Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

EU Yaongeza Ushuru kwa Bidhaa Kutoka Marekani

$
0
0
EU Yaongeza Ushuru kwa Bidhaa Kutoka Marekani
Jumuiya ya Ulaya EU imeanzisha ongezeko jipya la tozo kwa bidha zinazotoka Marekani kama hatua ya kulipa kisasi dhidi ya sera ya kibiashara ya Rais Trump iliyotangaza ongezeko tozo ya uingizwaji wa bidhaa za chuma na bati nchini humo.

Ongezeko hilo jipya la tozo lililotangazwa na EU linazilenga bidhaa za Marekani kama vile vinywaji vikali,Pikipiki zinzotengenezwa Marekani pamoja na maji ya matunda ya machungwa.

Ongezeko hili la tozo mpya ya EU kama hatua ya kujibu mapigo dhidi ya Marekani dhidi ya Marekani itaziathiri bidha kama tumbaku,piki piki maarufu za Harley Davidson,siagi ya karanga bidhaa ambazo kwa sasa zitakumbana na ongezeko la asilimia 25 sawa na kiasi cha yuro bilion 2.8 ambapo utekelezwaji wake unaanza rasmi leo.

Rais wa jumuiya ya Ulaya Jean-Claude Juncker amesema tozo iliyoanzishwa na Marekani dhidi ya umoja huo inakwenda kinyume na hali halisi na historia ya uhusiano uliokuwepo kibiashara kati ya EU na Marekani.

Nigeria Ni Kufa au Kupona Leo

$
0
0
Nigeria Ni Kufa au Kupona Leo
Wawakilishi wa Afrika kwenye kinyang’anyiro cha Kombe la Dunia 2018 timu ya taifa ya Nigeria ‘Super Eagles’ leo jioni itashuka dimbani katika mchezo muhimu watakaolazimika kucheza kufa au kupona kupata matokeo.

Nigeria iliyo kundi D itaivaa Iceland, ikiwa na kumbukumbu za kupoteza mchezo wa kwanza kwa kupigwa mabao 2-0 na Croatia, hivyo kipigo katika mchezo wa leo kitaifanya iyaage mashindano hayo.

Kwa kujua hilo Kocha Gernot Roh, atalazimika kukipanga vema kikosi chake baada ya kuiona Iceland inayoshiriki kwa mara ya kwanza fainali za Kombe la Dunia, ikionyesha kuwa imekuja kushindana na sio kushiriki baada ya kuibana Argentina na kutoka nayo sare ya bao 1-1.

Mbali ya mechi hiyo pia kuna mchezo unaosubiriwa kwa hamu wa kundi E, utakaopigwa leo saa 9:00 alasiri kati ya Brazil iliyoanza fainali za mwaka huu kwa sare dhidi ya Uswisi, itaikabili Costa Rica na baaye utapigwa mchezo kati ya Serbia na Uswisi saa 3:00 usiku.

Brazil nayo itashuku dimbani ikifahamu fika kuwa Costa Rica iliyo jeruhiwa katika mchezo uliopita kwa kupigwa bao 1-0 na Serbia, itashuka dimbani kama Nyati aliyejeruhiwa ikisaka ushindi kwa udi na uvumba.

Kutokana na hilo na kile kilichowakuta majirani zao Argentina jana walipopokea kichapo cha kustusha cha mabao 3-0 kutoka kwa Croatia, ni wazi kuwa kutakua na patashika dimbani.

Kauli ya Mbowe Baada ya Kufiwa na Kaka Yake

$
0
0
Kauli ya Mbowe Baada ya Kufiwa na Kaka Yake
Mwenyekiti wa Chadema Taifa na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe amewashukuru wote walioenda kuwaona baada ya kusikia kifo cha kaka yake, Marehemu Henry Mbowe na kufika kanisani kwaajili ya kuuaga mwili wa kaka yake huyo.



Mbowe ametumia kurasa zake za mitandao ya kijamii, amesema hata wale waliompigia na kutoa pole amepokea pole zao kwa mikono miwili.

Kwa mara nyingine nawashukuru wote mliotukimbilia kama familia baada ya kusikia kifo cha kaka yangu mpendwa sana Henry, mlioweza kufika nyumbani au pale Kanisani Usharika wa Kunduchi Dar es salaam, kwa ajili ya kumuaga kaka na kutoa heshima za mwisho kwa wale ambao wasingepata nafasi ya kusafiri nasi kuelekea mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya maziko hapo kesho nawashukuru sana.

Wengine wamenipa pole kwa kwa kunipgia simu kwa sababu wasingeweza kufika kwa wakati kutokana na shughuli mbalimbali za kila siku zinazotukabili sisi kama wanaadamu, nimepokea pole zenu kwa mikono miwili ahsanteni sana.

Nawashukuru sana sana wote, tunategemea Mungu akipenda kesho tutampumzisha kaka katika nyumba yake ya milele nyumbani Machame kijijini Nshara. Nawashukuruni Mungu awabariki sana ndugu zangu.

Majambazi Wavamia Duka la Jumla Waua Mlinzi kwa Risasi

$
0
0
Majambazi Wavamia Duka la Jumla Waua Mlinzi kwa Risasi
Mkazi wa Kata ya Bugogwa wilayani Ilemela jijini hapa, aliyetambulika kwa jina moja la Saytaa ameuawa kwa kupigwa risasi kifuani wakati akijaribu kupambana na majambazi waliovamia maduka.

Akizungumzia tukio hilo, leo Juni 22, Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilayani Ilemela, Khadija Nyembo amesema tukio hilo limetokea jana Juni 21 saa sita na nusu usiku.

Amesema baada ya mlinzi huyo kusikia mlio wa bunduki alienda sehemu ya tukio kutoa msaada wa kuwadhibiti wahalifu hao ndipo alipouawa.

Majambazi hao wanaodhaniwa walikuwa na silaha za moto walivamia duka la jumla la vifaa vya ujenzi na duka la nguo lililokuwa pia lina huduma za kifedha na kupora fedha kisha kumuua mlinzi huyo.

Nyembo ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa wilaya hiyo amesema: “Watu waliposikia mlio wa bunduki hawakutoka lakini yeye alienda, katika kupambana nao bila kuchukua tahadhari wakampiga risasi.”

Mwenyekiti wa Mtaa wa Bugogwa, Alphonce Bundege amesema, licha ya mtaa wao kuwa na askari wa doria lakini siku ya tukio walichelewa.

Nikki Mbishi amchana P Funk kupitia Harmorapa

$
0
0

Baada ya producer Mkongwe Bongo, P Funk Majani kueleza kuwa ameka tamaa na sanaa ya Bongo hadi kufikiri kwenda kufanya kazi zake nje, rapper Nikki Mbishi ameeleza anapofeli producer huyo.

Awali P Funk akipiga stori na Clouds TV alieleza kuwa amekuwa hasikiki kwa sasa kutokana na changamoto zilizopo kwenye game ingawa mchango wake ni mkubwa katika muziki huo.

“Inanikatisha tamaa na hadi sasa hivi nataka niweke vitu sawa labda nikajaribu Amerika kwa sababu muda unaenda, nazeeka,” alisema P Funk.

Sasa Nikki Mbishi ameeleza kuwa P Funk amefikia hatua hiyo kutokana na kuanza kufuata trend, majina na fedha na sio vipaja. Kupitia Instagram ameandika;

Majani tatizo siku hizi huamini vipaji vikali tena unaamini majina tu na hela ndio maana yanatokea hayo,we still have that opportunity to make it since giving up ain’t an option.

Unaacha kutupa midundo mikali wenye contents zetu una-deal na trends na kiki za akina Harmorapa, I find no use for you to complain.Unadhani hatupendi kufanya kazi na wewe?.

Hata hivyo Nikki Mbishi amekuwa si rapper wa kufanya kazi sana na ma-producer wakongwe, mara nyingi amesikika kwenye midundo ya ma-producer kama Duke Tachez, Texa, Mujwahuki, Palla Midundo, Bunduki Midundo, Teknohama na wengineo.

Bongo5

Tunatibu na Kuponesha Kabisa Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha Bila Kupasua na Vidonda vya Tumbo

$
0
0


TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME BUSHA BILA BILA KUPASUA NA VIDONDA VYA TUMBO: kwa nini uhendelee kuteseka NA kujiona mpweke pale ukutanapo NA mke au mpenzi wako kwa sababu tu hunaupunguvu wa nguvu za kiume na uume mdogo

MAPRO POWER NO 2 ndio tiba sahii ya kukurudishia heshima ya ndoa yako 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni mda wa dakika 15-20 kwa tendo LA kwanza 2 itaufanya uume wako uhonekane mkubwa hasa kwa wale wanaume ambao wamefanyiwa tohara wakiwa wadogo sana au wakiwa watu wazima kwani ipo dawa ya kuimalisha misuli ya uume 3 itakupa uwezo wa kurudia tendo LA ndoa zaidi ya Mara tatu 4 uhuimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa ?

WAI SASA UPATE TIBA YA UKWELI NA UHAKIKA NA NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA ata wazee wa miaka 80 wanatumia na kupona kabisa ? Tunatoa dawa za uzazi maumivu ya mgongo na kiuno ,kupunguza kitambi ,matiti makubwa,dawa za kisukari,presha,dawa za mvuto wa mpenzi ambaye akutaki au hakuhudumii ipasavyo kutengeneza shepu kwa kina Dada, fika ofisini kwetu MBAGALA ZAKHEMU BARABARA YA JESHINI HIENDA KIBONDEMAJI utaona ifisi himeandikwa MABULA CLINIC

AU PIGA SIMU NO 0743362017 DR AGU

KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUFIKA OFISINI UDUMA HII UTALETEWA

Mwarabu Fighter Asimulia Yaliyomkuta

$
0
0
Hali ya Mwarabu Fighter Asimulia Yaliyomkuta
KUFUATIA Bodigadi wa Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz, Mwarabu Fighter aliyepata ajali mbaya alfajiri ya leo katika eneo la Mbezi Afrikana jijini Dar es Salaam na kupasuka kwenye uso, majeruhi huyo ameeleza kuwa kwa sasa anaendelea vizuri baada ya kupatiwa huduma ya kwanza katika Hospitali ya Lugalo iliyopo Mwenge jijini Dar kisha kuhamishiwa Muhimbili kwa matibabu zaidi.




Akizungumza kwa taabu na Global TV Online akiwa Muhimbili, Mwarabu Fighter anasema alikuwa amepakizwa kwenye bodaboda ambapo dereva wake alikiwa akilipita caterpillar, ghafla mbele yao alitokea dereva mwingine wa bodaboda na kusababisha ajali hiyo.


Anaeleza kwamba alipoteza fahamu kwa zaidi ya dakika ishirini kutokana na kutokwa na damu nyingi lakini anawashukuru madaktari kwa jinsi walivyompigania.

"Serikali Imewapa Watanzania Ugali,Tembele" Mtolea

$
0
0
"Serikali imewapa Watanzania ugali,tembele" Mtolea
Mbunge wa Temeke, (CUF) Abdallah Mtolea, amesema kwamba serikali inajua kwamba inawadhihaki watanzania kwa kudai kuwa uchumi unakuwa huku kiuhalisia wanafahamu fika hakuna kilichoongezeka ndiyo maana majukwaani hawazungumzii suala la mlo bora kwa watanzania bali wanakuwa wanazungumzia sifa

Mh. Mtolea ameyasema hayo wakati akichangia hoja katika mjadala wa kupitisha Bajeti Kuu ya serikali 2018 / 2019 iliyowasilishwa Bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philip Mpango.

Amesema kabla ya Waziri kuwasilisha Bajeti alizungumzia hali ya uhumi nchi kwamba inazidi kukua lakini kiuhalisia alichokiona yeye kilichoandikwa kina lengo la kuwafurahisha wazungu au Benki ya Dunia ili kuonyesha kuwa serikali ya Tanzania bado ina sifa ya kuweza kukopa.

Mtolea amesema kwamba kitendo cha serikali kudaii kuwa wamewezesha pato la kila mtanzania kuongezeka ni kejeli kwani hicho kiasi kilichoongezeka ni kiasi ambacho hakimpatii mtanzania milo mitatu zaidi ya kwamba itamptia ugali na tembele la kuchemsha.

"Serikali ya CCM inapenda sifa sana ndiyo maana majukwaani utasikia inasema kwamba wamenunua ndege, sijui miradi ya  Stigler's Gorge,, Standard Gauge lakini husikii wakisifia kuwa tumewezesha kula ugali na tembele la kuchemsha kwa sababu wanajua kuwa siyo sifa bali ni kejeli kubwa kwa watanzania" Mtolea.

Hata hivyo Mtolea ameongeza kwamba hata kitendo cha serikali kusema umri wa kuishi wa watanzania umeongezeka ni kejeli na kwamba mu kufikisha miaka 64 ni kawaida  na siyo ajabu kwa watu wenye maisha duni kutimiza umri huo endapo wataakuwa hawapati magonjwa.

Mbunge CCM Amwagia Sifa Alikiba Bungeni "Nikiingia Kwenye Gari Napiga Nyimbo za Alikiba tu Hadi Nashuka"

$
0
0
Mbunge CCM Amzimia Alikiba "Nikiingia Kwenye Gari Napiga Nyimbo za Alikiba tu Hadi Nashuka"
Siku chache baada ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amesema ni mpenzi mkubwa wa nyimbo za msanii wa Bongo Fleva, Ally Kiba.



Akizungumza na MCL Digital katika mahojiano maalum, Dk Bashiru amesema hata dereva wake anafahamu kuwa anampenda msanii  huyo na kwamba akiingia katika gari hupiga nyimbo za Ali Kiba hadi mwisho wa safari yake.



“Kwa upande wa wasanii, mimi napenda sana nyimbo za Ally Kiba,  dereva wangu ameshajua nikiingia kwenye gari anapiga tu nyimbo zote zinafululiza mpaka nashuka,”amesema.



“Ila sijui kama Ali Kiba ni mwana CCM ama la. Sitajali kama ni mwana-CCM kwasababu nyimbo zake zinafanya kazi niliyoisema ya kujengea watanzania hari ya kujiamini.”



Amesema wasanii wamewapamba sana Watanzania  kitaifa na hata kimataifa na kwamba hata nafasi ya waafrika katika tasnia hiyo iko juu jambo ambalo limeleta heshima.



“Mimi sijali mahadhi kama ni ya kigeni ama kikabila kama ni ya Kiswahili kama ni taarabu ili mradi una maudhui kuna ujumbe. Na ndani ya CCM sisi tunadhamini sana sanaa na tunakitengo maalum ambacho kipo chini ya uenezi kinaongozwa na Polepole (Katibu wa Itikadi na Uenezi Humprey Polepole) ,”amesema.



Amesema ndani ya chama wana kikundi cha TOT na Vijana Jazz ambavyo anataka viimarike na kufanya kazi ya kukitangaza chama kuhusu mazuri ya nchi.



Amesema bila ya kuwa na michezo, Taifa halitatambuliwa, umoja hautokuwepo na hata hatua za maendeleo hazitatambuliwa na mataifa mengine.



Amesema CCM wanamiliki viwanja lakini bado haviko katika hali nzuri na kwamba atajaribu kuwekeza na kuvifufua ili viwe na mchango katika jamii.

Waliovamia Pori la Akiba Wapewa Siku 30 Kuondoka

$
0
0
Waliovamia Pori la Akiba Wapewa Siku 30 Kuondoka
Serikali ya awamu ya tano kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imewapa siku 30 wananchi waliovamia pori la akiba Swagaswaga na kuendesha shughuli zao ikiwemo kilimo, makazi na ufugaji ndani ya pori hilo na kutakiwa waondoke kwa hiara yao kabla ya kuondolewa kwa nguvu.

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Handa Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma wakati wa ziara yake ya kikazi ya kutatua mgogoro wa ardhi kwenye hifadhi hiyo wilayani humo.

"Tunawapa siku 30 muanze kutoka wenyewe, baada ya siku 30 tunatoa notisi ya siku nyingine 30 za kutumia nguvu, kwahiyo kuanzia sasa hivi anzeni kujipanga wenyewe na kuondoka wakati Halmashauri ikifanya tathmini ya maeneo ya vijiji ambavyo ni halali ya kuwagawia kwa wale watakaopenda kupewa maeneo huko", amesema Dkt. Kigwangalla.

Aidha, Waziri Kigwangalla amesema sheria za uhifadhi haziruhusu mtu yeyote kuingia ndani ya maeneo ya hifadhi na kuendesha shughuli za kibinadamu na kwamba kufanya hivyo ni kudharau Sheria na Malmlaka zilizopo.

Kwa upande mwingine, Dkt. Kigwangalla amesema kwa upande wa wananchi wa kijiji cha Handa ambacho kilianzishwa kimakosa ndani ya pori hilo wataendelea kubaki mpaka pale wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Tamisemi na Ardhi zitakapoamua hatma yao ikiwemo ama kulipwa fidia kupisha eneo hilo au waendelee kubaki na mipaka ya hifadhi isogezwe.

Kesi ya Mbowe na Wenzake Kusikilizwa Siku Tano Mfululizo

$
0
0
Kesi ya Mbowe na Wenzake Kusikilizwa Siku Tano Mfululizo
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  itawasomea maelezo ya awali (PH) na kuanza rasmi kuisikiliza kesi ya jinai inayowakabili viongozi tisa wa Chadema akiwamo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kwa siku tano mfululizo, kuanzia Juni 25 hadi 29, 2018.



Mbowe na wenzake walipaswa kusomewa maelezo ya awali leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri lakini ilishindikana  kwa sababu mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Freeman  Mbowe amefiwa na kaka yake Henry Mbowe na amekwenda msibani, Moshi.



Pia, Mahakama imemtaka mshtakiwa wa tano katika kesi hiyo, Esther Matiko mbunge wa Tarime mjini ambaye ni mgonjwa ahudhurie mahakamani bila ya kukosa na  asipofanya hivyo hatua dhidi yake zitachukuliwa.



Hata hivyo, mawakili wanaowatetea washtakiwa hao Peter Kibatala na Jeremiah Mtobesya hawakuwapo mahakamani, Kibatala alikuwa amehudhuria kesi  Mahakama Kuu, huku Mtobesy, akihudhuria kesi Mahakama ya Afrika Mashariki  Arusha.



Hivyo waliwakilishwa mahakamani hapo na mawakili Nashon Nkungu, Frederick Kihwelo na Hekima Mwesigwa.



Awali,  wakili wa  Serikali Mkuu,  Faraja Nchimbi   alieleza mbele ya Hakimu  Mashauri kuwa kesi ilipangwa kwa ajili ya washtakiwa kusomewa Maelezo ya awali na  kwamba wamejipanga kuendelea.



Lakini ilishindikana kwa sababu Mshtakiwa

Mbowe hakuwapo mahakamani  kwa sababu amefiwa na kaka yake Henry Mbowe na amekwenda Moshi katika mazishi. 



Mbowe aliwakilishwa mahakamani hapo na mdhamini wake Grayson Celestine ambaye aliwasilisha nakala ya cheti cha kifo mahakamani ili kuithibitishia Mahakama.



Kwa upande wa mshtakiwa Esther Matiko aliwakilishwa na mdhamini wake, Patrick John aliyeieleza Mahakama kuwa anaumwa na akawasilisha nyaraka ya mapumziko kutoka kituo cha afya.

Hata hivyo, nyaraka hiyo ilipingwa na wakili Nchimbi kwa madai kuwa ni batili haina Maelezo yanayojitosheleza ambayo yanayoweza kuishawishi mahakama kuamini Matiko ni mgonjwa na anapaswa kupumzika kwa siku saba.



Washtakiwa waliokuwapo mahakamani ni mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu Katibu Mkuu Bara na John Mnyika.



Katibu wa chama hicho, Dk Vicenti Mashinji, mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee na mbunge wa Bunda, Esther Bulaya.



Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 13 ikiwamo kufanya mkusanyiko usio halali, na kusababisha ghasia. Pia wanadaiwa Februari mwaka huu walikiuka agizo la kuwataka kutawanyika na kusababisha uvunjifu wa amani. 

Tuzo za Mchezaji Bora Kutolewe Kesho

$
0
0
Tuzo za Mchezaji Bora Kutolewe Kesho
Tuzo za Ligi Kuu Tanzania bara msimu wa mwaka 2017/18 zinatarajiwa kutolewa kesho Jumamosi Juni 23,2018 kwenye ukumbi wa Mlimani City na mdhamini mkuu wa ligi hiyo baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika tangu Juni 20 mwaka huu.

Hayo yamebainishwa na Afisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Cliford Ndimbo wakati akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya kumalizika kwa zoezi la upigaji kura kinachofuata ni kutangazwa kwa washindi walioshinda katika vinyang'anyiro mbalimbali vilivyokuwa vinagombewa na washiriki hao.

"Zoezi la upigaji kura lilihusisha Makocha wa Ligi kuu, Manahodha wa Timu za Ligi Kuu pamoja na wahariri wa habari za Michezo", amesema Ndimbo.

Kwenye Tuzo hizo timu ya Simba SC ambayo ndio mabingwa wapya wa ligi kuu wamefanikiwa kubakisha majina matatu ya wachezaji kati ya 15 waliokuwa wanawania Tuzo ya mchezaji bora ambao ni Emmanuel Okwi, John Bocco na Erasto Nyoni.

Serikali Yagoma Kufuta Tozo ya Kuvukia Daraja la Kigamboni

$
0
0
 Serikali Yaweka Ngumu Kufuta Tozo ya Kuvukia Daraja la Kigamboni
Serikali ya awamu ya tano kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Watu wenye ulemavu imesema haioni haja ya kufuta tozo ya kuvukia daraja la Kigamboni na watu pamoja na vyombo vya moto kupita bure kwasababu daraja hilo limefanyiwa uwekezaji ili iweze kuingia pato serikali.

Hayo yamesemwa leo Juni 22, 2018 Bungeni Jijii Dodoma na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, na Walemavu, Anthony Mavunde wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa viti maalum Zainab Mndolwa Amiri aliyetaka kufahamu ni lini serikali itasitisha tozo katika daraja la kigamboni kwa kuwa madaraja yote watu hupita bure.

"Ninaomba ieleweke kwamba daraja la Kigamboni ni sehemu ya uwekezaji la Shirika la Taifa Hifadhi ya Jamii (NSSF), na fedha iliyotumika kwaajili ya uwekezaji huo ni fedha ya wanachama ambapo mwishoni pia fedha hiyo hiyo huwa inatumika kwenda kulipia mafao ya watu. Hivyo hatuwezi katika hali ya kawaida kufuta tozo na watu wakapita bure katika eneo hilo kwasababu ni eneo la uwekezaji", amesema Antony Mavunde.

Kwa upande mwingine, Antony Mavunde amesema Serikali kupitia shirika la taifa hifadhi ya jamii NSSF ambao ndio wanasimamia uendeshaji wa daraja hilo hadi kufikia mwezi Machi 2018 limeshakusanya kiasi cha takribani shilingi Bilioni 19.7 tangu daraja hilo lilipoanza kutumika rasmi mwezi Mei mwaka 2016.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0



Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Barua ya IGP kujiuzulu yakubaliwa na Rais

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Gambia amelazimika kujiuzulu baada ya watu watatu kuuawa mapema wiki hii katika eneo la Faraba Banta, kusini mwa mji mkuu wa nchi hiyo Banjul, kufuatia polisi kuwafyatulia risasi waandamanaji. 

Wakazi wa mji huo walikusanyika na kuandamana kupinga uchimbaji wa mchanga ambao umekua ukitishia mazingira na mashamba yao ya mchele. 

Barua ya kujiuzulu ya Landing Kinteh ilikubaliwa na Rais Adama Barrow jana Alhamisi wiki hii baada ya kukosolewa na upinzani kufuatia vurugu za Faraba Banta. Hata hivyo amedai hakuwaamrisha polisi kuwafyatulia risasi waandamanaji. 

Rais Adama Barrow anatarajia kuzuru mji huo wa Faraba Banta leo ili kukutana na familia za waathirika ambapo pia shughuli za uchimbaji mchanga zimesimamishwa kwa muda.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo. 

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa. 

MIHAYO: 
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako. 

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521 

Tupo Mbagala

Katibu Mkuu NECTA Ashambuliwa na Wananchi

$
0
0

Katibu mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk Charles Msonde ameshambuliwa na kujeruhiwa na wananchi baada ya gari alilokuwa amepanda kugonga pikipiki na kusababisha kifo cha dereva.


Tukio hilo lilitokea juzi saa kumi jioni katika Kijiji cha Inala, Kata ya Ndevelwa katika Manispaa ya Tabora.


Dk Msonde amesema anaendelea vizuri na kwamba ajali ilitokea akiwa katika utekelezaji wa majukumu yake ya kazi.


“Ninaendelea vizuri. Haya maumivu ninayoyasikia yanatokana na kipigo kutoka kwa wananchi waliotuvamia baada ya ajali ile kutokea,” alisema Dk Msonde.


Hata hivyo, katibu mtendaji huyo hakuwa tayari kueleza kwa kina chanzo cha ajali na namna walivyoshambuliwa. “Naomba itoshe kusema ninaendelea vizuri.”


Ofisa habari wa Necta, John Nchimbi alisema Dk Msonde aliruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kidete jana alikokuwa akipatiwa matibabu.


Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tabora, Nestory Didi alisema gari alilopanda Dk Msonde lilimgonga Mzee Salum (23) alipokuwa akikata kona kuingia nyumbani kwake.


Alisema kutokana na ajali hiyo wananchi walifanya vurugu ndipo dereva alipokimbia na kumwacha Dk Msonde.


Didi alisema Dk Msonde alitibiwa na kuruhusiwa na hakuwa na madhara makubwa mwilini kama baadhi ya watu wanavyodai.


Kamanda huyo aliwataka wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake waache sheria ichukue mkondo wake.


Chanzo: Mwananchi

Bashe ajitofautisha kwa wabunge wenzake

$
0
0

MBUNGE wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), amewataka wabunge wenzake kuiacha Kampuni ya SICPA ya Uswisi iliyopewa tenda ya kutekeleza mradi wa stempu za kielektroniki, ifanye kazi yake. 

Alitoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma juzi alipokuwa akichangia mapendekezo ya bajeti kuu ya serikali kwa mwaka ujao wa fedha na Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017. 

Alisema wafanyabiashara wana kawaida ya kutumia mianya ya kukwepa kodi na serikali imekuwa na jitihada za kuziba mianya hiyo kwa kuboresha sheria zake na ndiyo maana Waziri wa Fedha na Mpango, Dk. Philip Mpango amekuja na mfumo huo wa stempu mpya za kielektroniki. 

“Mheshimiwa Spika, moja ya eneo ambalo wafanyabiashara hutumia nafasi ya 'ku-avoid' (kukwepa) kodi ni kwenye VAT (Kodi ya Ongezeko la Thamani). Eneo hili liko 'connected' (linaunganishwa) na 'production' (uzalishaji)," Bashe alisema. 

Alimtaka Waziri Mpango kufanyia kazi mawazo yote yaliyotolewa na wabunge, akisisitiza kuwa tathmini na utendaji kazi unaonyesha maeneo ambayo SICPA imewahi kufanya kazi yamekuwa na mafanikio. 

“Pale ambapo tumejua wamekuwa na kesi na rushwa, Mheshimiwa Spika suala la rushwa ni suala la watu kama mfumo utaruhusu watoe rushwa, waweze 'ku-win' (kushinda) 'more' (zaidi), 'it is our weakness' (ni udhaifu wetu)," Bashe alisema na kufafanua zaidi: 

“Lakini, kama mfumo wao huu utatusaidia kufanya 'production count' (hesabu za uzalishaji), kama utatuongezea mapato, nikuombe Mheshimiwa Waziri, tunapokuja mwaka kesho ambapo tutakuwa na miezi sita ya utekelezaji wa bajeti, tuletee taarifa ya 'performance' (utendaji) wa hii kampuni."

Mbunge huyo alisema ikiwa baada ya miezi sita ya utekelezaji, kampuni hiyo haitafanya vizuri, basi serikali ichukue hatua. 

“Kuhofia kwa sababu watu watatoa rushwa, kama kuna watu walitoa rushwa 'it is their problem' (ni tatizo lao), watu wetu wakipewa rushwa 'it is our problem' (ni tatizo letu), tuwaache wafanye kazi,”alisema Bashe. 

Katika mjadala huo, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Sugu', alidai asilimia 98 ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi wamejawa unafiki kwa kuwa wanapokuwa nje wanalalamika mambo hayaendi vizuri, lakini wakifika ndani ya Bunge wanasifia. 

"Mheshimiwa Spika, asilimia 98 ya wabunge wa CCM wamejaa unafiki, huko nje tukiwa tunakunywa chai kantini, wanalalamika mambo yanavyokwenda lakini wakija humu ndani hawasemi," Sugu alisema. 

"Nimewagundua wala hawampendi Rais John Magufuli kwa sababu mtu unayempenda siku zote unamweleza ukweli." 

Sasa Nigeria vs Argentina itakuwa fainali

$
0
0

Timu ya taifa ya Nigeria baada ya kupokea kipigo chake cha kwanza katika mchezo wao dhidi ya Croatia kwa magoli 2-0, leo ilicheza mchezo wake wa pili wa World Cup 2018 dhidi ya Iceland.

Nigeria leo dhidi ya Iceland wamefanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-0, shukrani za kipekee kwa Ahmed Musa aliyefunga magoli yote mawili dakika ya 48 na 74 kutokana na kuwa na utulivu katika eneo la hatari na kuzitumia nafasi zote mbili kwa ufasaha.

Ushindi huo sasa unawaweka pazuri Nigeria na kuwapa imani Argentina kuwa wanaweza kufuzu hatua ya 16 bora kwani kufuzu kwaArgentina na Nigeria kutatokana na timu zote mbili kupata ushindi zitakapo kutana June 26 ila Nigeria hata sare inamvusha hatua inayofuata.

Croatia tayari amefuzu hatua ya 16 kutokana na kupata ushindi mechi mbili na kuwa na point 6, wakati Nigeria wao wapo nafasi ya pili kwa kuwa na point tatu, Iceland nafasi ya tatu kwa kuwa na point moja sawa na Argentina walio nafasi ya nne kwa kutofautiana magoli ya kufungwa.

Panya wamevamia mtambo wa ATM na 'kutafuna' pesa zote zilizokuwepo kwenye mashine hiyo

$
0
0

Ni baada ya Mafundi waliofika kuukarabati mtambo huo wa ATM ambao ulikuwa umeharibika kwa siku 12 katika jimbo moja nchini India walipigwa na butwaa walipoufungua kubaini tatizo lilikuwa wapi.

Noti za thamani ya rupia 1.2m (£13,300; $17,600) zilikuwa zimechanwa na kuraruliwa na panya katika benki hiyo jimbo la Assam.

Polisi wanasema panya hao pengine waliingia ndani ya mtambo huo kwa kupitia kwenye tundu lililokuwa litumiwe kuingizia nyaya, gazeti la Hindustan Times limeripoti.

Mafundi waliofungua mtambo huo walipata noti za rupia 2,000 na rupia 500 zikiwa zimeharibiwa.

Walifanikiwa kunusuru noti za jumla ya thamani ya rupia 1.7 milioni. 
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images