Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Mkubwa Fella Afunguka Kuhusu Media Zisizopiga Nyimbo za WCB

$
0
0
Mkubwa Fella Afunguka Kuhusu Media Zisizopiga Nyimbo za WCB
Meneja wa Mkubwa na Wanae na WCB, Said Fella amedai kauli ya WCB iliyotolewa hivi karibuni ya kuzitaka baadhi ya media kuendelea kuacha kupiga ngoma za wasanii wa label hiyo, ilizungumzwa kwa hasira kutokana na mambo yanayoendelea kwenye tasnia ya muziki.

 Fella ambaye pia ni diwani wa kata ya Kilungule amedai alitegemea baada ya media kuona wasanii wa WCB bado wanafanya vizuri licha ya kutopiga ngoma zao, wangekaa meza moja na WCB na kuweza kujadili matatizo yao.

"

Mlipuko Mkubwa Watokea Katika wa Waziri Mkuu wa Ethiopia

$
0
0
Mlipuko Mkubwa Watokea Katika wa Waziri Mkuu wa Ethiopia
Mlipuko mkubwa katika mkutano wa waziri mkuu mpya wa Ethiopia, Abiy Ahmed

Haijulikani wazi idadi ya watu walioathirika lakini imebidi kiongozi huyo aondoshwe kwa haraka muda mfupi baada ya kutoa hotuba yake.

Maelfu walikuwa wamekusanyika katika bustani kuu ya Meskel mjini Addis Ababa.

Vyombo vya habari nchini vinaripoti kuwa watu kadhaa wamejeruhiwa na wamepelekwa katika kituo cha afya kilicho karibu na bustani hiyo kupokea matibabu.

Mwandishi wa BBC nchini Ethiopia Emmanuel Igunza aliyekuwa katika eneo hilo anasema kulikuwa na kelele nzito na kubwa iliyosikika karibu na jukwaa walipokaa watumashuhuri muda mfupi baada ya waziri mkuu Abiy Mahmed kumaliza kuuhotubia umati.

Hali ya utulivu sasa imerejea na duru za polisi zinasema wanachunguza tukio hilo.

Umati mkubwa wa watu ulikusanyika katika mkutano huo ulioandliwa kuiunga mkono serikali ya kiongozi huyo mpya anayeidhinisha mageuzi ambayo hayajawahi kushuhudiwa nchini .

Kuhusu Picha Tata za Uwoya Dogo Janja Asema Haya "Irene ni Staa Mapaparazi Hawakoso"

$
0
0

Kuhusu Picha Tata za Uwoya Dogo Janja Asema Haya "Irene ni Staa Mapaparazi Hawakoso"
Msanii Dogo Janja amefunguka kuhusu kusakamwa kwa mke wake, Irene Uwoya kufuatia picha zake alizoweka kwenye mitandao ambazo kwa asilimia kubwa ziliacha wazi umbile lake.

Dogo Janja amesema si kweli mke wake alikuwa uchi kama inavyoelezwa bali ni vazi la kawaida kwa maeneo ya ufukweni, pia mke wake ni staa hivyo mambo kama hayo ni kawaida kutokana na kufuatiliwa na mapaparazi.

“Irene kuvaa vile kwanza alikuwa ufukweni, Irene ni staa popote anapokuwa lazima kuwe na kamera, paparazi hawakosi, kwa hiyo popote wanapoenda paparazi kwao ni content, so alikuwa pale beach kabiga picha kavaa nguo hakuwa uchi,” amesema.

Si Dogo Janja pekee aliyemkingia kifua Irene Uwoya kutokana na picha hizo, bali hata mwingizaji wa filamu Bongo, Shamsa Ford alieleza kuwa Irene alikuwa sahihi kuvaa vile kutokana na eneo husika (ufukweni).

Trump: Korea Kaskazini Bado ni Tishio Kubwa

$
0
0
Trump: Korea Kaskazini Bado ni Tishio Kubwa
Rais wa Marekani Donald Trump ameidhinisha upya vikwazo dhidi ya Korea kaskazini akitaja taifa hilo kuwa 'tishio liliso la kawaida' kutokana na silaha zake za nyuklia - siku 10 tu baada ya kutamka kwamba hakuna hatari yoyote kutoka kwa Pyongyang.

"Hakuna tena tishio kutoka Korea kaskazini," alituma ujumbe mnamo Juni 13, siku moja baada ya kukutana na kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-un huko Singapore.

Hatua hiyo imekuja wakati Marekani na Korea kusini zimefutilia mbali mazoezi mawili ya pamoja ya kijeshi.

Wizara ya ulinzi Marekani Pentagon imesema lengo ni kuunga mkono majadiliano ya kidiplomasia.
Inafuata uamuzi wa mapema wiki hii kusitisha mazoezi makubwa ya kijeshi ya pamoja katiya Marekani na Korea kusini yaliopangwa Agosti.

Rais Trump ameahidi kusitisha 'uchokozi wa kivita' wa kila mwaka kati ya washirika katika hatua ambayohaikutarajiwa kwenye mkutano wake na Kim, akiutaja kuwa "uchokozi" na "ulio na gharama kubwa".

Hilo limezusha mshtuko kwa wengi, kutokana na kuwa katika siku za nyuma Marekani imelalamika kuwa mazoezi hayo ni ya ulinzi tu na yalio muhimu kwa muungano wake wa kijeshi na Seoul.

Ndivyo inavyoonekana, lakini Marekani imekuwa na 'hali ya dharura kitaifa' iliyoidhinishwa kuhusiana na Korea kaskazini tangu 2008.

Tangu hapo marais wamekuwa wakiidhinisha hali hiyo kuendelea mtawalia na vikwazo dhidi ya Pyongyang.

Rais Trump aliendeleza hali hiyo ya dharura Ijumaa kutokana na 'uwepo wa hatari ya kuongezeka kwa silaha katika rasi ya Korea na hatua na sera za serikali ya Korea kaskazini'.


Haya "yanaendelea kuzusha tishio lisilo la kawaida kwa usalama wa kitaifa, sera ya nchi za nje na uchumi wa Marekani", alisema katika taarifa kwa bunge.

Wanachama wa Democratic wanasema tamko la sasa kutoka ikulu ya White House linakwenda kinyume na majigambo ya awali ya rais Trump kuhusu ufanisi wa mkutano wa Singapore.

Alichotabiri Wema Sepetu kwa England Kombe la Dunia

$
0
0
Alichotabiri Wema Sepetu kwa England Kombe la Dunia
ACHA kabisa kwani mastaa mbalimbali wameonekana kufuatilia kwa ukaribu mkubwa michuano ya Kombe la Dunia, sasa muigazaji Wema Sepetu amesema anaamini timu ya Taifa ya England ndiyo mabingwa wa michuano hiyo mwaka huu.

England imeanza vyema michuano ya Kombe la Dunia inayofanyika Urusi baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 kwenye mchezo wao wa kwanza dhidi ya Tunisia.

Wema amejigamba mbele ya mwandishi wa Championi Jumamosi kuwa, England itabeba kombe kwa sababu wachezaji wake wengi ni vijana na wana vipaji vikubwa.

“England ndiyo timu yangu nayoishabikia, kama hujui pia ni shabiki mkubwa wa Man United na wachezaji wengi waliopo Urusi wanachezea United kwa hiyo sikuona haja ya kwenda mbali wakati nyota wa klabu yangu wapo England. Matumaini ni makubwa sana ya kutwaa ubingwa kwani hata ukiangalia mchezo wa kwanza tulipata ushindi mzuri wa mabao mawili tofauti na timu nyingine ambazo zinapewa nafasi,” alisema Wema.

Mzee Majuto Asimulia Jinsi India Ilivyonusuru Maisha Yake

$
0
0
Mzee Majuto Asimulia Jinsi India Ilivyonusuru Maisha Yake
Mchekeshaji maarufu nchini Amri Athumani maarufu kama Mzee Majuto, amerejea nchini kutoka India alikokuwa akifanyiwa matibabu ya tezi dume.

Ambapo amefunguka kuwa sasa anaendelea vizuri mara baada ya kupatiwa matibabu ya hali ya juu .Amesema kuwa endapo asingefanyiwa matibabu hayo huenda angepoteza maisha.

”Mimi sijambo nashukuru, Hospitali ni Hospitali isipokuwa wenzetu wapo mbali zaidi, nimefanyiwa mambo mengi sana ambayo kama nisingefanyiwa ningeondoka mapema sana namshukuru Mungu” amesema Majuto.

Mzee Majuto ameongeza kuwa baada ya kumaliza matibabu hayo anataka kutenga muda mwingi kwaajili ya kupumzika zaidi na kuacha kujihusisha na masuala ya sanaa ya uchekeshaji na kudai kuwa Tanzania bado kunawachekeshaji wengi ambao wataweza kuendeleza sanaa hiyo.

Muigizaji huyo wa vichekesho kwasasa amepokelewa na yupo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Mei 4, 2018 Mzee Majuto alisafirishwa kwa gharama za serikali, kwenda nchini India kwa matibabu ya tezi dume baada ya kusumbuliwa na ugonjwa huo kwa kipindi cha muda mrefu.

Shirika la Reli Tanzania Laanza Kusafirisha Mizigo Uganda

$
0
0
Shirika la Reli Tanzania {TRC} limeanza kusafirisha mizigo kwenda Kampala nchini Uganda ikiwa ni miaka takribani 10 tangu usafiri wa mizigo kwenda Uganda kupitia reli usitishwe.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa .Amesema kuwa Treni hiyo huvuka ziwa Victoria kwa kutumia MV Umoja.

“Shirika la Reli Tanzania {TRC} laanza kusafirisha mizigo kwenda Kampala Uganda ikiwa ni miaka takribani 10 tangu usafiri wa mizigo kwenda Uganda kupitia reli usitishwe. Treni hii huvuka ziwa Victoria kwa kutumia MV Umoja.Hongera Serikali ya Awamu ya Tano,” ameandika Msigwa kupitia ukurasa wake wa Twitter.

 Msigwa ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Tunatibu na Kuponesha Kabisa Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume, Busha Bila Kupasua na Vidonda vya Tumbo

$
0
0

TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME BUSHA BILA BILA KUPASUA NA VIDONDA VYA TUMBO: kwa nini uhendelee kuteseka NA kujiona mpweke pale ukutanapo NA mke au mpenzi wako kwa sababu tu hunaupunguvu wa nguvu za kiume na uume mdogo 

MAPRO POWER NO 2 ndio tiba sahii ya kukurudishia heshima ya ndoa yako 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni mda wa dakika 15-20 kwa tendo LA kwanza 2 itaufanya uume wako uhonekane mkubwa hasa kwa wale wanaume ambao wamefanyiwa tohara wakiwa wadogo sana au wakiwa watu wazima kwani ipo dawa ya kuimalisha misuli ya uume 3 itakupa uwezo wa kurudia tendo LA ndoa zaidi ya Mara tatu 4 uhuimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa ? 

WAI SASA UPATE TIBA YA UKWELI NA UHAKIKA NA NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA ata wazee wa miaka 80 wanatumia na kupona kabisa ? Tunatoa dawa za uzazi maumivu ya mgongo na kiuno ,kupunguza kitambi ,matiti makubwa,dawa za kisukari,presha,dawa za mvuto wa mpenzi ambaye akutaki au hakuhudumii ipasavyo kutengeneza shepu kwa kina Dada, fika ofisini kwetu MBAGALA ZAKHEMU BARABARA YA JESHINI HIENDA KIBONDEMAJI utaona ifisi himeandikwa MABULA CLINIC 

AU PIGA SIMU NO 0743362017 DR AGU 

KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUFIKA OFISINI UDUMA HII UTALETEWA

Mtuhumiwa Mauaji ya XXXTentacion Akamatwa

$
0
0
Mtuhumiwa Mauaji ya XXXTentacion Akamatwa
MMOJA wa watu wanaotuhumiwa kumwua mwanamuziki wa Marekani, XXXTentacion, aliyetajwa kwa jina la Dedrick Williams, amekamatwa.

Mwanamuziki huyo aliuawa na watu wanaosemekana walikuwa wawili wakati anaondoka katika duka la pikipiki huko Pompano Beach, Florida, Jumatatu wiki hii.

Watu hao wanasemekana walikuwa wamefika dukani hapo na baadaye kumsubiri wakati anatoka nje na kumwua ambapo walichukua mfuko mdogo kutoka katika gari la marehemu na kuondoka.

Kamera za usalama zimemwonyesha mtu aliyekuwa amevaa T-shirt nyeupe na ‘kandamili’ za rangi ya machungwa iliyochuja, jambo ambalo polisi wamesema mtuhumiwa huyo ni Dedrick, kwani hata picha yake moja kwenye mtandao wa Facebook imeonyesha ana mavazi hayo.

Dogo Janja Aifananisha Tip Top na WCB

$
0
0
Dogo Janja Azifananisha Tip Top na WCB
Msanii wa muziki Bongo, Dogo Janja amefunguka mchango wa Babu Tale ndani ya Tip Top Connection kwa sasa.

Hii ni baada ya Babu Tale kuwa sehemu ya menejimenti ndani ya lebo ya WCB na kuibua madai kuwa meneja huyo kaitelekeza Tip Top Connection.

Dogo Janja akiwa katika la Tamasha la Kuibua Vipaji vya Muziki mkoani Arusha amesema kuwa hilo halina ukweli wowote kwani wamekuwa wakishirikiana kwa mambo mengi.

“Hapana sio kweli, Babu Tale anasimamia kazi zangu sana sana ila kwamba huku Tip Top sisi hatuko bize kama Wasafi ndio maana unaoa muda wote yupo kule, hatuna matukio,” amesema.

“Lakini nikiachia wimbo utaona redioni nitaenda na Babu Tale, so mimi sina matukio mengi ndio maana kwenye kazi zangu anakuwa mara chache sana pale ninapomuhitaji,” ameeleza Dogo Janja.

Hata hivyo licha ya Dogo Janja kuwa Tip Top Connection anapata mchango mkubwa kutoka kwa Manzese Music Baby (MMB), menejimenti ambayo imeanzishwa na Madee.

Mlipuko Wajeruhi 80 Uliotokea Kwenye Mkutano wa Waziri Mkuu wa Ethiopia

$
0
0
Mripuko Wajeruhi 80 Uliotokea Kwenye Mkutano wa Waziri Mkuu wa Ethiopia
Watu 83 wamejeruhiwa kufuatia mripuko wa bomu katika mkutano wa kwanza wa hadhara wa waziri mkuu mpya wa Ethiopia, Abiy Ahmed, katika mji mkuu wa nchi hiyo ambao ulihudhuriwa na maelfu ya watu.

Mripuko huo ulisikika muda mchache baada ya Abiy kumaliza hotuba yake katikati ya Addis Ababa, na kuwasababishia watu kukimbia kunusuru maisha yao. Waziri mkuu huyo aliwahiwa kukimbizwa akiwa salama.

Awali Abiy alikuwa ameliambia shirika la habari la FBC kuwa "watu wachache wameuawa na ni mashahidi wa upendo na amani," lakini taarifa za baadaye kutoka ofisi yake zilisema hakuna aliyepoteza maisha kwenye mripuko huo.

Waziri mkuu huyo mwenye umri wa miaka 42 alisema mripuko huo "yalikuwa mashambulizi yaliyopangwa vyema lakini yaliyoshindwa." Hata hivyo, hakurusha lawama zake kwa kundi lolote, ingawa alisema polisi wanaendelea na uchunguzi, akiongeza kuwa "mashambulizi hayo yalikuwa ya kitoto na yasiyokubalika. Daima mapenzi yatashinda. Kuwauwa wengine ni kushindwa. Kwa wale wanaojaribu kutugawa, nataka kuwaambia kuwa hamujafanikiwa."

Mripuko huo kwenye Uwanja wa Meskel uliokuwa umejaa watu mjini Addis Ababa, ulitokea baada ya wiki kadhaa za mageuzi makubwa kabisa ambayo yamewashitua wengi kwenye taifa hilo la pili kwa idadi ya watu barani Afrika, na baada ya miaka kadhaa ya hasira kali dhidi ya serikali, hali ya hatari, watu kukamatwa ovyo na kufungiwa kwa huduma za intaneti.

Waziri mkuu ndiye aliyelengwa?

 Äthiopien Kundgebung Premierminister Abiy Ahmed in Addis Ababa | Explosion (Getty Images/AFP/Y. Tadese)
Mara tu ulipotokea, watu walianza kuwashambulia polisi waliokuwepo kwenye mkutano huo, huku wakipiga mayowe: "Woyane chini, chini, Woyane ni wezi", wakitumia jina la dhihaka dhidi ya serikali, na kuwashutumu polisi kujaribu kuirejesha nchi kwenye machafuko.

Sababu ya mripuko huo hadi sasa haijaelezwa, lakini mmoja wa waandaaji wa mkutano huo wa hadhara aliliambia shirika la habari la Ujerumani, dpa, kwamba yalikuwa mashambulizi yaliyomlenga waziri mkuu binafsi.

"Waziri mkuu ndiye aliyekuwa shabaha ya tukio hili," alisema Seyoum Teshome, akiongeza kwamba: "Kuna mtu alijaribu kurusha bomu la mkono kwenye jukwaa ambako waziri mkuu alikuwa amekaa, lakini akazuiwa na umati wa watu." Kwa mujibu wa Teshome, watuhumiwa watatu walikamatwa kwenye tukio hilo, mmoja wao akiwa mwanamke.

Huu ulikuwa mkutano wa kwanza wa hadhara wa Abiy kwenye mji mkuu huo tangu kuingia madarakani mwezi Aprili, ingawa alishatembelea na kuhutubia maeneo mbalimbali ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.

"Ethiopia itakuwa ya juu tena, na misingi yetu itakuwa upendo, umoja na ujumuishaji," alisema kwenye mkutano huo wa Jumamosi (Juni 23) akiwa amevalia fulana ya kijani na kofia.

 Äthiopien Premierminister Abiy Ahmed in Addis Ababa | Demonstration mit Anhängern (Reuters)
Ndani ya kipindi hiki cha miezi mitatu, Abiy amefanya mabadiliko makubwa nchini Ethiopia, yakiwemo ya kuubadili mfumo wa vyombo vya ulinzi, kuwaachia huru wapinzani wa kisiasa, kuanzisha hatua za kuelekea uchumi wa soko huria na kutatua mzozo wa miongo miwili kati ya nchi yake na hasimu wake mkuu, Eritrea.

Abiy alichukuwa nafasi ya Hailemariam Desalegn, aliyejiuzulu mwezi Februari kufuatia wimbi kubwa la maandamano ya umma dhidi ya serikali yake yaliyoanza tangu mwaka 2015 na kusababisha vifo vya watu kadhaa.

Licha ya mageuzi anayoyasimamia kuonekana kuungwa mkono na umma, kuna mashaka ya kukubalika kwake ndani ya chama tawala cha Ethiopian People's Revolutionary Democratic Front (EPRDF), ambacho makada wake wanajiona kutengwa kando na hatua za waziri mkuu huyu mpya.

Siku ya Ijumaa (Juni 22), kundi la upinzani liitwalo Ginbot 7 lilitangaza kusitisha mashambulizi yake ya silaha kufuatia mageuzi yaliyotangazwa na serikali ya Abiy.

Mwezi uliopita, Ethiopia ilimuachia huru kiongozi wa ngazi za juu wa Ginbot 7, Andargachew Tsige, na pia waendesha mashitaka wakaondoa kesi dhidi ya kiongozi wa kundi hilo, Berhanu Nega, anayeishi nje ya nchi na ambaye tangu mwaka 2009 alikuwa amehukumiwa kifo kwa tuhuma za kupanga jaribio la mauaji.

Nabii Awataka Waumini Wamlipe Milioni 4 Ili Kuwasaidia Nigeria Kushinda Kombe la Dunia

$
0
0
Natii Awataka Waumini Wamlipe Milioni 4 Ili Kuwasaidia Nigeria Kushinda Kombe la Dunia
Nabii wa kujitawaza nchini Nigeria anayejulikana kama Tommy Yisa Aika amewataka waumini wake wamlipe kiasi cha naira 750,000 sawa na zaidi ya Milioni 4 za Kitanzania ili atume kikosi chake cha mashujaa wa maombi kiwasaidie timu ya taifa ya Nigeria kushinda kombe la dunia nchini Urusi.

Kwa upande mwingine Nabii huyo alisema kuwa timu hiyo ya taifa ya Nigeria ilipokea kichapo kutoka kwa Croatia kwa sababu Mungu alikuwa anaawadhibu kwa kumchagua kocha mzungu ambaye ni Gernot Rohr.

Katika mechi hiyo Nigeria walichapwa 2-0 na Croatia ambayo ndio ilikuwa mechi yao ya kwanza katika Kombe la Dunia Urusi.

Aidha Nabii huyo amesema kuwa waumini wake maalum wako tayari kuanza kazi na kurekebisha kosa walilolifanya na kupata neema ya Mungu katika michuano hiyo.

Nigeria watakutana na Argentina katika mechi yao ya mwisho Kundi D na ndio itakayoamua hatma ya timu hiyo kusonga mbele katika michuano hiyo.

DRC Kuweka kwa Kinga Marais wa Zamani ya Kutoshtakiwa

$
0
0
DRC Kuweka kwa Kinga Marais wa Zamani Kutoshtakiwa
Pendekezo la sheria ya kinga ya kutoshitakiwa marais wa zamani nchini Kongo limeanza kujadiliwa kwenye baraza la seneti mjini Kinshasa, ikielezwa kuwa ni njia ya rais Joseph Kabila kuondoka madarakani.

   
 Angola | Ankunft des kongolesischen Präsidenten Joseph Kabila bei einem meeting der süd- und zentralafrikanischen Staaten in Angola (REUTERS/K. Katombe)
Hata hivyo, upinzani umesema bado sheria hiyo ni lazima kutowahusisha viongozi wa taasisi zingine ambazo wengi wao wamehusika na ukiukaji wa haki za binadamu. Pendekezo hilo la sheria limeanza kusomwa upya miaka mitatu baada ya Seneta Modeste Mutinga kulipendekeza kwenye baraza la seneti kufuatia kile alicholelezea kuwa ni kinga ya kisheria kwa marais wa zamani mara watakapoachia madaraka.

Katiba ya Kongo inaelezea kwamba rais wa zamani ambaye alichaguliwa kidemokrasia anabaki kuwa seneta mnamo kipindi cha maisha yake yote.

 Demokratische Republik Kongo Wahlmaschine (Getty Images/AFP/J. Wessels)
Vifaa vya uchaguzi nchini DRC vitakavyotumika uchaguzi wa mwaka huu

Lakini Rais Kabila aliamuru wiki iliyopita kwamba kuweko na sheria mpya kuhusu kinga kwa marais wa zamani. Tume maalumu ya seneti iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza kwa kina pendekezo hilo, inaelezea kwamba ikulu ya rais Joseph Kabila ilipendekeza kwamba kinga hiyo iwahusishe pia viongozi wa taasisi na idara kadhaa za kitaifa, hususan maspika wa bunge na seneti, wakuu wa jeshi na polisi na wale wa idara za upelelezi na uhamiaji.

Upinzani umetupilia mbali pendekezo hilo na kusema ukimuacha rais, kila mtu ni lazima aweze kujibu kwa makosa aliyoyafanya ikiwa kuna vitendo vya rushwa na uhalifu. Sheria hiyo inapendekeza kwamba rais wa zamani ambaye alichaguliwa kidemokrasia mara ynapostaafu anapewa ulinzi wake binafsi na familia yake, na bajeti ambayo itamruhusu kuishi maisha mazuri, ikiwemo kupewa makaazi. Na ikiwa amefariki, mkewe na watoto wa chini ya umri wa miaka 18 wataendelea kufaidika na fedha hizo. Gregoire Lusenge, mbunge wa kutoka jimbo la Haut-Uele amesema kwamba kuweko na sheria hiyo kutawapa imani viongozi walioko madarakani kuhusu mustakbali wao na familia zao.

Kikao hiki maalumu cha bunge kilipendekezwa na Rais Joseph Kabila ambaye anatarajiwa kuhutubia taifa kuhusu hali ya kisiasa na kiusalama nchini. Baada ya kusomwa kwenye baraza la seneti pendekezo hilo la sheria litasomwa pia bungeni kabla ya kuidhinishwa na Rais Kabila.

 Kongo Protest & Ausschreitungen gegen Präsident Joseph Kabila in Kinshasa (picture-alliance/AP Photo/J. Bompengo)
Vijana wakishiriki katika maandamano ya kumpinga rais Joseph Kabila

Wadadisi wa maswala ya kisiasa wanaelezea kwamba kuidhinishwa kwa sheria hiyo ni ishara kwamba Rais Kabila hatowania muhula wa tatu kama wanavyoelezea wapinzani. Hivi sasa mjadala ni kuhusu matumizi ya mfumo wa kieletroniki wakati wa uchaguzi, ambapo tume huru ya uchaguzi imetangaza kupokea shehena ya  kompyuta 1,200 miongoni mwa laki moja zinazosubiriwa ifikapo Septemba mwaka huu.

Naibu mwenyekiti wa CENI, Norbert Basengezi, amesema kwamba kompyuta hizo zitasambazwa kila mahala kabla ya uchaguzi na kila mpigaji kura anatakiwa kujaribu kompyuta hiyo kabla ya Desemba 23. Upinzani na mashirika ya kiraia wanaelezea wasiwasi wao kuhusu matumizi ya kompyuta hizo ambazo wanasema huenda yakachangia wizi wa kura kwa manufaa ya chama tawala. Madai ambayo yanatupilia mbali na tume ya uchaguzi, CENI.

Aikon, Daimond na Rommy Jones Wanusurika Kifo Baada ya Kupata Ajari Marekani

$
0
0
Aikon, Daimond na Rommy Jones Wanusurika Kifo Baada ya Kupata Ajari Marekani
Msanii wa Bongo Flava, Diamond Platnumz amenusurika katika ajali ya gari nchini Marekani ambapo upo kwa ajili ya tour ya albamu yake ‘A Boy From Tandale’

Muimbaji huyo amepata ajali hiyo wakati akitokea kwenye show. Kupitia mtandao wa Instagram ameandika;

Dah Tumepata ajali na kunusurika kufa usiku wa leo wakati tunatoka kwenye show….ila Mwenyez Mungu ametupa nafasi nyingine tena ya kuishi na kuendelea kushikana mkono na vijana wenzangu mtaani kwa pamoja tuziokoe familia zetu duni🙏🏻….

Diamond ni ndiye mwanzilishi na mmiliki wa label ya WCB ambayo inasimamia wasanii kama Harmonize, Rayvanny, Rich Mavoko, Queen Darleen, Lava Lava na Mbosso.

Daina Kimaro Akanusha Kutoka Kimapenzi na Aslay

$
0
0
Daina Kimaro Akanusha Kutoka na Aslay
Muigizaji wa filamu Diana Kimaro amekanusha kutoka kimapenzi ya muimbaji Aslay baada ya kuonekana kuwa karibu zaidi katika siku hizi za usoni.


Wawili hao kila mmoja amekuwa akipost picha ya mwenzake na kutoa ujumbe ambao unatafsiriwa na wengi kwamba wawili hao wako kwenye mapenzi mazito.



Akiongea katika kipindi cha U heard cha Clouds FM, Diana amedai hamjui Aslay huku akienda mbali zaidi kwa kudai kwa sasa hayupo kwenye mahusiano.

“Mimi sina mahusiano na mtu yeyeto, mbona huyo mtu simjui,” alisema mrembo huyo ambaye ni mara chache sana kuonekana akijiachia na wanaume.

Aslay ambaye hivi karibuni ameachana na mama watoto wake, hajazungumza chochote kuhusiana na picha zake zinazosambaa mtandaoni na mrembo huyo

Watuhumiwa 28 Wanaosafirisha Watoto kwa Magendo Wakamatwa

$
0
0
Watuhumiwa 28 Wakamatwa kwa Kusafirisha Watoto Kimagendo
Shirika la polisi la EU limetangaza siku ya Ijumaa kuwa watuhumiwa 28 wamekamatwa nchini Uhispania kwa makosa ya kuwapitisha watoto kimagendo kutoka Morocco hadi Ulaya.
Katika operesheni hiyo Europol imetoa taarifa hiyo kuwa watuhumiwa 28 wamekamatwa kwa kuwasafirisha kimagendo watoto kueleka Ulaya.
Watuhumiwa wanaaminika kuwa waliwachukua watoto wadogo 100 kutoka Morocco hadi Uhispania na kisha kukamatwa nchini Hispania.
Europol pia imesema kuwa watoto walipelekwa Ulaya kwa € 2,000 (dola 2,330) hadi € 8,000 (dola 9,320) na waliingia Uhispania kinyume cha sheria kwa njia za hatari za usafiri kama vile boti za mbao, jet skis au boti za uvuvi au kwa magari na malori .
Aidha, polisi wamekamata nyaraka bandia, vifaa vya kuhifadhi data na simu za mkononi katika uendeshaji huo.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH mzee khamisi Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH mzee khamisi Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mzee khamisi Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Mzee khamisi Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi whatsapp +255 623448511 au 0783636592 au +255 622588038
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Nabii Nchini Nigeria Ataka Milion 4 Kuisaidia Nigeria Kushinda Kombe la Dunia

$
0
0

NABII NCHINI NIGERIA ATAKA MILLIONI 4 KUISAIDIA NIGERIA KUSHINDA KOMBE LA DUNIA 2018:
Nabii wa kujitawaza nchini Nigeria anayejulikana kama Tommy Yisa Aika amewataka waumini wake wamlipe kiasi cha naira 750,000 sawa na zaidi ya Milioni 4 za Kitanzania ili atume kikosi chake cha mashujaa wa maombi kiwasaidie timu ya taifa ya Nigeria kushinda kombe la dunia nchini Urusi.

Kwa upande mwingine Nabii huyo alisema kuwa timu hiyo ya taifa ya Nigeria ilipokea kichapo kutoka kwa Croatia kwa sababu Mungu alikuwa anaawadhibu kwa kumchagua kocha mzungu ambaye ni Gernot Rohr.

Katika mechi hiyo Nigeria walichapwa 2-0 na Croatia ambayo ndio ilikuwa mechi yao ya kwanza katika Kombe la Dunia Urusi.

Aidha Nabii huyo amesema kuwa waumini wake maalum wako tayari kuanza kazi na kurekebisha kosa walilolifanya na kupata neema ya Mungu katika michuano hiyo.

Nigeria watakutana na Argentina katika mechi yao ya mwisho Kundi D na ndio itakayoamua hatma ya timu hiyo kusonga mbele katika michuano hiyo.

Sokwe aliyekuwa anaongea lugha ya ishara amefariki

$
0
0

Leo June 23, 2018 Koko ni sokwe ambaye alikuwa amejifunza Lugha ya ishara ya Marekani, amefariki huko California akiwa na umri wa miaka 46.

Sokwe huyo wa Magharibi Kaskazini mwa Marekani alikufa akiwa usingizini katika hifadhi ya Milima ya Santa Cruz California Jumanne, kulingana na mtunzaji wa hifadhi ya sokwe huyo.

“Koko – Sokwe ambaye alijulikana kwa ujuzi wake wa ajabu wa lugha ya ishara, na kama balozi mkuu wa wanyama wake waliohatarishwa alikufa jana asubuhi,” taarifa kutoka kwa Mtunzaji wa hifadhi 

Kuvaa Shanga Miguu au Vikuku Kwa Mwanamke Kuna Maana Yoyote Mbaya?

$
0
0

Kumekuwa na tetesi nyingi kuhusu urembo huu wa kuvaa cheni za miguuni. Wengi wamekuwa wakisema kuwa cheni hizo zinamaanisha kwamba mvaaji anaonyesha kwamba yeye anaweza mapenzi ya kinyume na maumbile, au analika pande zote tetesi hizi zimeleta mchanganyiko kidogo kwenye urembo huu.

Watu wengine wamediriki hata kukataza kabisa wapenzi wao wasivae urembo huo, mimi binafsi siwezi kuongozana na mtu amevaa kitu kama hicho. Haya sasa kazi kwako mdau, wewe unaonaje ni sawa urembo huo kutumika, na je mwenza wako akivaa urembo huo, utaafiki? 
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images