Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live

Aslay Ndani Ya Penzi Zito na Mrembo Mwingine

$
0
0

Staa wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Nibebe’ Aslay Isihaka ameweka wazi penzi lake zito na Mrembo ambaye ni Muigizaji wa Bongo movie Diana Kimary.

Wiki chache zilizopita Aslay alithibitisha kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Tessy Chocolate  ambaye pia ni mama wa mtoto wake mmoja wa kike anayeitwa Moza.

Aslay na Tessy hawa kuweka wazi sababu za kuachana lakini kila mmoja alisisitiza wameachana kwa wema na hawana chuki baina yao.

Siku ya jana Aslay amemuanika Rasmi mpenzi wake Mrembo Diana Kimary Kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo amemposti mara mbili huku akionyesha wazi kuwa wana Mahusiano zaidi ya urafiki.


Kwenye picha hizo Aslay alisindikiza kwa maneno kama “Mashallah” na “Sasa ndio nini Mke wangu”.

Kibenteni Kilinigeuza Mimi ‘ATM’ Yake – Nisha

$
0
0

Muigizaji wa Bongo movie ambaye hivi karibuni amegeukia tasnia ya Bongo fleva na kuachia wimbo wake unaojulikana kama ‘Bachela’ amefunguka jinsi kibenteni chake kilivyokuwa kinamchuna.

Nisha amefunguka na kuelezea jinsi alivyowahi kuteswa na penzi la kijana mwenye umri mdogo kuliko yeye kwani ilibidi yeye ndio awe anampa huduma zote kijana yule.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Nisha amesema kuwa wakati akiwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na kibenteni huyo ambaye hakutaka kumtaja jina alikuwa akimnunulia kila kitu na kumpa fedha na kumuhudumia kama mtoto wake lakini baadaye alikuja kushtuka kuwa anachunwa na kua­mua kuachana naye.

Nimejifunza sana na nime­koma kuwa na uhusiano na mwanaume ninayemzidi umri na kipato maana nilijikuta nime­ingia kwenye uhusiano huo bila kujua kwamba kibenteni huyo ni tege­mezi ambaye alinifanya kama mashine yake ya ATM na kuniko­moa kuja kushtuka ameshanikwan­gua vya kutosha”.

Nisha ingawa amekiri kuwa mara ya kwanza wakati anaanza mapenzi na kijana huyo hakujua kuwa ni mdogo lakini baada alimpenda na kuendelea naye jambo ambalo anajutia kupita kiasi.

KIMENUKA..Baba Diamond na Baba Ommy Dimpoz Warushiana Maneno

$
0
0
Baba mzazi wa Staa wa Bongo fleva Ommy Dimpoz,  Mzee Faraji Nyembo amemtolea povu Baba wa staa Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma kutokana na tabia yake ya kumsema mwanaye vibaya.


Gazeti la Risasi Mchanganyiko  linaripoti kuwa Kwenye mahojiano waliyofanya na Baba Ommy Dimpoz alitoa taarifa ya mtoto wake kuendelea vizuri na kusisitiza hata kama mtoto wake hamsaidii kwa lolote maishani lakini hawezi kumsema vibaya kama Baba Diamond anavyofanyaga kwa mwanaye.

Unajua mimi ni mzazi wa tofauti sana, siwezi kumlalamikia au kumsemea mabaya mwanangu kwenye vyombo vya habari kama anavyofanya baba Diamond, ninachofanya huwa namuombea mwanangu awe na maisha mazuri maana nikimuombea mabaya anaweza kupoteza dira ya maisha yake nitakuwa nimefaidika na nini.

Namshauri baba Diamond awe anamuombea mwanaye mafanikio, aungane naye wawe kitu kimoja, afurahie mafanikio yake ipo siku Mungu atamrudisha kwake amsaidie na siyo kumzungumzia maneno ya kumlaani na kumlalamikia kila siku.

Aige mfano wangu maana mimi huwa simlazimishi mtoto anisaidie bali huwa napambana na hali yangu kwa kufanya kazi kwa bidii na ninampenda sana mwanangu Dimpoz na siwezi kumlaani au kumlaumu maana jina nililompa la Omary ni la baba yangu inakuwaje sasa nimlaani ni sawa na kumlaani baba yangu”.

Baada ya povu hilo gazeti hilo lilimsaka Baba Diamond na kumuhoji kuhusu kile alichosema Baba Dimpoz na alimwaga povu hili:

Sitaki shobo, huyo baba Dimpoz simfahamu kama hana la kuongea anyamaze, amzungumzie mwanaye hata kama niliongea kuhusu Diamond si mtoto wangu yeye inamuhusu nini?”.

Kuhusu huyo Diamond sihitaji kuzungumza chochote kuhusu yeye wala watoto wangu maana hawana faida yoyote kwangu kwa sasa”.

Miujiza ya Maalim Khatibu Kutoka Bagamoyo Pwani

$
0
0
MAALIM KHATIBU anawashukuru wale wote wanaopiga simu za shukrani, na wale ambao bado wanamatatizo musikate tamaa kwa kuchelewa kupokelewa simu zenu,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

MAALIM KHATIBU Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN dawa za asili ya afrika na njiwa,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu MAALIM KHATIBU sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata maelekezo yake,

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 710-332103
WhatsApp +255 766-705404
Instagram: Follow@maalim_khatibu

USHAURI: Ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate msaada kwa wakati.

Trump Arudi Nyuma Katika Sera Yake ya Kuzitenganisha Familia

$
0
0
Trump Arudi Nyuma Katika Sera Yake ya Kuzitenganisha Familia
Rais Donald Trump wa Marekani amesitisha sera yake uhamiaji iliyokuwa inalazimu kuzitenganisha familia za wahamiaji wanaobainika kuvuka mipaka kinyume cha sheria na watoto wao.

Pamoja na kulegeza msimamo huo kutokana na kulalamikiwa kwa sera hiyo ndani na nje ya taifa hilo, Trump amesisitiza kwamba bado ataendelea kuilinda mipaka yake.

Rais Trump ambaye tangu kuingia kwake madarakani alionekana kuhitaji sheria kali zaidi ya kukomesha suala la uhamiaji haramu, amejikuta matatani, safari na hasa baada ya picha zenye mguso za watoto waliotenganishwa na wazazi wao katika mpaka wa Marekani na Mexico kuanza kusambaa na kuleta mshituko mkubwa kwa raia wa Marekani.

Bunge, makundi ya haki za binadamu na hata Bi.Melania Trump yaani mkewe rais Trump mwenyewe na wake wa marais wastaafu.

Rais Magufuli Afanya Uteuzi Mwingine.... Amteua CAG Mstaafu Ludovick Utouh

$
0
0
Rais Magufuli Afanya Uteuzi Mwingine.... Amteua CAG Mstaafu Ludovick Utouh
RAIS Magufuli amemteua CAG Mstaafu, Ludovick Utouh kuwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali za Madini, Mafuta na gesi Asilia Tanzania.

Hiki Hapa Chanzo cha Mkurugenzi NHC Nehemia Mchechu Kutumbuliwa

$
0
0
Hiki Hapa Chanzo cha Mkurugenzi NHC Nehemia Mchechu Kutumbuliwa
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ametengua uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Nehemia Mchechu.


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi(kulia), na aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Nehemia Mchechu.

Kupitia Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Dorothy Mwanyika imesema kuwa kwa mamlaka aliyonayo waziri Lukuvi chini ya kifungu cha 18(1) cha sheria ya Shirika la Nyumba la taifa amesitisha uteuzi huo kuanzia leo Juni 20, 2018.

“Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi kwa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 18(I) cha sheria ya Shirika la Nyumba la Taifa ya mwaka 1990 pamoja na marekebisho yake mwaka 2005, ametengua uteuzi wa mkurugenzi wa shirika hilo”, imesema Taarifa.

Awali katika taarifa iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi Disemba 16, 2017 ilimtaka mkurugenzi huyo kusimama majukumu yake ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zikimkabiri za utendaji mbovu.

Hiki Kikosi cha Simba cha Sasa Kufuru Tupu

$
0
0
Hiki Kikosi cha Simba cha Sasa Kufuru Tupu
SIMBA walianza kumsainisha Marcel Kaheza wa Majimaji, akafuatia Adam Salamba wa Lipuli. Mashabiki wakaguna…aaah jamaniieee watacheza wapi wote hao mastraika?



Huku na huku mara wakamshusha tena Mohammed Rashid wa Prisons, Yanga wakaibuka wakaaanza kulalamika kwamba Simba wanatibua tu michongo yao makusudi kwa vile wana mkwanja.



Wadau walikuwa wakigunia usajili wa mastraika hao watatu kwa vile wote wana sifa zinazokaribiana na waliongoza kwenye timu zao msimu uliopita. Salamba alikuwa na mabao sita pale Lipuli, Rashid alikuwa na 10 huko Prisons na Kaheza 14 pale Majimaji.



Kumbe bwana hicho kilichofanyika siyo bahati mbaya ni mipango matata sana ya mwekezaji wa Simba, Mohammed Dewji ‘MO’ kuhusiana na usajili mpya wa kikosi hicho msimu ujao.



MO amewaambia viongozi wa Simba kwamba usajili wa msimu ujao anataka uwe wa tofauti sana na ndiyo maana utafanyika na watu wachache sana akiwemo yeye na Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah ‘try again’ chini ya muongozo wa ripoti ya makocha.



Kiongozi huyo anayefahamika Afrika nzima kwa utajiri na mbinu za ujasiriamali amewaambia vigogo wa Simba kwamba anataka kila nafasi uwanjani iwe na wachezaji wawili imara sana yaani aliyeko kwenye benchi awe mkali kuliko aliyeanza ili iwe bandika bandua.



Championi Jumatano, limebaini kwamba huku akiendelea kusuka kikosi hicho tayari mazungumzo baina yake na makocha kadhaa kutoka Ulaya Kaskazini na Ubelgiji anaotaka waje kuinoa Simba yamefikia pazuri lakini ni siri kubwa hata viongozi wengine hawajui ni nini kinaendelea.



“Kila nafasi anataka iwe na wachezaji imara sana yaani kwenye benchi kuwe na straika mkali kuliko Okwi na Bocco. Na anataka hilo lifanyike kwenye nafasi zote, kuwepo na vikosi viwili imara sana ambavyo havitazuilika kwenye ligi za ndani na michuano ya kimataifa.



“Lakini hao wachezaji imekuwa ni siri sana anafanya yeye na Salim, hakuna yale mambo ya kamati kama zamani,”alidokeza kiongozi mmoja wa Simba ambaye aliongeza kwamba hata Obrey Chirwa wa Yanga alikuwa kwenye mipango yao lakini wamesikia amepata dili Misri katika klabu kongwe ya Ismailia,” kilisema chanzo hicho.



Habari za ndani zinasema kwamba MO ambaye ni Simba wa kulia machozi hatumii tena kamati maalum ya usajili kama ilivyokuwa siku za nyuma ndio maana mambo mengi yanakwenda kwa siri sana na habari zinasema amekuwa akisisitiza hivyo pia ili kuepuka ‘cha juu’.



Habari zinasema kwamba viongozi wengi wa Simba ambayo imeshampiga chini straika kipenzi cha msemaji wa Simba, Haji Manara, aitwae King Laudit Mavugo wameafiki anachofanya MO kwa sasa kwenye usajili kwani kitajenga timu imara ambayo itakuwa na ushindani mkubwa na itawasaidia kuonyesha mabadiliko ambayo yameanza kuonekana kwenye uendeshaji.



Habari zinasema kwamba MO amepania kusajili mchezaji wa gharama yoyote ndani ya Afrika na hata kwenye mkutano mkuu wa wanachama alithibitisha hilo na kupigiwa makofi yenye kilo nyingi.



Simba ambayo itashiriki michuano ya Kagame inayoanza Juni 29, Jijini Dar es Salaam, inajiandaa pia na Ligi ya Mabingwa Afrika inayoanza Desemba mwaka huu badala ya Februari kama ilivyozoeleka.



Baadhi ya timu ngumu za Afrika ambazo mpaka sasa zimefuzu Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao ni pamoja na Esperance na Club African za Tunisia, Al Ahly na Ismailia zote za Misri.

Mbunge CCM Aibua Upya Sakata la Ununuzi wa Bombardier

$
0
0
Mbunge CCM Aibua Upya Sakata la Ununuzi wa Bombardier
Mbunge wa Ulyankulu (CCM), John Kadutu amesema ununuzi wa ndege za Bombardier uliofanywa na Serikali hauna tija kwa wananchi wa jimbo lake iwapo huduma za afya na barabara hazijaboreshwa.

Kadutu ametoa kauli hiyo leo Jumatano Juni 20, 2018 katika mjadala wa bajeti ya Serikali mwaka 2018/19 bungeni mjini Dodoma.

Amesema umebaki mwaka mmoja kabla ya nchi kuingia katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, hivyo ahadi zilizotolewa zinapaswa kutekelezwa.

“Serikali imejenga reli, inanunua ndege hebu twendeni kwa wananchi, ujue ukienda kule Ulyankulu ukauliza Bombardier hawakuelwi, barabara mbovu, afya mbovu hawakuelewi,” amesema Kadutu.

“Pelekeni fedha barabara ziboreshwe, Tarura (Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini) wapewe fedha. Bajeti iliyobaki ni moja ya kujadili kwa utulivu kwani akili itakuwa majimboni tu, tusaidieni ili mwaka 2020 tupete,” amesema.

Akigusia  ahadi za kampeni za uchaguzi, Kadutu amesema waliahidiwa jimbo la Ulyankulu litakuwa wilaya lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa.

“Hamtaki kutupa eneo lakini mnasema ahadi za Rais zitatekelezwa, sasa hii ni ahadi ya Rais, alisema akiingia siku tatu tu tunapata wilaya,” amesema.

“Sasa imebaki mwaka mmoja tu na nusu yako mengi, mmetuahidi lami tena kilomita tatu tu lakini tunaona mambo ambayo hayako katika ilani yanatekelezwa. Tukisema…,mimi watu wa Ulyankulu wamenituma.”

Mbunge huyo amesema anashangazwa na mawaziri kutotembelea jimboni kwake huku wakionekana kupishana katika majimbo mengine jambo linalokatisha tamaa wananchi.

Irani Yaingia Katika Historia Yawaruhusu Wanawake Kuingia Uwanjani kwa Mara ya Kwanza

$
0
0
Irani Yaingia Katika Historia Yawaruhusu Wanawake Kuingia Uwanjani kwa Mara ya Kwanza
Taifa la Iran June 20 2018 limeingia katika historia mpya katika michuano ya Kombe la Dunia 2018 inayoendelea nchini Urusi baada ya kuruhusu mashabiki wake wa kike waingie uwanjani kwenda kuishangilia timu yao ikicheza dhidi ya Hispania.

Iran ambao hadi wanaingia katika uwanja wa Azadi jijini Tehran kucheza dhidi ya Hispania walikuwa na point tatu, wameambulia kipigo cha goli 1-0, goli pekee la Hispania lilifungwa na Diego Costa dakika ya 54, pamoja na Iran kuongeza nguvu ya mashabiki wake wa kike uwanjani lakini haikusaidia.



Kama ufahamu tu nchi ya Iran imeruhusu mashabiki wake wa kike kuingia uwanjani kutazama mpira kwa mara ya kwanza June 20 baada ya miaka 37 toka tukio kama hilo litokee 1979, Iran ni miongoni mwa baadhi ya nchi za kiharabu ambazo haziruhusu wanawake kwenda uwanjani.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Mpenzi wa Ronaldo Ashindwa Kuficha Hisia Zake Aiweka Kando Argentina

$
0
0
Mpenzi wa Ronaldo Ashindwa Kuficha Hisia Zake Aiweka Kando Argentina
Mwanadada Georgina Rodriguez ambaye ni raia wa Argentina, amedhihirisha kuwa mapenzi yanaweza kuwa na nguvu na uzalendo ukafuatia baadaye, baada ya kuonyesha anaiunga mkono nchi aliyozaliwa mpenzi wake Christiano Ronaldo.


Nahodha wa Ureno, Cristiano Ronaldo kushoto, aliyevalia jezi ya Ureno ni mpenzi wake Georgina Rodriguez

Georgina ni mpenzi wa nahodha wa Ureno, Cristiano Ronaldo ambaye jana amefunga bao lake la nne katika michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Urusi.

Bao hilo la nne amefunga Ureno ikipata ushindi wa kwanza kwa kuitwanga Morocco kwa bao 1-0 huku Georgina ambaye ni raia wa Argentina akisherekea jukwaani akiwa na jezi ya Ureno namba 7 ambayo huvaliwa na Ronaldo.

Hivi karibuni, Ronaldo aliwahi kusema ataiunga mkono pia Argentina wakati wa michuano ya Kombe la Dunia kwa kuwa mpenzi wake huyo ni mzaliwa na uraia wa Argentina.

Ndugai Awaongoza Wabunge Kupimwa Ukimwi

$
0
0
Upimwaji Ukimwi kwa Hiari kwa Wabunge Kuzinduliwa Leo na Spika Ndugai
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai leo anazindua zoezi la kupima Ukimwi kwa Wabunge kwa hiari.

Akizungumza leo, Juni 21, 2018 Bungeni Jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali na Majibu, Naibu Spika, Tulia Ackson amesema ni vizuri wabunge wote ambao hawajapimwa wakapime Virusi Vya Ukimwi kwa hiari.

“Waheshimu wabunge leo Mh. Spika anatarajiwa kuzindua zoezi la kupima virusi vya Ukimwi kwa hiari hapa Bungeni kwa waheshimiwa Wabunge lakini pia na wafanyakazi wa Bunge na atazindua zoezi hilo saa nne leo hii kwenye viwanja vya vilivyopo nyuma ya ukumbi wa Mh. Pius Msekwa,” amesema Dkt. Tulia Ackson.

“Kwahiyo Waheshimiwa Wabunge hasa wale wenye Kamati ya Ukimwi mnaombwa kuhudhuria zoezi la uzinduzi alafu waheshimiwa Wabunge wale wote ambao hawajapima wanaomba kuanzia saa 7 waende kupimwa kwa hiari ili wabunge tuwe tunafahamu afya zetu vizuri.”

Ben Pol Kufanya Tour Nje ya Tanzania

$
0
0
Ben Pol Kufanya Tour Nje ya Tanzania
Msanii wa muziki Bongo, Ben Pol ametangaza tour yake ambayo itapita katika nchi mbali mbali.

Muimbaji huyo anayetamba na ngoma ‘Zai’ amesema tour hiyo inakuja baada ya kufanya tour kadhaa Bongo kama Sophia Tour na Moyo Mashine Night.

“Pia mwaka huu nitafanya tour lakini nataka kutoka kidogo, ni nje ya Tanzania nitaenda Europe, USA, nitakuwepo pia Kenya, halafu China,” Ben Pol ameiambia Bongo5.

Utakumbuka hivi karibuni Vanessa Mdee na Jux walitangaza tour yao’ In Love & Money’ ambayo itapita katika mikoa kama Mwanza, Arusha, Mtwara, Dar es Salaam n.k.


Wakurugenzi Halotel, Zantel Wahukumiwa Miaka 40 Jela

$
0
0
Wakurugenzi Halotel, Zantel Wahukumiwa Jela miaka 40
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imewahukumu watu sita na kampuni mbili, wakiwamo wakurugenzi watendaji wa kampuni za simu za mkononi, Le Van Dai (35) wa Halotel na Sherif El-Barary wa Zantel,kulipa faini ya Sh. milioni 139 au kwenda jela miaka 40 baada ya kukiri tuhuma za uhujumu uchumi.

Washtakiwa wote walikiri jana tuhuma zilizokuwa zinawakabili zikiwamo za kula njama, kuingiza, kufunga mitambo, matumizi ya laini za simu bila usajili wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), na kuisababishia serikali hasara ya Sh. 1,131,936,000.

Hukumu hiyo ilitolewa na mahakama hiyo chini ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi, Kevin Mhina, baada ya washtakiwa kusomewa mashtaka yao 12 na kukiri.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na mawakili wa serikali Jacqueline Nyantori na Batilda Mushi.

Nyantori aliwataja washtakiwa wengine kuwa ni, Lei Cao maarufu kama Peter (28), Huang Yu Meng (27), Msimamizi wa Biashara wa Halotel Zanzibar, Jimmy Mosha (26), Meneja Masoko wa Halotel, Willy Ndoni (29), Kampuni ya Viettel Tanzania Ltd maarufu kama Halotel iliyoko Kinondoni na Kampuni ya Zanzibar Telecommunication PLC, maarufu kama Zantel, iliyoko Msasani, Dar es Salaam.

Alidai katika shtaka la kwanza, kati ya Januari Mosi, 2017 na Aprili 30, mwaka huu nchini Tanzania, mshtakiwa wa kwanza hadi wa sita, walikula njama ya kutenda kosa la kutumia huduma za mawasiliano kwa njia ya udanganyifu.

Katika shtaka la pili, kati ya Mei Mosi, 2017 na Aprili 30, mwaka huu, katika jengo la Spring lililoko Mbezi mshtakiwa wa kwanza hadi wa sita, kwa pamoja walifunga mitambo ya mawasiliano kwa njia ya udanganyifu na kujipatia huduma za mtandao wa Halotel na Zantel bila kibali cha TCRA .

Shtaka la tatu, nne, tano na sita, kati ya Januari Mosi na Desemba 31, 2017, Aprili 30, mwaka huu jijini Dar es Salaam, mshtakiwa wa tatu na wa nne, waliingiza nchini, waliifunga na kuendesha mitambo ya mawasiliano kwa kuunganisha na kampuni hizo za simu bila kibali cha TCRA.

Shtaka la nane, kati ya Mei Mosi, 2017 na Aprili 30, mwaka huu katika jengo la Spring City, mshtakiwa wa tatu na wa nne, walikutwa wakitumia laini za simu za mkononi zisizosajiliwa na TCRA 281,272 za Halotel na 11,920 za Zantel.

Upande huo wa Jamhuri ulidai katika shtaka la 10 kuwa kati ya Mei, 2017 na Aprili 30, mwaka huu katika matawi ya Zantel ya Dar es Salaam, mshtakiwa wa pili na wa nane walitumia kwa makusudi laini za simu 11,920 zisizokuwa na usajili wa TCRA.

Shtaka la 11 na 12, kati ya Mei Mosi, 2017 na Aprili 30, mwaka huu washtakiwa waliisababishia serikali hasara ya Sh. 1,131,936,400.

Kwa mujibu wa mashtaka yanayowakabili washtakiwa kisheria kesi hiyo washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote hadi upelelezi utakapokamilika itasikilizwa Mahakama Kuu Tanzania, Divisheni ya Uhujumu Uchumi au kwa kibali maalumu kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP).

Aidha washtakiwa walikiri maelezo yote ya awali.

Hakimu Mhina aliahirisha kesi hiyo saa 8:05 na kurejea saa 8:30 kuwasomea washtakiwa hukumu.

Hakimu alisema katika shtaka la kwanza na la pili, washtakiwa wanatakiwa kulipa faini ya Sh. milioni 20 au jela miaka sita na kwa kosa la tatu mpaka la sita, walipe faini ya Sh. milioni 20 au kwenda jela miaka minane.

Kwa kosa la saba mpaka la 10, aliamuru walipe faini ya Sh. milioni 22 au kwenda jela miaka 12 na kwa kosa la 11 na la 12, walipe faini Sh. milioni 20 au kwenda jela miaka 14.

Pia mahakama hiyo ilisema washtakiwa walipe fidia ya zaidi ya Sh. bilioni moja wanayodaiwa kuisababishia serikali hasara na mali zote ikiwamo mitambo na kadi za simu wanazodaiwa kukutwa navyo, washtakiwa viteketezwe.

Pia hakimu aliuamuru upande wa Jamhuri uwarejeshee washtakiwa hati zao za kusafiria, vibali vya kuishi nchini na leseni za biashara.

Vigogo hao walilipa faini kuepuka kifungo, kasoro washtakiwa Lei Cao na Huang Meng ambao walipelekwa gerezani.

Tyga Abanwa Kurudisha Fedha Alizotapeli

$
0
0
Tyga Abanwa Kurudisha Fedha Alizotapeli
MWANAMUZIKI wa Marekani, Tyga,  anadaiwa aarudishe fedha aliyopewa na gharama za tiketi alizokatiwa yeye na kundi lake kwa ajili ya kufanya shoo nchini Dubai kwa vile hakutokea.

Tyga alikuwa anatakiwa kutumbuiza sehemu mbalimbali katika Falme za Kiarabu mwezi Aprili mwaka huu na akawa amepewa fedha ya mwanzo ambazo ni $120k  na $21k za tiketi, hivyo anadaiwa kurejesha jumla ya $141k ambazo ni sawa na Sh. mil.  320.

Zaidi ya hapo anadaiwa kulipa $600k (Sh. bil. 1.3) kwa ajili ya hasara iliyopatikana kwa ajili ya matayarisho ya shoo hizo.

Obama Amshtumu Trump Kuwatenganisha Watoto na Familia Zao

$
0
0
Obama Amshtumu Trump Kuwatenganisha Watoto na Familia Zao
RAIS mstaafu wa Marekani Barack Obama aliitumia Siku ya Wakimbizi Duniani kumshutumu Rais wa Marekani,   Donald Trump  katika sera yake ya kuwatenganisha watoto na familia zao.

Obama aliyasema hayo kupitia mtandao wa Facebook akiuliza iwapo Marekani inakubali ukatili wa kuwatengenisha watoto na wazazi wao.

Aliongeza kwamba: “Tuthibitishe kupitia sera, sheria na vitendo vyetu kwamba tunathamini familia zetu na zingine zote.”

Former President Barack Obama used World Refugee Day to criticize President Donald Trump's policy of separating migrant children and families
Obama.

Rais Trump amekuwa akiendesha sera ya kuwatenganisha watoto wakimbizi na familia zao hasa wale wanaoingia Marekani, hili limo katika amri aliyosaini karibuni.

President Trump signed an executive order on Wednesday reversing the separation policy
Rais Trump.
Hata hivyo, utawala wa Obama uliwahi kuwaweka kizuizini watoto na familia zao wakati wakisubiri mashitaka mbalimbali.
Katika sera ya Trump, utawala wake umewatenganisha watoto 1,995 kutoka kwa wazazi wao 1,940 tangu Aprili hadi Mei 31 mwaka huu kufuatia matukio mbalimbali, yakiwemo ya uhamiaji.

Vijana Wana Uwezo wa Kufanya Kazi Nitaendelea Kuwateua- Rais Magufuli

$
0
0
Vijana Wana Uwezo wa Kufanya Kazi Nitaendelea Kuwateua- Rais Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli ameweka bayana kwamba atakuwa akiendelea kuteua na kuwapa nafasi vijana kwani wana uwezo wa kufanya kazi.


Rais Magufuli ameyasema hayo, leo wakati akipokea gawio la Serikali kutoka Shirika la Simu Tanzania{TTCL} na kuzindua upanuzi wa huduma za TTCL.

Dk. Magufuli amesema kwamba "Vijana wakipewa majukumu wanaweza lakini akitaka kuharibu anaharibu kwelikweli, hii ndo sababu ya kuteua vijana katika nafasi Serikalini, kwa bahati nzuri wengi niliowateua hawajaniangusha ukiondoa wachache".

"Naahidi kuendelea kuwateua katika nafasi mbalimbali.kwaajili ya kufanya kazi"- Rais Magufuli

Pamoja na hayo Dk. Magufulia ameipongeza TTCL kwa kutoa gawio la Bilioni 1.5 ambapo amekiri ni miaka mingi sana imepita toka kampuni hiyo itoe gawio kwa serikali.

"Kuanzia 2001 TTCL haikutoa gawio lolote kwa serikali hata senti 5, lakini baada ya miaka miwili tu leo TTCL imetoa gawio la Bilioni  1.5. Nashindwa kujua tulikuwa tunaibiwa, au hujuma, au utendaji ulikuwa mbaya" Rais Magufuli

Kila Kukicha Kusimangwa Ningekuwa na Mimba Ingetoka- Hamissa Mobetto

$
0
0
Kila Kukicha Kusimangwa  Ningekuwa na Mimba Ingetoka- Hamissa Mobetto
MWANAMITINDO maarufu na mzazi mwenziye mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, Hamisa Mobeto amefunguka kuwa hana ujauzito kama watu wanavyoeneza uvumi huo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii.



Akizungumza na Amani, wakati akitoa msaada kwenye kituo cha watoto yatima cha CHAKUWAMA, kilichopo Sinza-Mori jijini Dar, Mobeto alisema haiwezekani akawa mjamzito kwa kipindi hiki sababu kwanza mtoto wake bado ni mdogo na maneno mengi ya kejeli yanatolewa dhidi yake mtandaoni.



“Watu naona wanachukulia kubeba mimba ni kitu rahisi sana lakini wangetambua mimi nina mtoto mdogo sana lakini kitu kingine waangalie kuwa hata kama ningeshika ujauzito lazima ungetoka maana kila kukicha ni kusimangwa ila muda wangu sahihi ukifika wa kuzaa mtoto mwingine nitafanya hivyo tu,” alisema Mobeto.
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live




Latest Images