Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Diallo Afunguka Amlipua Lowassa, Jisomee Hapa

$
0
0
Tuhuma za Kundi la Makuwadi wa EL dhidi yangu hayana msingi wowote na kama ni kweli Edward amewapa waziseme kwangu na kuhusisha Mheshimiwa Rais ni mwendelezo wa EL kumdharau Rais ambaye alimpa madaraka makubwa na kosa likiwa kukubali ajiudhuru baada ya kufanya madudu aliyoyafanya. Huu ni mwendelezo wa kumsumbus Rais ambao ulianza tangu 2008 baada ya kujiuzulu uwaziri mkuu. Anayoyasema haya sipendi kuyajibu ila kwa ajili ya kuweka kumbukumbu sawa, imebidi niyajibu lakini nikizingatia kuwa sitaweza kuyajibu yale ninayoyajua chini ya kiapo:

1: Sijamtuma Mzee yeyote kwenda kwa Lowasa kwa sababu sio waziri mkuu tena na hata kama angekuwa bado waziri mkuu nisingeweza kumwambia mtu akaniombee vyeo kwa Lowassa. Hao wazee aliowataja wapo Mwanza na mnaweza kupata namba zao za simu na kuwauliza kama nilishawahi kufanya hivyo. Pili, mwaka 2003/4 haukuwa mwaka wa uchaguzi, ilikuwaje niende kuomba cheo wakati niliingia baraza la Mhe. Rais Mkapa 2001? Wakati huo Lowassa hakuwa waziri mkuu! Tatu, mwaka 2004 sijaonana na JK na Karamagi hajanishawishi kumuunga mkono JK mwaka 2005. Mimi ndiye niliyetumwa kumwambia Lowassa asigombee 2005 kwavile dhambi na tuhuma dhidi yake zilizotolewa na Mwalimu zilikuwa kwenye mioyo ya watanzania na asingeweza kupata kura za ushindi isipokuwa angempunguzia JK kura zake na wote kukosa. Karamagi tumekutana naye bungeni baada ya kuchaguliwa ubunge baada ya kifo cha Mhe. Kinyondo. Mimi nimezaliwa na kukua kwa kuzingatia nidhamu ya Kisukuma, sijalelewa kihuni kufika kumsema mtu kama JK. Namsema EL kwa sababu ni mchafu, na sasa sitayasema yaliyo mazito au machafu zaidi dhidi yake, hadi nitakapoona kweli kachukua fomu kugombea Urais! Mimi sijasema Lowassa alidhulumu CCM kupata hisa Vodacom, nilichosema CCM ilikuwa iwe mbia wa MTN, kampuni iliyonyimwa leseni wakijua fika kuwa ilikuwa ikisaidie chama, badala yake wakafanya njama kuvunja tume ya mawasiliano kihuni, na hapohapo wakaipatia vodacom leseni lowasa kwa kutumia watoto wake, alipata walikipata. Ushahidi kuhusu hili ni kampuni yake kupewa U-Super Dealer wa Vodacom ambayo uliwafanya wanufaike kwa kuuza simu nchi nzima.

Kama wanasema Lowassa ni mzima, naomba akakimbie uwanja wa Taifa azunguke hata mara moja kama hataishia ICU. Na kama ni mzima, anatumia fedha za nchi kwenda kutibiwa nini ujerumani kila wakati au Ujerumani nako siku hizi kuna waganga wa kienyeji? Pili kwanini alikwenda kuombewa kwa Emmanuel Ministries huko Nigeria? Kampeni za Urais zinahitaji afya nzuri, sio mzaha kuweka mgonjwa akatufia kwenye jukwaa! Kuhusu tuhuma ya rushwa toka kwa Kimaro, nina hakika Kimaro bado yupo hai, na kama ni mkweli aseme ukweli. Kimaro ni rafiki yangu na nilimshawishi akawekeza hoteli ya Nyumbani sasa ni JB Belmonte, Mwanza. Sijachukua fedha ili nimpatie kitalu kwavile yeye sio mwindaji na sijasikia kuwa ana hiyo biashara. Ninachofahamu ana mahoteli na ndiyo biashara yake. Rais yupo kama alishaniita kunieleza hilo anaweza akasema, ni mkweli. Tuhuma za mimi kuhongwa na Kimaro alizianzisha Lowassa baada ya mimi kutaka kumuondoa Mkurugenzi wanyama pori wizara ya Maliasili. Mkurugenzi huyo alikuwa na mahusiano naye na baadae walikuja kuoza watoto wao. Hilo kila mtanzania analifahamu, na alimtetea sana abaki wizarani wakati huo. Lowassa yupo kwenye mtandao wa yote yanayosemwa kuhusu wanyama pori. Pia tuhuma za kumtapeli aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Mhe Karume ndio nazisikia leo. Karume sijafika nyumbani kwake Zanzibar na wala hata alipokuwa Ikulu Zanzibar. Yupo na anaweza kuulizwa, ni mkweli atasema yaliyo kweli.

Huyo msichana anayesemekana nilimpa mimba, mhudumu wa Dodoma hotel, ndiyo namsikia leo, na kama yupo aniletee mtoto huyo kwani ndio nasikia kwenye watu wa Lowassa baada ya kuweweseka na machache tu tuliyoyaweka hadharani. Mwisho la kupewa fedha na mtuhumiwa wa IPTL nalo jipya simfahamu, labda Lowassa anamfahamu! Tatizo la huyu Lowassa, ni kupata URAIS, asipoupata sijui kama atabaki na afya ya kuridhisha. Anatuhumu watu tusiounga mkono jitihada zake tu, je wanaogombea watakuwa na hali gani mbele yake? Ushauri wa bure kwa wapambe wa Lowassa: Kuleni fedha yake maana ni halali yenu, fedha za kukwapua kwa njia zisizo halali ni haki ya kila mtu kuzitafuna, ila Urais hatopata.Kidumu Ccm.

Wema Sepetu:Wanaoniponda Wengi Wao Wanatumia Tecno na Huawei

$
0
0
Katika hali iliyoshangaza wengi,beautiful oninye mwenye endless fame mnyange Wema Sepetu amesema watu wengi wanaomsema kwenye mtandao they don't have life na wengi wao wanatumia Tecno na Huawei kulog in kwenye mitandao ya kijamii na kuanza kumponda, akichezesha taya na Ephraim Kibonde katika kipindi cha jahazi amesema watu hao hawampi shida hata kidogo kwani wamepigika na yupo juu zaidi yao.

My Take:Hivi Sister wema hizo simu ulizozidharau unazijua vizuri kweli? Hivi unaweza ku-compare features za Huawei Ascend P7/Tecno H7 na Samsung Gallaxy S4?

Video: Marekani yatoa video inayoonesha mashambulizi ya anga dhidi ya ISIS nchini Syria

$
0
0
Makao Makuu ya Ulinzi, Pentagon Marekani imetoa kipande cha video inayoonesha jinsi walivyotekeleza na kufanikisha mashambulizi ya kwanza nchini Syria dhidi ya kundi linalojiita Islamic State Of Syria and Iraq (ISIS).

September 23 jeshi la Marekani lilitekeleza mashambulizi ya anga katika makao makuu ya kundi hilo Ar Raqqah, Syria.

Marekani na washirika wake wamelenga kushambulia na kutokomeza kundi hilo linalotekeleza mauaji na kuwachinja raia wa Marekani na Uingereza huku wakionesha katika vipande vya video.


'Si Lazima Kujua Kingereza Kwani Mie Muingereza, Hata Messi Hajui' - Ray

$
0
0
Mkurugenzi wa Kampuni ya filamu Rj Company,Vicenti Kigosi amesema si lazima kujua Kingereza maana hata Messi hajui, Ray amesema hayo alipokuwa akichat Live na mashabiki zake kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live

kinachokukutanisha na watu mahiri kila siku ya jumatano kuanzia saa sita za mchana mpaka nane kamili.
SI LAZIMA NIJUE KIINGEREZA
Mkali huyo ambae kwa sasa anachukuliwa kama moja ya watu wenye mafanikio katika tasnia ya filamu nchini ambae pia ameshawishi vijana kibao kuingia katika tasnia hiyo amefunguka na kuweka wazi kuwa suala la lugha ya kiingereza kwake ni changamoto lakini si jambo la ajabu sabgabu kuna watu wengi maarufu duniani wanapigwa chenga na lugha ya kiingereza.
Prince Dully >>>>Mbona haujui kingereza au uliishia darasa la saba,nini?
RAY Kigosi >>>>>>Hata messi hajui kiingereza kwani mimi muingereza nijue Kiingereza.
CHUCHU MCHUMBA WANGU
Msanii Vicent Kigosi ambae katika hizi siku za karibuni ilisikika kuwa yupo katika mahusiano na msanii mwingine wa filamu ambae anafahamika kama Chuchu Hansi hivyo ilipelekea mashabiki wa ukurasa wa facebook wa EATV kutaka kujua ukweli juu ya mahusiano hayo na kama kweli jamaa anampango wa kumuoa binti huyo au laah,na majibu ya Ray uyalikuwa kwamba wawe watulivu muda utakapofika ndio watajua ukweli wote juu ya suala hilo.

Ray Kigosi Amekana Kutoka kimapenzi na Msanii Blandina Chagula (Johari)

$
0
0
Ray amekana kutoka kimapenzi na msanii Blandina Chagula na kuwa mtaani kuna habari nyingi sana na nyingi hazina ukweli lakini kwa kuwa sisi ni kioo cha jamii hivyo jamii inakuwa inatuzungumzia kwa mambo mengi sana lakini ukweli ni kwamba sijawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Johari na wala sijawahi kuweka wazi juu ya maisha yangu ya mapenzi bali baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikizusha na kudanganya umma lakini Johari ni Mkurugenzi mwenzangu katika kampuni yetu na sii mpenzi wangu wala si mchumba wangu

Mwigizaji Jack Wolper Afunguka Kuwa Sasa Yupo Tayari Kuwa Mke

$
0
0
STAA mkali wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper amefunguka kuwa kwa sasa yuko tayari kuolewa kwani anaamini anastahili kuwa mke.

Wolper alisema, katika maisha siku zote anaamini kuna kipindi kinapita cha kufanya ujana ambacho tayari ameshakipitia na sasa ni muda wa yeye kutengeneza familia.

“Naamini kabisa huu sasa ni muda muafaka kwangu, niko tayari kabisa kuwa mke maana nimepitia vitu vingi ambavyo mara nyingi wengi wao huwa wanakimbilia kwenye ndoa wakiwa bado hawajavimaliza halafu mwisho wa siku wanazishindwa, mimi nishamaliza vyote,” alisema Wolper pasipo kufafanua kama tayari ameshampata mchumba au la.

Wolper amewahi kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na  mastaa kadhaa akiwemo Mohamed Mtoro ‘Dalas’ ambaye alimbadilisha dini ili waweze kufunga ndoa lakini ikaota mbawa.

'Kamwe Sijawahi Kutoa Rushwa ya Ngono kwa ‘Dairekta’ na Wala Sifikirii Kufanya Hivyo….” Sandra

$
0
0
MSANII wa siku nyingi katika tansia ya filamu Bongo, Salama Salmin ‘Sandra’ amefunguka kuwa tangu ameanza kujihusisha na mambo ya sanaa hajawahi kuwa na bwana ndani ya klabu ya Bongo Movies na wala hajawahi kutoa rushwa ya ngono kwa ‘dairekta’ kama ilivyo kwa wengine.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni, Sandra alisema kuna baadhi ya wasanii wanafikiri kuwa na mwanaume ndani ya Klabu ya Bongo Movie ndiyo kutimiza ndoto zao kumbe ni kujidharaulisha tu.

“Sina bwana wala sijawahi kutoa rushwa ya ngono kwa ‘dairekta’ na sifikirii kufanya hivyo kamwe, maana ni kujishushia heshima yangu  wakati mimi ni mke wa mtu na wala siwezi  kunadi mwili wangu,” alisema Sandra.

Taarifa Mbaya Kutoka Simba Kuhusu Kuvunjika Kwa Ivo Mapunda

$
0
0
Wakati zikiwa zimebakia takribani wiki mbili kabla ya kukutana na mahasimu wao wa jadi, klabu ya Simba imepata pigo kubwa katika timu.
Kipa namba moja wa timu hiyo, Ivo Philip Mapunda amevunjika kidole mazoezini Zanzibar jaa asubuhi na anatakiwa kuwa nje kwa wiki nane- maana yake hataweza kusimama langoni timu hiyo ikimenyana na watani, Yanga SC Oktoba 12.
Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe amesema kwamba, Ivo aliumia wakati anachupia mpira katika mazoezi ya asubuhi na kwa bahati mbaya mpira ukamgonga kwenye kidole kidogo cha mwisho mkono wa kulia.
Gembe amesema Ivo alitoka mazoezini baada ya tukio hilo na baadaye akapelekwa hospitali ya Mnazi Mmoja kisiwani humo, ambako baada ya vipimo ikagundulika amevunjika sana. “Si kuvunjika kwa mzaha, amevunjika sana na anatakiwa kupumzika kwa wiki nane, baada ya hapo aanze taratibu, ina maana makadirio ya kurudi tena uwanjani ni hadi baada ya miezi mitatu,”amesema Gembe.
Kuumia kwa Ivo kunatoa nafasi kwa makipa chipukizi, Hussein Sharrif ‘Cassilas’ na Peter Manyika kujibidiisha ili kuziba pengo lake.
Ivo anafanya idadi ya wachezaji wanne tegemeo majeruhi Simba SC, baada ya Paul Kiongera anayetakiwa kuwa nje wiki sita, Haroun Chanongo na Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ ambao hawatahitaji zaidi ya wiki ya moja ya kuwa nje ya UwanJa

Mchongo Mpya Alioupata Diamond Platnumz, Huu Unahusu Application ya Simu.

$
0
0
Ingawa hajaweka wazi namna dili hii itakavyokuwa lakini kupitia ukurasa wake wa Instagram,Diamond Platnumz amepost picha ambayo imebeba maandishi yasemayo ‘Ningependa kukutaarifu shabiki wangu pendwa kuwa kijana wako sasa ni balozi wa application mpya iitwayo Mziiki’.
Hii ni application ambayo itatumiwa na watu wenye simu za androad kusikiliza muziki huu ndiyo muonekano wake utakapokuwa ume instal kwenye simu yako.

Meninah Aongelea Issue ya Yeye Kufunga Ndoa na Mwanamuziki Diamond Platnumz

$
0
0
"Yaani sijui hata nianzie wapi kuzungumzia hili la kutaka kufunga ndoa na Diamond, naomba niseme ukweli kwamba nashangaa, kwanza sijui chochote, nimekuwa nikiandikwa mara kwa mara lakini taarifa hizo wala hazina ukweli wowote.

“Mimi na Diamond ni tofauti kabisa, sijawahi kuwa na ukaribu naye. Kwanza naumia sana na kutokwa na machozi kuendelea kusikia taarifa hizi kuwa naolewa naye kitu ambacho hakipo kabisa, hata yeye mwenyewe akisikia hivi anaweza kumtafuta mtu ambaye anasemwa kuwa anatoka naye jambo ambalo si la kweli.”

“Wema namheshimu kama dada yangu, mtu ninayemjua kwenye tasnia ya filamu Bongo, kwanza wote tunafanya sanaa japokuwa kwa upande wake anafanya filamu na mimi muziki. Hizo taarifa juu ya kuniwinda sijui na sijazisikia. Kiukweli zimenishtua sana.” Meninah

Diamond alipotafutwa kuzungumzia ishu hiyo hakupatikana kwa kuwa alikuwa ziarani barani Ulaya.

Ukweli Kuhusu Tetesi za Mwanamuziki Tunda Man Kufukuzwa Kundi la Tip Top Connection

$
0
0
Manager wa Tiptop Bab Tale amesema msanii Tunda Man hajasimamishwa kazi Tiptop na sio kawaida kwa Tiptop kusimamisha wasanii wake ila kila msanii ana mfumo wake wa kurekodi na kutoa kazi mpya. Tetesi za Tunda Man kusimamishwa kazi zilisambaa hivi karibuni zikichangiwa na ukimya wa Tunda Man baada ya kutoa video ya Msambinungwa February mwaka 2014.

Simu za iphone 6 Kimenuka, Watumiaji wa Simu Hizo Walalamika Zinapinda

$
0
0
Watafiti wamechanganyikiwa kuhusu ikiwa kampuni ya Apple inapaswa kutoa kauli yake kuhusu ripoti kuwa simu yake mpya ya iPhone 6 inajipinda mtumiaji anapoishi kuiweka ndani ya mfuko wa suruale yake.
Watu kadhaa ambao ni watumiaji wa iPhone 6 wamekuwa wakituma picha zao kwenye mtandao wa MacRumors ambazo zineonekana kuonyesha simu zao zikiwa na tatizo hilo.
Mwandishi wa habari kwenye mtandao wa 'Geek.com' pia aliripoti kuwa simu yake ye iPhone 6 imejipinda.
Na haijulikani nini hasa kinachoifanya simu hiyo kujipinda, baadhi wakisema huenda ni gamba lake ambalo limetengezwa kwa madini ya Aluminium ambalo linaifanya rahisi kwa simu hiyo kujipinda.
Taarifa za iPhone 6 kujipinda hazijaripotiwa tu kwenye blogu za habari za kiteknolojia bali pia kwenye vyombo vya habari kama Independent, the Washington Post, India Today na the Sydney Morning Herald.


Aibu! Mrembo asababisha Steve Nyerere kuzomewa uwanjani

$
0
0
NYOTA wa kuigiza sauti za watu maarufu aliye pia mwigizaji wa sinema za Kibongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ wikiendi iliyopita alijikuta akiaibika kwa kuzomewa na kupopolewa kwa chupa za maji na mashabiki wa Klabu ya Simba baada ya kuingia uwanjani na demu aliyevaa ‘kihasarahasara’.Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’akiwa na mrembo huyo.Ishu hiyo ilijiri Jumamosi ya Septemba 20, 2014 ndani ya Uwanja wa Jamhuri mjini hapa wakati wa pambano kati ya Yanga na Mtibwa Sugar katika Ligi Kuu Tanzania Bara ambapo wenyeji walishinda 2-0.

Steve alitinga uwanjani saa 11:00 jioni akiwa na demu huyo mrefu kwake,aliyetinga kipensi cha jinzi kifupi na tisheti ya njano na kijani (zinazotumiwa na Yanga).
Wakati wawili hao wakipita kwenye jukwaa la mashabiki wa Simba, ndipo walipozomewa na wengine kuwarushia chupa za maji kwa kile kilichodaiwa kuwa, demu huyo alivunja maadili ya Kitanzania kwa kuvaa kihasara hadharani

Afande Sele Anaswa na Demu Mpya..Mwenyewe Adai ni Maswala Yake Binafsi Asiulizwe

$
0
0
MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya Seleman Msindi ‘Afande Sele’, juzikati alinaswa akiwa na demu mpya akiwa ni siku moja tu baada ya kufanyika kwa 40 ya aliyekuwa mzazi mwenzake, marehemu mama Tunda.

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Septemba 21 mwaka huu ndani ya Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro wakati staa huyo aliyekuwa mmoja wa watoa burudani katika tamasha la Fiesta, alipoonekana akiingia akiwa ameambatana na mrembo mmoja akiwa ameshikana naye kimahaba.

Akiwa ndani ya uwanja huo, mkali huyo wa mashairi yenye vina kwa muda mwingi alikuwa pamoja na msichana huyo ambaye hakufahamika jina, wakiwa na dalili zote za wapendanao.

Alipoulizwa juu ya suala hilo, Afande Sele alicheka na kumtaka paparazzi wetu kuachana na masuala hayo aliyoyaita binafsi, badala yake asubiri apande jukwaani apate picha za kazi atakayofanya.

Taarifa za Mchezaji Asamoah Gyan Kumuua Rafiki yake na Kumtoa Kafara Hizi Hapa

$
0
0
Nahodha na mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ghana, Asamoah Gyan, amekanusha madai kuwa alimtoa kafara yake ambaye pia alikuwa mwanamuziki mashuhuri nchini Ghana Castro.

Gyan amesema tetesi hizo ni za kushangaza sana wala hazina msingi.

Mwanamuziki huyo aliyekuwa anaiimba nyimbo za mtindo wa Afrobeats, ambaye jina lake halisi ni Theophilus Tagoe, alitoweka pamoja na rafiki yake Janet Bandu, mnamo mwezi Julai.

Wawili hao walitoweka wakati walipokuwa wamekwenda likizo na Gyan ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa Sunderland, katika mji wa Ada.

Madai katika vyombo vya habari nchini Ghana yanasema kuwa kutoweka kwa rafiki ya Gyan kumezua wasiwasi baadhi wakidai kuwa huenda alimtoa kafara mwanamuziki huyo

Castro na rafiki yake Bandu, walionekana kwa mara ya mwisho wakielekea baharini na baadaye iliarifiwa kuwa walizama.

Miili ya wawili hao haikuwahi kupatikana na madai yaliendelea kusambazwa mwezi huu wakati ambapo kakake Gyan, Baffour Gyan alidaiwa kuwa mmoja wa genge la vijana waliowashambulia wandishi wa habari waliohoji maswali kuhusu madai hayo.

Hata hivyo baadaye aliachiliwa na polisi waliokuwa wamemkata kwa lengo la kumfungulia mashitaka.

Tetesi hizo zilimfanya Gyan kuitisha mkutano na wandishi wa habari kuzungumzia madai hayo.

Wakili wake Kissi Agbyabeng alitoa taarifa akisema kuwa familia ya Gyan imeshangazwa sana na madai hayo na iliamua kutosema chochote ili polisi waendelee na uchunguzi wao.

Taarifa hiyo ilisema: " Tumekuwa kimya huku madai na tetesi zikienezwa kila upande katika vyombo vya habari. Tumekuwa kimya sio eti kwa sababu tunaficha ukweli, bali kwa sababu hatuoni umuhimu wa kusema kilichojiri mjini Ada. Tumekuwa kimya kwa sababu tunataka polisi wafanye kazi yao bila kuingiliwa.''

Mwanzilishi wa Kampuni ya 'Apple' Aliwazuia Watoto wake Kutumia iPad, iPhone na iPod, Fahamu Sababu

$
0
0
Bidhaa za kampuni ya Apple zina mashabiki na wateja wengi duniani, hii inathibitishwa na foleni kubwa ya watu waliojitokeza kwenye vituo mbalimbali duniani kununua toleo jipya la iPhone6.

Tumesikia watu wakiachana ama familia zikitengana kwa sababu tu baba ameshindwa kununua bidhaa za kielekroniki za kampuni ya Apple. Mwaka jana familia moja nchini China iliwauza watoto wao ili kupata pesa ya kununua iPhone5.

Kwa kuzingatia hayo, huenda ukadhani watoto wa mwanzilishi wa kampuni ya Apple na mgunduzi wa bidhaa hizo, Steve Jobs wanafaidi zaidi bidhaa hizo.

Na huenda ukadhani hata kuta za nyumba yao zingeweza kuwa za mfumo wa simu za kisasa za kupangusa ‘Screen Touch’ na mawasiliano ya hali ya juu ndani ya nyumba hiyo kwa mfumo huo.

Lakini ukweli ni kwamba, marehemu Steve Jobs hakuwaruhusu hata kidogo watoto wake kutumia iPhones, iPods wala iPads nyumbani kwake.

Katika article iliyoandikwa na New York Times wiki hii, mwandishi wa habari Nick Bilton ameeleza jinsi ambavyo alishangaa majibu ya Steve Jobs alipomuuliza jinsi ambavyo watoto wake wanapenda bidhaa za kampuni hiyo.

“Hawajawahi kutumia kabisa. Tunadhibiti kiasi ambacho watoto wetu wanatumia teknolojia nyumbani.” Alijibu Steve Jobs.

Nae mwandishi maalum wa Steve Jobs, Walter Isaacson ambaye alikuwa akitumia muda mwingi nyumbani kwa boss wake huyo alithibitisha kuwa maoengezi ya uso kwa uso yalitawala katika nyumba hiyo.

“Kila jioni Steve alikuwa akipata chakula cha usiku na familia yake kwenye meza kubwa jikoni, wakijadili vitabu na historia na vitu vingine vingi. Hakuna mtu aliyekuwa na iPad au computer. Watoto hawakuonekana kuwa addicted hata kidogo na vifaa hivyo.” Alieleza Isaacson.

Utafiti uliofanywa katika eneo la Chuo Kikuu cha California, Los Angeles na kuchapishwa hivi karibuni unaonesha kuwa siku chache baada ya kuzuia watoto kutumia vifaa vya kieletroniki vya simu, ufaulu wa watoto katika masomo ulipanda ghafla.

Utafiti unaonesha kuwa kwa wastani watoto nchini Marekani hutumia zaidi ya saa saba na nusu kwa siku katika matumizi ya simu za kupangusa na vifaa vingine vya kielekroniki kama iPads, iPod n.k.

Uamuzi ni wako, kumnunulia mwanao vifaa vya hivyo au kumuweka mbali na mapinduzi hayo ya kiteknolojia.

Hotel ya Blue Pearl Iliyoko Ubungo Yafungwa Kwa Aibu Kisa Kizima Hichi Hapa

$
0
0
Services at the Blue Pearl hotel in Dar es Salaam’s Ubungo suburb have been affected after the owner of the business allegedly failed to pay rent amounting to about Sh6 billion ($3,800,000).

Yesterday afternoon officials from Majembe Auction Mart arrived at the hotel and started taking out furniture and packing them into a lorry.

Customers were told to vacate the hotel premises because it had been closed down and services were no longer being provided.

The executive director of Majembe Auction Mart, Mr Seth Motto, said his organisation was called into action after the management of Ubungo Plaza Ltd, which is the owner of the building, assigned them to carry out the operation.

Mahakama Yatoa Hukumu Kesi iliyofunguliwa na Mwandishi wa Habari Saed Kubenea

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo imetoa hukumu ya kesi ya namba 28 ya mwaka 2014 ambayo iliitaka mahakama hiyo kutoa tafsri sahihi ya mamlaka na mipaka ya Bunge maalum ya katiba iliyofunguliwa na mwandishi wa Habari Saed Kubenea.

Akisoma hati ya amri ya mahakama Jaji Augustino Mwarija kwa niaba ya majaji watatu waliosikiliza shauri hilo,amesema kumekuwepo na Utata katika kifungu cha 25(2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 katika lugha mbili zilizotumika kuandika sheria hiyo. Na kusema kuwa kutokana na kifungu hicho kinaipa mamlaka bunge maalumu la Katiba kuijadili rasimu ya katiba,kubadili au kuboresha na kuwa Bunge hilo lina mipaka kwa kuzingatia kifungu cha 9(2) cha sheria ya mabadiliko ya katiba.
Akizungumza baada ya amri hiyo nje ya mahakama kuu Wakili wa Saed Kubenea, Peter Kibatala amesema wanafurahi kuona mahakama imetoa maamuzi kwa wakati na kueleza kuwa tasfiri iliyotolewa ni katika kusaidia wananchi kupata katiba iliyotokana na maoni yao.
Katika kesi hiyo, Kubenea aliiiomba mahakama itoe tafsiri sahihi ya Mamlaka ya Bunge la Katiba kwa kuzingatia kifungu cha 25 (1) na (2) cha Sheria ya Marekebisho ya Katiba Namba 83 ya mwaka 2011. na kuiomba Mahakama itamke kama Bunge hilo lina mamlaka ya kubadilisha maudhui ya Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba

Nakala ya Rasimu ya Katiba Mpya iliyopendekezwa: Ibara 28 Zimefutwa, 42 Zimeongezwa….47 Zimebaki Kama Zilivyo na 186 Zimerekebishwa

$
0
0
Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba jana ilikabidhi bungeni Rasimu ya Katiba inayopendekezwa ikiwa na ibara 289 kulinganisha na 271 za Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Warioba.

Rasimu hiyo pia ina sura mpya mbili ambazo ni Mamlaka na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na nyingine inayohusu Ardhi, Maliasili na Mazingira.

Akiwasilisha rasimu hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Andrew Chenge aliliambia Bunge kuwa Ibara 233 za rasimu hiyo zinatokana na Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Chenge, ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), alisema ibara 47 za Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba zimebaki kama zilivyokuwa, 186 zimefanyiwa marekebisho, 28 zimefutwa na 41 ni mpya.

Rasimu hiyo ya Katiba inayopendekezwa imefuta kabisa muundo wa Muungano wa shirikisho ambao ungezaa muundo wa serikali tatu na badala yake imerudisha muundo wa sasa wa serikali mbili.

Chenge alisema kamati za Bunge hilo pamoja na wajumbe walio wengi, waliona kuingiza muundo wa shirikisho ilikuwa ni kukiuka makubaliano ya Muungano yaliyofikiwa mwaka 1964.

Kwa kurejesha muundo wa serikali mbili uliokuwa ukipigiwa chapuo na CCM, Rasimu hiyo imependekeza kuwapo kwa makamu watatu wa rais.

Chenge alisema uongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mgombea mwenza atakayekuwa makamu wa kwanza wa rais.

Chini ya muundo huo, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), atakuwa makamu wa pili wa rais ilhali Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakuwa makamu wa tatu wa rais.

Chenge alisema mapendekezo hayo yamezingatia ukweli kuwa kuwapo kwa mgombea mwenza anayekuwa makamu wa kwanza wa rais, kutafanya rais na makamu wake kutoka chama kimoja.

Rasimu hiyo inayopendekezwa, imepunguza Tunu za Taifa kutoka saba zilizokuwamo kwenye Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba hadi nne huku mambo ya muungano yakiongezwa kutoka saba hadi 14.

TCU Yakifungia Chuo cha IMTU Kudahiri Wanafunzi Wapya

$
0
0
Tume ya vyuo vikuu nchini Tanzania imesitisha udahili wa wanafunzi wapya katika chuo kikuu cha IMTU kwa mwaka wa masomo 2014/15 na kukipa muda wa miezi 3 chuo hiko kurekebisha kasoro zinazojitokeza mara kwa mara ikiwemo kudahili wanafunzi wengi.

Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es salaam leo Kaimu katibu mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Prof. Magishi Mgasa amezitaja kasoro nyingine zilizopelekea tume hiyo kukifungia udahili chuo hicho ni pamoja na kuendesha program ya ngazi ya cheti bila ya ithbati ya TCU sambamba na kukaidi agizo lilitolewa na Tume hiyo la kusitisha programu hiyo

Amesema katika kipindi cha miezi mitatu ambacho chuo hicho kitakuwa kimesimamishwa kufanya shughuli za udahili TCU itakuwa ikikifuatilia kwa karibu kuona iwapo chuo hicho kitatekeleza na kufuata taratibu zinazotakiwa.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images