Natamani kupenda with all my heart, soul, mind, body and my everything, nataka kupenda kamili kamili, kwa kila kitu, mpenzi wangu awe kila kitu, awe ndio dunia na maisha yangu.

Trust me I want to love like nothing else,

Hivi ni mimi tu?

Nafasi za Ajira zilizotangazwa Leo

Kinana Awaaga Wabunge wa CCM kwa Maneneo Mazito "Ninyi Ndiyo Mtakaonihukumu"

$
0
0
Nilijituma Kazi kwa Maarifa Yangu Yote Ninyi Ndiyo Mtakaonihukumu- Kinana
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amewaaga rasmi wabunge wa chama hicho huku akiwataka kutokubali mgawanyiko ndani ya chama pamoja na bunge kwa tofauti ndogo ndogo.


Kinana amesema hayo katika halfa iliyoandaliwa na wabunge wa CCM ya kumuaga na kumkaribisha Katibu Mkuu, Dk Bashiru Ally iliyofanyika katika hoteli ya Morena jijini Dodoma.

Akitoa hotuba yake ya kuaga wabunge hao, Kinana amesema kwamba kama wabunge wa chama kimoja wanapaswa kutumia kanuni, kubishana kwa hoja na siyo vitisho au mambo mengneyo."

"Tusirushusu tofauti za maoni yetu kuwa chanzo cha mgawanyiko wa chama na bungeni, Mbishane kwa hoja na siyo vitisho. Kanuni za CCM zinapaswa kufanyiwa marekebisho kwani ziliandaliwa toka miaka 20 iliyopita. Zinapaswa kurekebishwa ili kuendana na mahitaji ya sasa" Kinana.

Aidha Kinana ameenda mbali zaidi na kusema "Nilijitahidi kujitolea, kufanya kazi, kujituma kwa maarifa yangu yote na ninyi ndio mtakaonihukumu kama nilifanya kazi ipasavyo. Kama kuna upungufu uliojitokeza nakiri kwamba ni wangu binafsi na kama kuna mafanikio hayakuwa na maarifa na juhudi zangu bali ni matokeo ya juhudi za wana CCM na wabunge wote".

Aidha Katibu Mkuu huyo Mstaafu amewahusia Wabunge hao  kuendelea kujenga imani kwa wananchi kupitia serikali iliyopo madarakani ambayo inaongozwa na CCM.

“Serikali ikitimiza ahadi zake kwa wananchi, itaendelea kuaminika na serikali ikipokea matatizo ya wananchi na kutimiza yale wanayoyataka, watafarijika na mtaendelea kuchaguliwa kwa idadi kubwa na mwisho wa siku CCM itapata ridhaa ya kuendelea kuongoza.”

Pamoja na hayo Kinana amewaambia Wabunge hao wa CCM kwamba ameamua kwenda kupumzika.

“Kuna wakati wa kuchukua dhamana na kukubali kuondoka, kuna wakati wa kukubali kazi moja na kwenda kufanya nyingine, kuna wakati wa kufanya kazi na kuna wakati wa kupumzika. Nimeamua kwenda kupumzika,” amesema.

Marekani Yajitoa Katika Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binaadamu

$
0
0
Marekani Yajitoa Katika Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binaadamu
Marekani imejitoa katika baraza la haki za binaadamu la Umoja wa Mataifa na kulitaja kuwa na 'unafiki wa kisiasa na lenye upendeleo'.

"Taasisi hiyo ya "unafiki na upendeleo inakejeli haki za binaadamu", amesema mjumbe wa Marekani katika Umoja huo Nikki Haley.

Bi Haley mwaka jana alilishutumu baraza hilo kwa kuwa na "upendeleo mkali dhidi ya Israel" na kusema Marekani inatafakari uwanachama wake.

Baraza hilo lililoundwa mnamo 2006, lililo na makao yake Geneva limeshutumiwa kwa kuruhusu mataifa yenye rekodi yakutiliwa shaka ya haki za binaadamu kuwa wanachama.

Lakini wanaharakati wanasema hatua hiyo ya Marekani huenda ikaathiri jitihada za kuangalia na kushughulikia ukiukaji wa haki za binaadamu kote duniani.

Bi Haley alitangaza nia ya Marekani kujitoa katika baraza hilo katika mkutano wa pamoja wa waandishi habari kiwa na waziri wa mambo ya nje Mike Pompeo, aliyelitaja baraza hilo kuwa "mteteaji duni wa haki za binaadamu".

Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa António Guterres, katika taarifa iliyotolewa kupitia msemaji wake, amejibu kwa kusema ange 'pendelea zaidi' kwa Marekani kusalia katika baraza hilo.

Kamishna wa haki za binaadamu katika Umoja wa mataifa Zeid Ra'ad Al Hussein, ameitaja hatua hiyo ya 'kusikitisha' na habari ya kushangaza mno". Israel, kwa upande wake imepongeza hatua hiyo.


Hatua hiyo imejiri wakati kukiwa na shutuma kali kuhusu sera ya utawala wa Trump ya kuwatenganisha watoto wahamiaji kutoka kwa wazazi wao katika mpaka wa Marekani na Mexico.

Baada ya Maofisa Kupima Samaki kwa Rula Waziri Aomba Radhi

$
0
0
Baada ya Maofisa Kupima Samaki kwa Rula Waziri Aomba Radhi
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameliomba radhi Bunge kwa kitendo cha maofisa wa wizara yake kuingia kwenye mgahawa wa Bunge Dodoma na kupima kwa rula samaki waliopikwa kwa ajili ya kitoweo.

Rosa Ree Aivujisha Mipaka Hip Hop ya Tanzania..Tazama Alivyomkimbiza Emtee

$
0
0

Rosa Ree Aivujisha Mipaka Hip Hop ya Tanzania..Tazama Alivyomkimbiza Emtee
Bonyeza Play Kutazama:

Rama Dee Afunguka Haya Kuhusu Diamond

$
0
0
Rama Dee Afunguka Haya Kuhusu Diamond
Mkali wa muziki wa RnB Bongo, Rama Dee amempongeza Diamond Platnumz kwa namna anavyopigania sanaa yake.

Muimbaji huyo amesema hatua aliyofikia Diamond inampa furaha. Kupitia Instagram yake ameandika;

Msanii wa kwanza Tanzania kupata freedom, nasikia furaha sana kuona msanii anaweza kuongea Kama msanii sio Mtumwa wa fikra…. Big up Nasibu, Mungu akuongezee maisha!

Utakumbuka leo June 19, 2018 Diamond alikuwa na mkutano na waandishi wa habari na kuzungumza mambo kadhaa kuhusu sanaa na upande wa Wasafi Media,

Kikubwa kilichogonga vichwa vya habari ni ujio wa Wasafi Festival ambapo ameeleza itapita kwenye mikoa mbali mbali na kujumuisha wasanii hata wale walio nje ya WCB na kusisitiza wote watalipwa vizuri.

Tunatibu na Kuponesha Kabisa Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha Bila Kupasua na Vidonda vya Tumbo

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME BUSHA BILA BILA KUPASUA NA VIDONDA VYA TUMBO: kwa nini uhendelee kuteseka NA kujiona mpweke pale ukutanapo NA mke au mpenzi wako kwa sababu tu hunaupunguvu wa nguvu za kiume na uume mdogo

MAPRO POWER NO 2 ndio tiba sahii ya kukurudishia heshima ya ndoa yako 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni mda wa dakika 15-20 kwa tendo LA kwanza 2 itaufanya uume wako uhonekane mkubwa hasa kwa wale wanaume ambao wamefanyiwa tohara wakiwa wadogo sana au wakiwa watu wazima kwani ipo dawa ya kuimalisha misuli ya uume 3 itakupa uwezo wa kurudia tendo LA ndoa zaidi ya Mara tatu 4 uhuimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa ?

WAI SASA UPATE TIBA YA UKWELI NA UHAKIKA NA NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA ata wazee wa miaka 80 wanatumia na kupona kabisa ? Tunatoa dawa za uzazi maumivu ya mgongo na kiuno ,kupunguza kitambi ,matiti makubwa,dawa za kisukari,presha,dawa za mvuto wa mpenzi ambaye akutaki au hakuhudumii ipasavyo kutengeneza shepu kwa kina Dada, fika ofisini kwetu MBAGALA ZAKHEMU BARABARA YA JESHINI HIENDA KIBONDEMAJI utaona ifisi himeandikwa MABULA CLINIC

AU PIGA SIMU NO 0743362017 DR AGU

KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUFIKA OFISINI UDUMA HII UTALETEWA

Kagera Sugar Yashindwana na Kaseja Yamruhusu Kwenda Popote

$
0
0
Kagera Sugar Yashindwana na Kaseja Yamruhusu Kwenda Popote
NI kama uongozi wa Kagera Sugar umeamua kumruhusu mlinda mlango wao mahiri, Juma Kaseja, kujiunga na timu yoyote ambako ataona yeye kunamfaa baada ya kushindwana na uongozi wa timu hiyo.



Kaseja ambaye alishawahi kuzitumikia klabu za Simba na Yanga kabla ya kujiunga na Mbeya City na kisha kujiunga na Kagera Sugar ameshaelezwa kuwa anaweza kuondoka hapo.



Akizungumza na Championi Jumatano, Meneja wa Kagera Sugar, Mohamed Hussein, alisema kuwa walikaa kikao jana kujadili juu ya kuongeza wachezaji wapya katika timu yao baada ya kocha wao kuwasilisha ripoti yake juzi.



“Mwalimu alitupatia ripoti Jumapili baada ya kumaliza sikukuu ya Eid na Jumatatu tulikaa kikao na viongozi wengine na yeye kocha (Mecky Mexime), nadhani hatutasajili wachezaji wengi ila tutaangalia wachezaji ambao wataondoka, lazima tuangalie wachezaji mbadala.



“Juma Kaseja tupo naye kwenye mazungumzo, lakini kama atapata timu ya kwenda, tunamruhusu kwenda.

“Sisi tunaamini kuna wachezaji wengi wenye kipaji kama Kaseja, hatuwezi kumlazimisha mchezaji kama anataka kuondoka.



“Sisi siyo kama timu nyingine kwamba tunapatana na mchezaji tutampa kiasi hiki, hatuwezi kuvuka hapo hata aje nani na huo ndiyo utaratibu wetu, sasa kama ameona sehemu kuna maslahi sisi tunamruhusu kwenda,” alisema.

Waendelee Kushinikiza Wafanyakazi Wao Wasipige Nyimbo Zetu na Sisi Tunawakataa- Babu Tale

$
0
0
Waendelee Kushinikiza Wafanyakazi Wao Wasipige Nyimbo Zetu na Sisi Tunawakataa- Babu Tale
Wasanii wa  kundi la  WCB wamezungumza kuhusu baadhi ya vyombo vya habari kutopiga nyimbo za wasanii wao.

Miongoni mwa mameneja wa WCB, Babu Tale  katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam  jana alisema kwa vile vyombo hivyo viliwakataa mwanzo na sasa waendelee hivyo hivyo.

‘Tunaendelea kuwaomba waendelee kushinikiza wafanyakazi wao wasipige nyimbo zetu..

“Hatutaki kuona wanapiga nyimbo zetu wala kutoa habari zetu kwa sababu wao walitukataa mwanzo, tunawakataa kwa sababu wao walitukataa,” alisema Babu Tale kwa msisitizo.

Hapo awali Diamond Platnumz alisema siku zote katika tasnia mbalimbali michezo ya kubaniana ipo ila hawezi kulaumu.

Diamond  alisema kufuatia hatua hiyo iliyochukuliwa na vyombo hivyo  iliwapa nguvu timu nzima ya Wasafi kufanya kazi kwa bidii ili waweze kuwasaidia wasanii wengine ambao wanakutana na changamoto hiyo.

Irene Uwoya Awatolea Povu Mashabiki "Mume Wangu Kaipenda Balaah Yani"

$
0
0
Irene Uwoya Awatolea Povu Mashabiki "Mume Wangu Kaipenda Balaah Yani"
Msanii wa filamu nchini Irene Uwoya na mke halali wa mwanamuziki Dogo Janja amewatolea uvivu mashabiki zake kwenye mtandaoo wa kijamii kuwa sio wa kwanza yeye kuvaa nguo za ufukweni hivyo wasimpangie chakufanya kwa madai vazi hilo mume wake amelipenda nasio vinginevyo.


Uwoya ametoa kauli hiyo asubuhi ya leo kupitia mtandao wake wa kijamii baada ya kupita siku moja tokea alipo-post picha aliyokuwa amevalia vazi jeupe lililokuwa linaonesha maumbile yake ya mwili na kusababisha mashabiki zake kumtolea maneno makali kuwa haeshimu ndoa yake wala mume wake kwa kuwa anachokifanya sasa hakipendezi na wadhfa wake aliokuwa nao.

"Ukivaa nguo kawaida ana kigodoro, nikim-post mume oonh mdogo na nisipo post kwanini hum-post mara humpendi. Nikivaa nguo za ufukweni nipo uchi mke wa mtu, sasa nasema hivi kwa wale iliyowauma poleni sana siku nyingine ntawashirikisha nikitaka ku-post. Hivi kwani mimi ni wa kwanza bongo kuvaa hivi maeneo ya ufukweni. Mume wangu kaipenda balaah yani", ameandika Uwoya.

Kwa tamaduni za kiafrika na kitanzania mara zote watu wanaamini endapo mwanamke atakapokuwa ameolewa basi kuna mavazi huwa anaepuka kuyavaa hata kama akiwa kwenye fukwe za bahari na hicho ndicho mashabiki zake walichokiamini lakini kwa bahati mbaya leo wamekutana na jambo la utofauti.

Irene Uwoya Aachia Picha za Utata Mtandaoni na Kusema Haya..

$
0
0

Msanii wa filamu nchini Irene Uwoya na mke halali wa mwanamuziki Dogo Janja amewatolea uvivu mashabiki zake kwenye mtandaoo wa kijamii kuwa sio wa kwanza yeye kuvaa nguo za ufukweni hivyo wasimpangie chakufanya kwa madai vazi hilo mume wake amelipenda nasio vinginevyo.

Uwoya ametoa kauli hiyo asubuhi ya leo kupitia mtandao wake wa kijamii baada ya kupita siku moja tokea alipo-post picha aliyokuwa amevalia vazi jeupe lililokuwa linaonesha maumbile yake ya mwili na kusababisha mashabiki zake kumtolea maneno makali kuwa haeshimu ndoa yake wala mume wake kwa kuwa anachokifanya sasa hakipendezi na wadhfa wake aliokuwa nao.
"Ukivaa nguo kawaida ana kigodoro, nikim-post mume oonh mdogo na nisipo post kwanini hum-post mara humpendi. Nikivaa nguo za ufukweni nipo uchi mke wa mtu, sasa nasema hivi kwa wale iliyowauma poleni sana siku nyingine ntawashirikisha nikitaka ku-post. Hivi kwani mimi ni wa kwanza bongo kuvaa hivi maeneo ya ufukweni. Mume wangu kaipenda balaah yani", ameandika Uwoya.
Kwa tamaduni za kiafrika na kitanzania mara zote watu wanaamini endapo mwanamke atakapokuwa ameolewa basi kuna mavazi huwa anaepuka kuyavaa hata kama akiwa kwenye fukwe za bahari na hicho ndicho mashabiki zake walichokiamini lakini kwa bahati mbaya leo wamekutana na jambo la utofauti.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live




Latest Images